#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 26
Tumerejea baada ya Mapumnziko ya nusu saa.
Anaanza Wakili wa waleta maombi Adv. Emmanuel Ukashu kumuhoji Maswali Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Ukashu: shahidi umewahi kuisikia TLS?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio naifahamu.
Adv. Ukashu: Ili mtu aingie Gerezani inahitajika wewe ndio umruhusu aingie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Ukashu: Ni sahihi ukipewa maelekezo yoyote lazima utekeleze na Kamishna General?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi
Adv. Ukashu: Maelekezo kutoka juu maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni maagizo ya kiutendaji unayopaswa kutekeleza.
Adv. Ukashu: Usipoyatekeleza unaweza kufukuzwa kazi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kwa mujibu wa sheria.
Adv. Ukashu: Unaweza kumbishia Boss wako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Siwezi kufanya hivyo.
Adv. Ukashu: Soma SUPP 4 tar. 12/03/2026 entry no. 8 hebu isome hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela): Huruma Tehejas mfungwa aliyekuja kumtembelea ni mfungwa na shida ya kisheria. Maoni hapakujazwa. Na sahihi hamna.
Adv. Ukashu: Sasa alienda wapi huyu Wakili kama hakuna uliposaini na maoni hukuweka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nilisahau kujaza na naamini hakukataliwa pia.
Watu wanacheka. 😂😂😂😂
Adv. Ukashu: Kwanini usifukuzwe kazi kwa uzembe wa aina hii? Maana haijulikani alikuja kufanya nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nifukuzwe tu kazi kama unaweza kunifukuza. Fanya hivyo ila mimi nimesema nilijisahau.
Adv. Ukashu: Unafahamu kazi ya uwakili ina maadili yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila kazi ina maadili.
Adv. Ukashu: Maadili ya magereza tumeshayaona hapa hujajaza nyaraka na hujui wakili alipoingia alielekea wapi? Sasa tuzungumze maadili ya mawakili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : siyajui mi sio wakili.
Adv. Ukashu: Unaijua Mandela Principle?
Ntamamiro (Bwana Jela): yes
Adv. Ukashu: soma hapa inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Mfungwa atazungumza na wakili wake kuwa atazungumza bila kikwazo.
Adv. Ukashu: Umeitekeleza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inasema nizingatie sheria za ndani pia?
Adv. Ukashu: Sasa tuambie ni kifungu gani cha sheria ya ndani ambacho kiko kinyume na Mandela Principle.
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakipo.
Adv. Ukashu: Nimemaliza. Naomba Wakili Neema aendelee.
Anasimama Wakili Neema Saruni.
Adv. Neema Saruni: Nitakuwa sahihi nikisema mtu anayekuja kumuona mfungwa anapaswa kuwa na sababu ya msingi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi kwa mujibu wa Sheria.
Adv. Neema Saruni : Ulisema mjibu maombi wa nne alikuwa na orodha yake hivyo basi alipotokea hayupo mlimrudisha?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio tulifanya hivyo.
Adv. Neema Saruni : Nitakuwa sahihi nikisema hamkumpatia haki yake ya kusikiliza.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sahihi.
Adv. Neema Saruni: Nilipokuja mimi kumuona Lissu nilikuwa kwenye orodha yake?
Ntamamiro (Bwana Jela): Haukuwepo.
Adv. Neema Saruni : Nilipofika ikawaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): tulienda kumuuliza lissu.
Adv. Neema Saruni : akasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Akaruhusu ukamuone.
Adv. Neema Saruni: Kwanini huyo mwingine mlimrudisha bila kwenda kuuliza Lissu anasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hapo sasa ndio kuna utata.
Watu wanacheka 😂😂😂
Adv. Neema Saruni: Nimemaliza.
Haya wanasimama mawakili wa Serikali, anaanza Wakili wa Serikali anaitwa Wisdom
Wakili wa Serikali Wisdom: Ulitekeleza majukumu yako kwa mujibu wa nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): masharti yapo kwenye sheria ikiwemo PSO.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba asitaje kabisa PSO maana jana haikuwepo na hatukumuuliza. Asiulize. Sect. 156(3) ya Evidence Act iko wazi kuhusu Re- examination.
Jaji: Sasa Wakili wa Serikali Wisdom uko tayari kuendelea na njia hiyo ili tumruhusu Lissu nae aanze kuuliza kwenye PSO.
Wakili wa Serikali Wisdom: Naomba tu niishie hapo. Sitaendelea mbele.
Watu wanacheka 😂😂😂😂
Part 27 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 25
Wakili wa Waleta maombi Edson Kilatu anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Kilatu: Ni sahihi ili tujue maduhu ni muongo anasema alifika Ukonga lakini hakufika kumbe ulipaswa kuleta kitabu cha watu wanaohudhuria ukonga wakifika pale getini wanaandika.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Kilatu: Umeleta?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijaleta.
Adv. Kilatu: unakumbuka kuhusu huwa hamsomi nyaraka anazopelekewa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Adv. Kilatu: umeleta kiapo chochote cha unaowatuma kusimamia kuwa wanasema hatujawahi kusoma nyaraka za Lissu tukitekeleza majukumu yetu.
Ntamamiro (Bwana Jela): nimeleta mimi kwa niaba yao.
Adv. Kilatu: Lissu alipeleka orodha ya mawakili wa kumtembelea?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Kuruhusu watu kumuona sio lazima wawepo kwenye orodha?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio kuna mazingira alikuwa anaomba Lissu mwenyewe.
Adv. Kilatu: Umeyasema mazingira hayo kwenye kiapo chako au kuna siku Lissu aliomba mtu ambae hayupo kwenye orodha ili amuapishe aingie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijasema kwa kiapo changu.
Adv. Kilatu: unajua maana ya retainership ya mawakili kwa mteja uliyoisema kwenye kiapo chako.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui ila uliza swali tu.
Adv. Kilatu: Basi tutarudi hapo kama hujui.
Soma paragraph nyingine hapo umesema shauri hili lilipaswa kuwa judicial review sio la kikatiba?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Una uelewa wowote kuhusu Judicial Review?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina uelewa wa hili.
Adv. Kilatu: Basi sitakuuliza kwenye hilo nikuache.
Sasa nenda kwenye originating summons soma ibara za Katiba zilizotajwa humo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : zipo ibara ya 13 na zingine.
Adv. Kilatu: Asome ibara ya 30 aielewe halafu nimuulize swali.
Jaji: Asome au ajisomee?
Adv. Kilatu: Ajisomeee mwenyewe aelewe halafu nimuulize swali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tayari
Adv. Kilatu: Je ibara hiyo inasema mtu anaweza kuja kwa judicial review mahakamani kupitia ibara hiyo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hapana.
Adv. Kilatu: Soma para 4 ya kiapo chako kuwa ulimkataaa Kisabo kwasababu sio wakili wa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela): lakini baadae lissu alileta ombi maalamu.
Adv. Kilatu: Sasa muambie Jaji hiyo paragraph nyingine uliyosema kulikuwa na ombi maalumu ni paragraph ya ngapi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haipo.
Adv. Kilatu: Sasa ili wakili aingie gerezani ni lazima kuwepo na orodha ya mawakili iliyoandikwa na mfungwa.
Ntamamiro (Bwana Jela): Utaratibu ni kukagua kitambulisho na kumruhusu.
Adv. Kilatu: Sasa kwenye kiapo chako ukimjibu Maduhu unasema kulikuwa hakuna proof of retainership? Hiyo ndio requirement ya sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nafikiri sifahamu.
Adv. Kilatu. Nimemaliza. Mh. Jaji.
Jaji twende mapumnziko kwa nusu saa.
Tukutane hapa baada ya dakika 30.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 24
Anaendelea John Seka
Seka Anamuongelesha anasema unanisikia au hunisikii. Anatumia sauti ndogo sana. Umenisikia?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nakusikia
John Seka: Pale ofisi ya Admission si kuna Meza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ukubwa wa meza zilizopo hapo admission ukoje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sikumbuki.
John Seka: Katika maisha yako uliwahi kumuona wakili na mteja wake gerezani wanaongea?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Huwa wanakaaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wanakaa kutazamana katikati yake kuna meza?
John Seka: Sasa narudi hapo. Kabla ya kesi hii uliwahi mfahamu Nashon Nkungu, Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nimewahi kukutana nao.
John Seka: Ulikutana nao wapi? Katika mazingira yapi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Akija kuongea na mteja wake gerezani.
John Seka: Ulituambia stage za wakili akifika. Anaandika jina nje, kitabu kinaletwa kwako. Unaruhusu. Sasa tuambie unamuona wakati gani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ofisi zote ni zangu.
Jaji: Jibu ni wapi hapo Gerezani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nilikutana nae Kwa Recha.
John Seka: Kumbe hata Kisabo ulimfahamuje?
Ntamamiro (Bwana jela) : hivyo hivyo kumuona akizungumza na mteja.
John Seka: Umewahi kuwaona wakifanya mahojiano?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Umekumbuka wakati Lissu anafanya mahojiano nani na nani anakuwa ndani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wanakuwa nje wote. Lakini wanachungulia kwa mlangoni.
John Seka: Unakumbuka tarehe ipi na ipi ulikuwepo na ipi haukuwepo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Siwezi kukumbuka.
John Seka: Sasa nitakupitisha tarehe moja hadi nyingine?
Jaji: Amesema hakumbuki nafikiri huko muache acha libaki hivyo.
John Seka: Nitakuwa sahihi nikisema wewe hujawahi hudhuria majadiliano kati ya Lissu na mawakili wake?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Mengi yaliyotokana na hayo wewe hukuwa unahusika moja kwa moja zaidi ya mrejesho.
Ntamamiro (Bwana jela): sio lazima feedback
John Seka: wewe hujawahi hudhuria mazungumzo ya Lissu na wanasheria wake. Huwa unapita tu. Unayoyaona.
Ntamamiro (Bwana jela) : nakagua napita.
Jaji: Hebu sikia kati ya wewe na hao akina Recha, Mumbii anaeweza kuelezea?
Ntamamiro (Bwana jela): Ni sahihi.
John Seka: Sasa tutajie majina yake.
Ntamamiro (Bwana jela): Siwakumbuki.
John Seka: Wakati wote maelekezo yako yalikuwa yanafuatwa ukiwaagiza kwenda kusimamia?
Ntamamiro (Bwana jela) : Mimi ni Mkuu wa Gereza sio lazima niambiwe feedback naweza kujua kwa namna nyingine.
John Seka: Kumbe ulijua kuwa mahojiano na Lissu na mawakili wake yamefuata taratibu kupitia mbinu zako zingine.
Ntamamiro (Bwana jela) : ndio
John Seka: Hao waliokufikishia hizo taarifa au hizo mbinu zako zingine umezielezea kwenye kiapo chako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hapana.
