@MariaSTsehai Huyu hakuna kitu anaweza kufanya tofauti na mfumo wa chama ni wakuweka pembeni tuendelee na harakati zetu.Kwa jinsi ya mfumo CCM hakuna mgawanyiko.
7/7 is approaching, Samia, Abdul and their murderous cabal are scared! The security forces and public servants will be given orders that will be impossible to defend morally, rationally on every level. Everyone will have to make the decision to defend their actions because saying “I was following orders���, “I just wanted to keep my job” - will not cut it! This time around all crimes against humanity will be monitored more closely, and if internarional intervention fails, these crimes will be adjudicated in special tribunals set up by citizens themselves! We refuse to be victims, we will fight back and hold everyone accountable! There is no hiding behind the so called government!
The World needs to warn this murderous regime! Allow the people to take back their power without shedding blood!
#SamiaMustGo #CCMmustgo
‼️MPANGO WA JESHI LA POLISI DHIDI YA CHADEMA‼️
Kama mtakumbuka siku kadhaa zilizopita ilisambaa taarifa kuhusu Jeshi la Polisi kuvamia nyumbani kwa Yoramu Mbyela (Huyu kwenye picha) ambae ni mfanyabiashara anaeuza vifaa vya CHADEMA ikiwemo matisheti, bendera, madera, kombati, n.k
Polisi wakiwa na gari aina ya FUSO walivamia nyumbani kwake, wakamlazimisha mke wa Mbyela afungue duka, kisha wakabeba na kuondoka na mzigo wote wa vifaa vya CHADEMA ambao waliukuta dukani kwake.
Mke wa Mbyela pamoja na Wakili wao wamefuatilia huo mzigo wao, Polisi wakarudisha baadhi ya vitu lakin mzigo mkubwa wakakataa kurudisha mpaka leo bado wamebaki nao.
Sasa nimejulishwa kwamba Jeshi la Polisi wamebaki na huo mzigo kwasababu wanampango wa kuutumia kufanikisha mpango wao dhidi ya CHADEMA hii ni kutokana na hofu waliyonayo kuhusu Maandamano ya 7/7 yani Julai 7, 2026.
Wamepanga kuwavalisha nguo za CHADEMA watu wao ambao ni Green guard, UVCCM na baadhi ya migambo kisha watawapeleka huko porini ambapo badae Polisi watajifanya kwamba wamevamia eneo hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa Wananchi kwamba waliona kuna kundi la watu ambao hawajui ni akina nan.
Baada ya Polisi kuvamia eneo hilo watautangazia umma kwamba Vijana wa CHADEMA wamekamatwa huko porini wakiwa wanapewa mafunzo ya kijeshi kwa ajili ya Maandamano ya Julai 7 ili Msajili apate sababu ya kuingilia kati aseme kwamba CHADEMA imevuja sheria ya vyama vya Siasa maana Sheria ya Vyama vya Siasa ilipiga marufuku vikundi vya ulinzi na mafunzo ya kijeshi mwisho wa siku CHAMA kinaweza kufutwa.
Lakin pia Jeshi la Polisi litakuwa linawavalisha UVCCM hizo nguo za CHADEMA kisha wanawatuma kwenye mikutano ya hadhara ya CHADEMA kufanya fujo ili ionekane CHADEMA wanagombana wao kwa wao.
Sasa ni muhimu sana Wanachama wenzangu mnapoenda kwenda Mikutano, hakikisha unamtambua mtu ambae umekaaa nae jirani ukiona kuna mtu/watu huwaelewi toa taarifa kwa Viongozi wa CHAMA, hawa wahuni wakivamia mikutano yetu inatakiwa muwape HAKI YAO YA KIKATIBA.
Kwanini kesi ya Mwenyekiti wetu isogezwe mbele kwa mda mrefu kiasi hiki mara tu baada ya chama kueleza mpango mbovu wa polisi hapo kesho.
Chama kimeeleza nia ovu ya polisi dhidi ya chama chetu alafu kesi inasogezwa mbele!!!
Mahakama ya Tanzania inaondoa imani ya wananchi na kuchochea chuki kwa matendo kama haya.
KWAKUWA NI HALALI KWA WAZANZIBARI KULINDA HAKI ZA WAZANZIBARI HAIWEZI KUWA HARAMU KWA WATANGANYIKA KULINDA HAKI ZA WATANGANYIKA.
Kwa yanayoendelea kujitokeza katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar kuhusu kujitanabaisha kwa misingi ya Uzanzibari na kulinda maslahi ya Zanzibar, je, si wakati sasa kwa Watanganyika nao kuzungumza kwa uwazi, kuhoji kwa uhalali na kujadili kwa kina masuala yanayohusu haki, hadhi na maslahi ya Tanganyika?
