Nakutakia Christimas Njema wewe pamoja na familia yako, barikiwa na mwimbaji Frank na Musabwa kupitia Cover ya wimbo wa Uniondolee Majivuno ulioimbwa na nguli wa muziki wa injili Rose Muhando. SALA na KAZI
Wakati unapambana kutafuta Maisha kuna watu wataku "Block" kwenye simu zao wakidhani unawasumbua, kuna watu hawatapokea simu zako wala jumbe zako unazowatumia wakidhani unawasumbua, kuna wengine watakuwa na chuki nawe kila wakikuona wakidhani unawasumbua. SALA na KAZI
Baada ya majukumu ya kikazi Mjini Kigali nimelazimika kuzuru katika uwanja mkubwa wa michezo nchini Rwanda wa Amahoro wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 45,508 kwa wakati moja ili kujionea mechi ya kirafiki kati ya Young Africans dhidi ya Rayon Sports ya Rwanda. SALA na KAZI
Nimezuru eneo la mpakani kati ya DRC na Rwanda tawi la magharibi la Bonde la Ufa kujionea maeneo Oevu ya ziwa Kivu katika uhifadhi wa Uchumi na Utalii ni moja kati ya Maziwa makubwa Afrika, Maji yake yanatoka kupitia mto Ruzizi unaoelekea kusini hadi ziwa Tanganyika. SALA na KAZI
Nimetembelea makao makuu ya Mikoa 5 ya Rwanda ambayo ni Kigali, Nyanza, Kibuye, Musanze na Rwamagana, Rwanda unaweza kutembea nchi nzima bila kukutana na aina yoyote ya uchafu umetupwa ama ulizagaa hovyo hovyo. Ni eneo dogo lenye mkakati makini wa kilimo pia. SALA na KAZI
Nimezuru kijiji cha Nyamashekhe kilichopo mkoa wa Magharibi nchini Rwanda ambapo kumekithiri utamaduni wa wanawake kulipa pesa kwa mwanaume ili waolewe, ni utamaduni wa kipekee ukifika kwetu Tz hakika utaanza na ndugu yangu Iddy Mwema amenihakikishia ana shauku kubwa.SALA na KAZI
Una watu wengi wanakuja na kupita kwenye maisha yako, wakiondoka unasikitika, unaumia. Sikiliza utaishi maisha ya raha sana kama utakubali kuachilia baadhi ya mambo, ruhusu marafiki wapite, wacha waende, kuachilia na kukubali wapite ina imarisha amani ya nafsi. SALA na KAZI
Dar es salaam...!
Ndoa yako ikawe na heri nyingi mdogo wangu Happiness Nyamhandi hiki ni chama chenye baraka nyingi, Mungu amekupa mume kayaishi maandiko matakatifu na utakatifu wa ndoa ukatimie. SALA na KAZI
Nimekuwa na wasaa mzuri kuzungumza na Mhe Dkt Ritta Kabati ambaye ni Mbunge wa Vitimaalum Mkoa wa Iringa kuhusu mtazamo wake kuelekea uchaguzi mkuu, amenihakikishia bado yupo sana nami nimemtakia kila la heri kuelekea kinyang'anyiro chake na eneo aliloamua kugombea. SALA na KAZI
Nimekuwa na wasaa mzuri kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Innocent Bashungwa ameniambia Ukimchukia mtu usidhani atateseka, Mungu hatoki kijijini kwenu wala hamna vinasaba vyovyote. Mungu ni wa wote anatoa riziki kwa mipaka na matakwa yake. SALA na KAZI
Dar es salaam...!
Kama hutaki kuamini endelea kushupaza shingo lakini jambo kubwa la msingi unapaswa kufahamu Kabla ya kuwa jiwe kuu la Pembeni sifa yake kubwa ilikuwa ni kukataliwa na waashi na ndipo baadae likawa jiwe kuu la pembeni. SALA na KAZI
Teteatete na Mtu bingwa, Mwamba, Mwalimu na nguli katika sekta ya habari ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Ndg Gerson Msigwa, Mimi ni mwanafunzi kwake naendelea kuchota Weledi na nidhamu katika uwajibikaji.SALA na KAZI
Nizungumza na Eng Lutengano Mwandambo Mhandisi Mkazi Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere pia Mhandisi Mkuu wa TECU, hakika nimejifunza namna uzalendo mkubwa uliotumika katika usimamizi wa mradi huo ambalo kwa sasa mradi umekamilika kwa 100% na Trilioni 6.4 zimetumika.SALA na KAZI
Kiomboi, Iramba-Singida...!
Nimejiandikisha ikiwa ni sehemu ya kuboresha taarifa zangu kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura katika kituo cha Kihohede mjini Kiomboi-Iramba, niwasihi watanzania wenzangu kuhakikisha sote tunajiandikisha ili tutumie haki yetu kikatiba. SALA na KAZI
Tete Atete na Mbunge wa Jimbo la Ikungi Mashariki Mhe Miraji Mtaturu Bungeni Jijini Dodoma naendelea kupokea pongezi hakika nimepata heshima kubwa sana kwa wabunge wetu.
Nimepata heshima kupongezwa na Waziri wa Fedha Dkt Mwigulu Nchemba baada ya ushindi wa Tuzo 2 za SAMIA KALAMU AWARDS, Dkt Nchemba ni mbunge wangu wa jimbo la Iramba Mashariki na tunajivunia yeye. Ingekuwa ni amri yangu na sio Demokrasia ningesema mitano tena kwake. SALA na KAZI
Nimezungumza na Mtu bingwa Prof Carolyne Nombo Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, mtaalamu wa masuala ya Maendeleo vijijini, Jinsia, Usalama wa chakula, Sera za umma, na mbinu za utafiti wa kimaendeleo. SALA na KAZI
Asanteni sana Wabunge kwa heshima mliyonipa kwa shangwe kubwa baada ya Mwenyekiti wa Bunge Mhe Najma kunitambulisha Bungeni baada ya ushindi wa Tuzo mbili za SAMIA KALAMU AWARDS zilizotolewa hivi karibuni Jijini Dar es salaam.