#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 225
Mhe. Lissu anaendelea hapa.
Kama mtakumbuka nilisema ninavyoishi Ukonga, siruhusiwi kuonana na Mawakili wangu in private.
Mnaruhusiwa kutembelea Magereza naomba mliangalie na hili kama itawapendeza inawapa Mamlaka ya kutoa mapendekezo na mamlaka za Magereza kurekebisha masuala yanayohusu wafungwa kama haya niliyosema.
Ni muhimu kwamba kuwasiliana na washauri wangu wa kisheria ilindwe kama sheria inavyosema bila kusikilizwa na maafisa wa Magereza.
Ni hayo tu Waheshimiwa
Mhe. Tundu Lissu amemaliza na amekaa sasa.
Majaji wanaandika hapa.
Anasimama Renatus Mkude kuwa tutampatia hizi nyaraka ndani ya siku 14 tutampatia.
Hili la masuala ya utawala wa mambo ya magereza kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha National Prosecution Act na sisi ofisi ya DPP tutatembelea ili kuhakisha kunakuwa na fair trial.
Wameombwa Majaji anasema DPP ataenda eti huko Magereza kuangalia haki za Mtuhumiwa. Uongo uongo uongo. Hawana hata aibu hawa jamaa.
Majaji wanaandika baada ya kusikia hayo kutoka kwa Wakili wa Serikali, Renatus Mkude.
Majaji wanajadili pale.
Yuko Jaji muda wote yeye huwa anacheka anafurahi tu sijui huwa anatabasamu jambo gani? Wanaofika hapa Mahakamani wanamfahamu vizuri.
Jaji Ndunguru: Tumesikia hoja za Jamhuri na Hoja za Mshitakiwa nae kama ambavyo mshitakiwa ameturahisishia kuwa mikono yetu imefungwa kwamba yapo hayo maombi ya marejeo Mahakama ya Rufani.
Sasa shauri hili linasimama hadi pale Mahakama ya Rufani itakapotoa uamuzi.
Suala la Gerezani wakili wa Serikali amesema na sisi pia tumelichukua.
Mwenendo wa shauri hili unasimama hadi pale mambo ya Court of Appeal yatakapoisha.
So kesi hii imeahirishwa hadi hapo itakapoitwa tena.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 224
Majaji wameingia muda huu saa nane Kamili Mchana.
Wanaandika pale juu.
Mheshimiwa Lissu ameingia na kuteta jambo na Dr. Nshala tunamsikia anasema waende kokote watakapotaka kwenda tutakutana nao huko. Sasa sijui ni wapi anamaanisha.
Anasimama Renatus Mkude Wakili wa Serikali kwa niaba ya jopo la Mawakili wa Serikali tunaomba radhi kwani tulifikiri tungetumia lisaa limoja.
Mchana huu nipo na Ajuaye, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Kwa wote tunawakilisha jamhuri na Mshitakiwa yupo.
Shauri lilipangwa kuendelea na mashahidi. Lakini tumetafakari na tunaitafsiri kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Appellate Jurisdiction Act na kanuni ya 65(1) ya kanuni za Mahakama ya Rufani.
Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) anatoa taarifa ya kuwasilisha taarifa ya mapitio (revision)
Hapa kwanza anakosea Mapitio ni Review alipaswa kusema Marejeo ndio Revision sijui kasoma wapi nae huyu jamaa.😂😂😂
Anaendelea hapa Renatus Mkude, kuwa Notice of motion hiyo imeambatanishwa na kiapo cha Cathbert Mbiringe Wakili wa Serikali ambayo taarifa hii ya kutoa notice kwenda Mahakama ya Rufani imesainiwa leo Tar. 24/02/2026.
Na kupokelewa kwa mifumo ya kielektroniki inayotambulika na Mahakama na kusajili kama. CRIMINAL REVISION NO. 7203216/2026 imepokelewa na Mahakama ya Rufani Tanzania hapa Dar es salaam.
Ambalo chimbuko lake ni Criminal Sessions No. 19605/2025 ambayo iko mbele yenu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu. (Ndunguru, Karyemaha, Kiwonde)
Kwa kuwa shahidi wetu aliyekuwa anafuata ACP Mahamba tuliyemuombea notice additional substamce of evidence na ikakataliwa.
Ni Rai yetu kwamba kwa kuwa shauri hili limeshapokelewa Mahakama ya Rufani haiwezi kusimama ili kuweza kutoa nafasi kwa shauri husika huko Mahakama ya Rufani kuweza kuamuliwa.
Ni hayo tu kwa sasa.
Tunamsubiri Mh. Lissu atajibu nini?
Mhe. Lissu anaanza.
Baada ya kuzikiliza wasilisho la upande wa Mashitaka nina haya ya kusema.
1. Kwa vile mimi nipo gerezani na wanajua nataka wanipatie hiyo nakala ya Notice of Motion waliyofile niweze kuiona.
2. Ninafahamu na ninatumaini na wao wanajua kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 8(2)(d) cha Sheria ya Mamlaka ya Rufaa ambacho wamekitaja (Appellate Jurisdiction Act) wanafahamu kwamba hakiruhusu rufaa wala mapitio wala marejeo ya maamuzi ya Mahakama ambayo hayamalizi shauri la msingi. (Interlocutory decisions) sina shaka na wao wanalifahamu hilo.
3. Waheshimiwa Majaji siwaombi mtoe uamuzi wowote kuhusu hili ninalolisema.
Nataka iwe kwenye record kwamba nafahamu na naamini upande wa mashitaka wanafahamu lengo la kupeleka ombi la marejeo Mahakama ya rufani na wanafahamu hairuhusiwi ni kurefusha mashauri haya ili niendelee kukaa Gerezani. Ni hilo tu.
Kwamba tupeleke Mahakama ya Rufani ili huyu mbaya wao ambae ni mimi aendelee kukaa Gerezani.
Kwa vile wananipeleka kwe ye Mahakama ya Rufani nataka niwaeleze kuwa nitawafuata huko huko naenda kuwashughulikia huko huko.
Kama ambavyo kesi yao is dead on arrival najua hata hii revision yao pia imeshakufa.
Tutarudi hapa yakiisha huko ya Mahakama ya rufani tutarejea hapa na nitawashughulikia tukirudi.
Jambo la Mwisho Mawakili wangu wametaka kunipa nyaraka hapa lakini siwezi kupewa hadi nyie mseme.
Sijui wanaogopa nini watu wa magereza nisipewe huo uamuzi hapo ni makaratasi tu.
Naambiwa ni hukumu kutoka huko Umoja Wa Mataifa lakini Magereza wanaogopa nisipewe.
Tena ni uamuzi unaohusiana na mimi kuwepo Gerezani. Tatizo liko wapi?
Jaji anasema uko wapi? Umepelekwa wameuona wamesema wape Mawakili wa Serikali.
Wako wanasoma hapa Mawakili wa Serikali huo uamuzi.
Anasimama Renatus Mkude anasema mimi ni member wa working group za UN Human Rights Council.
Jaji: Tumesema apewe au asipewe?
Renatus Mkude: Apewe tu.
Part 225 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 24, 2026
Last time tuliishia Part 222 so leo tunaendelea na-;
Part 223
Majaji wameingia na Mshitakiwa pia ameingia.
Karani anasoma shauri hapa.
Anasimama Renatus Mkude anasema yupo na Ajuaye, Katuga, Thawabu, Cathbert Mbiringe.
Anasema leo tumekuja kwa ajili ya kupokea ruling na sisi tuko tayari.
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa unasemaje?
Mhe. Lissu: Na mimi niko tayari.
Jaji anaanza kusoma hapa UAMUZI.
Uamuzi huu unatokana na pingamizi lililowekwa na pingamizi la mshitakiwa kutokana na taarifa ya kuongezwa kwa ushahidi.
Taarifa hiyo ililetwa tarehe 18/02/2026 na upande wa Mashitaka kwamba unatokana na pingamizi lililowasilishwa na mshitakiwa.
Notice hiyo ililetwa kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Mshitakiwa alieleza Mahakama kwamba kifungu hicho kinaelezea shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa wakati wa mwenendo kabidhi na hivyo walichokileta upande wa mashitaka ni kuleta ushahidi mpya.
Upande wa mashitaka walijibu notice ipo halali kwa mujibu wa sheria na imekibidhi matakwa ya kisheria na ipo kwa mujibu wa sheria.
Huo ndio ulikuwa msingi wa hoja za pande zote mbili.
Mahakama imeona hoja inayopaswa kuamuliwa ni je notice hiyo ipo kwa mujibu wa sheria?
Ili kurahisisha Mahakama imeona ili reproduce notice hiyo inavyosema.
Anasoma notice inavyosema kwamba ni notice ya kuongeza maelezo ya ziada ya shahidi husika ambae ni Amin Mahamba.
Hakuna mashaka kwamba upande wa mashitaka wanataka kuongeza ushahidi wa Amin Mahamba.
Kwa vile Amin Mahamba ni shahidi na statement yake ilishasomwa wakati wa committal ilishasomwa.
Notice inasema ushahidi unaotaka kuletwa ni wakati wa uchaguzi wa tar. 29/10/2026.
Anasoma kifungu cha 308 cha CPA kinavyosema.
Ukiangalia kifungu hicho kinatoa masharti au mazingira ambayo notice hiyo ni reasonable au laaa.
Masharti ni kwamba
1. Maelezo yatoke kwa shahidi
2. Uwe ni ule ushahidi ambao haukusomwa wakati wa committal
3. Uwe ni ushahidi ambao haukusomwa wakati wa proceedings
Kifungu cha 308 ndio kinachosema hawezi kutoa ushahidi hadi watakapoleta notice na hivyo basi ukiangalia hayo kifungu hicho cha 308 kinafungua mlango kwa shahidi ambae alikuwepo na bahati mbaya maelezo yake hayakuletwa.
Amin Mahamba maelezo yake yalikuwepo wakati wa commital, anataka kuleta mambo ya Uchaguzi ambayo hayakuwepo wakati wa committal.
Ipo kinyume na kifungu cha 308 cha CPA.
Hivyo basi kifungu cha 308 kinaweza kuruhusu notice hiyo tumeona kwamba kifungu hicho hakiruhusu kabisa.
Shauri la Remina Omary Abdul tumeona linahusiana na vielelezo vya wakati wa committal. Shauri hilo haliwezi kutibu chochote katika hoja iliyopo mbele yetu.
Hiyo notice ya kuongezwa kwa ushahidi ambayo imeletwa na upande wa mashitaka haitambuliwi na kifungu cha 308 cha CPA.
Kimsingi tunasema kwamba fundamentally haiko sahihi na baada ya kusema hayo basi notice hiyo ni incompetent na tiba pekeee iliyopo ni kwamba notice hiyo lazima iwe struck out. Ni hayo tu.
Anasimaa. RENATUS MKUDE anasema baada ya kupokea ruling tunatafakari tunaomba ahirisho ya lisaa limoja.
Twende kutafakari.
Bado majaji wanashauriana pale juu.
Nafikiri leo KATUGA atajua vizuri nani ni Bingwa wa Sheria😂
Anasimama Mh. Lissu anasema mmesema kuwa mashahidi waletwe leo na mlisema tutasikiliza uamuzi wa pingamizi na tutasikiliza shauri leo.
Sasa wanasema tuahirishe kusikiliza ili wakatafakari.
Wanaenda kutafakari nini? Ili iweje? Huu uamuzi haukatiwi rufaa.
Tusipoteze muda kila tunapopoteza muda anayeumia ni mimi sasa wao walipaswa kuleta mashahidi na wasitupotezee muda kabisa, tuendelee kusikiliza shauri hili.