John Seka: Paul Kisabo na Nashon Nkungu. Wakiwa kwenye mahojiano kunakuwa na askari wanakaaa kulia na kushoto kwa Lissu na Kwa Nashon na kisabo nyakati zote.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
John Seka: Ulikuwepo muda wote mahojiano yanapofanyika?
Ntamamiro (Bwana jela) : Napata taarifa kupitia vyanzo yangu.
John Seka: Nimemaliza Majaji. Aendeleee Edson Kilatu.
Anasimama Wakili Edson Kilatu
Adv Kilatu: Ukifika ukonga getini kuna kitabu cha ku register magari?
Ntamamiro (Bwana jela): Sahihi
Adv Kilatu: Anayeshughulikia registration zote sio wewe kwenye vitabu vya kuingia vya magari, raia wa kawaida na kitabu cha mawakili?
Ntamamiro (Bwana jela): Ni sahihi
Adv. Kilatu: Ni sahihi hakuna kiapo cha mtu anayesimamia hizo registration pale Ukonga? Hakijaja hapa mahakamani.
Ntamamiro (Bwana jela) : Hakipo.
Adv. Kilatu: Hii Register book uliyoileta hapa Mahakamani SUPP 1,2,3 ni nyaraka ya magereza hakuna sahihi za mawakili mle. Ni nyaraka yenu tu.
Ntamamiro (Bwana jela): sahihi
Part 25 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 23
Wakili wa waleta maombi John Seka anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Andrew Shaban Ntamamiro (Bwana jela)
John Seka: Moja ya sheria ni sheria ya magereza ambae umeisomea na kuibobea?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Kanuni za magereza je?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nazo ni muhimu sana. Zinatumika.
John Seka: Kwenye kanuni hizo unapaswa kutii kanuni ya 13 ya uendeshaji wa kanuni za Magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ibara ya 29(1) inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Kila mtu anayo haki ya msingi ya kufaidi haki za binadamu kama zilivyofafanuliwa ibara ya 12 hadi 28 ya Katiba hii.
John Seka: Ni nani na nani wana haki ya kufaidi haki mbalimbali?
Ntamamiro (Bwana jela) : Watu wote.
John Seka: Hata wewe?
Ntamamiro (Bwana jela) : hata mimi.
John Seka: Hata Tundu Lissu:
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Lissu.
John Seka: Hata Kisabo?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Kisabo
John Seka: Hata Maduhu na Nashon
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Maduhu
John Seka: Nashon Je?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Nashon.
Watu wanacheka. Wanamuona zamwamwa sijui 😂😂😂
John Seka: Haya rudi ibara ya12 sasa kule.
John Seka: soma ibara 29(2) na useme inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : kila mtu ana haki ya kupata hifadhi sawa chini ya sheria.
John Seka: Hadi Lissu akiwa mikononi mwako Ukonga?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sahihi
John Seka: Nenda Kanuni ya 13 ya kanuni za Magereza na utuambie miaka 31 ya uzoefu wako ni lini uliifahamu kanuni hii?
Ntamamiro (Bwana jela) : Tangu nilipoanza Kazi.
John Seka: Isome kwanza.
Ntamamiro (Bwana jela) : mfungwa atapewa haki ya kuongea na wakili wake kwa faragha lakini awe anaonekana lakini sio kuwasikiliza.
John Seka: Umeielewa kweli hicho kifungu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio mfungwa atapewa nafasi ya kuongea na wakili wake na kufanyika kwa kuona lakini sio kusikiliza.
John Seka: Kuna haki ya mfungwa na kuna haki ya mshauri wa kisheria kwenye kanuni hiyo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Haki ya mfungwa kusaidiwa kupewa nafasi ya kuongea na mshauri wake wa kisheria yaani Wakili.
Ntamamiro (Bwana jela): Ndio
John Seka: haki ya pili ni ya mawakili kupata fursa ya kuongea na mfungwa kwa faragha bila ya kusikilizwa ni kutazamwa tu.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Hii haki huwa unasomewa au ni uzoefu? Hii kanuni ya 13.
Ntamamiro (Bwana jela): Sijaelewa swali.
Seka: ili uwe na ujuzi huo wa kutazama bila kusikiliza kuna chuo kinachofundisha? Au ni uzoefu wa kazi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Katika uzoefu wa kazi unasema hapa natazama na sisikilizi.
John Seka: Kwahiyo utekelezaji wa jambo hili unategemea mtu na mtu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hakuna standard zilizowekwa.
John Seka: Kwenye nyaraka zako na maelezo yako ulikuwa unasema simamia? Maana yake ulikuwa unasema simamia lakini wasisikilize.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ukubwa wa Chumba cha Ofisi yako ukoje?
Ntamamiro (Bwana jela) : wakutosha tu.
John Seka: Huwezi kukadiria?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
Jaji: Ofisi yako hujui ina ukubwa gani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wakutosha.
Jaji: Tunatosha wote humu ndani tukija ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hamuwezi kuingia.
Jaji: Bado unasema ni ukubwa wa kutosha?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio
Jaji: Haya jibu swali sasa.
Anasimama Nalindwa Sect. 93 ya Prison Act inasema ramani ya gereza isitolewe. Ukubwa wa hizo ofisi ni hatari.
Jaji Mruma: Hakuna ramani ya gereza wala kifungu hakisemi hivyo. Shahidi jibu swali tunataka sana kujua ukubwa wa ofisi yako ni jambo muhimu sana.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni ofisi iko umbali kutoka hapa nilipo hadi hapo kwako.
John Seka: Sasa ofisi yako ya kaimu wako Recha ni ofisi ya nani kubwa?
Ntamamiro (Bwana jela): Yakwangu ndio kubwa.
Part 24 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Leo July 23, 2026
Jana tuliishia part 21 so leo tunaendelea na-;
Part 22
Majaji wameingia.
Mawakili wapande zote mbili wapo na Mhe. Lissu nae yupo.
Karani anasoma maombi hapa.
Leo tunaendelea na Maswali ya Dodoso kwa Shahidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga ambae Andrew Shabani Ntamamiro (Bwana Jela)
Jaji anauliza kama pande zote ziko tayari. Wanakiri wako tayari.
Jaji sasa na nyie watu wa TLS ninawaruhusu mtapata nafasi ya ku cross.
Anaanza John Seka Wakili wa Waleta maombi.
John Seka : Umekuja kwa niaba ya Gereza la Ukonga
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Una muwakilisha pia kamishna wa magereza Tanzania.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Unamuwakilisha pia Mwanasheria mkuu wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
John Seka: Wameona unafaa kabisa kuwawakilisha wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Unafahamu Katiba ya Tanzania na haki inazotoa zile za Binadamu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Soma ibara 13 inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Watu wote ni sawa mbele ya sheria
John Seka: Watu hao ni pamoja na Lissu hivi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Jaji mbona hatumsikii.
John Seka: Afande tumia MIC halafu tumia ile sauti yako ya kijeshi.
John Seka: Jeshi la magereza lina wajibu wa kulinda raia pia?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Jeshi la Magereza ni miongoni mwa vyombo vya serikali vinavyopaswa kulinda haki za binadamu
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Pia haki za mawakili zinatakiwa kulindwa na kuamuliwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Msimamizi wa gereza za Ukonga wewe ndio msimamizi mkuu wa haki hizo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Wajibu huo wa Kikatiba umeutekeleza umeutekeleza kipindi chochote ambacho sisi tunakilalamikia hapa mahakamani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Kifungu cha 13(6)(a) inasema kuhusu haki ya kusikilizwa unafahamu?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio.
John Seka: Kumbe kwa mujibu wa Katiba hii unapaswa kutoa fursa ya kumsikiliza mtu kabla ya kufanya maamuzi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Wakati unatekeleza majukumu yako, Bwana Tundu Lissu alikuwa na haki ya kusikilizwa kwa ukamilifu?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: je hawa waleta maombi watatu walikuwa na haki hiyi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Ibara ya 16 inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Utaratibu wa sheria utawekwa kuhusu hali ya mtu ya faragha na mambo yake ya faragha bila kuathiri sheria.
John Seka: Kwa mujibu wa ibara hiyo mamlaka mbalimbali zinazoweza kuingilia faragha ya mtu kwa kufuata taratibu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Je mawasiliano binafsi ya mtu ni faragha pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Wakati wote wakati mtu atamnyima mfungwa haki ya faragha anajua kama anaingilia na kuvunja ibara ya 16?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Je wakati unashugjulika na Tundu Lissu ulijua ibara hii ipo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nimetekeleza hilo.
John Seka: Ibara ya 22(1) ya Katiba ya Tanzania inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kila mtu ana haki ya kufanya kazi.
John Seka: Wewe kazi yako unayoifanya ni haki yako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Kumbe na Mawakili pia wana haki ya kufanya kazi yao vilevile hadi ndani ya Magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Na mawakili hawa walalamikaji kuja ukonga ni kuja kazini kwao pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Soma ibara ua 26(1) inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila mtu ana wajibu wa kufuata sheria
John Seka: Kila mtu maana yake hadi wewe? Au wewe haupo kwenye kila mti.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hadi mimi.
John Seka: Una wajibu wa kuheshimu sheria za nchi kumbe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Part 23 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Leo July 22, 2026
Jana tuliishia part 10 so leo tunaendelea na
Part 11.
Leo tunaendelea na Andrew Shabani Ntamamiro ambae ni Mkuu wa Gereza yaani Bwana Jela.
Mhe. Lissu: Wewe ndio Mkuu wa Gereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu : una cheo cha ACP?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni Kweli
Mhe. Lissu: Unawajibika kufuata sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Ni jukumu lako wewe na maafisa wengine mnatekeleza majukumu yenu kwa mujibu wa sheria ya magereza na kanuni zake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Unaifahamu vizuri sheria ya Magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Unaifahamu.
Mhe. Lissu: Yote niliyokuuliza ni maswala ambayo yapo katika sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Yote niliyokuuliza yapo kwenye kifungu cha nane cha sheria ya magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Anaguna
Mhe. Lissu: Sikutegei jibu swali au omba sheria usome kifungu cha 8.
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: kuna kanuni za mwaka 1968 na pia kuna PSO yaani Prison Standing Orders?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Naifahamu.
Mhe. Lissu: Ni ya mwaka gani? Tumeitafuta hatuipati sisi. Unaweza kuniazima?
Watu wanacheka 😂😂😂
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hapa sina ila naifahamu.
Jaji: Ofisini unayo hiyo PSO?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ninayo ndio.
Jaji: Itasaidia sana ukituletea na ukamletea Lissu pia aitumie.
Mhe. Lissu: Nawashukuru sana majaji nataka kushughulika nae kupitia hiyo sheria.
