#TajiriLaKihaya
WAISLAMU Kwa WAKRISTO Sisi ni Ndugu….
Tumeoana, tunaishi pamoja,Sisi ni marafiki… tunafanya biashara pamoja,Tunazika pamoja,tunahudhuria sherehe pamoja… katika familia zetu ni mix ya Wakristo na waislamu…
Kama mjomba wako sio dini tofauti basi atakuwa shangazi yako… Kama sio Binamu yako basi atakuwa shemeji yako…
kuna Waislamu wamesoma shule za wakatoliki na kuna Wakristo wamesoma Islamic schools…
Hata siku moja tusikubali kutengana,tusikubali kuchukiana…
Adui wetu sio Dini zetu… infact Sisi ni Ndugu…
Kila mtu hapa Akiulizwa vizazi 20 nyuma- mababu wa mababu zetu hawakua na hizi DINI… Sisi ni waafrika Sisi ni Watanzania…
hata siku moja kodi haichagui dini, sera mbaya zikitungwa bungeni hazichagui dini… mvua ikinyesha haiwanyeshei waislamu tu au wakristo tu… kifo kikija hakichagui Dini, wote tunakufa, Umasikini au Utajiri hauchagui DINI…
Kama Mungu Hatubagui,iweje Sisi tuanze kujibagua???
Tusikubali huu mchezo Divide and rule,,, tusikubali hii Tenga utawale inayoletwa kimya kimya….
Tusijadili DINI zetu maana mwisho wa siku itamfaidisha anaeleta hizi agenda…
Juzi tu tuliona- Zile Risasi hazikua zinachagua Dini… Lockdown haikua Kwa wakristo tu hata waislamu tulikua ndani… mtandao ulipokatwa hawakukatiwa Wakristo tu hata waislamu tulikatiwa…
Tusikubali kutumiwa…
Hata iweje hata siku moja KIJANA usifikirie Kuchoma MSIKITI Au KANISA…
Hata siku moja KIJANA usikubali kuchoma Qur’an au Biblia…
Vita za Dini ni mbaya saana … tusiende huko!
SISI TUNATAKA KATIBA MPYA, Tunataka tume Huru ya Uchaguzi, Tunataka KURA yetu iheshimiwa- Our votes must Count , tunataka viongozi tuliowachagua wenyewe… tunataka wafungwa wote wa kisiasa waachiwe… haijalishi ni Dini gani!
Tunataka Uhuru wa Vyombo vya habari, tunataka uhuru wa kutoa maoni, Utekaji ukomeshwe,watu wasiojulikana wafahimike…
ADUI WETU SISI SIO WAKATOLIKI AU WAISLAMU…
Adui wetu Sisi sio DINI zetu…
FOCUS 💯
Nadhan hii context inafifisha matumaini ya watanzania ndani ya akina heche while unajua si kweli brother !
Walikuwa vituo tofauti!
Hakuna sehemu wamekubali maridhiano
#TajiriLaKihaya
Hivi sikuhizi Kesi za UHAINI zina Dhamana kumbe😅
Au ni kwa viongozi tu!
Au Heche alikataa maridhiano akasema labda wawaulize wenzake kwanza… ikabidi wawaite chap?
Wote imekuaje wawekwe selo moja,OysterBay?
Mmmh SIASA ni mchezo mchafu saana na usiweke rohoni💔
Uzuri Gen z kwa sasa Hawana Chama cha Siasa wala Kiongozi…