#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 219
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross Examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Coplo Amani.: mimi sijalisema tu kama wewe umelisema basi ndio umesema.
Mhe. Lissu: Ni kweli kwamba P3 alikwambia kuwa ni mwanachama wa CHADEMA, kweli au si kweli
Coplo Amani : sio kweli
Mhe. Lissu: Wewe ndio uliandika maelezo yake kielelezo D12
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Sasa ngoja nikusomee… “mimi pia ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA” kweli si kweli.
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako uliyasema hayo
Coplo Amani : sikuyasema
Mhe. Lissu: Alikuonyesha kadi yake cha chama
Coplo Amani : sikutaka anionyeshe
Mhe. Lissu: alikwambia wafuasi wa chadema wana alama gani?
Coplo Amani : sikumuuliza mm
Mhe. Lissu: ndo maana nasema huyu ni askari wa kitengo cha intelijensi halafu mnasema ni shahidi.
Mhe. Lissu: Turudi kwa Inspekta Jorum, ni kweli polisi inapopokea watu waliofanya uhalifu , Polisi wanafungua investigation register?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waelezze majaji kama kwenye maelezo yako polisi walifungua investigation register
Shahidi: sijui
Mhe. Lissu: Waeleze majaji baada ya maafa yote hayo ya October 29 kama mmemchukulia hatua yoyote huyu baada ya kusema atapiga watu mawe?
Coplo Amani: Simfahamu chochote kuhusu swali lako
Mhe. Lissu: inaingia akilini hii
Coplo Amani : Mimi sifahamu chochote kwa kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unajua mashahidi wote wa kificho walisema waliona hiyo video yangu maarufu tarehe 4 april
Coplo Amani : Mimi sio mpelelezi wa mafile yote
Mhe. Lissu: Na unahabari wote waliokuja hapa ni boda boda na machinga hakuna afisa wa serikali au n.k
Coplo Amani : sina habari
Mhe. Lissu: Ulipomuachilia P3 kwa dhamana ulichukua hatua gani kuhakikisha aendelei na kupiga watu mawe na uasi?
Coplo Amani : sikupewa hilo jukumu
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji mimi sina maswali ya ziada.
Serikali: Kwa leo tulikua na shahidi huyu tu mmoja, tunaomba ahirisho kwasababu hali ya hewa ya Dar es salaam imebadilika na zimebaki dakika 20.
Kwasababu za kiusalama tunaomba ahirisho hadi siku ya Jumatatu ili tuje kuendelea kusikiliza juu ya notice tuliyoileta
Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji kwa dakika 20 kwangu si haba, mimi ninaomba hizi dakika 20 kwasababu nilishasema nina mapingamizi, naomba niongee juu ya hayo leo ili tusiathiri muda wa mashahidi wengine Jumatatu.
Naomba nipate hizi dakika 20 kwasababu mimi niliyepo Gerezani ndiye ninayepata shida, kwahiyo naomba tutumie hizi dakika jambo lifanyike.
Wakili wa Serikali: Waheshimiwa sisi tunaomba ahirisho lakin vilevile kama mnavyojua dini zote mbili tupo kwenye mfungo kwahiyo tunaomba ahirisho.
Lakini vilevile PO yake haijasajiliwa bado kwahiyo kama ataweza kuisajili na kuisikiliza basi aisajili na sisi tupewe nafasi ya kuiona ili tu-submit
Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji sikutarajia kwamba hili litakua na kubishana namna hii, nililetewa hii notice jana na nikatoa notice ya mdomo kwamba naipinga tena immediately nilipopatiwa tu notice hii.
Naijua sheria, sasa wanaposema tuahirishe ili niendelee kukaa gerezani ni sawa tukutane Jumatatu ili tuzungumzie PO yangu niliyoileta jana.
Na jana nilisema kabisa PO ni ya kisheria na itaenda na kifungu icho icho cha 308(1) cha CPA, mimi nakaa gerezani kwasababu ya michezo hii mnayoleta mawakili wa serikali kila siku.
Jaji Ndunguru anasema shauri litaendelea siku ya Jumatatu, tunatarajia serikali mlete mashahidi, tutaanza na hoja ya notice, tukimaliza tutaendelea na mashahidi wengine.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 218
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Angalia D14 tuambie wapi alisema alimuona Tundu Lissu akihamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025?
Coplo Amani : Hayo maneno kufanya vurugu hayapo kwenye kielelezo
Mhe. Lissu: April 17, 2025 kwenye ushahidi wako wa hii siku unasema ulikuwa kituo cha Polisi Ilomba na ukapewa maelekezo na inspekta Jorum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana na alichoeleza juu ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu kuhusu kauli yake na akahamasika na akashawishi wenzake wafanye vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu 2025, eleza kama maelezo hayo yapo
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo
Mhe. Lissu: Coplo Amani shahidi haya yote ambayo nimekuuliza kama yapo au hayapo ma umesema hayapo katika maelezo yako, swali langu ni uliyasema hapa mahakamani kwasababu ni mambo muhimu kwa mahakama kuyasikia, kweli au si kweli.
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji naomba nitoe ufafanuzi.
Mhe. Lissu: Hapana naomba ujibu swali langu
Coplo Amani: nawaomba majaji
Mhe. Lissu: hapana
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Umewaeleza waheshimiwa majaji kwanini hayo mambo muhumu hayapo katika maelezo yako??
Coplo Amani : bado nina muda
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Coplo Amani : sijayasema na sijayaeleza kwasababu ninazozijua Mimi.
Mhe. Lissu: Nataka uangalie icho kielelezo D14 ni nataka uangalie halafu uniambie kama nakosea umeandika baada ya kupata maelezo ya kazi ya Jorum nilianza ufuatiliaji Isyesye mtaa wa Mwantengule, kwa maneno hayo nitakuwa sahihi nikisema kwamba ulikwenda Mwantengule ukiwa tayari unamjua P3
Coplo Amani: nilikua simfahamu
Mhe. Lissu: Kama ulikua humfahamu uliendaje moja kwa moja ukamkamata
Coplo Amani : Nilishasema nilionyeshwa na askari wa intelijensi
Mhe. Lissu: hayapo kwenye maelezo yako and it is too bad.
Mhe, Lissu: P3 ni dereva wa boda boda sio
Coplo Amani : ndio
Mhe. Lissu: Na umesema askari wa intelijensi huwa wanajichanganya hata kwa boda boda
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: sasa waambie waheshimiwa majaji kama huyu P3 sio askari wa kweli wa intelijensia
Coplo Amani : si kweli
Mhe. Lissu: umesema P3 alipanga kupiga watu mawe, kuasi nchi halafu umesema Jorum alikwambia umuachie kwa dhamana, inaingia akilini??
Coplo Amani : inaingia akilini
Mhe. Lissu: mtu anayepanga uasi na kupiga watu mawe mnampa dhamana?! Kwanin tushangae yaliyotokea October 2025!
Coplo Amani : mimi sijui bwana muulize Jorum
Mhe. Lissu: Jorum hayupo kwenye kizimba
Mhe. Lissu: kwahiyo nyinyi Polisi ndo mlipanga mambo ya October 29
Coplo Amani : Mimi sina majibu ya hilo.
Mhe. Lissu: Eleza kama umeleta pikipiki uliyomkamata nayo
Coplo Amani : sijaonyesha
Mhe. Lissu: usajili wa Bodaboda
Coplo Amani : Hakuna
Mhe. Lissu:Kadi ya bodaboda
Coplo Amani : hakuna
Mhe. Lissu: Na huyu jamaa tunamtambua kama P3, hatujui jina lake, amejificha kwenye kibox hatujamuona tutajuaje kama ni boda boda?
Coplo Amani : hayo mambo yanahusika vipi kwenye kesi hii
Mhe. Lissu: yanahusika
Mhe. Lissu: Huyu P3 ulivyomfikisha Ilomba ulimuweka mahabusu, kweli au si kweli
Coplo Amani : Si kweli
Mhe. Lissu: Naomba nimsomee shahidi kielelezo D12 jinsi P3 alivyofikishwa kituoni……”tulivyofika kituoni aliniweka mahabusu”
Sasa swali langu kati ya ushahidi wako ww na ushahidi wa P3 Mahakama ichukue upi kuwa ni ushahidi wa kweli?
Coplo Amani : hilo ni jukumu la mahakama.
Mhe. Lissu: naomba ujibu swali langu
Coplo Amani : hilo ni jibu la mahakama
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Katuga: Waheshimiwa shahidi ameshajibu sasa kama halimpendezi basi hilo ndio jibu
Mahakama: endelea na Cross
Mhe, Lissu: Kwenye ushahidi wako kizimbani umewaambia majaji kwamba P3 alikua anahamasisha watu kupiga mawe?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Kwanini hujalisema wakati upo kizimbani
Part 219 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 217
Anaendelea Mhe. Lissu na Cross examination.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi ili nikuhoji vizuri naomba uwaambie waheshimiwa majaji kama upo tayari maelezo yako yapokelewe kama kielelezo
Coplo Amani : nipo tayari
Serikali: hatuna pingamizi.
