Unataka kununua TV, je Budget Yako ni kiasi Gani? Unataka kwa ajili ya matumizi Gani? Ipi ni brand nzuri?
UZI 🧵
Kwa Sasa Kuna Makampuni mengi ya TV yanayofanya vizuri sokoni, kampuni kama Hisense, TCL, SKYWORTH, Alitop & Solarmax zinafanya vizuri sana..👇
Kwanini EFM wamefuta video hii?
Uchambuzi mzuri kama huu kwanini unafutwa?
Haya muda wa kuisambaza hii video kwa speed umefika.
REPOST 200
TUTAKUWEPO🫵😎
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 2
Anaendele kuzungumza Mhe. Lissu
Mimi niliyesema hayo maneno nitajitetea na niwasikilize hao wanaosema nimefanya uhaini kuwa nimetenda makosa hayo.
Naomba pia mfahamu kabla mahakama hii haijaniteulia mawakili toka tukiwa kisutu sijawahi kuwa na upungufu wa mawakili zaidi ya 50 na baadhi yao wapo hapa leo.
Niliwaambia ambayo nimesema haya kwenye kesi kama hii sitataka mtu anizungumzie nilisema hivyo toka Kisutu na tulielewana.
Nafahamu uzito wa kesi kama hii Waheshimiwa Majaji, anayeshtakiwa ana haki ya kuwakilishwa na mawakili hata kama hana uwezo mahakama itamtafutia Wakili wa kumsaidia.
Mimi uwezo ninao na suala la kwamba sina uwezo hilo halipo. Mimi uwezo ninao.
Pili watu wanaostahili kuwekewa mawakili ni wale ambao wanakabiliwa na makosa makubwa na hawawezi kujitetea wenyewe.
Mimi nina uwezo wa kujitetea mwenyewe. Mimi ni Wakili wa Mahakama hii kwa miaka 23 hadi leo kama Wakili.
Nimefanya kazi ya uanasheria huu ni mwaka wangu wa 31, There is no question whatsoever to defend my self.
Najitetea mwenyewe kwasababu this is ultimate test, huu ndio mtihani mkubwa kwa mfumo wetu wa kisheria.
On this one, kwa heshima zote I will take full responsibility for myself.
Nitaweza to the best of my ability..
This is about my life. I will defend myself to the fullest.
Naomba niseme jambo kuhusu hili jopo la Mawakili toka Kisutu naomba katika kesi hii waendelee kuwepo wanisaidie kwenye research maana gerezani hakuna mtandao hakuna library kule.
Waendelee kuwepo ili wanisaidie nijiteteee kwa ukamilifu.
Na kama hilo litawapendeza nitafurahi kama watatambulishwa na pia hata huyu Wakili Neema Saruni atakubali na yeye awe sehemu ya jopo hilo la Mawakili wataonisaidia kufanya research.
Majaji wanaandika kidogo hapa.
KATUGA anasema tumefuatilia wenzetu mshitakiwa pamoja na Wakili wake.
Kwa mujibu wa kifungu cha 329 cha sheria ya mwenendo wa jinai kinatoa haki kwa mshitakiwa kuwa na uwakilishi kwneye kesi inayomkabili.
Ingawa haki hii sio ya lazima, busara ya mahakama ilimpa Wakili kwa ridhaa yake anaiambia Mahakama hii kujitetea mwenyewe.
Kwenye hiyo hoja ya kujitetea mwenyewe kwakuwa amesema ni mbobezi wa sheria hatuna pingamizi kwenye hilo.
Lakini upande wa jamhuri unasita kukubaliana kwenye hoja ya kuwa ana mawakili ambao watamsaidia kufanya research na watambulishwe.
Hatupingi wao kumfanyia research lakini tunapinga wao kuingia kwenye rekodi. 🤣🤣huyu Baba ana wivu hata watu kutambulishwa, utadhan wakitambulishwa kuna kitu kitapungua kwenye mwili wake.
Anaendelea pale kunapokuwa na kesi ya pande mbili. Lazima Wakili apate nafasi ya kuwa na mtu anayemuwakilisha, hawa wasitambulishwe kabisa.
Jaji anaeongoza jopo la Majaji ni Mh. Dunstan Ndunguru
Huyu Katuga anaongea watu wana hasira nae ni kama wanataka kupasuka hivi sijui hata huyu ndugu anatafuta nini kuna mambo watu wanashangaa kwanini amekuwa na akili kama za mkaanga sumu.
