#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 27
Anaendelea Wakili wa Serikali wakuitwa Wisdom.
Wisdom : Ulipokuwa unasema wasaidizi wako watekeleze kwa mujibu wa sheria? Maana yake nini?
Bwana Jela: Kufanya kwa mujibu wa sheria tu. Kama mchungaji anaingia kwa mambo ya kiroho peke yake.
Wisdom: Uliulizwa umeleta kiapo kinzani kujibu majibu ya mjibu maombi wa nne. Ukasema hujaleta? Kwanini.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikuleta kwasababu yeye ni mjibu maombi kama mimi.
Wisdom: Ulisema mawakili wote lazima wakaguliwe maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): kufuata sheria tu. Kuandika comment au kutoandika kunazuia sheria.
Wisdom: hebu eleza huwa mnakaguaje nyaraka?
Ntamamiro (Bwana Jela : mfano kitabu tunakagua kuangalia kuna kitu chochote hatari ndani yake.
Wisdom: Nimemaliza.
Anasimama Narindwa Wakili wa Serikali.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani walioleta maombi ni akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela: Kulwa Maduhu, Nashon na Kisabo.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani Maduhu mlimzuia asiingie?
Ntamamiro (Bwana Jela: Hakuwepo kwenye orodha na pia hakukuwa na ombi kutoka kwa Lissu.
Wakili wa Serikali Narindwa : Nimemaliza na tumemaliza, hatuna la ziada.
Majaji wanaandika.
Jaji Rumisha Anamuuliza Seka. Mnataka kusema kuwa mnahitaji mawakili wawe na chumba chao au mnahitaji haki ya msingi ya faragha ya mawakili inalindwa?
Wakili John Seka : nafikiri tudeal na soft part of it. Haki ya msingi ni nini sio lazima chumba kiwepo.
Anasimama Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji msiwe na shaka vyumba vinaweza kuwepo.
Mimi naishi Ukonga na pale ukonga kuna vyumba havinaga kazi kabisa. Mfano viko vyumba viwili vya Mahakama ya mtandao. Huwa sio kila siku kuna kesi kama waliweza kuwa na Mahakama ya mtandao pale na vyumba vyake vipo kwanini chumba maalumu kabisa cha mawakili kisiwepo?
Jaji Rumisha: Nafikiri tutajielekeza kwenye kuhakikisha haki inalindwa sio lazima majengo.
Jaji Mruma anasemam sasa Maombi ya Msingi tulisema yatasikilizwa kwa njia ya maandishi.
Na scheduling order itakuwa kama ifuatavyo.
Submission za petitioners zitakuwa ni kabla ya Tarehe: Watajibu PO na kufile submission in chief yao. Kabla ya Tar. 24/08/2026. Rejoinder ya Petitioners kwenye majibu yao 07/09/2026.
Respondets Submission zao zitakuwa ni Tarehe: Submission P.O before 10/08/2026. Wataleta rejoinder ya PO na reply yao 07/09/2026.
Mention kabla ya uamuzi ni 16/09/2026.
Mhe. Lissu anasimama anasema na mimi mseme naleta majibu yangu lini?
Jaji Rumisha: Sasa na wewe kwenye PO ambayo wamewekewa waleta maombi unataka kujibu kama nani wakati wote ni washitakiwa au wajibu maombi?
Jaji Mruma: Amedakia, Mimi nakuelewa Lissu hata kwenye kesi za kawaida za madai defendants wanaweza kuwa na madai dhidi yao wenyewe na ikasikilizwa. Kwahiyo Lissu uko sahihi na tutakupatia haki hiyo hakuna shida.
ππππKwa kifupi Mruma ameingilia show. Naambiwa huyu Mzee ni miongoni mwa Ma Jaji senior sana wa Mahakama Kuu na uwezo wake ni mkubwa sana. Serikali imeshindwa kumpandisha cheo kwenda Mahakama ya Rufani kwasababu yeye huwa sio Chawa kabisa. Ni Mzee anayejielewa sana na yuko serious.
