#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 9, 2026
Last time tuliishia Part 150 so leo tutaendelea na-;
Part 151.
Ameingia Mheshimiwa Lissu, zimepigwa kelele nyingi sana hapa Mahakamani ni kelele za Rais! Rais! Rais!
Mhe. Lissu amepiga kombati ya kaki, ameingia kwa vibe sana.
Amebeba makabrasha yake, mavifurushi mengi sana ya vitabu.
Imepigwa sauti ya Courttttt ikiwa na ukali watu hawanyamazi wanaendelea na minong'ono fulani ya kushangilia.
Wameingia Majaji na kuketi eneo lao.
Jaji anasema tuendelee
Karani anasoma namba ya shauri.
Anasimama Renatus Mkude wakili wa Serikali Mkuu, yuko na Ajuaye, Nasoro Katuga, Cathbert Mbiringe, Thawabu Issa wanawakilisha upande wa Jamhuri na Mshitakiwa Tundu Lissu yupo.
Leo tumekuja kujibu hoja za Tundu Lissu kama yeye atakuwa tayari, sisi upande wa Serikali tuko tayari Waheshimiwa Majaji.
Mhe. Lissu anaulizwa uko tayari?
Anasema niko tayari lakini nahitaji kuzungumza mambo yaingie kwenye rekodi za Mahakama.
Niwatakie heri ya Mwaka Mpya nyie Majaji, Mawakili wa Serikali na wote waliopo hapo.
Maswala mawili kati ya matatu ninayotaka kuzungumza nitasema kwasababu kifungu cha 11(1)(2) cha sheria ya magereza nyie majaji ni visiting justices kule magereza.
Majaji wanaodhuru magereza mna wajibu wa kuhakikisha magereza yanaendeshwa kwa mujibu wa sheria na wafungwa iwe wamehukumiwa au mahabusu kama mimi wanapata treatment kwa mujibu wa Sheria.
Na kwa mujibu wa kifungu hicho mna mamlaka ya kutoa maelekezo na mapendekezo kuhusu treatment ya wafungwa na mahabusu.
Sisi tunaoishi huko magerezani tumepewa Haki kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria hiyo kuwaeleza juu ya mambo yalivyo na tunavyotendewa huko magereza.
Jambo la 1 ni kuhusu haki ya mfungwa kuwasiliana na Mawakili wake.
Wafungwa wana haki ya kufanya mawasiliano na mawakili au washauri wa kisheria bila kusikilizwa na maafisa wa magereza Kanuni ya 13 ya kanuni za uendeshaji wa magereza GN. NO. 60/1987. (Prison Management Regulations)
Kanuni inasema kila mfungwa atapewa fursa ya kuwasiliana na mwanasheria wake na atakapomtembelea maafisa wanaweza kumuona ila sio kumsikiliza. Anaisoma hiyo kanuni kwa kingereza hapa.
Sasa Waheshimiwa majaji kumekuwa na tatizo kubwa kuhusiana na haki yangu ya kuzungumza na mawakili wangu bila kusikilizwa na maafisa wa magereza.
Muda wote wako pembeni yangu hadi ninapozungumza na mawakili.
Tatizo hili sio jipya lilianza toka niko Kisutu.
Anasimama Nasoro Katuga anasema tulikuwa na concern aliweka pingamizi halijaamuliwa anaanza kusema mengine. Naomba mwongozo katika hili.
Jaji anaandika kidogo.
Anamuuliza Lissu unasemaje?
Lissu anasema kifungu cha 48 nilichosema kinasema ni draw attention yenu sio kuomba chochote. So i'm drawing the attention to you. Mkiona mnachakufanya fanyeni mkiona hamna msifanye. Wajibu wangu ni kuwaeleza kinachoendelea.
Jaji anasema nafikiri uendelee haya madai ya Katuga ameeelewa baada ya jibu lako.
Tarehe 12/11/2025 tulivyoahirisha kesi mambo yakabadilika tena wakili akifika anapelekwa ofisi ya Mkuu wa Usalama wa Gereza na mimi na Wakili wangu tunapelekwa huko huku wakitusikiliza nikiwa nazungumza na kikundi, kuanzia Mkuu wa Gereza, maafisa wengine zaidi ya watano wanatusikiliza wakati sheria haitaki hivyo.
Siku 88 toka kesi imeahirishwa mwaka jana wananisikiliza kila Mawakili wangu wanaponitembelea.
Mimi na Mawakili wangu tukiuliza, tunaambiwa ni Maagizo kutoka juu, Huko juu ni wapi juu mbinguni au wapi? Mungu anajua.
Hilo ni jambo langu la kwanza.
Nimewapa taarifa kwa mujibu wa kifungu cha 48 mtajua chakufanya ili kuhakikisha sheria inalindwa.
Jambo la Pili, linahusu kutembelewa na watu wengine wasiokuwa wanasheria. Kanuni zinasema unaruhusiwa kutembelewa na watu sio ndugu pekee.
Part 152 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako kwenye tweet hii.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 152
Anaendelea Mhe. Lissu.
