Member of Tanzania Chamber of Mines.
Approved Mining Local Content Consultant II Procurement & Supply Chain || Risk Management ||
E-mail: [email protected]
🇹🇿 Tanzania continues to strengthen its position as a premier destination for responsible and strategic mining investment.✨️
President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan, together with the Minister of Minerals, Hon. Anthony Mavunde, today held discussions with executives from Perseus Mining Limited and Sotta Mining Corporation Limited at Chamwino State House in Dodoma.
The engagement reflects Tanzania’s continued commitment to creating a stable, transparent and investor-friendly environment that supports sustainable growth of the mining sector, value addition, job creation and long-term economic transformation.
Under the leadership of H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan, Tanzania’s mining sector continues to attract global confidence and strategic partnerships that contribute to national development and shared prosperity. ⛏️🌍
#Tanzania #Mining #Investment #Minerals #Africa #EconomicGrowth #Leadership #MiningIndustry #TanzaniaMining #StrategicPartnerships
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde kwenye picha na Ujumbe wa Kampuni ya Perseus Mining Limited na Sotta Minining Corporation Limited mara baada ya mazungumzo yao, Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 6 Mei, 2026.
🚨 OPPORTUNITY ALERT | NYANZAGA GOLD PROJECT – TANZANIA 🇹🇿
Sotta Mining Corporation Limited (a joint venture between Perseus Mining Limited and the Government of Tanzania) has officially opened an Expression of Interest (EOI) for the supply of KSB parts and consumables at the Nyanza Gold Project.
This is more than a supply opportunity, it’s a gateway to participate in one of Tanzania’s strategic gold developments within the Lake Victoria Gold Fields.
🔍 What’s at stake?
✅️ Long-term supply of genuine KSB components
✅️ Integration into a large-scale mining value chain
✅️ Opportunity to demonstrate technical capability & local content compliance
✅️ Strong preference for 100% Tanzanian-owned companies
⚙️ Key expectations:
✅️ Proven experience in mining sector supply chains
✅️ Ability to maintain reliable stock availability locally
✅️ Demonstrated HSE compliance and financial capacity
✅️ Capability to support end-to-end supply logistics
📅 Deadline:
13 April 2026
💡 Strategic insight:
This EOI signals a deliberate push toward local supplier empowerment and operational efficiency in Tanzania’s mining sector. Companies that combine technical credibility, compliance, and local presence will be strongly positioned.
📩 If your company operates within industrial supply, mining services, or engineering logistics, this is a call to step forward.
#MiningTanzania #LocalContent #SupplyChain #InvestmentOpportunity #GoldMining #PerseusMining #NyanzaProject #IndustrialSupply #AfricaMining
For the first time in Tanzania, East & Central Africa, unlocking a new era of value in Mbeya. 🇹🇿✨
A landmark milestone in the strategic minerals journey, positioning Tanzania at the forefront of global niobium production and industrial transformation.
#NiobiumTZ
#StrategicMinerals
#ChuiFerroniobium
#ChuiNiobium
Integrated Mining Technical Training (IMTT) - VETA MOSHI
The Veta Centre, Moshi. Inaugurated by the then President of Tanzania, Julius Nyerere on 3rd July 1984, remains to be one of the best facility.
Kudos to all involved.
#LocalContent
Executive Program on ESG Governance and Leadership - I will be Facilitating on the Role of Procurement and Supply Chain in ESG Governance.
Join us and be part of the Learning Process
#LocalContent
DKT. KIRUSWA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI MKATABA KATI YA STAMICO NA PLANTCOR
DKT. Biteko awataka wananchi wa Bukombe kuchangamkia fursa
Dkt. Mwasse Mkataba kati ya STAMICO na PLANTCOR umelenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati
Shigella amesema Geita imebarikiwa aina mbalimbali za madini
Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, ameshuhudia Hafla ya Utiaji Saini wa mkataba wa ushirikiano kati ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) na Kampuni ya Plantcor Mining and Plant Hire (Pty) Ltd kutoka Afrika Kusini kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa utafiti na uchimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo la Kigosi, Wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita.
Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kiruswa amesema uwekezaji huo unatarajiwa kufungua milango ya ajira kwa wananchi wa Bukombe na mkoa wa Geita kwa ujumla, kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani na kuongeza mapato ya Taifa.
