#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 230
Anaendelea Mhe. Lissu.
Waheshimiwa Majaji naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo, maombi haya yameletwa kwa lengo moja tu kurefusha mashauri na kuchelewesha kesi ya msingi ili mjibu maombi aendelee kukaa Ukonga gerezani.
Leo ni siku ya 139 kesi haifanyiki na mimi nakaa Gerezani I'm completely innocent but I'm in prison kwa mwaka mmoja na miezi mitatu.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania article 59.b.4 inazungumzia mamlaka ya DPP kutokuchekewesha muenendo wa Mahakama.
Kuzuia Mahakama kuu kuendelea na kesi kwa siku 139 kwa kuleta maombi ambayo wanayajua hayana msingi wowote, kama hii ni kutenda haki then inabidi tutafute tafsiri nyingine ya neno kutenda haki.
Mamlaka ya DPP ni kuwezesha uamuzi wa haki, wa haraka na usiokuwa wa gharama kubwa.
Niko Mahabusu muda wote huo je hiyo ni haki? DPP na Mawakili wake wamepuuza mamlaka ya kikatiba ya DPP kwa maneno yao wenyewe walishabakiza shahidi mmoja lakini haijaendelea kwa siku 139 kwa sababu ya maombi haya.
Mhe. Lissu anasema ombi langu siyo tu Mahakama hii iyakatae maombi hayo siyo tu hilo, maombi yangu Mahakama ya rufani ina mamlaka ya kutoa amri ambazo zingetolewa na Mahakama kuu.
Kwa kutumia kifungu cha 367 cha kutaka mleta maombi anilipe fidia kwa kunifanye nikae gerezani kwa siku 139 bila kesi kuendelea kwa sababu ya maombi yake.
Yakataeni haya maombi na muamuru DPP anlilipe fidia kwa usumbufu wote alionifanyia.
Mhe. Lissu anasema ni hayo tu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya rufani.
Anasimama Wakili wa Serikali Katuga.
Anasema tumeleta maombi yetu na tumeiomba Mahakama hii tukufu kwamba tumenyimwa haki ya kusikilizwa kwenye huo ushaidi tunaoomba uongezwe, ulikataliwa kabla ya kufika katika hiyo mahakama.
Mjibu maombi ameialika Mahakama hii kwenye proceedings kuanzia pg 391 akizungumzia submission ya uhalali wa notice yetu, tulipata nafasi ya kusikilizwa kuhusiana na notice yetu siyo nafasi ya kusikilizwa kuhusiana na huo ushahidi.
Hatueleweki harafu tunaambiwa tumefanya clever drafting, ushahidi umekataliwa kabla ya kuingizwa, tulisikilizwa kwenye notice tu.
Mjibu maombi anaposema tulipewa haki ya kusikilizwa hakutuelewa kwenye angle gani. Kuirejesha Mahakama hii katika kifungu cha 308 anasema ni kuomba rufaa kwa Mahakama hii sisi tulikuwa tunaonesha walichokifanya na kilichotakiwa kufanyika.
Katunga anaendelea kusema
Sisi hatujaleta maombi haya kuchelewesha kesi tumekuja hapa kuiomba Mahakama iwese kutafsiri Sheria. Kifungu cha 367 kinatumika pale Mahakama inapokuwa imesikiliza kesi na kuona kwamba kesi ni ya kutengenezwa.
Kwa mujibu wa Sheria tunasema maombi yetu ni ya muhimu tunaomba yakubaliwe na yatazamwe na kuita hizo proceedings kuangalia kile ambacho tunakilalamikia.
Jaji anasema basi baada ya kusikiliza pingamizi la awali pamoja na maombi haya tutakwenda kuamua kwanza kuhusu pingamizi la awali kama tutakuwa tumekubali basi itaishia hapo kama pingamizi litakataliwa basi tutaendelea.
Tutawajulisha tarehe ya uamuzi.
Inapigwa Court ya kinyonge ni kama jamaa mchana umepita kama upepo.
Nawatakia Ijumaa njema.
Julai 7, 2026 tukutune barabarani, usihau kubena bango lako lenye ujumbe wa madai yetu ya msingi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 229
Anasimama Mhe. Lissu.
Anasema baada ya kusikiliza hoja za Wakili wa mleta maombi naomba nianze kwa kunukuu maneno ambayo Mahakama hii iliyasema kwenye kesi ya Commissioner General of TRA Criminal case namba 62/2022 pale ambapo maombi ya mdaawa yamezuiliwa na sheria, hawezi kufanya drafting ya kuhadaa Mahakama.
Wanasema uamuzi ulifanyika bila wao kusikilizwa, mgogoro ulianza 19 February 2026 ukurasa 391 wa record, Ugomvi ambao umetuleta hapa ulianza siku Tano kabla ya maamuzi ya Mahakama.
Wakili wa Serikali mkuu Renatus Mkude alisema "waheshimiwa Majaji tuko tayari kuendelea na mashahidi 3 lakini kabla ya kuendelea tuna notice of additional substance of evidence, ambayo imejazwa electronically siku ya Jana"
Katika ukurasa wa 392 Mahakama ikaamua kuwa tuendelee na mashaidi kwanza baadae tutarudi kwenye hoja za notice.
February 20, 2026 ukiangalia ukurasa wa 405-419 utayaona maneno niliyoyasema.
Mahakama ikaamua tumesikiliza sehemu zote kesi hii anahairishwa hadi jumatatu ilikuwa 23 February 2026 kuanzia ukurasa 420 unaonesha hayo.
Mkude akasema wako tayari kuendelea na Katuga akafanya submission in chief pg 421, 423 Katuga akajibu PO, nikafanya rijoinder, pg 428 kuna ruling of the court.
Baada ya submission ya Renatus, submission in chief ya Katuga, rejoinder yangu na reexamination in chief ndipo Mahakama ilitoa uamuzi.
Kwa record hiyo yote nguvu ya kusema hawakusikilizwa wanaitoa wapi?
Kwasababu ya maombi haya leo ni siku ya 139 kesi haiendelei kwa sababu ya uongo wao kwamba hawakusikilizwa.
Haki ya kusikilizwa ni haki ya kikatiba ni kweli sasa kwa ushaidi huu wanawezaje wakasema hawakusikilizwa?
Mmemsikia Wakili Katuga akisema Mahakama ilikosea ilipaswa iangalie reasonablity ya hiyo notice, ipokee ushaidi, iangalie competence kisha iamue.
This is an appeal under 6.3 wanayoitaja, it's only clever drafting inayolenga kuiadaa Mahakama.
Iangalie TRA vs New Musoma textile industry kwenye orodha yangu ni kesi namba 7 hawaruhusiwi kuleta malalamiko kuhusiana na hiyo notice kwenye Mahakama hii. Kifungu 6.3 cha AJA mamlaka ya Mahakama hii siyo hiyo wanayoiomba wao.
Ukurasa wa 21 unaonesha mjadala mpana wa ninachokisema sasa na inamaliza huu mjadala, hamuwezi kuanza kuangalia hiki kilicholetwa ni kitu gani mnapaswa kutazama je huu uamuzi ni legal.
Wanasema hawakusikilizwa mnaangalia kwenye record, Je ni kweli hawa watu hawakusikilizwa, hamuendi kwenye huu usikilizwaji ulikuwaje, Mahakama hii haiangalii mambo superficial.
Waheshimiwa Majaji mleta maombi alisikilizwa hivyo ruling ya mahakama ni legal, imeandikwa na Majaji wenye mamlaka baada ya kusikiliza pande zote hata kama hauwafurahishi wanapaswa kukubaliana nao.
Waheshimiwa Majaji waleta maombi hawana hoja yeyote ya maana on the basis of this record. Section 308 ya CPA imetajwa kwa lengo la kuwaalika mtengue kilichoamuliwa na Mahakama kuu nawaombeni msiende huko.
Nitasema kwa kifupi sana juu ya section 308 ya CPA na nini Mahakama ilisema inakataa kuongezwa kwa ushahidi mpya inadeal na Shaidi mpya tu.
Inazungumzia ni katika mazingira gani shaidi ambaye hakutajwa kwenye commital proceedings anaweza kuongeza kwenye trial, mleta maombi hapa analeta ushahidi mpya wa shaidi ambaye ametajwa kwenye commital na siyo shaidi mpya kama Sheria inavyotaka.
Anaendelea Mhe. Lissu
Kwenye uamuzi huu hakuna sehemu ambayo Mahakama imesema ushaidi huo haufai bali imesema ni ushahidi mpya na haufai kisheria.
Hii clever drafting in order to avoid the legal power, kama wanataka kupinga uamuzi huo wasubiri kesi iishe kisha wakapinge uamuzi huo.
Part 230 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 228
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa Waheshimiwa Majaji naomba nimalizie nisiwachoshe.
Hoja yangu inahusika na maamuzi ambayo hayamalizi kesi, kesi bado ipo na tutakapoenda kwenye substance nitawaoneshe Majaji kwenye hicho walichokileta wao wenyewe ambavyo kesi bado inatusubiri.
Kwa bahati mbaya wametupotezea muda sana hivyo nawaombeni Waheshimiwa Majaji mkatae maombi hayo.
