Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) kilikaa Julai 29. Siku hiyo hiyo Jeshi la Polisi linatoa taarifa 'KURUHUSU' mikutano! Julai 30, mahakama ya Rufani inatoa 'ushindi' kwa Lissu dhidi ya DPP, huku mama Kizimkazi akikutana na wanasiasa Ikulu. Julai 31, kesi ya uhaini ya Lissu inapangiwa tarehe.
Bado unataka ushahidi gani kuona kuwa DPP, Jeshi & mahakama wote wanapokea maelekezo & kuwa kesi ya TAL ni ya KISIASA! Bado unataka ushahidi wa chama KUSHIKA HATAMU!
‼️ALERT ‼️
Leo Makamu Mhe. John Heche yupo Simuyu Wilaya ya Bariadi.
Hii Gari inamfuatilia Heche tangu asubuhi, tumeangalia kwenye usajili hii namba inaonekana ni Trailer la mizigo na sio ya Land Cruiser.
Hawa ndo watekaji wenyewe ndo maana wanatumia plate number feki ili kuficha utambulisho wao.
Leo, Wakili Philip Mwakilima, ame file Mahakamani maombi yanahusu malalamiko la ndugu Augustino Abdu Chaula, ambaye amekaa kizuizini toka tarehe 30/06/2026 kwa amri na matakwa binafsi ya Jeshi la polisi kupitia mkuu wa upelelezi wa mkoa wa Njombe ndugu Joseph Malongo
Kwamba katika kipindi chote hicho Jeshi la polisi mkoani Njombe limekataa kata kata kwa kumpeleka mahakamani au kumpatia dhamana ya Polisi mlalamikaji anaiyeitwa Augustino Abdu Chaula, hivyo lengo la maombi haya ni kuomba amri za mahakama ili yafuatayo yafanyike:
1. Kumwachia huru ndugu Augustino Abdu Chaula
2. Kumpatia dhamana ya polisi
3. Kumfikisha mahakamani kama hakika kuna kosa amefanya.
‼️ALERT ‼️
Muda huu huko Kilwa Madalali wamekusanya Watu wa CCM, wamewavalisha nguo za CHADEMA na kuwarekodi wakimshambulia Mhe. Heche kwa malipo ya laki moja moja.
Muda wowote kuanzia sasa mtaona video yao ambayo inatokana na hii picha niliyowapostia, Vibaraka wa Nduli Idd Amin Mama wanahangaika sana.😂😂😂
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 27
Anaendelea Wakili wa Serikali wakuitwa Wisdom.
Wisdom : Ulipokuwa unasema wasaidizi wako watekeleze kwa mujibu wa sheria? Maana yake nini?
Bwana Jela: Kufanya kwa mujibu wa sheria tu. Kama mchungaji anaingia kwa mambo ya kiroho peke yake.
Wisdom: Uliulizwa umeleta kiapo kinzani kujibu majibu ya mjibu maombi wa nne. Ukasema hujaleta? Kwanini.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikuleta kwasababu yeye ni mjibu maombi kama mimi.
Wisdom: Ulisema mawakili wote lazima wakaguliwe maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): kufuata sheria tu. Kuandika comment au kutoandika kunazuia sheria.
Wisdom: hebu eleza huwa mnakaguaje nyaraka?
Ntamamiro (Bwana Jela : mfano kitabu tunakagua kuangalia kuna kitu chochote hatari ndani yake.
Wisdom: Nimemaliza.
Anasimama Narindwa Wakili wa Serikali.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani walioleta maombi ni akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela: Kulwa Maduhu, Nashon na Kisabo.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani Maduhu mlimzuia asiingie?
Ntamamiro (Bwana Jela: Hakuwepo kwenye orodha na pia hakukuwa na ombi kutoka kwa Lissu.
Wakili wa Serikali Narindwa : Nimemaliza na tumemaliza, hatuna la ziada.
Majaji wanaandika.
Jaji Rumisha Anamuuliza Seka. Mnataka kusema kuwa mnahitaji mawakili wawe na chumba chao au mnahitaji haki ya msingi ya faragha ya mawakili inalindwa?
Wakili John Seka : nafikiri tudeal na soft part of it. Haki ya msingi ni nini sio lazima chumba kiwepo.
Anasimama Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji msiwe na shaka vyumba vinaweza kuwepo.
Mimi naishi Ukonga na pale ukonga kuna vyumba havinaga kazi kabisa. Mfano viko vyumba viwili vya Mahakama ya mtandao. Huwa sio kila siku kuna kesi kama waliweza kuwa na Mahakama ya mtandao pale na vyumba vyake vipo kwanini chumba maalumu kabisa cha mawakili kisiwepo?
Jaji Rumisha: Nafikiri tutajielekeza kwenye kuhakikisha haki inalindwa sio lazima majengo.
Jaji Mruma anasemam sasa Maombi ya Msingi tulisema yatasikilizwa kwa njia ya maandishi.