Mahakama; maelezo haya yanapokelewa kama exhibit D14
Mhe. Lissu: Waheshimiwa naomba exhibit D14.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi maelezo yako sasa ni kielelezo D14 naomba uyaangilie vizuri
Swali langu la kwanza umesema unafanya kazi katika kitengo cha upelelezi chini ya Mkuu wa upepelezi wilaya
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama hayo maneno yapo kwenye D14
Coplo Amani : yapo
Mhe. Lissu: wapi
Coplo Amani : angalia page ya pili
Mhe. Lissu: soma
Shahidi anasoma
Mhe. Lissu: Naomba niangalie hayo maelezo na waheshimiwa majaji naomba na nyie muangalie kwenye typed.
Mhe. Lissu: naomba na mimi nisome waheshimiwa majaji, yupo sahihi kama alivyosoma ya kwangu ndio yamekosewa.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako shahidi umesema wewe ni msaidizi katika shughuli zote za upelelezi wilaya ya Mbeya
Coplo Amani : sahihi kabisa
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama hayo maneno yapo kwenye kielelezo D14
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema ulikua unaelezea Kituo cha polisi Ilomba ulisema ni Kituo kidogo cha polisi kilicho chini kituo cha kati cha mbeya kama out post na ukisema ivi ina maana hakija-qualify kuwa Kituo cha Polisi?
Coplo Amani : sahihi
Mhe. Lissu: kama hayo maneno yapo kwenye maeleezo yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: 4 april 2024 kwa majibu wa maelezo yako ulipewa maelekezo na Jorum kwenda mtaa wa Mtengule
Coplo Amani : Kweli
Mhe. Lissu: Lakini alikupa namba ya simu askari wa intelijensia ili akuongoze ukamkamate mhalifu
Coplo Amani : sahihi
Mhe. Lissu: waambie kama hayo maneno kwamba ulipewa namba ya simu yapo kwenye maelezo yako.
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo katika kielelezo D14
Mhe. Lissu: uliwaeleze askari wa intelijensia kama askari wanaojichanganya na raia kama vile boda boda
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama huo ufafanuzi wako upo kwenye maelezo yako.
Coplo Amani : hakuna
Mhe. Lissu: : Baada ya kupewa namba ya mtu wa intelijensi uliwasiliana nae na badae ulikutana nae mtaa wa Mtengule
Coplo Amani : Kweli
Mhe. Lissu: waeleze kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema huyo Askari wa intelijensia alikuongoza na kukuonyesha huyo mtuhumiwa katika kijiwe cha boda boda na kulikua na watu wengi, waeleze kama hayo maneno yapo kwenye statement yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema taarifa ulizopewa mtuhumiwa ndiye anayehamasisha wenzake kufanya vurugu na kuzuia uchaguzi wa 2025
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: waonyeshe hayo maneno kama yapo katika maelezo yako.
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Sasa ushahidi wako unasema ivi baada ya kuonyeshwa huyo mtuhumiwa ulimfata na kumtoa pembeni ya kijiwe, kisha ukajitambulisha kwake kwa jina na ukamwambia tuhuma zake za kuhamasisha vurugu na kuzuia uchaguzi wa 2025, sasa angalia D14 na ueleze kama hayo maeno yapo?
Coplo Amani: hayapo.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema, ulimueleza kuwa anahitajika kituo cha polisi Ilomba na alikubali kwenda, ni kweli au si kweli
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Waeleze kama hayo maneno yapo katika maelezo yako D14
Coplo Amani: Ndio yapo
Mhe. Lissu: yapo wapi, utusomee?
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema kwamba, kwenye maelezo yako tuhuma iliyokuwa inamkabili ni kinyume na kifungu cha 390, waeleze waheshimiwa majaji kama kwenye maelezo yako yapo?
Coplo Amani : hayapo.
Mhe. Lissu: umesema baada ya kumhoji alikubali kuwa anashawishi wenzake juu ya vurugu na wakati akiangalia YouTube aliona Tundu Lissu akihamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025
Coplo Amani :Kweli
Part 218 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 216
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa Maswali ya Dodoso.
Anasimama Mheshimiwa Lissu kwa ajili ya kumfanyia Cross Examination Shahidi ambae anaitwa Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa kwa kuanzia naomba nipatiwe kielelezo D12, waheshimiwa majaji haya ni maelezo ya P3.
Mhe. Lissu : Sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama uliandika maelezo polisi
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama unaweza kuyatambua ukionyeshwa
Coplo Amani : nikionyeshwa nitaweza kuyatambua
Mhe. Lissu: naomba shahidi aonyeshwe maelezo yake aliyoandika polisi.
Coplo Amani : haya ndio maelezo yangu
Mhe. Lissu: asante sana, sasa shahidi hayo maelezo yako naomba uwaeleze majaji kama uliyaandika mwenyewe au uliandikiwa na askari mwingine?
Coplo Amani : haya maelezo niliandikiwa na askari mwingine
Mhe. Lissu: mtaje jina tafadhali
Coplo Amani : Anaitwa H9207 detective coplo Robert
Mhe. Lissu: Kwenye maelezo yako hayo waeleze majaji kama ni utaratibu mtu anayeandika maelezo ya shahidi hawezi akawa ndio mtu huyohuyo kama shahidi?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji pamoja na majibu mazuri ya shahidi huyu nataka ku-impeach credibility yake, nitamsomea maelezo yake, nitamuonyesha maeneo nitakayotaka kumuuliza maswali halafu nitamtaka ayawasilishe kama kilelezo.
Mhe. Lissu anamsomea maelezo yake
Mhe. Lissu : Haya ndio maelezo yako kama nilivyoyasoma?
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji mshtakiwa kuna maeneo amekosea naomba nimrekebishe, sio kata ya Isuesue ni Isyesye 😁
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji kwakua na nyie mnarekodi hii mimi nimeona imeandikwa isuesue waheshimiwa…
Kwenye maneno “ni dereva wa bodaboda isuesue Mwintengule”… kwenye original Isyesye… kwahiyo tutaenda na ya kwako.
Kuna eneo lingine ambalo lina shida?
Coplo Amani : hapana.
Mhe. Lissu : Sasa kuna maeneo nataka kukuhoji kwa ajili ya kukukanusha kama ifuatavyo;
1. Kwamba unafanya kazi chini ya OCCID Mbeya mjini
2. Kwamba wewe ni msaidizi wa upelelezi ndani ya Mbeya mjini
3. Umeelezea Kituo cha Polisi cha Ilomba kwamba ni kituo kidogo kilichopo chini ya kituo cha Kati Mbeya umesema ni kama out post.
4. Umeeleza kwamba kaimu OCCID Inspekta Jorum alipokupa maelekezo ya kwenda kumkamata P3 alikupa namba ya simu ya askari wa kitengo cha intelijensia kwa ajili ya kwenda kumkamata P3
5. Kwamba hawa askari huwa wanajichanganya na raia kama dereva boda boda n.k
6. Baada ya kupewa namba ya simu ukawasiliama nae na mkakutana Isyesye.
7. Kwamba kulikua na watu wengi na mlipita na akakuonyesha mtuhumiwa kwenye kituo cha boda boda.
8. Taarifa mlizopewa na Jorum ni mtuhumiwa ndiye anayehamasisha wenzake kufanya vurugu uchaguzi wa 2025
9. Baada ya kuonyeshwa huyo mtuhumiwa ulimfata na kumtoa pembeni ya kijiwe na kisha ulijitambulisha kwake kwa jina na kumueleza tuhuma zake.
10. Ulimwambia baada ya kumtoa pembeni kwamba anahitajika Kituo cha Polisi Ilomba na yeye alikubali kwenda.
11. Ni ushahidi wako maelezo aliyoandika mtuhumiwa ni uchochezi, kusababisha vurugu na kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025.
12. Shitaka uliloandika lilikua ni kukiuka masharti ya kifungu cha 390 cha Penal code
13. Wakati ukimhoji alikwambia kwamba aliona taarifa kwenye YouTube akamuona Lissu akiwa anahamisisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi 2025.
14. Baada ya kuandika maelezo yake ulimjulisha inspeka Jorum akakuelekea kumuachia kwa dhamana na we anaripoti kila baada ya siku tatu
15. Ni ushahidi unaohusu tareh 17 april 2025 kwamba siku hiyo wakati ukiwa Ilomba Kituo cha Polisi ulielekezwa na inspekta Horum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana maelezo ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu na yeye kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vijana wenzake kufanya vurugu.
16. Baada ya kurekodi malezo hayo na ulimjulisha Inspekta Jorum na ukamkabidhi malezo hayo.
Part 217 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 215
Katuga anaendelea kumuongoza Shahidi ambae ni Coplo Amani
Wakili wa Serikali: Kikafuata nini?
Coplo Amani: Baada ya kuonyeshwa mtu huyo, nilimfata na nikamuita nikamtoa eneo hilo la bodaboda tukakaa pembeni kidogo, nikajitambulisha kwake kwamba mimi ni G9304 natoka Kituo cha Polisi kati Mbeya, baada ya hapo nilimueleza tuhuma yake ya kuhamsisha vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025.
Wakili: Uchaguzi ulihusu nini?
Coplo Amani : Uchaguzi ulikua unahusu rais, wabunge pamoja na madiwani.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Baada ya kumueleza tuhuma zake nikamueleza kwamba anahitajika Kituo cha Polisi Ilomba.
Wakili: kikafuata nini?
Coplo Amani : Baada ya hapo hakubisha na alikubali kwenda kituo cha polisi Ilomba.
Wakili: ukafanya nini?
