Nimesikitishwa na kifo cha Ndugu Joseph Sebastian Pande, aliyekuwa akitumikia nchi yetu katika nafasi ya Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka. Nawapa pole Mkurugenzi wa Mashtaka, Ndugu Sylvester Mwakitalu, familia, wakuu wa divisheni na vitengo, wafanyakazi wote katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, ndugu, jamaa na marafiki. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema. Amina.