Na scheduling order itakuwa kama ifuatavyo.
Submission za petitioners zitakuwa ni kabla ya Tarehe: Watajibu PO na kufile submission in chief yao. Kabla ya Tar. 24/08/2026. Rejoinder ya Petitioners kwenye majibu yao 07/09/2026.
Respondets Submission zao zitakuwa ni Tarehe: Submission P.O before 10/08/2026. Wataleta rejoinder ya PO na reply yao 07/09/2026.
Mention kabla ya uamuzi ni 16/09/2026.
Mhe. Lissu anasimama anasema na mimi mseme naleta majibu yangu lini?
Jaji Rumisha: Sasa na wewe kwenye PO ambayo wamewekewa waleta maombi unataka kujibu kama nani wakati wote ni washitakiwa au wajibu maombi?
Jaji Mruma: Amedakia, Mimi nakuelewa Lissu hata kwenye kesi za kawaida za madai defendants wanaweza kuwa na madai dhidi yao wenyewe na ikasikilizwa. Kwahiyo Lissu uko sahihi na tutakupatia haki hiyo hakuna shida.
😂😂😂😂Kwa kifupi Mruma ameingilia show. Naambiwa huyu Mzee ni miongoni mwa Ma Jaji senior sana wa Mahakama Kuu na uwezo wake ni mkubwa sana. Serikali imeshindwa kumpandisha cheo kwenda Mahakama ya Rufani kwasababu yeye huwa sio Chawa kabisa. Ni Mzee anayejielewa sana na yuko serious.
Tumekuwa tukishuhudia kesi nyingi hapa Mahakama kuu kwa mara ya kwanza tumeshuhudia Jaji ambae kwakweli anajua kazi yake.
Anasimama Wakili Ukashu anasema Mh. Jaji na mimi interested party hujatutaja kabisa? Tunafile lini?
Anasimama Narindwa anasema hata sisi tunashangaa huyu Ukashu na TLS wanataka kujibu PO wao ni akina nani?
Jaji Mruma: Sasa sikilizeni msichanganyikiwe. Sisi wengine tumekaa humu miaka 30. Mimi nimefanya hizi kazi mwaka wa 30 huu. Hakuna jipya. Wewe Ukashu utatumia tarehe za 4th Respondent kujibu. Msichanganyane kabisa.
Naahirisha kesi kwa tarehe nilizosema.
NB. Nakuomba usisahau kuchangia #ToneTone ili kufanikisha BARAZA KUU.
M-Pesa
Namba: 0744446969
Jina: CHADEMA HQ
NMB Bank
Namba ya Akaunti: 22606600140
Jina la Akaunti: Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 26
Tumerejea baada ya Mapumnziko ya nusu saa.
Anaanza Wakili wa waleta maombi Adv. Emmanuel Ukashu kumuhoji Maswali Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Ukashu: shahidi umewahi kuisikia TLS?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio naifahamu.
Adv. Ukashu: Ili mtu aingie Gerezani inahitajika wewe ndio umruhusu aingie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Ukashu: Ni sahihi ukipewa maelekezo yoyote lazima utekeleze na Kamishna General?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi
Adv. Ukashu: Maelekezo kutoka juu maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni maagizo ya kiutendaji unayopaswa kutekeleza.
Adv. Ukashu: Usipoyatekeleza unaweza kufukuzwa kazi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kwa mujibu wa sheria.
Adv. Ukashu: Unaweza kumbishia Boss wako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Siwezi kufanya hivyo.
Adv. Ukashu: Soma SUPP 4 tar. 12/03/2026 entry no. 8 hebu isome hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela): Huruma Tehejas mfungwa aliyekuja kumtembelea ni mfungwa na shida ya kisheria. Maoni hapakujazwa. Na sahihi hamna.
Adv. Ukashu: Sasa alienda wapi huyu Wakili kama hakuna uliposaini na maoni hukuweka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nilisahau kujaza na naamini hakukataliwa pia.
Watu wanacheka. 😂😂😂😂
Adv. Ukashu: Kwanini usifukuzwe kazi kwa uzembe wa aina hii? Maana haijulikani alikuja kufanya nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nifukuzwe tu kazi kama unaweza kunifukuza. Fanya hivyo ila mimi nimesema nilijisahau.
Adv. Ukashu: Unafahamu kazi ya uwakili ina maadili yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila kazi ina maadili.
Adv. Ukashu: Maadili ya magereza tumeshayaona hapa hujajaza nyaraka na hujui wakili alipoingia alielekea wapi? Sasa tuzungumze maadili ya mawakili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : siyajui mi sio wakili.
Adv. Ukashu: Unaijua Mandela Principle?
Ntamamiro (Bwana Jela): yes
Adv. Ukashu: soma hapa inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Mfungwa atazungumza na wakili wake kuwa atazungumza bila kikwazo.
