Historia imeandikwa kwa Sekta ya Afya Nchini! Hatimae leo tumeweza kuhitimisha safari tuliyoianza mwaka 2016! Haikuwa safari rahisi lakini waswahili wanasema "kawia ufike"! Hakika Tumeitendea haki sekta ya Afya; Tumewatendea haki watanzania. Na tumeitendea haki nchi yetu. #BimaYaAfyaKwaWote #UniversalHealthInsurance #UHI #Tanzania
---
Mapema leo niliwasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote wa mwaka 2022. Kipekee ninawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kujadili na kupitisha Muswada huu. Hakika Bunge la 13 chini ya Uongozi imara wa Spika Dkt @tulia.ackson Dkt limeweka historia ya kuweka msingi madhubuti na endelevu wa kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora za afya bila ya kikwazo cha Fedha. Asante kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge wa Afya na masuala ya UKIMWI chini ya Mhe @stanslaus_nyongo Mb. kwa kazi kubwa na nzuri ya kuuchambua Muswada huu na kutoa ushauri mzuri wa kuuboresha.
Kipekee, ninamshukuru Rais wetu Dkt @samia_suluhu_hassan kwa dhamira yake na utashi wake wa kisiasa wa kuhakikisha tunatunga Sheria hii ili kuwezesha watanzania kupata huduma za afya bila kikwazo cha fedha pindi wanapohitaji huduma hizo na hatimae kuepuka kuingia katika maradhi zaidi, ulemavu wa kudumu, vifo au umaskini kutokana na kukosa fedha za kulipia huduma za afya papo kwa papo.
Shukrani za kipekee kwa Waziri wa Fedha Mhe Dkt @mwigulunchemba kwa ushirikiano mkubwa aliotupatia katika mchakato huu. Aidha ninamshukuru Naibu Waziri wa Afya @dr_mollel na Watendaji wote wa Wizara ya Afya na Taasisi zake, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa mchango wao ktk kuandaa na kuwezesha kupitishwa kwa Mswada huu. Sasa ni rasmi Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote namba 8 ya Mwaka 2022 ni sehemu ya Sheria za Tanzania.
Hatubweteki! Tutafanyia kazi maoni na ushauri uliotolewa na Wabunge ili kuhakikisha tunatengeneza mfumo imara wa Bima ya Afya kwa wote. Na pia kuhakikisha watanzania wanapata huduma bora za Afya katika ngazi zote kuanzia ngazi ya Msingi.
#KaziIendelee.
Hongera! According to the survey conducted by KPMG, ๐น๐ฟ is the most preferred investment destination in East Africa in the next 2 years and counts among the 10 biggest recipients of FDI in Africa. A good business environment will surely bring more external investments for TZ.
Warda Mohamed anayefanya kazi Tanzania voice of Humanity akizungumzia jinsi wadau wanaweza kushirikiana kuwasaidia watoto wenye matatizo ya jinsia
Kongamano la Afya na ustawi wa watoto Tanzania
Landed in New Delhi for a state visit, at the invitation of India national leaders. To Tanzanians, India is our extended family, a strategic ally, and one of our largest bilateral trading partners. I am looking forward to a productive visit in expanding trade and investment between India and Tanzania, a foundation for prosperity for the people of our two countries.
We're excited to announce that the President of Zanzibar & Chairman of The Revolutionary Council H.E Dr.Hussein Ali Mwinyi will grace the #10thAnniversaryOfTHS at JNICC in Dar es Salaam today.
Theme: Strengthening Health Systems for UHC, focusing on Primary Health Care #THS2023
Today is the day! All roads head to JNICC in Dar es Salaam for #THS2023
1๏ธโฃ3:00 PM - 3:40 PM: Opening Sessions
2๏ธโฃ3:40 PM - 4:40 PM: Theme Presentations
3๏ธโฃ4:40 PM - 6:00 PM: Speeches
The Guest of Honour, President of Zanzibar H.E Dr Hussein Mwinyi is expected to grace the summit.
It wish to commend all those involved in giving life to the @DrSalimArchive, chronicling the extraordinary work and achievements of Dr Salim Ahmed Salim.
ย
In a lifetime of public service, Dr Salim has been recognised as a leading figure in the global struggle for independence, freedom, peace and cooperation. He has secured a distinctive and distinguished position in the history of Tanzania, the African continent and the United Nations.
ย
He will forever occupy a cherished place in the hearts of the people of South Africa for his tireless efforts to end apartheid and his commitment to the achievement of a non-racial democracy in South Africa.
ย
This digital archive is more than a remarkable historical record. It is an affirmation of the values by which Dr Salim has lived, the mission for which he has strived and the legacy that he passes on to future generations.
ย
Through the power of technology, this digital archive is accessible around the world. It is my hope that this archive will be used by people of all nations as a site of learning and a source of inspiration.
Congrats to the inauguration of the Dr. Salim Ahmed Salim Archives! Dr. Salim is an old friend of China & has made great contributions to ๐จ๐ณ-๐น๐ฟ relations. His journey in public service & his role in international diplomacy still inspire us to fight for a brighter future.
