“Sisi Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) hatutafuti sababu ya kutolipa fidia, bali tunatafuta sababu ya kulipa fidia. Wanahabari tusaidieni kuwaelimisha waajiri na wafanyakazi wote. kuna faida kubwa WCF ,”Silvanus Kuloshe, Afisa Madai Mkuu WCF, Ofisi ya Kinondoni,Dar es Salaam
Umuhimu wa habari haujashuka, jambo la msingi tunafanyaje ili kuwa na vyanzo vingine vya mapato katika vyombo vyetu vya habari. Kwa sasa mapato hayajapungua kwenye vyombo vya habari pekee - Deodatus Balile, M/kiti TEF wakati wa Mkutano Maalumu wa Marekebisho ya Katiba, DSM.
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) limeeleza kukerwa Ofisi za Gazeti la Pambazuko kuvamiwa, laomba mamlaka husika kufuatilia na hatua za kisheria kuchukuliwa.
Wanawake kutoka Sekta ya Mawasiliano nchini, wamekubaliana kuweka msingi wa pamoja wa uanzishwaji wa Tanzania Women in Communication Association (TWICA), kama chombo kitakachowaunganisha kwenye sekta hiyo.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile (wa kwanza kushoto), Mjumbe wa Kamati ya Utendaji TEF, Joseph Kulangwa (katikati) na Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEF, William Shao wakiwa msibani kwa aliyekuwa mwanachama wa TEF, Revocatus Makaranga Kimara, Dar es Salaam
Mwandishi mkongwe na Mwanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Revocatus Makaranga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Makaranga aliyewahi kufanya kazi katika kampuni binafsi ya Mwananchi Communions Ltd na New Habari Corporation, alifikwa na mauti Muhimbili.
Mratibu wa Jukwaa la Wahairi Tanzania (TEF), Anita Mendoza (kushoto) na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji TEF, Tausi Mbowe wakiwa ni sehemu ya wahariri walioshiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyoratibiwa na Shirika la Umeme wa Ugavi nchini (TANESCO), Jijini DSM.
Wahariri ni chanzo cha kuonesha changamoto katika jamii, sisi kama serikali tupo tayari kupokea changamoto hizo na kuzifanyia kazi kwa maslahi ya umma - Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo akizungumza na wahariri katika semina iliyoandaliwa na Tume ya Ushindani nchini (FCC).
Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile (kushoto), akiwa Aga Khan University, Nairobi, kwenye Mkutano wa Jukwaa la Wahariri Afrika. Katikati ni Mtendaji Mkuu wa Exim Bank Afrika Mashariki, Dk. Joshua Oigara na kulia ni Rais wa Jukwaa la Wahariri wa Afrika (TAEF), Churchill Otieno.