Nikisikia hizi habari za watu kutekwa najisikia vibaya sana. Watu zaidi ya saba mnakwenda kumteka kijana asiyekuwa hatari kwa usalama wa nchi nyumbani kwao mbele ya familia yake? Mnaelewa kweli trauma mnayotengeneza kwa hizi familia? Mnajua chuki mnayoipandikiza kwa jamii? Watu waliomteka Damour Nyakairo, @Ninja_Damour muachieni huko mafichoni aendelee na maisha yake. Hatutaki kuona kijana mwingine anatekwa na kupotezwa. Hatuwezi wote kufikiri na kuwaza sawa. Taifa letu litajengwa kwa msigano wa mawazo. #FreeNinjaDamour
Kuna kazi mtu unafanya.
Zinakupa pesa.
Ila,
Sio kazi ambazo ni guarantee ya maisha ya leo, kesho na vizazi vyako.
Ni PATH ya kukutoa sehemu moja kwenda nyingine.
Mfano.
Udereva wa magari yote.
Ujenzi
Boda
Agent
Dalali
Fundi wa furniture
Fundi wa AC
Uchomeleaji
Freelancing
Mawawinga
Na kazi nyingi au zote zinazokupa pesa ndogo ndogo ya kila siku.
Fikiria madereva ambao hawakujiandaa kupokea uzee wana hali gani.
Fikiria na hao wote katika uzee watakuwa na hali gani wanapo relax.
Boda mzee?
Agent wa magari mzee?
Badala yake.
Ile ni fursa ya kuandaa maisha bora ya baadae nje ya hiyo kazi.
Kwake na vizazi vyake.
Changamoto ni kwamba.
Katika umri wa ujana ambapo hizo fursa zinawapa pesa.
Watu tuna relax na kutumia pesa katika mambo ya ajabu kama.
Pombe.
Kubadili wanawake.
Kusomesha na
Kuzaa zaa among others.
Ndiomana baadae tunapata hawa wazee bodaboda.
Wazee content creator.
Wazee wa vijiweni wanaosumbua watoto wao wanaopambania familia zao.
Baadae inakuwa lawama kwa ndugu wenye kipato mpaka kugombania mirathi na mambo kama hayo.
Lengo la hii tweet ni.
Ijue kazi yako na uifikirie in 30 years to come itaendelea kukupa pesa? Kama hamna basi usi relax bro.
Normalize kutolidhika hatakama sisi wote tutakufa. Angalia watoto wako wataishije baada ya wewe kutokuwepo.
Angalia katika miaka yako 50 utakuwa umeshika nini cha kukupa pesa bila wewe kushughulika kwa nguvu.
Fanya kazi yako kama path ya kukupa kikubwa zaidi.
Save pesa kwa malengo ya kufanya kitu kikubwa zaidi.
Duka la simu linaweza kufa.
U winga unaisha.
Udalali unaisha.
U content creator unaisha
Kuwa boda au bajaji kuna mwisho.
Kuwa dereva kuna mwisho.
Sasa baada ya hapo utakuwaje? Hizo kazi zitaisha ukiwa umejenga mazingira salama bila wewe kushugulika?
Utakuwa na hardware kubwa watoto wako waendeleze?
Utakuwa na nyumba nyingi?
Utaendelea kuwa content creator?
Utakuwa na lodge nyingi?
Utakuwa ume diversify assets zako?
Pambana sasa bila kuchoka huku ukijiweka bora kwaajili ya kesho.
KULA UJANA VIBAYA UPATE TABU KUMEZA UZEE.
Hicho CHUMA na hizo nati ndio vilikuwa TAYA yangu kwa siku 646.
Hii ilikuwa Operation iliyokuwa inaniwazisha sana akili yangu kwa muda mrefu.
NAMSHUKURU MUNGU HILI GUMU LIMEPITA-JAPO NIMEPOTEZA MENO YANGU MAWILI.
Kwangu hii bado ni nafasi ya upendeleo MUNGU anaendelea kunipa.