Mhe. Lissu: Sasa hizo PSO zimetungwa na kamishna wa magereza na kanuni za usimamizi wa magereza zimetungwa na waziri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Na PSO zinatungwa na kamishna wa magereza baada ya ruhusa ya waziri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijui
Mhe. Lissu: Sasa shika sheria soma section 5(2) Prison Service
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kumbe kweli. Inasema hivyo ndio.
Mhe. Lissu: Angalia kifungu cha 105 cha Sheria hiyo ya magereza na kinasema waziri amepewa mamlaka hayo kwa mujibu wa sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli nimeona.
Mhe. Lissu: Yapi ni mamlaka ya kamishna mkuu wa magereza kwa mujibu wa sheria hiyo? Soma ile 5(2)
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nimeona.
Mhe. Lissu: Hayo mamlaka ya Kamishna mkuu ya kutunga PSO na Circulars. Je yanahusu maafisa wa magereza peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yuko kimya.
Mhe.Lissu: jibu swali sasa.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Soma sasa hicho kifungu
Ntamamiro (Bwana Jela) : anakisoma kwa sauti.
Mhe. Lissu: Hiyo ni 5(2) kweli?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hii ni 5(1)
Mhe. Lissu: Sasa nimesema ni 5(2) afande wangu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Naomba tuanze na 5(1)
Mhe. Lissu: Kinahusu nani na nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : wafungwa na maaskari.
Mhe. Lissu: Wambie majaji kuwa neno Prisons linajumuisha na wafungwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Kifungu kinasema taratibu zinaongoza Prison and officers?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Kama ni hivyo kwanini Prisons inajumuisha hadi Prisoners na officers kwanini kifungu kitaje sasa hao Prison Officers?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio mtaalamu wa sheria.
Mhe. Lissu: Mtu pekee mwenye mamlaka ya kutunga kanuni ni waziri peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio mtaalamu wa sheria ni mtekelezaji tu.
Jaji: Shahidi umeelewa lengo la swali unaulizwa ili atake kujua unatekeleza sheria ambazo unajua zimetungwa na nani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Aniulize tena.
Mhe. Lissu: Ni kweli kanuni zinazohusu wafungwa mwenye mamlaka ya kuzitunga ni Waziri peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sifahamu.
Mhe. Lissu: Soma kifungu 105(1)(j) kuhusu kusearch wafungwa, askari ni waziri ndio anayetunga.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Mhe. Lissu: Soma.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Basi ni kweli.
Part 12 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 230
Anaendelea Mhe. Lissu.
Waheshimiwa Majaji naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo, maombi haya yameletwa kwa lengo moja tu kurefusha mashauri na kuchelewesha kesi ya msingi ili mjibu maombi aendelee kukaa Ukonga gerezani.
Leo ni siku ya 139 kesi haifanyiki na mimi nakaa Gerezani I'm completely innocent but I'm in prison kwa mwaka mmoja na miezi mitatu.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania article 59.b.4 inazungumzia mamlaka ya DPP kutokuchekewesha muenendo wa Mahakama.
Kuzuia Mahakama kuu kuendelea na kesi kwa siku 139 kwa kuleta maombi ambayo wanayajua hayana msingi wowote, kama hii ni kutenda haki then inabidi tutafute tafsiri nyingine ya neno kutenda haki.
Mamlaka ya DPP ni kuwezesha uamuzi wa haki, wa haraka na usiokuwa wa gharama kubwa.
Niko Mahabusu muda wote huo je hiyo ni haki? DPP na Mawakili wake wamepuuza mamlaka ya kikatiba ya DPP kwa maneno yao wenyewe walishabakiza shahidi mmoja lakini haijaendelea kwa siku 139 kwa sababu ya maombi haya.
Mhe. Lissu anasema ombi langu siyo tu Mahakama hii iyakatae maombi hayo siyo tu hilo, maombi yangu Mahakama ya rufani ina mamlaka ya kutoa amri ambazo zingetolewa na Mahakama kuu.
Kwa kutumia kifungu cha 367 cha kutaka mleta maombi anilipe fidia kwa kunifanye nikae gerezani kwa siku 139 bila kesi kuendelea kwa sababu ya maombi yake.
Yakataeni haya maombi na muamuru DPP anlilipe fidia kwa usumbufu wote alionifanyia.
Mhe. Lissu anasema ni hayo tu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya rufani.
Anasimama Wakili wa Serikali Katuga.
Anasema tumeleta maombi yetu na tumeiomba Mahakama hii tukufu kwamba tumenyimwa haki ya kusikilizwa kwenye huo ushaidi tunaoomba uongezwe, ulikataliwa kabla ya kufika katika hiyo mahakama.
Mjibu maombi ameialika Mahakama hii kwenye proceedings kuanzia pg 391 akizungumzia submission ya uhalali wa notice yetu, tulipata nafasi ya kusikilizwa kuhusiana na notice yetu siyo nafasi ya kusikilizwa kuhusiana na huo ushahidi.
Hatueleweki harafu tunaambiwa tumefanya clever drafting, ushahidi umekataliwa kabla ya kuingizwa, tulisikilizwa kwenye notice tu.
Mjibu maombi anaposema tulipewa haki ya kusikilizwa hakutuelewa kwenye angle gani. Kuirejesha Mahakama hii katika kifungu cha 308 anasema ni kuomba rufaa kwa Mahakama hii sisi tulikuwa tunaonesha walichokifanya na kilichotakiwa kufanyika.
Katunga anaendelea kusema
Sisi hatujaleta maombi haya kuchelewesha kesi tumekuja hapa kuiomba Mahakama iwese kutafsiri Sheria. Kifungu cha 367 kinatumika pale Mahakama inapokuwa imesikiliza kesi na kuona kwamba kesi ni ya kutengenezwa.
Kwa mujibu wa Sheria tunasema maombi yetu ni ya muhimu tunaomba yakubaliwe na yatazamwe na kuita hizo proceedings kuangalia kile ambacho tunakilalamikia.
Jaji anasema basi baada ya kusikiliza pingamizi la awali pamoja na maombi haya tutakwenda kuamua kwanza kuhusu pingamizi la awali kama tutakuwa tumekubali basi itaishia hapo kama pingamizi litakataliwa basi tutaendelea.
Tutawajulisha tarehe ya uamuzi.
Inapigwa Court ya kinyonge ni kama jamaa mchana umepita kama upepo.
Nawatakia Ijumaa njema.
Julai 7, 2026 tukutune barabarani, usihau kubena bango lako lenye ujumbe wa madai yetu ya msingi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 229
Anasimama Mhe. Lissu.
Anasema baada ya kusikiliza hoja za Wakili wa mleta maombi naomba nianze kwa kunukuu maneno ambayo Mahakama hii iliyasema kwenye kesi ya Commissioner General of TRA Criminal case namba 62/2022 pale ambapo maombi ya mdaawa yamezuiliwa na sheria, hawezi kufanya drafting ya kuhadaa Mahakama.
Wanasema uamuzi ulifanyika bila wao kusikilizwa, mgogoro ulianza 19 February 2026 ukurasa 391 wa record, Ugomvi ambao umetuleta hapa ulianza siku Tano kabla ya maamuzi ya Mahakama.
Wakili wa Serikali mkuu Renatus Mkude alisema "waheshimiwa Majaji tuko tayari kuendelea na mashahidi 3 lakini kabla ya kuendelea tuna notice of additional substance of evidence, ambayo imejazwa electronically siku ya Jana"
Katika ukurasa wa 392 Mahakama ikaamua kuwa tuendelee na mashaidi kwanza baadae tutarudi kwenye hoja za notice.
February 20, 2026 ukiangalia ukurasa wa 405-419 utayaona maneno niliyoyasema.
Mahakama ikaamua tumesikiliza sehemu zote kesi hii anahairishwa hadi jumatatu ilikuwa 23 February 2026 kuanzia ukurasa 420 unaonesha hayo.
Mkude akasema wako tayari kuendelea na Katuga akafanya submission in chief pg 421, 423 Katuga akajibu PO, nikafanya rijoinder, pg 428 kuna ruling of the court.
Baada ya submission ya Renatus, submission in chief ya Katuga, rejoinder yangu na reexamination in chief ndipo Mahakama ilitoa uamuzi.
Kwa record hiyo yote nguvu ya kusema hawakusikilizwa wanaitoa wapi?
Kwasababu ya maombi haya leo ni siku ya 139 kesi haiendelei kwa sababu ya uongo wao kwamba hawakusikilizwa.
Haki ya kusikilizwa ni haki ya kikatiba ni kweli sasa kwa ushaidi huu wanawezaje wakasema hawakusikilizwa?
Mmemsikia Wakili Katuga akisema Mahakama ilikosea ilipaswa iangalie reasonablity ya hiyo notice, ipokee ushaidi, iangalie competence kisha iamue.
This is an appeal under 6.3 wanayoitaja, it's only clever drafting inayolenga kuiadaa Mahakama.
Iangalie TRA vs New Musoma textile industry kwenye orodha yangu ni kesi namba 7 hawaruhusiwi kuleta malalamiko kuhusiana na hiyo notice kwenye Mahakama hii. Kifungu 6.3 cha AJA mamlaka ya Mahakama hii siyo hiyo wanayoiomba wao.
Ukurasa wa 21 unaonesha mjadala mpana wa ninachokisema sasa na inamaliza huu mjadala, hamuwezi kuanza kuangalia hiki kilicholetwa ni kitu gani mnapaswa kutazama je huu uamuzi ni legal.
Wanasema hawakusikilizwa mnaangalia kwenye record, Je ni kweli hawa watu hawakusikilizwa, hamuendi kwenye huu usikilizwaji ulikuwaje, Mahakama hii haiangalii mambo superficial.
Waheshimiwa Majaji mleta maombi alisikilizwa hivyo ruling ya mahakama ni legal, imeandikwa na Majaji wenye mamlaka baada ya kusikiliza pande zote hata kama hauwafurahishi wanapaswa kukubaliana nao.
Waheshimiwa Majaji waleta maombi hawana hoja yeyote ya maana on the basis of this record. Section 308 ya CPA imetajwa kwa lengo la kuwaalika mtengue kilichoamuliwa na Mahakama kuu nawaombeni msiende huko.
Nitasema kwa kifupi sana juu ya section 308 ya CPA na nini Mahakama ilisema inakataa kuongezwa kwa ushahidi mpya inadeal na Shaidi mpya tu.
Inazungumzia ni katika mazingira gani shaidi ambaye hakutajwa kwenye commital proceedings anaweza kuongeza kwenye trial, mleta maombi hapa analeta ushahidi mpya wa shaidi ambaye ametajwa kwenye commital na siyo shaidi mpya kama Sheria inavyotaka.
Anaendelea Mhe. Lissu
Kwenye uamuzi huu hakuna sehemu ambayo Mahakama imesema ushaidi huo haufai bali imesema ni ushahidi mpya na haufai kisheria.