Amesisitiza umuhimu wa kampuni husika kutekeleza wajibu wake kwa jamii (CSR) pamoja na kuhakikisha ushirikishwaji wa wananchi katika mnyororo wa thamani wa sekta ya madini kupitia sera ya Local Content.
Ameeleza kuwa baada ya kukamilika kwa utafiti wa kijiolojia, Plantcor itawasilisha taarifa za kina za maeneo yanayozunguka mradi wa Kigosi ili kuwawezesha wachimbaji wengine wenye leseni katika eneo hilo kunufaika na taarifa hizo kwa maendeleo ya shughuli zao.
Aidha, Dkt. Kiruswa ameitaka Menejimenti ya STAMICO kushirikiana kwa karibu na Plantcor ili kuhakikisha mradi unasimamiwa kwa weledi, uwazi na kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa. Vilevile, amewataka wawekezaji hao kutimiza ahadi zote za uwekezaji, uhamishaji wa teknolojia na kuzingatia Sheria za nchi ili mradi huo uwe mfano bora wa ubia kati ya Serikali na Sekta Binafsi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya STAMICO, Balozi Simon Sirro, amesema utiaji saini wa mkataba huo ni ishara ya kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji nchini, akibainisha kuwa ubia huo unatekelezwa kwa mujibu wa Sheria huku maslahi ya wananchi yakilindwa kwa uwazi.
Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dkt. Venance Mwasse, amesema mkataba huo unalenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika utafiti na uchimbaji wa dhahabu Kigosi. Ameongeza kuwa STAMICO inaendelea kuwa lango la kuvutia mitaji na teknolojia za kisasa kwa manufaa ya Taifa.
Amesema ushirikiano huo utawezesha kufanyika kwa tafiti za anga (airborne survey) zitakazohusisha matumizi ya ndege maalum kwa ajili ya uchunguzi wa kijiolojia, si tu katika eneo la STAMICO bali pia maeneo mengine ya Kigosi, hatua itakayowanufaisha wachimbaji wengi zaidi kupata taarifazakijiolojiakatika maeneo yao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Plantcor, Joseph Wilmans, amesema kampuni hiyo ina uzoefu wa zaidi ya miongo miwili katika shughuli za madini kuanzia utafiti, uchimbaji, uchenjuaji hadi usambazaji wa bidhaa sokoni.
Amebainisha kuwa kampuni imeleta utaalamu wa kiteknolojia na kifedha utakaosaidia kuongeza uzalishaji na ajira kwa Watanzania, huku akiishukuru Serikali kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini.
Sambamba na hao, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigella, amesema mkoa huo umebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi za madini, na akamshukuru Rais kwa uamuzi wa kuufungua mradi wa Kigosi, hatua aliyosema imeendelea kuimarisha uchumi wa mkoa huo.
💛 Activity is in full swing at @buckreefgold !
Cut 01 is clearing drill pads while Cut 02 is keeping the load and haul operations moving efficiently. Progress is strong as we kick off the year with momentum! 🚜⛏️
#TRXGold#OnSiteatBuckreef#MiningUpdate#GoldMining
Serikali Yaainisha Orodha ya Bidhaa na Huduma za Migodini Ambazo Hazipaswi kufanywa na Wageni
▪️Ni utekelezaji wa maelekezo ya Mh Rais Samia juu ya ushiriki wa watanzania kwenye sekta ya madini
▪️Ni kupitia Marekebisho ya Kanuni ya Ushirikishwaji Watanzania Sekta ya Madini
▪️Manunuzi na Bidhaa Migodini Yafikia Shilingi Trilioni 5 mwaka 2024
▪️Waziri Mavunde ataka Sekta Binafsi kuchangamkia fursa
📍 Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Madini imetangaza rasmi orodha ya Huduma na Bidhaa 20 zinazopaswa kutolewa Migodini kupitia kampuni zinazomilikiwa na watanzania kwa asilimia 100 ikilenga kuongeza wigo wa ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu kwenye mnyororo mzimawa sekta ya madini.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde Januari 5, 2025 jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari na kueleza kuwa, hatua hiyo imefanyika baada ya kufanywa marekebisho ya Kanuni za Ushirikishwaji wa Watanzania kwenye Sekta ya Madini za Mwaka 2018.