Anasimama Katuga anasema Waheshimiwa Majaji maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii na kanuni ya 65 kanuni ndogo ya 1. Waheshimiwa Majaji ukisoma notice yetu inataja kifungu cha 6 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii, Waheshimiwa Majaji lalamiko la mjibu maombi lisingekuwepo kama angeipitia kanuni ya 48.
Jaji anamwambia Katuga ulishamaliza usilete jambo jipya nenda moja kwa moja kwenye maombi.
Katuga anaendelea
Waheshimiwa Majaji maombi yetu yamejikita kuiomba Mahakama hii tukufu iweze kuangalia uhalali na usawa wa muenendo wa shauri lililoko mbele ya Mahakama kuu.
Maombi haya yametokana na mzizi wa upande wa Jamhuri kuleta notice ya kuongeza ushaidi ambao haukusomwa wakati wa commital na upande wa Jamhuri ulifanya vile kuendana na kifungu cha 308 cha CPA, kifungu hiki Waheshimiwa Majaji kinaweka zuio kwamba hakutakuwa na ushahidi ambao utaongezwa Mahakamani kama ushahidi huo haukusomwa hautaruhusiwa kuongezwa unless upande wa Jamhuri utatoa notice ya kuongeza ushaidi huo.
Tunatakiwa kutoa notice ili mshitakiwa asikutane nayo by surprise, kifungu hicho kinaitaka Mahakama wakati inafanya reasonablity ya notice ifanye vitu gani.
Mahakama wakati inatakiwa kutambua reasonablity ya notice inapaswa kuzingatia kifungu cha 308 kifungu kidogo cha 3 inatakiwa kuuchambua ushaidi wenyewe.
Naona Job Mrema ni kama kambonyeza Katuga ameinama sijui wanaongea nini na wenzake,
Halafu sio mara moja kila baada ya sentence kadhaa vikao vinakuwa vingi.😤
Anaendelea Katunga
Mahakama ilienda kuangalia huo ushahidi katika ukurasa wa 431 wa muenendo wa Mahakama kuu na kuita ni ushaidi mpya umekusanywa baadae na hivyo wamekataa.
Ushaidi unakatakiwa pale ambapo unakuwa umefikishwa Mahakamani baada ya kuwa umepimwa ndipo Mahakama inaamua uingie au usiingie, upokelewe au usipokelewe lakini hauwezi kuamuliwa wakati unakuwa introduced.
Kifungu cha 308 kimetoa nini Mahakama inafanya, ndo maana kwenye maombi yetu tunasema tumenyimwa haki ya kusikilizwa in relation na huo ushahidi.
Haki ya kusikilizwa ni haki ya kikatiba, maana ya hii haki ya kusikilizwa ni kumpa mtu haki ya kumsikiliza full kwa utimamu ndo maana Mahakama ina vitu vitatu vya kupima.
Ushaidi unapimwa unapokuwa umefika Mahakamani, kusema ushaidi ni mpya usiletwe ni kuukataa ushaidi kabla hata haujafika Mahakamani.
Mahakama hata haikuusikia ushaidi lakini ikaenda kusema ushaidi huo ni irrelevant.
Utaratibu wa proceeding ulikuwa umekiukwa na ukiukaji ambao unaenda kwenye shauri yenyewe na ndiyo maana upande wa Jamhuri tukaona kwa busara zenu muangalie hizo proceedings hatuwezi kuendelea na hizo illegalities.
Anaendelea Katuga
Tunataka Mahakama iangalie ni kwa namna gani kwa muda gani ushaidi unaangaliwa na kuwekwa kama ushaidi.
Kwenye kifungu hakuna sehemu tuliposema Mahakama iende ikaupime huo ushahidi ilikuwa ni notice tu, ushaidi kuja Mahakamani na kufukuzwa kabla ya kusikilizwa huko ni kutunyima haki.
Ni vigumu kupima ushaidi ambao hauko hata mahakamani.
Ukurasa wa 431 wa proceedings naomba muuangalie waheshimiwa Majaji, jambo hili lilikiuka taratibu za mienendo ya proceedings.
Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya rufani tunaomba maombi yetu yaangaliwe na yakubaliwe.
Waheshimiwa Majaji ya kwetu ni hayo tu.
Part 229 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 227
Anasimama Wakili wa Serikali Mrema
Anasema naomba kuongeza kidogo kwenye mawasilisho yaliyofanywa na Wakili mkuu wa Serikali Katuga, naomba kuongeza yafuatayo.
Waheshimiwa Majaji hii obligation inayowasilishwa mbele ya mahakama ya rufani lazima iwe na uwezo wa kuondoa shauri hilo lililoko mbele ya Mahakama hii, nikirejea shauri alilolilejea, shauri la DPP dhidi ya Mohammed Ussi naomba kuialika Mahakama hii kwenye kifungu cha 5 kifungu kidogo cha 2.
Mleta maombi amefanya reference kwa kifungu ambacho kimepitwa na wakati it's not applicable.
Kifungu hiki kukihusianisha na kesi ya Mohammed Ussi na kukileta kwenye Sheria ya sasa it's not applicable.
Kifungu cha 8 kinazungumzia mashauri ya madai, swali la kujiuliza ni je shauri hili ni la madai.
Jaji anawasha kipaza anauliza. Katuga ulisema Mrema anaongezea sasa mbona anarudia yaleyale.
Watu wanacheka😂😂😂😂😂
Jaji anamwambia Mrema aendelee ila asirudie mambo ambayo tayari Katuga ameongea.
Mrema anasimama anasema waheshimiwa Majaji ni hayo tu.
Watu wanacheka maana ni kama alichosema Jaji kimemto kabisa Mrema kwenye mood.😂😂😂😂
Anasimama Mhe. Lissu
Waheshimiwa Majaji naomba mniruhusu nijibu hoja za waleta moambi.
Wanacholalamikia siyo order wanalalakikia findings.
Waheshimiwa Majaji wanacholalamikia wamekileta wenyewe kwenye hati yao ya maombi hicho kiko kati ya ukurasa wa 428-431 wanalalamikia rulling, uamuzi.
Uamuzi wanaoulalamikia unajadili ushaidi wanaotaka kuuingiza, na Mahakama ikajadili ushaidi huo kwamba ni kinyume na Sheria hautaingizwa.
Kama wasingekuwa wanalalamikia hii ruling wasingeileta mbele ya Mahakama yako. Finding is not similar to a decision.
Waheshimiwa tuasume Mawakili hawa wako sahihi finding is similar to decision, tuangalie Mahakama inasema nini juu ya aina hii ya ushaidi, Mahakama ikasema ni kinyume na Sheria hauruhusiwi kuingia.
Mawakili waleta maombi wameleta kesi muhimu sana kesi ya Peter Michael Madeleka, kuna mahali katika kesi hiyo ambako Mawakili wa Serikali wamepakimbia kama ukoma, ukurasa wa 9 Mahakama ilisema hivi kuhusiana na hicho kifungu hayampi mamlaka ya kuimove Mahakama.
Mhe. Lissu anawambia Mawakili wa Serikali ahsanteni sana kwa kuleta kesi ya Madeleka.
Watu wanacheka 😂😂😂😂 maana akina Katuga wameleta kesi ambayo badala ya kuwasaidia kumkandamiza Mhe. Lissu yenyewe ndo imekuwa msaada kwa Mhe. Lissu.
Anaendelea Mhe. Lissu
Mamlaka ya Mahakama ya rufani kuitisha Suo moto ni mamlaka yake yenyewe haiwezi kuwa moved na waleta maombi.
Kama Mahakama haijaiona yenyewe haiwezi kuletewa maombi.
Wanasema nisiwafundishe lakini mkiangalia record waliandika barua, walileta maombi kisha wakaandika barua wanataka kuimove Mahakama.
Katuga amesema maombi yao wameyaleta under 6.3, Waheshimiwa Majaji nawaomba muangalie maombi hayo kama kuna sehemu wametaja kifungu hicho. In their notice of motion hakuna sehemu wametaja ni 6 ipi kati ya vifungu 6 vya Sheria hiyo hawawezi kuja hapa kuzungumza kitu tofauti na maombi yanavyozungumza.
Nirudi kwenye hoja ya Job Mrema, mmealikwa Majaji kukubaliana na hoja kwamba Sheria imeshabadilika ni vifungu tofauti, Waheshimiwa Majaji mimi nina revised Act of 2023 inasema section 5 haina marekebisho ya kabla ya 2023 kwa hiyo hii hoja ya kwamba kuna Sheria imebadilika ni vitu tofauti ni hoja ambayo nachelea kusema haina mashiko.
Waheshimiwa Majaji wakili ametaja rule 48.1,
Waheshimiwa Majaji inazungumzia PO must have a capacity to dispose of application na kwa maana hiyo anasema pingamizi langu halina uwezo wa kumaliza madai,
Je kwenye hoja ya kwangu hii kwamba maombi haya hauruhusiwi kwasababu hayana uwezo wa kuyafuta maombi kama inasema imeletwa chini ya kifungu cha 8.2.d? hakuna hoja hapo.
Part 228 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 226
Anaendelea Mhe. Lissu.
Waheshimiwa Majaji uamuzi uliotolewa na Mahakama ya rufani katika kesi ya Katibu Mkuu wa CHADEMA na bodi ya wadhamini wa CHADEMA vs Saidi Issa Mohammed na wenzake inasema kwamba kama mdaawa (Mleta maombi) analeta maombi mwenyewe ni yale yaliyoko kifungu cha 6 kifungu kidogo cha e, maombi mengine ni Mahakama yenyewe ndiyo inaamua bila kusukumwa na yeyote au kuletewa maombi yenye hati ya kiapo.