Adv. Ukashu: Umeitekeleza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inasema nizingatie sheria za ndani pia?
Adv. Ukashu: Sasa tuambie ni kifungu gani cha sheria ya ndani ambacho kiko kinyume na Mandela Principle.
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakipo.
Adv. Ukashu: Nimemaliza. Naomba Wakili Neema aendelee.
Anasimama Wakili Neema Saruni.
Adv. Neema Saruni: Nitakuwa sahihi nikisema mtu anayekuja kumuona mfungwa anapaswa kuwa na sababu ya msingi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi kwa mujibu wa Sheria.
Adv. Neema Saruni : Ulisema mjibu maombi wa nne alikuwa na orodha yake hivyo basi alipotokea hayupo mlimrudisha?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio tulifanya hivyo.
Adv. Neema Saruni : Nitakuwa sahihi nikisema hamkumpatia haki yake ya kusikiliza.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sahihi.
Adv. Neema Saruni: Nilipokuja mimi kumuona Lissu nilikuwa kwenye orodha yake?
Ntamamiro (Bwana Jela): Haukuwepo.
Adv. Neema Saruni : Nilipofika ikawaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): tulienda kumuuliza lissu.
Adv. Neema Saruni : akasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Akaruhusu ukamuone.
Adv. Neema Saruni: Kwanini huyo mwingine mlimrudisha bila kwenda kuuliza Lissu anasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hapo sasa ndio kuna utata.
Watu wanacheka 😂😂😂
Adv. Neema Saruni: Nimemaliza.
Haya wanasimama mawakili wa Serikali, anaanza Wakili wa Serikali anaitwa Wisdom
Wakili wa Serikali Wisdom: Ulitekeleza majukumu yako kwa mujibu wa nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): masharti yapo kwenye sheria ikiwemo PSO.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba asitaje kabisa PSO maana jana haikuwepo na hatukumuuliza. Asiulize. Sect. 156(3) ya Evidence Act iko wazi kuhusu Re- examination.
Jaji: Sasa Wakili wa Serikali Wisdom uko tayari kuendelea na njia hiyo ili tumruhusu Lissu nae aanze kuuliza kwenye PSO.
Wakili wa Serikali Wisdom: Naomba tu niishie hapo. Sitaendelea mbele.
Watu wanacheka 😂😂😂😂
Part 27 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 25
Wakili wa Waleta maombi Edson Kilatu anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Kilatu: Ni sahihi ili tujue maduhu ni muongo anasema alifika Ukonga lakini hakufika kumbe ulipaswa kuleta kitabu cha watu wanaohudhuria ukonga wakifika pale getini wanaandika.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Kilatu: Umeleta?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijaleta.
Adv. Kilatu: unakumbuka kuhusu huwa hamsomi nyaraka anazopelekewa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Adv. Kilatu: umeleta kiapo chochote cha unaowatuma kusimamia kuwa wanasema hatujawahi kusoma nyaraka za Lissu tukitekeleza majukumu yetu.
Ntamamiro (Bwana Jela): nimeleta mimi kwa niaba yao.
Adv. Kilatu: Lissu alipeleka orodha ya mawakili wa kumtembelea?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Kuruhusu watu kumuona sio lazima wawepo kwenye orodha?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio kuna mazingira alikuwa anaomba Lissu mwenyewe.
Adv. Kilatu: Umeyasema mazingira hayo kwenye kiapo chako au kuna siku Lissu aliomba mtu ambae hayupo kwenye orodha ili amuapishe aingie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijasema kwa kiapo changu.
Adv. Kilatu: unajua maana ya retainership ya mawakili kwa mteja uliyoisema kwenye kiapo chako.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui ila uliza swali tu.
Adv. Kilatu: Basi tutarudi hapo kama hujui.
Soma paragraph nyingine hapo umesema shauri hili lilipaswa kuwa judicial review sio la kikatiba?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Una uelewa wowote kuhusu Judicial Review?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina uelewa wa hili.
Adv. Kilatu: Basi sitakuuliza kwenye hilo nikuache.
Sasa nenda kwenye originating summons soma ibara za Katiba zilizotajwa humo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : zipo ibara ya 13 na zingine.
Adv. Kilatu: Asome ibara ya 30 aielewe halafu nimuulize swali.
Jaji: Asome au ajisomee?
Adv. Kilatu: Ajisomeee mwenyewe aelewe halafu nimuulize swali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tayari
Adv. Kilatu: Je ibara hiyo inasema mtu anaweza kuja kwa judicial review mahakamani kupitia ibara hiyo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hapana.
Adv. Kilatu: Soma para 4 ya kiapo chako kuwa ulimkataaa Kisabo kwasababu sio wakili wa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela): lakini baadae lissu alileta ombi maalamu.
Adv. Kilatu: Sasa muambie Jaji hiyo paragraph nyingine uliyosema kulikuwa na ombi maalumu ni paragraph ya ngapi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haipo.
