@mangekimambi@HecheJohn@TunduALissu Mtu alijitoa mwenyewe CDM kaenda panapo mfaa anatukana na kukashifu chama!alafu mnakubali vipi kumrudisha mtu aliye wasaliti? This is unprofessional 😎
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 228
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa Waheshimiwa Majaji naomba nimalizie nisiwachoshe.
Hoja yangu inahusika na maamuzi ambayo hayamalizi kesi, kesi bado ipo na tutakapoenda kwenye substance nitawaoneshe Majaji kwenye hicho walichokileta wao wenyewe ambavyo kesi bado inatusubiri.
Kwa bahati mbaya wametupotezea muda sana hivyo nawaombeni Waheshimiwa Majaji mkatae maombi hayo.
Anasimama Katuga anasema Waheshimiwa Majaji maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii na kanuni ya 65 kanuni ndogo ya 1. Waheshimiwa Majaji ukisoma notice yetu inataja kifungu cha 6 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii, Waheshimiwa Majaji lalamiko la mjibu maombi lisingekuwepo kama angeipitia kanuni ya 48.
Jaji anamwambia Katuga ulishamaliza usilete jambo jipya nenda moja kwa moja kwenye maombi.
Katuga anaendelea
Waheshimiwa Majaji maombi yetu yamejikita kuiomba Mahakama hii tukufu iweze kuangalia uhalali na usawa wa muenendo wa shauri lililoko mbele ya Mahakama kuu.
Maombi haya yametokana na mzizi wa upande wa Jamhuri kuleta notice ya kuongeza ushaidi ambao haukusomwa wakati wa commital na upande wa Jamhuri ulifanya vile kuendana na kifungu cha 308 cha CPA, kifungu hiki Waheshimiwa Majaji kinaweka zuio kwamba hakutakuwa na ushahidi ambao utaongezwa Mahakamani kama ushahidi huo haukusomwa hautaruhusiwa kuongezwa unless upande wa Jamhuri utatoa notice ya kuongeza ushaidi huo.
Tunatakiwa kutoa notice ili mshitakiwa asikutane nayo by surprise, kifungu hicho kinaitaka Mahakama wakati inafanya reasonablity ya notice ifanye vitu gani.
Mahakama wakati inatakiwa kutambua reasonablity ya notice inapaswa kuzingatia kifungu cha 308 kifungu kidogo cha 3 inatakiwa kuuchambua ushaidi wenyewe.
Naona Job Mrema ni kama kambonyeza Katuga ameinama sijui wanaongea nini na wenzake,
Halafu sio mara moja kila baada ya sentence kadhaa vikao vinakuwa vingi.😤
Anaendelea Katunga
Mahakama ilienda kuangalia huo ushahidi katika ukurasa wa 431 wa muenendo wa Mahakama kuu na kuita ni ushaidi mpya umekusanywa baadae na hivyo wamekataa.
Ushaidi unakatakiwa pale ambapo unakuwa umefikishwa Mahakamani baada ya kuwa umepimwa ndipo Mahakama inaamua uingie au usiingie, upokelewe au usipokelewe lakini hauwezi kuamuliwa wakati unakuwa introduced.
Kifungu cha 308 kimetoa nini Mahakama inafanya, ndo maana kwenye maombi yetu tunasema tumenyimwa haki ya kusikilizwa in relation na huo ushahidi.
Haki ya kusikilizwa ni haki ya kikatiba, maana ya hii haki ya kusikilizwa ni kumpa mtu haki ya kumsikiliza full kwa utimamu ndo maana Mahakama ina vitu vitatu vya kupima.
Ushaidi unapimwa unapokuwa umefika Mahakamani, kusema ushaidi ni mpya usiletwe ni kuukataa ushaidi kabla hata haujafika Mahakamani.
Mahakama hata haikuusikia ushaidi lakini ikaenda kusema ushaidi huo ni irrelevant.
Utaratibu wa proceeding ulikuwa umekiukwa na ukiukaji ambao unaenda kwenye shauri yenyewe na ndiyo maana upande wa Jamhuri tukaona kwa busara zenu muangalie hizo proceedings hatuwezi kuendelea na hizo illegalities.