Waheshimiwa Majaji kwa vyovyote vile maombi hayo hayako halali mbele ya mahakama hii kwani hayakuletwa katika utaratibu wa kisheria kwani Mahakama hii haijaamua maombi haya yaje yenyewe Suo moto kwa hiyo Mahakama isikubali kusikiliza maombi hayo kwasababu ambazo nimezisema.
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa waheshimiwa Majaji sijui kama mnaniruhusi niendelee au wajibu kwanza.
Jaji anasema Jamhuri wajibu kwanza PO kisha tutaendelea.
Anasimama Wakili Katuga anasema Waheshimiwa Majaji tukirejea mapingamizi yake ya awali yameletwa chini ya kifunga cha 8.2.d hiki ni kifungu mahususi kwa mashauri ya madai.
kifungu hiki kilikopwa kikatumika kwenye madai kwenye mashauri ya rufaa, hata kama Mahakama yenu tukufu kwa rejea hizo za Mahakama hii ikakikopa kitumike kwenye maombi yetu haya bado tunasema kwamba maombi yetu yako sahihi mbele ya mahakama hii tukufu tofauti na kile ambacho mjibu maombi amekileta kama pingamizi la awali.
Maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 specifically kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya Mahakama. Kanuni ya 65 na kanuni ya 45 ya kanuni za Mahakama ya Rufani inasuport maombi yetu.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa Majaji ukiyasoma maombi yetu kwenye notice of motion hakuna sehemu yeyote tunayoiomba Mahakama hii tukufu ipitie order ya Mahakama au uamuzi wa Mahakama, pale mwisho tunasema Mahakama idiscuss kukataa ushahidi hatujazungumzia kukataa notice, sisi tunazungumzia kuuchambua na kuukataa ushahidi.
Hakuna sehemu kwenye maombi haya tunalalamikia order, Mahakama yenu itaona kwamba pingamizi la mjibu maombi limekuwa mislead hakuconsue sawasawa maombi yetu.
Pale ambapo neno or litatumika kwenye Sheria yeyote maana yake maneno haya hayako similar yanatumika tofauti, Waheshimiwa Majaji nimewarejesha humu muweze kukitafsiri kifungu cha sita. Haya maneno yanatakiwa yatafisiriwe tofauti hayaendi pamoja ama hayategemeani, inaweza kuwa kimoja wapo kati ya haya.
Kama mahakama yenu imekikopa kifungu cha 8.2.d kinazungumzia katazo la decision or order ndo hauwezi kuziombea appeal or revision.
Sasa tunapata wapi nguvu za kuleta pingamizi kwa tafsiri hiyo tunaiomba Mahakama hii ikaangalie maana ya maneno haya.
Waheshimiwa nawarejesha kwenye kamusi kwa sababu nayo ni kati ya vitu vinavyopaswa kutumika kutafsiri Sheria. Katika ukurasa wa 129 kamusi inadefine order ni nini?
Kwenye application yetu hakuna sehemu tumeombea decision or order, kwenye kifungu cha 8 hata kama kimekopwa hakiwezi kucocer maombi yetu.
Mahakama yenu ilishawahi kuiamulia hili kwenye kifungu 394 cha CPA, katika kesi ya Peter Michael Madeleka dhidi ya jamhuri.
Kutaja kitu fulani means exclusion ya kitu kingine, kitendo cha kifungu cha 8 kutaja findings and order means haijatuzuia kwa maana hiyo findings hapa haijazuiwa kwa maana hiyo tunachotaka kuiambia Mahakama yako ni kwamba ule ushahidi ulikataliwa kabla ya wakati wake.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa naomba niishie hapo kwenye hilo ili tusiende mbali kwa kuyasema hayo mtaona kwamba kesi ambazo mshitakiwa amewapitisha ni distinguishable kwenye mazingira yetu.
Hii kauli ya kwamba hatuna mamlaka ya kuomba Mahakama iitishe ‘Suo moto’ sisi tunasema mamlaka tunayo.
Katiba anasema naomba Mrema anisaidie anayo nyongeza.
Anasimama Wakili wa Serikali huyu anaitwa Job Mrema anakipara kama Mrema wa ubwabwani, sijui na yeye huwa anakunywa visungura kama mwenzake, anyway
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo July 3, 2026
Last time kwenye ya Uhaini dhidi ya Mhe. Lissu tuliishia part 224 so leo tunaendelea na -;
Part 225
Mheshimiwa Tundu Lissu anaingia ndani ya chumba cha mahakama, ukumbi namba 01 wa Mahakama Kuu.
Anaonekana mwenye tabasamu na furaha usoni kwake kama ilivyo siku zote.
Upande wa Jamhuri wapo kama kawaida yao
Inapigwa Court…..
Jopo la Majaji watatu wanaingia,
Kesi inatajwa
Anasimama Wakili wa Serikali anajitambulisha jina lake Ajuaye kisha anatambulisha Mawakili wenzake.
Jaji anaamuliza Mhe. Lissu kama yupo tayari
Mhe. Lissu anasema yuko tayari kuendelea.
Kama kawaida yao anasimama Wakili wa Serikali Katuga kuweka pingamizi.
Mhe. Lissu anapendekeza maombi yake ya sikilizwe kwanza ndo pingamizi lao lijibiwe.
Majaji wanasema tuanze kwanza kusikiliza PO, kisha taratibu nyingine zitafuata.
Anaanza Mhe. Lissu Waheshimiwa Majaji kesi hii inatokana na maombi namba 19065 ya mwaka 2025, Juu ya maombi ya kuongeza ushahidi katika muendelezo wa kesi, uamuzi wa tarehe 24 February 2026 wa Mahakama Kuu wa kukataa kuingizwa kwa ushahidi mpya.
Waheshimiwa Majaji uamuzi wa February 24, 2026 ni uamuzi mdogo, uamuzi ambao haujamaliza shauri na kwa mantiki hiyo kisheria kabisa haupaswi kukatiwa rufaa au pingamizi.
Waheshimiwa Majaji wa rufaa, Mahakama hii katika kesi ya Mkurugenzi wa Mashitaka dhidi ya Mohammed Mussa Ussi criminal appeal namba 521 ya mwaka 2023 Mahakama ikiwa imeketi Zanzibar ilisema msingi wa kukataza rufaa ama mrejesho (revision) ya jinai msingi wa hiyo hoja ni kifungu cha 8.2.d kutokana na marejeo ya mwaka 2023 mahakama hii ilisema uamuzi huo hauwezi kukatiwa rufaa kwani ni uamuzi usiomaliza shauri.
Anaendelea Mhe.Lissu
Kesi ambazo nimeziwasilisha mbele yenu waheshimiwa Majaji zinazungumzia uamuzi mdogo ni wa aina gani na uamuzi unaoweza kutolewa kama uamuzi wa mwisho unaoweza kuombewa revision ni wa aina gani.
Uamuzi unaomaliza kesi na kunyima haki za wadaawa ndiyo unaopaswa kukatiwa rufaa, uamuzi unaokuwa treated as the final order ndiyo unaomaliza haki za msingi za wadaawa lakini kama uamuzi haufanyi hivyo hauwezi kukatiwa rufaa.
Sasa waheshimiwa Majaji baada ya kuwapitisha kwenye kesi hizo nirudi kwenye hoja yangu ya msingi je uamuzi wa February 24 mwaka huu ulimaliza kesi hii?
Kama ni hivo ulimaliza kesi hii na kwamba Sasa hivi sina kesi ya uhaini basi hoja yangu haina msingi na maombi haya hayawezi kusikilizwa.
Hoja yangu waheshimiwa Majaji ni kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu wa February 24, 2026 haukumaliza kesi namba 19065/2025 na kwasababu haukumaliza maombi haya ya revision yanakatazwa kuletwa Mahakama ya Rufaa.
Anaendelea Mhe.Lissu
Waheshimiwa Majaji uamuzi huo unasema nini, ili tujue kama ulimaliza kesi lazima tuusome huo uamuzi unasema nini.?
Rulling yenyewe iko ukurasa wa 405-432, kwenye ukurasa wa 431 paragraph ya mwisho waheshimiwa Majaji mtaona Mahakama ilichokiamua.
Kilichokataliwa kupokelewa na Mahakama ni notice of additional substance of evidence, Mahakama Kuu haikusema kesi haitaendelea. Mahakama kuu ilitoa Mwongozo haikutoa uamuzi wa mwisho wa kesi, uamuzi wao ulikataa subodinate issue.
Waheshimiwa Majaji ushaidi mwingine huko kwenye maombi yenyewe yaliyoletwa. Mahakama inasema ilijadili na kukataa notice yao ya kuongeza ushahidi haisemi kesi ilifia hapo kutokana na uamuzi huo.
Mahakama imekata notice of additional substance of evidence, kwahiyo wanalalamikia uamuzi wa notice kukataliwa.
Jambo la pili ni Je mleta maombi anayo mamlaka ya kuiambia Mahakama itumie mamlaka yake ya kupitia kumbukumbu ili kuridhisha matakwa yake mwenyewe?