Tumekuwa tukishuhudia kesi nyingi hapa Mahakama kuu kwa mara ya kwanza tumeshuhudia Jaji ambae kwakweli anajua kazi yake.
Anasimama Wakili Ukashu anasema Mh. Jaji na mimi interested party hujatutaja kabisa? Tunafile lini?
Anasimama Narindwa anasema hata sisi tunashangaa huyu Ukashu na TLS wanataka kujibu PO wao ni akina nani?
Jaji Mruma: Sasa sikilizeni msichanganyikiwe. Sisi wengine tumekaa humu miaka 30. Mimi nimefanya hizi kazi mwaka wa 30 huu. Hakuna jipya. Wewe Ukashu utatumia tarehe za 4th Respondent kujibu. Msichanganyane kabisa.
Naahirisha kesi kwa tarehe nilizosema.
NB. Nakuomba usisahau kuchangia #ToneTone ili kufanikisha BARAZA KUU.
M-Pesa
Namba: 0744446969
Jina: CHADEMA HQ
NMB Bank
Namba ya Akaunti: 22606600140
Jina la Akaunti: Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 26
Tumerejea baada ya Mapumnziko ya nusu saa.
Anaanza Wakili wa waleta maombi Adv. Emmanuel Ukashu kumuhoji Maswali Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Ukashu: shahidi umewahi kuisikia TLS?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio naifahamu.
Adv. Ukashu: Ili mtu aingie Gerezani inahitajika wewe ndio umruhusu aingie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Ukashu: Ni sahihi ukipewa maelekezo yoyote lazima utekeleze na Kamishna General?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi
Adv. Ukashu: Maelekezo kutoka juu maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni maagizo ya kiutendaji unayopaswa kutekeleza.
Adv. Ukashu: Usipoyatekeleza unaweza kufukuzwa kazi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kwa mujibu wa sheria.
Adv. Ukashu: Unaweza kumbishia Boss wako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Siwezi kufanya hivyo.
Adv. Ukashu: Soma SUPP 4 tar. 12/03/2026 entry no. 8 hebu isome hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela): Huruma Tehejas mfungwa aliyekuja kumtembelea ni mfungwa na shida ya kisheria. Maoni hapakujazwa. Na sahihi hamna.
Adv. Ukashu: Sasa alienda wapi huyu Wakili kama hakuna uliposaini na maoni hukuweka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nilisahau kujaza na naamini hakukataliwa pia.
Watu wanacheka. ππππ
Adv. Ukashu: Kwanini usifukuzwe kazi kwa uzembe wa aina hii? Maana haijulikani alikuja kufanya nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nifukuzwe tu kazi kama unaweza kunifukuza. Fanya hivyo ila mimi nimesema nilijisahau.
Adv. Ukashu: Unafahamu kazi ya uwakili ina maadili yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila kazi ina maadili.
Adv. Ukashu: Maadili ya magereza tumeshayaona hapa hujajaza nyaraka na hujui wakili alipoingia alielekea wapi? Sasa tuzungumze maadili ya mawakili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : siyajui mi sio wakili.
Adv. Ukashu: Unaijua Mandela Principle?
Ntamamiro (Bwana Jela): yes
Adv. Ukashu: soma hapa inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Mfungwa atazungumza na wakili wake kuwa atazungumza bila kikwazo.
Adv. Ukashu: Umeitekeleza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inasema nizingatie sheria za ndani pia?
Adv. Ukashu: Sasa tuambie ni kifungu gani cha sheria ya ndani ambacho kiko kinyume na Mandela Principle.
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakipo.
Adv. Ukashu: Nimemaliza. Naomba Wakili Neema aendelee.
Anasimama Wakili Neema Saruni.