Majaji wanaandika kidogo
Anasimama Renatus Mkude anasema tumemsikia Mshitakiwa
Tuna mambo mawili.
1. Tumepokea ruling ya Mahakama na tumeikubali
2. Jambo la pili ni kwamba tulimtaja shahidi ambae lazima tuwezi kumuandaa shahidi yetu
Jaji Ndunguru anasema tulisema muwe na mashahidi wakutosha. Tukiendelea kubishana tutapoteza muda, turudi mahakaman saa 5 kamili
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 218
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Angalia D14 tuambie wapi alisema alimuona Tundu Lissu akihamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025?
Coplo Amani : Hayo maneno kufanya vurugu hayapo kwenye kielelezo
Mhe. Lissu: April 17, 2025 kwenye ushahidi wako wa hii siku unasema ulikuwa kituo cha Polisi Ilomba na ukapewa maelekezo na inspekta Jorum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana na alichoeleza juu ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu kuhusu kauli yake na akahamasika na akashawishi wenzake wafanye vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu 2025, eleza kama maelezo hayo yapo
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo
Mhe. Lissu: Coplo Amani shahidi haya yote ambayo nimekuuliza kama yapo au hayapo ma umesema hayapo katika maelezo yako, swali langu ni uliyasema hapa mahakamani kwasababu ni mambo muhimu kwa mahakama kuyasikia, kweli au si kweli.
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji naomba nitoe ufafanuzi.
Mhe. Lissu: Hapana naomba ujibu swali langu
Coplo Amani: nawaomba majaji
Mhe. Lissu: hapana
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Umewaeleza waheshimiwa majaji kwanini hayo mambo muhumu hayapo katika maelezo yako??
Coplo Amani : bado nina muda
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Coplo Amani : sijayasema na sijayaeleza kwasababu ninazozijua Mimi.
Mhe. Lissu: Nataka uangalie icho kielelezo D14 ni nataka uangalie halafu uniambie kama nakosea umeandika baada ya kupata maelezo ya kazi ya Jorum nilianza ufuatiliaji Isyesye mtaa wa Mwantengule, kwa maneno hayo nitakuwa sahihi nikisema kwamba ulikwenda Mwantengule ukiwa tayari unamjua P3
Coplo Amani: nilikua simfahamu
Mhe. Lissu: Kama ulikua humfahamu uliendaje moja kwa moja ukamkamata
Coplo Amani : Nilishasema nilionyeshwa na askari wa intelijensi
Mhe. Lissu: hayapo kwenye maelezo yako and it is too bad.
Mhe, Lissu: P3 ni dereva wa boda boda sio
Coplo Amani : ndio
Mhe. Lissu: Na umesema askari wa intelijensi huwa wanajichanganya hata kwa boda boda
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: sasa waambie waheshimiwa majaji kama huyu P3 sio askari wa kweli wa intelijensia
Coplo Amani : si kweli
Mhe. Lissu: umesema P3 alipanga kupiga watu mawe, kuasi nchi halafu umesema Jorum alikwambia umuachie kwa dhamana, inaingia akilini??
Coplo Amani : inaingia akilini
Mhe. Lissu: mtu anayepanga uasi na kupiga watu mawe mnampa dhamana?! Kwanin tushangae yaliyotokea October 2025!
Coplo Amani : mimi sijui bwana muulize Jorum
Mhe. Lissu: Jorum hayupo kwenye kizimba
Mhe. Lissu: kwahiyo nyinyi Polisi ndo mlipanga mambo ya October 29
Coplo Amani : Mimi sina majibu ya hilo.
Mhe. Lissu: Eleza kama umeleta pikipiki uliyomkamata nayo
Coplo Amani : sijaonyesha
Mhe. Lissu: usajili wa Bodaboda
Coplo Amani : Hakuna
Mhe. Lissu:Kadi ya bodaboda
Coplo Amani : hakuna
Mhe. Lissu: Na huyu jamaa tunamtambua kama P3, hatujui jina lake, amejificha kwenye kibox hatujamuona tutajuaje kama ni boda boda?
Coplo Amani : hayo mambo yanahusika vipi kwenye kesi hii
Mhe. Lissu: yanahusika
Mhe. Lissu: Huyu P3 ulivyomfikisha Ilomba ulimuweka mahabusu, kweli au si kweli
Coplo Amani : Si kweli
Mhe. Lissu: Naomba nimsomee shahidi kielelezo D12 jinsi P3 alivyofikishwa kituoni……”tulivyofika kituoni aliniweka mahabusu”
Sasa swali langu kati ya ushahidi wako ww na ushahidi wa P3 Mahakama ichukue upi kuwa ni ushahidi wa kweli?
Coplo Amani : hilo ni jukumu la mahakama.
Mhe. Lissu: naomba ujibu swali langu
Coplo Amani : hilo ni jibu la mahakama
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Katuga: Waheshimiwa shahidi ameshajibu sasa kama halimpendezi basi hilo ndio jibu
Mahakama: endelea na Cross
Mhe, Lissu: Kwenye ushahidi wako kizimbani umewaambia majaji kwamba P3 alikua anahamasisha watu kupiga mawe?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Kwanini hujalisema wakati upo kizimbani
Part 219 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 217
Anaendelea Mhe. Lissu na Cross examination.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi ili nikuhoji vizuri naomba uwaambie waheshimiwa majaji kama upo tayari maelezo yako yapokelewe kama kielelezo
Coplo Amani : nipo tayari
Serikali: hatuna pingamizi.
Mahakama; maelezo haya yanapokelewa kama exhibit D14
Mhe. Lissu: Waheshimiwa naomba exhibit D14.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi maelezo yako sasa ni kielelezo D14 naomba uyaangilie vizuri
Swali langu la kwanza umesema unafanya kazi katika kitengo cha upelelezi chini ya Mkuu wa upepelezi wilaya
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama hayo maneno yapo kwenye D14
Coplo Amani : yapo
Mhe. Lissu: wapi
Coplo Amani : angalia page ya pili
Mhe. Lissu: soma
Shahidi anasoma
Mhe. Lissu: Naomba niangalie hayo maelezo na waheshimiwa majaji naomba na nyie muangalie kwenye typed.
Mhe. Lissu: naomba na mimi nisome waheshimiwa majaji, yupo sahihi kama alivyosoma ya kwangu ndio yamekosewa.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako shahidi umesema wewe ni msaidizi katika shughuli zote za upelelezi wilaya ya Mbeya
Coplo Amani : sahihi kabisa
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama hayo maneno yapo kwenye kielelezo D14
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema ulikua unaelezea Kituo cha polisi Ilomba ulisema ni Kituo kidogo cha polisi kilicho chini kituo cha kati cha mbeya kama out post na ukisema ivi ina maana hakija-qualify kuwa Kituo cha Polisi?
Coplo Amani : sahihi
Mhe. Lissu: kama hayo maneno yapo kwenye maeleezo yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: 4 april 2024 kwa majibu wa maelezo yako ulipewa maelekezo na Jorum kwenda mtaa wa Mtengule
Coplo Amani : Kweli
Mhe. Lissu: Lakini alikupa namba ya simu askari wa intelijensia ili akuongoze ukamkamate mhalifu
Coplo Amani : sahihi
Mhe. Lissu: waambie kama hayo maneno kwamba ulipewa namba ya simu yapo kwenye maelezo yako.
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo katika kielelezo D14
Mhe. Lissu: uliwaeleze askari wa intelijensia kama askari wanaojichanganya na raia kama vile boda boda
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama huo ufafanuzi wako upo kwenye maelezo yako.
Coplo Amani : hakuna
Mhe. Lissu: : Baada ya kupewa namba ya mtu wa intelijensi uliwasiliana nae na badae ulikutana nae mtaa wa Mtengule
Coplo Amani : Kweli
Mhe. Lissu: waeleze kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema huyo Askari wa intelijensia alikuongoza na kukuonyesha huyo mtuhumiwa katika kijiwe cha boda boda na kulikua na watu wengi, waeleze kama hayo maneno yapo kwenye statement yako
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema taarifa ulizopewa mtuhumiwa ndiye anayehamasisha wenzake kufanya vurugu na kuzuia uchaguzi wa 2025
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: waonyeshe hayo maneno kama yapo katika maelezo yako.
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Sasa ushahidi wako unasema ivi baada ya kuonyeshwa huyo mtuhumiwa ulimfata na kumtoa pembeni ya kijiwe, kisha ukajitambulisha kwake kwa jina na ukamwambia tuhuma zake za kuhamasisha vurugu na kuzuia uchaguzi wa 2025, sasa angalia D14 na ueleze kama hayo maeno yapo?
Coplo Amani: hayapo.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako umesema, ulimueleza kuwa anahitajika kituo cha polisi Ilomba na alikubali kwenda, ni kweli au si kweli
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Waeleze kama hayo maneno yapo katika maelezo yako D14
Coplo Amani: Ndio yapo
Mhe. Lissu: yapo wapi, utusomee?
Coplo Amani : hayapo
Mhe. Lissu: Umesema kwamba, kwenye maelezo yako tuhuma iliyokuwa inamkabili ni kinyume na kifungu cha 390, waeleze waheshimiwa majaji kama kwenye maelezo yako yapo?
Coplo Amani : hayapo.
Mhe. Lissu: umesema baada ya kumhoji alikubali kuwa anashawishi wenzake juu ya vurugu na wakati akiangalia YouTube aliona Tundu Lissu akihamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025
Coplo Amani :Kweli
Part 218 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 216
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa Maswali ya Dodoso.
Anasimama Mheshimiwa Lissu kwa ajili ya kumfanyia Cross Examination Shahidi ambae anaitwa Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa kwa kuanzia naomba nipatiwe kielelezo D12, waheshimiwa majaji haya ni maelezo ya P3.
Mhe. Lissu : Sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama uliandika maelezo polisi
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama unaweza kuyatambua ukionyeshwa
Coplo Amani : nikionyeshwa nitaweza kuyatambua
Mhe. Lissu: naomba shahidi aonyeshwe maelezo yake aliyoandika polisi.
Coplo Amani : haya ndio maelezo yangu
Mhe. Lissu: asante sana, sasa shahidi hayo maelezo yako naomba uwaeleze majaji kama uliyaandika mwenyewe au uliandikiwa na askari mwingine?
Coplo Amani : haya maelezo niliandikiwa na askari mwingine
Mhe. Lissu: mtaje jina tafadhali
Coplo Amani : Anaitwa H9207 detective coplo Robert
Mhe. Lissu: Kwenye maelezo yako hayo waeleze majaji kama ni utaratibu mtu anayeandika maelezo ya shahidi hawezi akawa ndio mtu huyohuyo kama shahidi?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji pamoja na majibu mazuri ya shahidi huyu nataka ku-impeach credibility yake, nitamsomea maelezo yake, nitamuonyesha maeneo nitakayotaka kumuuliza maswali halafu nitamtaka ayawasilishe kama kilelezo.
Mhe. Lissu anamsomea maelezo yake
Mhe. Lissu : Haya ndio maelezo yako kama nilivyoyasoma?
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji mshtakiwa kuna maeneo amekosea naomba nimrekebishe, sio kata ya Isuesue ni Isyesye 😁
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji kwakua na nyie mnarekodi hii mimi nimeona imeandikwa isuesue waheshimiwa…
Kwenye maneno “ni dereva wa bodaboda isuesue Mwintengule”… kwenye original Isyesye… kwahiyo tutaenda na ya kwako.
Kuna eneo lingine ambalo lina shida?