Coplo Amani : niliondoka nae mpaka Kituo cha Polisi Ilomba
Wakili: ukafanya nini?
Coplo Amani : Baada ya kufika kituo cha Polisi nilimjulisha Inspekta Joram, akanipa maelekezo ya kumuandika mtuhumiwa maelezo.
Wakili: anaitwa nani huyo mtuhumiwa?
Coplo Amani: Mtuhumiwa huyo katika shauri hili anajulikana kama P3.
Wakili: Ikawaje?
Coplo Amani : Nilimuandika maelezo kwa tuhuma za uchochezi na kuhamasisha kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Nini kikafuata?
Coplo Amani : Baada ya hayo maelekezo nilimuandika maelezo kama nilivyoelekezwa na nilimuandika maelezo kama mtuhumiwa.
Wakili: kwa kosa gani?
Coplo Amani : makosa hayo ni kinyume cha kifungu cha 390 cha sheria ya kanuni ya adhabu
Wakili: Ikawaje?
Coplo Amani :. Baada ya kumhoji mtuhumiwa alinieleza kwamba ni kweli alihamasisha wenzake kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025
Wakili: Nini Kingine?
Shahidi: Pia alinieleza siku hiyo ya tarehe 4 April 2025 alikua akipitia taarifa mbalimbali na wakati anaendelea kupitia taarifa kwenye mtandao wa youtube alisikia mtu ambaye alimtaja kama Mwenyekiti wa CHADEMA anayeitwa Tundu Antiphas Lissu akiomgea na kutoa kauli za kuhamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Wakili: kikafuata nini?
Coplo Amani : Baada ya kumaliza kumuandika maelezo nilimjulisha Inspekta Joram na akanipa maelezo kwamba mtuhumiwa adhamimiwe na aripoti kituo cha polisi Ilomba na aripoti kila baada ya siku tatu.
Wakili: nini kilifanyika Tarehe 17 April
Coplo Amani : Tarehe 17 april 2025 nikiwa kituo cha polisi Ilomba nilipewa maelekezo na Inspekta Joram ya kuandika maelezo kama shahidi.
Wakili: Kingine?
Coplo Amani : Nilipewa maelekezo ya kumwandika kama shahidi kuhusiana na kile alichoeleza kwenye maelezo yake kwamba aliona mwenyekiti wake wa CHADEMA akihamasisha vurugu na kuharinubuchaguzi mkuu wa 2025 na kwamba baada ya kuona kauli ile yeye kama mfuasi wa CHADEMA, alihamasika kutokana na kauli zile na alikua tayari kuwashawishi vijana wenzake kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Baada ya hapo?
Coplo Amani : Baada ya kumaliza kumuandika maelezo nilimjulisha Inspekta Joram.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Hayo maelezo nilimkabidhi inspekta Joram.
Wakili wa Serikali : Waheshimiwa majaji ni hayo tu kwa shahidi huyu.
Part 216 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 214
Leo Mhe. Lissu ameingia Mahakamani akiwa amepiga Jeans na T-Shirt fulani hivi nyeusi yenye neno moja lililoandikwa kwa herufi kubwa "DUDA"
Kaka David Jumbe anasema DUDA ni neno la Kinyaturu ambalo maana yake ni mtoto ambae anapendwa sana.
Majaji wameingia,
Naona wanaandika kidogo pale juu.
Wakili wa Serikali anasimama, anasema upande wa Serikali wapo Kama walivokuwa asubuhi.
Wakili wa serikali: Shahidi anayefata sio shahidi wa kulindwa, anaitwa Coplo Amani.
Shahidi anaingia Mahakamani.
Jaji anamuuliza unaitwa nani?
Naitwa G9304 detective Coplo Amani
Una miaka mingapi: Nina miaka 35
Dini yako: Shahidi: mkristo
Kazi yako: Shahidi: mimi ni askari polisi.
Wakili wa Serikali : Toka lini?
Coplo Amani : Nimekua askari polisi tangu 2012
Wakili: unaifanyia wapi hiyo kazi?
Coplo Amani : Kazi yangu naifanyia mkoa wa Mbeya wilaya wa Mbeya mjini, kituo cha polisi cha kati Mbeya.
Wakili: Kituo gani?
Coplo Amani : Kituo cha Kati Mbeya nipo tangu 2012
Wakili: Una elimu gani ya Polisi?
Coplo Amani : Elimu yangu niliipata 2011-2012 ndani ya chuo cha polisi Moshi
Wakili: Ulivyohitimu ikawaje?
Coplo Amani: Baada ya kuhitimu mafunzo nilipangiwa Kituo cha Polisi Kati Mbeya Mkoa wa Mbeya.
Wakili: Kitengo gani upo?
Coplo Amani : Kituo cha Polisi Kati Mbeya nipo kitengo cha upelelezi wa makosa ya jinai
Wakili: Unafanya kazi chini ya nani hapo?
Coplo Amani : Nikiwa chini ya ofisi ya mpelelezi wa wilaya ya Mbeya kwa kifupi ni OCCID
Wakili: Kingine?
Coplo Amani: Katika ofisi hiyo nipo kama msaidizi wa shughuli zote za upelelezi ndani ya wilaya ya Mbeya mjini.
Wakili: Majukumu yako ni yapi?
Coplo Amani: Majukumu yangu ni kufanya doria, kupeleleza kesi zote za jinai, kukamata watuhumiwa wote wa makosa ya jinai na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote wa jinai
Wakili: Unakumbuka nini tarehe 04 April?
Coplo Amani : April 4, 2025 nakumbuka nilikua Kituo cha Polisi Ilomba ambacho kipo Wilaya ya Mbeya Mjini, Mkoa wa Mbaya, hiki ni kituo kidogo cha polisi kinajulikana kama outpost
Wakili: Unajua nini kuhusu hicho kituo cha Polisi?
Coplo Amani : Kituo cha Polisi Ilomba kipo chini ya kituo cha polisi kati Mbeya.
Wakili: Nini kikaendelea?
Coplo Amani: Nilipewa maelekezo na Inspekta Joram, ambaye ni kaimu wa upelele Wilaya ya Mbeya mjini.
Wakili: Akakwambia nini?
Coplo Amani : Alinipa maelekezo ya kwenda Isyesye mtaa wa Mwamtengule ambapo alinieleza kwamba kuna watu wanapanga njama za kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Wakili: kingine?
Coplo Amani: Lakini pia alinipa namba ya simu kwamba niwasiliane na askari mwenzangu, ambaye yupo kitengo cha intelijensia ili aende akanionyeshe watu hao wanaojipanga kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Kazi yako inahusiana na nini?
Coplo Amani: Askari ambaye yupo intelijensi ni askari wanaofanya kazi ya kujichanganya na wananchi ili wapate taarifa mbalimbali za uhalifu.
Wakili: mnafanyaje kazi?
Coplo Amani: Askari wa intelijensia huwa wanajichanganya katika shughuli mbalimbali za wananchi, wengine ni bodaboda n.k ili kupata taarifa za makosa ya jinai.
Wakili: nini kilifuata?
Coplo Amani : Baada ya maelekezo hayo niliwasiliana na huyo askari tukakutana Isyesye mtaa wa Mwantengule
Wakili: Mkafanya nini?
Coplo Amani : Tulivyokutana akaniongoza na kunionyesha mtuhumiwa ambaye nilipaswa kumkamata.
Wakili: Kulikuwaje?
Coplo Amani : Pale kulikua na watu wengi tukapita kwa siri na akanionyesha mtuhumiwa katika kijiwe cha bodaboda akiwa na wenzake.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Huyo mtu niliyetakiwa kumkamata ndiye aliyekuwa anahamasisha wenzake kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Part 215 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 213
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa kificho P9
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji hilo pingamizi la Wakili la Serikali halina maana yoyote, kwasababu shahidi mwenyewe amesema kwamba summons alipelekewa summons na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Mwenyekiti ni ofisa wa serikali, lakini vilevile Mahakama haitaweza kujua kama huyu shahidi ni mkweli au ni muongo kwahiyo swali langu ni halali na ninaomba pingamizi lao litupitiliwe mbali, lakini huyo Mwenyekiti sio mtu ambaye amelindwa na sheria.
Katuga: Sisi tunaomba swali hilo shahidi asiulizwa kwasababu swali hilo litapelekea utambuzi wa shahidi huyu na kama tunavyojua humu ndani kuna wafuasi wake, researchers wake wanaweza wakaenda kumtafuta ili kumtambua shahidi huyu.
Mhe. Lissu: naomba ondoa hiyo kauli yako mimi sijazungumzia kuhusu wafuasi wangu humu.
Katuga: Naondoa hiyo ilikua ni by the way lakini msimamo wetu ni kwamba swali hilo shahidi asiulizwe
Mahakama: tunadhani uendelee na x-examination bila hilo jina.
Mhe.Lissu: Lakin waheshimiwa majaji mnaweza kuona namna cross examination yangu inavyokua limited lakini naomba niendelee.
Mhe. Lissu: shahidi umekujaje hapa
Shahidi wa kificho P9: nimependa bus
Mhe. Lissu: nani amekulipia nauli
Shahidi wa kificho P9 : nimejilipia mwenyewe
Mhe. Lissu: Umefikia wapi
Shahidi wa kificho P9 : Kwa ndugu yangu.