Anaendelea Katuga
Tunataka Mahakama iangalie ni kwa namna gani kwa muda gani ushaidi unaangaliwa na kuwekwa kama ushaidi.
Kwenye kifungu hakuna sehemu tuliposema Mahakama iende ikaupime huo ushahidi ilikuwa ni notice tu, ushaidi kuja Mahakamani na kufukuzwa kabla ya kusikilizwa huko ni kutunyima haki.
Ni vigumu kupima ushaidi ambao hauko hata mahakamani.
Ukurasa wa 431 wa proceedings naomba muuangalie waheshimiwa Majaji, jambo hili lilikiuka taratibu za mienendo ya proceedings.
Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya rufani tunaomba maombi yetu yaangaliwe na yakubaliwe.
Waheshimiwa Majaji ya kwetu ni hayo tu.
Part 229 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 227
Anasimama Wakili wa Serikali Mrema
Anasema naomba kuongeza kidogo kwenye mawasilisho yaliyofanywa na Wakili mkuu wa Serikali Katuga, naomba kuongeza yafuatayo.
Waheshimiwa Majaji hii obligation inayowasilishwa mbele ya mahakama ya rufani lazima iwe na uwezo wa kuondoa shauri hilo lililoko mbele ya Mahakama hii, nikirejea shauri alilolilejea, shauri la DPP dhidi ya Mohammed Ussi naomba kuialika Mahakama hii kwenye kifungu cha 5 kifungu kidogo cha 2.
Mleta maombi amefanya reference kwa kifungu ambacho kimepitwa na wakati it's not applicable.
Kifungu hiki kukihusianisha na kesi ya Mohammed Ussi na kukileta kwenye Sheria ya sasa it's not applicable.
Kifungu cha 8 kinazungumzia mashauri ya madai, swali la kujiuliza ni je shauri hili ni la madai.
Jaji anawasha kipaza anauliza. Katuga ulisema Mrema anaongezea sasa mbona anarudia yaleyale.
Watu wanacheka😂😂😂😂😂
Jaji anamwambia Mrema aendelee ila asirudie mambo ambayo tayari Katuga ameongea.
Mrema anasimama anasema waheshimiwa Majaji ni hayo tu.
Watu wanacheka maana ni kama alichosema Jaji kimemto kabisa Mrema kwenye mood.😂😂😂😂
Anasimama Mhe. Lissu
Waheshimiwa Majaji naomba mniruhusu nijibu hoja za waleta moambi.
Wanacholalamikia siyo order wanalalakikia findings.
Waheshimiwa Majaji wanacholalamikia wamekileta wenyewe kwenye hati yao ya maombi hicho kiko kati ya ukurasa wa 428-431 wanalalamikia rulling, uamuzi.
Uamuzi wanaoulalamikia unajadili ushaidi wanaotaka kuuingiza, na Mahakama ikajadili ushaidi huo kwamba ni kinyume na Sheria hautaingizwa.
Kama wasingekuwa wanalalamikia hii ruling wasingeileta mbele ya Mahakama yako. Finding is not similar to a decision.
Waheshimiwa tuasume Mawakili hawa wako sahihi finding is similar to decision, tuangalie Mahakama inasema nini juu ya aina hii ya ushaidi, Mahakama ikasema ni kinyume na Sheria hauruhusiwi kuingia.
Mawakili waleta maombi wameleta kesi muhimu sana kesi ya Peter Michael Madeleka, kuna mahali katika kesi hiyo ambako Mawakili wa Serikali wamepakimbia kama ukoma, ukurasa wa 9 Mahakama ilisema hivi kuhusiana na hicho kifungu hayampi mamlaka ya kuimove Mahakama.
Mhe. Lissu anawambia Mawakili wa Serikali ahsanteni sana kwa kuleta kesi ya Madeleka.
Watu wanacheka 😂😂😂😂 maana akina Katuga wameleta kesi ambayo badala ya kuwasaidia kumkandamiza Mhe. Lissu yenyewe ndo imekuwa msaada kwa Mhe. Lissu.