Asubuhi nyingine kama vijana tunakumbushana kwa uzuri tu.
Mwanaume unaehisi unapendwa sana na mwanamke mwenye mtoto/watoto huku Baba wa kids yupo unajidanganya.
Pengine bila kuwa na hao watoto basi wewe usingempata kabisa.
Yuko na wewe kwasababu amepungukiwa options.
Yaani, you the best thing she can do kwa muda huo, bila kuwa na mtoto asingekupa hiyo nafasi hata kwa bahati mbaya.
Unafanywa last option na unachekelea, kazi kwako.
Mwanamke amekuwa aki'fuck na wazee wako twice as old ili avimbe mjini kwa pesa anazopata in her 23s.
Then wewe uje ukutane nae in her 28+ ufanye kumpenda kisa mauno anayokupa uoe na kuoa.
Enyewe past yake ni muhimu na kuoa umri ukiwa umeenda sana should not be intertained.
If you must take her kuwa makini na usiwe mtu wa kumzingatia sana otherwise trauma zitakuuwa.
Mwanamke aolewe kutoka kwao, hawa wapangaji wasio na kazi ya kueleweka mjini ni stress.
Imagine being a wife.
Ufue nguo za watoto na mume
Upike asubuhi, mchana na jioni
Udeki nyumba
Utandike ma vitanda
Uhakikishe maji yamo ndani and likes.
Afu mme akimbie majukumu ya kuleta ka kitu mezani + madharau + awe na wanawake nje na anakuonyeshea wazi.
Hapo unatimiza hayo majukumu halafu ukete na ka kitu mezani tena mwanamke.
Respect your wife man
Ladies poleni🥲
Wanawake ni watu ambao wako very direct kukuonyesha madharau na jinsi gani hathamini hizo calls na sms zako kama hakupendi.
Usiforce any mawasiliano na mwanamke ambae amesha onyesha dalili zote za kuku-ignore
Withdrawal u'r attention futa nàmba then ishi maisha yako bro.
Mwanaume Ukioa manzi mnyenyekevu kutoka kwenye familia duni au vyovyote vile ambaye pia sio bikira,
Tena umelipia posa au bride price.
Basi umekula loss kwa kuwa cheated kama mwanaume hasa kama wewe una mafanikio ambayo umeyapambania kwa muda mrefu.
Urembo wake hauwezi kufidia ukweli kwamba wanaume waliokutangulia walipata kilicho bora kwake bure.
Cha kusikitisha ni kwamba wewe umebidi ulipie makombo na mabaki yao.
Mdude Mpaluka Nyagali Polisi makao makuu waliunda mpaka Kamati kuchunguza mpaka sasa kimyaa japo afisa wao alitajwa bayana.
Mzee Kibao uchunguzi unaendelea,Soka na wenzake Mahakama ikaamuru Polisi wa chunguze mpaka leo kimyaa labada bado wanachunguza amri ya mahakama ,
soka na wenzake uchunguzi unaendelea?! Banjo katekwa na kuuwawa eneo lenye vifaa saidizi na kuzungukwa na ulinzi pale Arusha Uchunguzi unaendelea?!
Humphrey Polepole tunasikia mpaka baadhi ya Maafisa walirudi kuvunja gari lake na kuondoka na nyaraka...uchunguzi unaendelea
Namna pekee na sahihi ya kupata majawabu kuhusu utendaji wa polisi na vitendo vya utekaji ni kulichunguza Jeshi la Polisi.
Uchunguzi huru,Jumuishi na wakimataifa utategua kitenda wili cha mtekaji na muwezeshaji wa utekaji.
HAKI,UKWELI NA UWAJIBIKIJA UTALIPONYA TAIFA....siyo maombi ya kidini ya kisanii wala maridhiano ya jumla jumla na ya hadaa .
Zamu hii hatutakubali tena kupelekwa machinjoni kama kondoo wa kafara.
BAK MWABUKUSI.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 219
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross Examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Coplo Amani.: mimi sijalisema tu kama wewe umelisema basi ndio umesema.