‘’Kwa awamu ya kwanza tarehe 14 Novemba, 2025 Tume ya Madini ilitangaza orodha ya bidhaa na huduma zinazotakiwa kutolewa na kampuni zinazomilikiwa na kampuni za kitanzania kwa asilimia 100, ambapo kwa mara ya kwanza Tume ya Madini itatatangaza kupitia Kanuni 13A,’’ amesema Waziri Mavunde.
Akizungumzia manunuzi ya huduma na bidhaa kwa kampuni za kitanzania amesema yameongezeka kutoka kiasi cha Shilingi trilioni 1.85 kati ya manunuzi ya huduma na bidhaa za jumla ya kiasi cha Shilingi trilioni 3.01 sawa na asilimia 62 kwa mwaka 2018 hadi kufikia Shilingi trilioni 4.41 ambayo ni sawa na asilimia 88 ya kiasi cha Shilingi trilioni 5.00 ya manunuzi yote yaliyofanyika mwaka 2024.
Kwa upande wa ajira kwenye miradi ya madini, amesema kumeshuhudiwa ongezeko la ajira kwa watanzania kutoka ajira 6,668 kati ya ajira 7,003 sawa na asilimia 95 kwa mwaka 2018 hadi kufikia ajira 18,853 kati ya ajira 19,356 sawa na asilimia 97 kufikia Desemba 2024.
‘’katika nafasi zinazohitaji kupata uzoefu kutokana na kukua kwa teknolojia duniani, kumekuwa na utaratibu wa kisheria wa urithishwaji wa Watanzania kwa nafasi zinazoshikiliwa na Wataalamu wa Kigeni,’’ na kutolea mfano wa mgodi wa dhahabu wa North Mara unaomilikiwa na Kampuni ya Twiga Minerals Corporation (Barrick Gold) ambapo nafasi zote za juu za uongozi zinashikiliwa na Watanzania kwa asilimia 100.
Samamba na hayo, amesema Serikali inaendelea kufungua wigo kwa ushiriki wa watanzania katika sekta ya madini na kuongeza manufaa ya rasilimali madini kwa kutenga eneo maalum la uwekezaji la ulipokuwa Mgodi wa uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu la Buzwagi lenye ukubwa wa ekari 1331, kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kuzalisha bidhaa za migodini na kusema tayari viwanda sita vimekwisha jengwa huku wamiliki wa viwanda 15 wakionesha nia ya kujenga viwanda katika eneo hilo.
Waziri Mavunde ameitaka sekta binafsi nchini Tanzania kuchangamkia fursa ya usambazaji wa bidhaa na utoaji wa huduma migodini ili kuhakikisha fedha kiasi kikubwa inabaki nchini Tanzania na kuchochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
Amewasisitiza wawekezaji wote kuzingatia Sheria za madini na utekelezaji wa Kanuni za Ushirikishwaji Watanzania kwenye sekta ya madini sambambamba na kuwataka watanzania kuchangamkia fursa zilizopo katika miradi ya madini ili kukabiliana na changamoto za ajira kwa manufaa ya mtu mmoja mmoja na manufaa ya taifa.
Vision 2030:Madini ni Maisha na Utajiri
Via @KoreaTimescokr
POSCO Future M will supply secondary battery materials to a major automobile company for up to 10yrs from 2027, the deal worth 671 billion won ($470 million).
POSCO is a strategic alliance partner of #BKT, working towards developing the Mahenge #Graphite Project.
https://t.co/f24LRWpWOv
Via @MiningNewsNet
$BKT.AX has commenced early works for its 84%-owned Mahenge #graphite project in Tanzania, with the program to support a rapid ramp-up of construction activity once #BKT is fully funded and then makes a final investment decision.
https://t.co/b8dm69FqWz
#ASXNews
$BKT.AX advises that following a formal groundbreaking ceremony held at the Mahenge #Graphite Project on 9 October 2025, the Early Works program for the Project has officially started. The Hon. Anthony Mavunde officiated the event.