Jibu ni hapana hiyo siyo haki yao kisheria kwani wajibu wa kuangalia record ni wa mamlaka yenyewe.
Part 226 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 8
Anasimama Wakili Hekima Mwasipu kutoka upande wa waleta maombi.
Anasema kuhusu haki ya kusikilizwa tunaomba kusema kwamba respondents baada ya Jebra kujiondoa hawakuambiwa chochote.
Descretion tunasema inapaswa kuzingatia haki na Katiba ya nchi sasa alichokifanya Jaji Mwanga ni kuendelea na kesi kinyume na Matakwa ya kuexercise judiciously hiyo descretion.
Anasimama Dr. Nshala Ruge anasema sisi tulisema cause of action ilianza lini na sisi tulisema walianza 2016
Para zote walizosema ukianza na Para ya 7 wanasema wamemaliza kujenga jengo la Chama hawajasema kama kulikuwa na ugomvi.
Wanasema hadi tarehe fulani chama kilikuwa na mali hizi, sasa mgogoro ni nini?
Hakuna mahali walisema walikuwa na migogoro au mgogoro wao ulianza lini? Hawajasema chochote.
Dr. Nshala nina miaka 30 nafanya haya masuala ya sheria ndio nimesikia hizi paragraph ni contexual tu. Sasa hakuna kitu kama hicho.
Hoja yetu ni hizi para zao zinazungumzia mambo ya Kikatiba.
Pia nahisi wenzetu hawasikilizi nilisema S. 22(1) ya Political Party Act Msajili anajukumu la kuhakikisha sheria inatekelezwa. Sect. 4 the function and implemention of this Act amepewa Msajili wa Vyama vya siasa.
Dr. Nshala yuko moto sana.
Anaendelea kuwa huwezi kutoa injuction dhidi ya Chama cha siasa kesi ya Lyatonga Mrema imesema hivyo.
Wakati mwingine unaweza kupata ugonjwa wa moyo ukiwa unafanya hizi kazi.
Jaji sasa Dr. Nshala nikushauri jambo
Dr. Nshala samahani Jaji naomba niache.
Jaji sasa sikiliza nataka kukushauri mimi.
Dr.Nshala sawa Nishauri hakuna shida.
Jaji nataka usubmit hapa Mahakamani ukiwa umerelax ili usipate ugonjwa wa moyo.
Dr. Nshala sawa Ahsante nimepokea.
Watu wanacheka.😂
Dr. Nshala anaendelea
Huyu Marijan amesema conditions za Attilio vs Mbowe hazijawa met hata moja kabisa. Hata ku attach ile petition hawajafanya hivyo. Naweza kutumia maneno mazito lakini naomba niseme hili ni jambo la hovyo sana.
Chama cha siasa kinazuiwa kufanya siasa mwaka wa uchaguzi. Naomba Mahakama ya Rufani ilirudie tena uamuzi wake kuhusu Chama cha siasa hakipaswi kuzuiwa.
Naomba pia Mahakama ya Rufani iseme Jambo fulani juu ya huyu Jaji Mwanga maana mambo aliyofanya ni ya hovyo sana. Naomba mtufungulie hata leo tu.
Jaji sasa tunawashukuru sana.
Tunaenda kutafakari na tutawaambieni ni lini tutawapatieni huo uamuzi. Mtajulishwa. Tunawashukuru sana.
Tunaahirisha hadi kikao kijacho.
Mahakama imehairisha mpaka hapo tutakapoitwa tena kwa ajili ya kusikiliza uamuzi wa Majaji.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 7
Kesi ya Haruni David vs Kangi Lugola Civil appeal No. 36 inasema headings and marginal notes sio sehemu ya sheria.
Sasa temporary injuction inayoongelewa kwenye sub rule 3 ya O.XXXVII hapa tunachokisema trial judge alikuwa sahihi kuitoa na hakuitoa chini ya sub rule 3.
Jaji sasa ulitupeleka kwenye marginal notes ni kama umetuacha tena hiyo sub rule 3 order zinazoweza kutolewa hapo ni zipi?
Anasimama Wakili Mulabuzi anasema s. 105 ya CPC inaipa mamlaka Mahakama kuu inherent power kutoa order hata nje ya sheria
Jaji kwahiyo unataka na sisi tutumie hiyo Section 105 ya CPC?
Wakili ndio muitumie.
Anaendelea hapa Wakili kuwa hakuna single paragraph inayounganisha value ya subject matter lakini hata kama ziko separate ukiangalia aggregate yake inazidi mamlaka za Mahakama za Chini kwahiyo ilikuwa ni lazima ipelekwe Mahakama Kuu.
Jambo la Mwisho la time limit kuhusu cause of action sisi tulisema ilianzia mwaka 2019 hadi 2024 miaka 6 haijazidi.
Nilitaka kurudia hayo mambo mawili na kwa ujumla upande wa Applicant kulikuwa hakuna serious irregularity kuonesha proceedings zilikuwa na shida.
Kama kuna mapungufu basi tunaamini ni madogo sana na tunaomba mwenendo urudishwe mapema mahakama kuu ili tukaendelee na pande zote zipate haki yake. Tunaishia hapo.
Wazee wanaandika hapa, unasubiri maelekezo yao.
Jaji sasa lile suala la kwamba jambo hili lilipaswa kuanzia kwa Msajili wa Vyama vya siasa mnasemaje?
Wakili ukiangalia ukurasa wa 5 kuna juhudi zilifanyika na hazikuzaa matunda na kwenda kwa msajili ni kama unataka kufuta chama sisi wateja wetu walikuwa hawana nia ya kufuta Chama.
Msajili wa Chama asingekuwa na mamlaka ya kutoa nafuu zilizoombwa hapa.
Lakini pia maombi ya kwamba hii kesi ni constitutional au judicial review huko tusingetaka kwenda.
Jaji unasemaje Mpale Mpoki.
Tuna mambo kadhaaa
1. Angalau wamekubali kuwa kesi yao ilikuwa under CPC na wanajua O.VII inasemaje nini kiwepo kwenye proveedings. Mahakama hii ya rufani imesaidiwa kwamba value hawajaweka, hawajesema cause of action imerise lini?
2. Wame admit pia hakuweka value ya subject matter na kuhusu payment nayo hawajasema na Mawakili wanapaswa kujua sheria, akija mteja unapaswa kumwambia gharama za kufungua kesi sasa wao walijiendea.
3. Wameadmit kuhusu hii sio Constitutional case sasa ukisoma hii kesi kila mahali utaona inaitwa ni Public Interest Litigation.
4. Wanaadmit kuwa hii case haijaletwa chini ya Sheria yoyote na reliefs walizoomba ndio zinaelezea aina ya kesi na relief zao ni kesi ya Kikatiba.
Ukiangalia wanachoomba ni kuwalazimisha watu fulani wafanye jambo fulani na hii kwa uelewa wangu ni order ya Mandamus. Isingeweza kuwa Normal Civil Case.
5. Jambo lingine wanasema wako exempted. Ili plaimtif awe exempted under law of limitation anapaswa kusema tuko nje ya muda lakini tuwe exempted ni kwa mujibu O. VII r. 6 sasa hizo grounds za exemption zimetolewa kwa mujibu wa sheria.
Category za exemption lazima ziwe pleaded na useme kwanini hukufungua kesi ndani ya muda mfano nilikuwa naumwa, nilikuwa nimesafiri. Hawajasema lolote kuhusu hayo sasa.
Naomba nimkaribishe Hekima Mwasipu
Part 8 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 6
Anaendelea Wakili wa Said Issa na wenzake
Suala la amri ya zuio inamuhusu nani?
Record yenyewe ya Revision inajieleza nani inamuhusu. Page 153 imewaeleza wanaouzuiwa. Wametajwa bodi ya wadhamini na katibu mkuuu.
O.XXXVII ya CPC inasema kuwa order ya bodi ya wadhamini itawahusu wahusika pekeee. Sasa ukiitaja bodi ya wadhamini maana yake ni Chama chote.
Jaji kwani order inaposema na waliopo chini yake Katibu Mkuu ni chini hadi wapi?
Jaji mwingine anasema walisema kuwa servants na wengine wote wanaofanya kwa niaba sasa je kuna yeyote ambae angeweza kufanya shughuli nyingine?
Wakili naomba niendeleee
Jaji kabla hujaendelea sasa tusaidie mahusiano ya madai ya mali na kufanya shughuli za Chama?
Wakili anajibu waheshimiwa madai hapa sio mgawanyo wa mali lakini kweli mgawanyo wa Mali ni madai ila kitu cha msingi ni kifungu cha 6 cha Political Party Act.
Jaji hebu kisome halafu tuambie kinasemaje na maana yake.
Anakisoma hapa.
Anasema sasa matendo ya viongozi wa Chama yaliwakera wananchi wa Zanzibar.
Jaji wananchi wa wapi?
Wakili Mhe. Jaji namaanisha wakazi wa zanzibar.
Jaji una hakika wakazi wa zanzibar hawakufurahia
Wakili ni wanachama tu.
Jaji unajua kanuni za kutoa interim order hilo zuio?
Jaji mwingine na utuambie nani angepata athari zaidi kwa mfano nyie mmgeshindwa hiyo petition yenu kati yenu na respondents nani angeathirika zaidi?