Anaendelea Mhe. Lissu
Mamlaka ya Mahakama ya rufani kuitisha Suo moto ni mamlaka yake yenyewe haiwezi kuwa moved na waleta maombi.
Kama Mahakama haijaiona yenyewe haiwezi kuletewa maombi.
Wanasema nisiwafundishe lakini mkiangalia record waliandika barua, walileta maombi kisha wakaandika barua wanataka kuimove Mahakama.
Katuga amesema maombi yao wameyaleta under 6.3, Waheshimiwa Majaji nawaomba muangalie maombi hayo kama kuna sehemu wametaja kifungu hicho. In their notice of motion hakuna sehemu wametaja ni 6 ipi kati ya vifungu 6 vya Sheria hiyo hawawezi kuja hapa kuzungumza kitu tofauti na maombi yanavyozungumza.
Nirudi kwenye hoja ya Job Mrema, mmealikwa Majaji kukubaliana na hoja kwamba Sheria imeshabadilika ni vifungu tofauti, Waheshimiwa Majaji mimi nina revised Act of 2023 inasema section 5 haina marekebisho ya kabla ya 2023 kwa hiyo hii hoja ya kwamba kuna Sheria imebadilika ni vitu tofauti ni hoja ambayo nachelea kusema haina mashiko.
Waheshimiwa Majaji wakili ametaja rule 48.1,
Waheshimiwa Majaji inazungumzia PO must have a capacity to dispose of application na kwa maana hiyo anasema pingamizi langu halina uwezo wa kumaliza madai,
Je kwenye hoja ya kwangu hii kwamba maombi haya hauruhusiwi kwasababu hayana uwezo wa kuyafuta maombi kama inasema imeletwa chini ya kifungu cha 8.2.d? hakuna hoja hapo.
Part 228 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 226
Anaendelea Mhe. Lissu.
Waheshimiwa Majaji uamuzi uliotolewa na Mahakama ya rufani katika kesi ya Katibu Mkuu wa CHADEMA na bodi ya wadhamini wa CHADEMA vs Saidi Issa Mohammed na wenzake inasema kwamba kama mdaawa (Mleta maombi) analeta maombi mwenyewe ni yale yaliyoko kifungu cha 6 kifungu kidogo cha e, maombi mengine ni Mahakama yenyewe ndiyo inaamua bila kusukumwa na yeyote au kuletewa maombi yenye hati ya kiapo.
Waheshimiwa Majaji kwa vyovyote vile maombi hayo hayako halali mbele ya mahakama hii kwani hayakuletwa katika utaratibu wa kisheria kwani Mahakama hii haijaamua maombi haya yaje yenyewe Suo moto kwa hiyo Mahakama isikubali kusikiliza maombi hayo kwasababu ambazo nimezisema.
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa waheshimiwa Majaji sijui kama mnaniruhusi niendelee au wajibu kwanza.
Jaji anasema Jamhuri wajibu kwanza PO kisha tutaendelea.
Anasimama Wakili Katuga anasema Waheshimiwa Majaji tukirejea mapingamizi yake ya awali yameletwa chini ya kifunga cha 8.2.d hiki ni kifungu mahususi kwa mashauri ya madai.
kifungu hiki kilikopwa kikatumika kwenye madai kwenye mashauri ya rufaa, hata kama Mahakama yenu tukufu kwa rejea hizo za Mahakama hii ikakikopa kitumike kwenye maombi yetu haya bado tunasema kwamba maombi yetu yako sahihi mbele ya mahakama hii tukufu tofauti na kile ambacho mjibu maombi amekileta kama pingamizi la awali.
Maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 specifically kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya Mahakama. Kanuni ya 65 na kanuni ya 45 ya kanuni za Mahakama ya Rufani inasuport maombi yetu.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa Majaji ukiyasoma maombi yetu kwenye notice of motion hakuna sehemu yeyote tunayoiomba Mahakama hii tukufu ipitie order ya Mahakama au uamuzi wa Mahakama, pale mwisho tunasema Mahakama idiscuss kukataa ushahidi hatujazungumzia kukataa notice, sisi tunazungumzia kuuchambua na kuukataa ushahidi.