Adv. Neema Saruni: Nitakuwa sahihi nikisema mtu anayekuja kumuona mfungwa anapaswa kuwa na sababu ya msingi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi kwa mujibu wa Sheria.
Adv. Neema Saruni : Ulisema mjibu maombi wa nne alikuwa na orodha yake hivyo basi alipotokea hayupo mlimrudisha?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio tulifanya hivyo.
Adv. Neema Saruni : Nitakuwa sahihi nikisema hamkumpatia haki yake ya kusikiliza.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sahihi.
Adv. Neema Saruni: Nilipokuja mimi kumuona Lissu nilikuwa kwenye orodha yake?
Ntamamiro (Bwana Jela): Haukuwepo.
Adv. Neema Saruni : Nilipofika ikawaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): tulienda kumuuliza lissu.
Adv. Neema Saruni : akasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Akaruhusu ukamuone.
Adv. Neema Saruni: Kwanini huyo mwingine mlimrudisha bila kwenda kuuliza Lissu anasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hapo sasa ndio kuna utata.
Watu wanacheka πππ
Adv. Neema Saruni: Nimemaliza.
Haya wanasimama mawakili wa Serikali, anaanza Wakili wa Serikali anaitwa Wisdom
Wakili wa Serikali Wisdom: Ulitekeleza majukumu yako kwa mujibu wa nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): masharti yapo kwenye sheria ikiwemo PSO.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba asitaje kabisa PSO maana jana haikuwepo na hatukumuuliza. Asiulize. Sect. 156(3) ya Evidence Act iko wazi kuhusu Re- examination.
Jaji: Sasa Wakili wa Serikali Wisdom uko tayari kuendelea na njia hiyo ili tumruhusu Lissu nae aanze kuuliza kwenye PSO.
Wakili wa Serikali Wisdom: Naomba tu niishie hapo. Sitaendelea mbele.
Watu wanacheka ππππ
Part 27 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 23
Wakili wa waleta maombi John Seka anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Andrew Shaban Ntamamiro (Bwana jela)
John Seka: Moja ya sheria ni sheria ya magereza ambae umeisomea na kuibobea?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Kanuni za magereza je?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nazo ni muhimu sana. Zinatumika.
John Seka: Kwenye kanuni hizo unapaswa kutii kanuni ya 13 ya uendeshaji wa kanuni za Magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ibara ya 29(1) inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Kila mtu anayo haki ya msingi ya kufaidi haki za binadamu kama zilivyofafanuliwa ibara ya 12 hadi 28 ya Katiba hii.
John Seka: Ni nani na nani wana haki ya kufaidi haki mbalimbali?
Ntamamiro (Bwana jela) : Watu wote.
John Seka: Hata wewe?
Ntamamiro (Bwana jela) : hata mimi.
John Seka: Hata Tundu Lissu:
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Lissu.
John Seka: Hata Kisabo?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Kisabo
John Seka: Hata Maduhu na Nashon
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Maduhu
John Seka: Nashon Je?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Nashon.
Watu wanacheka. Wanamuona zamwamwa sijui πππ
John Seka: Haya rudi ibara ya12 sasa kule.
John Seka: soma ibara 29(2) na useme inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : kila mtu ana haki ya kupata hifadhi sawa chini ya sheria.
John Seka: Hadi Lissu akiwa mikononi mwako Ukonga?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sahihi
John Seka: Nenda Kanuni ya 13 ya kanuni za Magereza na utuambie miaka 31 ya uzoefu wako ni lini uliifahamu kanuni hii?
Ntamamiro (Bwana jela) : Tangu nilipoanza Kazi.
John Seka: Isome kwanza.
Ntamamiro (Bwana jela) : mfungwa atapewa haki ya kuongea na wakili wake kwa faragha lakini awe anaonekana lakini sio kuwasikiliza.
John Seka: Umeielewa kweli hicho kifungu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio mfungwa atapewa nafasi ya kuongea na wakili wake na kufanyika kwa kuona lakini sio kusikiliza.