Je, Watanganyika hawana haki ya kuhoji na kulinda:
1. Bandari zilizopo ndani ya Tanganyika.
2. Misitu na rasilimali za mazingira za Tanganyika.
3. Rasilimali za asili zilizopo katika eneo la Tanganyika.
4. Hadhi, haki na umiliki wa ardhi ya Tanganyika.
5. Nafasi, haki na uwepo wa watu wasio Watanganyika katika idara na taasisi ambazo si za Muungano.
6. Uhalali wa viongozi wasio Watanganyika kuingia au kusaini mikataba inayohusu rasilimali za Tanganyika, hususan pale ambapo baadhi ya masuala hayo tayari yameondolewa katika eneo la Muungano kwa upande wa Zanzibar.
7.Kuhoji mchango wa Zanzibar katika kugharimia gharama za uendeshaji wa shughuli za Muungano na Ulipwaji wa Deni la Taifa.
Ikiwa ni halali kwa Wazanzibari kujadili, kuhoji na kulinda maslahi ya Zanzibar kwa misingi ya utambulisho wao wa kisiasa na kikatiba, kwa mantiki hiyo hiyo haipaswi kuwa kosa kwa Watanganyika kuhoji, kujadili na kutetea maslahi ya Tanganyika.
Katika mfumo wowote wa haki, usawa na kuheshimiana ndani ya Muungano, haki ya kulinda maslahi ya Zanzibar haiwezi kutenganishwa na haki ya Watanganyika kulinda maslahi ya Tanganyika.
Haki hizo zinapaswa kutambuliwa kwa usawa, bila upendeleo na bila kuonekana kuwa ni tishio kwa Muungano, bali kama sehemu ya kujenga Muungano wenye misingi ya haki, uwazi na kuheshimiana.
UKWELI,HAKI NA UWAJIBIKAJI ndiyo Msingi bora wa kuliongoza Taifa kutoka katika vitendo vya Ukatili dhidi ya ubinadamu,ukiukwaji wa Haki za Raia na,Mauwaji na Utekaji vilivyofanyika kanla,wakati na Baada ya Tarehe 29 Oktoba 2026.
BAK MWABUKUSI.
Utawala dhalimu wa damu, mmeua maelfu ya watu kujitangaza bila ridhaa ya umma..
Mmeteka na Mnateka watu ili kuwajaza watu hofu..
Mnawategea wengine sumu ili kuwaua na kumaliza kila anaewakosoa..
Ushirika wa kidhalimu huwa haudumu, hakuna mwenye unafuu miongoni mwenu…
Wote mmekalia viti vya damu na vyeo vya uongo…
Damu ya Watanzania itaendelea kuwanenea kila baya nyie na familia zenu.
Ni muhimu mmeanza kumalizana, kama boss anaweza kutuma mtu kuita msaidizi wake majina (YUDA)
Watanzania tutashinda vita hii, hakuna mwenye nafuu ccm wote ni walewale.
MAHAKAMA YA RUFAA KUSIKILIZA KESI DHIDI YA Mhe. Tundu Antipas Lissu June 11, 2026
Mahakama ya Rufaa inatarajiwa kusikiliza maombi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini dhidi ya Mwenyekiti wa chama Taifa Alhamisi tarehe 11 Juni, 2026.
Haya ni maombi ya Jamhuri yaliyowasilishwa baada ya Mahakama Kuu kukubali pingamizi la Mhe. Lissu dhidi ya ombi la Serikali la kuongeza maelezo ya nyongeza ya shahidi.
Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa waliopangwa kusikiliza shauri hilo ni:
Mhe. Jaji Mwalija
Mhe. Jaji Muruke
Mhe. Jaji Khamisi
Tu repost kwa wingi wakuu iwafikie watu wengi media zetu haziwezi kufanya hivyo kwahoyo hii ni shughuli ni yetu✊🏽
Wanasiasa Tujifunze: Siasa za Upinzani Tanzania si Ushindani wa Vyama, ni Mapambano ya Maadili!
Katika anga ya kisiasa ya Tanzania, upinzani sio tu jukwaa mbadala la kusaka madaraka—ni mstari wa mbele unaotenganisha mifumo miwili inayokinzana kiitikadi na kiutu. Siasa zetu zimegawanyika kati ya:
• Utu uliotukuka dhidi ya Unyama wa mfumo.
• Uhuru wa kweli dhidi ya Ukandamizaji wa kikatili.
• Haki ya wanyonge dhidi ya Dhuluma.
• Ustaarabu dhidi ya Ukatili wa zama za giza.
• Ulinzi wa Rasilimali za Umma dhidi ya ufisadi
Unapoamua kuondoka upinzani na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), hujabadili tu nembo ya chama au rangi ya sare; umeamua kusaliti mapambano ya kudai Utu, Uhuru, Haki, na Ustaarabu. Umesaliti.