Mhe. Lissu: Ni kweli kwamba P3 alikwambia kuwa ni mwanachama wa CHADEMA, kweli au si kweli
Coplo Amani : sio kweli
Mhe. Lissu: Wewe ndio uliandika maelezo yake kielelezo D12
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Sasa ngoja nikusomee… “mimi pia ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA” kweli si kweli.
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako uliyasema hayo
Coplo Amani : sikuyasema
Mhe. Lissu: Alikuonyesha kadi yake cha chama
Coplo Amani : sikutaka anionyeshe
Mhe. Lissu: alikwambia wafuasi wa chadema wana alama gani?
Coplo Amani : sikumuuliza mm
Mhe. Lissu: ndo maana nasema huyu ni askari wa kitengo cha intelijensi halafu mnasema ni shahidi.
Mhe. Lissu: Turudi kwa Inspekta Jorum, ni kweli polisi inapopokea watu waliofanya uhalifu , Polisi wanafungua investigation register?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waelezze majaji kama kwenye maelezo yako polisi walifungua investigation register
Shahidi: sijui
Mhe. Lissu: Waeleze majaji baada ya maafa yote hayo ya October 29 kama mmemchukulia hatua yoyote huyu baada ya kusema atapiga watu mawe?
Coplo Amani: Simfahamu chochote kuhusu swali lako
Mhe. Lissu: inaingia akilini hii
Coplo Amani : Mimi sifahamu chochote kwa kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unajua mashahidi wote wa kificho walisema waliona hiyo video yangu maarufu tarehe 4 april
Coplo Amani : Mimi sio mpelelezi wa mafile yote
Mhe. Lissu: Na unahabari wote waliokuja hapa ni boda boda na machinga hakuna afisa wa serikali au n.k
Coplo Amani : sina habari
Mhe. Lissu: Ulipomuachilia P3 kwa dhamana ulichukua hatua gani kuhakikisha aendelei na kupiga watu mawe na uasi?
Coplo Amani : sikupewa hilo jukumu
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji mimi sina maswali ya ziada.
Serikali: Kwa leo tulikua na shahidi huyu tu mmoja, tunaomba ahirisho kwasababu hali ya hewa ya Dar es salaam imebadilika na zimebaki dakika 20.
Kwasababu za kiusalama tunaomba ahirisho hadi siku ya Jumatatu ili tuje kuendelea kusikiliza juu ya notice tuliyoileta
Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji kwa dakika 20 kwangu si haba, mimi ninaomba hizi dakika 20 kwasababu nilishasema nina mapingamizi, naomba niongee juu ya hayo leo ili tusiathiri muda wa mashahidi wengine Jumatatu.
Naomba nipate hizi dakika 20 kwasababu mimi niliyepo Gerezani ndiye ninayepata shida, kwahiyo naomba tutumie hizi dakika jambo lifanyike.
Wakili wa Serikali: Waheshimiwa sisi tunaomba ahirisho lakin vilevile kama mnavyojua dini zote mbili tupo kwenye mfungo kwahiyo tunaomba ahirisho.
Lakini vilevile PO yake haijasajiliwa bado kwahiyo kama ataweza kuisajili na kuisikiliza basi aisajili na sisi tupewe nafasi ya kuiona ili tu-submit
Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji sikutarajia kwamba hili litakua na kubishana namna hii, nililetewa hii notice jana na nikatoa notice ya mdomo kwamba naipinga tena immediately nilipopatiwa tu notice hii.
Naijua sheria, sasa wanaposema tuahirishe ili niendelee kukaa gerezani ni sawa tukutane Jumatatu ili tuzungumzie PO yangu niliyoileta jana.
Na jana nilisema kabisa PO ni ya kisheria na itaenda na kifungu icho icho cha 308(1) cha CPA, mimi nakaa gerezani kwasababu ya michezo hii mnayoleta mawakili wa serikali kila siku.