Adv. Kilatu: Sasa ili wakili aingie gerezani ni lazima kuwepo na orodha ya mawakili iliyoandikwa na mfungwa.
Ntamamiro (Bwana Jela): Utaratibu ni kukagua kitambulisho na kumruhusu.
Adv. Kilatu: Sasa kwenye kiapo chako ukimjibu Maduhu unasema kulikuwa hakuna proof of retainership? Hiyo ndio requirement ya sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nafikiri sifahamu.
Adv. Kilatu. Nimemaliza. Mh. Jaji.
Jaji twende mapumnziko kwa nusu saa.
Tukutane hapa baada ya dakika 30.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 24
Anaendelea John Seka
Seka Anamuongelesha anasema unanisikia au hunisikii. Anatumia sauti ndogo sana. Umenisikia?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nakusikia
John Seka: Pale ofisi ya Admission si kuna Meza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ukubwa wa meza zilizopo hapo admission ukoje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sikumbuki.
John Seka: Katika maisha yako uliwahi kumuona wakili na mteja wake gerezani wanaongea?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Huwa wanakaaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wanakaa kutazamana katikati yake kuna meza?
John Seka: Sasa narudi hapo. Kabla ya kesi hii uliwahi mfahamu Nashon Nkungu, Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nimewahi kukutana nao.
John Seka: Ulikutana nao wapi? Katika mazingira yapi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Akija kuongea na mteja wake gerezani.
John Seka: Ulituambia stage za wakili akifika. Anaandika jina nje, kitabu kinaletwa kwako. Unaruhusu. Sasa tuambie unamuona wakati gani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ofisi zote ni zangu.
Jaji: Jibu ni wapi hapo Gerezani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nilikutana nae Kwa Recha.
John Seka: Kumbe hata Kisabo ulimfahamuje?
Ntamamiro (Bwana jela) : hivyo hivyo kumuona akizungumza na mteja.
John Seka: Umewahi kuwaona wakifanya mahojiano?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Umekumbuka wakati Lissu anafanya mahojiano nani na nani anakuwa ndani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wanakuwa nje wote. Lakini wanachungulia kwa mlangoni.
John Seka: Unakumbuka tarehe ipi na ipi ulikuwepo na ipi haukuwepo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Siwezi kukumbuka.
John Seka: Sasa nitakupitisha tarehe moja hadi nyingine?
Jaji: Amesema hakumbuki nafikiri huko muache acha libaki hivyo.
John Seka: Nitakuwa sahihi nikisema wewe hujawahi hudhuria majadiliano kati ya Lissu na mawakili wake?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Mengi yaliyotokana na hayo wewe hukuwa unahusika moja kwa moja zaidi ya mrejesho.
Ntamamiro (Bwana jela): sio lazima feedback
John Seka: wewe hujawahi hudhuria mazungumzo ya Lissu na wanasheria wake. Huwa unapita tu. Unayoyaona.
Ntamamiro (Bwana jela) : nakagua napita.
Jaji: Hebu sikia kati ya wewe na hao akina Recha, Mumbii anaeweza kuelezea?
Ntamamiro (Bwana jela): Ni sahihi.
John Seka: Sasa tutajie majina yake.
Ntamamiro (Bwana jela): Siwakumbuki.
John Seka: Wakati wote maelekezo yako yalikuwa yanafuatwa ukiwaagiza kwenda kusimamia?
Ntamamiro (Bwana jela) : Mimi ni Mkuu wa Gereza sio lazima niambiwe feedback naweza kujua kwa namna nyingine.
John Seka: Kumbe ulijua kuwa mahojiano na Lissu na mawakili wake yamefuata taratibu kupitia mbinu zako zingine.
Ntamamiro (Bwana jela) : ndio
John Seka: Hao waliokufikishia hizo taarifa au hizo mbinu zako zingine umezielezea kwenye kiapo chako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hapana.
John Seka: Paul Kisabo na Nashon Nkungu. Wakiwa kwenye mahojiano kunakuwa na askari wanakaaa kulia na kushoto kwa Lissu na Kwa Nashon na kisabo nyakati zote.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
John Seka: Ulikuwepo muda wote mahojiano yanapofanyika?
Ntamamiro (Bwana jela) : Napata taarifa kupitia vyanzo yangu.
John Seka: Nimemaliza Majaji. Aendeleee Edson Kilatu.
Anasimama Wakili Edson Kilatu
Adv Kilatu: Ukifika ukonga getini kuna kitabu cha ku register magari?
Ntamamiro (Bwana jela): Sahihi
Adv Kilatu: Anayeshughulikia registration zote sio wewe kwenye vitabu vya kuingia vya magari, raia wa kawaida na kitabu cha mawakili?
Ntamamiro (Bwana jela): Ni sahihi
Adv. Kilatu: Ni sahihi hakuna kiapo cha mtu anayesimamia hizo registration pale Ukonga? Hakijaja hapa mahakamani.
