NIMR Amani Research Centre in Muheza Tanga, has officially been granted by South African National Accreditation System (SANAS) a Certificate of GLP Accreditation as a Centre for R & D and Evaluation of Novel Vector Control Tools and Products in Africa. This is a great achievement
FEDHA ZA MIRADI ZIKAGUSE CHANGAMOTO ZA WANANCHI VIJIJINI
Na WAF- Kagera
NAIBU Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel ametoa wito kwa Wadau na watendaji wote wa Serikali kuhakikisha fedha zote zinazoingia nchini na zinazotoka Serikalini kupitia ziara za nje za Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan zikatatue changamoto zilizokusudiwa za wananchi katika vijiji kuliko kwenye semina na warsha.
Dkt. Mollel ametoa wito huo leo Agosti 07, 2023 wakati akizindua kampeni ya ugawaji wa vyandarua katika maeneo yote ya mikoa ya Kagera na Tabora inayoambatana na elimu itayosaidia katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria katika mikoa hiyo.
"Niwaasa taasisi zote za Serikali na zisizo za Serikali, Rais wetu anapoenda kuzunguka kwenda kwenye makampuni makubwa na mashirika makubwa duniani ili kutafuta fedha, vipaumbele vyake ni kwenda kumfikia Mtanzania mnyonge kutatua changamoto katika vijiji". Amesema Dkt. Mollel.
Sambamba na hilo, Dkt. Mollel amewataka Wadau kupunguza semina, warsha na mafunzo na fedha hizo ambazo zimetumika huko zielekezwe katika kuongeza nguvu kutatua changamoto zinazowagusa Watanzania wenye uhitaji ikiwemo changamoto za afya.
Aidha, Dkt. Mollel ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera kutumia vyandarua vilivyo na dawa na kusikiliza vizuri maelekezo na ushauri kutoka kwa Wataalamu wa afya hasa kwenye afua mbalimbali za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ili kufanikisha dhamira ya Serikali ya kuutokemeza ugonjwa huo nchini.
Kwa upande wake mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Erasto Sima ameomba Serikali kupitia Wizara ya Afya kuupa Mkoa wa Kagera kipaumbele kwenye eneo la rasilimali fedha na watu ili kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa wa Malaria kwani Mkoa huo ni moja kati ya mikoa inayoongoza kuwa na maambukizi ya Ugonjwa wa Malaria.
Pia, amewashauri wananchi kujenga tabia ya kupima ugonjwa wa Malaria kabla ya kutumia dawa ili kuondoa usugu wa dawa, huku akibainisha kama mkoa wataendelea kutekeleza juhudi za mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ikiwemo kusafisha mazingira na kutoa elimu ya mapambano dhidi ya ugonjwa huo
NIMR Gonja Research Station is an amazing "stony area", with a swimming pool for relaxation! The Director General, Prof Said Aboud paid a visit at the station on 8th June 2023 and directed to establish a "Research Diagnostic Centre" with immediate effect to serve the community.
Wafanyakazi wa Kituo cha Nimr Amani wakiwa kwenye Maadhimisho ya Kilele cha siku ya wafanyakazi Duniani 01 May 2023 katika Viwanja vya Mkwakwani Tanga.
"Ushuhuda wa wananchi kuhusu huduma ya vipimo inayotolewa na NIMR" katika kuhitimisha sherehe za Muungano ("Clients' feedback" on the NIMR's free diagonstic services provided during the commemoration of UNION day 26th April 2023).
"Ushuhuda wa wananchi kuhusu huduma ya vipimo inayotolewa na NIMR" ("Clients' feedback" on the NIMR's free diagonstic services provided during the commemoration of UNION day 26th April 2023).
Siku ya kilele cha Maadhimisho ya Miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,Kituo cha Nimr Amani kikitoa Huduma ya upimaji Afya BURE kwa wananchi waliofika kwenye Viwanja Vya Nimr Amani.#Umoja na Mshikamano ndio nguzo ya Uchumi wetu#
Siku ya kilele cha Sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Tarehe 26/04/2023,Wafanyakazi wa kituo cha Nimr Amani wakishirikiana na Wafanyakazi wa Halimashauri ya Muheza na Chuo cha Afya Vector Kufanya usafi wa Mazingira maeneo ya Kituo cha Afya UBWARI.
Kaimu Meneja wa kituo Cha NIMR Amani Dr. Veneranda Bwana akiongoza watumishi wa kituo hicho katika zoezi la upandaji wa miti katika kuadhimisha miaka 59 ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar.
Katika kuadhimisha Miaka 59 ya sherehe za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kituo cha NIMR Amani kinapokea miti kutoka Tanzania Forest Services (TFS) kwa ajili ya Zoezi la Upandaji Miti.
#Katika kuelekea siku ya Wanawake duniani (8th March, 2023), wakina mama wa NIMR vituo vya Amani na Tanga walikwenda kupeleka msaada wa mahitaji muhimu kwa wafungwa katika gereza la Maweni Tanga
#Wafanyakazi wa Kituo cha NIMR Amani wakiwa kwenye picha ya pamoja na wawezeshaji wa Mafunzo juu ya elimu ya masuala ya UKIMWI mahala pa kazi kutoka ofisi ya Mganga Mkuu (W), Muheza.Tarehe 28/02/2023.