Mhe. Lissu: Waambie waheshimiwa majaji kama kuna kiongozi au mfuasi anajua kama unakuja kutoa ushahidi
Shahidi wa kificho P9: Ndio wapo baadhi
Mhe. Lissu: waliwahi kukutishia
Shahidi wa kificho P9 : ndio
Mhe. Lissu: unajua hilo ni kosa
Shahidi wa kificho P9 : hilo ni kosa la jinai
Mhe. Lissu: umewataja,
Shahidi wa kificho P9 : siwezi kuwataja kwa usalama
Mhe.Lissu: waeleze majaji kama ulitoa taarifa kituo cha polis
Shahidi wa kificho P9 : ndio
Mhe. Lissu: Kituo cha polisi kipi?
Shahidi wa kificho P9: Sasa nikitoa taarifa hiyo hapa si itakua navunja usalama?
Mhe. Lissu: Hebu jibu swali bwana tusisumbuane
Mahakama: Shahidi hebu jibu hilo swali
Shahidi wa kificho P9: Nilitoa kituo cha polisi Ilomba
Mhe. Lissu: Ulipewa RB
Shahidi wa kificho P9: ndio
Mhe. Lissu: umeitoa hapa mahakamani?
Shahidi wa kificho P9 : hapana
Mhe. Lissu: Polisi walichukua hatua gani?
Shahidi wa kificho P9: Walisema watafatilia
Mhe. Lissu: waambie waheshimiwa majaji kama kuna mtu yoyote amekamatwa
Shahidi wa kificho P9 : hapana
Mhe. Lissu: Waambie kama kuna mtu yoyote amepelekwa mahakamani:
Shahidi wa kificho P9 : hakuna
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji sina swali lingine kwa shahidi huyu.
Wakili wa Serikali: Leo tunashahidi mmoja, tunaomba break kidogo halafu tuje na shahidi mmoja aliyebaki, kwasababu jana hatukupumzika.
Mahakama: Mshitakiwa unasemaje
Mhe. Lissu: Tukienda kwa utaratibu huu tutachukua mida mrefu sana, Mahakama ilisema upande wa serikali ulete mashahidi wasiopungua watatu, kwanin hawajaleta hao mashahidi wengine.
Upande wa mashtaka wanatakiwa wawe na mshahidi wengine kama walivyotakiwa na Mahakama.
Katuga: Jana tulisema tutakuja na shahidi mmoja then twende kuargue application yetu, hatujaweza kuja na mashahidi wengi ili tupate muda wa kutosha kwasababu yeye alisema ana-objection.
Mahakama: Nadhani twende break fupi kwanza ili tukirudi tuendelee na huyo shahidi halafu tukimalizana nae mambo mengine yatafata.
Part 2014 itaendelea tukirudi.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 210
Anaendelea Mhe. Lissu na Cross Examination.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba shahidi apewe kielelezo D13
Mhe Lissu: Jana kwenye ushahidi wako uliulizwa unaishi wapi na ukasema unaishi katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli.
Mhe. Lissu: Naomba uangalie maelezo yako, nenda palipo andikwa makazi usome pameandikwa makazi yako wapi?
Shahidi wa kificho P9: Pameandiwa Mwakibete.
Mhe. Lissu: Kwenye mstari wa kwanza kabisa sema palivoandikwa hapo? Kwamba unaishi?
Shahidi wa kificho P9 : Pameandikwa Mwakibete lakin nilihojiwa Mbeya.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unafahamu kwamba haya maeneo huwa yanatangazwa kwenye gazeti la serikali na waziri wa TAMISEMI
Shahidi wa kificho P9 : sifahamu
Mhe. Lissu: Umeonyesha gazeti la Serikali linaloonyesha Mwakibete ni Mbeya,?
Shahidi wa kificho P9; Hapana.
Mhe. Lissu: unafikri unaandika andika tu unaingizwa chaka na mapolisi na wewe unaandika tu.
Mhe. Lissu: Uliulizwa unafanya shughuli gani na ulisema unafanya kazi ya fundi umeme na kazi zako unafanya katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako unafanya kazi gani?
Shahidi wa kificho P9 : Mkulima
Mhe. Lissu: Kazi ni mkulima hapa unajifanya fundi umeme, lugha gongana.
Watu wanacheka: 😂😂😂😂
Mhe. Lissu: nyie Waha wa kigoma wajanja sana nyie na mimi napenda watu wajanja kama wewe.
Mhe. Lissu: Uliulizwa unakumbuka kitu gani kilikukuta 2024, ukasema nilivutiwa na sera za CHADEMA na nikawanafatilia matangazo, mikutano n.k haya sasa soma maelezo yako mjanja wa Jiji la Mbeya…😁
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji hayo maelezo uliyosoma hapo kama yapo na ulivyosema jana
Shahidi wa kificho P9 : Hayapo
Mhe. Lissu : Uliandika kwa mapolisi wakakupuuza wakaandika ya kwao.
Mhe. Lissu: Katika matukio mengi uliyofatilia ulitaja matembezi ya yaliyoongozwa na Lissu yalianzia Uyole, na Heche Isanga, mwambie jaji kama Mhe. Heche yupo katika maelezo kayo
Shahidi wa kificho P9: Nilieleza ni Mnyika sio Heche.
Mhe. Lissu: Jana ulisema Heche alianzia Isanga, unataka niwasumbue majaji wakusomee ulichokisema??
Shahidi wa kificho P9: inawezekana nilikosea
Mhe. Lissu: Kazi yangu ni kukamata watu waongo kama wewe.
Shahidi wa kificho P9 : Hiyo unasema ww
Mhe. Lissu: ndio nasema.
Mhe. Lissu: Ulisema mnamo tarehe 3 April 2025 ukiwa nyumbani kwako wakati unaperuzi mitandao kupitia simu yako aina ya Samsung 8 pro, kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : kweli
Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako waeleze majaji kama kuna mahala popote ulikua unaangalia mitandao kupitia aina ya Samsung 8 pro.
Shahidi wa kificho P9: hayajaandikwa.
Mhe. Lissu: Asante, mmeuzwa na mapolisi.
Mhe. Lissu: Ulisema kwamba uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uweze kuimgia instagram lazima uwe na simu janja, account na bundle, hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P9 : hayapo.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana ulisema wakati unaingia kwenye instagram uliona video ya Tundu lissu na ukasema huo mtandao umeusahau.
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nimeusahau.
Mhe. Lissu: Kama umesahau inamaana, kwenye maelezo yako utakua umeandika.
Shahidi wa kificho P9: Sasa wewe unaniuliza mambo waliyoniuliza mawakili.
Mhe. Lissu: Jibu swali langu. Unanifundisha namna ya kukuhoji?
Shahidi wa kificho P9 : Ndio hakuna
Mhe. Lissu: Uliulizwa muonekano wa Tundu Lissu, ukasema alikua ukumbini alivaa kombati za kaki za chadema na tshirt nyeusi na bendera ya taifa na rangi za CHADEMA, kweli si kwei?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Sasa waeleze waheshimiwa majaji kama yapo katika maelezo yako.
Shahidi wa kificho P9 : Hakuna
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana uliulizwa alisema atauzuiaje ukasema tutafanya vurugu na kuuvuruga uchaguzi huo.
Shahidi wa kificho P9: Kweli
Part 211 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 20, 2026
Jana tuliishia Part 208 so leo tunaendelea na-;
Part 209.
Imepigwa high Court ya kikakamavu,
Majaji wameingia wapo watatu kama kawaida yao.
Mhe. Lissu nae yupo
Karani anasoma criminal session No. 19605/ 2025 Republic v. Tundu Lissu
Mawakili wa Serikali wanajitambulisha kama kawaida yao japo leo hawajaja kama utitiri.
Wakili wa Serikali anasema, shauri linakuja kuendelea kusikilizwa na tuna shahidi wa 14 kwa ajili ya maswali ya dodoso.
Jaji Ndunguru anamuuliza Mhe. Lissu kama yupo tayari.
Mhe. Tundu Lissu anasema mimi nipo tayari.
Jaji Ndunguru anamkumbusha Shahidi kwamba yupo chini ya kiapa.
Ikumbukwe kwamba leo tunaendelea na Shahidi wa kificho P9.
Mhe. Lissu: Shahidi habari za asubuhi
Shahidi wa kificho P9 : salama.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama uliandika maelezo tarehe 22 aprill 2025
Shahidi wa kificho P9: Ndio
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ukionyeshwa maelezo hayo utayatambua.
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nitayatambua
SHAHIDI ANAPELEKEWA MAELEZO YAKE.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama hayo ndio maelezo yako uliyoandika polisi tarehe 22 April 2025?
Shahidi wa kificho P9 : ndio ni yenyewe
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji nataka ku-impeach credit ya huyu witness, kwahiyo nitamsomea maelezo yake, nitamuonyesha maeneo ambayo nataka kumuhoji halafu nitamuomba ayawasilishe yapokelewe kama kielelezo.
Mhe. Lissu: Shahidi nitakusomea maelezo yako halafu tutahojiana kwasababu kuna mambo hayapo sawa kwenye maelezo yako, anamsomea maelezo shahidi…
Mhe. Lissu: Sasa shahidi umesikia nilichokisoma, waeleze waheshimiwa majaji kama nilichokisoma ndicho kilichopo kwako.