Ntamamiro (Bwana jela) : Hakipo.
Adv. Kilatu: Hii Register book uliyoileta hapa Mahakamani SUPP 1,2,3 ni nyaraka ya magereza hakuna sahihi za mawakili mle. Ni nyaraka yenu tu.
Ntamamiro (Bwana jela): sahihi
Part 25 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 23
Wakili wa waleta maombi John Seka anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Andrew Shaban Ntamamiro (Bwana jela)
John Seka: Moja ya sheria ni sheria ya magereza ambae umeisomea na kuibobea?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
John Seka: Kanuni za magereza je?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nazo ni muhimu sana. Zinatumika.
John Seka: Kwenye kanuni hizo unapaswa kutii kanuni ya 13 ya uendeshaji wa kanuni za Magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ibara ya 29(1) inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : Kila mtu anayo haki ya msingi ya kufaidi haki za binadamu kama zilivyofafanuliwa ibara ya 12 hadi 28 ya Katiba hii.
John Seka: Ni nani na nani wana haki ya kufaidi haki mbalimbali?
Ntamamiro (Bwana jela) : Watu wote.
John Seka: Hata wewe?
Ntamamiro (Bwana jela) : hata mimi.
John Seka: Hata Tundu Lissu:
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Lissu.
John Seka: Hata Kisabo?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Kisabo
John Seka: Hata Maduhu na Nashon
Ntamamiro (Bwana jela) : Hata Maduhu
John Seka: Nashon Je?
Ntamamiro (Bwana jela): Hata Nashon.
Watu wanacheka. Wanamuona zamwamwa sijui 😂😂😂
John Seka: Haya rudi ibara ya12 sasa kule.
John Seka: soma ibara 29(2) na useme inasemaje?
Ntamamiro (Bwana jela) : kila mtu ana haki ya kupata hifadhi sawa chini ya sheria.
John Seka: Hadi Lissu akiwa mikononi mwako Ukonga?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sahihi
John Seka: Nenda Kanuni ya 13 ya kanuni za Magereza na utuambie miaka 31 ya uzoefu wako ni lini uliifahamu kanuni hii?
Ntamamiro (Bwana jela) : Tangu nilipoanza Kazi.
John Seka: Isome kwanza.
Ntamamiro (Bwana jela) : mfungwa atapewa haki ya kuongea na wakili wake kwa faragha lakini awe anaonekana lakini sio kuwasikiliza.
John Seka: Umeielewa kweli hicho kifungu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio mfungwa atapewa nafasi ya kuongea na wakili wake na kufanyika kwa kuona lakini sio kusikiliza.
John Seka: Kuna haki ya mfungwa na kuna haki ya mshauri wa kisheria kwenye kanuni hiyo?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Haki ya mfungwa kusaidiwa kupewa nafasi ya kuongea na mshauri wake wa kisheria yaani Wakili.
Ntamamiro (Bwana jela): Ndio
John Seka: haki ya pili ni ya mawakili kupata fursa ya kuongea na mfungwa kwa faragha bila ya kusikilizwa ni kutazamwa tu.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Hii haki huwa unasomewa au ni uzoefu? Hii kanuni ya 13.
Ntamamiro (Bwana jela): Sijaelewa swali.
Seka: ili uwe na ujuzi huo wa kutazama bila kusikiliza kuna chuo kinachofundisha? Au ni uzoefu wa kazi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Katika uzoefu wa kazi unasema hapa natazama na sisikilizi.
John Seka: Kwahiyo utekelezaji wa jambo hili unategemea mtu na mtu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hakuna standard zilizowekwa.
John Seka: Kwenye nyaraka zako na maelezo yako ulikuwa unasema simamia? Maana yake ulikuwa unasema simamia lakini wasisikilize.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio.
John Seka: Ukubwa wa Chumba cha Ofisi yako ukoje?
Ntamamiro (Bwana jela) : wakutosha tu.
John Seka: Huwezi kukadiria?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ndio
Jaji: Ofisi yako hujui ina ukubwa gani?
Ntamamiro (Bwana jela) : Wakutosha.
Jaji: Tunatosha wote humu ndani tukija ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hamuwezi kuingia.
Jaji: Bado unasema ni ukubwa wa kutosha?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio
Jaji: Haya jibu swali sasa.
Anasimama Nalindwa Sect. 93 ya Prison Act inasema ramani ya gereza isitolewe. Ukubwa wa hizo ofisi ni hatari.
Jaji Mruma: Hakuna ramani ya gereza wala kifungu hakisemi hivyo. Shahidi jibu swali tunataka sana kujua ukubwa wa ofisi yako ni jambo muhimu sana.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni ofisi iko umbali kutoka hapa nilipo hadi hapo kwako.
John Seka: Sasa ofisi yako ya kaimu wako Recha ni ofisi ya nani kubwa?