Hapo ndipo usaliti wa mtu mmoja unapokuwa donda ndugu linalovuja damu nyingi sana; linakuwa tukio chungu, tukio la kikatili, na tukio lenye kukatisha tamaa kwa mamilioni ya Watanzania wengi.
Raia wanabaki nyuma wakisaga meno katika tanuru la mateso, umaskini, na hofu. Ni sawa na askari anayeasi mstari wa mbele wa vita na kukimbilia upande wa adui anayeshambulia kijiji chake.
Tukitaka kuelewa tulipo, tutazame jirani zetu, Kenya.
Kenya, wanasiasa wanaweza kutofautiana vikali, lakini wanatofautiana kuhusu ni kikundi gani kitakachoshika usukani wa nchi. Tofauti hizo za uhasama wa kutekana hadi kuua usiowapenda
Hata hivyo, wote—kuanzia rais hadi mwananchi wa kawaida—wanafurahia, wanalinda, na kuogelea katika anga pana ya kidemokrasia na ustaarabu wa kisiasa (Democratic space and civilization).
Rais wa Kenya anaweza kusimama jukwaani, akacheka akijibu mapigo ya wapinzani wake na kusema: “Hawa jamaa wa upinzani hawana ajenda, kazi yao kila siku ni kuniita ‘Kasongo’ tu!”
Pamoja na kejeli hizo za wazi kwa Rais, Hakuna anayetekwa na kupotezwa, hakuna anayemiminiwa risasi, na hakuna anayeuawa kwa kutoa maoni yake. Siasa zao zina ushindani, lakini zina UTU.
Kwetu Tanzania, hali ni tofauti kabisa.
Wakati jirani zetu wakipiga hatua mbele na kulinda hiyo democratic space, kwetu bado tunapambana na siasa za kishamba za kuona anayekukosoa anastahili kufutwa duniani au kuwekewa vizuizi kila kona.
Huwezi kujenga taifa imara kwa kutumia misingi ya uoga na ukatili; taifa bora linajengwa pale ambapo mawazo mbadala yanakaribishwa na kuheshimiwa.
Hapa kwetu, kumtania Rais ni ‘mwiko’ na kumkosoa tu ni kujikana nafsi na kuamua liwalo na liwe! Mazingira ya hofu yanadhihirisha kuwa hatushindani kwa hoja, tunashindana na nguvu ya dola.
Wito kwa Wanasiasa wa upinzani: Simamani Imara!
Ni wajibu wetu sasa kama wapigania haki kushiriki kikamilifu katika hatua zote za kutengeneza mazingira mazuri na sahihi yatakayomruhusu kila Mtanzania kufanya siasa za kistaarabu bila woga.
Na safari hii lazima ipiganwe tukiwa upande wa umma, tukiwa upinzani. mazingira yatakayomruhusu kila kijana, mwanamke, na mzee kufanya siasa za kistaarabu bila hofu ya kutoona jua la kesho.
Siyo lazima kuwa ‘chawa’ wa watawala hawa katili wanaonyanyasa ndugu zenu. Unapoamua kuhama upinzani kwa kufuata tonge la ugali au cheo cha muda mfupi, unapoteza vitu vitatu vikubwa:
(i) Unapoteza Utu wako: Unakuwa mtumwa wa fikra unazozichukia moyoni mwako, huwezi kuziishi.
(ii) Unajifuta kwenye Historia: Unakuwa takataka ya inayokumbukwa kwa usaliti badala ya ukombozi.
(iii) Unasaliti harakati: Unakuwa mshirika wa wale waliomwaga damu na kutesa wapigania haki.
Kama siasa kwako ni utumishi, utumishi wa kweli ni kusimama imara na wanyonge kwenye dhiki, hadi haki yao ipatikane. Tufanye siasa za dhamiri (politics of conscience) badala ya siasa za tumbo na fursa.
Ukikimbilia kwenye meza ya watesi wako ili ule makombo ya meza za ikulu, wewe si mwanasiasa tena; wewe ni mnada wa bei rahisi. Unanunulika. Thamani yako ina bei. Sokoni unanunulika.
Tujifunze, tusimame imara, Aluta Continua!
MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.
Hao ndio watu wasio na dhamira hai. Ni watu wanaoamini kuonea Watanzania wenzao na wanawataka Watanzania wakubali kunyanyaswa na kupuuzwa nao. Lakini wao wakiambiwa matendo yao ni ya kishetani wanahamaki na kulalama kama mtoto aliyenyang'anywa peremende. Wakati wa kuwajibika ni sasa na lazima wawajibike. Watachukuliwa vitandani kama Maduro na afadhali Maduro alikuwa na mkewe wao watachukuliwa wakiwa na mahawara wao.
