#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 187
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi ASP Geofrey Lutufye.
Mhe. Lissu: Mnajifanya mapolisi mnawasingizia watu vitu vya bure haya itakushangaza hao mliowakamata baada ya kesi yao kuisha ni mashahidi wa kesi hii?
ASP Geofrey Lutufye : Hainishangazi.
Mhe. Lissu: haikushangazi kwasababu huo ndio utaratibu wenu mapolisi wa Tanzania.
Mhe. Lissu: Au unabisha nikufungulie ripoti ya Jaji Mkuu Othman Chande amesema mnawafungulia watu makosa ya uongo.
Sasa nikuulize swali lingine, umewahi kuona video mimi nikiwa nazungumza habari za huo uchaguzi mkuu?
ASP Geofrey Lutufye : amekaa kimya
Mhe. Lissu: Unajua kwanini nimeshitakiwa kwa Uhaini ASP geofrey lutufye? Unajua sababu.
ASP Geofrey Lutufye : Sababu ya ile kauli uliyotoa.
Mhe. Lissu: Ipi hiyo?
ASP Geofrey Lutufye : Ulisema utazuia uchaguzi wa mwaka 2025.
Mhe. Lissu: Ndio nakuuliza uliiona hiyo video?
ASP Geofrey Lutufye : Sikumbuki.
Mhe. Lissu: Hawa ndio kesho watakuwa ma RPC siku inayofuata utashangaa anakuwa IGP,
Sina maswali mengine Waheshimiwa majaji.
Watu wanasonya tu hapa.
Anasimama Wakili wa Serikali Renatus Mkude kwa ajili ya Re-examination
Maelezo yako uliandika kama nani?
ASP Geofrey Lutufye : Kama shahidi.
Wakili: Unalizungumziaje kuhusu kujiandika mwenyewe?
ASP Geofrey Lutufye : naweza kujiandika mwenyewe au kuandikwa.
Renatus Mkude: Sina swali lingine. Re Examination imeishia hapo.
Jaji anamruhusu Shahidi.
Shahidi anatoka akiwa ameshika kipaza sauti.
Jaji Ndunguru: Unasahau maji yako hapo.
Shahidi: Hapana siyataki tena.
Jaji: Basi turudishie hiyo MIC tafadhali.
Anairudisha na kutoka nje akiwa anatikisa kichwa.
Watu wanacheka.πππ
Kesi inaahirishwa watu wakale.
Tutaendelea baada ya lisaa limoja.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Oktoba 7, 2025
Jana tuliishia part 53 so leo tunaendelea na
Part 54
Imepigwa High Courrrrrttttttttttt ni sauti ya Askari inatoka kizembe kabisa.
Watu wote wanasimama kwa utii mkubwa sana.
Majaji wanaingia na kutoa heshima ya kuinama mahakama yote inafanya bowing.
Mh. Lissu ameingia anawaambia watu changanyachanganya ile style ya kukunja ngumi na kuizungusha.
Muda huu anatoa makabrasha yake ni mengi sana.
Anayafungua fungua kwa vibe.
Shahidi hajaingia bado Mahakamani.
Namuona anaingia amevaa kaunda na kanyoa kipara.
Huyu Afande George ni mfupi wa kimo.
Leo amepanda kizimbani anacheka cheka.
Majaji wanaandika hapa.
Kesi haijaanza.
Kimya kidogo kimetanda hakuna kinachoendelea kama dakika 5 hivi.
Anasimama karani Criminal session No. 19605/2025.
Anasimama Renatus Mkude, Wakili Mkuu wa serikali, Johari, Katuga, Mrema, Cathbert Mbiringe na Winniwa Kasawa.
Amemaliza kuwatambulisha mawakili wake.
Mhe. Lissu anaulizwa kama yuko tayari.
Nasikitika kusema Dr. Stephen amezuiliwa kuja mahakamani na amezuiliwa na afisa wa uhamiaji.
Idara ya Uhamiaji wanazuiaje mtu kuingia mtu mahakamani.?
Lakini pia mgeni aliyeingia ndani ya nchi na ana Visa hawezi kukatazwa kuingia mahakamani.
Sasa hawa Uhamiaji wanahusika nini na hawa watu wanaozuia watu kuja mahakamani.?
Mimi jukumu langu ni kusema tu hata ikija kutokea mkaamua kunipeleka kokote mtakapoamua baada ya uamuzi wetu nitaenda huko nikiwa na amani (happily) lakini siwezi kunyamaza.
Niko tayari kuendelea.
Majaji wanaandika hapa.
Majaji wameteta kidogo hapa. Kuhusu swala alilolizungumza Mh. Lissu.
Jaji anawasha kipaza sauti muda huu, tumekusikia mshitakiwa tutafuatilia na tutawasiliana na Msajili.
Mhe. Lissu anadakia kuwa huyo yupo na hataondoka nimemwambia asiondoke kabisa.
Jaji anasema ni sawa.
Jaji anamkumbusha shahidi kuwa yuko chini ya kiapo. Lissu anaanza.
Mhe. Lissu . Jina lako ni George
George : ni jina langu.
Sasa nakuuliza maswali nataka ndio au hapana.
Nikisema toa maelezo toa.
Sitaki rongorongo.
George : sawa.
Mhe Lissu. Wambie majaji kama uliandika maelezo huko nyuma.
George . Ndio niliandika.
Mhe Lissu : ni kweli au si kweli uliandika maelezo mara mbili. Tar. 08 na 10 April 2025.
George : Niliandika mara moja aaaaaa ni kweli niliandika mara mbili.π
Mhe. Lissu : waeleze kama ukionyeshwe hayo maelezo yako utayatambua?
George :Nikionyeshwa nitayatambua.
Mhe. Lissu : Na mimi ninayo. Sasa niliyo nayo ni copy. Waheshimiwa majaji naomba shahidi aonyeshwe maelezo ya maandishi ya mkono wake nisitumie haya copy ya kwangu.
Mawakili wa Serikali: wanatafuta hayo maelezo, wanafungua makabrasha yao hapa.
Part 55 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako kwenye tweet hii
Wapendwa
Mawakili wa Chama wamefika Central wamefanikiwa kumuona na kuzungumza na Frida Mkoroti, Kiduku na Izack.
Kwasasa wanapambana kuona kama watapewa dhamana au kufikishwa Mahakamani.
Tuendelee kupaza sauti kwa ajili yao.
#FreeFridaMikoroti#FreeKiduku#FreeIzack
Kuna uwezekano mkubwa sana tukashinda dau nono around milioni kumi Jumatatu hii pale Sportybet. Goli moja lipatikane kila mechi, Jumla ya Mechi ni 50.
Mkeka una odds 327+
Stakeπ31K | Payoutπ10.2M
Retweet upewe Code mapema