Sasa nataka nikueleze maeneeo nayotaka nikuhoji;-
1. Jana ulisema wewe ni mkazi wa Mbeya mjini, nataka nikuhoji hapo
2. Kwamba wewe kazi yako ni fundi umeme na unafanya kazi ndani ya maeneo ya Jiji la Halmashauri ya Mbeya
3. 2024 ulivutiwa na sera za CHADEMA na ukaamua kuwa mfuasi na ukawa unafatilia kwa karibu mikutano, matangazo na hotuba za vipngozi wa CHADEMA.
4. Ulizungumzia matembezi ya amani yaliyofanyika Mbeya 2024 na ukasema Mbowe alianzia Songwe na Lissu Uyole na Heche Isanga.
5. April 3, 2025 ukiwa nyumbani kwako ulikua unaperuzi mitandao ya kijamii kwa simu aina Samsung 8 pro nataka nikuhoji kuhusu hiyo simu.
6. Uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uingie kwenye mtandao huo lazima uwe na account na simu janja na bundle ili kuweza kuangalia picha na videos.
7. Wakati unaperuzi mtandao wa instagram uliona video ya Tundu Lissu lakini umesahau ilikua ni account ya nani.
8. Huyo Lissu uliyemuona alikua amevaa kombati ya kaki za chadema na tshirt nyeusi na alikua ukimbini na kulikua na bendera ya taifa na rangi za bendera ya CHADEMA.
9. Alisema tutavuruga uchaguzi kwa kufanya vurugu na kuvuruga uchaguzi huo.
10. Lissu alisema lazima tukichafue.
11. Ulipofika kwenye Kituo cha Polisi Mwanjelwa walikwambia wanataka wakufanyie tena mahojiano.
12. Nilihojiwa na mtu mmoja na mwingine wa pili alinihoji kwenye maswali mbalimbali.
13. Wakati unamjibu huyo anae kuhoji kwa mara ya pili niliona video ya Tundu Lissu, ndio nikaanza kufanya makosa.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi waeleze majaji kama ungependa maelezo yako yaingie kama kielelezo mahakamani?
Shahidi wa kificho P9: haina shida.
Upande wa Serikali : hatuna pingamizi
Mahakama: Yamepokelewa kama kielelezo D13
Part 210 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 208
Wakili wa Serikali
Cathbert: Eeh nini kiliendelea?
Shahidi wa kificho P9 : Nilienda kituo cha Polisi na nilipofika waliniambia ya kuwa nahitajika kama Shahidi hivyo natakiwa nihojiwe tena
Cathbert: Eeh endelea shahidi
Shahidi wa kificho P9 : Walinihoji na kuniandika maelezo yangu na baada ya kumaliza waliniruhusu kuondoka na kuniambia ya kuwa ntapohitajika watanitafuta na aliyenihoja na kuniandika maelezo ni mmoja na mwingine alikuwa akichangia kuniuliza maswali mbalimbali.
Cathbert: Aliyekuhoji kama shahidi alikuhoji kwa ajili ya jambo gani?
Shahidi wa kificho P9 : Alinihoji juu ya kuhamasisha kuzuia uchaguzi na hilo jambo lilianzaje ambapo nilimueleza ya kuwa niliona clip katika mtandao kuhusu huo uhamasishaji na hiyo clip ilikuwa ni ya Lissu akihamasisha kuzuia uchaguzi.
Cathbert: Wahe. Majaji kwa Shahidi huyu ni hayo tu.
Anasimama Wakili wa Serikali Mkude
Mkude: Tuna Hoja hapa kwa kuwa Shahidi kamaliza na muda uliofika tulikuwa tunaomba kama hakuna pingamizi kwa upande wa Lissu tuweze kuendelea kesho na Cross Examination
Mhe. Lissu: Sina Objection
Mahakama : Mhe. Lissu hizi dakika 19 hazitoshi kumaliza Cross yako
Mhe. Lissu: Wahe. Majaji naweza kwenda kwenda ila siwezi ku-promise ya kuwa nitamaliza
Mahakama : Basi for consistency nzuri ya ushahidi tuharuhusu kuendelea kesho asubuhi na mapema na ile hoja ya submission on the notice of List of Additional tunaifanyaje?
Mhe. Lissu: Nilikuwa naomba tukimalizana na P9 kwa kesho tuendelee na mashahidi wengine kisha mwisho turudi kwenye hoja za hiyo submission on Notice of List of Additional.
Mkude: No objection.
Mahakama imehairishwa mpaka kesho saa tatu asubuhi.
Mnisamehe sana leo updates zimesuasua kwasababu afya yangu imeyumba kidogo.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 207
Wakili wa Serikali Cuthbert anaendelea kumuongoza Shahidi wa kificho P9.
Cathbert: Unakumbuka nini kuhusu 3/4/2025?
Shahidi wa kificho P9 : nilikuwa nyumbani kwa tarehe hiyo na nilikuwa nikiperuzi kwenye mitandao
Catherbert: Simu ilikuwa ni ya Aina gani?
Shahidi wa kificho P9 : Simu yangu ilikuwa ni Samsung 8 Pro na nilikuwa naperuzi kwa kuingia katika Akaunti ya IG ambao ni mtandao wa kijamii ambao unakuhitaji uwe na Akaunti ya kuweza kuingia na pia uwe na simu janja pamoja na bundle la internet ili kuangalia vitu humo Instagram.
Cathbert: Kwenye IG unaangalia Nini humo?
Shahidi wa kificho P9: picha na video
Cathbert: Eeh baada ya kufungua?
Shahidi wa kificho P9 : Baada ya kufungua IG na kuingia niliona video ya Lissu ambayo ilitumwa katika Akaunti ambayo nimeisahau.
Cathbert: Eeh uliona nini katika hiyo video?
Shahidi wa kificho P9 : Nilimuona Lissu akihamasisha kufanya vurugu na kuzuia uchaguzi.
Cathbert: Mazingira ya Video yalikuwaje?
Shahidi wa kificho P9 : Mazingira yalikuwa ni ya ukumbi
Cathbert: Na Lissu alikuwa vipi?
Shahidi wa kificho P9: Lissu alikuwa kavalia Kombati la Chadema, ndani kavaa Tshirt nyeusi pia kulikuwa kuna bendera ya Taifa na bendera ya Chadema.
Cathbert: Huo uchaguzi alikuwa anauongelea kuuzuia ni upi?
Shahidi wa kificho P9: Ni uchaguzi wa Raisi, Wabunge na Madiwani.
Cathbert: Lissu alisema atauvuruga uchaguzi kwa namna gani?
Shahidi wa kificho P9 : Alisema atafanya vurugu na kuzuia uchaguzi ili usifanyike kwa kusema ya kuwa "Ni lazima tukichafue"
Bwana P9 nae anaendelea hapa kutueleza mambo yake.😂
Cathbert: Eeh baada ya wewe kusikia hotuba hiyo ulichukua hatua gani?
Shahidi wa kificho P9 : kwa ukweli kwa kipindi kile mimi kama mfuasi wa Chama nilihamasika
Cathbert: Unakumbuka nini kuhusu tarehe 4/4/2025?
Shahidi wa kificho P9 : Hiyo tarehe nilikuwa nyumbani na majirani zangu tulikutana na kujadili hilo suala tuliloliona katika video kwa kusema ya kuwa kama Mwenyekiti kasema tukichafue na tuzuie uchaguzi itakuwaje sasa hivyo tukawa tunafanya majadiliano.
Cathbert: Eeh nini kiliendelea?
Shahidi wa kificho P9: Baada ya hapo kuna Jamaa yangu aliniomba namba yangu ya simu na kila mtu akaendelea na shughuli zake
Cathbert: Unakumbuka nini kuhusu tarehe 5/4/2025?
Shahidi wa kificho P9 : Hiyo tarehe nilipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha ya kuwa yeye ni mteja na anahitaji fundi Umeme wa kumfanyia kazi nyumbani kwake, na baada ya hapo nikamuelekeza nilipo ambapo akasema Sawa.
Cathbert: Eeeh nini kiliendelea
Shahidi wa kificho P9: Basi nkaenda sehemu tuliyopanga tuonane na nilivyofika akajitambulisha ya kuwa yeye ni Afisa wa Polisi na akanionyesha kitambulisho chake cha kazi na kusema anatokea kituo cha Polisi Mwanjelwa.
Cathbert: Eeh baada ya Utambulisho?
Shahidi wa kificho P9 : Aliniambia kwa sasa niko chini ya ulinzi kwa kosa la uchochezi na hivyo twende kituo cha Polisi
Cathbert: Eeh baada ya kufika kituo cha Polisi?
Shahidi wa kificho P9 : Alinikabidhi kituo cha Polisi ambako nilihojiwa na baadae jioni ndugu zangu walikuja kuniwekea dhamana na nikaambiwa natakiwa kuripoti kila siku ya ya Jumatatu
Cathbert: Unakumbuka nini kuhusu tarehe 22/4/2025?
Shahidi wa kificho P9: Nilipigiwa simu majira ya Asubuhi na mtu aliyejitambulisha kuwa ni Askari Polisi na ninahitaji Kituo cha Polisi Mwanjelwa.
Part 208 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 206
Ubishani unaendelea kati ya Mhe. Lissu na Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Mshitakiwa kama aliandika kwenye maelezo yake kufanya vurugu na yeye akajibu kuzuia uchaguzi ndiyo kufanya vurugu zenyewe, namuomba shahidi atueleze alivosema kuzuia uchaguzi ndiyo kufanya vurugu alimanisha nini.