Hakuna sehemu kwenye maombi haya tunalalamikia order, Mahakama yenu itaona kwamba pingamizi la mjibu maombi limekuwa mislead hakuconsue sawasawa maombi yetu.
Pale ambapo neno or litatumika kwenye Sheria yeyote maana yake maneno haya hayako similar yanatumika tofauti, Waheshimiwa Majaji nimewarejesha humu muweze kukitafsiri kifungu cha sita. Haya maneno yanatakiwa yatafisiriwe tofauti hayaendi pamoja ama hayategemeani, inaweza kuwa kimoja wapo kati ya haya.
Kama mahakama yenu imekikopa kifungu cha 8.2.d kinazungumzia katazo la decision or order ndo hauwezi kuziombea appeal or revision.
Sasa tunapata wapi nguvu za kuleta pingamizi kwa tafsiri hiyo tunaiomba Mahakama hii ikaangalie maana ya maneno haya.
Waheshimiwa nawarejesha kwenye kamusi kwa sababu nayo ni kati ya vitu vinavyopaswa kutumika kutafsiri Sheria. Katika ukurasa wa 129 kamusi inadefine order ni nini?
Kwenye application yetu hakuna sehemu tumeombea decision or order, kwenye kifungu cha 8 hata kama kimekopwa hakiwezi kucocer maombi yetu.
Mahakama yenu ilishawahi kuiamulia hili kwenye kifungu 394 cha CPA, katika kesi ya Peter Michael Madeleka dhidi ya jamhuri.
Kutaja kitu fulani means exclusion ya kitu kingine, kitendo cha kifungu cha 8 kutaja findings and order means haijatuzuia kwa maana hiyo findings hapa haijazuiwa kwa maana hiyo tunachotaka kuiambia Mahakama yako ni kwamba ule ushahidi ulikataliwa kabla ya wakati wake.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa naomba niishie hapo kwenye hilo ili tusiende mbali kwa kuyasema hayo mtaona kwamba kesi ambazo mshitakiwa amewapitisha ni distinguishable kwenye mazingira yetu.
Hii kauli ya kwamba hatuna mamlaka ya kuomba Mahakama iitishe ‘Suo moto’ sisi tunasema mamlaka tunayo.
Katiba anasema naomba Mrema anisaidie anayo nyongeza.
Anasimama Wakili wa Serikali huyu anaitwa Job Mrema anakipara kama Mrema wa ubwabwani, sijui na yeye huwa anakunywa visungura kama mwenzake, anyway
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo July 3, 2026
Last time kwenye ya Uhaini dhidi ya Mhe. Lissu tuliishia part 224 so leo tunaendelea na -;
Part 225
Mheshimiwa Tundu Lissu anaingia ndani ya chumba cha mahakama, ukumbi namba 01 wa Mahakama Kuu.
Anaonekana mwenye tabasamu na furaha usoni kwake kama ilivyo siku zote.
Upande wa Jamhuri wapo kama kawaida yao
Inapigwa Court…..
Jopo la Majaji watatu wanaingia,
Kesi inatajwa
Anasimama Wakili wa Serikali anajitambulisha jina lake Ajuaye kisha anatambulisha Mawakili wenzake.
Jaji anaamuliza Mhe. Lissu kama yupo tayari
Mhe. Lissu anasema yuko tayari kuendelea.
Kama kawaida yao anasimama Wakili wa Serikali Katuga kuweka pingamizi.
Mhe. Lissu anapendekeza maombi yake ya sikilizwe kwanza ndo pingamizi lao lijibiwe.
Majaji wanasema tuanze kwanza kusikiliza PO, kisha taratibu nyingine zitafuata.
Anaanza Mhe. Lissu Waheshimiwa Majaji kesi hii inatokana na maombi namba 19065 ya mwaka 2025, Juu ya maombi ya kuongeza ushahidi katika muendelezo wa kesi, uamuzi wa tarehe 24 February 2026 wa Mahakama Kuu wa kukataa kuingizwa kwa ushahidi mpya.