Hii clever drafting in order to avoid the legal power, kama wanataka kupinga uamuzi huo wasubiri kesi iishe kisha wakapinge uamuzi huo.
Part 230 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 228
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa Waheshimiwa Majaji naomba nimalizie nisiwachoshe.
Hoja yangu inahusika na maamuzi ambayo hayamalizi kesi, kesi bado ipo na tutakapoenda kwenye substance nitawaoneshe Majaji kwenye hicho walichokileta wao wenyewe ambavyo kesi bado inatusubiri.
Kwa bahati mbaya wametupotezea muda sana hivyo nawaombeni Waheshimiwa Majaji mkatae maombi hayo.
Anasimama Katuga anasema Waheshimiwa Majaji maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii na kanuni ya 65 kanuni ndogo ya 1. Waheshimiwa Majaji ukisoma notice yetu inataja kifungu cha 6 cha Sheria ya mamlaka ya rufaa ya mahakama hii, Waheshimiwa Majaji lalamiko la mjibu maombi lisingekuwepo kama angeipitia kanuni ya 48.
Jaji anamwambia Katuga ulishamaliza usilete jambo jipya nenda moja kwa moja kwenye maombi.
Katuga anaendelea
Waheshimiwa Majaji maombi yetu yamejikita kuiomba Mahakama hii tukufu iweze kuangalia uhalali na usawa wa muenendo wa shauri lililoko mbele ya Mahakama kuu.
Maombi haya yametokana na mzizi wa upande wa Jamhuri kuleta notice ya kuongeza ushaidi ambao haukusomwa wakati wa commital na upande wa Jamhuri ulifanya vile kuendana na kifungu cha 308 cha CPA, kifungu hiki Waheshimiwa Majaji kinaweka zuio kwamba hakutakuwa na ushahidi ambao utaongezwa Mahakamani kama ushahidi huo haukusomwa hautaruhusiwa kuongezwa unless upande wa Jamhuri utatoa notice ya kuongeza ushaidi huo.
Tunatakiwa kutoa notice ili mshitakiwa asikutane nayo by surprise, kifungu hicho kinaitaka Mahakama wakati inafanya reasonablity ya notice ifanye vitu gani.
Mahakama wakati inatakiwa kutambua reasonablity ya notice inapaswa kuzingatia kifungu cha 308 kifungu kidogo cha 3 inatakiwa kuuchambua ushaidi wenyewe.
Naona Job Mrema ni kama kambonyeza Katuga ameinama sijui wanaongea nini na wenzake,
Halafu sio mara moja kila baada ya sentence kadhaa vikao vinakuwa vingi.😤
Anaendelea Katunga
Mahakama ilienda kuangalia huo ushahidi katika ukurasa wa 431 wa muenendo wa Mahakama kuu na kuita ni ushaidi mpya umekusanywa baadae na hivyo wamekataa.
Ushaidi unakatakiwa pale ambapo unakuwa umefikishwa Mahakamani baada ya kuwa umepimwa ndipo Mahakama inaamua uingie au usiingie, upokelewe au usipokelewe lakini hauwezi kuamuliwa wakati unakuwa introduced.
Kifungu cha 308 kimetoa nini Mahakama inafanya, ndo maana kwenye maombi yetu tunasema tumenyimwa haki ya kusikilizwa in relation na huo ushahidi.
Haki ya kusikilizwa ni haki ya kikatiba, maana ya hii haki ya kusikilizwa ni kumpa mtu haki ya kumsikiliza full kwa utimamu ndo maana Mahakama ina vitu vitatu vya kupima.
Ushaidi unapimwa unapokuwa umefika Mahakamani, kusema ushaidi ni mpya usiletwe ni kuukataa ushaidi kabla hata haujafika Mahakamani.
Mahakama hata haikuusikia ushaidi lakini ikaenda kusema ushaidi huo ni irrelevant.
Utaratibu wa proceeding ulikuwa umekiukwa na ukiukaji ambao unaenda kwenye shauri yenyewe na ndiyo maana upande wa Jamhuri tukaona kwa busara zenu muangalie hizo proceedings hatuwezi kuendelea na hizo illegalities.
Anaendelea Katuga
Tunataka Mahakama iangalie ni kwa namna gani kwa muda gani ushaidi unaangaliwa na kuwekwa kama ushaidi.
Kwenye kifungu hakuna sehemu tuliposema Mahakama iende ikaupime huo ushahidi ilikuwa ni notice tu, ushaidi kuja Mahakamani na kufukuzwa kabla ya kusikilizwa huko ni kutunyima haki.
Ni vigumu kupima ushaidi ambao hauko hata mahakamani.
Ukurasa wa 431 wa proceedings naomba muuangalie waheshimiwa Majaji, jambo hili lilikiuka taratibu za mienendo ya proceedings.
Waheshimiwa Majaji wa Mahakama ya rufani tunaomba maombi yetu yaangaliwe na yakubaliwe.
Waheshimiwa Majaji ya kwetu ni hayo tu.
Part 229 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 227
Anasimama Wakili wa Serikali Mrema
Anasema naomba kuongeza kidogo kwenye mawasilisho yaliyofanywa na Wakili mkuu wa Serikali Katuga, naomba kuongeza yafuatayo.
Waheshimiwa Majaji hii obligation inayowasilishwa mbele ya mahakama ya rufani lazima iwe na uwezo wa kuondoa shauri hilo lililoko mbele ya Mahakama hii, nikirejea shauri alilolilejea, shauri la DPP dhidi ya Mohammed Ussi naomba kuialika Mahakama hii kwenye kifungu cha 5 kifungu kidogo cha 2.
Mleta maombi amefanya reference kwa kifungu ambacho kimepitwa na wakati it's not applicable.
Kifungu hiki kukihusianisha na kesi ya Mohammed Ussi na kukileta kwenye Sheria ya sasa it's not applicable.
Kifungu cha 8 kinazungumzia mashauri ya madai, swali la kujiuliza ni je shauri hili ni la madai.
Jaji anawasha kipaza anauliza. Katuga ulisema Mrema anaongezea sasa mbona anarudia yaleyale.
Watu wanacheka😂😂😂😂😂
Jaji anamwambia Mrema aendelee ila asirudie mambo ambayo tayari Katuga ameongea.
Mrema anasimama anasema waheshimiwa Majaji ni hayo tu.
Watu wanacheka maana ni kama alichosema Jaji kimemto kabisa Mrema kwenye mood.😂😂😂😂
Anasimama Mhe. Lissu
Waheshimiwa Majaji naomba mniruhusu nijibu hoja za waleta moambi.
Wanacholalamikia siyo order wanalalakikia findings.
Waheshimiwa Majaji wanacholalamikia wamekileta wenyewe kwenye hati yao ya maombi hicho kiko kati ya ukurasa wa 428-431 wanalalamikia rulling, uamuzi.
Uamuzi wanaoulalamikia unajadili ushaidi wanaotaka kuuingiza, na Mahakama ikajadili ushaidi huo kwamba ni kinyume na Sheria hautaingizwa.
Kama wasingekuwa wanalalamikia hii ruling wasingeileta mbele ya Mahakama yako. Finding is not similar to a decision.
Waheshimiwa tuasume Mawakili hawa wako sahihi finding is similar to decision, tuangalie Mahakama inasema nini juu ya aina hii ya ushaidi, Mahakama ikasema ni kinyume na Sheria hauruhusiwi kuingia.
Mawakili waleta maombi wameleta kesi muhimu sana kesi ya Peter Michael Madeleka, kuna mahali katika kesi hiyo ambako Mawakili wa Serikali wamepakimbia kama ukoma, ukurasa wa 9 Mahakama ilisema hivi kuhusiana na hicho kifungu hayampi mamlaka ya kuimove Mahakama.
Mhe. Lissu anawambia Mawakili wa Serikali ahsanteni sana kwa kuleta kesi ya Madeleka.
Watu wanacheka 😂😂😂😂 maana akina Katuga wameleta kesi ambayo badala ya kuwasaidia kumkandamiza Mhe. Lissu yenyewe ndo imekuwa msaada kwa Mhe. Lissu.
Anaendelea Mhe. Lissu
Mamlaka ya Mahakama ya rufani kuitisha Suo moto ni mamlaka yake yenyewe haiwezi kuwa moved na waleta maombi.
Kama Mahakama haijaiona yenyewe haiwezi kuletewa maombi.
Wanasema nisiwafundishe lakini mkiangalia record waliandika barua, walileta maombi kisha wakaandika barua wanataka kuimove Mahakama.
Katuga amesema maombi yao wameyaleta under 6.3, Waheshimiwa Majaji nawaomba muangalie maombi hayo kama kuna sehemu wametaja kifungu hicho. In their notice of motion hakuna sehemu wametaja ni 6 ipi kati ya vifungu 6 vya Sheria hiyo hawawezi kuja hapa kuzungumza kitu tofauti na maombi yanavyozungumza.
Nirudi kwenye hoja ya Job Mrema, mmealikwa Majaji kukubaliana na hoja kwamba Sheria imeshabadilika ni vifungu tofauti, Waheshimiwa Majaji mimi nina revised Act of 2023 inasema section 5 haina marekebisho ya kabla ya 2023 kwa hiyo hii hoja ya kwamba kuna Sheria imebadilika ni vitu tofauti ni hoja ambayo nachelea kusema haina mashiko.
Waheshimiwa Majaji wakili ametaja rule 48.1,
Waheshimiwa Majaji inazungumzia PO must have a capacity to dispose of application na kwa maana hiyo anasema pingamizi langu halina uwezo wa kumaliza madai,
Je kwenye hoja ya kwangu hii kwamba maombi haya hauruhusiwi kwasababu hayana uwezo wa kuyafuta maombi kama inasema imeletwa chini ya kifungu cha 8.2.d? hakuna hoja hapo.
Part 228 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 226
Anaendelea Mhe. Lissu.
Waheshimiwa Majaji uamuzi uliotolewa na Mahakama ya rufani katika kesi ya Katibu Mkuu wa CHADEMA na bodi ya wadhamini wa CHADEMA vs Saidi Issa Mohammed na wenzake inasema kwamba kama mdaawa (Mleta maombi) analeta maombi mwenyewe ni yale yaliyoko kifungu cha 6 kifungu kidogo cha e, maombi mengine ni Mahakama yenyewe ndiyo inaamua bila kusukumwa na yeyote au kuletewa maombi yenye hati ya kiapo.
Waheshimiwa Majaji kwa vyovyote vile maombi hayo hayako halali mbele ya mahakama hii kwani hayakuletwa katika utaratibu wa kisheria kwani Mahakama hii haijaamua maombi haya yaje yenyewe Suo moto kwa hiyo Mahakama isikubali kusikiliza maombi hayo kwasababu ambazo nimezisema.
Anaendelea Mhe. Lissu
Sasa waheshimiwa Majaji sijui kama mnaniruhusi niendelee au wajibu kwanza.