Jaji Ndunguru anasema shauri litaendelea siku ya Jumatatu, tunatarajia serikali mlete mashahidi, tutaanza na hoja ya notice, tukimaliza tutaendelea na mashahidi wengine.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 203
Mhe. Lissu anaendelea na Cross Examination,
Jaji Ndunguru: upande wa mashitaka.
Mkude: No objection.
Jaji Ndunguru : turejee kifungu 194 cha CPA.
Mkude: kifungu cha 194 kwa ujumla wake ni kuhusu protection ya ushahidi, kwa sababu shahidi au mshitakiwa anaweza akaomba impeachment, pale anapoomba shahidi apewe kielelezo hivo tunaweza kuendelea mheshimiwa Jaji.
Mhe.Lissu: Iko hivyo waheshimiwa Majaji, sikuwa nataka kuona jina lake kwenye kielelezo hicho bali nataka asome maelezo yake.
Mhe.Lissu: kwa hiyo shahidi ulitaka kuficha ukweli mahakamani.
Shahidi wa kificho P3 : hapana.
Mhe.Lissu: mbona haukusoma kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA na umeiandika kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi wa CHADEMA labda askari aliyeandika maelezo yangu alikosea.
Mhe.Lissu unaidanganya mahakama, soma kama ilivoandikwa.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi/ mwanachama wa CHADEMA.
Mhe.Lissu: Sasa ulikuwa unaficha nini. Shahidi swali langu la pili kwenye maelezo yako umesema kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Sasa waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Shahidi wa kificho P3 : kongamano hilo halikufanikiwa.
Mhe.Lissu: hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Mhe.Lissu: shahidi umesema kwa bahati mbaya au nzuri kongamano hilo halikufanyika lilizuiliwa na serikali kweli au si kweli.
Shahidi wa kificho P3 : kweli.
Mhe.Lissu: wewe mfuasi wa CHADEMA kongamano la CHADEMA shughuli halali ya chama kuzuiliwa kwako ni bahati nzuri.
Shahidi wa kificho P3: sijui, mimi sielewei
Mhe.Lissu: ndiyo maana nikakuuliza tutajuaje kama wewe siyo pandikizi.
Shahidi wa kificho P3 : hilo swali nimeshalijibu tuendelee.
Mhe: Lissu: usijali tutaendelea kwenye maelezo yako ya Leo umesema ulikuwa na simu, Sasa kwenye hayo maelezo yako ya Polisi kuna sehemu uliandika kama ulikuwa na simu.
Shahidi wa kificho P3 : haipo.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua au haujui kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia compyuta.
Shahidi wa kificho P3 : sijui, mimi sina utaalamu huo wa kutumia compyuta.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia Television.
Shahidi wa kificho P3 : utaalamu huo sina.
Mhe.Lissu: unajua kama unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia tablet.
Shahidi wa kificho P3 : sijui huo utaalamu.
Mhe.Lissu: Kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa ulikuwa na simu
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe.Lissu: kwenye maelezo yako umesema uliyasikia maneno yangu kupitia video YouTube, kuna mashahidi wengine wamesema video hiyo ilikuwa na masaa 3 na madakika, waeleze waheshimiwa Majaji kama kuna sehemu umeandika video hiyo ilikuwa na muda gani.
Shahidi wa kificho P3 : hakuna
Mhe.Lissu: umesema umemfahamu mheshimiwa Lissu kupitia mitandao ya kijamii. Waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako umeandika hilo jambo.
Shahidi wa kificho P3 : hapana hayapo.
Mhe.Lissu: umesema mwezi march 2025 ulihudhuria mkutano uliohutubiwa na Mheshimiwa Tundu Lissu katika viwanja vya Ruanda nzovwe, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3: hayapo
Mhe.Lissu: umesema wakati ukiwahamasisha vijana wenzako hapo kijiweni alikuja mtu aliyejitambulisha kuwa ni Askari Polisi na kukuita pembeni kwamba njoo tuongee, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : napitia kidogo
Mhe.Lissu: haujapaona hadi mwishoni kwenye paragraph ya mwisho.