John Seka: Kuna haki ya mfungwa na kuna haki ya mshauri wa kisheria kwenye kanuni hiyo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Haki ya mfungwa kusaidiwa kupewa nafasi ya kuongea na mshauri wake wa kisheria yaani Wakili.
Ntamamiro (Bwana jela): Ndio
John Seka: haki ya pili ni ya mawakili kupata fursa ya kuongea na mfungwa kwa faragha bila ya kusikilizwa ni kutazamwa tu.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Hii haki huwa unasomewa au ni uzoefu? Hii kanuni ya 13.
Ntamamiro (Bwana jela): Sijaelewa swali.
Seka: ili uwe na ujuzi huo wa kutazama bila kusikiliza kuna chuo kinachofundisha? Au ni uzoefu wa kazi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Katika uzoefu wa kazi unasema hapa natazama na sisikilizi.
John Seka: Kwahiyo utekelezaji wa jambo hili unategemea mtu na mtu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hakuna standard zilizowekwa.
John Seka: Kwenye nyaraka zako na maelezo yako ulikuwa unasema simamia? Maana yake ulikuwa unasema simamia lakini wasisikilize.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ukubwa wa Chumba cha Ofisi yako ukoje?
Ntamamiro (Bwana jela) : wakutosha tu.
John Seka: Huwezi kukadiria?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
Jaji: Ofisi yako hujui ina ukubwa gani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wakutosha.
Jaji: Tunatosha wote humu ndani tukija ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hamuwezi kuingia.
Jaji: Bado unasema ni ukubwa wa kutosha?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio
Jaji: Haya jibu swali sasa.
Anasimama Nalindwa Sect. 93 ya Prison Act inasema ramani ya gereza isitolewe. Ukubwa wa hizo ofisi ni hatari.
Jaji Mruma: Hakuna ramani ya gereza wala kifungu hakisemi hivyo. Shahidi jibu swali tunataka sana kujua ukubwa wa ofisi yako ni jambo muhimu sana.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni ofisi iko umbali kutoka hapa nilipo hadi hapo kwako.
John Seka: Sasa ofisi yako ya kaimu wako Recha ni ofisi ya nani kubwa?
Ntamamiro (Bwana jela): Yakwangu ndio kubwa.
Part 24 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
@HildaNewton21 Mahakamani Siyo poa pasikie tu kuna daktari aliuzwa swali na mtuhiwa wa kubaka ni mara ngapi unakuja kutoa ushahidi batili Dr akajibu leo ππ
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 20.
Mhe. Lissu anaendelea kumshona Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Wakati wote mawakili wakija gerezani, simamia, wapekuliwe na wamepekuliwa. Swali ni kwamba ni je wewe Bwana jela wa Ukonga unawashuku na una wasiwasi na mawakili 37 waliokuja kuona wateja Ukonga? Kumbuka kanuni inasena ili uwasearch ni lazima uwe na wasiwasi nao.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sitegemei kanuni.
Mhe. Lissu: Sasa twende kwenye sheria yenyewe kwenye Prisons Act kuwa unaweza kusearch mgeni kama hautakuwa na wasiwasi nae? Kifungu gani hicho?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa Majaji mtu yeyote anayeingia Gerezani awe mfungwa au mahabusu lazima apekuliwe.
Mhe. Lissu: Lazima apekuliwe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yuko kimya.
Mhe. Lissu: Kama kweli ni lazima. Twende kwa Mawakili wa Serikali waliokuja Ukonga kama uliamuru wapekuliwe. Twende kwa hao sasa. Wah. Majaji SUPP 4 tarehe 19/11/2025 nenda haraka tumalize hii ngoma. Na Tarahe 21/01 mwaka huu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kila anayeingia lazima akaguliwe.