Coplo Amani : hapana.
Mhe. Lissu : Sasa kuna maeneo nataka kukuhoji kwa ajili ya kukukanusha kama ifuatavyo;
1. Kwamba unafanya kazi chini ya OCCID Mbeya mjini
2. Kwamba wewe ni msaidizi wa upelelezi ndani ya Mbeya mjini
3. Umeelezea Kituo cha Polisi cha Ilomba kwamba ni kituo kidogo kilichopo chini ya kituo cha Kati Mbeya umesema ni kama out post.
4. Umeeleza kwamba kaimu OCCID Inspekta Jorum alipokupa maelekezo ya kwenda kumkamata P3 alikupa namba ya simu ya askari wa kitengo cha intelijensia kwa ajili ya kwenda kumkamata P3
5. Kwamba hawa askari huwa wanajichanganya na raia kama dereva boda boda n.k
6. Baada ya kupewa namba ya simu ukawasiliama nae na mkakutana Isyesye.
7. Kwamba kulikua na watu wengi na mlipita na akakuonyesha mtuhumiwa kwenye kituo cha boda boda.
8. Taarifa mlizopewa na Jorum ni mtuhumiwa ndiye anayehamasisha wenzake kufanya vurugu uchaguzi wa 2025
9. Baada ya kuonyeshwa huyo mtuhumiwa ulimfata na kumtoa pembeni ya kijiwe na kisha ulijitambulisha kwake kwa jina na kumueleza tuhuma zake.
10. Ulimwambia baada ya kumtoa pembeni kwamba anahitajika Kituo cha Polisi Ilomba na yeye alikubali kwenda.
11. Ni ushahidi wako maelezo aliyoandika mtuhumiwa ni uchochezi, kusababisha vurugu na kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025.
12. Shitaka uliloandika lilikua ni kukiuka masharti ya kifungu cha 390 cha Penal code
13. Wakati ukimhoji alikwambia kwamba aliona taarifa kwenye YouTube akamuona Lissu akiwa anahamisisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi 2025.
14. Baada ya kuandika maelezo yake ulimjulisha inspeka Jorum akakuelekea kumuachia kwa dhamana na we anaripoti kila baada ya siku tatu
15. Ni ushahidi unaohusu tareh 17 april 2025 kwamba siku hiyo wakati ukiwa Ilomba Kituo cha Polisi ulielekezwa na inspekta Horum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana maelezo ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu na yeye kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vijana wenzake kufanya vurugu.
16. Baada ya kurekodi malezo hayo na ulimjulisha Inspekta Jorum na ukamkabidhi malezo hayo.
Part 217 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 215
Katuga anaendelea kumuongoza Shahidi ambae ni Coplo Amani
Wakili wa Serikali: Kikafuata nini?
Coplo Amani: Baada ya kuonyeshwa mtu huyo, nilimfata na nikamuita nikamtoa eneo hilo la bodaboda tukakaa pembeni kidogo, nikajitambulisha kwake kwamba mimi ni G9304 natoka Kituo cha Polisi kati Mbeya, baada ya hapo nilimueleza tuhuma yake ya kuhamsisha vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025.
Wakili: Uchaguzi ulihusu nini?
Coplo Amani : Uchaguzi ulikua unahusu rais, wabunge pamoja na madiwani.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Baada ya kumueleza tuhuma zake nikamueleza kwamba anahitajika Kituo cha Polisi Ilomba.
Wakili: kikafuata nini?
Coplo Amani : Baada ya hapo hakubisha na alikubali kwenda kituo cha polisi Ilomba.
Wakili: ukafanya nini?
Coplo Amani : niliondoka nae mpaka Kituo cha Polisi Ilomba
Wakili: ukafanya nini?
Coplo Amani : Baada ya kufika kituo cha Polisi nilimjulisha Inspekta Joram, akanipa maelekezo ya kumuandika mtuhumiwa maelezo.
Wakili: anaitwa nani huyo mtuhumiwa?
Coplo Amani: Mtuhumiwa huyo katika shauri hili anajulikana kama P3.
Wakili: Ikawaje?
Coplo Amani : Nilimuandika maelezo kwa tuhuma za uchochezi na kuhamasisha kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Nini kikafuata?
Coplo Amani : Baada ya hayo maelekezo nilimuandika maelezo kama nilivyoelekezwa na nilimuandika maelezo kama mtuhumiwa.
Wakili: kwa kosa gani?
Coplo Amani : makosa hayo ni kinyume cha kifungu cha 390 cha sheria ya kanuni ya adhabu
Wakili: Ikawaje?
Coplo Amani :. Baada ya kumhoji mtuhumiwa alinieleza kwamba ni kweli alihamasisha wenzake kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025
Wakili: Nini Kingine?
Shahidi: Pia alinieleza siku hiyo ya tarehe 4 April 2025 alikua akipitia taarifa mbalimbali na wakati anaendelea kupitia taarifa kwenye mtandao wa youtube alisikia mtu ambaye alimtaja kama Mwenyekiti wa CHADEMA anayeitwa Tundu Antiphas Lissu akiomgea na kutoa kauli za kuhamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Wakili: kikafuata nini?
Coplo Amani : Baada ya kumaliza kumuandika maelezo nilimjulisha Inspekta Joram na akanipa maelezo kwamba mtuhumiwa adhamimiwe na aripoti kituo cha polisi Ilomba na aripoti kila baada ya siku tatu.
Wakili: nini kilifanyika Tarehe 17 April
Coplo Amani : Tarehe 17 april 2025 nikiwa kituo cha polisi Ilomba nilipewa maelekezo na Inspekta Joram ya kuandika maelezo kama shahidi.
Wakili: Kingine?
Coplo Amani : Nilipewa maelekezo ya kumwandika kama shahidi kuhusiana na kile alichoeleza kwenye maelezo yake kwamba aliona mwenyekiti wake wa CHADEMA akihamasisha vurugu na kuharinubuchaguzi mkuu wa 2025 na kwamba baada ya kuona kauli ile yeye kama mfuasi wa CHADEMA, alihamasika kutokana na kauli zile na alikua tayari kuwashawishi vijana wenzake kuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Baada ya hapo?
Coplo Amani : Baada ya kumaliza kumuandika maelezo nilimjulisha Inspekta Joram.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Hayo maelezo nilimkabidhi inspekta Joram.
Wakili wa Serikali : Waheshimiwa majaji ni hayo tu kwa shahidi huyu.
Part 216 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 214
Leo Mhe. Lissu ameingia Mahakamani akiwa amepiga Jeans na T-Shirt fulani hivi nyeusi yenye neno moja lililoandikwa kwa herufi kubwa "DUDA"
Kaka David Jumbe anasema DUDA ni neno la Kinyaturu ambalo maana yake ni mtoto ambae anapendwa sana.
Majaji wameingia,
Naona wanaandika kidogo pale juu.
Wakili wa Serikali anasimama, anasema upande wa Serikali wapo Kama walivokuwa asubuhi.
Wakili wa serikali: Shahidi anayefata sio shahidi wa kulindwa, anaitwa Coplo Amani.
Shahidi anaingia Mahakamani.
Jaji anamuuliza unaitwa nani?
Naitwa G9304 detective Coplo Amani
Una miaka mingapi: Nina miaka 35
Dini yako: Shahidi: mkristo
Kazi yako: Shahidi: mimi ni askari polisi.
Wakili wa Serikali : Toka lini?
Coplo Amani : Nimekua askari polisi tangu 2012
Wakili: unaifanyia wapi hiyo kazi?
Coplo Amani : Kazi yangu naifanyia mkoa wa Mbeya wilaya wa Mbeya mjini, kituo cha polisi cha kati Mbeya.
Wakili: Kituo gani?
Coplo Amani : Kituo cha Kati Mbeya nipo tangu 2012
Wakili: Una elimu gani ya Polisi?
Coplo Amani : Elimu yangu niliipata 2011-2012 ndani ya chuo cha polisi Moshi
Wakili: Ulivyohitimu ikawaje?
Coplo Amani: Baada ya kuhitimu mafunzo nilipangiwa Kituo cha Polisi Kati Mbeya Mkoa wa Mbeya.
Wakili: Kitengo gani upo?
Coplo Amani : Kituo cha Polisi Kati Mbeya nipo kitengo cha upelelezi wa makosa ya jinai
Wakili: Unafanya kazi chini ya nani hapo?
Coplo Amani : Nikiwa chini ya ofisi ya mpelelezi wa wilaya ya Mbeya kwa kifupi ni OCCID
Wakili: Kingine?
Coplo Amani: Katika ofisi hiyo nipo kama msaidizi wa shughuli zote za upelelezi ndani ya wilaya ya Mbeya mjini.
Wakili: Majukumu yako ni yapi?
Coplo Amani: Majukumu yangu ni kufanya doria, kupeleleza kesi zote za jinai, kukamata watuhumiwa wote wa makosa ya jinai na kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote wa jinai
Wakili: Unakumbuka nini tarehe 04 April?
Coplo Amani : April 4, 2025 nakumbuka nilikua Kituo cha Polisi Ilomba ambacho kipo Wilaya ya Mbeya Mjini, Mkoa wa Mbaya, hiki ni kituo kidogo cha polisi kinajulikana kama outpost
Wakili: Unajua nini kuhusu hicho kituo cha Polisi?
Coplo Amani : Kituo cha Polisi Ilomba kipo chini ya kituo cha polisi kati Mbeya.
Wakili: Nini kikaendelea?
Coplo Amani: Nilipewa maelekezo na Inspekta Joram, ambaye ni kaimu wa upelele Wilaya ya Mbeya mjini.
Wakili: Akakwambia nini?
Coplo Amani : Alinipa maelekezo ya kwenda Isyesye mtaa wa Mwamtengule ambapo alinieleza kwamba kuna watu wanapanga njama za kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Wakili: kingine?
Coplo Amani: Lakini pia alinipa namba ya simu kwamba niwasiliane na askari mwenzangu, ambaye yupo kitengo cha intelijensia ili aende akanionyeshe watu hao wanaojipanga kufanya fujo na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Kazi yako inahusiana na nini?
Coplo Amani: Askari ambaye yupo intelijensi ni askari wanaofanya kazi ya kujichanganya na wananchi ili wapate taarifa mbalimbali za uhalifu.
Wakili: mnafanyaje kazi?
Coplo Amani: Askari wa intelijensia huwa wanajichanganya katika shughuli mbalimbali za wananchi, wengine ni bodaboda n.k ili kupata taarifa za makosa ya jinai.
Wakili: nini kilifuata?
Coplo Amani : Baada ya maelekezo hayo niliwasiliana na huyo askari tukakutana Isyesye mtaa wa Mwantengule
Wakili: Mkafanya nini?
Coplo Amani : Tulivyokutana akaniongoza na kunionyesha mtuhumiwa ambaye nilipaswa kumkamata.
Wakili: Kulikuwaje?
Coplo Amani : Pale kulikua na watu wengi tukapita kwa siri na akanionyesha mtuhumiwa katika kijiwe cha bodaboda akiwa na wenzake.
Wakili: Ukafanya nini?
Coplo Amani : Huyo mtu niliyetakiwa kumkamata ndiye aliyekuwa anahamasisha wenzake kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu wa 2025.
Part 215 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 210
Anaendelea Mhe. Lissu na Cross Examination.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji naomba shahidi apewe kielelezo D13
Mhe Lissu: Jana kwenye ushahidi wako uliulizwa unaishi wapi na ukasema unaishi katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli.
Mhe. Lissu: Naomba uangalie maelezo yako, nenda palipo andikwa makazi usome pameandikwa makazi yako wapi?