โUTARATIBU WA BIMA YA AFYA NI KUCHANGIANA SIO LAZIMA MPAKA UUGUEโ โ DKT. MOLLEL
Na. WAF โ Dar es Salaam
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema lengo la kuwepo na Mifuko ya Bima ya Afya ni wananchi kuchangiana gharama za matibabu kabla ya kuugua ili kuepusha familia hasa za masikini kwa kutumia fedha nyingi kugharamia matibabu.
Dkt. Mollel amesema hayo leo Septemba 25, 2023 jijini Dare Es Salaam wakati akiongea na Vyombo vya Habari ili kuelezea mafaniko ya Sekta ya Afya katika kipindi cha miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
"Katika kipindi cha awamu zote sita, Serikali imefanikiwa kuboresha Sekta ya Afya kwa ujumla, changamoto kubwa iliyobaki na inawayolikabili kundi kubwa la wananchi ni namna ya kuwawezesha kugharamia huduma za afya. Kwahiyo, ili kufikia dhamira ya Serikali ya Afya Bora kwa Wote ni lazima kama nchi kuwa na mfumo endelevu na imara wa uchangiaji wa gharama za matibabu kabla ya kuugua (Bima ya Afya)". Amesema Dkt. Mollel.
Aidha, Dkt. Mollel amesema Mwaka 2016 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ulianzisha mpango wa bima ya afya kwa watoto walio chini ya miaka 18 (Toto Afya Kadi) kwa lengo la kuwezesha kundi la watoto kwa ujumla wao kujiunga kupitia shule za awali, msingi na sekondari ili kunufaika na mpango huo.
โHata hivyo, pamoja na uhamasishaji uliofanyika kwa kupindi cha takriban miaka saba (7) bado mwitikio haukuwa wa kuridhisha kwani idadi ya watoto waliojiandikisha ilikuwa ni 210,000 kati ya lengo la watoto milioni 25 kwa kipindi hichoโ. Amesema Dkt. Mollel
Dkt. Mollel ameongeza kuwa, kupitia uandikishaji wa kundi hilo, asilimia 99 ya watoto walioandikishwa walikuwa tayari na matatizo ya kiafya ambapo kati ya takriban shilingi bilioni 5 zilizokusanywa kama michango yao, shilingi bilioni 40 zilitumika kugharamia matibabu hali iliyoenda kinyume na dhana na misingi ya uendeshaji wa mfumo wa bima ya afya.
Amesema, pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika Sekta ya Afya kupitia mfumo wa bima ya afya, bado kuna changamoto katika ujumuishwaji wa wananchi katika mfumo huo kutoka katika sekta rasmi binafsi na isiyo rasmi. Changamoto hiyo ni uhiari wa kujiunga kwa makundi hayo kwakuwa wengi hujiunga wakiwa tayari ni wagonjwa.
"Katika kutatua changamoto zilizopo, Serikali inakamilisha muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambayo inalenga kuimarisha Mfumo wa Bima ya Afya nchini kwa kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanajiunga zaidi na utaratibu huu ikilinganishwa na hali ilivyo sasaโ. Amesema Dkt. Mollel
Mwisho, ametoa rai kwa wananchi wote ambao bado hawajajiunga na utaratibu wa bima, wajiunge sasa na pia pindi maamuzi yatakapofanyika ya kupitishwa kwa Bima ya Afya kwa wote wajitokeze kwa wingi kujiunga na Mfumo huu.
"Serikali ilianzisha mfumo wa malipo kabla ya kuugua (Bima ya Afya) kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya @nhiftz kwa kuanza na kundi la watumishi wa umma na wategemezi wao ambao hujiunga kwa mujibu wa Sheria Sura
Hata hivyo, kutokana na uhitaji wa bima ya afya kwa makundi mengine ya wananchi, Serikali imekuwa ilifanya marekebisho ya Sheria ili kuruhusu makundi hayo kujiunga kwa hiari. Takwimu zinaonesha kuwa hadi kufikia Juni 2023, wanufaika wa Mfuko wa NHIF walikuwa 4,821,233 sawa na asilimia 8 ya wananchi wote".
Dkt. Godwin Mollel.
"Katika kipindi cha awamu zote sita, Serikali imefanikiwa kuboresha Sekta ya Afya kwa ujumla, changamoto kubwa iliyobaki na inawayolikabili kundi kubwa la wananchi ni namna ya kuwawezesha wananchi kugharamia huduma za afya. Kwahiyo, ili kufikia dhamira ya Serikali ya Afya Bora kwa Wote ni lazima kama nchi kuwa na mfumo endelevu na imara wa uchangiaji wa gharama za matibabu kabla ya kuugua (bima ya afya)".
Dkt. Godwin Mollel.
"Katika kutatua changamoto zilizopo, Serikali inakamilisha muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote ambayo inalenga kuimarisha Mfumo wa Bima ya Afya nchini kwa kuhakikisha kuwa wananchi wengi wanajiunga zaidi na utaratibu huu ikilinganishwa na hali ilivyo sasa. Nitoe rai kwa wananchi wote ambao bado hawajajiunga na utaratibu wa bima, wajiunge sasa na pia pindi maamuzi yatakapofanyika, wajitokeze kwa wingi kujiunga na Mfumo huu".
Dkt. Godwin Mollel.