Wakili sasa waheshimiwa majaji naona kama mnazungumzia kesi ya Attilio vs Mbowe
Bila kuzuia wasitumie hizi property basi wote wasingetumia na zingekuwa salama kwa wote.
Pia kufanya political activities lilikuwa ni zuio la muda tu, zingeachwa zingeendelea kutengeneza friction baina ya members.
Jaji sasa tuambie irreperable loss ni ipi?
Wakili tulisema sera za Chama zinaenda kuwa damaged.
Jaji tena anamuuliza Marijan kwahiyo unasemaje kuhusu kilichoombwa kwenye main case ni kama kilishatolewa kwenye ombi la zuio?
Wakili ni kama vinafanana lakini vinatofautiana.
Jaji huoni amri ya kwenye maombi madogo inaweza kuwafanya waleta maombi wakaona wameshamaliza kesi yao wakaanza kuchelewesha kesi ya msingi au wakaona haina msingi?
Wakili washemiwa nafikiri hakuna mwenye nia ya kupoteza muda kwenye shauri la msingi hivi.
Majaji wanatabasamu na kucheka ki kituristi kidogo halafu wanaandika kwa umakini mkubwa.
Jaji sasa mlisema hii kesi ni ya aina gani?
Wakili sisi tunasema haki zilikuwa infringed
Jaji hizo haki zipo wapi si Article 30?
Wakili ndio ni Article 30.
Jaji sasa kama ni Article 30 ya Katiba ndio zimevunjwa. Swali letu hii ni kesi gani? Ya Kikatiba au sio ya Kikatiba.
Jaji mwingine anasema sasa hapa una address jambo gani hebu tuambie maana kila kitu kina utaratibu wake sasa tueleze.
Anasimama Wakili Kiharuzi kuwa applicants hawahangaiki na haki za kikatiba.
Ila wanachosema ni maombi ambayo yanawaomba ku comply na matakwa ya kisheria hii ni CIVIL Case. Inawalazimisha
Jaji hebu subiri kwanza hoja hapa ni kwamba order ya zuio inaathiri haki zingine za Kikatiba, unasemaje?
Wakili sisi tunasema hayo ndio matokeo ya kosa walilolifanya.
Jaji kwahiyo unasema ni sahihi kuwa constitutional right zimekuwa infringed au vipi? Usituambie mambo ya inawezekana. Tujibu kuwa haki za kikatiba za wanachadema zimenyimwa au hazijanyimwa kwa maoni yako sasa?
Je haki ya kufanya siasa ni haki ya kikatiba au sio? Je mtu akizuiwa ni sahihi?
Sisi hatukufika kwenye Katiba anasema Wakili.
Jaji ndio tunawauliza hii kesi yenu ni Civil Case?
Wakili ndio hii ni Civil Case.
Jaji sasa kwanini hamkuiita Plaint na iwe ni Civil Case.
Jaji mwingine kwahiyo hii mnasema kuwa ni Suit under Civil Procedure na haikuletwa kwa njia ya Plaint? Unasemaje hapa.
Wakili, Mheshimiwa Jaji hii ni Civil Case.
Anakaaa anasimama tena Manywele Waheshimiwa Majaji kuhusu suala amri ya zuio inadumu kwa miezi sita tu.
Part 7 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 5
Anasimama Marijani wakili wa Said Issa na wenzake ana manywele mengi kichwani, anazungumza.. nae anapigwa maswali ya haraka haraka.
Jaji kwahiyo unataka kutuambia kuwa political party act nayo inazuia discrimination
Wakili ndio Mheshimiwa.
Sasa naomba niende kwenye hoja ya kwamba kesi ilifunguliwa nje ya muda.
Kwa mujibu wa Para 7 wa petition inasema chama kilimaliza kununu jengo la Chama na ilikuwa mwaka 2019 hivyo basi kuanzia hii tarehe hii hadi 2024 ilikuwa ni miaka sita tu. Kwahiyo ilikuwa ndani ya muda.
Jaji hebu soma para 10 tuone
Para ya 8 pia inasema kipindi ambacho kipo ndani ya muda.
Jaji kwahiyo tarehe ya kumiliki mali ndio cause of action inaanzia?
Wakili ndio inaanzia hapo kwenye para ya 9 pia imesema.
Jaji sasa uliwasikia wenzako kuhusu O.VII wewe unasemaje?
Wakili hiyo haiapply kabisa.
Jaji lakini Wakili umeelewa kweli hiyo O.VII r.1(e)
Wakili sasa jaji hiyo sasa ipo na ilikuwa stated kwenye petition kwenye paragraph nyingi.
Jaji kwahiyo matakwa ya hiyo O.VII yamezingatiwa na ilikuwa stated direct?
Mheshimiwa hiyo nayo haikuwepo direct lakini.
Kwa mujibu wa Section 18(1) ya Limitation Act
Jaji isome kwanza tusikie.
Anaisoma sasa.
Jaji sasa ina apply kwenye hii kesi?
Wakili ndio.
Anayetaka ku recover ni nani kwahiyo? Anamuuliza Jaji.
Wakili anajibu ni hawa wateja wetu.
Kumbe ni hivyo, haya tuendeleee. 😂
Kuhusu issue ya Locus Stand kwa mujibu wa Para. 6 na page 2 ya records
Jaji anasema hebu subiri wenzenu walisema wajumbe wa bodi kujishitaki wenyewe? Mnasemaje?
Wakili Bodi ya wadhamini inashitakiwa tu.
Jaji sasa walikuwa wanashitaki kwa maslahi ya nani?
Wakili walikuwa wanashitaki kwa maslahi ya Chama.
Jaji sasa wenzio wamesema utaratibu wa bodi ya wadhamini kushitaki ikiwa ni pamoja na kuwashitaki trustee wengine maana maamuzi ya bodi ya wadhamini yanapitishwa kwa kura na yanakuwa maamuzi ya Chama.
Wakili sheria nafikiri haisemi hivyo.
Jaji umemaliza au bado?
Wakili nimemaliza.
Anasimama Wakili mwingine anaitwa GIDO anasema kwenye right to be heard nasema kwamba wenzetu walipewa kabisa haki yao ya kusikilizwa.
Sasa ukisoma Tarehe 10 corum inaonesha mawakili wa pande zote walikuwepo. Jebra na sisi tulikuwepo.
Jebra aliomba shauri liahirishwe hadi siku ya ijumaa, Wakili Mulamuzi alijibu na kupinga ombi hilo na baada ya hapo proceedings ziliendelea na Jaji wa Mahakamu kuu alitoa maamuzi na kusema kesi hii hakuna sababu za msingi za kuahirisha.
Hivyo Waheshimiwa majaji hadi eneo hilo haki ya kusikilizwa walipewa wenzetu.
Mahakama ilisema kuwa sababu alizotoa Jebra kujiondoa basi ajiondoe.
Jaji sasa wateja wamemtuma wakili na yeye amejitoa huyo Wakili. Sasa kajitoa inakuwaje kwa aliyemtuma nae tunamsaidiaje?
Mh. Jaji alisema Mawakili walikuwepo wengi
Jaji sasa sisi tunataka hali ikiwa hivyo tunafanyaje?
Jaji wapili anasema naongezea hapo hukuona kuna umuhimu wa wateja kujulishwa.
Anasema Jaji wa tatu na mimi naongezea tusaidia una authority yoyote katika unayosema?
Hii inaitwa Mbwa Kala Mbwa hawa wazee ni watanzania kweli? 😂 mbona kama leo wamebadilika. Wanapeleka moto sana. Kama hawataki vile.
Wakili anajibu sasa, hata kesi walizoleta ni za Mahakama kuu kuhusu haki ya kusikilizwa haiwalazimishi muifuate.
Jaji sasa wewe yakwako ya Mahakama ya Rufani iko wapi?
Zile sababu Jaji aliziona ni delay tactic.
Jaji sasa hilo lipo wapi kwenye hukumu? Hivi hujawahi kukutana na uamuzi wa Mahakama unaosema makosa ya Wakili hapaswi kuumizwa mteja?
Jaji mwingine tena anasema tena Wakili alijitoa wakati Mahakama ilishasema hapa leo tutaendelea. Sasa huoni kulikuwa na umuhimu wa wateja kuambiwa.
Wakili anajibu anasema Respondent walipewa haki ya kusikilizwa na muwakilishi waliyemtuma hakutaka kuitumia haki hiyo.
Anasimama Marijan anasema naomba ni address inshu zingine.
Part 6 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 4.
Mahakama imerejea.
Anasimama Mpale Mpoki na kusema uwakilishi kwa upande wetu ni kama ilivyokuwa awali.
Kwa upande wetu na sisi upande wa waleta maombi uwakilishi uko vile vile.
Alban Fidelis Kairu anasimama na kuanza kusema kwa niaba ya akina Said Issa nitajikita kwenye areas mlizozisema.
Naomba ruling ya Said Issa kuadapt Sect. 4 ya Appellate Jurisdiction naomba kuitumia ruling hiyo katika kujenga hoja zangu.
Hoja ya tukishindwa kuelezea value ya subject matter.
It is proper kwa mujibu wa para 7,8,11, 12 na 14 and 15 ya Petition waliweza ku state value ya subject matter za property ambazo ni mali za Chama.
Pia walisema Chama kilikuwa kina own property zenye thamani ya bilioni 4.
Para 11 ya petition hao petitioners wali allege kuhusu pesa ambazo Chama kilikuwa kinamiliki kwenye Account number za Chama.