Mhe. Lissu: SUPP 4 inasemaje kuhusu Tarehe 19/11 walikuja mawakili wafuatao Debora Mushi kutoka NPS, Caroline Nana kutoka NPS pia, Cleoface Leonce ambae ni investigator na alikuja Justo Dimba au Simba kutoka kwa ZCO. na mwingine kutoka DCEA. Wote hawa shida walioijia gerezani walikuja kuongea na mahabusu. Maoni yako ukasema nini? Wasomeee majaji.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Wasikilizwe kwa utaratibu.
Mhe. Lissu: Wakija mawakili wengine simamia mazungumzo yao, wapekuliwe, wapekue, Simamia kwa ukaribu. Lakini wa serikali wakija wasikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Mawakili 37 wote nipe mfano mmoja tu w wakili uliyesema asikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Naomba Tar. 20/01 wakili hapo nimesema SIMAMIA.
Mhe.!Lissu: Ahsante sana. Sasa kwa mawakili wa serikali wapi hata mara moja umeandika SIMAMIA?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio lazima niandike.
Mhe. Lissu: Wabelgiji nilipokaa wanasema Papiere yaani Paper. Tunaenda na maandishi. Onesha maandishi acha rongorongo maneno mengi unatumalizia.
Sasa angalia majina yanayofuata. Hapo kuhusu mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela): Niliandika Waletwe.
Mhe. Lissu: Maafisa wa Madawa ya kulevya na Mawakili wao waliokuja 28/11 kazi yao ni kutukamata na kutupeleka Mahakamani ndio unaosema wasikilizwe?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hatoi jibu.
Mhe. Lissu: Hawa watu ni watumishi wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wanalipwa mshahara wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio lakini.
Mhe. Lissu: Lakini utawapa mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa mawakili wa serikali huwa wanakuja kuongea na wote?
Mhe. Lissu: tuambie ni wapi umeandika kuwa walikuja kuongea na wote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijaandika.
Mhe. Lissu: Ni sahihi kuwa kuna wakati nyaraka zinakataliwa na zinazokubaliwa lazima mseme zote. Kweli sio kweli mnafanya hivyo kwa mawakili wangu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sio kweli zinasomwa. Ila zinakaguliwa.
Mhe. Lissu: la kwamba zinakataliwa pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Katika nyaraka ambazo zinaletwa kwangu ni pamoja na hotuba ya Chande ya matukio ya tar. 29/10?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Lissu: Shahidi Paul Kisabo amesema wiki iliyopita Tar. 14/07 alikuletea waraka unaotoka common wealth kuwa niachiliwe ndani ya siku 30 na mliposoma mkakataaa.
Bwana Jela: Sio kweli.
Part 21 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 16
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza
Mhe. Lissu: Twende Taratibu. Hiki ulicholeta mahakamani ni photocopy?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Original unayo ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Angalia Tar. 29 na Tar. 30 Sept. 2025. Kuna majina ya wageni kabla ya Tarehe hizo wapo wageni hawaonekani walikuja tarehe gani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni kweli
Mhe. Lissu: Hawa watu wanne walikuja tarehe ngapi? Wambie majaji sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haioneshi.
Mhe. Lissu: Wewe unajua sasa? Walikuja tarehe ngapi? Maana original unayo wewe.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tarehe haioneshi.
Mhe. Lissu: Je katika hao watu wa nne. Mtu wa 10 ni nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Paul Kisabo.
Mhe. Lissu: Alikuja kumuona nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : wewe hapo imeandikwa. Alikuja kukuona wewe.
Mhe. Lissu: Soma Tar. 30 Sept. Kwenye karatasi hiyo hiyo. Mtu wa kwanza ni Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Tusiende mbali sasa: Tufafanulie jambo hapa kuna sehemu imenadikwa jina la ndugu, ID no. Simu namba, atokapo mgeni na maoni ya OIC. Sasa hiyo OIC ni Officer in Charge yani wewe hapo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Tar. 30/09 kwenye jina la Kisabo uliandika A/Zamu maana yake Afisa wa Zamu. Na kuna mahali umeandika ADM maana yake ni admission office in charge. Na kuna mahali umeandika IO maana yake intelligence officer?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli kabisa.
