Ninawatakia kila la kheri wanafunzi wote 595,816 wa Kidato cha Nne ambao leo mnaanza mtihani wa kuhitimu elimu ya sekondari katika shule za sekondari 5,868 nchini. Idadi hii ya shule inatokana na nyongeza ya shule 305 mpya, ambazo ni mara yake ya kwanza kufanya Mitihani wa Kidato cha Nne. Shule hizi ni matokeo ya kazi tunayoendelea kufanya kuhakikisha kila mtoto wa Tanzania ana uhakika wa kupata elimu bora.
Mwenyezi Mungu Mtukufu aliyewaongoza tangu elimu ya awali hadi leo awajalie utulivu mwifanye na kukamilisha vyema hatua hii muhimu kwenye maisha yenu.
Ninawaombea pia mwendelee kuwa na nidhamu, upendo na bidii katika hatua zinazofuata kwenye maisha yenu. Serikali itaendelea kufanya kila inachoweza kuhakikisha ndoto zenu njema zinapata fursa na nafasi ya kukua na kustawi kwa manufaa yetu sote.