Shahidi wa kificho P3 : naomba nikusomee, alikuja mtu aliyejitambulisha ni Askari Polisi.
Mhe.Lissu: swali langu ni kwamba hayo maneno akaniita pembeni akaniambia njoo tuongee, hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Part 204 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 195
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi
Mhe. Lissu: Kwanini umepewa Jina la P7?
Shahidi wa kificho P7 : Kwasababu ya usalama wangu.
Mhe. Lissu: Si umesema hakuna aliyekutishia.
Shahidi wa kificho P7 : Ndio hivyo sasa.
Mhe. Lissu: Sina Maswali mengine.
Jaji: Karibu upande wa Serikali kwa Re Examination.
Wakili wa Serikali: Hatuna maswali kwa shahidi huyu.
Upande wa Serikali walisema wana shahidi mmoja tu kwahiyo kesi itaendelea kesho saa tatu asubuhi bila shaka.
Majaji wanaandika kidogo pale mbele.
Wakili wa Serikali: Renatus Mkude anasimama anasema kama tulivyosema asubuhi naomba tuahirishe hadi kesho asubuhi.
Jaji: Tafadhali tukutane hiyo Kesho Tarehe 19 saa tatu asubuhi.
Inapigwa high court
Watu wote tunasimama,
Majaji wanaondoka,
Watu wanaanza kutawanyika.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 189
Wakili wa Serikali anaendelea kumuongoza shahidi wa kificho P4
Wakili: Nini kingine?
Shahidi wa kificho P4 : Tulivyoenda kuripoti Tarehe 17/04 tuliambiwa tusubiri tuandikwe maelezo, nikaandikwa hayo maelezo.
Wakili: Unamfahamuje huyo Tundu Lissu?
Shahidi wa kificho P4 : Namtambua kama Mwanasiasa Mkubwa kwenye hii Nchi.
Wakili wa Serikali Winiwa Kasawa anasema Waheshimiwa Majaji ni hayo tu.
Jaji Ndunguru: Maswali ya Dodoso Karibu Mshitakiwa.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi jibu maswali kama hujui sema hujui sema najua kama unajua na kama umesahau sema nimesahau.
Mhe. Lissu: Umesema unakaa Arusha?
Shahidi wa kificho P4 : Kweli
Mhe. Lissu: Wambie Majaji umekuja Dar es salaam lini?
Shahidi wa kificho P4 : Leo nina siku ya pili.
Mhe. Lissu: kwahiyo umekuja Jumapili ya juzi?
Shahidi wa kificho P4: Ndio.
Mhe. Lissu: Nani alikwambia uje Dar es salaam
Shahidi wa kificho P4 : Hiyo nashindwa kusema hapa.
Mhe. Lissu: Utasema tu. Mimi sikuoni na watu hawakuoni. Wambie majaji ndio wanaokuona pekee kuwa nani alikwambia uje Dar es salaam
Shahidi wa kificho P4 : Nilipigiwa simu.
Mhe. Lissu: Na nani alikupigia simu.
Shahidi wa kificho P4 : Mtu alijitambulisha kuwa ni Wakili wa Serikali.
Mhe. Lissu: Alikwambia jina lake?
Shahidi wa kificho P4 : Ninazo sababu binafsi
Mhe. Lissu: Kwahiyo majaji waandike kuwa umekataa kusema sababu kwanini hutaki kumtaja aliyekuita Dar es salaam sawa muraaaaa
Shahidi wa kificho P4 : Ndio.
Mhe. Lissu: wapo wakurya wenzako humu.
Mhe. Lissu: Ieleze Mahakama kama ulipata summons ya Mahakama?
Shahidi wa kificho P4 : nilipigiwa simu nikaenda kituoni nilipata barua ya Mahakama.
Mhe. Lissu: Nani aliyekulipia nauli ya kutoka Arusha Kuja Dar es salaam?
Shahidi wa kificho P4 : Nilikuja na nauli nililipa mwenyewe maana nilikuja kwenye shughuli zingine binafsi.