Mhe.Lissu: naomba mahakama imsomee record wakili labda itamsaidia kumuongoza vizuri.
Jaji Ndunguru: Upande wa mashitaka bado mnasimamia hilo.
Wakili Mkude: kwasababu mshitakiwa amesema twende kwenye swali specific naomba tusomewe ili iweze kutuongoza.
Jaji Ndunguru : mshitakiwa aliuliza Mwenyekiti Tundu Lissu alisema “tukafanye vurugu" maneno hayo yapo kwenye statement yake D12 shahidi akaseme hayapo.
Wakili wa Serikali: sawa waheshimiwa Majaji, shahidi umeulizwa kuwa ulitakiwa kuripoti Polisi Kila baada ya siku tatu na ukaulizwa kama maneno hayo yapo kwenye maelezo yako ukajibuje?
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Wakili wa Serikali; shahidi kutoka kwenye kielelezo hicho soma mstari wa 12 kutoka juu.
Shahidi wa kificho P3 : ilipofika jioni walikuja ndugu zangu wakanidhamini huku nikitakiwa kuripoti Kila baada ya siku tatu.
Mhe.Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba niweke pingamizi kwa hilo swali, shahidi amezungumzia jambo la kuripoti mara mbili, mara ya kwanza ni alipochukuliwa maelezo ya kwanza na kudhaminiwa kwenye ushahidi wa leo amesema aliambiwa kuripoti kila baada ya siku tatu alipoandika maelezo ya mara ya pili, hakuna sehemu nyingine amezungumzia jambo hilo hivyo basi wakili anapaswa kuuliza katika maeneo hayo.
Jaji Ndunguru : Upande wa mashitaka.
Wakili wa Serikali: shahidi aliulizwa na akajibu na wote tumesikia.
Jaji Ndunguru : upande wa mashitaka kuna shida hapo.
Wakili wa Serikali: hapana shida Mheshimiwa Jaji.
Mahakama inaangua kicheko 😃😃😃
Wakili wa Serikali: Shahidi umeulizwa maswali mengi kuhusiana na kwamba kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA, kama mshitakiwa anakufahamu, kama ulijiandikisha na kujiorodhesha. Shahidi wakati unajiunga na CHADEMA ni nani alikuwa Mwenyekiti wa CHADEMA.
Jaji Ndunguru : wakili hilo ni swali jipya kabisa, tuzingatie record.
Mhe.Lissu: Mawakili kama hamna maswali si mnanyamaza.
Jaji Ndunguru : tuendelee. Shahidi umeshamaliza kutoa ushahidi wako Sasa unaweza kuondoka.
Wakili wa Serikali anasema wako na Shahidi mwingine ambae ni P9 huyu nae ni Shahidi wa kificho.
Anaingizwa kwenye kila kibanda umiza, naambiwa ukiingia mle ndani ya iko kibanda joto ni kali sana kama upo Sudan
Huyu P9 na ni Shahidi wa 14 wa Jamhuri
Umri - 35
Dini - Mkristo
Anapewa Bible then anakula kiapo.
Mkude Wakili wa Serikali anasema Wakili Cathbert Mbilinge atamuongoza P9 shahidi wetu.
Wakili Cathbert: Shahidi wewe ni mkazi wa wapi?
Shahidi wa kificho P9: mimi ni mkazi wa Mbeya na shughuli zangu ni za fundi Umeme na ninafanya mbeya yote kwa maana ya popote ntapohitajika.
Wakili wa Cuthbet : Ulikuwaje fundi Umeme
Shahidi wa kificho P9 : Nilipita chuo cha ufundi veta kusoma mafunzo ya Umeme 2008 to 2010 kwa Umeme wa viwandani na majumbani.
Cathbert: Shahidi unakumbuka nini kuhusu mwaka 2024 kwa mambo ya siasa
Shahidi wa kificho P9 : nakumbuka kwa masuala ya kisiasa kwa 2024 nilivutiwa na sera za Chama cha CHADEMA na hivyo nikawa mfuasi wa Chama.
Cathbert: Ulichukua hatua gani baada ya kuvutiwa na sera za Chadema?
Shahidi wa kificho P9 : Nilianza kufatilia kwa karibu shughuli, hotuba na mikutano ya CHADEMA.
Cathbert: Ni tukio gani ulilolifatilia kwa karibu?
Shahidi wa kificho P9 : nimefatilia matukio mengi ikiwemo maandamano ya Amani ambayo yalikuwa kutoka Uyole kwenda Kabwe, Isanga kwenda kabwe na Airport Songwe kwenda Kabwe.
Cathbert: Ni viongozi gani walioongoza hayo matukio
Shahidi wa kificho P9 : Kiongozi wa kutoka Uyole kwenda Kabwe alikuwa ni Lissu, Isanga kwenda kabwe alikuwa Heche na wa Airport Songwe kwenda Kabwe simkumbuki.
Part 207 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 205
Mhe. Lissu anaendelea na Cross Examination.
Mhe. Lissu: katika maelezo yako kuna sehemu yoyote umesema mwenyekiti Tundu Lissu amesema tufanye vurugu?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana hakuna hayo maelezo
Mhe. Lissu: unafahamu maana ya neno uasi.
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: Ngoja nikwambia, waheshimiwa majaji namsomea shahidi maana ya uasi kutoka katika kamusi ya Kiswahili…swali langu kaka, waeleze waheshimiwa majaji kwa kuwapinga wenye mamlaka au taratibu zilizopo ni uhaini?
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: Shahidi mimi ninasheria ya uchaguzi hapa ya urais, madiwani na ubunge, sheria hiyo haina popote iliposema kuzuia uchaguzi ni kosa la jinai, wewe unasemaje?
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: hapa nina sheria kuu ya makosa ya jinai na hakuna popote iliposema kuzuia uchaguzi ni kosa la jinai, wewe unasemaje?
Shahidi wa kificho P3 : mimi sijui.
Mhe. Lissu: umeeleza mahakama kwamba ulipokamatwa tarehe 4 april 2025 na kwenda kuandikwa maelezo kwa tuhuma za kupanga njama za kuzuia uchaguzi, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : kweli.
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji hizo tuhuma ziliishia wapi?
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama umefunguliwa mashtaka ya jinai ya kupiga watu mawe na kupanga njama za kufanya vurugu
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: ulipaanga njama na mapolisi ujifanye mwanachadema uje kutoa ushahidi hapa?
Shahidi wa kificho P3 : si kweli
Mhe. Lissu: kama si kweli kwanini hujafunguliwa mashtaka
Shahidi wa kificho P3 : sijui
Mhe. Lissu: kwa muda wote wa miezi mitano uliyokua unaenda kuripoti polisi, walikua wanakwambia nini?
Shahidi wa kificho P3 : walikua hawaniambii chochote, wananiambia niende
Mhe. Lissu: waambie majaji kama wakati wote unaripoti polisi waliwahi kukuuliza chochote kuhusu tuhuma zako za kupiga watu mawe?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: nani alikulipia nauli ya kutoka Mbeya mpaka Dar es salaam
Shahidi wa kificho P3 : nimejilipia mwenyewe
Mhe. Lissu: hapa Dar es salaam umefikia wapi?
Shahidi wa kificho P3 : nimefikia guest
Mhe. Lissu: nani anakulipia?
Shahidi wa kificho P3 : najilipia mwenyewe
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji kama mpaka leo hii kuna kiongozi au mwanachama wa chadema aliyekutishia chochote juu ya maisha yako
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: waambie washeshimiwa majaji kama kuna kiongozi au mfuasi yoyote wa CHADEMA ametishia familia yako
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: Kuna polisi ameleta kiapo mahakamani akisema kwamba shahidi kama wewe umetishiwa maisha.
Shahidi wa kificho P3 : Hapana mimi sijawahi kutishiwa maisha.
Mhe. Lissu: sina maswali tena kwa shahidi huyu.
Jaji Ndunguru : Re-examination upande wa mashitaka.
Wakili wa Serikali: Sasa shahidi umeulizwa swali kuhusu huyo askari Polisi aliyekukamata, mheshimiwa Jaji naomba kielelezo, shahidi Sasa naomba usome kielelezo ukurasa wa mwisho mstari wa tatu.
Shahidi wa kificho P3 : wakati tunaendelea kubishana alikuja mtu aliyejitambulisha kwangu kuwa yeye ni Askari Polisi.
Wakili wa Serikali; kwa hiyo alijitambulisha kwako kuwa yeye ni?
Shahidi wa kificho P3 : kuwa yeye ni Askari Polisi.
Wakili wa Serikali: Shahidi umeulizwa swali na mshitakiwa kwamba kama kuna neno katika maelezo yako ‘kufanya vurugu’ ukajibu yapo, alivyokuonesha ukasema kuzuia Uchaguzi ndiyo kufanya vurugu zenyewe, sasa onesha uhusihano kati ya maneno kufanya vurugu na kuzuia uchaguzi.
Mhe.Lissu: waheshimiwa Majaji Sasa naona Wakili anataka kuelezea mambo ambayo shahidi ameyakataa, anataka kuintroduce kitu kipya.
Kama Mahakama itamruhusu kufanya hivyo nitaomba nimcross examine shahidi upya kwenye suala hilo.
Part 206 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 204
Mhe. Lissu anaendelea na Cross examination.