Shahidi wa kificho P9: Pameandiwa Mwakibete.
Mhe. Lissu: Kwenye mstari wa kwanza kabisa sema palivoandikwa hapo? Kwamba unaishi?
Shahidi wa kificho P9 : Pameandikwa Mwakibete lakin nilihojiwa Mbeya.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unafahamu kwamba haya maeneo huwa yanatangazwa kwenye gazeti la serikali na waziri wa TAMISEMI
Shahidi wa kificho P9 : sifahamu
Mhe. Lissu: Umeonyesha gazeti la Serikali linaloonyesha Mwakibete ni Mbeya,?
Shahidi wa kificho P9; Hapana.
Mhe. Lissu: unafikri unaandika andika tu unaingizwa chaka na mapolisi na wewe unaandika tu.
Mhe. Lissu: Uliulizwa unafanya shughuli gani na ulisema unafanya kazi ya fundi umeme na kazi zako unafanya katika Halmashauri ya Mbeya, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako unafanya kazi gani?
Shahidi wa kificho P9 : Mkulima
Mhe. Lissu: Kazi ni mkulima hapa unajifanya fundi umeme, lugha gongana.
Watu wanacheka: 😂😂😂😂
Mhe. Lissu: nyie Waha wa kigoma wajanja sana nyie na mimi napenda watu wajanja kama wewe.
Mhe. Lissu: Uliulizwa unakumbuka kitu gani kilikukuta 2024, ukasema nilivutiwa na sera za CHADEMA na nikawanafatilia matangazo, mikutano n.k haya sasa soma maelezo yako mjanja wa Jiji la Mbeya…😁
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji hayo maelezo uliyosoma hapo kama yapo na ulivyosema jana
Shahidi wa kificho P9 : Hayapo
Mhe. Lissu : Uliandika kwa mapolisi wakakupuuza wakaandika ya kwao.
Mhe. Lissu: Katika matukio mengi uliyofatilia ulitaja matembezi ya yaliyoongozwa na Lissu yalianzia Uyole, na Heche Isanga, mwambie jaji kama Mhe. Heche yupo katika maelezo kayo
Shahidi wa kificho P9: Nilieleza ni Mnyika sio Heche.
Mhe. Lissu: Jana ulisema Heche alianzia Isanga, unataka niwasumbue majaji wakusomee ulichokisema??
Shahidi wa kificho P9: inawezekana nilikosea
Mhe. Lissu: Kazi yangu ni kukamata watu waongo kama wewe.
Shahidi wa kificho P9 : Hiyo unasema ww
Mhe. Lissu: ndio nasema.
Mhe. Lissu: Ulisema mnamo tarehe 3 April 2025 ukiwa nyumbani kwako wakati unaperuzi mitandao kupitia simu yako aina ya Samsung 8 pro, kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : kweli
Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako waeleze majaji kama kuna mahala popote ulikua unaangalia mitandao kupitia aina ya Samsung 8 pro.
Shahidi wa kificho P9: hayajaandikwa.
Mhe. Lissu: Asante, mmeuzwa na mapolisi.
Mhe. Lissu: Ulisema kwamba uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uweze kuimgia instagram lazima uwe na simu janja, account na bundle, hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P9 : hayapo.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana ulisema wakati unaingia kwenye instagram uliona video ya Tundu lissu na ukasema huo mtandao umeusahau.
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nimeusahau.
Mhe. Lissu: Kama umesahau inamaana, kwenye maelezo yako utakua umeandika.
Shahidi wa kificho P9: Sasa wewe unaniuliza mambo waliyoniuliza mawakili.
Mhe. Lissu: Jibu swali langu. Unanifundisha namna ya kukuhoji?
Shahidi wa kificho P9 : Ndio hakuna
Mhe. Lissu: Uliulizwa muonekano wa Tundu Lissu, ukasema alikua ukumbini alivaa kombati za kaki za chadema na tshirt nyeusi na bendera ya taifa na rangi za CHADEMA, kweli si kwei?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Sasa waeleze waheshimiwa majaji kama yapo katika maelezo yako.
Shahidi wa kificho P9 : Hakuna
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana uliulizwa alisema atauzuiaje ukasema tutafanya vurugu na kuuvuruga uchaguzi huo.
Shahidi wa kificho P9: Kweli
Part 211 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 211
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross examination Shahidi wa kificho P9
Mhe. Lissu: Waambie majaji kama tutafanya vurugu na kuuvuruga uchaguzi huo kama yapo kwenye maelezo yako…nasubiri jibu shahidi!
Shahidi wa kificho P9: Hayapo
Mhe. Lissu: Uliendelea kusema, alisema lazima tukichafue, kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : kweli.
Mhe. Lissu: hayo maneno yapo au hapo.
Shahidi wa kificho P9 : sasa mbona unarudia maswali. hayapo.
Mhe. Lissu: Twende kwa yaliyotokea 22 April 2025, ulisema siku hiyo ulipigiwa simu na polisi kwenda Kituo cha Polisi Mwanjelwa.
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Sasa soma pale palipoanzia na leo Tarehe 22 April 2025 mpaka nitakapokwambia basi…
Shahidi wa kificho P9 Anasoma…
Mhe. Lissu: Kwenye hiyo sehemu kuna sehemu kumeandikwa kituo cha polisi Mwanjelwa.?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli haijaandikwa
Mhe. Lissu: Na ukasema ulipofika walisema wanataka kukuhoji tena kwa matukio yaliyokuleta hapa.
Shahidi wa kificho P9: Kweli.
Mhe.Lissu : Waambie kama hayo maneno yapo kwa tukio lililokuleta hapa.
Shahidi wa kificho P9 : Hayapo.
Mhe. Lissu: Kwenye ushahidi wako jana, ulisema nilihojiwa na mtu mmoja na mwingine alichangia kwa kuniuliza maswali mbalimbali, waeleze majaji kama hayo maneno yapo katika maelezo yako?
Shahidi wa kificho P9 : Hayapo.
Mhe. Lissu: Niliona clip ya Tundu Lissu ndio nikaanza, waeleze hayo maneno kama yapo katika maelezo yako.
Shahidi wa kificho P9 : hayapo.
Mhe. Lissu: Sijamalizana na wewe, nataka ukitoka hapa ukawaeleze Mapolisi kwamba kule hakufai!
Watu wanacheka: 😂😂😂😁
Mhe. Lissu: Ulisema mimi kama mwananchama wa CHADEMA nilishawishika na kwamba nitafanya uasi, hayo maneno yapo au hayapo?
Shahidi wa kificho P9: Yapo.
Mhe. Lissu: Sasa nataka uwaambie majaji kwamba wewe ni Mwanachama wa CHADEMA au sio?
Shahidi wa kificho P9 : Mimi sio mwanachama wa CHADEMA.
Mhe. Lissu: Kwenye maelezo yako na ushahidi wako wa jana, ulisema mwaka 2024 ulivutiwa na sera na kuamua kuwa mwanachama wa CHADEMA, kweli au sio kweli?
Shahidi wa kificho P9 :Kweli.
Mhe. Lissu: waambie majaji wafuasi wa CHADEMA huwa wanaandikishwa wapi.
Shahidi wa kificho P9: sifahamu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama wafuasi huwa wanatambulishwa wapi.
Shahidi wa kificho P9: Sijui
Mhe. Lissu: Waeleze kama huwa wanaalama usoni?
Shahidi wa kificho P9: Hapana
Mhe. Lissu: Na ulisema baada ya kuwa mfuasi ulishiriki katika matembezi ya amani, kweli au sio kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli
Mhe. Lissu: Waambie waheshimiwa kama ulijiandikisha sehemu yoyote?
Shahidi wa kificho P9 : Hapana
Mhe. Lissu: Sasa shahidi hukuwahi kujiandikisha popote, huna alama yoyote kuwa ni mfuasi wa CHADEMA, waeleze majaji wataamini vipi kwamba wewe ni mfuasi wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P9 : Mimi sijui hilo ni suala la amani.
Mhe. Lissu: Unasema tulihamasishwa kushiriki kongamano la vijana lililopangwa kufanyika Mbeya, waambie kama uliwahi kupewa mualiko wowote hata wa simu?
Shahidi wa kificho P9 ; hapana sikupewa mualiko wowote.
Mhe. Lissu: kama kiongozi wa chama aliwahi kukufata ili kukupa taarifa ya kongamano.
Shahidi wa kificho P9 : hawakunifata.
Mhe. Lissu: Kama hawakukufata inamaana hawakujui.
Shahidi wa kificho P9 : Sio lazima wanijue wote.
Mhe. Lissu: Kwa maelezo yako ya ushahidi ya jana, umesema ulisoma VETA Mbeya kati ya 2008-2010 ulipohitimu, kweli au sio kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama umewasilisha cheti cha kuhitimu?
Shahidi wa kificho P9 : sijawasilisha kwasababu hakina umuhimu.
Mhe. Lissu: wataaminije? Kwasababu maneno matupu hayavunji mfupa.
Mhe. Lissu: Umesajiliwa kama fundi umeme wa majumbani na viwandani.
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nimesjiliwa.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama umeleta hati ya kusajiliwa?
Shahidi wa kificho P9: Hapana.
Part 212 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 213
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa kificho P9
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji hilo pingamizi la Wakili la Serikali halina maana yoyote, kwasababu shahidi mwenyewe amesema kwamba summons alipelekewa summons na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Mwenyekiti ni ofisa wa serikali, lakini vilevile Mahakama haitaweza kujua kama huyu shahidi ni mkweli au ni muongo kwahiyo swali langu ni halali na ninaomba pingamizi lao litupitiliwe mbali, lakini huyo Mwenyekiti sio mtu ambaye amelindwa na sheria.
Katuga: Sisi tunaomba swali hilo shahidi asiulizwa kwasababu swali hilo litapelekea utambuzi wa shahidi huyu na kama tunavyojua humu ndani kuna wafuasi wake, researchers wake wanaweza wakaenda kumtafuta ili kumtambua shahidi huyu.
Mhe. Lissu: naomba ondoa hiyo kauli yako mimi sijazungumzia kuhusu wafuasi wangu humu.
Katuga: Naondoa hiyo ilikua ni by the way lakini msimamo wetu ni kwamba swali hilo shahidi asiulizwe
Mahakama: tunadhani uendelee na x-examination bila hilo jina.
Mhe.Lissu: Lakin waheshimiwa majaji mnaweza kuona namna cross examination yangu inavyokua limited lakini naomba niendelee.
Mhe. Lissu: shahidi umekujaje hapa
Shahidi wa kificho P9: nimependa bus
Mhe. Lissu: nani amekulipia nauli
Shahidi wa kificho P9 : nimejilipia mwenyewe
Mhe. Lissu: Umefikia wapi
Shahidi wa kificho P9 : Kwa ndugu yangu.
Mhe. Lissu: Waambie waheshimiwa majaji kama kuna kiongozi au mfuasi anajua kama unakuja kutoa ushahidi
Shahidi wa kificho P9: Ndio wapo baadhi
Mhe. Lissu: waliwahi kukutishia
Shahidi wa kificho P9 : ndio
Mhe. Lissu: unajua hilo ni kosa
Shahidi wa kificho P9 : hilo ni kosa la jinai
Mhe. Lissu: umewataja,
Shahidi wa kificho P9 : siwezi kuwataja kwa usalama
Mhe.Lissu: waeleze majaji kama ulitoa taarifa kituo cha polis
Shahidi wa kificho P9 : ndio
Mhe. Lissu: Kituo cha polisi kipi?