Jaji anasema Jamhuri wajibu kwanza PO kisha tutaendelea.
Anasimama Wakili Katuga anasema Waheshimiwa Majaji tukirejea mapingamizi yake ya awali yameletwa chini ya kifunga cha 8.2.d hiki ni kifungu mahususi kwa mashauri ya madai.
kifungu hiki kilikopwa kikatumika kwenye madai kwenye mashauri ya rufaa, hata kama Mahakama yenu tukufu kwa rejea hizo za Mahakama hii ikakikopa kitumike kwenye maombi yetu haya bado tunasema kwamba maombi yetu yako sahihi mbele ya mahakama hii tukufu tofauti na kile ambacho mjibu maombi amekileta kama pingamizi la awali.
Maombi yetu yameletwa chini ya kifungu cha 6 specifically kifungu kidogo cha 3 cha Sheria ya mamlaka ya Mahakama. Kanuni ya 65 na kanuni ya 45 ya kanuni za Mahakama ya Rufani inasuport maombi yetu.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa Majaji ukiyasoma maombi yetu kwenye notice of motion hakuna sehemu yeyote tunayoiomba Mahakama hii tukufu ipitie order ya Mahakama au uamuzi wa Mahakama, pale mwisho tunasema Mahakama idiscuss kukataa ushahidi hatujazungumzia kukataa notice, sisi tunazungumzia kuuchambua na kuukataa ushahidi.
Hakuna sehemu kwenye maombi haya tunalalamikia order, Mahakama yenu itaona kwamba pingamizi la mjibu maombi limekuwa mislead hakuconsue sawasawa maombi yetu.
Pale ambapo neno or litatumika kwenye Sheria yeyote maana yake maneno haya hayako similar yanatumika tofauti, Waheshimiwa Majaji nimewarejesha humu muweze kukitafsiri kifungu cha sita. Haya maneno yanatakiwa yatafisiriwe tofauti hayaendi pamoja ama hayategemeani, inaweza kuwa kimoja wapo kati ya haya.
Kama mahakama yenu imekikopa kifungu cha 8.2.d kinazungumzia katazo la decision or order ndo hauwezi kuziombea appeal or revision.
Sasa tunapata wapi nguvu za kuleta pingamizi kwa tafsiri hiyo tunaiomba Mahakama hii ikaangalie maana ya maneno haya.
Waheshimiwa nawarejesha kwenye kamusi kwa sababu nayo ni kati ya vitu vinavyopaswa kutumika kutafsiri Sheria. Katika ukurasa wa 129 kamusi inadefine order ni nini?
Kwenye application yetu hakuna sehemu tumeombea decision or order, kwenye kifungu cha 8 hata kama kimekopwa hakiwezi kucocer maombi yetu.
Mahakama yenu ilishawahi kuiamulia hili kwenye kifungu 394 cha CPA, katika kesi ya Peter Michael Madeleka dhidi ya jamhuri.
Kutaja kitu fulani means exclusion ya kitu kingine, kitendo cha kifungu cha 8 kutaja findings and order means haijatuzuia kwa maana hiyo findings hapa haijazuiwa kwa maana hiyo tunachotaka kuiambia Mahakama yako ni kwamba ule ushahidi ulikataliwa kabla ya wakati wake.
Anaendelea Wakili wa Serikali Katuga
Waheshimiwa naomba niishie hapo kwenye hilo ili tusiende mbali kwa kuyasema hayo mtaona kwamba kesi ambazo mshitakiwa amewapitisha ni distinguishable kwenye mazingira yetu.
Hii kauli ya kwamba hatuna mamlaka ya kuomba Mahakama iitishe ‘Suo moto’ sisi tunasema mamlaka tunayo.
Katiba anasema naomba Mrema anisaidie anayo nyongeza.
Anasimama Wakili wa Serikali huyu anaitwa Job Mrema anakipara kama Mrema wa ubwabwani, sijui na yeye huwa anakunywa visungura kama mwenzake, anyway
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo July 3, 2026
Last time kwenye ya Uhaini dhidi ya Mhe. Lissu tuliishia part 224 so leo tunaendelea na -;
Part 225
Mheshimiwa Tundu Lissu anaingia ndani ya chumba cha mahakama, ukumbi namba 01 wa Mahakama Kuu.
Anaonekana mwenye tabasamu na furaha usoni kwake kama ilivyo siku zote.
Upande wa Jamhuri wapo kama kawaida yao
Inapigwa Court…..
Jopo la Majaji watatu wanaingia,
Kesi inatajwa
Anasimama Wakili wa Serikali anajitambulisha jina lake Ajuaye kisha anatambulisha Mawakili wenzake.
Jaji anaamuliza Mhe. Lissu kama yupo tayari
Mhe. Lissu anasema yuko tayari kuendelea.
Kama kawaida yao anasimama Wakili wa Serikali Katuga kuweka pingamizi.
Mhe. Lissu anapendekeza maombi yake ya sikilizwe kwanza ndo pingamizi lao lijibiwe.
Majaji wanasema tuanze kwanza kusikiliza PO, kisha taratibu nyingine zitafuata.
Anaanza Mhe. Lissu Waheshimiwa Majaji kesi hii inatokana na maombi namba 19065 ya mwaka 2025, Juu ya maombi ya kuongeza ushahidi katika muendelezo wa kesi, uamuzi wa tarehe 24 February 2026 wa Mahakama Kuu wa kukataa kuingizwa kwa ushahidi mpya.
Waheshimiwa Majaji uamuzi wa February 24, 2026 ni uamuzi mdogo, uamuzi ambao haujamaliza shauri na kwa mantiki hiyo kisheria kabisa haupaswi kukatiwa rufaa au pingamizi.
Waheshimiwa Majaji wa rufaa, Mahakama hii katika kesi ya Mkurugenzi wa Mashitaka dhidi ya Mohammed Mussa Ussi criminal appeal namba 521 ya mwaka 2023 Mahakama ikiwa imeketi Zanzibar ilisema msingi wa kukataza rufaa ama mrejesho (revision) ya jinai msingi wa hiyo hoja ni kifungu cha 8.2.d kutokana na marejeo ya mwaka 2023 mahakama hii ilisema uamuzi huo hauwezi kukatiwa rufaa kwani ni uamuzi usiomaliza shauri.
Anaendelea Mhe.Lissu
Kesi ambazo nimeziwasilisha mbele yenu waheshimiwa Majaji zinazungumzia uamuzi mdogo ni wa aina gani na uamuzi unaoweza kutolewa kama uamuzi wa mwisho unaoweza kuombewa revision ni wa aina gani.
Uamuzi unaomaliza kesi na kunyima haki za wadaawa ndiyo unaopaswa kukatiwa rufaa, uamuzi unaokuwa treated as the final order ndiyo unaomaliza haki za msingi za wadaawa lakini kama uamuzi haufanyi hivyo hauwezi kukatiwa rufaa.
Sasa waheshimiwa Majaji baada ya kuwapitisha kwenye kesi hizo nirudi kwenye hoja yangu ya msingi je uamuzi wa February 24 mwaka huu ulimaliza kesi hii?
Kama ni hivo ulimaliza kesi hii na kwamba Sasa hivi sina kesi ya uhaini basi hoja yangu haina msingi na maombi haya hayawezi kusikilizwa.
Hoja yangu waheshimiwa Majaji ni kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu wa February 24, 2026 haukumaliza kesi namba 19065/2025 na kwasababu haukumaliza maombi haya ya revision yanakatazwa kuletwa Mahakama ya Rufaa.
Anaendelea Mhe.Lissu
Waheshimiwa Majaji uamuzi huo unasema nini, ili tujue kama ulimaliza kesi lazima tuusome huo uamuzi unasema nini.?
Rulling yenyewe iko ukurasa wa 405-432, kwenye ukurasa wa 431 paragraph ya mwisho waheshimiwa Majaji mtaona Mahakama ilichokiamua.
Kilichokataliwa kupokelewa na Mahakama ni notice of additional substance of evidence, Mahakama Kuu haikusema kesi haitaendelea. Mahakama kuu ilitoa Mwongozo haikutoa uamuzi wa mwisho wa kesi, uamuzi wao ulikataa subodinate issue.
Waheshimiwa Majaji ushaidi mwingine huko kwenye maombi yenyewe yaliyoletwa. Mahakama inasema ilijadili na kukataa notice yao ya kuongeza ushahidi haisemi kesi ilifia hapo kutokana na uamuzi huo.
Mahakama imekata notice of additional substance of evidence, kwahiyo wanalalamikia uamuzi wa notice kukataliwa.
Jambo la pili ni Je mleta maombi anayo mamlaka ya kuiambia Mahakama itumie mamlaka yake ya kupitia kumbukumbu ili kuridhisha matakwa yake mwenyewe?
Jibu ni hapana hiyo siyo haki yao kisheria kwani wajibu wa kuangalia record ni wa mamlaka yenyewe.
Part 226 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 225
Mhe. Lissu anaendelea hapa.
Kama mtakumbuka nilisema ninavyoishi Ukonga, siruhusiwi kuonana na Mawakili wangu in private.
Mnaruhusiwa kutembelea Magereza naomba mliangalie na hili kama itawapendeza inawapa Mamlaka ya kutoa mapendekezo na mamlaka za Magereza kurekebisha masuala yanayohusu wafungwa kama haya niliyosema.
Ni muhimu kwamba kuwasiliana na washauri wangu wa kisheria ilindwe kama sheria inavyosema bila kusikilizwa na maafisa wa Magereza.
Ni hayo tu Waheshimiwa
Mhe. Tundu Lissu amemaliza na amekaa sasa.
Majaji wanaandika hapa.
Anasimama Renatus Mkude kuwa tutampatia hizi nyaraka ndani ya siku 14 tutampatia.
Hili la masuala ya utawala wa mambo ya magereza kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha National Prosecution Act na sisi ofisi ya DPP tutatembelea ili kuhakisha kunakuwa na fair trial.
Wameombwa Majaji anasema DPP ataenda eti huko Magereza kuangalia haki za Mtuhumiwa. Uongo uongo uongo. Hawana hata aibu hawa jamaa.
Majaji wanaandika baada ya kusikia hayo kutoka kwa Wakili wa Serikali, Renatus Mkude.
Majaji wanajadili pale.
Yuko Jaji muda wote yeye huwa anacheka anafurahi tu sijui huwa anatabasamu jambo gani? Wanaofika hapa Mahakamani wanamfahamu vizuri.
Jaji Ndunguru: Tumesikia hoja za Jamhuri na Hoja za Mshitakiwa nae kama ambavyo mshitakiwa ameturahisishia kuwa mikono yetu imefungwa kwamba yapo hayo maombi ya marejeo Mahakama ya Rufani.