Mhe.Lissu: ulivosogea pembeni akakwambie twende kituoni ukatoe maelezo, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo?
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Mhe.Lissu: badala yake yapo maneno yanayosema kwamba alikuja mtu aliyejitambulisha kuwa ni Askari Polisi na kunikakamata. Ni sahihi
Shahidi wa kificho P3 : ndiyo ni sahihi.
Mhe.Lissu: kwa hiyo hapakuwepo na maongezi alifika na kukukamata.
Shahidi wa kificho P3: sahihi
Mhe.Lissu: umesema ulipofika kituoni alikuweka mahabusu na baadae ukahojiwa kuwa unahamasisha uasi sasa waeleze waheshimiwa Majaji kama kuna maneno kwanini ulikuwa unahamasisha uasi.
Shahidi wa kificho P3: hapana hayapo.
Mhe.Lissu: Ahsante.
Mhe. Lissu: Twende tarehe 17 April 2025 waeleze waheshimiwa majaji kama katika maelezo yako kuna sehemu umesema kuwa aliyekuandika maelezo mwanzo ya terehe 4 april 2025 ndio aliyekuandika maelezo tarehe 17 april 2025?
Shahidi wa kificho P3 : Hayapo.
Mhe. Lissu: umesema ulipoandika maelezo mara ya pili akakwambia uendelee kuripoti kila baada ya siku tatu, yapo katika maelezo yako?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana.
Mhe. Lissu: umesema kwamba wewe kazi yako ni dereva wa boda boda kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : kweli
Mhe. Lissu: waambie waheshimiwa majaji kama umeonyesha leseni
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe. Lissu: boda boda ni pikipiki kweli si kweli
Shahidi wa kificho P3 : Ni kweli
Mhe. Lissu: Umewaambia usajili wa hiyo pikipiki?
Shahidi wa kificho P3: Hapana
Mhe. Lissu: umewaonyesha waheshimiwa majaji kadi ya usajili wa hiyo pikipiki
Shahidi wa kificho P3: Hapana.
Mhe. Lissu: Shahidi naomba unisaidie, kwasababu kijiwe chako hatukijui kwasababu kimefichwa, kadi huna, leseni huna, je pikipiki umeleta?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: kwa hali hii kuna mtu ataweza kuthibitisha kwamba wewe ni dereva boda boda?
Shahidi wa kificho P3 : Mimi sijui.
Mhe. Lissu: unasema uliwahi kushiriki maandamano aliyowahi kuongozwa na Mbowe, ulijiandikisha sehemu yoyote.
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: Hata uliwahi kupigwa picha ukiwa kwenye maandamano hayo.
Shahidi wa kificho P3 : hata sijui
Mhe. Lissu: Unasema uliwahi kushiriki katika kongamano la vijana, uliwahi kujiandikisha?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: Uliwahi hata kujiandikisha kwa viongozi wa BAVICHA Mkoa wa Mbeya?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana.
Mhe. Lissu: sasa kwanini tusiseme wewe ni pandikizi la akina Kingai na mapolisi wake.
Shahidi wa kifichoP3 : Kimya
Mhe. Lissu: unasema ulishiriki mkutano wangu, ulijiandikisha popote?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: sasa weleze waheshimiwa Majaji wataamini vipi kuwa wewe ni mfuasi wangu na mwanachama wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3 : Mimi sijui sasa, kama unanikataa mm sio mfuasi wako sawa.
Mhe. Lissu: sikukatai kaka, mimi sikujui na ninaogopa watu wasiojulikana kwasababu wanateka watu, wanabambikia watu kesi na kuua kwahiyo tutajua kama sio wewe mmoja wapo?
Shahidi wa kificho P3 : mimi sijui.
Mhe. Lissu: umesema ulikua na vijana wenzako kijiweni ukiwashawishi, waeleze waheshimiwa majaji kama umetaja orodha yao na majina yao.?
Shahidi wa kificho P3 : sijawataja.
Mhe. Lissu: Umeeleza kwamba ulikamatwa na askari Polisi, umemtaja kwa jina huyo askari polisi? Au hata namba yake tu na cheo je?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Mhe. Lissu: tunaendelea, ninachukizwa na nyie mapandikizi ya polisi mnaletwa hapa halafu mnafichwa ndani ya kizimba, ngoja tuendelee.
Mhe. Lissu: unasema mlifikia uamuazi wa kupiga watu mawe watakaoenda kupiga kura, kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : kweli
Mhe. Lissu: na huo ulikua ni uamuzi wako binafsi, kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : Lakini kutoka na ushawishi wako.
Mhe. Lissu: kuna mahali popote katika maelezo yako umesema Mwenyekiti Tundu Lissu amesema tupige watu mawe?
Shahidi wa kificho P3 : Hapana
Part 205 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 203
Mhe. Lissu anaendelea na Cross Examination,
Jaji Ndunguru: upande wa mashitaka.
Mkude: No objection.
Jaji Ndunguru : turejee kifungu 194 cha CPA.
Mkude: kifungu cha 194 kwa ujumla wake ni kuhusu protection ya ushahidi, kwa sababu shahidi au mshitakiwa anaweza akaomba impeachment, pale anapoomba shahidi apewe kielelezo hivo tunaweza kuendelea mheshimiwa Jaji.
Mhe.Lissu: Iko hivyo waheshimiwa Majaji, sikuwa nataka kuona jina lake kwenye kielelezo hicho bali nataka asome maelezo yake.
Mhe.Lissu: kwa hiyo shahidi ulitaka kuficha ukweli mahakamani.
Shahidi wa kificho P3 : hapana.
Mhe.Lissu: mbona haukusoma kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA na umeiandika kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi wa CHADEMA labda askari aliyeandika maelezo yangu alikosea.
Mhe.Lissu unaidanganya mahakama, soma kama ilivoandikwa.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi/ mwanachama wa CHADEMA.
Mhe.Lissu: Sasa ulikuwa unaficha nini. Shahidi swali langu la pili kwenye maelezo yako umesema kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Sasa waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Shahidi wa kificho P3 : kongamano hilo halikufanikiwa.
Mhe.Lissu: hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Mhe.Lissu: shahidi umesema kwa bahati mbaya au nzuri kongamano hilo halikufanyika lilizuiliwa na serikali kweli au si kweli.
Shahidi wa kificho P3 : kweli.
Mhe.Lissu: wewe mfuasi wa CHADEMA kongamano la CHADEMA shughuli halali ya chama kuzuiliwa kwako ni bahati nzuri.
Shahidi wa kificho P3: sijui, mimi sielewei
Mhe.Lissu: ndiyo maana nikakuuliza tutajuaje kama wewe siyo pandikizi.
Shahidi wa kificho P3 : hilo swali nimeshalijibu tuendelee.
Mhe: Lissu: usijali tutaendelea kwenye maelezo yako ya Leo umesema ulikuwa na simu, Sasa kwenye hayo maelezo yako ya Polisi kuna sehemu uliandika kama ulikuwa na simu.
Shahidi wa kificho P3 : haipo.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua au haujui kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia compyuta.
Shahidi wa kificho P3 : sijui, mimi sina utaalamu huo wa kutumia compyuta.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia Television.
Shahidi wa kificho P3 : utaalamu huo sina.
Mhe.Lissu: unajua kama unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia tablet.
Shahidi wa kificho P3 : sijui huo utaalamu.
Mhe.Lissu: Kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa ulikuwa na simu
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe.Lissu: kwenye maelezo yako umesema uliyasikia maneno yangu kupitia video YouTube, kuna mashahidi wengine wamesema video hiyo ilikuwa na masaa 3 na madakika, waeleze waheshimiwa Majaji kama kuna sehemu umeandika video hiyo ilikuwa na muda gani.
Shahidi wa kificho P3 : hakuna
Mhe.Lissu: umesema umemfahamu mheshimiwa Lissu kupitia mitandao ya kijamii. Waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako umeandika hilo jambo.
Shahidi wa kificho P3 : hapana hayapo.
Mhe.Lissu: umesema mwezi march 2025 ulihudhuria mkutano uliohutubiwa na Mheshimiwa Tundu Lissu katika viwanja vya Ruanda nzovwe, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3: hayapo
Mhe.Lissu: umesema wakati ukiwahamasisha vijana wenzako hapo kijiweni alikuja mtu aliyejitambulisha kuwa ni Askari Polisi na kukuita pembeni kwamba njoo tuongee, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : napitia kidogo
Mhe.Lissu: haujapaona hadi mwishoni kwenye paragraph ya mwisho.
Shahidi wa kificho P3 : naomba nikusomee, alikuja mtu aliyejitambulisha ni Askari Polisi.
Mhe.Lissu: swali langu ni kwamba hayo maneno akaniita pembeni akaniambia njoo tuongee, hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Part 204 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 202
Mhe. Lissu ameanza kumfanyia Cross examination Shahidi wa kificho P3.
Mhe. Lissu: shahidi hapo ulipo unaweza kuniona?
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe. Lissu: kwa taarifa yako hata mm siwezi kukuona kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : sahihi.
Mhe. Lissu: nataka nikuhoji kutokana na ushahidi wako na nashukuru umesema wewe ni mfuasi wa CHADEMA, sasa naomba uwaeleze majaji, mfuasi wa CHADEMA anakua na kutambulisho gani?
Shahidi wa kificho P3 ; anakua hana kitambulisho kwasababu anakua bado hajawa mwanachama.