Ukiangalia kwenye reply yao walipinga mambo hayo sasa kwa vile wao walipinga basi halikuwa pure point of law.
Jaji anamuuliza kwani uamuzi wa Jaji ulikuwaje kuhusu suala hilo la value ya subject matter?
Ilisema kuwa monetary value haikuwa issue kwasababu hawakudai masuala ya mgawanyo wa pesa.
Jaji sasa tuambie value ilikuwa shilingi ngapi?
Mheshimiwa jaji para ya 7 inasema hivyo.
Jaji tuambie sasa mliandika wapi kwenye petition yenu value ya subject matter.
Mhe. Jaji sasa hapa
Hivi soma CPC kuhusu value ya subject matter inasemaje?
Jaji amemwambia asome sheria inasema kuwa lazima kuwe na statement inayoonesha value ya subject matter.
Expressely haipo lakini impliedly ipo, inasema huyu Bwana mdogo.😂
Jaji hebu sema sasa hiyo Para. 25 unayoase.a inasemaje? Au ndio hiyo ina statememt?
Haya uamuzi wa Jaji umesemaje kuhusu suala hilo maana naona kama ndio unajibu leo haya mambo.
Mheshimiwa Jaji value hazikuunganishwa.
Jaji anamuuliza kwahiyo hiyo ipo kwa mujibu wa O.VII?
Jamaaa amechanganyikiwa hawa wazee wanapiga sana maswali.
Majaji wa Mahakamaa ya Rufani ni kama wao ndio Mawakili aiseee.😂
Alban Fidelis Kairu anaendelea kuhusu Court fees hilo ni suala la Mahakama halikuwa suala letu.
Uamuzi wa Mahakama kuu uliotolewa ni kweli haikuwa Kesi ya Kikatiba. Na Appllicants walikuwa wanalalamikia under Political Party Act.
Jaji sasa kama haikuwa Constitutional case ilikuwa ni kesi gani?
Wakili wa akina Said Issa hii kesi yetu ilikuwa ni Petition. Inaanzia ukurasa wa kwanza.
Jaji wa Mahakama ya Rufani isome kama ilivyo.
Wakili anasema imeandikwa CIVIL CAUSE.
Jaji na huko chini imeandikwaje?
Wakili amasema imeandikwa Petition.
Jaji: Sasa hapo nini ni nini?
Mheshimiwa haya mambo magumu lakini ndio yako hivyo. 😂
Jaji sasa katika suit kuna civil case, constitutional case. Hii ni ipi?
It is suit under political parties Act anajibu wakili wa serikali.
Jaji labda tuendelee na wenzako pengine watakusaidia. Haya endelea tu.
Naomba niwasomee uamuzi wa Mahakama kuu ulivyosema. Anausoma hapa.
Kwa kifupi huyu jamaa anayeitwa Wakili anayoongea hata Majaji hawamuelewi. Wanangonga maswali yakutosha. Kwanza sauti yake imeisha kabisa sasa hivi hatumsikii. Ananong'oneza tu kule mbele. 😂
Waheshimiwa Majaji ukurasa wa 720
Jaji sasa hiyo si ni ile barua?
Wakili anajibu ndio.
Jaji sasa hiyo barua inaelezea ruling na ruling ndio inapingwa wewe hatukuelewi hapa unasema nini?
Wakili mimi nasema Jaji alikuwa sahihi tu.
Jaji sasa yale madai yenu yana affect constitutional right wewe unasemaje?
Wakili anasema hizo rights tulizosema tuna refer kwenye Political Party Act.
Jaji unataka nikukumbushe kila walichosema ili uweze kujibu? Wewe hukuwasikia?
Waheshimiwa walitaja Article 12 na 30 hazihusiani na kesi iliyopo Mahakamani. Hakuna constitutional demand iliyopo.
Jaji kwahiyo unasema ulikuwa una demand nini?
Sisi tunademand kuvunjwa kwa Katiba ya Chadema na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa.
Part 5 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 3
Anaendelea Wakili wa upande wa waleta maombi Hekima Mwasipu
Sasa amri ya Mahakama iliyotolewa ilisema Respondents hawapaswi kutekeleza majukumu yao hadi kesi ya msingi itapoisha.
Sheria imesema ikiisha miezi sita walioenda kuomba order wanapaswa kuomba kuongezewa muda.
Hivyo ni wasilisho letu kuwa kutokusema kipindi cha zuio hilo ni kosa kisheria.
Niende kwenye hoja nyingine sasa:
Anaendelea Hekima Mwasipu kuwa order ilizuia Respondents kufanya shughuli za siasa.
Ibara ya 21(1) ya Katiba yetu inasema shughuli za siasa na utawala ni haki ya Kikatiba.
Ibara ya 20 haki ya kukutana na kutoa maoni yao, Mahakama kuu imetoa order ya Chama kisikutane na kufanya shughuli zake.
Kesi ya Augustino Lyatonga Mrema pia ilisema Mahakama hii ya Rufani ilisema baada ya Mrema kwenda kuondoa viongozi wa TLP na ombi la kutaka mahakama itoe amri ya kuzuia shughuli za siasa kwa Mrema kwani ni kuwazuia hadi innocent people kufanya siasa.
Hili halina tofauti na kilichotokea kwa Chadema kuzuia wanachama wote kufanya shughuli za siasa hii haiko sahihi.
Lakini Waheshimiwa Majaji pia kuna barua ya mawakili wa waleta maombi wanaomba msajili wa Mahakama kuu atoe ufafanuzi wa order ya zuio kwa Chadema.
Ni wasilisho letu kuwa hata Mawakili wa waleta maombi hawakuelewa amri ya Mahakama.
Kesi ya Mrema inasema amri ya zuio kwa Chama ni hatari na haitekelezeki.
Naomba nimkaribishe tena Dr. Nshala.
Dr. Nshala kesi ya Jidawi, Jaji alisema board of trustee should not be eqquited with other activities of the party.
Jukumu lake ni moja tu kumiliki mali za Chama, shughuli za Chama na wanachama huwezi kusema watawajibika kwa bodi ya wadhamini.
Kuna swali la Jaji Maige Mahakama inaweza kutoa amri ya injuction lakini hii amri waliyotoa wamemzuia Katibu Mkuu kutumia Mali wakati yeye sio mmiliki wa mali hizo.
Lakini pia imewazuia bodi ya wadhamini kufanya siasa wakati wao sio kazi yao kufanya siasa.
Ni amri ya zuio ambayo imejichanganya, haieleweki na haitelelezeki.
Sasa Jaji alitoa amri ambayo hana mamlaka nayo.
Attilio vs Mbowe inasema lazima kuwepo na Prima facie case lakini katika hili hakuna prima facie case ambayo imekuwa established na pia vigezo vingine Mahakama ilisema kama chakwanza kipo basi na vingine vipo.
Amemaliza Dr. Nshala anasema naomba aje Wakili Mpoki kufunga.
Mpoki naomba sasa tumalizie hapo.
Jaji wa Mahakama ya rufani amesema tukutane baada ya nusu saa so tunaenda mapumziko.
Tukirudi tutaendelea na part 4
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 2
Anaendelea Dr. @rugemeleza
Uamuzi huo wa Jaji aliutoa bila kuelewa trustees zinavyofanya kazi.
Wakifungua Trustee yao ni watu wamoja na kama itatokea mgongano mmoja anafungua kesi basi anashitaki wenzake kwa nafsi zao.
Kifungu cha 14 cha Trustees Incoporation Act, kinasema all trustees inco. under this Act, they should be answerable in their acts as if there is no such trustee incorporation.....
Sasa kwahiyo tuna incompetent suit hawa 2nd and 3rd ni trustee na kwa mujibu wa sheria walipaswa kuwashitaki other trustee kwa majina yao wenyewe na sio kuishitaki Trustee.
Jaji wa Mahakama kuu alipaswa kuifuta na kuifukuza hii kesi kwa mujibu wa vifungu vya Sheria.
Logic behind ni kwamba trustees wana fiduciary relationship to each other ni lazima useme wenzangu wamekosea nini?
Madai mbele yenu kulikuwa na makosa ya Mahakama kuu na hakukuwa na competent suit before the Court of Law.
Kwenye hoja ya Jurisdiction ni kwamba nani ana mamlaka na Vyama vya siasa?
Kama unasema kumekuwa na ukiukwaji na Sheria ya Vyama vya siasa madai kama hayo yanaenda kwa Msajili ndo maana Msajili wa Vyama vya siasa amepewa mamlaka hata ya kufuta Chama cha siasa kama Chama husika hakijatekeleza matakwa ya Sheria ya Vyama vya siasa.
Jaji sasa katika kuamua jambo hilo alisema sio suala la ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, hilo ni suala la kisheria.
Kesi ya Mbeya Rukwa Mahakama ya Rufani ilisema jambo ambalo mamlaka fulani au taasisi ya kiserikali imepewa mamlaka ya kulishughulikia.
Basi Mahakama isiingilie kabla mamlaka hiyo husika haijafanya maamuzi.
Dr. Nshala anasema amemaliza sasa anaomba Wakili Hekima Mwasipu nae aendeleee.
Anaendelea Mwasipu
Ni ukweli kwamba Order 10/06/2025 ilitolewa bila Respondent kuwepo Mahakamani.
