Maumivu na uchungu ambao anapitia mama ake James Temba ni Mungu pekee ndo anaejua.
Halafu unamskia Jaji Chande anasema kama ni watu kutekwa na kupotezwa mbona hata Ulaya wanatekwa.
Serikali haram haijali kabisa kuhusu uhai wa Watanzania ndo maana yanatokea mauaji ya kikatili kama haya.
Pumzika kwa Aman James Temba.🙏😭😭
Gen Z si adui; Ni wateja wa siasa na uchumi wa kesho.
Making Africa Work: A Handbook (waandishi ni Greg Mills, Jeffrey Herbst, Olusegun Obasanjo, na Dickie Davis). Kitabu kinasisitiza kuwa Afrika inapitia ongezeko kubwa la watu kuliko bara lingine lolote.
Mmoja wa waandishi, Olusegun Obasanjo (Rais wa zamani wa Nigeria), ameandika kwamba “Making Africa Work” kunahitaji uongozi wenye maono ya mbali sana, siyo uongozi wa kuzima moto wa maandamano.
Idadi ya watu itaongezeka mara mbili hadi kufikia bilioni 2 ifikapo mwaka 2045. Zaidi ya nusu ya Waafrika wataishi mijini. Kundi hili litakuwa na vijana ambao wanaunganishwa kupitia simu na mitandao ya kijamii.
Hadi kufikia 2050, robo ya idadi ya watu duniani itakuwa Afrika. Ongezeko linaweza kuwa baraka ikiwa vijana watapata kazi na elimu, au likawa janga ikiwa serikali zitashindwa kuweka mifumo ya kiuchumi
Kitabu kinaeleza; Ikiwa (Gen Z) watapewa fursa za kiuchumi, watakuwa nguvu ya mabadiliko na ukuaji (demographic dividend). Lakini ikiwa hakuna ajira, uchumi na fursa, itakuwa janga la kisiasa na kijamii.
Waandishi wa “Making Africa Work” wanaeleza kuwa (Gen Z) wanaishi mijini zaidi na wameunganishwa na mtandao (digital connectivity). Tofauti na vizazi vilivyopita ambavyo vilikuwa vijijini na vilitawanyika
Gen Z siyo Taasisi iliyosajiliwa, ni wazo (Idea). Tofauti na vyama vya siasa ambavyo vina ofisi, viongozi wa kukamatwa, ruzuku za kuzuia, Gen Z ni kizazi chenye itikadi inayozungumza haki, ukweli, na teknolojia.
Gen Z Hawana “central command”. Wao wanakutana ‘online’ tu. Ukimkamata mmoja, wengine elfu kumi wanazaliwa mtandaoni. Huwezi kuua wazo lao ambalo halina ofisi wala msemaji mkuu mmoja. Never.
Gen Z hawana kiongozi mmoja (leaderless movement), hivyo hakuna mtu mmoja wa kumnyamazisha ili harakati zao zifariki. Decentralization haitawezekana kamwe katika Ulimwengu huu wa sasa wa kidijitali.
Habari inasafiri kwa sekunde. Ukijaribu kufunika ukweli mmoja, video 100 zinatokea TikTok au X (Twitter) au Instagram au Facebook. Information speed ni kubwa sana. Huwezi kutengeneza uongo na kuutea uongo.
Usiwaone Gen Z kama adui, waone kama mtaji katika uwekezaji wa baadaye; Wanaishi katika ulimwengu tofauti na vizazi vilivyotangulia. Wao wanafikiria digital, wanataka uwazi, haki, na fursa za kiuchumi.
Huwezi kufungia “spirit” ya watu wanaozungumza lugha moja kupitia mitandao. Washauri wa watawala wanatumia mbinu za karne ya 20 (mabavu, propaganda, na vitisho) kukabiliana na matatizo ya karne ya 21.
Mtawala anayewaona vijana kama maadui anajitenga na uhalisia. Badala ya kutumia nguvu (force), alipaswa kutumia ushawishi (influence). Vijana hawataki kupindua nchi; wanataka nchi ifanye kazi kwa ajili yao.
Kitabu hiki kimeweka msisitizo mkubwa kwamba, Viongozi wanaotaka kuendelea kubaki madarakani lazima waendelee na ukuaji wa kiuchumi wa kweli na kuunda ajira — si kupambana na raia wao wenyewe.
Fanyeni tafiti (research) halisi, si hizi tafiti zenu za uongo za kufurahisha genge; Washauri wa watawala huwaeleza watawala lugha ambayo wanadhani wanayotakiwa kusikia. Hawaelezi ukweli na uhalisia.
Mnatakiwa kutumia data halisi, surveys zisizopendelea upande, na mazungumzo ya moja kwa moja na vijana (bila kuwakamata au kuwatisha). Kuujificha nyuma ya “wanasiasa wana wachochea” ni kukimbia ukweli.