Mhe. Lissu: mimi kiongozi wa CHADEMA na mtu yoyote aliyeopo hapa mahakamani atajuaje kama wewe ni mfuasi wa CHADEMA, huna kitambulisho na pia sikuoni?
Shahidi wa kificho P3 : hilo ni suala la imani
Mhe. Lissu: twende taratibu kaka, waeleze majaji kama wafuasi wa chadema huwa wanaorodheshwa mahali ili kuwatambua.
Shahidi wa kificho P3 : binafsi sijajua huwa wanaorodheshwa wapi?
Mhe. Lissu: kwahiyo hujaorodheshwa?
Shahidi wa kificho P3 : sahihi.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama wafuasi wa CHADEMA kuna mahali huwa wanaenda kujitambulisha ili wajulikane
Shahidi wa kificho P3 : hakuna.
Mhe. Lissu: hapo ulipo kwenye kiboksi na mimi hapa nilipo kama kuna namna mimi naweza nikaelewa au kujua kama wewe ni mfuasi wa CCM na sio CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3 : sijui utajuaje ila mm ni mfuasi wa CHADEMA
Mhe. Lissu: na nitajua kama ww sio pandikizi la Polisi kwasababu hujajiandikisha popote wala huna chochote cha kukutambulisha kuwa ni mfuasi wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3 : itabidi uamini tu na uiamini mahakama tukufu kwasababu mimi sijui kwa kweli utawezaje kunitambua.
Mhe. Lissu: mfusi wa CHADEMA huwa anaalama usoni au kifuani kuwa yeye ni mfuasi wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3: sijui
Mhe. Lissu : waeleze majaji kama uliandika maelezo Polisi tarehe 17 april 2025?
Shahidi wa kificho P3 : ndio
Mhe. Lissu: ukionyeshwa hayo maelezo yako utayatambua?
Shahidi wa kificho P3 : ndio
Mhe. Lissu: naomba shahidi apewe maelezo yake ya tarehe 17 april 2025.
Mkude: Hatuna pingamizi.
SHAHIDI ANAPEWA MAELEZO YAKE.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama hayo ndio maelezo uliyoyaandika tarehe 17 april 2025?
Shahidi wa kificho P3 : ngoja kidogo nayapitia.
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji kama hayo ni maelezo yako?
Shahidi wa kificho P3 : ndio yenyewe
Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji nataka ku-impeach credit ya shahidi huyu, nitamsomea maelezo yake, nitaonyesha maeneo ambayo nataka kumhoji halafu nikimaliza nitakuomba uyawasilishe kama kielelezo.
Shahidi wa kificho P3 : sawasawa.
Mhe.Lissu: anamsomea shahidi maelezo yake.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama nilichokisoma ndicho kilichoko kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : ndiyo ulichokisoma ndicho kilichoko kwenye maelezo yangu.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi nataka nikuhoji kwenye eneo unalosema wewe ni mfuasi wa CHADEMA na maeneo mengine kadri nitakavyokuhoji kutokana na ushahidi wako.
Mheshimiwa Lissu anamsomea shahidi maeneo yote anayotaka kumhoji.
Maeneo 8.
Mhe.Lissu: Sasa hili nikuhoji sawasawa naomba uwaeleze waheshimiwa Majaji kama ungependa maelezo yako yapokelewe kama kielelezo mahakamani.
Shahidi wa kificho P3: ndiyo napendelea iwe hivyo.
Mhe.Jaji: itakuwa D12
Mhe.Lissu: ahsante waheshimiwa Majaji, naomba shahidi apewe kielelezo D12
Mhe.Lissu: Sasa swali langu la kwanza ni kwamba kwenye ushahidi wako leo umeieleza mahakama kuwa wewe ni mfuasi wa CHADEMA tangu mwaka 2021, ni kweli au si kweli.
Shahidi wa kificho P3 : ni kweli.
Mhe.Lissu: kwenye kielelezo D12 wasomee waheshimiwa Majaji pale unapoanzia mimi pia ni........ endelea hadi nitakapokwambia inatosha.
Shahidi wa kificho P3 : mimi pia ni mfuasi wa chama hicho.....
Shahidi anasitasita katika kusoma.
Mhe.Lissu: naomba pia nipewe kielelezo hicho naona kama shahidi anatupoteza.
Part 203 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 201
Anasimama Wakili wa Serikali Mkude anasema tunashahidi mwingie wa kulindwa ni P3,
Mpaka sasa huyu ni shahidi wa 13.
Shahidi ameingia kwenye kijumba cha mbao tayari.
Sasa anajitambulisha.
Shahidi wa kificho P3 : Nina miaka 35
Shahidi wa kificho P3: dini yangu muislamu
Shahidi wa kificho P3: naishi halmashauri ya Mbeya mjini, mtaa wa Mwamtengule kata ya Syesye
Shahidi wa kificho P3: najishughulisha na kazi ya dereva boda boda
Shahidi wa kificho P3: shughuli zangu nafanyia katika halmashauri ya jiji la Mbeya.
Shahidi wa kificho P3: nina miaka nane tangu naendesha boda boda
Shahidi wa kificho P3: mimi ni mfuasi wa CHADEMA
Shahidi wa kificho P3: nimekua mfuasi tangu 2021 mpaka sasa bado ni mfuasi
Shahidi wa kificho P3: nimewahi kushiriki matukio baadhi kama kongamano la kutoka Mbalizi mpaka Kabwe tulipoenda kumpokea Mhe. Mbowe mwaka 2024.
Tukio lingine ni kongamano la vijana lakin bahati mbaya au nzuri hatukufanikiwa kwasababu serikali ilizuia.
Shahidi wa kificho P5: tarehe 4 april 2025 nakumbuka kijiweni kwangu kwenye boda boda nilikua nachezea simu yangu nikapata kuona hotuba fupi ambayo Mhe. Tundu Lissu akizungumzia uchaguzi uliopangwa kufanyika 2025.
Shahidi wa kificho P3 : hotuba niliiona youtube.
Shahidi wa kificho P3 : namfahamu Tundu Lissu kupitia mitandao ya kijamii baada ya kuwa nafatilia sana chama cha CHADEMA tangu mwaka 2021.
Katika chama Tundu Lissu ni mwenyekiti wa CHADEMA, baada ya kusikiliza ile hotuba pale kijiweni nikaanza kuwashirikisha wanachama wenzangu wa boda boda na kuanza kuwashawishi wengine wenye mapenzi na CHADEMA kufanya yale mh. Tundu Lissu ameyasema.
Niliwashawishi tuwe kitu kimoja kupambana kuzuia uchaguzi 2025, tulipanga kuzuia uchaguzi kwa namna ya kwamba watu watakaoenda kupiga kura kuwafanyia fujo ikiwepo kupigwa mawe, ushawishi nilikua naufanyia katika kijiwe changu cha pikipiki, baada ya kushawishi wenzangu kuna baadhi waliliridhika na ushawishi wangu na baadhi hawakuridhika.
Shahidi wa kificho P3 : baada ya hapo alitokea mtu mmoja akanipoint kwenye kijiwe na akaniomba tuongee mara moja, nikaenda kumsikiliza na akajitambulisha kuwa. Yeye ni ofisa wa polisi, akaniambia nahitajika twende kituo cha polisi kwa mahojiano yangu mimi na yeye nilivyofika kituo cha polisi wakaniambia nitoe viatu na mkanda na wakaniweka mahabusu.
Wakili: Shahidi P3 baada ya kukaa mahabusu nini kilifuata
Shahidi wa kificho P3 : baada ya muda mchache nikapelekwa kwenye chumba kingine wakaanza kunihoji kwamba nilikuwa naongea nini pale kijiweni, kwanini nilikuwa nahamasisha kufanya uasi.
Wakili: walikuuliza kwa nini unahamasisha uasi gani kama unakumbuka.
Shahidi wa kificho P3: kwanini nahamasisha uasi wa kuzuia uchaguzi wa 2025.
Wakili: Sasa shahidi baada ya maelezo hayo nini kilifuatia.
Shahidi wa kificho P3: waliniambia nitafute mtu wa kunidhamini ili niweze kuendelea na taratibu nyingine.
Wakili: ikawaje.
Shahidi wa kificho P3: nilimpata ndugu yangu akaja kunidhamini.
Wakili: nini kilifuata
Shahidi wa kificho P3: nilipata ndugu yangu akaja kunidhamini. Nikaambiwa niwe naripoti Kila baada ya siku tatu.
Wakili: ulikuwa unaripoti wapi.
Shahidi wa kificho P: nilienda kuripoti Kituo cha Polisi Ilonga.
Wakili: ulivoenda kuripoti ikawaje.
Shahidi wa kificho P3: nikaingia ndani kituoni na kukutana na huyo askari aliyeniandika maelezo toka mwanzo.
Wakili: huyo Askari aliyekuandika maelezo kutoka Mwanzo anaitwa nani kama unakumbuka.
Shahidi wa kificho P3 : namkumbuka kwa jina moja anaitwa Amani.
Wakili: baada ya kukutana na Amani mlifanya nini.
Shahidi wa kificho P3: aliniandika maelezo tena na kuniambia naendelee na utaratibu wa kuripoti.
Wakili: waheshimiwa Majaji wa Mahakama kuu kwa Shahidi huyu ni hayo tu
Part 202 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.