The chickens are coming home to roost!
Waliopo Dar es Salaam wamekushuhudia leo mahakamani.
Walio mbali na Dar es Salaam, pamoja na wale walioshindwa kufika mahakamani, wamekuona kupitia TV na mitandao ya kijamii.
Na wasio na uwezo wa kufuatilia huko, wameambiwa tu kuwa leo ulikuwa mahakamani.
Ninachotaka kusema ni kwamba kila wananchi wanapokuona au kusikia hata sauti yako, wanapata furaha, hamasa na matumaini mapya na makubwa.
Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda, hasa afya yako iendelee kuwa imara, akupe moyo wa ujasiri na akuondolee hofu ya kukata tamaa.
Mitaa inaimba jina lako comrade🫡
Tundu Lissu will be free 💪🏽 sooner than later 💯
Mark this post!
Yaani madhulmat wanahaha lakini wapi!
No weapon formed against him shall prosper 🙏🏽
Mungu aendelee kujidhihirisha katika maisha yake - tuseme AMEN!
#FreeTunduLissu
Tundu A.M Lissu alikamatwa akiwa Mbinga, Ruvuma Aprili 9, 2025. Tangu tarehe hiyo ya kukamatwa (Aprili 9, 2025) hadi leo (Mei 20, 2026), zimepita siku 406.
Februari 24, 2026, Mahakama Kuu ya Tanzania (Masjala Ndogo ya Dar es Salaam) iliahirisha kesi hiyo kwa muda usiojulikana (sine die). Shauri la msingi likasimama.
Hatua hii ilikuja baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha shauri la mapitio/rufaa katika Mahakama ya Rufani ya Tanzania kupinga uamuzi mdogo wa Mahakama Kuu.
Tangu upande wa Jamhuri ukimbilie Mahakama ya Rufaa na kesi ya msingi kusimamishwa (Februari 24, 2026) hadi leo (Mei 20, 2026), jumla zimepita siku 85.
Tunawauliza Serikali, hamtaki kuendelea na kesi yenu dhidi ya Tundu Lissu? Ushahidi wenu hautoshelezi? Vielelezo vya kuthibitisha kesi yanu vimeyeyuka?
Tunawauliza @judiciarytz, hamtaki kesi dhidi ya Tundu Lissu iendelee? Kwanini tarehe haipangwi baada ya siku 85 kupita? Majaji wa mahakama ya rufaa hawapo?
Kama hamtaki kuendelea na kesi kwa njia za mahakama, muachieni huru Tundu A.M Lissu. Kama mnataka kuendelea na kesi yenu, pangeni tarehe haraka sana.
Vinginevyo, mnaulazimisha UMMA kusimama na kumdai Tundu A.M Lissu. CHADEMA tunamtaka kiongozi wa chama chetu, uraiani. Tunasisitiza, #FreeTunduLissu.
Leo na kesho tuhakimishe #FreeTunduLissu inatrend
Andika post, weka picba weka hashtag nq share, repost kila post hata za zamani za Lissu
Tuwe serious people! Siku 405 ??!!
Agenda zetu:
1. Lissu atolewe bila masharti au kesi iendelee.
2. Katiba mpya.
3. Serikali na bunge wawajibike hakukua na uchaguzi ila vita.
4. Wauwaji wa 29.10.2025 wawajibike na kuwajibishwa.
5. Iundwe tume huru wananchi wachague viongozi wanaowayaka.
Usitolewe ktk agenda hizo.
‼️🚨HATUTAKUBALI LONGOLONGO KWENYE AFYA YA LISSU‼️
Jamani eh! Mdau anadai huko gerezani wanafanya vipimo waje kusema Lissu ana food poisoning sijui madudu gani! Ni hivi masuala ya chakula kuharibika tumboni na kugeuka sumu ama kalishwa sumu hatutaelewa! Kama vipi apelekwe Aga Khan tutamchangia ila afanyiwe vipimo! Na kwa usalama wa nchi MWACHIENI mara moja!
Mlishaonywa na Polepole muache huu upumbavu wa kumweka ndani - yakitokea ya kutokea mtajiteteaje? Mkaishia kumteka na Polepole! Mijitu mikatili ninyi 🚮
#FreeTunduLissu
TAL ni Kiongozi wa Taifa zima si tu wa CHADEMA. Hivyo, ni WAJIBU kila mmoja wetu, pasipo kujali ITIKADI zetu za kisiasa KUHAKIKISHA tunapaza sauti Lissu atoke gerezani. Mahakama IMESHINDWA kufanya kazi kwa UHURU. Lissu atatoka kwa nguvu ya Umma tu. #FreeTunduLissu#FreeTunduLissu