Kitabu kinakataa mifumo ya kufadhiliwa na rushwa (patronage) na kuendesha mambo tu bila mpango (muddling through). Kinasisitiza kuwa ongezeko hili la watu linafanya mifumo ya zamani isifanye kazi tena.
Kitabu hiki kimeandika kwamba, ulinzi wa kweli hautokani na silaha, bali unatokana na raia walioridhika. Kupambana na “Gen Z” ni sawa na kupambana na injini ya gari lako mwenyewe ukiwa barabarani.
Unapochagua mabavu dhidi ya raia wako, unajenga Deep-seated Resentment. Hiki ndicho kizazi chenye nguvu kazi, wabunifu, na walaji wa kesho. Ukiwavunja moyo, unaharibu uchumi wa nchi muda mrefu.
Ukiziba njia zote za kidemokrasia na mazungumzo, unawalazimisha kutafuta njia mbadala ambazo mara nyingi huwa ni za machafuko zaidi. Hapa ndipo inaibuka dhana ya ‘Radicalization’ ili wapate kupumua vizuri.
Kitabu kinaeleza huwezi kuwadhibiti watu ambao wanajua haki zao na wanaona maendeleo ya nchi zingine kwa kutumia mabavu. Gen Z hawawezi kufungwa macho kirahisi. Ulimwengu upo kiganjani.
Badala ya kupambana nao, waweke katika meza ya mazungumzo. Washirikishe katika maamuzi badala ya kuwafanyia maamuzi. Wana maoni makali kwa sababu wanaona matatizo moja kwa moja kupitia mitandao.
Kiongozi unatakiwa kujenga uaminifu mkubwa kupitia vitendo, si maneno; Punguza gharama za maisha kwa vitendo. Pambana na ufisadi bila kuchagua. Toa fursa za kiuchumi kwa vijana (ajira, mikopo, elimu bora).
Tumia mitandao kuwajibu moja kwa moja, si kuwazima ili sauti zao zisikike tena. Msiifungue hiyo mitandao. Msiifanye kama ni majukwaa haramu kuyatumia. Tumia lugha yao kupitia mitandao, memes, na uwazi.
Usiwaone Gen Z kama watu kutoka nje — ndiyo wapiga kura wengi wa baadaye. Miaka mitano ijayo, hawa walio na umri wa miaka 15 had 18 watakuwa na miaka 20 hadi 23 na ndiyo watakuwa wapiga kura wenu wengi.
Watawala mnatakiwa kuanza kufanya town halls za kidijitali na za kimwili (physical) bila kuwakamata. Wajenge uwezo — elimu bora, stadi za tech, na nafasi katika uongozi (youth quotas bunge na serikali).
Tumia Youth Councils na hizi Youth Development Forum ili kupata malalamiko ya vijana. Tumieni data halisi (si kutegemea taarifa za intelligence tu) kuelewa malalamiko halisi ya gharama ya maisha na ajira.
Kitabu kinatoa takwimu Afrika inahitaji kutengeneza mamilioni ya ajira kila mwaka ili kukidhi hitaji la vijana wanaoingia sokoni. Serikali lazima zifanye mageuzi makubwa sana ya kiuchumi (economic reforms).
Toeni mikopo ya vijana (kama SIDO au TIB) bila siasa, anzisheni digital hubs katika mikoa. Tengenezeni National Youth Dialogue Forum na hakikisheni isifanywe kuwa jukwaa la kisiasa la vijana wa mbogamboga.
Vijana si kikwazo, ni kipimo cha uongozi wako; Kiongozi mkubwa si yule anayeshindana na vijana, bali yule anayewaelewa na kuwaongoza kuelekea mustakabali bora. Gen Z wataendelea kukua na kuwa wengi zaidi.
Usipambane na kizazi chako. Kipambane na matatizo yanayowatesa. Kama utawaelewa na kuwahudumia, watakufanya uwe na urithi mkubwa. Kama utawapuuza au kuwapiga, watakuandika kama sehemu ya tatizo.
Kitabu kinathibitisha suluhisho la Afrika siyo bunduki, bali ni sera sahihi, utawala bora, na kutoa nafasi kwa Gen Z kuongoza mabadiliko ya kiuchumi. Mtawala anayewazuia, anazuia maendeleo ya nchi yake.
Watawala someni kitabu, mtaelewa Afrika iko njiapanda. Upande mmoja ni mafanikio makubwa kupitia nguvu ya vijana, na upande mwingine ni machafuko ya kudumu ikiwa mahitaji ya vijana ya kudumu yatapuuzwa.
Huwezi kushinda vita dhidi ya wakati. New generation (hawa ambao tunawaita Generation Z) ni wakati unaokuja, na kamwe, huwezi kuuzuia jua lisioneke kwa kutumia kiganja cha mkono. Msiwachukie Gen Z.
Mimi nimeshauri tu kama mwananchi wa kawaida, mkitaka chukueni ushauri, msipotaka acheni.