Mhe. Lissu: na kuna sehemu umeandika legal unamaanisha Legal Officer Stima.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Hiyo sehemu ya maoni yako ni maelekezo yako kwa hawa niliowataja? Wewe ndio Boss.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila ofisa ana kazi yake. Kwahiyo ni maelekezo yangu kwao.
Mhe. Lissu: Kwahiyo unakuwa umewapa amri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Nenda Kwenye kilelezo SUPP 3 pia ni orodha ya mawakili waliokuja Ukonga. Nashon Nkungu lipo hapo ambae ni mlalamikaji wa pili. Andrew Mathew Chima pia alikuja kuniona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Je Andrew Chima yupo kwenye orodha ile ya mawakili wangu niliowaletea ile SUPP 1?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo. Naomba nifafanue.
Mhe. Lissu: Sitaki. Utawafafanulia wa Serikali.
Haya huko mwisho kabisa KULWA MADUHU yupo au hayupo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yupo namuona hapa.
Mhe.Lissu: Na kule mwisho kwenye maoni yako umesema aruhusiwe mwenye kibali. Maduhu hana kibali huko mbele sioni.
Ntamamiro (Bwana Jela): hayuko kwenye orodha ya mawakili wa mahabusu huyu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kuna sharti lolote la kisheria kwamba mfungwa yeyote mwenye wakili au wakili anapaswa kuwasilisha orodha ya mawakili wake kwa Bwana Jela?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Halipo kisheria. Lakini mfungwa ana haki ya kuchagua nani amtembelee.
Mhe Lissu: Nilichagua kuwa Kulwa William Maduhu na umemkatalia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuwepo kwenye orodha.
Mhe. Lissu: Andrea Chima alikuja kuniona yupo kwenye orodha gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo.
Mhe. Lissu: SUPP 5 twende sasa tar. 24/12/2025 angalia kwenye entry kuna Nashon Nkungu na Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio wanaonekana wote.
Mhe. Lissu: Je Victoria Mgonja alikuja kumuona Jonson Muhanjo. Uliandkka kwenye maoni yako kuwa Adm. Simamia mazungumzo yao. Na mazungumzo hayo yalifanyikia kwenye ofisi ya Admn
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina kumbukumbu yalifanyikia wapi?
Mhe. Lissu: Kwamba tangu juzi tunazungumza kuhusu mazungumzo ya mawakili yalifanyikia wapi hujaenda kutafuta.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijui inaweza kuwa kwa Mkuu wa Gereza au Adm.
Mhe. Lissu: Mazungumzo na Nashon ulisema asimamiwe kwa Makamu mkuu wa gereza na kuwataka wasaidizi wako wanne wasimamie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Part 17 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 14
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Mmeleta PSO hapa?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio mawakili wangu waliileta.
Jaji: Wakili wa serikali nenda kaongee na shahidi wako anajua.
Mhe. Lissu: Sasa Shahidi nataka tuzungumze juu ya utaratibu wa mazungumzo kwa wafungwa au mahabusu? Tuanzie hapo. Soma kanuni ya 9(h) ya kanuni za usimamizi wa magereza. Je ni kweli wafungwa wana haki ya kutembelewa gerezani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni kweli.
Mhe. Lissu: Wafungwa watatimiza haki hiyo kwa mujibu wa kanuni ya 12 ya kanuni hizo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni kweli
Mhe. Lissu: Soma kanuni ya 12(5) inasemaje? Je kwa kanuni hiyo wafungwa wanapotembelewa na wageni wao mazungumzo yao yatafanyika kwa kuona na kusikilizwa na afisa gereza mmoja?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sawa kwa kanuni hii.