Shahidi wa kificho P9: Sasa nikitoa taarifa hiyo hapa si itakua navunja usalama?
Mhe. Lissu: Hebu jibu swali bwana tusisumbuane
Mahakama: Shahidi hebu jibu hilo swali
Shahidi wa kificho P9: Nilitoa kituo cha polisi Ilomba
Mhe. Lissu: Ulipewa RB
Shahidi wa kificho P9: ndio
Mhe. Lissu: umeitoa hapa mahakamani?
Shahidi wa kificho P9 : hapana
Mhe. Lissu: Polisi walichukua hatua gani?
Shahidi wa kificho P9: Walisema watafatilia
Mhe. Lissu: waambie waheshimiwa majaji kama kuna mtu yoyote amekamatwa
Shahidi wa kificho P9 : hapana
Mhe. Lissu: Waambie kama kuna mtu yoyote amepelekwa mahakamani:
Shahidi wa kificho P9 : hakuna
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji sina swali lingine kwa shahidi huyu.
Wakili wa Serikali: Leo tunashahidi mmoja, tunaomba break kidogo halafu tuje na shahidi mmoja aliyebaki, kwasababu jana hatukupumzika.
Mahakama: Mshitakiwa unasemaje
Mhe. Lissu: Tukienda kwa utaratibu huu tutachukua mida mrefu sana, Mahakama ilisema upande wa serikali ulete mashahidi wasiopungua watatu, kwanin hawajaleta hao mashahidi wengine.
Upande wa mashtaka wanatakiwa wawe na mshahidi wengine kama walivyotakiwa na Mahakama.
Katuga: Jana tulisema tutakuja na shahidi mmoja then twende kuargue application yetu, hatujaweza kuja na mashahidi wengi ili tupate muda wa kutosha kwasababu yeye alisema ana-objection.
Mahakama: Nadhani twende break fupi kwanza ili tukirudi tuendelee na huyo shahidi halafu tukimalizana nae mambo mengine yatafata.
Part 2014 itaendelea tukirudi.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 212
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa kificho P9
Mhe. Lissu: Shahidi umesema tarehe 4 april 2024 ukiwa na jamaa zako nyumbani kwako, “Tukawa tunajadili kauli ya Mwenyekiti kwamba tukichafue, ni kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Umewataja hao jamaa zako wakati unatoa ushahidi?
Shahidi wa kificho P9 : Hapana.
Mhe. Lissu: Wakati tunazungumza jamaa yangu akaniomba namba yangu ya simu, jamaa ambaye simfahamu, unakumbuka hayo maneno?
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nakumbuka.
Mhe. Lissu: inawezekana mtu usiyemfahamu kuwa jamaa yako, hiyo inaingia akilini!
Shahidi wa kificho P9: Inawezekana.
Mhe. Lissu; Na jamaa yako ambaye humfahamu akakuomba namba yako ya simu na ukampatia? Inaingia akilini?
Shahidi wa kificho P9 : ndio inaingia akilini.
Mhe. Lissu: ndivyo ulivyofundishwa na mapolisi.
Mhe. Lissu: Kwa vile unafanya kazi ya fundi umeme kwa malipo, una leseni ya biashara?
Shahidi wa kificho P9: Sina leseni ya biashara kwasababu sina ofisi
Mhe. Lissu: Una TIN number?
Shahidi wa kificho P9: Ndio
Mhe. Lissu: Umeionyesha?
Shahidi wa kificho P9 : hapana kwasabb haijahitajika.
Mhe. Lissu: Tarehe 5 April 2024 siku ambayo unakamatwa, unasema ulipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni mteja, na ukasema tulipoonana akajitambulisha kuwa ni afisa wa polisi na akanionyesha kitambulisho chake, waambie waheshimiwa majaji kama unakumbuka jina la icho kitambulisho?
Shahidi wa kificho P9: Nakumbuka ni Vicent
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama hilo jina lipo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P9: Halipo.
Mhe. Lissu: Hiyo tarehe 5 April 2024 uliandika maelezo kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P9 : Kweli.
Mhe. Lissu: Na maelezo ya siku hiyo yalihusu uchochezi na kuzuia uchaguzi, kweli au si kweli?
Shahidi wa kificho P9: Kweli
Mhe. Lissu: Waambie majaji hiyo tuhuma ya uchochezi na kuzuia uchaguzi imeishia wapi?
Shahidi wa kificho P9 : Sijui
Mhe. Lissu: Waeleze majaji tangu tarehe 5 april 2024 umepelekwa Mahakamani kwa tuhuma hizo?
Shahidi wa kificho P9 : sijawahi kupelekwa
Mhe. Lissu: Waeleze majaji ulipoitwa polisi kwa mara ya pili 22 april 2025 kama ulielezwa tuhuma za uchochezi na kuzuia uchaguzi?
Shahidi wa kificho P9: Ndio nilielezwa.
Mhe. Lissu: Angalia maelezo yako shahidi halafu tuonyeshe wapi uliuzwa juu ya tuhuma hizo
Shahidi wa kificho P9: Mimi nilieleza lakini wao hawakuandika.
Mhe. Lissu: Imekula kwako kwasababu wanasema haya ni maelezo yako.
Mhe. Lissu: Wewe ni shahidi kwenye kesi dhidi yangu, kweli si kweli.?
Shahidi wa kificho P9 : kweli
Mhe. Lissu: Na ndio maana umekuja kutoa ushahhidi jana na leo, kweli si kweli.
Shahidi wa kificho P9 : kweli.
Mhe. Lissu: Nikisema walikukamata tu ili uje kutia ushahidi dhidi yangu nitakua nakosea??
Shahidi wa kificho P9 : Mimi sifahamu.
Mhe. Lissu: Waambie waheshimiwa majaji kama unajua kuwa hakuna kosa la kuzuia uchaguzi?
Shahidi wa kificho P9 : ni kosa.
Mhe. Lissu: waambie majaji ni kwa mujibu wa sheria gani?
Shahidi wa kificho P9 : mimi sio mwanasheria.
Mhe. Lissu: ni sheria gani.
Shahidi wa kificho P9 ; Mimi najua kuzuia uchaguz kwa njia ya vurugu ni kosa lakini sheria gani sijui
Mhe. Lissu: Kama hujui sema sijui, sio kuleta ujuaji tu.
Mhe. Lissu: Kwani mimi nimeshatakiwa kwa kosa la vurugu.
Shahidi wa kificho P9 : umeshtakiwa kwa uhaini.
Mhe.Lissu: Shahidi ulikujaje Dar es salaam
Shahidi wa kificho P9: Nilipanda bus
Mhe. Lissu: Nani alikwambia uje kutoa ushahidi
Shahidi wa kificho P9 : Nililetewa wito
Mhe. Lissu: nani alikuletea?
Shahidi wa kificho P9 : aliniletea Mwenyekiti wa serikali za mtaa.
Mhe. Lissu: anaitwa nani?
Shahidi wa kificho P9 : Siwezi kukutajia kwasababu za kiusalama.
Katuga: sisi tunapinga hilo swali kwasababu za kiusalama. Kwahyo tunaomba hilo swali asiulizwe.
Part 213 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 20, 2026
Jana tuliishia Part 208 so leo tunaendelea na-;
Part 209.
Imepigwa high Court ya kikakamavu,
Majaji wameingia wapo watatu kama kawaida yao.
Mhe. Lissu nae yupo
Karani anasoma criminal session No. 19605/ 2025 Republic v. Tundu Lissu
Mawakili wa Serikali wanajitambulisha kama kawaida yao japo leo hawajaja kama utitiri.
Wakili wa Serikali anasema, shauri linakuja kuendelea kusikilizwa na tuna shahidi wa 14 kwa ajili ya maswali ya dodoso.
Jaji Ndunguru anamuuliza Mhe. Lissu kama yupo tayari.
Mhe. Tundu Lissu anasema mimi nipo tayari.
Jaji Ndunguru anamkumbusha Shahidi kwamba yupo chini ya kiapa.
Ikumbukwe kwamba leo tunaendelea na Shahidi wa kificho P9.
Mhe. Lissu: Shahidi habari za asubuhi
Shahidi wa kificho P9 : salama.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama uliandika maelezo tarehe 22 aprill 2025
Shahidi wa kificho P9: Ndio
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ukionyeshwa maelezo hayo utayatambua.
Shahidi wa kificho P9 : Ndio nitayatambua
SHAHIDI ANAPELEKEWA MAELEZO YAKE.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama hayo ndio maelezo yako uliyoandika polisi tarehe 22 April 2025?
Shahidi wa kificho P9 : ndio ni yenyewe
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji nataka ku-impeach credit ya huyu witness, kwahiyo nitamsomea maelezo yake, nitamuonyesha maeneo ambayo nataka kumuhoji halafu nitamuomba ayawasilishe yapokelewe kama kielelezo.
Mhe. Lissu: Shahidi nitakusomea maelezo yako halafu tutahojiana kwasababu kuna mambo hayapo sawa kwenye maelezo yako, anamsomea maelezo shahidi…
Mhe. Lissu: Sasa shahidi umesikia nilichokisoma, waeleze waheshimiwa majaji kama nilichokisoma ndicho kilichopo kwako.
Sasa nataka nikueleze maeneeo nayotaka nikuhoji;-
1. Jana ulisema wewe ni mkazi wa Mbeya mjini, nataka nikuhoji hapo
2. Kwamba wewe kazi yako ni fundi umeme na unafanya kazi ndani ya maeneo ya Jiji la Halmashauri ya Mbeya
3. 2024 ulivutiwa na sera za CHADEMA na ukaamua kuwa mfuasi na ukawa unafatilia kwa karibu mikutano, matangazo na hotuba za vipngozi wa CHADEMA.
4. Ulizungumzia matembezi ya amani yaliyofanyika Mbeya 2024 na ukasema Mbowe alianzia Songwe na Lissu Uyole na Heche Isanga.
5. April 3, 2025 ukiwa nyumbani kwako ulikua unaperuzi mitandao ya kijamii kwa simu aina Samsung 8 pro nataka nikuhoji kuhusu hiyo simu.
6. Uliingia kwenye mtandao wa instagram na ili uingie kwenye mtandao huo lazima uwe na account na simu janja na bundle ili kuweza kuangalia picha na videos.
7. Wakati unaperuzi mtandao wa instagram uliona video ya Tundu Lissu lakini umesahau ilikua ni account ya nani.
8. Huyo Lissu uliyemuona alikua amevaa kombati ya kaki za chadema na tshirt nyeusi na alikua ukimbini na kulikua na bendera ya taifa na rangi za bendera ya CHADEMA.
9. Alisema tutavuruga uchaguzi kwa kufanya vurugu na kuvuruga uchaguzi huo.
10. Lissu alisema lazima tukichafue.
11. Ulipofika kwenye Kituo cha Polisi Mwanjelwa walikwambia wanataka wakufanyie tena mahojiano.
12. Nilihojiwa na mtu mmoja na mwingine wa pili alinihoji kwenye maswali mbalimbali.
13. Wakati unamjibu huyo anae kuhoji kwa mara ya pili niliona video ya Tundu Lissu, ndio nikaanza kufanya makosa.
Mhe. Lissu: Sasa shahidi waeleze majaji kama ungependa maelezo yako yaingie kama kielelezo mahakamani?
Shahidi wa kificho P9: haina shida.
Upande wa Serikali : hatuna pingamizi
Mahakama: Yamepokelewa kama kielelezo D13
Part 210 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 203
Mhe. Lissu anaendelea na Cross Examination,
Jaji Ndunguru: upande wa mashitaka.