Ntamamiro (Bwana jela): Yakwangu ndio kubwa.
Part 24 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Leo July 23, 2026
Jana tuliishia part 21 so leo tunaendelea na-;
Part 22
Majaji wameingia.
Mawakili wapande zote mbili wapo na Mhe. Lissu nae yupo.
Karani anasoma maombi hapa.
Leo tunaendelea na Maswali ya Dodoso kwa Shahidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga ambae Andrew Shabani Ntamamiro (Bwana Jela)
Jaji anauliza kama pande zote ziko tayari. Wanakiri wako tayari.
Jaji sasa na nyie watu wa TLS ninawaruhusu mtapata nafasi ya ku cross.
Anaanza John Seka Wakili wa Waleta maombi.
John Seka : Umekuja kwa niaba ya Gereza la Ukonga
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Una muwakilisha pia kamishna wa magereza Tanzania.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Unamuwakilisha pia Mwanasheria mkuu wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
John Seka: Wameona unafaa kabisa kuwawakilisha wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Unafahamu Katiba ya Tanzania na haki inazotoa zile za Binadamu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Soma ibara 13 inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Watu wote ni sawa mbele ya sheria
John Seka: Watu hao ni pamoja na Lissu hivi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Jaji mbona hatumsikii.
John Seka: Afande tumia MIC halafu tumia ile sauti yako ya kijeshi.
John Seka: Jeshi la magereza lina wajibu wa kulinda raia pia?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Jeshi la Magereza ni miongoni mwa vyombo vya serikali vinavyopaswa kulinda haki za binadamu
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Pia haki za mawakili zinatakiwa kulindwa na kuamuliwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Msimamizi wa gereza za Ukonga wewe ndio msimamizi mkuu wa haki hizo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Wajibu huo wa Kikatiba umeutekeleza umeutekeleza kipindi chochote ambacho sisi tunakilalamikia hapa mahakamani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Kifungu cha 13(6)(a) inasema kuhusu haki ya kusikilizwa unafahamu?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio.
John Seka: Kumbe kwa mujibu wa Katiba hii unapaswa kutoa fursa ya kumsikiliza mtu kabla ya kufanya maamuzi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: Wakati unatekeleza majukumu yako, Bwana Tundu Lissu alikuwa na haki ya kusikilizwa kwa ukamilifu?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
John Seka: je hawa waleta maombi watatu walikuwa na haki hiyi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Ibara ya 16 inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Utaratibu wa sheria utawekwa kuhusu hali ya mtu ya faragha na mambo yake ya faragha bila kuathiri sheria.
John Seka: Kwa mujibu wa ibara hiyo mamlaka mbalimbali zinazoweza kuingilia faragha ya mtu kwa kufuata taratibu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Je mawasiliano binafsi ya mtu ni faragha pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Wakati wote wakati mtu atamnyima mfungwa haki ya faragha anajua kama anaingilia na kuvunja ibara ya 16?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
John Seka: Je wakati unashugjulika na Tundu Lissu ulijua ibara hii ipo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nimetekeleza hilo.
John Seka: Ibara ya 22(1) ya Katiba ya Tanzania inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kila mtu ana haki ya kufanya kazi.
John Seka: Wewe kazi yako unayoifanya ni haki yako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Kumbe na Mawakili pia wana haki ya kufanya kazi yao vilevile hadi ndani ya Magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Na mawakili hawa walalamikaji kuja ukonga ni kuja kazini kwao pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
John Seka: Soma ibara ua 26(1) inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila mtu ana wajibu wa kufuata sheria
John Seka: Kila mtu maana yake hadi wewe? Au wewe haupo kwenye kila mti.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hadi mimi.
John Seka: Una wajibu wa kuheshimu sheria za nchi kumbe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Part 23 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 21
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana jela)
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kuwa maafisa Magereza. Wanapaswa kukagua barua inayotoka ndani au kuingia ndio inapaswa kusomwa.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Soma kifungu cha 46 Cha Sheria na kanuni ya 10 na 11 ya kanuni za Magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Anahangaika haoni.
Mhe. Lissu: Sasa wambie majaji kama kanuni ya 10 na 11 inahusu barua wanazoandika na wanazoandikiwa wafungwa.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Na wanaosoma ni wewe au maafisa wako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe, Lissu: Ukiikataa barua unamrudishia na kumwambia sababu. Na kama ikikataliwa kwa aliyemletea pia unamrudishia na kumpa sababu. Na kama barua ni ndefu sana na huyapendi ni sahihi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kama nje ya barua kwa wafungwa au kutoka kwa wafungwa una mamlaka ya kukagua na kusoma nyaraka nyingine yoyote.
Ntamamiro (Bwana jela) : Naomba soma Section 12 ya Prison Act.
Mhe. Lissu: Kwa kanuni hizi unaruhusa ya kusoma nyaraka nyingine.