Mhe. Lissu: Inahusu wageni wote wa wafungwa?
Ntamamiro (Bwana Jela): inategemea.
Mhe. Lissu: Utaratibu wa kutembelea wafungwa wa kifo na wa kawaida ni tofauti?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inategemea.
Mhe. Lissu: Je askari mmoja kwa wafungwa wa kawaida na askari wawili wa wafungwa wa kifo. Utaratibu wa kutembelewa kwa wafungwa na watu wa kawaida na mawakili wao ni sawa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kwa mawakili askari ataona lakini hatasikiliza.
Jaji Rumisha: Si unaona tunaenda vizuri sasa Lissu.
Mhe. Lissu: Vizuri kabisa sasa shaidi tuambie mkuu wa gereza la ukonga una matatizo ya kusikia au hauna?
Ntamamiro (Bwana Jela): niko vizuri mimi. Nasikia.
Mhe.Lissu: Assistant Commisiomer on Prison Recha. Ana matatizo ya kuona na kusikia au hana?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui.
Watu wanacheka kimya kimya. Boss hajui kama msaidizi wake anasikia vizuri au laaπ
Mhe. Lissu: Je ACP Mumbii nae ana matatizo ya kusikia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio Daktari sijui.
Mhe. Lissu: Je ACP Mohamed nae?
Ntamamiro (Bwana Jela): nae pia sijui kama ana matatizo ya kusikia.
Mhe. Lissu: SGT. Hamisi vipi nae anasikia au hasikii?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijui.
Mhe. Lissu : Insp. Stima legal officer nae vipi anasikia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nae pia sijui.
Mhe. Lissu: Wale akina mama watatu wanaofanya kazi admission office wana matatizo ya kusikia na kuona au hawana?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui.
Kwa Kifupi kesi imeanza sasa.πππ
Mhe. Lissu: Koplo Dani mtunza fedha nae vipi ana matatizo ya kusikia au vipi? Maana na yeye mara zote huwa yuko ofisi ya admission?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijui.
Mhe. Lissu: Wale maaskari ambao huwa wanatoka na mimi ninakolala na kunileta kwako Insp. Kaisi na Mwingia wakiongoza nao pia huwa wanatatizo la kusikia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijui.
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji umefanya kazi Magereza kwa miaka mingapi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni mingi tu.
Mhe. Lissu: Mingapi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Zaidi ya 25
Mhe. Lissu: Uliingia mwaka gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : 1995.
Mhe. Lissu: Kwahiyo ni miaka 31?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Mhe. Lissu: Umepitia mafunzo mbalimbali jadi kufikia cheo ulichonacho sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni sahihi.
Mhe.Lissu: kwahiyo wewe ni msomi wa masuala ya magereza hadi umefikia hapo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Mhe. Lissu: Je kwa uzoefu wako jeshi la magereza linaweza kuajiri askari haoni au hasikii?
Ntamamiro (Bwana Jela) : haliwezi kuajiri. Lakini unaweza kuumwa ukiwa kazini.
Mhe. Lissu: akiajiriwa haoni akapofuka ataendelea kuwa askari magereza.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio daktari
Watu wanacheka.ππππ
Mhe. Lissu: Kama atakuwa hasikii je ataendelea kuwa askari magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina jibu.
Mhe. Lissu: Hata kutokuwa na jibu ni jibu pia.
Mhe. Lissu: Je askari magereza ambae hasikii au hauoni atashuhudiaje mazungumzo ya mfungwa na ndugu zake watakapokuja kumtembelea.
Part 15 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 15
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Je askari magereza ambae hasikii au hauoni atashuhudiaje mazungumzo ya mfungwa na ndugu zake watakapokuja kumtembelea
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayo ni masuala ya kidaktari.