Kilichotokea ni kwamba maombi ya Revision yalikuja kusikilizwa lakini wakati wa kuanza kusikilizwa Wakili Jebra Kambole aliomba kesi iahirishwe aende kumsindikiza Wakili mwenzake kuzika.
Mahakama ikamkatalia na ikaendelea na kusikiliza maombi husika.
Pia Wakili Jebra Kambole akaomba kwenda kuhudhuria msiba wa Dada yake Hekima Mwasipu.
Jaji akakataaa tena.
Jebra Kambole alisema naomba kuondoa instructions yangu kwasababu sitaweza kuwawakilisha wateja wangu vizuri.
Wakili wa waleta maombi alisema tunaomba kuendelea exparte kwasababu respondents hawapo.
Sasa sisi hoja yetu ni kwamba je ni utaratibu gani unapaswa kufuatwa wakili anapoondoa instruction kwa wateja.
Kesi ya Abdala Chuga vs Halima Ismail ni kesi ya Mahakama kuu haiwabani waheshimiwa Majaji wa Mahakama kuu katika uamuzi huu ambao hauwabani lakini tunaomba kuwashawishi muukubali na kuutumia.
Mahakama Kuu ilisema baada ya Wakili kujiondoa katika kesi basi Mahakama kuu inapaswa kuwatumia summons wateja wa wakili husika na kumpa taarifa.
Kesi ya Andrew Gwande Sule Vs Republic nayo pia inasema ni lazima respondents ni lazima mteja apewe notice lakini jambo hili halikufanyika.
Implication yake ni nini?
Respondents hawakupewa ni ibara ya 13(6)(a) ya Katiba inasema linapoamuliwa suala lolote kuhusu haki yake ni lazima sasa mtu huyo apewe haki ya kusikilizwa.
Kesi ya Mbeya Rukwa inasema Natural right ni haki ya Kikatiba na sio suala ambalo tumelipokea kama mapokeo tu bali ni takwa la Sheria zetu.
Sasa remedy ya mambo haya ni nini?
Kesi ya Ntagazwa ni reported na Mahakama ya Rufani ilisema kuwanyima haki ya kusikilizwa maana yake proceedings zote ni haramu na ziondolewe.
Na sisi ndio ombi letu kuwa proceedings zote baada ya Wakili Kambole kujiondoa basi Mahakama inapaswa kufuta yote yaliyoendelea baada ya hapo.
Naomba niende kwenye hoja nyingine.
Kwa mujibu wa CPC inasema ukitoka kutoa amri ya zuio isizidi miezi 6 kama itatokea jambo hilo bado lipo Mahakamani basi atatakiwa kwenda kuomba kuongezewa muda.
Part 3 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MGAWANYO_MALI_ZA_CHADEMA
Part 1
Mahakama imeanza!
Mawakili wa pande zote mbili wapo.
Anaanza Wakili wa upande wa waleta maombi Mzee Mpale Kaba Mpoki @MpaleMpoki
Kuhusu hoja ya Cause of action ilianza lini yani madai ya akina Said Issa na wenzake yalianza lini wao wanasema ni mwaka 2016.
Kwa Mujibu wa Sheria ya Law Limitation Act kipindi cha mwisho kwa kesi ambazo hazijaelezwa na sheria itakuwa ni miaka 6 lakini wao wameleta kesi hii baada ya miaka 9.
Na jambo hili hawajalisema kwenye kesi yao ya msingi hata hiyo ya kuwa cause action ilianza mwaka 2016.
Wamekuja kuisema baadae kwenye pingamizi lao kuwa Mwenyekiti wa Chama asiunganishwe kwenye maombi yao ya msingi.
Sasa sisi tunasema kwenye shauri/maombi ya msingi hawakusema cause of action ilianza lini lakini hata hili la 2016 walilolisema liko nje ya muda.
Labda ingekuwa kesi ya Kikatiba wangeweza kuruhusiwa maana hakuna limitation of time.
Lakini hii kesi yao sio ya Kikatiba kwasababu kwanza imesikilizwa na Jaji mmoja na hakuna kesi ya Kikatiba inasikilizwa na Jaji mmoja.
Sasa Effect ya kutokuweka Cause of Action O. VI r.11 ya Civil Procedure Code katika hali ya kawaida hii kesi ilipaswa kuwa rejected na Court kwasababu haikuonesha ni lini Cause of action arouse.
Eneo lingine ni Failure to raise the value of the property. Takwa la ku disclose cause of action pia iko O. VII r. 1(i) ya CPC. The value of the subject matter of the Suit is of paramount importance for the case to be admitted.
Sheria inasema tunaweka value ya subject matter ili kuonesha pecuniary jurisdiction lakini kuisaidia mahakama kujua inacharge kiasi gani ili kuilipia gharama za kusajili kesi husika.
Sasa Ukurasa wa tano wa bando tulilowapa. Mara nyingi tungeona wamesema value ya subject matter lakini hawajasema.
Madai yao yaliyopo ukurasa wa nne wanadai distribution un even distribution of party asserts na pia paragraph 7 inasema tuna nyumba mikocheni yenye thamani ya milioni 726, landed property zenye thamani ya bilioni 2 na usheee, kulikuwa na magari 8 yenye thamani ya 576 milioni, Pikipiki 478.
Sasa hawajasema thamani ya wanachokidai ni shilingi ngapi?
Tumeangalia kwenye filing system imelipiwa kama fees ya shilingi elfu 50.
Sasa naomba niwapeleke kwenye GN. No. 247/2018 Court Fees Rules ambayo inasema inazidi kiwango cha juu zaidi inapaswa kulipiwa milioni 5.
Receipt ambayo tumeiona ni ya elfu 50, mtu ambae anaamua walipe shilingi ngapi angesema walipe milioni 5 na sio elfu 50.
A case has been deemed proper filed once the proper fess has been paid accordingly and as it is required by the law. Sasa ni wasilisho letu ni kwamba order ya injuction haikuwa sahihi kutokana na hakukuwa na kesi iliyofailiwa Mahakamani. Na tunaona lilikuwa ni pungufu kubwa sana.
Sasa naomba Dr. Rugemeleza Nshala aendeleee.
Dr. @rugemeleza anaanza. Nawashukuru sana kwa nafasi.
Naomba nizungumze hoja moja kwanza ukurasa wa 4 wa petition yao. Kwenye hoja ya Kikatiba.
Anasoma maneno yao ambayo wanasema viongozi wakuu wamekuwa wakisema maneno dhidi ya Zanzibar ambayo yanatishia Muungano na utendaji kazi wao kama wazanzibari.
Sasa Maneno haya yanaonesha madai yao ni ya Kikatiba. Na kesi hii ilipaswa kuwa ya Kikatiba. Lakini kesi hii imesikilizwa na Jaji mmoja na haikuwa kabisa kesi ya Kikatiba.
Jaji alipelekewa suala hili akasema mambo ya Kikatiba tuachane nayo. Hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana. Ilikuwa ni hatari sana kwa Jaji mmoja kujivika madaraka ambayo hana.
Kesi za Kikatiba yanaletwa chini ya BRADEA au kwa mujibu wa ibara ya 108 ya Katiba. Hawajafanya hivyo.
Haya Madai yao yana UVUNDO sina Lugha nyingine ya kutumia Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.
Sasa Dr. Nshala anaendelea hapa.
Wafungua maombi wa 2 na 3 wamesema wao ni member wa Board of Trustees ya Chama.
Sasa sisi tunasema hawawezi kufanya hivyo kwasababu wanapingana na Trustee Incorparation Act.
Part 2 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 225
Mhe. Lissu anaendelea hapa.
Kama mtakumbuka nilisema ninavyoishi Ukonga, siruhusiwi kuonana na Mawakili wangu in private.
Mnaruhusiwa kutembelea Magereza naomba mliangalie na hili kama itawapendeza inawapa Mamlaka ya kutoa mapendekezo na mamlaka za Magereza kurekebisha masuala yanayohusu wafungwa kama haya niliyosema.
Ni muhimu kwamba kuwasiliana na washauri wangu wa kisheria ilindwe kama sheria inavyosema bila kusikilizwa na maafisa wa Magereza.
Ni hayo tu Waheshimiwa
Mhe. Tundu Lissu amemaliza na amekaa sasa.
Majaji wanaandika hapa.
Anasimama Renatus Mkude kuwa tutampatia hizi nyaraka ndani ya siku 14 tutampatia.
Hili la masuala ya utawala wa mambo ya magereza kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha National Prosecution Act na sisi ofisi ya DPP tutatembelea ili kuhakisha kunakuwa na fair trial.
Wameombwa Majaji anasema DPP ataenda eti huko Magereza kuangalia haki za Mtuhumiwa. Uongo uongo uongo. Hawana hata aibu hawa jamaa.
Majaji wanaandika baada ya kusikia hayo kutoka kwa Wakili wa Serikali, Renatus Mkude.
Majaji wanajadili pale.
Yuko Jaji muda wote yeye huwa anacheka anafurahi tu sijui huwa anatabasamu jambo gani? Wanaofika hapa Mahakamani wanamfahamu vizuri.
Jaji Ndunguru: Tumesikia hoja za Jamhuri na Hoja za Mshitakiwa nae kama ambavyo mshitakiwa ameturahisishia kuwa mikono yetu imefungwa kwamba yapo hayo maombi ya marejeo Mahakama ya Rufani.