Wanateta jambo mawakili wa Serikali.
Mh. Lissu ameulizwa unasemaje anasema mimi sina shida hata tusipowatambulisha. Tuendelee kwenye mambo ya msingi.
Nilidhani ni jambo dogo lisingekuwa na nongwa kama wenzetu wameona ni nongwa basi tuendelee na kazi ya leo, Mimi sina shida.
Part 3 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako kwenye tweet hii
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 1
Mh. Lissu ameingia tayari akiwa na vibe kubwa sana.
Majaji pia wameingia.
Kesi hii itasikilizwa na majaji watatu wa Mahakama Kuu na wao pia wameshaingia.
Nitawapa majina ya hawa majaji watatu.
Wakatikati yuko bize kuandika hawa wawili wengine tunaangaliana nao uso kwa macho.
Kesi haijaitwa bado.
Jaji anateta kidogo na mwenzake. Anawasha kipauza sauti.
Anasimama kalani anasema Criminal case No. 19605/2025 Jamhuri dhidi ya Tundu Lissu.
Anasimama Nassoro Katuga wakili wa serikali tupo pamoja na
Job Mrema, Thawabu Issa, Mossie Kahima, Harrison Lukosi, Cathbert Mbiringi na Winiwa Kasala.
Hao ndio Mawakili saba wanaoiwakilisha Jamhuri mbele ya mahakama hii.
Mshitakiwa yupo naomba upande wa utetezi waweze kujitambulisha.
Anasimama mwanadada.
Anasema naitwa Neema Saruni ni Wakili. Mdada mrefu ananywele nyinginyingi.
Namuwakilisha mtuhumiwa aliyepo mbele ya mahakama hii tukufu.
Na kwa uwakilishi huo kwa mujibu wa PROBONO na nilipata wasaaa wa kuonana mteja wangu nikakutana nae.
Naomba mahakama impatie nafasi aweze kuelezea.
Watu wameshangaa ngoja tuone sasa.
Jaji anaandika kidogo.
Naambiwa kiutaratibu kesi kubwa watuhumiwa hupewa mawakili na mahakama.
Ngoja tuone.
Jaji anasema ngoja kwanza upande wa mshitaka waseme kesi imekuja kwa hatua gani.
Katuga anasema kesi ilikuja kwa ajili ya Preliminary hearing na sisi tuko tayari.
Kabla ya kuendelea na shauri hili Katuga anasema upande wa Jamhuri ulikuwa na Concern kadhaa kama tutapewa nafasi kuelezea.
Tuko tayari na plea taking na preliminary hearing.
Jaji anamwambia subiri kwanza.
Anaandika kidogo.
Amesimama Neema Saruni anasema tumemsikia Wakili wa Serikali Katuga lakini lipo suala la Uwakilishi wangu ikipendeza mteja apewe nafasi.
Jaji amesema sema wewe kwanza, niliwasiliana na mteja akasema atajiwakilisha mwenyewe, hayuko tayari nimuwakilishe.
Tulianza kushangaaa mbona anasimama wakili ambae hatumfahamu wakati Akina Mzee Mpoki wapo.
Anaanza Mh. Lissu kusema anasema nawashukuru Majaji kwa kunipatia Mawakili.
Pamoja na kwamba mimi sikumuomba na simfahamu wakili Neema Saruni alikuja mwenyewe kuniona kwenye gereza la Ukonga alijitambulisha na kuniambia yeye ndio amepewa hilo jukumu.
Nilifurahi kwa yeye kufanya hivyo. Walifanya vizuri sana.
Sasa Mh. Jaji alivyokuja na kunieleza nilimjulisha kuwa kwenye kesi kubwa kama hii ambayo ni kosa kubwa kuliko yote kwa mujibu wa ibara ya 28.
Kwenye kosa linaloshitakiwa kwa kusema maneno.
Kosa la aina hii nitajitetea Mwenyewe.
Kwasababu inabidi tuambiwe na nchi hii ukisema maneno yasiyowapendeza watu fulani fulani unaweza kuhukumiwa kifo.
Kwasababu hiyo nikasema nitajitetea mwenyewe.
Part 2 itaendele kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako kwenye tweet hii.
Tanzanian activist Edgar Mwakabela, known as Sativa, says he was kidnapped, beaten and shot after criticising the ruling party.
He blames security forces, as abductions of government critics rise ahead of October’s election.
https://t.co/JYwrLBxBqq