Mhe. Lissu: Sasa Bwana Jela hujui kama wasaidizi wako wote hao kuwa hujui kama wanasikia au hawaoni wewe ni mkuu wa gereza wa aina gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sik daktari.
Mhe. Lissu: Wewe ni Mkuu wa Gereza wa aina gani? Usiyejua afya za wasaidizi wako?
Ntamamiro (Bwana Jela): Nastahili kuwa kwenye nafasi hii.
Mhe. Lissu: Ndio maana nchi imekwama. Kama watu wenyewe ndio nyie na akili hizi
Mhe. Lissu: Umekuwa Officer incharge tangu lini pale Ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sept. 2025.
Mhe.Lissu: Ulihamishiwa Ukonga ukitokea gereza kuu la maweni Tanga?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio.
Mhe.Lissu: Ulikuja ukonga kuchukua nafasi ya Juma Mwaibaku?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli.
Mhe. Lissu: Ulipohamishiwa Ukonga mimi tayari nilishakuwa mahabusu ukonga toka April 2025?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta nakaa kwenye special wing pale ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wakati unahamia pia ulinikuta naishi huko pamoja na wafungwa wa adhabu ya kifo 100?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sikuwakuta.
Mhe. Lissu: Je ulinikuta nakaa peke yangu au sio peke yangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio peke yako.
Mhe. Lissu: Wafungwa gani hao?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mmoja.
Mhe. Lissu: Je kwa miezi 5 ambayo hukuwepo nilikuwa naishi na wafungwa wa kifo takribani 100?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sifahamu.
Mhe. Lissu: Umeona record ya maandishi ya waliokuwepo special wing umeiona au hujaiona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijapitia hiyo records.
Mhe: Lissu: Hili suala nilishalilalamikia na lipo kwenye nyaraka za mahakama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu. Tuendelee na maswali mengine.
Mhe/ Lissu: Utaratibu wa wageni kuja kuniona ni weekend?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: Utaratibu wa wageni wangu kuja kuniona weekend ni kwamba siku moja wanakuja ndugu zangu na siku nyingine wanakuja viongozi wa Chama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu.
Mhe.Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta utaratibu wa kutembelewa na mawakili wangu ilikuwa nimepeleka orodha kwa mkuu wa Gereza kwa mkuu wa gereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Orodha ya kwanza uliiambatanisha kwenye hati yako ya kiapo kinzani ile ambayo nilikuwa na mawakili 10.
Ntamamiro (Bwana Jela): Orodha hiyo hiyo moja.
Mhe. Lissu: Kwahiyo hakukuwa na orodha yenye jina la Deogratias Mahinyila, Paul Kisabo na Dickson Matata na Mary Stephano.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna hiyo.
Mhe. Lissu: Angalia kielelezo SUPP 1. Ukishakiona niambie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Anapekenyua hapa..
Mhe. Lissu: Jina la Nashon Nkungu limo kwenye hiyo orodha lipo au halipo? Ambae ni mleta maombi wa pili.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio lipo.
Mhe. Lissu: Je jina la Kisabo na Maduhu mawakili wangu yapo au hayapo kwenye hiyo SUPP 1
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa hawapo kwenye hii orodha.
Mhe. Lissu: Sasa hao wawili wamesema kwa kiapo na kusema hapa Mahakamani kuwa kabla hujahamia ukonga walishaingia gerezani kuonana na mimi walishaingia karibia mara tatu. Wewe unasemaje? Yaani wakati ACP Juma Mwaibako akiwa Mkuu wa Gereza walihudhuria
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulikuwepo wakati huo?
Bwana Jela: Sikuwepo wakati huo. Ila nyaraka zinasema.
Mhe. Lissu: Nenda kielelezo ambacho ni SUPP 2 hapo.
Jaji: SUPP 2 ni nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hiki ni kiambatanisho na. 2 kinahusu orodha ya wageni na mawakili waliotembelea gereza la Ukonga.
Part 16 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.