MMM, Martin Maranja Masese, Mtikila.
Kitendo cha Magereza na Mahakama kumpeleka Mwenyekiti wetu mahakamani bila taarifa ya mawakili wa chama na chama ni aibu na kutia mashaka sana .
Tumezuiliwa kumuona kiongozi wetu kwa miezi Karibia sita kinyume cha sheria..
Sasa anapelekwa mahakamani kwa siri na kificho nia yenu ni ipi?
Lissu ni kiongozi wa umma haiwezekani kumfanyia mambo ya ajabu kama haya.
Jaribio la kuifuta Chadema ni jaribio la kuzika matumaini ya Watanzania…
Ni jaribio la hatari na halitakubalika… washauri wa hivi ni washauri wanaotaka kuteketeza Nchi yetu kwa tamaa zao…
Watanzania hawatakubali mfute matumaini pekee ya maisha yao.
Tundu A.M Lissu alichaguliwa na mkutano mkuu wa CHADEMA. Hakuna kiumbe mwingine yeyote anaweza kumuondoa zaidi ya mkutano mkuu wa chama Taifa ambao ulimchagua. Hizo porojo nyingine za mazombi ya mbogamboga ni za wapumbavu waliolewa visungura tu na hawaelewi katiba ya CHADEMA.
“Mpinzani wangu wa kisiasa si adui yangu. Tunaweza kutofautiana kuhusu mawazo na sera, na bado tukaishi kama Zambia Moja, Taifa Moja. Hii ndiyo amani ambayo Wazambia wanastahili.” Hakainde Hichilema, Rais wa Zambia leo hii. Itakumbwa kuwa mwezi August wanafanya Uchaguzi Mkuu.
Jaji Mwambegele, Kailima na tume yenu… Nyie ni wahusika wa moja kwa moja ya kile kilichotokea tarehe 29/10.
Nyie kwa kiburi na dharau mmeingiza Nchi yetu kwenye matatizo makubwa…
Mauaji, dhuluma na maumivu makubwa waliyofanyiwa Watanzania.. Nyie ni sehemu ya wahusika wa kupika na kutekeleza huo uovu.
Watanzania hawapaswi na hawatasahau, mpaka haki itakapotendeka.
CAF imesema itaunda TUME YA MARIDHIANO itakayoshirikisha WADAU WOTE ili KUDUMISHA AMANI kwenye FAINALI ZA AFCON 2026. Lengo ni kuhakikisha yaliyotokea tarehe 4 Januari 2026 kwenye MECHI kati ya MOROCCO na TANZANIA, HAYATOKEI TENA.
Kwa ufahamu wa kawaida tu, mtu mwenye akili inayomuongoza kuteka, kutesa, kubambikia kesi, kuua watu kwa ajili ya madaraka, mtu huyohuyo hawezi kuwa na akili ya kujenga nchi. Akili hizi mbili kamwe haziwezi kuishi kwenye kichwa kimoja. Matokeo yake tunajionea wenyewe.
VIDEO:
Askofu wa Kanisa la Uamsho la Moravian Tanzania, Emmaus Mwamakula amesema yeye hajawahi kuwa swahiba (rafiki wa karibu) wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) bali amekuwa ni mtetezi wa haki nchini kwa yeyote ambaye haki inaonekata kupokwa au kutaka kupokwa.
Askofu Mwamakula ameyasema hayo alipozungumza na Jambo TV katika mahojiano maalum jijini Dar es salaam.
"CHADEMA imeumizwa, Polepole ametekwa, nilipiga kelele sana hivyo yeyote anapoumizwa nakuja kumtetea", amesema Askofu Mwamakula.
Force Exclusive:
Mwanasiasa mkongwe na mchambuzi wa siasa, Said Miraj, ametoa mtazamo wake kuhusu mabadiliko ya uongozi ndani ya CHADEMA, akisema tofauti ya mitazamo kati ya Freeman Mbowe na Tundu Lissu ndiyo iliyopelekea nguvu kubwa ya mabadiliko ndani ya chama hicho.
Nani anaweza kusema huu ni uongo…
Bunge la hovyo lisiloweza kusimamia serikali..
Tulia na bunge lake waliogopa kujadili hata suala la utekaji, kama hauwezi kujadili jambo hilo la wananchi upo kwaajili ya nani?
Kuna sababu gani ya kuwa na muhimili unaitwa bunge kama hausaidii wananchi?
Bado Tulia na kujipendekeza kote!!!!
“CHADEMA inapigania uchaguzi wa uhuru na haki nchini, na wanashindana na CCM ambayo pia inaendesha shughuli zake kwa njia zinazokosoa uhuru huo. Kwa hiyo, ilikuwa lazima CHADEMA iwe mfano wa uchaguzi wa uhuru na haki, na ndiyo maana walikubali kuwahusisha wanahabari" Said Miraj