Namshukuru Mwenyezi Mungu jana baada ya kula kiapo cha uaminifu mbele ya Mkuu Mkoa wa Morogoro Mhe. Fatma A. Mwasa (leo) Jumamosi 28 Januari 2023 nimeripoti Rasmi kituo changu cha kazi Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilosa tayari kwa kuanza utekelezaji wa majukumu ya kiserikali.
Namshukuru Mwenyezi Mungu, Ijumaa 27/01/2023 nimeandika historia kwa kula kiapo cha uaminifu, utumishi serikalini. Kwa dhati kabisa namshukuru sana Rais JMT Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuniamini na kuniteua kuwa Mkuu wa wilaya ya Kilosa, Morogoro.
#KaziIendelee
Hakika umestahili Shahada hii ya heshima inayotambua weledi wako kwenye masuala ya uongozi, utawala, nadharia ya maendeleo ya uchumi, Jamii na siasa.
Hongera sana Dkt Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
#KaziIendelee
Chama Cha Mapinduzi na watanzania wazalendo tunaridhika na tunajivunia utendaji na uchapakazi wa Rais Ndugu Samia Suluhu Hassan. Tutayasema na kuyatangaza yote mazuri unayoifanyia Nchi yetu ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2020-2025.
#CCMImara#KaziIendelee
Rais Samia Suluhu Hassan anaishi kwa vitendo misingi, dira, muelekeo na maono ya Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere. Miaka 23 kumbukizi ya Kifo chake, Umoja na mshikamano umeendelea kutamalaki katika Taifa.
Mkutano Mkuu wa uchaguzi wa viongozi CCM Wilaya Dimani, Oktoba 2, 2022, Nimeelezea juu ya mpango na umuhimu wa CCM kuwajengea uwezo viongozi wapya waliochaguliwa, ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mkti wa CCM Taifa Ndugu Samia Suluhu Hassan katika hatua ya kujiimarisha zaidi.
Oktoba 01, 2022nimekuwa miongoni mamia walioshiriki mbio za NMB zilizofanyika viwanja vya Leaders Kinondoni, DSM, Kauli mbiu 'Mwendo wa Upendo' zilizolenga kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu ya Fistula kwa wanawake wenye tatizo hilo kupitia CCBRT.
#CCMImara#KaziIendelee
Ukihesabiwa
Tukihesabiwa
Nikihesabiwa
Tutakuwa, Tumehesabiwa, Shiriki Sensa ya watu na Makaazi 2022.
Mimi nimehesabiwa wewe jee?
#Sensakwamaendeleo#Tujitokezekuhesabiwa
Siasa na darasa kwa vitendo................
Cde. Abdulrahman O. Kinana ni Chuo Kikuu cha Siasa kinachotembea, tunayo mengi ya kujifunza kwake gwiji la siasa za ndani na nje nchi.
#CCMImara#KaziIendelee
Watanzania ni mashuhuda wa hatua ambazo serikali inachukua chini ya Rais Samia Suluhu Hassan zinavyozaa matunda ikiwemo biashara kufufuliwa, biashara mpya kufunguliwa na biashara kurejeshwa nchini. Hivyo Chama tunampongeza kwa dhati Mhe Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri.
Tulipotoka ni kuzuri, Tulipo ni kuzuri zaidi, Tunapokwenda matarajio ni Makubwa zaidi.
Ziara katika vyombo vya habari Wasafi TV, Habari leo, Mwananchi na Azam TV 04 Julai 2022.
#CCMImara#KaziIendelee
Nilipata nafasi ya kumtembelea na kumfariji Bi Amina Amos Mkazi wa Simiyu, Mama mzazi wa Watoto Pacha waliokuwa wameungana Rehema na Neema waliofanyiwa Upasuaji wa kuwatenganisha mnamo 01 Julai 2020 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar Es Salaam.
#ChamaImara#KaziIendelee