Waheshimiwa Majaji uamuzi wa February 24, 2026 ni uamuzi mdogo, uamuzi ambao haujamaliza shauri na kwa mantiki hiyo kisheria kabisa haupaswi kukatiwa rufaa au pingamizi.
Waheshimiwa Majaji wa rufaa, Mahakama hii katika kesi ya Mkurugenzi wa Mashitaka dhidi ya Mohammed Mussa Ussi criminal appeal namba 521 ya mwaka 2023 Mahakama ikiwa imeketi Zanzibar ilisema msingi wa kukataza rufaa ama mrejesho (revision) ya jinai msingi wa hiyo hoja ni kifungu cha 8.2.d kutokana na marejeo ya mwaka 2023 mahakama hii ilisema uamuzi huo hauwezi kukatiwa rufaa kwani ni uamuzi usiomaliza shauri.
Anaendelea Mhe.Lissu
Kesi ambazo nimeziwasilisha mbele yenu waheshimiwa Majaji zinazungumzia uamuzi mdogo ni wa aina gani na uamuzi unaoweza kutolewa kama uamuzi wa mwisho unaoweza kuombewa revision ni wa aina gani.
Uamuzi unaomaliza kesi na kunyima haki za wadaawa ndiyo unaopaswa kukatiwa rufaa, uamuzi unaokuwa treated as the final order ndiyo unaomaliza haki za msingi za wadaawa lakini kama uamuzi haufanyi hivyo hauwezi kukatiwa rufaa.
Sasa waheshimiwa Majaji baada ya kuwapitisha kwenye kesi hizo nirudi kwenye hoja yangu ya msingi je uamuzi wa February 24 mwaka huu ulimaliza kesi hii?
Kama ni hivo ulimaliza kesi hii na kwamba Sasa hivi sina kesi ya uhaini basi hoja yangu haina msingi na maombi haya hayawezi kusikilizwa.
Hoja yangu waheshimiwa Majaji ni kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu wa February 24, 2026 haukumaliza kesi namba 19065/2025 na kwasababu haukumaliza maombi haya ya revision yanakatazwa kuletwa Mahakama ya Rufaa.
Anaendelea Mhe.Lissu
Waheshimiwa Majaji uamuzi huo unasema nini, ili tujue kama ulimaliza kesi lazima tuusome huo uamuzi unasema nini.?
Rulling yenyewe iko ukurasa wa 405-432, kwenye ukurasa wa 431 paragraph ya mwisho waheshimiwa Majaji mtaona Mahakama ilichokiamua.
Kilichokataliwa kupokelewa na Mahakama ni notice of additional substance of evidence, Mahakama Kuu haikusema kesi haitaendelea. Mahakama kuu ilitoa Mwongozo haikutoa uamuzi wa mwisho wa kesi, uamuzi wao ulikataa subodinate issue.
Waheshimiwa Majaji ushaidi mwingine huko kwenye maombi yenyewe yaliyoletwa. Mahakama inasema ilijadili na kukataa notice yao ya kuongeza ushahidi haisemi kesi ilifia hapo kutokana na uamuzi huo.
Mahakama imekata notice of additional substance of evidence, kwahiyo wanalalamikia uamuzi wa notice kukataliwa.
Jambo la pili ni Je mleta maombi anayo mamlaka ya kuiambia Mahakama itumie mamlaka yake ya kupitia kumbukumbu ili kuridhisha matakwa yake mwenyewe?
Jibu ni hapana hiyo siyo haki yao kisheria kwani wajibu wa kuangalia record ni wa mamlaka yenyewe.
Part 226 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
Sanamu kubwa ya Mchezaji Nyota wa soka duniani Lionel Messi limezinduliwa nchini Argentina na kuvutia hisia tofauti kutoka kwa Wananchi na Mashabiki wa soka.
Sanamu hiyo yenye urefu wa takribani Mita 26 hadi 27 imejengwa katika Mji wa Cutral Có, ulioko katika eneo la Patagonia.