Ntamamiro (Bwana jela) : Soma kifungu cha 12 cha Sheria ya Magereza
Mhe. Lissu: Unauwezo wa kusoma nyaraka za mawakili wanaokuja nazo magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sipaswi kusoma.
Mhe. Lissu: Hicho kifungu cha 12 unachosema kinahusiana na upekuzi wa magari na kumkagua mtu sio nyaraka ndio maana sitaki hata kukisoma. Hakikusaidii chochote.
Mhe. Lissu: Kisabo alisema wakiwaambia muondoke ili azungumze na mimi mteja wake mnakataa. Kweli au sio kweli.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Na mimi nimesema kwenye viapo vyangu kuwa alikuja Wakili Alute Lissu. Na kusema nina ujumbe muhimu kutoka serikali nataka niongee nae Faragha. Mkamkatalia. Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana jela): Sikumbuki.
Mhe. Lissu: Umekuwa unaendeshwa na rimoti na Kamishna Mkuu na wanasiasa walioko serikalini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Kuna siku umeniita ofisini kwako kuwa kuna ujumbe wa jumuiya ya madola napaswa kupelekwa mjini? Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sina Jibu.
Mhe.Lissu: Siku hiyo aliyekuja kunichukua ni Mangara?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: sio kweli nini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hujawahi kupelekwa.
Mhe. Lissu: Siku nyingine ulinifuata na kusema Katibu Mkuu wa Chama cha Mabunge Duniani amekuja kuniona anaitwa Martin Chungong na nikapelekwe mjini na Senior Mangara.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Kuna siku Heche, Amani na Mnyika uliwaruhusu kutokana na kulikuwa na maelekezo kutoka juu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kabla hujaja walikuwa wanaruhusiwa na ulipokuja ukawazuia hayo mamlaka ulitoa wapi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nimeshajibu.
Jaji: Ulijibuje
Ntamamiro (Bwana jela): Sikuwakataza.
Mhe. Lissu: Alipokuja Lema Godbless, wewe ulipokuja na kutukuta ulimfukuza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Kama sio kweli kwanini haya yote hukuyajibu kwa nyaraka wakati mimi nimeyasema kwenye nyaraka zangu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sina jibu.
Mhe. Lissu: Sasa kama umewazuia walalamikaji watatu, mashahidi wangu, umewazuia mawakili wangu. Unanitakia nini kwenye kesi ya uhaini inayonikabili ambayo adhabu yake ni mimi kunyongwa?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nilishajibu.
Jaji Mruma: Umejibu nini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sijamzuia mtu yeyote kuja kuonana na Tundu Lissu.
Mhe. Lissu: Sina swali lingine.
Majaji wanamuuliza Wakili wa Serikali.
Anasema naomba tuahirishe tuendelee kesho.
Wakili John Seka: Naomba tuendelee bado muda tunao.
Jaji Mruma: Sasa hoja ya kuahirisha na logistics zilivyo, TLS nao kupewa nafasi wamuhoji shahidi. Sisi tunaomba kusema yafuatayo.
Leo tutaahirisha kutokana na sababu kama za jana, tunaamini leo tumefanya kazi kubwa, kesho tutasema mengine.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 20.
Mhe. Lissu anaendelea kumshona Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Wakati wote mawakili wakija gerezani, simamia, wapekuliwe na wamepekuliwa. Swali ni kwamba ni je wewe Bwana jela wa Ukonga unawashuku na una wasiwasi na mawakili 37 waliokuja kuona wateja Ukonga? Kumbuka kanuni inasena ili uwasearch ni lazima uwe na wasiwasi nao.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sitegemei kanuni.
Mhe. Lissu: Sasa twende kwenye sheria yenyewe kwenye Prisons Act kuwa unaweza kusearch mgeni kama hautakuwa na wasiwasi nae? Kifungu gani hicho?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa Majaji mtu yeyote anayeingia Gerezani awe mfungwa au mahabusu lazima apekuliwe.
Mhe. Lissu: Lazima apekuliwe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yuko kimya.
Mhe. Lissu: Kama kweli ni lazima. Twende kwa Mawakili wa Serikali waliokuja Ukonga kama uliamuru wapekuliwe. Twende kwa hao sasa. Wah. Majaji SUPP 4 tarehe 19/11/2025 nenda haraka tumalize hii ngoma. Na Tarahe 21/01 mwaka huu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kila anayeingia lazima akaguliwe.
Mhe. Lissu: SUPP 4 inasemaje kuhusu Tarehe 19/11 walikuja mawakili wafuatao Debora Mushi kutoka NPS, Caroline Nana kutoka NPS pia, Cleoface Leonce ambae ni investigator na alikuja Justo Dimba au Simba kutoka kwa ZCO. na mwingine kutoka DCEA. Wote hawa shida walioijia gerezani walikuja kuongea na mahabusu. Maoni yako ukasema nini? Wasomeee majaji.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Wasikilizwe kwa utaratibu.
