#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 284
Mahakama imereje
Mwenyekiti Lissu alipata wasaa wa kuongea na Mawakili na mashahidi wake kwa muda wa nusu saa aliongea na Katibu Mkuu wa Chama John Mnyika, Amani Golugwa Naibu na Brenda Rupia.
Anasimama Ajuaye Zengeli amesema wako tayari kumuuliza maswali shahidi ambae ni Tundu Lissu. Wako tayari kuendelea.
Majaji wanaaandika andika hapa.
Mhe. Lissu amekaa zake pale kizimbani. Anaulizwa uko tayari kuulizwa tuanze maana bado uko chini ya kiapo pia.
Tutauliza maswali wote na ataanza Nasoro na baadae wengine:
Anasimama Katuga. Anasema Shahidi Pole na ushahidi mrefu.
Katuga: ulisema kuwa sisi ni ndugu zako?
Mhe. Lissu: Nilisema ndio.
Katuga: ni kitu cha kisheria na hakuna tofauti yoyote ya mimi na wewe?
Mhe. Lissu: Sawa.
Katuga: Wewe ni mwanasheria
Mhe. Lissu: Kweli
Katuga: Una ujuzi wa kisheria
Mhe. Lissu: Ni kweli
Katuga: Kama una kumbukumbu Tanzania ilipata uhuru mwaka gani?
Mhe. Lissu: Tar. 09 December 1961
Katuga: Ni nchi huru?
Mhe. Lissu: Ni nchi huru.
Katuga: Ni chombo gani kina mamlaka ya mwisho?
Mhe. Lissu: Mahakama ya Rufani.
Katuga: Naishia Kwenye Mahakama mimi.
Lissu: Hilo ni lako mimi langu ni Mahakama ya Rufani.
Katuga: Basi kwa mujibu wa ibara ya 108 inasemaje?
Lissu: Ndio ni Mahakama ya Tanzania.
Katuga: Kwahiyo Mahakama haipangiwi na mtu yeyote?
Lissu: Haipangiwi
Katuga: Wewe ni Mwenyekiti wa Chadema?
Lissu: Sahihi
Katuga: Je uliiambiwa mahakama hii kuwa mwenyekiti wa Chadema ni kinga kushtakiwa?
Lissu: Sijaiambia na sina kinga hiyo.
Katuga: ulisema sifa nyingi zinazokuhusu ambazo mimi sizipingi. Je hizo tuzo zilikuwa kwenye utaratibu gani?
Lissu: Zipo ambazo zina maandishi na zingine unapewa kitu kama kombe la Dunia hivi.
Katuga: Hebu wambie Majaji haya matuzo yote haya?
Lissu: sijaleta na sina wajibu
Katuga: Ukienda hivyo tutaenda siku saba.
Lissu: nimekaaa jela mwaka mzima nitaogopa week moja yako kweli?
Katuga: Sasa ulileta ushahidi wako huo wa tuzo.
Lissu: Sijaleta sio kazi yangu ni kazi yako wewe.
Katuga: Sasa usilete ujuaji.
Lissu: Mimi ni mjuaji kweli kweli. Unataka nisilete kivipi sasa?
Katuga: Kamati gani ilisema uachiwe?
Lissu: Kamati ya Haki za Binadamu ya kimataifa
Katuga: Kuna sehemu yoyote umekanusha kuwa maneno yale ya kukinukisha, kuhamasisha uasi na sanasana .... umesema maneno hayo wameyatoa kwenye video yako. Je ulisema sio yako?
Lissu: Mimi nilisema mkitaka kuyaelewa sikiliza hotuba yote.
Katuga: Wewe ni kaka yangu siwezi kukuuliza lile swali la una akili au huna kama unavyowaulizaga watu
Lissu: Ukiona unaweza kusema nani amekukataza. Kama unaona sina akili sema tu au niulize nitakujibu.
Katuga: Haya maneno ni ya kwako au sio ya kwako?
Lissu: Hayo maneno sijawahi yakataa ni yakwangu sana.
Katuga: Historia pia umewahi kuisoma?
Lissu: Nimewahi.
Katuga: Waliwahi kuwalaghai babu zetu kihistoria hebu nikumbushe?
Lissu: Hawakulaghai waliingia nao mikataba.
Katuga: mikataba ya kilaghai ilikuwa?
Lissu: hiyo mikataba ilikuwa ya faida kwa hao viongozi wa kiafrika waliyoingia. Kwao waliiona ina faida.
Katuga: Si walikuwa wakoloni hao?
Lissu: Walikuwa wakoloni walioiumiza afrika kama ambavyo Samia ameiumiza nchi sasahivi.
Katuga: Wewe ni mtetezi wa mali za umma. Unakumbuka ulisemaje kuhusu makinikia. Ulisema hayatoki?
Lissu: Huna unachojua kama unataka niulize nitakwambia nilivyosema
Katuga: Si ulisema Tanzania ilishitakiwa je ilishitakiwa kweli mbona mimi sijui kama ilishitakiwa?
Lissu: Nani kakwambia kuwa kwenye international abitration imeshitakiwa unataka nikupeleke nitafanya hivyo hakuna shida.
Katuga: Kama nilikusikia wewe ni mtaalamu wa Sheria za Uchaguzi?
Lissu: Ni kweli
Katuga: Tanzania kupinga sheria fulani utaratibu wake ukoje?
Lissu: Uko namna nyingi? Mfano kupinga kwa njia ya maandamano kuhamaasisha wanachi waipinge hiyo sheria
Part 285 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.