Sasa shauri hili linasimama hadi pale Mahakama ya Rufani itakapotoa uamuzi.
Suala la Gerezani wakili wa Serikali amesema na sisi pia tumelichukua.
Mwenendo wa shauri hili unasimama hadi pale mambo ya Court of Appeal yatakapoisha.
So kesi hii imeahirishwa hadi hapo itakapoitwa tena.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 224
Majaji wameingia muda huu saa nane Kamili Mchana.
Wanaandika pale juu.
Mheshimiwa Lissu ameingia na kuteta jambo na Dr. Nshala tunamsikia anasema waende kokote watakapotaka kwenda tutakutana nao huko. Sasa sijui ni wapi anamaanisha.
Anasimama Renatus Mkude Wakili wa Serikali kwa niaba ya jopo la Mawakili wa Serikali tunaomba radhi kwani tulifikiri tungetumia lisaa limoja.
Mchana huu nipo na Ajuaye, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Kwa wote tunawakilisha jamhuri na Mshitakiwa yupo.
Shauri lilipangwa kuendelea na mashahidi. Lakini tumetafakari na tunaitafsiri kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Appellate Jurisdiction Act na kanuni ya 65(1) ya kanuni za Mahakama ya Rufani.
Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) anatoa taarifa ya kuwasilisha taarifa ya mapitio (revision)
Hapa kwanza anakosea Mapitio ni Review alipaswa kusema Marejeo ndio Revision sijui kasoma wapi nae huyu jamaa.😂😂😂
Anaendelea hapa Renatus Mkude, kuwa Notice of motion hiyo imeambatanishwa na kiapo cha Cathbert Mbiringe Wakili wa Serikali ambayo taarifa hii ya kutoa notice kwenda Mahakama ya Rufani imesainiwa leo Tar. 24/02/2026.
Na kupokelewa kwa mifumo ya kielektroniki inayotambulika na Mahakama na kusajili kama. CRIMINAL REVISION NO. 7203216/2026 imepokelewa na Mahakama ya Rufani Tanzania hapa Dar es salaam.
Ambalo chimbuko lake ni Criminal Sessions No. 19605/2025 ambayo iko mbele yenu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu. (Ndunguru, Karyemaha, Kiwonde)
Kwa kuwa shahidi wetu aliyekuwa anafuata ACP Mahamba tuliyemuombea notice additional substamce of evidence na ikakataliwa.
Ni Rai yetu kwamba kwa kuwa shauri hili limeshapokelewa Mahakama ya Rufani haiwezi kusimama ili kuweza kutoa nafasi kwa shauri husika huko Mahakama ya Rufani kuweza kuamuliwa.
Ni hayo tu kwa sasa.
Tunamsubiri Mh. Lissu atajibu nini?
Mhe. Lissu anaanza.
Baada ya kuzikiliza wasilisho la upande wa Mashitaka nina haya ya kusema.
1. Kwa vile mimi nipo gerezani na wanajua nataka wanipatie hiyo nakala ya Notice of Motion waliyofile niweze kuiona.
2. Ninafahamu na ninatumaini na wao wanajua kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 8(2)(d) cha Sheria ya Mamlaka ya Rufaa ambacho wamekitaja (Appellate Jurisdiction Act) wanafahamu kwamba hakiruhusu rufaa wala mapitio wala marejeo ya maamuzi ya Mahakama ambayo hayamalizi shauri la msingi. (Interlocutory decisions) sina shaka na wao wanalifahamu hilo.
3. Waheshimiwa Majaji siwaombi mtoe uamuzi wowote kuhusu hili ninalolisema.
Nataka iwe kwenye record kwamba nafahamu na naamini upande wa mashitaka wanafahamu lengo la kupeleka ombi la marejeo Mahakama ya rufani na wanafahamu hairuhusiwi ni kurefusha mashauri haya ili niendelee kukaa Gerezani. Ni hilo tu.
Kwamba tupeleke Mahakama ya Rufani ili huyu mbaya wao ambae ni mimi aendelee kukaa Gerezani.
Kwa vile wananipeleka kwe ye Mahakama ya Rufani nataka niwaeleze kuwa nitawafuata huko huko naenda kuwashughulikia huko huko.
Kama ambavyo kesi yao is dead on arrival najua hata hii revision yao pia imeshakufa.
Tutarudi hapa yakiisha huko ya Mahakama ya rufani tutarejea hapa na nitawashughulikia tukirudi.
Jambo la Mwisho Mawakili wangu wametaka kunipa nyaraka hapa lakini siwezi kupewa hadi nyie mseme.
Sijui wanaogopa nini watu wa magereza nisipewe huo uamuzi hapo ni makaratasi tu.
Naambiwa ni hukumu kutoka huko Umoja Wa Mataifa lakini Magereza wanaogopa nisipewe.
Tena ni uamuzi unaohusiana na mimi kuwepo Gerezani. Tatizo liko wapi?
Jaji anasema uko wapi? Umepelekwa wameuona wamesema wape Mawakili wa Serikali.
Wako wanasoma hapa Mawakili wa Serikali huo uamuzi.
Anasimama Renatus Mkude anasema mimi ni member wa working group za UN Human Rights Council.
Jaji: Tumesema apewe au asipewe?
Renatus Mkude: Apewe tu.
Part 225 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 24, 2026
Last time tuliishia Part 222 so leo tunaendelea na-;
Part 223
Majaji wameingia na Mshitakiwa pia ameingia.
Karani anasoma shauri hapa.
Anasimama Renatus Mkude anasema yupo na Ajuaye, Katuga, Thawabu, Cathbert Mbiringe.
Anasema leo tumekuja kwa ajili ya kupokea ruling na sisi tuko tayari.
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa unasemaje?
Mhe. Lissu: Na mimi niko tayari.
Jaji anaanza kusoma hapa UAMUZI.
Uamuzi huu unatokana na pingamizi lililowekwa na pingamizi la mshitakiwa kutokana na taarifa ya kuongezwa kwa ushahidi.
Taarifa hiyo ililetwa tarehe 18/02/2026 na upande wa Mashitaka kwamba unatokana na pingamizi lililowasilishwa na mshitakiwa.
Notice hiyo ililetwa kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Mshitakiwa alieleza Mahakama kwamba kifungu hicho kinaelezea shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa wakati wa mwenendo kabidhi na hivyo walichokileta upande wa mashitaka ni kuleta ushahidi mpya.
Upande wa mashitaka walijibu notice ipo halali kwa mujibu wa sheria na imekibidhi matakwa ya kisheria na ipo kwa mujibu wa sheria.
Huo ndio ulikuwa msingi wa hoja za pande zote mbili.
Mahakama imeona hoja inayopaswa kuamuliwa ni je notice hiyo ipo kwa mujibu wa sheria?
Ili kurahisisha Mahakama imeona ili reproduce notice hiyo inavyosema.
Anasoma notice inavyosema kwamba ni notice ya kuongeza maelezo ya ziada ya shahidi husika ambae ni Amin Mahamba.
Hakuna mashaka kwamba upande wa mashitaka wanataka kuongeza ushahidi wa Amin Mahamba.
Kwa vile Amin Mahamba ni shahidi na statement yake ilishasomwa wakati wa committal ilishasomwa.
Notice inasema ushahidi unaotaka kuletwa ni wakati wa uchaguzi wa tar. 29/10/2026.
Anasoma kifungu cha 308 cha CPA kinavyosema.
Ukiangalia kifungu hicho kinatoa masharti au mazingira ambayo notice hiyo ni reasonable au laaa.
Masharti ni kwamba
1. Maelezo yatoke kwa shahidi
2. Uwe ni ule ushahidi ambao haukusomwa wakati wa committal
3. Uwe ni ushahidi ambao haukusomwa wakati wa proceedings
Kifungu cha 308 ndio kinachosema hawezi kutoa ushahidi hadi watakapoleta notice na hivyo basi ukiangalia hayo kifungu hicho cha 308 kinafungua mlango kwa shahidi ambae alikuwepo na bahati mbaya maelezo yake hayakuletwa.
Amin Mahamba maelezo yake yalikuwepo wakati wa commital, anataka kuleta mambo ya Uchaguzi ambayo hayakuwepo wakati wa committal.
Ipo kinyume na kifungu cha 308 cha CPA.
Hivyo basi kifungu cha 308 kinaweza kuruhusu notice hiyo tumeona kwamba kifungu hicho hakiruhusu kabisa.
Shauri la Remina Omary Abdul tumeona linahusiana na vielelezo vya wakati wa committal. Shauri hilo haliwezi kutibu chochote katika hoja iliyopo mbele yetu.
Hiyo notice ya kuongezwa kwa ushahidi ambayo imeletwa na upande wa mashitaka haitambuliwi na kifungu cha 308 cha CPA.
Kimsingi tunasema kwamba fundamentally haiko sahihi na baada ya kusema hayo basi notice hiyo ni incompetent na tiba pekeee iliyopo ni kwamba notice hiyo lazima iwe struck out. Ni hayo tu.
Anasimaa. RENATUS MKUDE anasema baada ya kupokea ruling tunatafakari tunaomba ahirisho ya lisaa limoja.
Twende kutafakari.
Bado majaji wanashauriana pale juu.
Nafikiri leo KATUGA atajua vizuri nani ni Bingwa wa Sheria😂
Anasimama Mh. Lissu anasema mmesema kuwa mashahidi waletwe leo na mlisema tutasikiliza uamuzi wa pingamizi na tutasikiliza shauri leo.
Sasa wanasema tuahirishe kusikiliza ili wakatafakari.
Wanaenda kutafakari nini? Ili iweje? Huu uamuzi haukatiwi rufaa.
Tusipoteze muda kila tunapopoteza muda anayeumia ni mimi sasa wao walipaswa kuleta mashahidi na wasitupotezee muda kabisa, tuendelee kusikiliza shauri hili.
Majaji wanaandika kidogo
Anasimama Renatus Mkude anasema tumemsikia Mshitakiwa
Tuna mambo mawili.
1. Tumepokea ruling ya Mahakama na tumeikubali
2. Jambo la pili ni kwamba tulimtaja shahidi ambae lazima tuwezi kumuandaa shahidi yetu
Jaji Ndunguru anasema tulisema muwe na mashahidi wakutosha. Tukiendelea kubishana tutapoteza muda, turudi mahakaman saa 5 kamili
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 222
Katuga anasema kifungu cha 308 ni mlinzi wa kifungu cha 263 cha CPA ni kumfanya mshitakiwa awe aware na ushahidi wote anaokutana nao Mahakama kuu.
Ushahidi upo wa aina nne, real, documentary, testimonial na nyingine nimesahau nitaikumbuka.
Kwahiyo kwa maana ya aina ya shahidi nne zinatakiwa zioneshwe kwa mshitakiwa kabla ya kuwa committed kwenda High Court na kwakuwa kuna takwa hili la 263 kukawekwa kifungu cha 308 ambacho ni mlinzi sasa.