Mkude: No objection.
Jaji Ndunguru : turejee kifungu 194 cha CPA.
Mkude: kifungu cha 194 kwa ujumla wake ni kuhusu protection ya ushahidi, kwa sababu shahidi au mshitakiwa anaweza akaomba impeachment, pale anapoomba shahidi apewe kielelezo hivo tunaweza kuendelea mheshimiwa Jaji.
Mhe.Lissu: Iko hivyo waheshimiwa Majaji, sikuwa nataka kuona jina lake kwenye kielelezo hicho bali nataka asome maelezo yake.
Mhe.Lissu: kwa hiyo shahidi ulitaka kuficha ukweli mahakamani.
Shahidi wa kificho P3 : hapana.
Mhe.Lissu: mbona haukusoma kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA na umeiandika kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi wa CHADEMA labda askari aliyeandika maelezo yangu alikosea.
Mhe.Lissu unaidanganya mahakama, soma kama ilivoandikwa.
Shahidi wa kificho P3 : mimi ni mfuasi/ mwanachama wa CHADEMA.
Mhe.Lissu: Sasa ulikuwa unaficha nini. Shahidi swali langu la pili kwenye maelezo yako umesema kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Sasa waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa kongamano hilo halikufanyika kwa sababu tulitawanywa uwanjani.
Shahidi wa kificho P3 : kongamano hilo halikufanikiwa.
Mhe.Lissu: hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Mhe.Lissu: shahidi umesema kwa bahati mbaya au nzuri kongamano hilo halikufanyika lilizuiliwa na serikali kweli au si kweli.
Shahidi wa kificho P3 : kweli.
Mhe.Lissu: wewe mfuasi wa CHADEMA kongamano la CHADEMA shughuli halali ya chama kuzuiliwa kwako ni bahati nzuri.
Shahidi wa kificho P3: sijui, mimi sielewei
Mhe.Lissu: ndiyo maana nikakuuliza tutajuaje kama wewe siyo pandikizi.
Shahidi wa kificho P3 : hilo swali nimeshalijibu tuendelee.
Mhe: Lissu: usijali tutaendelea kwenye maelezo yako ya Leo umesema ulikuwa na simu, Sasa kwenye hayo maelezo yako ya Polisi kuna sehemu uliandika kama ulikuwa na simu.
Shahidi wa kificho P3 : haipo.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua au haujui kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia compyuta.
Shahidi wa kificho P3 : sijui, mimi sina utaalamu huo wa kutumia compyuta.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama unajua kuwa unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia Television.
Shahidi wa kificho P3 : utaalamu huo sina.
Mhe.Lissu: unajua kama unaweza kufuatilia YouTube kwa kutumia tablet.
Shahidi wa kificho P3 : sijui huo utaalamu.
Mhe.Lissu: Kwenye maelezo yako kuna sehemu umeandika kuwa ulikuwa na simu
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe.Lissu: kwenye maelezo yako umesema uliyasikia maneno yangu kupitia video YouTube, kuna mashahidi wengine wamesema video hiyo ilikuwa na masaa 3 na madakika, waeleze waheshimiwa Majaji kama kuna sehemu umeandika video hiyo ilikuwa na muda gani.
Shahidi wa kificho P3 : hakuna
Mhe.Lissu: umesema umemfahamu mheshimiwa Lissu kupitia mitandao ya kijamii. Waeleze waheshimiwa Majaji kama kwenye maelezo yako umeandika hilo jambo.
Shahidi wa kificho P3 : hapana hayapo.
Mhe.Lissu: umesema mwezi march 2025 ulihudhuria mkutano uliohutubiwa na Mheshimiwa Tundu Lissu katika viwanja vya Ruanda nzovwe, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3: hayapo
Mhe.Lissu: umesema wakati ukiwahamasisha vijana wenzako hapo kijiweni alikuja mtu aliyejitambulisha kuwa ni Askari Polisi na kukuita pembeni kwamba njoo tuongee, waeleze waheshimiwa Majaji kama hayo maneno yapo kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : napitia kidogo
Mhe.Lissu: haujapaona hadi mwishoni kwenye paragraph ya mwisho.
Shahidi wa kificho P3 : naomba nikusomee, alikuja mtu aliyejitambulisha ni Askari Polisi.
Mhe.Lissu: swali langu ni kwamba hayo maneno akaniita pembeni akaniambia njoo tuongee, hayo maneno yapo au hayapo.
Shahidi wa kificho P3 : hayapo.
Part 204 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 202
Mhe. Lissu ameanza kumfanyia Cross examination Shahidi wa kificho P3.
Mhe. Lissu: shahidi hapo ulipo unaweza kuniona?
Shahidi wa kificho P3 : hapana
Mhe. Lissu: kwa taarifa yako hata mm siwezi kukuona kweli si kweli?
Shahidi wa kificho P3 : sahihi.
Mhe. Lissu: nataka nikuhoji kutokana na ushahidi wako na nashukuru umesema wewe ni mfuasi wa CHADEMA, sasa naomba uwaeleze majaji, mfuasi wa CHADEMA anakua na kutambulisho gani?
Shahidi wa kificho P3 ; anakua hana kitambulisho kwasababu anakua bado hajawa mwanachama.
Mhe. Lissu: mimi kiongozi wa CHADEMA na mtu yoyote aliyeopo hapa mahakamani atajuaje kama wewe ni mfuasi wa CHADEMA, huna kitambulisho na pia sikuoni?
Shahidi wa kificho P3 : hilo ni suala la imani
Mhe. Lissu: twende taratibu kaka, waeleze majaji kama wafuasi wa chadema huwa wanaorodheshwa mahali ili kuwatambua.
Shahidi wa kificho P3 : binafsi sijajua huwa wanaorodheshwa wapi?
Mhe. Lissu: kwahiyo hujaorodheshwa?
Shahidi wa kificho P3 : sahihi.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama wafuasi wa CHADEMA kuna mahali huwa wanaenda kujitambulisha ili wajulikane
Shahidi wa kificho P3 : hakuna.
Mhe. Lissu: hapo ulipo kwenye kiboksi na mimi hapa nilipo kama kuna namna mimi naweza nikaelewa au kujua kama wewe ni mfuasi wa CCM na sio CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3 : sijui utajuaje ila mm ni mfuasi wa CHADEMA
Mhe. Lissu: na nitajua kama ww sio pandikizi la Polisi kwasababu hujajiandikisha popote wala huna chochote cha kukutambulisha kuwa ni mfuasi wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3 : itabidi uamini tu na uiamini mahakama tukufu kwasababu mimi sijui kwa kweli utawezaje kunitambua.
Mhe. Lissu: mfusi wa CHADEMA huwa anaalama usoni au kifuani kuwa yeye ni mfuasi wa CHADEMA?
Shahidi wa kificho P3: sijui
Mhe. Lissu : waeleze majaji kama uliandika maelezo Polisi tarehe 17 april 2025?
Shahidi wa kificho P3 : ndio
Mhe. Lissu: ukionyeshwa hayo maelezo yako utayatambua?
Shahidi wa kificho P3 : ndio
Mhe. Lissu: naomba shahidi apewe maelezo yake ya tarehe 17 april 2025.
Mkude: Hatuna pingamizi.
SHAHIDI ANAPEWA MAELEZO YAKE.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama hayo ndio maelezo uliyoyaandika tarehe 17 april 2025?
Shahidi wa kificho P3 : ngoja kidogo nayapitia.
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji kama hayo ni maelezo yako?
Shahidi wa kificho P3 : ndio yenyewe
Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji nataka ku-impeach credit ya shahidi huyu, nitamsomea maelezo yake, nitaonyesha maeneo ambayo nataka kumhoji halafu nikimaliza nitakuomba uyawasilishe kama kielelezo.
Shahidi wa kificho P3 : sawasawa.
Mhe.Lissu: anamsomea shahidi maelezo yake.
Mhe.Lissu: waeleze waheshimiwa Majaji kama nilichokisoma ndicho kilichoko kwenye maelezo yako.
Shahidi wa kificho P3 : ndiyo ulichokisoma ndicho kilichoko kwenye maelezo yangu.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi nataka nikuhoji kwenye eneo unalosema wewe ni mfuasi wa CHADEMA na maeneo mengine kadri nitakavyokuhoji kutokana na ushahidi wako.
Mheshimiwa Lissu anamsomea shahidi maeneo yote anayotaka kumhoji.
Maeneo 8.
Mhe.Lissu: Sasa hili nikuhoji sawasawa naomba uwaeleze waheshimiwa Majaji kama ungependa maelezo yako yapokelewe kama kielelezo mahakamani.
Shahidi wa kificho P3: ndiyo napendelea iwe hivyo.
Mhe.Jaji: itakuwa D12
Mhe.Lissu: ahsante waheshimiwa Majaji, naomba shahidi apewe kielelezo D12
Mhe.Lissu: Sasa swali langu la kwanza ni kwamba kwenye ushahidi wako leo umeieleza mahakama kuwa wewe ni mfuasi wa CHADEMA tangu mwaka 2021, ni kweli au si kweli.
Shahidi wa kificho P3 : ni kweli.
Mhe.Lissu: kwenye kielelezo D12 wasomee waheshimiwa Majaji pale unapoanzia mimi pia ni........ endelea hadi nitakapokwambia inatosha.
Shahidi wa kificho P3 : mimi pia ni mfuasi wa chama hicho.....
Shahidi anasitasita katika kusoma.
Mhe.Lissu: naomba pia nipewe kielelezo hicho naona kama shahidi anatupoteza.
Part 203 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 201
Anasimama Wakili wa Serikali Mkude anasema tunashahidi mwingie wa kulindwa ni P3,
Mpaka sasa huyu ni shahidi wa 13.
Shahidi ameingia kwenye kijumba cha mbao tayari.
Sasa anajitambulisha.
Shahidi wa kificho P3 : Nina miaka 35
Shahidi wa kificho P3: dini yangu muislamu
Shahidi wa kificho P3: naishi halmashauri ya Mbeya mjini, mtaa wa Mwamtengule kata ya Syesye
Shahidi wa kificho P3: najishughulisha na kazi ya dereva boda boda
Shahidi wa kificho P3: shughuli zangu nafanyia katika halmashauri ya jiji la Mbeya.
Shahidi wa kificho P3: nina miaka nane tangu naendesha boda boda
Shahidi wa kificho P3: mimi ni mfuasi wa CHADEMA
Shahidi wa kificho P3: nimekua mfuasi tangu 2021 mpaka sasa bado ni mfuasi
Shahidi wa kificho P3: nimewahi kushiriki matukio baadhi kama kongamano la kutoka Mbalizi mpaka Kabwe tulipoenda kumpokea Mhe. Mbowe mwaka 2024.
Tukio lingine ni kongamano la vijana lakin bahati mbaya au nzuri hatukufanikiwa kwasababu serikali ilizuia.
Shahidi wa kificho P5: tarehe 4 april 2025 nakumbuka kijiweni kwangu kwenye boda boda nilikua nachezea simu yangu nikapata kuona hotuba fupi ambayo Mhe. Tundu Lissu akizungumzia uchaguzi uliopangwa kufanyika 2025.
Shahidi wa kificho P3 : hotuba niliiona youtube.
Shahidi wa kificho P3 : namfahamu Tundu Lissu kupitia mitandao ya kijamii baada ya kuwa nafatilia sana chama cha CHADEMA tangu mwaka 2021.
Katika chama Tundu Lissu ni mwenyekiti wa CHADEMA, baada ya kusikiliza ile hotuba pale kijiweni nikaanza kuwashirikisha wanachama wenzangu wa boda boda na kuanza kuwashawishi wengine wenye mapenzi na CHADEMA kufanya yale mh. Tundu Lissu ameyasema.