Kwa mujibu wa taarifa, hii ni miongoni mwa Sanamu kubwa zaidi kuwahi kujengwa kumuenzi Messi duniani, na imewekwa kando ya barabara kuu inayopita eneo hilo.
Sanamu hiyo inamuonesha Messi akiwa amepiga magoti, huku akiashiria ushindi wa Kombe la Dunia, lakini kilichozua mjadala ni uwekaji wa kombe hilo ambalo limewekwa mbele kati ya miguu yake badala ya kuwa mikononi.
Baadhi ya mashabiki wamesema muundo huo haukuonyesha heshima ya kutosha, wakipendekeza kombe hilo lingekuwa mikononi mwa Messi kama ishara ya ushindi wake wa kihistoria.
Hata hivyo, wengine wameutetea muundo huo wakisema ni kazi ya kisanii inayolenga kuonyesha simulizi tofauti ya mafanikio yake.
Sanamu hiyo inaendelea kuvutia wageni wengi na kusambaa sana mitandaoni, huku mjadala ukiendelea kuhusu ubunifu wake.
#KitengeSports
🚨🇦🇷 Lionel Messi when asked how many World Cup goals he can reach: “I am tired now, I’m not thinking about that. I just want to enjoy the win with my teammates”.
Nina miaka takribani sita kwenye Ndoa sasa Baba yangu alibariki Uamuzi wangu nikiwa na miaka 22 tu, lakini katika miaka sita (6) hii ya ndoa nimegundua mambo kadhaa.
1- Ndoa yangu huyumba sana kipindi ambacho Mimi huwa nayumba yaani siketi katika mstari sahihi.
2- Ndoa yangu hustawi sana kipindi ambacho Mimi huwa nasimama imara kwenye mstari sahihi.
3- Mimi kama Baba wa Familia napaswa kuwa na mambo mengi lakini hayapaswi kuathiri familia yangu.
4- Naishi kwa kuamini Mimi sio Mkamilifu nina makosa na nakosea, ni sahihi kumwomba radhi Mke wangu napomkosea kwakuwa ni Ubinadamu, ni sahihi kuwaomba radhi Watoto wangu napowakosea kwakuwa ni Uungwana.
5- Hakuna Mwanamke Mkamilifu ila kila mmoja anapambana kufit kwenye Ndoa yake, tumetoka mazingira tofauti na Malezi tofauti hivyo kuelekezana na kustiriana huku tukisonga.
6- Talaka ni hatua ya mwisho sana ambayo sio baraka kwenye dini, sio sifa kwa Mtaliki wala Mtalikiwa na sio hatua njema kwa Wazazi wa pande zote mbili, hakuna kisichorekebishika kikitangulizwa na IBADA.
7- Kwenye sababu za KUOA haipaswi kuwa Makalio, Urembo ama sifa, hatuoi ili kuficha madhaifu bali tunaoa kwasababu tupo tayari kuingia kwenye darasa la furaha na huzuni lakini tutafika salama.
8- Ndoa ikileta baraka ya Watoto mtagundua tunaoana kwasababu ya Familia, kwasababu ya Watoto na hatupaswi kuwarithisha shida zetu sote tuishi na tusonge kwa ajili yao.
9- Ingali nimeoa Kijana najitahidi kutoleta Ujana kwenye Ndoa, Usela wa Masela kuja Maskani kila Wakati HAPANA, mapema kurudi home na kuchelewa kutoa taarifa ni MISINGI.
10- Mwalimu wa ndoa? Hayupo na hatotokea kwasababu kila mmoja ana Mtihani wake wenye maswali tofauti, jitahidi kujibu mtihani wako kwa mazingira yako naamini hivyo.
MWISHO, hakuna Mwalimu wa Mapenzi wala Ndoa, ni kudra za Mwenyezi Mungu katika kila kitu ukiweza hata kuvuka mwaka kwenye Ndoa basi shukuru Mungu, hii ni Ibada ina vita yake.
Mwenyezi Mungu awajalie kheri Wana Ndoa wote🙏 Taasisi yetu ya Migogoro hii unalala Kitanda kimoja na Adui yako na anakupikia unakula😀