Kwamba hakutakuwa na ushahidi utakaoingia hadi uwekwe wazi basi prosecution wampe notice kuhusiana na ushahidi huo ni lini prosecution wamegundua huo ushahidi. Je mshitakiwa alikuwa na reasonable time kuupitia.
Kif. 308(4) kinazungumzia substance or witness.
Kesi ya Remina Omary Abdul vs Jamhuri CA 189/2020 Mahakama ya Rufaa ilisema, INASEMA IF PART OF THE EVIDENCE IS NOT DISCLOSED.
Mahakama ili quote with approval maneno kuwa additional evidence is allowed.
Sisi tunasema mbali na statement yake kusomwa tunataka kuleta mambo mengine ambayo hayakujumuishwa.
Notice hii ina comply na tafsiri ya sheria na sio tafsiri ya mtu. Iko sheria na tunaomba ikubaliwe.
Katuga kuna maneno pia yamesemwa kuwa notice hii ikiachwa hizo sio hoja. Unamtisha nani? Naona kama anatutisha ni hoja ambayo itafungua pandora na hiyo pandora ni ipi?
Tunaomba mapingamizi yatupiliwe mbali.
Anasimama Mh. Lissu kumjibu Kituga.
Nimesikiliza majibu yao naomba niseme yafuatayo.
1. Kifungu cha 308 cha CPA kinahusu shahidi mpya. Shahidi mpya kimesema ni yule ambaye maelezo yake au substance ya maelezo yake haikusomwa kwenye committal. Kwahiyo kifungu hicho kinahusu shahidi mpya na sio ushahidi mpya. Suala ni shahidi wa ziada na sio ushahidi wa ziada wa shahidi ambae tayari maelezo yake yapo tayari.
2. Kwenye notice hii suala la kuamua sio reasonable au laa. Ni suala la kinacholetwa ni shahid mpya au laa.
3. Hiyo kesi ya Remina Omary Abdul waliyoleta si mara ya kwanza inazungumzwa kwenye Mahakama hii. Ililetwa kipindi kile cha Committal. Inahusu kifungu cha 263 tu. Ukurasa wa 32 ni kuhusu section 246 ambacho ni 263 ya sasa. Kwahiyo hiyo kesi inahusiana na mambo ya Committal basi kifanyeni kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Mlango wa Amin Mahamba ulifungwa kwenye committal kama mnataka tafuteni shahidi mwingine sio Amin Mahamba.
Hoja ya kwamba hili ni pingamizi limeletwa pre mature nasema liko timely maana yanayohusika na kesi hii yalishakamilika na kuletwa Mahakamani.
Effect yake ni kunibadilishia shitaka maana shitaka langu ni la tar. 03/04/2025 haya ya October ni mambo mapya.
Mkiyaruhusu kwa kuruhusu notice hiyo na nimesema niko tayari, je wao watayaweza? Kwasababu ya October kuna genocide kuna mass killings, mass murder. Ya October ni magumu sana.
Pingamizi langu litalinda integrity ya shauri hili na mashauri haya. I'm only trying to help them wanafikiri kuna deal pale hakuna deal yoyote.
Angalieni kifungu cha 308 cha CPA.
Hii notice ifutiliwe mbali, naomba hivyo.
Majaji wanateta hapa.
Tunasubiri uamuzi wao kuhusu pingamizi hili.
Jaji Ndunguru amejadiliana na wenzake kwa muda mrefu sana hapa.
Anasema ili tuweze kuandika uamuzi na tutarudi kesho saa tatu asubuhi na tutaendelea na mashahidi wengine.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 221
Jaji Ndunguru ameteta sana na wenzake kama dakika 10 hivi.
Sasa anawasha kipaza sauti.
Anasema yafuatayo: tumesikiliza hoja zote hivyo vijembe vyenu msivilete.
Sasa mshitakiwa alisema anapingamizi na tukasema upande wa mashitaka walete open statement ili Mahakama iamue.
Mambo mengine ya kwamba imeambatana na nini na nini kipo wapi hayo sio mambo ya msingi.
Mshitakiwa endelea sasa, hawa upande wa mashitaka mmemaliza hapo, presentation ya notice na justification ya notice.
Watu wanacheka hapa 😂😂😂😂
Nafikiri mpaka sasa Katuga ameelewa nani ni Bingwa wa Sheria.
Mhe. Lissu amasimam, sasa Waheshimiwa Majaji kwa kuanzia niseme hivi waliyosema wenzetu.
1. Upande wa mashitaka unasema notice yao haileti shahidi mpya bali inaongezea ushahidi wa shahidi ambae ushahidi wake ulishatolewa kwenye committal.
2. Wamemtaja huyo shahidi kwa jina kabisa.
3. Wamesema wameleta viambatanisho vinavyotakiwa kwa mujibu wa kifungu cha 308(2) cha CPA.
Sasa baada ya kusema twende kifungu kinavyosema cha 308
A witness whose statement or evidence was not read during committal......
Kifungu kinasema shahidi mpya.
Kinachotakiwa kuletwa ni jina la shahidi wa ziada, huyu ndio anaweza kutolewa notice.
Wamesema wenyewe hawaleti shahidi mpya bali wanaongezea ushahidi wa shahidi aliyepo.
Sasa huyu shahidi ambae tayari yupo na wamemtaja huyo Shahidi ACP Amin Mahamba.
Sasa waheshimiwa Majaji naomba niwaalike kwenye ukurasa wa 90 na 91 na 99 na 100 wa record ya committal proceedings na ukurasa wa 134 wa record ya Mahakama hii ambapo upande wa mashitaka ulitaja majina ya mashahidi wao.
Huyo Amin Mahamba yupo na mimi maelezo yake ninayo hapa sasa Waheshimiwa majaji hiyo notice inaingiaje mahakamani.
Ushahidi wake tayari upo mahakamani na notice inatakiwa iwe ya shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa mahakamani.
Hii sio notice ya additional witness ni notice ya additional evidence ambayo haipo kisheria nimetafuta CPA yote hicho wanachosema hakipo.
Jambo lingine ni kwamba wanaleta ushahidi wa mtu aliyefanya upelelezi wa matukio ya uchaguzi mkuu 2025 sasa Majaji matukio ya tukio ya tarehe 29/10 mimi tayari niko mahabusu
Anasimama Katuga anasema tunapinga anaanza kujadili ushahidi wetu kama mtakubali ni sawa tu.
Lissu: Si ndio kayaleta haya mwenyewe wanakatazaje nisiyazungumzie?
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa endelea.
Lissu: amesema mwenyewe kwa mdomo wake hapa Mahakamani. Nilimwambia asibwabwaje sana. Akang'ang'ania kuanza kusema mambo ya tarehe 29/10 ndio maana na mimi nasema hayo ya tarehe 29 mimi nilikuwa jela.
Wanafikiri hayo yatawasaidia maana wanataka kugeuza mashitaka kwa kuleta mambo ya tarehe 29/10/2026. They can not amend the information through the back door. Kama mnataka ku amend information nendeni kwenye kifungu cha 294 ch CPA.
Hiyo wanayoiita notice haipo kisheria. Haitambuliki. Hiyo notice muifutilie mbali. Yaani notice na yaliyomo.
Na mwisho, Wahe. Majaji hiyo notice ikiachwa ikawa sehemu ya record ya Mahakama itafungua sanduku la pandora ambalo lina kila aina ya mambo mabaya ambayo sidhani kama itaweza kushughulika mambo hayo.
Wanataka tuzungumze mambo ya October 29 mtakuwa mmefungulia balaa na isije ikawa shida. Mkifungua huo mlango tutaenda huko. Tutazungumzia mauaji ya kimbali na tutaulizana nani aliyeua watanzania. Hii kitu haina mashiko. Are they ready? Mimi niko tayari. Isiruhusiwe ikiruhusiwa niko tayari?
Jaji tafadhali naomba tusiende huko.
Katuga aliambiwa na Lissu kuwa huwezi kunifundisha Sheria akakataaa. Baada ya Lissu kumaliza hapa. Katuga amekuwa mdogo sana yani. Ni kama anataka kulia.
Katuga anasimama anasema napaswa kufanya nini reply au rejoinder
Mhe. Lissu anasema fanyeni reply halafu mimi ndio nitakuja kumaliza.
Wanakubaliana hivyo.
Part 222 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 23, 2026
Last time tuliishia Part 219 so leo tunaendelea na-;
Part 220
Mh. Tundu Lissu anaingia Mahakamani.
Mawakili wa Serikali wapo tayari na Majaji wana kila dalili ya kuingia muda wowote.
Kelele za Shujaa Shujaa Shujaa zinasikika.
Mh. Lissu ameingia anateta jambo pale na Wakili Kisabo na Mahinyila ni kama anawaagiza jambo.
Namuona Wakili Kisabo anachukua simu ni kama anafanya mawasiliano.
Majaji wameingia kuna mtu simu yake imeita, watu wanamshangaa.
Anasimama Kalani anasoma case number.
Anasimama Renatus Mkude, tupo Ajuaye, Katuga, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Shauri lilipangwa kwa ajili ya kusikiliza Notice ya kuongeza mashahidi na ushahidi na sisi tuko tayari.
Majaji wanaandika kidogo.
Wanamuuliza Mshitakiwa.
Mhe. Lissu anajibu na yeye kuwa yuko tayari.
Wanaitwa Upande wa Mshitaka anasimama Katuga kuanza.
Mhe. Lissu waheshimiwa Majaji nimepinga hiyo notice toka ijumaa kwahiyo ningesikilizwa.
Katuga Mheshimiwa Jaji utaratibu ni sisi kuiwasilisha ili yeye apinge kama ana hoja ya kupinga hii sio Application.
Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji hicho wanachoita notice sio notice kabisa na hakitambuliki kisheria.
Jaji sisi tulitaka waeleze nini kinaendelea tu.
Mhe. Lissu: Kama ni hivyo sawa.
Katuga: Mnamo tar. 18/02/2026 kwa njia ya mtandao tulifile notice ya kuongeza ushahidi (notice to file additional statement of evidence) tuliifile kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Pamoja na notice hiyo tuliambatanisha substance ya ushahidi huo, ushahidi huu haumleti shahidi mpya bali ni nyongeza ya Ushahidi wa ACP, Amin Mahamba.
Kwamba ushahidi huu haujakuwa committed Mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Notice hii inakuja kukidhi matakwa ya kifungu cha 308 cha CPA ambacho kinasema hakuna shahidi au maelezo ya shahidi vitatolewa mahakamani unless viwe vimesomwa wakati wa mwenendo kabidhi (committal)
Kifungu hicho kinafafanua maana ya substance of evidence ikiwa ni pamoja na kitu chochote ikiwemo nyaraka na vitu vingine vinavyoshikika.