Tuna haki yakutembelewa, waheshimiwa Majaji kuna masharti kwenye hiyo kanuni ikiwemo sharti la kutembelewa na mfungwa mwenzako, sharti lingine ni askari magereza wakuone na kukusikiliza ila kwa Mawakili kanuni haisemi hivyo.
Waheshimiwa Majaji tangu tarehe 10/04/2025 mpaka 12/11/2025 nilikuwa natembelewa bila tatizo.
Na ndugu, familia, marafiki na Mimi ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa, walikuwa wananitembelea wana Chadema
Tanzania nzima.
Niliitwa kwa Bwana Jela nikaambiwa ni marufu kwa viongozi na wanaChadema kukutembelea Gerezani.
Chadema ni Chama halali na sio kosa kwa wanaChadema na viongozi wenzangu kunitembelea lakini kuanzia Tar. 12/11/2025 hawajaruhusiwa.
Maafisa magereza ni maafisa wa umma so yale magereza sio mali zao binafsi.
Hawana mamlaka ya kubagua nani aje gerezani nani asije. Katiba inasema usibague watu kwa mtizamo wao wa kisiasa, dini au kabila na hili vilevile naomba niwaeleze mlifahamu kuhusu violation ya haki ya Mfungwa kutembelewa.
Waheshimiwa Majaji sasa naomba swala la tatu niliseme.
Linahusu uendeshaji wa kesi hii. Na naomba niweke wazi kuwa siwalaumu kwa chochote nitakachosema hapa. Na hiki nitakachosema siwalaumu mawakili wa serikali na nyie majaji.
Haki zangu zimekiukwa sio kwa kosa lenu wala la Mawakili wa Serikali.
Waheshimiwa Majaji leo hii ni siku ya 307 tangu niwekwe mahabusu.
Miezi 10 week 44 niko mahabusu. Waheshimiwa majaji katika siku zote hizi kesi hii imesikilizwa kwa siku 14 tu na leo ni siku ya 15 kesi hii inasikilizwa katika siku 307.
Kuna siku 88 ambazo kesi haijasikilizwa kabisa, niko gerezani hakuna kinachoendelea.
Haki iliyocheleweshwa ni haki iliyokiukwa. Justice delayed is justice denied.
Na Katiba yetu inaelekeza Mahakama ziendeshe mashauri kwa namna ambayo haitachelewesha Haki. Ibara ya 147 ya Katiba inasema.
Kifungu cha 5 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinasema mashauri yanaendeshwe kwa haraka.
Tatizo lipo kwenye utaratibu wa session ndio tatizo na hilo ni tatizo la wanaoamua kesi iendeshe kwa njia ya session.
Naomba niwasomee kilichosemwa na Tume ya Haki jinai kuhusu kuendesha mashauri ya jinai kwenye ripoti ya July 2023, ukurasa wa 17 na 18 unasema kuhusu vikao vya mahakama kuu (high court session) tume inasema uendeshaji wa mashauri kwa njia ya vikao huchelewesha mashauri hayo.
Kati ya mashauri 2000 ni mashauri 700 tu ndio yalisikilizwa pekee kwa mtindo wa session.
Hivyo basi uendeshaji wa kesi kwa kutumia session unaamuriwa na Jaji Mkuu zikiisha siku tunasubiri aseme tena ndo maana zimepita siku 88 bila kesi hii kuendelea hadi atakapopanga tena huyo Jaji Mkuu.
Ucheleweshaji huu sio kosa lenu wala mawakili wa Serikali ni kosa la utaratibu tulionao.
Je huu utaratibu wa session uko wapi kwenye CPA ambayo ni sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.
Leo hapa High Court Dar es salaam kuna majaji wakutosha lakini ili kesi yangu isikilizwe lazima Jaji atoke Songea, mwingine Mtwara sijui na lazima walipwe, Usafiri, Chakula na kila kitu.
Usipowalipa kesi haiendelei na mimi mtuhumiwa nateseka huko jela. Walishindwa nini kuwapangia majaji wa hapa ili kesi isikilizwe kila siku.
Zamani majaji walikuwa wachache sana lakini siku hizi kila mkoa kuna majaji. Nashangaaa mambo haya kwa utaratibu huu sasa.
Jaji anasema soma kifungu cha 185 na anakisoma hapa kinasema Mahakama inamamlaka ya ku conduct seatings.
Mhe. Lissu anasema kuna tofauti kati ya seatings na sessions.
Kwahiyo kwenye hili ni tofauti na ku conduct seatings. Mahakama kuu zote zinakaa kusikiliza kesi hizo ni seatings zote.
Mimi nasema utaratibu wa sessions ni mbaya zaidi kwa kesi kama ya Uhaini.
Jaji ameleta kifungu namna Lissu alivyolitafsiri ameishia kusema hebu tuendeleee basi mshitakiwa ๐๐๐
Kosa la Uhaini ni Sue Generis sio sawa na wizi wa kuku, ujambazi na makosa mengine.
Part 153 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.