Sasa shauri hili linasimama hadi pale Mahakama ya Rufani itakapotoa uamuzi.
Suala la Gerezani wakili wa Serikali amesema na sisi pia tumelichukua.
Mwenendo wa shauri hili unasimama hadi pale mambo ya Court of Appeal yatakapoisha.
So kesi hii imeahirishwa hadi hapo itakapoitwa tena.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 224
Majaji wameingia muda huu saa nane Kamili Mchana.
Wanaandika pale juu.
Mheshimiwa Lissu ameingia na kuteta jambo na Dr. Nshala tunamsikia anasema waende kokote watakapotaka kwenda tutakutana nao huko. Sasa sijui ni wapi anamaanisha.
Anasimama Renatus Mkude Wakili wa Serikali kwa niaba ya jopo la Mawakili wa Serikali tunaomba radhi kwani tulifikiri tungetumia lisaa limoja.
Mchana huu nipo na Ajuaye, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Kwa wote tunawakilisha jamhuri na Mshitakiwa yupo.
Shauri lilipangwa kuendelea na mashahidi. Lakini tumetafakari na tunaitafsiri kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Appellate Jurisdiction Act na kanuni ya 65(1) ya kanuni za Mahakama ya Rufani.
Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) anatoa taarifa ya kuwasilisha taarifa ya mapitio (revision)
Hapa kwanza anakosea Mapitio ni Review alipaswa kusema Marejeo ndio Revision sijui kasoma wapi nae huyu jamaa.😂😂😂
Anaendelea hapa Renatus Mkude, kuwa Notice of motion hiyo imeambatanishwa na kiapo cha Cathbert Mbiringe Wakili wa Serikali ambayo taarifa hii ya kutoa notice kwenda Mahakama ya Rufani imesainiwa leo Tar. 24/02/2026.
Na kupokelewa kwa mifumo ya kielektroniki inayotambulika na Mahakama na kusajili kama. CRIMINAL REVISION NO. 7203216/2026 imepokelewa na Mahakama ya Rufani Tanzania hapa Dar es salaam.
Ambalo chimbuko lake ni Criminal Sessions No. 19605/2025 ambayo iko mbele yenu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu. (Ndunguru, Karyemaha, Kiwonde)
Kwa kuwa shahidi wetu aliyekuwa anafuata ACP Mahamba tuliyemuombea notice additional substamce of evidence na ikakataliwa.
Ni Rai yetu kwamba kwa kuwa shauri hili limeshapokelewa Mahakama ya Rufani haiwezi kusimama ili kuweza kutoa nafasi kwa shauri husika huko Mahakama ya Rufani kuweza kuamuliwa.
Ni hayo tu kwa sasa.
Tunamsubiri Mh. Lissu atajibu nini?
Mhe. Lissu anaanza.
Baada ya kuzikiliza wasilisho la upande wa Mashitaka nina haya ya kusema.
1. Kwa vile mimi nipo gerezani na wanajua nataka wanipatie hiyo nakala ya Notice of Motion waliyofile niweze kuiona.
2. Ninafahamu na ninatumaini na wao wanajua kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 8(2)(d) cha Sheria ya Mamlaka ya Rufaa ambacho wamekitaja (Appellate Jurisdiction Act) wanafahamu kwamba hakiruhusu rufaa wala mapitio wala marejeo ya maamuzi ya Mahakama ambayo hayamalizi shauri la msingi. (Interlocutory decisions) sina shaka na wao wanalifahamu hilo.
3. Waheshimiwa Majaji siwaombi mtoe uamuzi wowote kuhusu hili ninalolisema.
Nataka iwe kwenye record kwamba nafahamu na naamini upande wa mashitaka wanafahamu lengo la kupeleka ombi la marejeo Mahakama ya rufani na wanafahamu hairuhusiwi ni kurefusha mashauri haya ili niendelee kukaa Gerezani. Ni hilo tu.
Kwamba tupeleke Mahakama ya Rufani ili huyu mbaya wao ambae ni mimi aendelee kukaa Gerezani.
Kwa vile wananipeleka kwe ye Mahakama ya Rufani nataka niwaeleze kuwa nitawafuata huko huko naenda kuwashughulikia huko huko.
Kama ambavyo kesi yao is dead on arrival najua hata hii revision yao pia imeshakufa.
Tutarudi hapa yakiisha huko ya Mahakama ya rufani tutarejea hapa na nitawashughulikia tukirudi.
Jambo la Mwisho Mawakili wangu wametaka kunipa nyaraka hapa lakini siwezi kupewa hadi nyie mseme.
Sijui wanaogopa nini watu wa magereza nisipewe huo uamuzi hapo ni makaratasi tu.
Naambiwa ni hukumu kutoka huko Umoja Wa Mataifa lakini Magereza wanaogopa nisipewe.
Tena ni uamuzi unaohusiana na mimi kuwepo Gerezani. Tatizo liko wapi?
Jaji anasema uko wapi? Umepelekwa wameuona wamesema wape Mawakili wa Serikali.
Wako wanasoma hapa Mawakili wa Serikali huo uamuzi.
Anasimama Renatus Mkude anasema mimi ni member wa working group za UN Human Rights Council.
Jaji: Tumesema apewe au asipewe?
Renatus Mkude: Apewe tu.
Part 225 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KUTOKA_MAHAKAMA_KUU
Majira ya saa nane kasoro tano, wameingia Mawakili wengine wa Serikali.
Ananitonya Wakili mmoja hapa kwamba amechungulia nyaraka aliyonayo Renatus Mkude ni Notice of Motion kwenda Mahakama ya Rufani nafikiri wanaenda kufanya Revision ya uamuzi uliofanywa leo na Majaji wa Mahakama kuu leo kuhusu ile notice ya kuongeza ushahidi wa Amin Mahamba.
Huku ni kupoteza muda wa shauri hili.
Kwa kifupi kisheria tunaambiwa kukata rufaa au kupeleka maombi ya kufanya marejeo mahakama ya rufani haizuii kesi kuendelea.
Mahakama inayo mamlaka pia kukataa maombi yoyote ya Jamhuri ya kutaka kuahirisha kesi hii ikiona wanachotaka kulifanya Jamhuri ni kupoteza muda na kukiuka haki za msingi za Mshitakiwa.
Muda mfupi ujao tutajua ukweli wa mambo.
Kwa sasa tunajaribu kuchokonoa kidogokidogo kinachoendelea.
Tuendelee kuwa pamoja.✊
#UPDATES_KUTOKA_MAHAKAMA_KUU
Muda huu saa nane kasoro mchana.
Ameingia Wakili wa Serikali Renatus Mkude, tunasubiri Majaji nao waingie, amekuja peke yake akiwa na kikaratasi kimoja kinachosadikika kuwa ni kiapo fulani ambacho wameshakifile Mahakamani.
Hatujui kinahusiana na kufuta mashitaka, kukata rufaa au jambo gani lakin amekuja peke yake na hako ka nyaraka kake.
Muda mfupi ujao tutajua nini ni nini? Au nini kinaendelea..
JAMBO LA KUSHANGAZA MAHAKAMANI.
Muda huu wameingia wasaidizi na walinzi wa Majaji wamechukua Computer na vifaa vya Mahakama wameondoka navyo.
Inaonekana muda huu kesi haiwezi kuendelea maana wanaondoa kila kitu Mahakamani.
Taarifa tuliyonayo Mawakili wa Serikali hawajaonekana na hawajarudi Mahakamani so muda huu Karani amesimama hapa na kusema kuwa kuna jambo limejitokeza anaenda kutafuta ufafanuzi kwa Msajili wa Mahakama atarudi kuleta mrejesho.
Kwahiyo tupo njiapanda hatujui kinachoendelea hadi sasa.
Kesi imewashinda wanalazimisha ni aibu kwa Mahakama kuiamuru Jamhuri kuwa ilete Mashahidi baada ya lisaa limoja kwasasa ni masaa mawili yanaelekea matatu hakuna kinachoendelea.
Mawakili wa Serikali wanaamua kesi iendelee au isiendelee.
Vituko, Vichekesho na Maajabu.
Tunaendelea tuone mwisho wa hizi drama zao.
Wako Muhabarishaji,
Hilda Newton.
#UPDATES_KUTOKA_MAHAKAMA_KUU
Muda huu ni saa sita nayo dakika 17 kesi ya mchongo ya uhaini dhidi ya Mhe. Lissu bado haijaanza na Mawakili wa Serikali hawaonekani.
Tetesi kutoka kwa msiri wetu zinasema wanapigiwa simu hawapokei na wengine wamezima simu.
Mawakili wa Serikali wamechimba. Majaji na Mahakama imeachwa solemba, haya mambo yanashangaza kabisa.
Jamhuri kama hii kesi imewashinda waiondoe au wakae na Lissu Gerezani bila kesi kuendelea tujue moja maana hapo awali leo Walisema wanahitaji lisaa limoja kutafakari muda huu yamefika masaa mawili. Hawaonekani na hawajulikani walipo.
Unaambiwa hakuna anayefanikiwa kuwapata Mawakili wa Serikali na hawajulikani wameenda wapi?
Sijui ndio kufuata maagizo kutoka juu.😂😂😂😂
Haya ni maajabu na ni mambo yanayoshangaza sana.