Niliwashawishi tuwe kitu kimoja kupambana kuzuia uchaguzi 2025, tulipanga kuzuia uchaguzi kwa namna ya kwamba watu watakaoenda kupiga kura kuwafanyia fujo ikiwepo kupigwa mawe, ushawishi nilikua naufanyia katika kijiwe changu cha pikipiki, baada ya kushawishi wenzangu kuna baadhi waliliridhika na ushawishi wangu na baadhi hawakuridhika.
Shahidi wa kificho P3 : baada ya hapo alitokea mtu mmoja akanipoint kwenye kijiwe na akaniomba tuongee mara moja, nikaenda kumsikiliza na akajitambulisha kuwa. Yeye ni ofisa wa polisi, akaniambia nahitajika twende kituo cha polisi kwa mahojiano yangu mimi na yeye nilivyofika kituo cha polisi wakaniambia nitoe viatu na mkanda na wakaniweka mahabusu.
Wakili: Shahidi P3 baada ya kukaa mahabusu nini kilifuata
Shahidi wa kificho P3 : baada ya muda mchache nikapelekwa kwenye chumba kingine wakaanza kunihoji kwamba nilikuwa naongea nini pale kijiweni, kwanini nilikuwa nahamasisha kufanya uasi.
Wakili: walikuuliza kwa nini unahamasisha uasi gani kama unakumbuka.
Shahidi wa kificho P3: kwanini nahamasisha uasi wa kuzuia uchaguzi wa 2025.
Wakili: Sasa shahidi baada ya maelezo hayo nini kilifuatia.
Shahidi wa kificho P3: waliniambia nitafute mtu wa kunidhamini ili niweze kuendelea na taratibu nyingine.
Wakili: ikawaje.
Shahidi wa kificho P3: nilimpata ndugu yangu akaja kunidhamini.
Wakili: nini kilifuata
Shahidi wa kificho P3: nilipata ndugu yangu akaja kunidhamini. Nikaambiwa niwe naripoti Kila baada ya siku tatu.
Wakili: ulikuwa unaripoti wapi.
Shahidi wa kificho P: nilienda kuripoti Kituo cha Polisi Ilonga.
Wakili: ulivoenda kuripoti ikawaje.
Shahidi wa kificho P3: nikaingia ndani kituoni na kukutana na huyo askari aliyeniandika maelezo toka mwanzo.
Wakili: huyo Askari aliyekuandika maelezo kutoka Mwanzo anaitwa nani kama unakumbuka.
Shahidi wa kificho P3 : namkumbuka kwa jina moja anaitwa Amani.
Wakili: baada ya kukutana na Amani mlifanya nini.
Shahidi wa kificho P3: aliniandika maelezo tena na kuniambia naendelee na utaratibu wa kuripoti.
Wakili: waheshimiwa Majaji wa Mahakama kuu kwa Shahidi huyu ni hayo tu
Part 202 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 200
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi Coplo Vicent.
Mhe. Lissu: waeleze wahesimiwa majaji kama kuna mtu yoyote alishuhudia ukiandiika hayo maelezo
Shahidi Coplo Vicent : hakuna niliandika mm mwenyewe
Mhe. Lissu: uliambiwa na OCS ukamkamate P9 kwamba anahamasisha watu kuchochea na kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025, waeleze waheshimiwa majaji ulimkamata kwa kosa gani?
Shahidi Coplo Vicent: wakati namkamata alikua hafanyi kosa lolote.
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama kwenye maelezo yako umetaja jina la mkuu wa kituo cha polisi Mwanjelwa?
Shahidi Coplo Vicent : hapana
Mhe. Lissu: kwenye maelezo yako umeeleza mahali popote kwamba huyu P9 alifanya makosa katika sehemu mbalimbali na majina yake?
Shahidi Coplo Vicent ; hapana
Mhe. Lissu : naomba kamusi, tuangalie neno “kijiwe” kwasababu umelitaja nataka tujue kijiwe maana yake nini kwa mujibu wa kamusi ya Kiswahili. Sasa jiji la mbeya lina vijiwe vingapi?
Shahidi Coplo Vicent: sifahamu.
Mhe. Lissu: waambie waheshimiwa majaji kama umetaja hivyo vijiwe?
Shahidi Coplo Vicent : sijataja
Mhe. Lissu: tarehe ya P9 aliyofanya makosa
Shahidi Coplo Vicent : ni tarehe 5 april
Mhe. Lissu: eleza kama umeeleza hayo kwenye maelezo yako.
Shahidi Coplo Vicent : anasoma
Mhe. Lissu: kwa akili yako hicho ulichosoma kinaonyesha alifanya makosa lini?
Shahidi Coplo Vicent : Hapana
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji kama kwenye maelezo yako umeeleza huyu P9 alikua anapanga njama na nani kwasababu njama haipangwi na mtu mtu mmoja?
Shahidi Coplo Vicent : sijaeleza
Mhe. Lissu: waeleze majaji kwa ufahamu wako kuna kosa la kuzuia uchaguzi mkuu usifanyike?
Shahidi Coplo Vicent : kosa lipo
Mhe. Lissu: kwa sheria gani au kwasababu wewe ni polisi.
Shahidi Coplo Vicent : mm sijui lkn hapo kosa lipo
Mhe. Lissu: acha ubabaifu nakuonyesha sheria ya uchaguzi wa rais, madiwani na wabunge ya 2024, hii haina sehemu yoyote kama hiyo unachokisema ni kosa, wewe unasemaje?
Shahidi Coplo Vicent : mimi sijui.
Mhe. Lissu : na kwenye sheria ya jinai Penal Code je?
Shahidi Coplo Vicent: Kwenye Penal Code lipo
Mhe. Lissu : waheshimiwa naomba shahidi asome hiyo sheria na atuonyeshe hilo kosa.
Renatus Mkude: shahidi hii sheria ni ya kiingereza sasa utaweza kuona?🤣🤣
Mhe. Lissu: Naomba Penal code yangu tusipotezeane muda kingereza hujui na hilo kosa hutaliona.
Mhe. Lissu : waeleze majaji baada ya kumpeleka P9 kituoni ulisema uliendelea na shughuli zako, waambie. Majaji kama unafahamu huyu P9 hajapelekwa mahakamani mpaka leo
Shahidi Coplo Vicent : sifahamu
Mhe. Lissu: utashangaa nikikwambia kwamba baada ya kukamatwa aligeuzwa kuwa shahidi katika kesi hii
Shahidi Coplo Vicent : siwezi kujua.
Mhe.Lissu: Je unafahamu kama P9 ni shahidi katika kesi hii na utashangaa nikikwambia hakufunguliwa mashitaka yeyote badala yake amegeuzwa shahidi katika kesi hii.
Shahidi Coplo Vicent : sifahamu
Mhe.Lissu: je unafahamu kosa ninaloshitakiwa nalo.
Shahidi Coplo Vicent : ndiyo unashitakiwa kwa kosa la uhaini, kutokana na matendo yako.
Mhe.Lissu: matendo yangu yapi.
Shahidi Coplo Vicent: nayafahamu machache kutokana na kauli zako, ninazifahamu chache.
Mhe.Lissu: mitandaoni kuna kauli zangu nyingi sana, kuna video nyingi mno ni zipi hizo chache unazozifahamu.
Shahidi Coplo Vicent : yaani uchaguzi wa mwaka huu daaah!!!!!
Mhe.Lissu: je umeiswailisha video hiyo ili Majaji waione
Shahidi Coplo Vicent: hapana sijaiwasilisha.
Mhe.Lissu: waheshimiwa Majaji kwa upande wangu sina maswali zaidi.
Mhe.Jaji: upande wa mashitaka re-examination.
Wakili wa Serikali: shahidi eleza onyo katika maelezo huwa inatumikaje.
Shahidi Coplo Vicent : huwa inatumika kumuonya mtuhumiwa.
Wakili: wewe unaruhusiwa kusaini mwenyewe.
Shahidi Coplo Vicent: ndiyo naruhusiwa.
Wakili: ni hayo tu mheshimiwa.
Mhe.Jaji: shahidi unaruhusiwa kuondoka.
Shahidi anavuta pumzi kubwa kisha anaondoka.
Part 201 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 199
Mhe. Lissu anaendelea na Cross examination.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba uwaeleze waheshimiwa Majaji kama niliyoyasoma yanalingana na maelezo yako ya police.
Coplo Vicent: ndiyo yanalingana.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba nikupitishe kwenye Maeneo ambayo nataka nikuhoji.
Mheshimiwa Lissu anamsomea shahidi maeneo anayotaka kumhoji.
Mhe. Lissu: ili niweze kukuhoji sawasawa waeleze waheshimiwa Majaji kama ungependa maelezo yako yapokelewe kama kielelezo.
Coplo Vicent: kwa jinsi ambavyo umenihoji naomba nisahihishe kwanza, naomba nirekebishe.
Mhe.Lissu: bado sijaanza kukuhoji, tutafika huko kubali kwanza maelezo yako yapokelewe.
Coplo Vicent: sawa nakubali yapokelewe kama kielelezo.
Mhe.Jaji: itakuwa D11
Mhe.Lissu: sawa mheshimiwa.
Mhe.Lissu: mheshimiwa Jaji naomba shahidi apewe kielelezo D11
Mhe.Lissu: Sasa shahidi hicho ni kielelezo mahakamani na swali la kwanza katika ushahidi wako Leo umesema wewe ni Askari police na unafanya kazi katika kituo cha Polisi Central Mbeya,
Sasa katika hayo maelezo yako naomba uwaambie waheshimiwa Majaji kama kuna sehemu umeandika kuwa unafanya kazi katika kituo cha police Central Mbeya
Coplo Vicent: hapa hakuna.
Mhe.Lissu: Shahidi swali langu la pili linahusu matukio ya tarehe 5 mwezi wa 4 mwaka jana, katika ushahidi wako unasema uliitwa na Mkuu wa kituo cha Polisi Mwanjelwa na kukuelekeza kwamba ukamkamate P9 kwa kuwa anahamasisha kwenye vijiwe mbalimbali na kuchochea uchaguzi mkuu wa 2025 usifanyike. Nataka nijue kama huo ndiyo ushahidi wako.
Coplo Vicent: bila shaka.
Mhe.Lissu: nataka uangalie kwenye maelezo yako uyasoke kuanzia pale unapoelekezwa ukamkamate P9, kama kuna maneno kwamba P9 alikuwa anahamasisha kwenye vijiwe mbalimbali uchaguzi mkuu usifanyike nataka kujua kama maneno hayo yapo.
Coplo Vicent : yapo.
Mhe.Lissu: naomba usome kuanzia hapo kwenye nakumbuka......
Coplo Vicent anasoma.
Mhe.Lissu: hayo maneno anahamasisha na kuchochea Uchaguzi Mkuu usifanyike hayo maneno yapo?
Coplo Vicent: hiyo haipo.
Mhe.Lissu: ahsante sana
Mhe.Lissu: Sasa shahidi kwenye ushahidi wako umesema baada ya kujitambulisha kwake wewe ni Polisi ulimuonesha kitambulisho chako, na ukaongozana nae hadi kituo cha Polisi Mwanjelwa. Kweli au si kweli.
Coplo Vicent: kweli
Mhe.Lissu: waambie Majaji kama hayo maneno yapo.
Coplo Vicent: Hayapo.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba uwaambie waheshimiwa Majaji ni nani aliyeandika maelezo yako.
