Mhe Rais, choonde mpe Mhe. Francis Ndulane second chance ya kuapa. Alikuogopa na adrenalin yake ikashuka na ikamchanganya. Mwite, kunywa nae chai, kisha ongozana nae kwenye meza ya kiapo.Ataapa vizuri! Unapomwadhibu, unaiweka afya yake katika hali mbaya sana.Forgive & save him.
Watanzania wenzangu kuna barua inasaambaa kwenye mitandao ya jamii inayodai kwamba mimi nimempongeza Rais kwa ushindi wa Urais.Barua hiyo ni fake na ipuuzeni. Kamwe siwezi kumpongeza kwa uchaguzi wa madudu kama huu. Sana sana nitamwandikia kumwomba ajiuzuru ili uchaguzi urudiwe.
Barua inayosambaa ya tarehe 24/9 ya kujiondoa kwenye mbio za Urais ni ya kweli.Niliandika baada ya kutofautiana na msimamo wa Viongozi wangu wa kutaka nimuunge mkono Tundu Lissu. Hata hivyo barua hiyo ilikataliwa kwa sababu maneno " msimamo wa viongozi wangu" yanawatia hatiani.
It is gratifying to see my Leader and Brother Hon. Zitto Kabwe recovering well at Aghakan Hospital. I wish him a very safe and a successful surgery that will be performed tomorrow. He has my prayers!
Mimi ndiyo Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ACT- Wazalendo. Mimi ndiye niliyekabidhiwa Ilani ya Chama hicho kuinadi kote nchini kwenye uchaguzi huu. Taarifa zinazosambaa kuwa tayari tumejiunga na Chadema katika ngazi ya Urais siyo za kweli.
Nafurahi kuufahamisha umma wa Tanzania kuwa hatimaye Msaidizi wangu Jerome Luanda ameachiliwa na Polisi leo saa 10 jioni baada ya kujiridhisha kuwa hausiki na tuhuma ya money laundering wala kosa jingine lolote. Asante Wakili Peter Kibatala kwa kufuatilia swala hili hadi mwisho.
Watanzania wenzangu! Taarifa kuwa kuna msaidizi wangu mwingine ametekwa au kushikiliwa na Polisi si za kweli hata kidogo! Sina msaidizi mwingine, wala ndugu, wala jamaa au rafiki anayeshikiliwa na Polisi mbali ya Jerome Luanda. Puuzeni taarifa hiyo!
Msaidizi wangu Jerome tunaambiwa anakabiliwa na tuhuma ya money laundering. Ni maajabu ya maajabu! Uliona wapi Mtu anakamatwa Airport bila hata senti moja mfukoni mwake na bila kuwa na hela yoyote kwenye bag yake anakamatwa na kutuhumiwa kwa kosa la Money Laundering! Tanzania!
Afande kama taarifa hii ni ya kweli: 1. Yupo kituo gani cha Polisi
na kwa tuhuma zipi ili sisi wanafamilia na wanasheria wetu tuende tukamwone? 2. Mbona amekaa Polisi zaidi ya masaa 24 muda ambao kisheria alitakiwa awe amehojiwa na kupelekwa mahakamani au kuachiwa huru?
Tukio la kutekwa kwa Msaidizi wangu Jerome Luanda jana mara baada ya kutua kwenye kiwanja cha Kimataifa cha JK Nyerere international Airport nitalizungumzia kwa undani Saa 10 kamili leo. Nimewapa wahusika wanaodhani siwajui masaa matatu wamwachie akiwa mzima na salama.
Wana ACT- Wazalendo na Watanzania wenzangu wote! Kesho Jumanne ya tarehe 15 Sept.saa 8.40 mchana, nitatua DSM nikitokea Dubai na nitafanya Press Conference Airport. Afya yangu imeimarika na sasa nipo tayari kwa Kampeni ya Urais inayoanzia Tabora wiki hii hadi October 26.
HATOKI MTU HAPA! Wale wote wanaodhani kuwa Nitajiondoa katika kinyang'anyiro cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo, wanaota ndoto za Mchana. Kimbunga kitakachoanza tarehe 15 September 2020 October ni Kimbunga kumba-kumba! Watanzania kaeni chonjo!
Nawaomba Viongozi wote wa Dini wa madhehebu yote popote mlipo, liombeeni taifa na wale mnaoweza kukemea kemeeni kwa nguvu zote mchakato huu wa uchaguzi ambao unahatarisha Usalama na Amani ya nchi yetu. Msingoje kesho!
Uteuzi wa CCM uliofanywa leo umenifurahisha sana! Nawapongeza wote waliobahatika kuteuliwa, lakini kubwa zaidi nawapa pole wale wote waliokatwa kwa sababu ya kuwa karibu nami. Hiyo ni baraka siyo balaa. Karibuni mjiunge na ACT- Wazalendo haraka ili safari iendelee!