Read: https://t.co/pWDD1c6Nes
KIWANDA CHA KUSAFISHA DHAHABU CHUNYA MBIONI, SERIKALI YATIMIZA AHADI*
Ni kupitia Kampuni ya Kitanzania ya Giant Equipment and Mashine’s Limited
Kina uwezo wa Kusafisha kilo 20 za Dhahabu kwa Siku
Chunya
Chunya, Mkoa wa Pili wa Kimadini kwa uzalishaji wa dhahabu nchini baada ya Geita, imepiga hatua kubwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Kiwanda cha Kusafisha Dhahabu cha Giant Equipment and Machine’s Limited. Kiwanda hiki kina uwezo wa kusafisha kilo 20 za dhahabu kwa siku kwa usafi (purity) wa asilimia 99.9 na kiko mbioni kuanza uzalishaji rasmi, baada ya kukamilika kwa baadhi ya taratibu za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) .
Akizungumza katika mahojiano maalum na timu ya Madini Diary kutoka Wizara ya Madini Oktoba 8, 2025, Meneja Uendeshaji wa Kampuni hiyo Hassan Pazi amesema tayari majaribio ya kusafisha dhahabu kiwandani hapo yamefanyika kwa awamu tatu tofauti na zote zimetoa matokeo ya kiwango cha kusafisha hadi asilimia 99.9, jambo linaloashiria kuwa dhahabu inayosafishwa na kiwanda hicho inakidhi vigezo vya kununuliwa na BoT kutumika kama amana ya Serikali na kusafirishwa nje.
‘’Awamu zote zilionesha purity ya asilimia 99.9 hii ni kiashiria tosha kwamba mashine zetu ziko vizuri na tumefikia lengo letu hivyo, wachimbaji wawe tayari muda si mrefu tutaanza rasmi kusafisha dhahabu hapa Chunya. Kwa sasa zipo taratibu tunazikamilisha na BoT,’’ amesema Pazi.
Ameongeza kwamba, hatua ya Chunya kuanza kusafisha dhahabu itasaidia kupunguza adha ya wachimbaji na wafanyabiashara kusafiri umbali mrefu hadi katika mikoa ya Dodoma, Geita na Mwanza kwa ajili ya kupata huduma hiyo.
Kutokana na hatua iliyofikiwa na kampuni hiyo, imeipongeza Serikali kwa kutoa eneo ambalo limewezesha kujengwa kwa kiwanda hicho ikiwemo kutembelewa mara kwa mara na wataalam kwa ajili ya ushauri na maelekezo yaliyowezsha kukamilisha taratibu zote.
Akizungumzia kuhusu ajira, Pazi amesema kiwanda hicho kitaendeshwa kwa asilimia 100 na watanzania na kwamba watalamu wa kitanzania walihusika katika hatua zote tangu ujenzi kikihusisha wahandisi, watoa huduma na wajenzi hadi kufikia hatua ya kuelekea kwenye uzalishaji.
Mbali na kusafisha dhahabu, kampuni hiyo inamiliki kiwanda cha kuchenjua dhahabu chenye mitambo ya uwezo wa kubeba kilo 650 za kaboni kila mmoja. Pia, kampuni hiyo inajihusisha na biashara ya kuuza kemikali za aina zote, vifaa kinga na kudhamini wachimbaji wadogo.
Kukamilika kwa kiwanda hicho kunaendelea kuonesha dhamira ya dhati ya Serikali ya kuongeza thamani ya madini hapa nchini na kutekeleza mikakati ya sekta hiyo kwa vitendo. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, alikielezea kiwanda hicho bungeni katika hotuba ya bajeti ya mwaka 2025/26 na sasa, ahadi hizo zimetia mwanzoni tu mwa robo ya pili ya mwaka.
Mbali na kuongeza ajira na kukuza uchumi wa Chunya, Serikali itanufaika kupitia kodi na tozo mbalimbali sambamba na Halmashauri ya Wilaya ambayo itanufaika moja kwa moja na mapato yatokanayo na shughuli za kiwanda.
Kukamilika kwa kiwanda hichi kunafanya idadi ya viwanda vya kusafisha dhahabu nchini kufikia vinane.
#Uongezaji Thamani Madini
#Value Addition
Vision 2030: Madini ni Maisha na Utajiri
#Madini ni Ajira,Uchumi na Maendeleo