Kama ambavyo notice inajieleza, substance ya ushahidi kwamba Amin Mahamba alikuwa ni kiongozi wa timu ya upelelezi wakati wa uchaguzi wa 2025 na baada ya uchaguzi.
Na kile alichokipata kutokana na upelelezi ni kitu ambacho haukusomwa pale kwenye committal.
Ushahidi huo tumeupata na kuugundua wakati tumejiandaa kumuita ACP Amin Mahamba siku ya tarehe 16/02/2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA hakijaeleza ni kwa jinsi gani notice itakuwa. Hata kwenye zile prescribed form zilizopo kwenye Sheria hii haijawekwa.
Kifungu hicho kinasema notice ieleze jina la shahidi, substance ya ushahidi na details za shahidi kiujumla kwa mujibu wa kifungu cha 308 (2) cha CPA.
Hivyo vyote tumefanya kwenye notice yetu kucover matukio ya tarehe 29/10/2025.
Anasimama Mhe. Lissu, anasema waheshimiwa mbona kama anaendelea kufanya mambo ambayo hamjamuelekeza.
Katuga waheshimiwa kwani hiyo introduction iko chini ya Sheria gani? Sisi tunaintroduce kwa namna tunayoona ili mwenzetu.
Mhe, Lissu: Asinifundishe Sheria, asijaribu kabisa kunifundisha Sheria, anaanzaje kufanya submission ya hiyo notice kabla uhalali wake haujaamuliwa.
Katuga: Waheshimiwa hakuna bingwa wa Sheria, mabingwa ni nyie tu Majaji.
Majaji wanateta pale juu.
Tunasubiri muongozo wao.
Part 221 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 219
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross Examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Coplo Amani.: mimi sijalisema tu kama wewe umelisema basi ndio umesema.
Mhe. Lissu: Ni kweli kwamba P3 alikwambia kuwa ni mwanachama wa CHADEMA, kweli au si kweli
Coplo Amani : sio kweli
Mhe. Lissu: Wewe ndio uliandika maelezo yake kielelezo D12
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Sasa ngoja nikusomee… “mimi pia ni mfuasi na mwanachama wa CHADEMA” kweli si kweli.
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kwenye maelezo yako uliyasema hayo
Coplo Amani : sikuyasema
Mhe. Lissu: Alikuonyesha kadi yake cha chama
Coplo Amani : sikutaka anionyeshe
Mhe. Lissu: alikwambia wafuasi wa chadema wana alama gani?
Coplo Amani : sikumuuliza mm
Mhe. Lissu: ndo maana nasema huyu ni askari wa kitengo cha intelijensi halafu mnasema ni shahidi.
Mhe. Lissu: Turudi kwa Inspekta Jorum, ni kweli polisi inapopokea watu waliofanya uhalifu , Polisi wanafungua investigation register?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waelezze majaji kama kwenye maelezo yako polisi walifungua investigation register
Shahidi: sijui
Mhe. Lissu: Waeleze majaji baada ya maafa yote hayo ya October 29 kama mmemchukulia hatua yoyote huyu baada ya kusema atapiga watu mawe?
Coplo Amani: Simfahamu chochote kuhusu swali lako
Mhe. Lissu: inaingia akilini hii
Coplo Amani : Mimi sifahamu chochote kwa kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama unajua mashahidi wote wa kificho walisema waliona hiyo video yangu maarufu tarehe 4 april
Coplo Amani : Mimi sio mpelelezi wa mafile yote
Mhe. Lissu: Na unahabari wote waliokuja hapa ni boda boda na machinga hakuna afisa wa serikali au n.k
Coplo Amani : sina habari
Mhe. Lissu: Ulipomuachilia P3 kwa dhamana ulichukua hatua gani kuhakikisha aendelei na kupiga watu mawe na uasi?
Coplo Amani : sikupewa hilo jukumu
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji mimi sina maswali ya ziada.
Serikali: Kwa leo tulikua na shahidi huyu tu mmoja, tunaomba ahirisho kwasababu hali ya hewa ya Dar es salaam imebadilika na zimebaki dakika 20.
Kwasababu za kiusalama tunaomba ahirisho hadi siku ya Jumatatu ili tuje kuendelea kusikiliza juu ya notice tuliyoileta
Mhe. Lissu: Waheshimiwa Majaji kwa dakika 20 kwangu si haba, mimi ninaomba hizi dakika 20 kwasababu nilishasema nina mapingamizi, naomba niongee juu ya hayo leo ili tusiathiri muda wa mashahidi wengine Jumatatu.
Naomba nipate hizi dakika 20 kwasababu mimi niliyepo Gerezani ndiye ninayepata shida, kwahiyo naomba tutumie hizi dakika jambo lifanyike.
Wakili wa Serikali: Waheshimiwa sisi tunaomba ahirisho lakin vilevile kama mnavyojua dini zote mbili tupo kwenye mfungo kwahiyo tunaomba ahirisho.
Lakini vilevile PO yake haijasajiliwa bado kwahiyo kama ataweza kuisajili na kuisikiliza basi aisajili na sisi tupewe nafasi ya kuiona ili tu-submit
Mhe. Lissu: waheshimiwa majaji sikutarajia kwamba hili litakua na kubishana namna hii, nililetewa hii notice jana na nikatoa notice ya mdomo kwamba naipinga tena immediately nilipopatiwa tu notice hii.
Naijua sheria, sasa wanaposema tuahirishe ili niendelee kukaa gerezani ni sawa tukutane Jumatatu ili tuzungumzie PO yangu niliyoileta jana.
Na jana nilisema kabisa PO ni ya kisheria na itaenda na kifungu icho icho cha 308(1) cha CPA, mimi nakaa gerezani kwasababu ya michezo hii mnayoleta mawakili wa serikali kila siku.
Jaji Ndunguru anasema shauri litaendelea siku ya Jumatatu, tunatarajia serikali mlete mashahidi, tutaanza na hoja ya notice, tukimaliza tutaendelea na mashahidi wengine.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 218
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross examination Shahidi wa Jamhuri Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Angalia D14 tuambie wapi alisema alimuona Tundu Lissu akihamasisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi wa 2025?
Coplo Amani : Hayo maneno kufanya vurugu hayapo kwenye kielelezo
Mhe. Lissu: April 17, 2025 kwenye ushahidi wako wa hii siku unasema ulikuwa kituo cha Polisi Ilomba na ukapewa maelekezo na inspekta Jorum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana na alichoeleza juu ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu kuhusu kauli yake na akahamasika na akashawishi wenzake wafanye vurugu na kuharibu uchaguzi mkuu 2025, eleza kama maelezo hayo yapo
Coplo Amani : hayo maelezo hayapo
Mhe. Lissu: Coplo Amani shahidi haya yote ambayo nimekuuliza kama yapo au hayapo ma umesema hayapo katika maelezo yako, swali langu ni uliyasema hapa mahakamani kwasababu ni mambo muhimu kwa mahakama kuyasikia, kweli au si kweli.
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji naomba nitoe ufafanuzi.
Mhe. Lissu: Hapana naomba ujibu swali langu
Coplo Amani: nawaomba majaji
Mhe. Lissu: hapana
Coplo Amani : ni kweli
Mhe. Lissu: Umewaeleza waheshimiwa majaji kwanini hayo mambo muhumu hayapo katika maelezo yako??
Coplo Amani : bado nina muda
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Coplo Amani : sijayasema na sijayaeleza kwasababu ninazozijua Mimi.
Mhe. Lissu: Nataka uangalie icho kielelezo D14 ni nataka uangalie halafu uniambie kama nakosea umeandika baada ya kupata maelezo ya kazi ya Jorum nilianza ufuatiliaji Isyesye mtaa wa Mwantengule, kwa maneno hayo nitakuwa sahihi nikisema kwamba ulikwenda Mwantengule ukiwa tayari unamjua P3
Coplo Amani: nilikua simfahamu
Mhe. Lissu: Kama ulikua humfahamu uliendaje moja kwa moja ukamkamata
Coplo Amani : Nilishasema nilionyeshwa na askari wa intelijensi
Mhe. Lissu: hayapo kwenye maelezo yako and it is too bad.
Mhe, Lissu: P3 ni dereva wa boda boda sio
Coplo Amani : ndio
Mhe. Lissu: Na umesema askari wa intelijensi huwa wanajichanganya hata kwa boda boda
Coplo Amani : kweli
Mhe. Lissu: sasa waambie waheshimiwa majaji kama huyu P3 sio askari wa kweli wa intelijensia
Coplo Amani : si kweli
Mhe. Lissu: umesema P3 alipanga kupiga watu mawe, kuasi nchi halafu umesema Jorum alikwambia umuachie kwa dhamana, inaingia akilini??
Coplo Amani : inaingia akilini
Mhe. Lissu: mtu anayepanga uasi na kupiga watu mawe mnampa dhamana?! Kwanin tushangae yaliyotokea October 2025!
Coplo Amani : mimi sijui bwana muulize Jorum
Mhe. Lissu: Jorum hayupo kwenye kizimba
Mhe. Lissu: kwahiyo nyinyi Polisi ndo mlipanga mambo ya October 29
Coplo Amani : Mimi sina majibu ya hilo.
Mhe. Lissu: Eleza kama umeleta pikipiki uliyomkamata nayo
Coplo Amani : sijaonyesha
Mhe. Lissu: usajili wa Bodaboda
Coplo Amani : Hakuna
Mhe. Lissu:Kadi ya bodaboda
Coplo Amani : hakuna
Mhe. Lissu: Na huyu jamaa tunamtambua kama P3, hatujui jina lake, amejificha kwenye kibox hatujamuona tutajuaje kama ni boda boda?
Coplo Amani : hayo mambo yanahusika vipi kwenye kesi hii
Mhe. Lissu: yanahusika
Mhe. Lissu: Huyu P3 ulivyomfikisha Ilomba ulimuweka mahabusu, kweli au si kweli
Coplo Amani : Si kweli
Mhe. Lissu: Naomba nimsomee shahidi kielelezo D12 jinsi P3 alivyofikishwa kituoni……”tulivyofika kituoni aliniweka mahabusu”
Sasa swali langu kati ya ushahidi wako ww na ushahidi wa P3 Mahakama ichukue upi kuwa ni ushahidi wa kweli?
Coplo Amani : hilo ni jukumu la mahakama.
Mhe. Lissu: naomba ujibu swali langu
Coplo Amani : hilo ni jibu la mahakama
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba shahidi ajibu swali langu
Katuga: Waheshimiwa shahidi ameshajibu sasa kama halimpendezi basi hilo ndio jibu
Mahakama: endelea na Cross
Mhe, Lissu: Kwenye ushahidi wako kizimbani umewaambia majaji kwamba P3 alikua anahamasisha watu kupiga mawe?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Kwanini hujalisema wakati upo kizimbani
Part 219 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.