Mhe. Lissu: Una nyumba hapa?
Shahidi wa kificho P4 : Sina.
Mhe. Lissu: Nani anayelipa gharama za kula na kila kitu?
Shahidi wa kificho P4 : leo nimekuja na gari ya wanasheria
Mhe. Lissu: Tarehe 03/04/2025 ulipelekwa kituo cha Polisi mjini na kabla ulikuwa kituo cha Muriet
Shahidi wa kificho P4 : Ndio
Mhe, Lissu: Hayo maelezo yalikiwa yanahusu kosa gani?
Shahidi wa kificho P4 : Walisema tuna kesi ya kutaka kuzuia Uchaguzi.
Mhe. Lissu: umewahi kupelekwa Arusha kwa hilo kosa ulilokamatwa nalo?
Shahidi wa kificho P4: Sikuwahi kupelekwa Mahakamani.
Mhe. Lissu: Hiyo kesi iliishia wapi?
Shahidi wa kificho P4 : Mimi sijui.
Mhe. Lissu: Hayo maelezo ya Tarehe 03/04 yako wapi?
Shahidi wa kificho P4 : Sijui.
Mhe. Lissu: Nilikwambia kwamba ulikamatwa bure tu hukuwa na kosa lolote we utasemaje?
Shahidi wa kificho P4 : Sijui mimi.
Mhe. Lissu: Siku hiyo ya Tarehe 03/04 wewe na wenzako mlikuwa mnazungumza juu ya maneno mlioyaona kwenye mtandao na wengi mliyaunga mkono
Shahidi wa kificho P4 : Ndio.
Mhe. Lissu: Je hilo lilikuwa kosa nyie kuunga mkono na kuzungumza kauli hizo.
Shahidi wa kificho P4 : Sijui
Mhe. Lissu: Maelezo yako ya 17/04 ukionyeshwa unaweza kuyatambua?
Shahidi wa kificho P4 : Naweza
Shahidi wa kificho P4 ameyatambua maelezo yake na Mh. Lissu anamsomea Maelezo ambayo shahidi aliyaandika pale Polisi.
Mhe. Lissu: Niliyosoma hapa ni sawa na maelezo uliyonayo hapo.
Shahidi wa kificho P4 : Ndio
Mhe. Lissu: Sasa shahidi nataka kukuhoji kuhusu hayo maelezo.
Shahidi wa kificho P4 : Sawa.
Mhe. Lissu: Maeneo hayo ni
1. Uliperuzi kwa simu yako
2. Nilisema tutakinukisha
Anamtajia maeneo kama 8 hivi ambayo atamuuliza maswali.
Mhe. Lissu: Je ungependa yawe sehemu ya ushahidi?
Shahidi wa kificho P4 : ndio.
Jaji: Jamhuri mnasemaje?
Wakili Renatus: sina pingamizi.
Jaji: Hiyo itakuwa ni D9 upande wa utetezi.
Part 190 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 9, 2026
Last time tuliishia Part 150 so leo tutaendelea na-;
Part 151.
Ameingia Mheshimiwa Lissu, zimepigwa kelele nyingi sana hapa Mahakamani ni kelele za Rais! Rais! Rais!
Mhe. Lissu amepiga kombati ya kaki, ameingia kwa vibe sana.
Amebeba makabrasha yake, mavifurushi mengi sana ya vitabu.
Imepigwa sauti ya Courttttt ikiwa na ukali watu hawanyamazi wanaendelea na minong'ono fulani ya kushangilia.
Wameingia Majaji na kuketi eneo lao.
Jaji anasema tuendelee
Karani anasoma namba ya shauri.
Anasimama Renatus Mkude wakili wa Serikali Mkuu, yuko na Ajuaye, Nasoro Katuga, Cathbert Mbiringe, Thawabu Issa wanawakilisha upande wa Jamhuri na Mshitakiwa Tundu Lissu yupo.