Coplo Vicent : niliandika Mwenyewe.
Mhe.Lissu: shahidi waeleze waheshimiwa Majaji kama wakati wa kuandika maelezo huwa kuna sehemu ya onyo.
Coplo Vicent : huwa hakuna onyo.
Mhe.Lissu: hakuna Yale maneno kuwa nitasema ukweli, ukweli mtupu nikisema uongo nishitakiwe.
Coplo Vicent : hyo siyo onyo.
Mhe.Lissu: hiyo huwa ni nini.
Coplo Vicent : huwa ninajiambia nitasema ukweli, najiandika maelezo.
Mhe.Lissu: huo ndo utaratibu wenu Mapolisi, mnajiambia wenyewe.
Mhe.Lissu: unaifahamu PGO.
Coplo Vicent : ndiyo
Mhe.Lissu: shahidi unaifahamu PGO number 236.
Coplo Vicent: siifahamu.
Mhe.Lissu: Mhe.Jaji naomba shahidi apewe PGO
Mhe.Lissu: Shahidi soma PGO 236.
Coplo Vicent : hii PGO ni ya kingereza siwezi kusoma.
Mhe.Lissu: Wambura ameandika kingereza anaamimi nyote mnajua kingereza kwahiyo huwezi kusoma kwa sababu ni kingereza.
Coplo Vicent : kuna ya kiswahili.
Mhe.Lissu: ujue kingereza au usijue swali langu utalijibu. Naomba PGO yangu.
Mhe.Lissu: shahidi kwenye kielelezo D11 pale mwishoni kuna udhibitisho wa majina yako na sahihi yako. Umeyaona hayo maneno
Coplo Vicent: Hayapo hayo maneno.
Mhe.Lissu: Mheshimiwa Jaji naomba shahidi aoneshwe sehemu ya udhibitisho wake kwenye D11, kifungu cha 10.3.C
Coplo Vicent: wapi, hapa mwisho kabisa au.
Mhe.Lissu: kipindi unaandika haya maelezo kulikuwepo na kufungu cha 10.3.C
Coplo Vicent : ndiyo kulikuwepo mwaka Jana.
Mhe.Lissu: ni nani alikushuhudia wakati ukiandika maelezo yako
Coplo Vicent : hakuwepo mtu yeyote
Part 200 itaendelea post inayofuata,
Naomba repost
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 198
Anaingia jamaa mmoja mrefu, kavaa kaundasuti nyeusi anakitambi ila sio mnene wala mwembamba anaingia hapa.
Jaji anauliza Shahidi unaitwa nani?
H937 Detective Vincent
36 umri,
Mkristo,
Anapewa biblia kwa ajili ya kuapa anasema atasema Ukweli, Ukweli mtupu. 😂
Ataongozwa na wakili wa Serikali hapa.
Wakili: anauliza jina na anapoishi?
Coplo Vincent.: Anajitambilisha na anasema anaishi Mbeya.
Wakili: Sehemu gani?
Coplo Vincent : Anasema Mbeya mjini.
Wakili: Unafanya kazi gani?
Coplo Vincent : Police Wilaya ya Mbeya
Tangu mwaka 2012.
Wakili: Umejiunga mwaka gani?
Coplo Vincent.: Anajibu 2012
Mafunzo ya awali ya upolice kule Moshi 30/3/2012 baada ya kuhitimu nilipangiwa Mkoa wa Rukwa.
Wakili: Majukumu yako ya kila siku ni yapi?
Coplo Vincent: kupeleleza kesi kukamata na kutoa ushahidi Mahakamani katika kitengo cha upelelezi nina miaka Miaka 6.
Wakili: Sasa ieleze Mahakama mnamo Tarehe 5/4/2025 ulikua wapi?
Coplo Vincent : Nilikua kituoni Mwanjelwa naendelea na majukumu yangu.
Wakili: Unakumbuka Nini?
Coplo Vincent : Niliitwa na Mkuu wa kituo na kupewa maelelekezo ya kumtafuta P9.
Wakili: Alikua anakabiliwa na nini mpaka uende kumtafuta?
Coplo Vincent : P9 alikua anahamasisha vijiweni uchaguzi 2025 usifanyike hivyo nikaenda kumkamata.
Wakili: Baada ya kupewa maelekezo hayo ulifanyaje?
Coplo Vincent : Mkuu wa kituo alinipatia namba ya simu ya P9, Mkuu wa kituo hizo namba alizipata kupitia msiri wake ambaye alimletea.
Wakili: nini kiliendelea baada ya kupata mawasiliano ya mtu unayetakiwa kumkamata.
Coplo Vincent: baada ya kufuatilia shughuli zake nikagundua kuwa ni fundi umeme, hivyo nikatumia njia ya kujifanya kama mteja ili niweze kumkamata.
Wakili: nini kilifata?
Coplo Vincent: tulikubaliana kukutana maeneo ya kabwe ili niweze kumpeleka eneo la kazi.
Wakili: nini kilifuatia?
Coplo Vincent : baada ya hapo nikawa nimefika Kabwe kwani hapakuwa mbali, kweli nikakutana nae.
Wakili: baada ya kukutana nae nini kilifuatia.
Coplo Vincent : Nilimwambia mimi shida yangu siyo umeme, nikajitambulisha kuwa mimi ni Askari police nikamuonesha kitambulisho changu.
Wakili: baada ya kuonesha kitambulisho nini kilifuata?
Coplo Vincent : Nilimwambia nimekuja kumkamata anakabiliwa na tuhuma za kufanya uchochezi pamoja na kuhamasisha vurugu za kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025.
Wakili: Mwisho wake ulikuwaje.
Coplo Vincent: bahati nzuri alikuwa muelewa, sikutumia nguvu nyingi hakuwa mtu wa vurugu niliongozana nae hadi kituo cha police kati Mbeya then nikaendelea na majukumu yangu.
Wakili wa Serikali Ignas Mwinuka anasema Waheshimiwa Majaji ni hayo tu kwa shahidi huyu.
Jaji anasema karibu Mshitakiwa kwa ajili ya maswali ya Dodoso.
Mhe. Lissu: umesema unaitwa Coplo Vicent ni sawa?
Coplo Vincent : Mimi naitwa coplo H937 vicent.
Mhe. Lissu; ukienda kwa baba yako na mama yako utawaambia unaitwa coplo H937 Coplo Vicent.? 😂
Coplo Vincent: Hapana.
Mhe. Lissu: nasikia wewe ni homeboy wangu.
Coplo Vincent: Ni kweli.
Mhe. Lissu: bila shaka uliandika maelezo yako ya shahidi na ukionyeshwa utayatambua?
Coplo Vincent: ndio.
‘Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji naomba shahidi aonyeshwe maelezo yake.
Mkude: waheshimiwa hatuna pingamizi.
Shahidi Coplo Vincent anaonyeshwa maelezo yake.
Mhe. Lissu: waeleze waheshimiwa majaji kama hayo maelezo ni yako.
Coplo Vincent: ni sahihi ni yangu.
Mhe. Lissu: waheshimiwa nataka ku-impeach credit ya huyu shahidi nataka kuhoji sifa au uaminifu wake, namsoea maelezo yake kisha nitasoma maeneo nayotaka kum-contradict na nitaomba akubali yapokelewe kama kielelezo.
Part 199 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 197
Katuga anasema: Kuna chama kinasema lazima mashahidi wote wa kificho watajulikana, sisi ni rai yetu kwamba ipo siku hata mimi nitakuja kuambiwa nilishawahi kuwa shahidi wa kificho, kwahiyo tunaomba mahakama itolee maamuzi ili kuondoa shida ya kupunguza uaminifu wa mahakama;
Wengine ni mawakili kabisa wanazungumzia hii kesi kwa upotoshaji tena ni wanasheria wakubwa kabisa wanaheshimika katika jamii.
Mhe. Lissu anasimama: waheshimiwa majaji mimi nawaomba msikubali huo mualiko mnaopewa na mawakili wa serikali, malalamiko yao ni malalamiko ya kijinai ambayo hayajafanyika mbele yenu, hamjayaona, hamjayasikia na wala hamjaambiwa ni kitu gani, Hayo mambo yote hayajatokea mbele yenu mahakama ikiwa inaendelea.
Mkiambiwa mtolee maamuzi juu ya mambo hayo mtakua mmefungua mambo yasiyowezekana.
Kama wanahisi kuna jinai waende kwenye mahakama proper wakafungue kesi, kama ni mawakili kuna utaratibu wa kudeal na mawakili wanaokiuka taratibu za kiuwakili.
Kwahiyo mnaalikwa kwenye uwanja ambao hauna rules, sio uwanja wa kisheria.
La mwisho na hii ni hofu yangu wanataka giza katika kesi kubwa kama hii, kwenye kesi ya uhaini hawataki kuwe na mjadala wanazungumzia Umma kitu ambacho hakiwezekani, mnataka kuwafunga, mtafunga nchi nzima na hamtaweza. Ni hayo tu waheshimiwa.
Katuga anasimama: tuliialika mahakama chini ya kifungu 114, sisi tunasisitiza vinavyoendelea ni kutoa uthibitisho wa mashahidi wa kificho na sisi inatupa shida katika kuleta mashahidi wetu, tusipovisema ivi vitu proceedings hazitakuwa sawa.
Kuna vingine hatuvisemi kwanini mashahidi hawaji yeye anaulizia kila siku lakini ni vitu kama hivyo.
Katuga anadai hizi proceedings za kinachondelea Mahakamani zinachapishwa pia mtandaoni sasa hii haiwezi kuwa sawa.😂
Mawakili wa Serikali wanataka kesi iwe Gizani mazima ili Watanzania na Dunia isijue nini kinaendelea kwenye shauri hili.
Kwa kifupi hawa ndugu wmaechanganyikiwa na mambo yanavyokwenda. Wanaona wako uchi kabisa. Kila kitu chao kiko hadharani. Naona hapa wanataka kusema mashahidi wanagoma kuja kwasababu wanaogopa kuwekwa hadharani.
Nafikiri wangekuwa wakweli waseme mashahidi wanaogopa kudhalilishwa hata kama hawaonekani kwenye kile kibox chao. Naona joto la mle kwenye mambao ukichanganya na maswali wanahadisiana huko waliko. 😂😂
Kumbuka hizo discussion Majaji wamesema wanazifanya off record kwanza. Ni kama zinapigwa soga ili kuona ni vitu vya msingi au sio vya msingi. 😂
Majaji wamemaliza kuteta sasa.
Jaji Nduguru anasema amesikia hoja zote anasema siku zote anasisitiza Matumizi ya kifungu 114 kama kunamambo hayako sawaa hawawezi kusubiri mtu aliibue jambo hilo. Wao pia wanaona na watachukua hatua.
Hivyo anaendelea kusisitiza kifungu Cha 114 na kusema tujiepushe na uvunjifu wa kifungu hicho.
Matumizi ya kifungu Cha 114 ni domain ya Mahakama itatumia kifungu hicho endapo itaona kunaulazima wa kukitumia hivyo tuendelee mashahidi.
Wakili wa Serikali anasemaa anasema tuendelee na mashahidi Leo ni shahidi wa wazi wa 12 wa upande wa mashitaka.
Kwa Maneno mengine tukitafsiri kilichosemwa na Majaji ni kwamba wamewaambia Jamhuri acheni umbea. Fanyeni Kesi. Msitufundishe kazi. Tunajua tunachofanya. 😂😂😂
Wamenywea sana hapa.
Ngoja tukomae na huyo Polisi anaekuja muda huu.
Part 198 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba nisaidie kushare ujumbe uende mbali.