#TajiriLaKihaya
KUNA MASWALI MAKUBWA YANAYOPASWA KUJIBIWA MUHIMBILI NA JKCI.
Leo familia yetu imepoteza mdogo wetu. Moyo wangu umejaa huzuni, uchungu na maswali mengi ambayo hadi sasa hayajajibiwa.
Siku ya kwanza nilipofanikiwa kumpeleka mdogo wangu JKCI na kupata chumba cha VIP, nilifurahi sana. Niliona kama tumepata mwanga wa matumaini. Baada ya vipimo, tuliambiwa tatizo lake la moyo lilihitaji upasuaji mdogo tu na angeweza kuendelea na maisha yake kawaida.
Tukaahidiwa upasuaji ungefanyika ndani ya siku mbili au tatu.
Lakini siku zikageuka wiki.
Kabla hata ya kulazwa, tulikuwa tumepambana kwa zaidi ya mwezi mzima tukizungushwa kutoka leo hadi kesho. Mara daktari hayupo, mara jopo la wataalamu halijakaa, mara kipimo kirudiwe, mara tusubiri dawa zifanye kazi kwanza. Kila siku ilikuwa ni ahadi mpya na tarehe mpya.
Baada ya kulazwa tuliamini safari ngumu imekwisha. Lakini ndipo mateso makubwa zaidi yalipoanza.
Mdogo wangu aliingia hospitalini akiwa bado anaweza kutembea, kuongea, kula na kujitambua. Kila siku tulisubiri upasuaji ulioahidiwa, lakini haukufanyika. Badala yake hali yake ilianza kuzorota mbele ya macho yetu.
Wiki moja ikapita.
Wiki mbili zikapita hadi wiki tatu
Hakukuwa na upasuaji.
Kulikuwa na sababu mpya kila siku.
Kisha tukahamishwa kutoka chumba tulichokuwa tumepewa kwa madai kuwa kingefanyiwa fumigation. Lakini usiku huo huo mgonjwa mwingine akawekwa kwenye chumba hicho. Hadi leo hatujui ukweli ulikuwa nini- lazima UFISADI ULITUMIKA HAPA!
Tulihamishiwa chumba kingine JAPO kilikua VIP… ila hakikua kwenye standard sawa!
Hata nakumbuka kuna Daktari wa Kihindi alikuja kusoma vipimo akasema ile MONITOR haipo sawa! Mapigo ya moyo na oxygen haisomeki kwa usahihi…
Sasa kwa nn tulihamishwa chumba? Kutoka chumba kizuri kuja hiki?? Kwa nn kile tulichokuwepo alipewa mwingine usiku huo tumehamishwa? CORRUPTION!
Baada ya hapo hali ya mdogo wangu ilizidi kuwa mbaya zaidi. Akapoteza nguvu, akashindwa kuzungumza, akashindwa hata kuwatambua watu waliomzunguka.
Tulikuwa tunauliza maswali. Tulikuwa tunaomba msaada. Tulikuwa tunaomba hatua zichukuliwe haraka.
Lakini muda uliendelea kwenda.
Leo asubuhi mdogo wangu amefariki dunia.
Siandiki haya kwa hasira pekee. Naandika kwa maumivu ya familia iliyokuwa na matumaini makubwa ya kumuona mpendwa wao akirudi nyumbani akiwa mzima.
Kama kweli kulikuwa na uzembe, kucheleweshwa kwa huduma, ukosefu wa uwajibikaji au mifumo mibovu ya utoaji huduma, basi kuna haja ya uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa. Maisha ya Watanzania yana thamani. Wagonjwa hawapaswi kupoteza maisha wakisubiri tarehe nyingine, kikao kingine au ahadi nyingine.
Tunataka majibu.
Tunataka uwajibikaji.
Na zaidi ya yote, tunataka familia nyingine isipitie maumivu tuliyoyapitia sisi.
Kama hapa ni VIP… je wagonjwa wa kawaida wanapata huduma gani???
Pumzika kwa amani mdogo wangu. Tulipambana kwa kila tulichoweza. Mungu akupokee katika makao ya milele. 💔🕊️
Kadıköy Rıhtımı’nda yapımına başlanan cami hakkında konuşan Kadıköy sakini:
Camiye ihtiyaç olduğunu düşünmüyorum. Kadıköylü gitmez, dışarıdan gelirler. Bir süre gelirler Çamlıca Camii gibi, sonra yok olurlar.
هكذا أصبح المنظر في جزيرة "لامبيدوزا" الإيطالية بعدما وصلها أكثر من 10,000 مهاجر غير شرعي عبر القوارب من أفريقيا وأصبح عددهم أكثر من عدد السكان الذي يبلغ 6,000 نسمة فقط.
بعض التقارير تقول أن عددهم وصل إلى 18,000 مهاجر ووصف الإيطاليون ما حدث بالغزو
Tigers are naturally solitary, valuing space, silence, and independence.
Lions, on the other hand, are social and always surrounded by their pride, sometimes getting way too comfortable in shared space
It’s a fascinating contrast in the wild one prefers solitude and control of its territory, while the other thrives in closeness and group energy, even if it means occasionally invading personal space
In a bold statement, Trump Claims U.S. Victory Over Iran Amid Strait Tensions, sparking debates about the implications for foreign policy and regional stability. What do you think this means for the future?
R-Truth is making waves again! His incredible charisma and unmatched energy continue to capture fans' hearts. Whether in the ring or on the mic, he proves that age is just a number in wrestling. #RTruth
Just saw all the buzz about Fabio! It's fascinating how his influence is still making waves in culture today. Can't believe how many people resonate with his iconic style and charisma. #Fabio
Just when you think you can trust the digital currency world, stories about #CryptoScam pop up like weeds. Stay vigilant, do your research, and don't let greed cloud your judgment.
Just saw a discussion about how far 100 USD can really go these days. It’s crazy to think about inflation and rising costs. What do you think is the best way to make the most of it? #100USD