Leo tumekuja kujibu hoja za Tundu Lissu kama yeye atakuwa tayari, sisi upande wa Serikali tuko tayari Waheshimiwa Majaji.
Mhe. Lissu anaulizwa uko tayari?
Anasema niko tayari lakini nahitaji kuzungumza mambo yaingie kwenye rekodi za Mahakama.
Niwatakie heri ya Mwaka Mpya nyie Majaji, Mawakili wa Serikali na wote waliopo hapo.
Maswala mawili kati ya matatu ninayotaka kuzungumza nitasema kwasababu kifungu cha 11(1)(2) cha sheria ya magereza nyie majaji ni visiting justices kule magereza.
Majaji wanaodhuru magereza mna wajibu wa kuhakikisha magereza yanaendeshwa kwa mujibu wa sheria na wafungwa iwe wamehukumiwa au mahabusu kama mimi wanapata treatment kwa mujibu wa Sheria.
Na kwa mujibu wa kifungu hicho mna mamlaka ya kutoa maelekezo na mapendekezo kuhusu treatment ya wafungwa na mahabusu.
Sisi tunaoishi huko magerezani tumepewa Haki kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria hiyo kuwaeleza juu ya mambo yalivyo na tunavyotendewa huko magereza.
Jambo la 1 ni kuhusu haki ya mfungwa kuwasiliana na Mawakili wake.
Wafungwa wana haki ya kufanya mawasiliano na mawakili au washauri wa kisheria bila kusikilizwa na maafisa wa magereza Kanuni ya 13 ya kanuni za uendeshaji wa magereza GN. NO. 60/1987. (Prison Management Regulations)
Kanuni inasema kila mfungwa atapewa fursa ya kuwasiliana na mwanasheria wake na atakapomtembelea maafisa wanaweza kumuona ila sio kumsikiliza. Anaisoma hiyo kanuni kwa kingereza hapa.
Sasa Waheshimiwa majaji kumekuwa na tatizo kubwa kuhusiana na haki yangu ya kuzungumza na mawakili wangu bila kusikilizwa na maafisa wa magereza.
Muda wote wako pembeni yangu hadi ninapozungumza na mawakili.
Tatizo hili sio jipya lilianza toka niko Kisutu.
Anasimama Nasoro Katuga anasema tulikuwa na concern aliweka pingamizi halijaamuliwa anaanza kusema mengine. Naomba mwongozo katika hili.
Jaji anaandika kidogo.
Anamuuliza Lissu unasemaje?
Lissu anasema kifungu cha 48 nilichosema kinasema ni draw attention yenu sio kuomba chochote. So i'm drawing the attention to you. Mkiona mnachakufanya fanyeni mkiona hamna msifanye. Wajibu wangu ni kuwaeleza kinachoendelea.
Jaji anasema nafikiri uendelee haya madai ya Katuga ameeelewa baada ya jibu lako.
Tarehe 12/11/2025 tulivyoahirisha kesi mambo yakabadilika tena wakili akifika anapelekwa ofisi ya Mkuu wa Usalama wa Gereza na mimi na Wakili wangu tunapelekwa huko huku wakitusikiliza nikiwa nazungumza na kikundi, kuanzia Mkuu wa Gereza, maafisa wengine zaidi ya watano wanatusikiliza wakati sheria haitaki hivyo.
Siku 88 toka kesi imeahirishwa mwaka jana wananisikiliza kila Mawakili wangu wanaponitembelea.
Mimi na Mawakili wangu tukiuliza, tunaambiwa ni Maagizo kutoka juu, Huko juu ni wapi juu mbinguni au wapi? Mungu anajua.
Hilo ni jambo langu la kwanza.
Nimewapa taarifa kwa mujibu wa kifungu cha 48 mtajua chakufanya ili kuhakikisha sheria inalindwa.
Jambo la Pili, linahusu kutembelewa na watu wengine wasiokuwa wanasheria. Kanuni zinasema unaruhusiwa kutembelewa na watu sio ndugu pekee.
Part 152 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako kwenye tweet hii.