WALALA HOI WAKO VIZURI:Hata hivyo ni rahisi kuwaunganisha watu dhidi ya WAHAFIDHINA,na mfano wa hao.Lakini ni kazi ngumu sana kuwaunganisha baada ya kuwaondoa.Kwa uzoefu kila mtu (au chama)huwa na fikra yake baada ya mafanikio
ELIMU KWA UMMA: Leo hii duniani madikteta wako juu na watu wa haki wako chini. Sababu madikteta na wakandamizaji wengine wanazungumza na kueneza sera zao mbaya na watu wa Haki hawazungumzi ipasavyo. Kuelekea Oktoba 2020, umma uelimishwe kujua na kutetea haki zao.
SAMAKI MKUBWA TANZANIA: Nilipoiona picha hii nikatafakari “kumbe tamba utakavyo lakini wakati ukifika na wavuvi wakiungana utatolewa tu!”. Wavuvi wetu watafakari kwa kina ujumbe wa picha hii. UMOJA NI NGUVU UTENGANO… https://t.co/Ubn3hrLIi8
SAMAKI MKUBWA TANZANIA: Nilipoiona picha hii nikatafakari “kumbe tamba utakavyo lakini wakati ukifika na wavuvi wakiungana utatolewa tu!”. Wavuvi wetu watafakari kwa kina ujumbe wa picha hii. UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU.
MASHEIKH NA MAASKOFU: Hawapaswi kujisalimisha mbele ya ukandamizaji au misukosuko. Badala yake hayo yanatakiwa kuwafanya kuwa na nguvu zaidi kutekeleza wajibu wao kwa maslahi ya umma. Dhana za kiliberali kwamba “anaye kuzidi nguvu ungananaye” hazifai kabisa kwa viongozi wa Dini.
UMUHIMU WA VYAMA KUUNGANA SASA: Ni muhimu kwa namna mbili: Kwanza inawezekana vikakidhi matakwa yao Oktoba 2020. Pili ikiwa 2020, hawatafuzu, nguvu yao itamudu kusukuma Katiba mpya 2021. Bila ya Katiba mpya “hakitaeleweka”.
Watanzania tuchague viongozi watakaoimarisha mfumo wa haki na uhuru. Ni moja ya matatizo makubwa ya taifa letu. Pichani tukitoka mahabusu Central Police Dar es Salaam, tuhuma ilikuwa kwenda Nairopi Hospitali (Kenya) kumuona Mgonjwa (Tundu Lisu) .
TISHIO LA KUFUTA VYAMA NA WAGOMBEA: Maendeleo hayaletwi na chama kimoja cha siasa pekeyake. Kabla ya kufanya uamuzi huo tujishughulishe na kuelewa kwa kina dhana ya uhuru, haki na maendeleo. Kuhujumu vyama vya siasa na watu mahiri katika siasa ni kulirudisha nyuma Taifa.
TAAZIA YA MZEE MOYO. Mapinduzi Zanzibar 1964, yalikuwa na hasara kubwa. Moja ni kuwatimua wasomi wake. Mataifa yaliwanyang’anyia ikiwemo Tanganyika. Mmoja wa wasomi walionufaisha Tanganyika ni Nassoro Moyo. Tuwalipe fadhila Wazanzibari japo kwa uhuru wa kujiamulia mambo yao.