Mhe. Lissu: Wakija mawakili wengine simamia mazungumzo yao, wapekuliwe, wapekue, Simamia kwa ukaribu. Lakini wa serikali wakija wasikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Mawakili 37 wote nipe mfano mmoja tu w wakili uliyesema asikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Naomba Tar. 20/01 wakili hapo nimesema SIMAMIA.
Mhe.!Lissu: Ahsante sana. Sasa kwa mawakili wa serikali wapi hata mara moja umeandika SIMAMIA?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio lazima niandike.
Mhe. Lissu: Wabelgiji nilipokaa wanasema Papiere yaani Paper. Tunaenda na maandishi. Onesha maandishi acha rongorongo maneno mengi unatumalizia.
Sasa angalia majina yanayofuata. Hapo kuhusu mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela): Niliandika Waletwe.
Mhe. Lissu: Maafisa wa Madawa ya kulevya na Mawakili wao waliokuja 28/11 kazi yao ni kutukamata na kutupeleka Mahakamani ndio unaosema wasikilizwe?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hatoi jibu.
Mhe. Lissu: Hawa watu ni watumishi wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wanalipwa mshahara wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio lakini.
Mhe. Lissu: Lakini utawapa mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa mawakili wa serikali huwa wanakuja kuongea na wote?
Mhe. Lissu: tuambie ni wapi umeandika kuwa walikuja kuongea na wote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijaandika.
Mhe. Lissu: Ni sahihi kuwa kuna wakati nyaraka zinakataliwa na zinazokubaliwa lazima mseme zote. Kweli sio kweli mnafanya hivyo kwa mawakili wangu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sio kweli zinasomwa. Ila zinakaguliwa.
Mhe. Lissu: la kwamba zinakataliwa pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Katika nyaraka ambazo zinaletwa kwangu ni pamoja na hotuba ya Chande ya matukio ya tar. 29/10?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Lissu: Shahidi Paul Kisabo amesema wiki iliyopita Tar. 14/07 alikuletea waraka unaotoka common wealth kuwa niachiliwe ndani ya siku 30 na mliposoma mkakataaa.
Bwana Jela: Sio kweli.
Part 21 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 19
Mahakama Imerejea.
Majaji wameingia.
Wakili wa Serikali amesimama kujitambulisha anaitwa Narindwa Sekimanga.
Shaidi Mkuu wa Gereza nae yuko pale kizimbani yeye muda wote amekaa tu pale kizimbani.
Hajajihangaisha kusimama labda kwa vile ni mrefu na hicho kitambi anachoka kusimama pengine.😂
Jaji Mruma: Shaidi nakukumbusha bado uko chini ya kiapo.
Mhe Lissu: Sasa turudi kwa viongozi wangu wa Chama uliowakatalia wasije kuniona kule Gerezani. Angalia majibu yangu na uangalie kiapo kinzani kuhusiana na kiapo kinzani nilichomjibu Kisabo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ametoa macho. Hafanyi lolote.
Mhe. Lissu: Mawakili wa Serikali mnafanya nini si mumsaidie shahidi wenu azione hizo nyaraka naona ananiangalia tu.
Wakili wa Serikali anaenda.
Mhe. Lissu: Hizo aya kwenye kwenye kiapo changu kinzani zinaonesha namna ulivyowazuia viongozi na wanachama ikiwemo mashahidi na mawakili watatu ambao ni Dickson Matata, Deogratias Mahinyila na Gaston Garubindi. Swali langu waeleze majaji kama umewahi kupinga haya maelezo yangu yaliyopo kwenye kiapo changu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa Majaji nimeshalijibu hilo.
Jaji: Umeelewa swali lake kweli.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina jibu.
Mhe. Lissu: Nalo ni jibu pia. Haya kwenye aya ya nne wewe umefanya kampeni ya muda mrefu ya wewe na mlalamikiwa wa pili kamishna mkuu mmehakikisha nashindwa kujitetea wala kuandaa utetezi wangu na matukio nimeyasema kwenye para H na Y. kwamba umewazuia mawakili wangu watatu ambao Ni Mahinyila, Matata na Garubindi kama umewahi kujibu hili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli nimewazuia.
Mhe. Lissu: Je umeleta supplimentary affidavit? Au majibu yoyote kwenye jambo hilo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : anatoa macho. Anashika makaratasi na kuyaacha.
Jaji: Umeelewa swali?
Mhe. Lissu: Ulileta counter affidavit mara ya kwanza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Baadae ukaleta suplimentary affidavit?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Sasa kwenye hizo nyaraka zako mbili kuna mahali kokote ulijibu tuhuma za kuwa umewazuia mawakili wangu na viongozi wa Chama?
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijajibu.
Mhe. Lissu: Tuhuma dhidi yako na maafisa wako kusearch mawakili na nyaraka zao kisheria. Jibu swali kwamba waleta maombi wote watatu wamesema wanasearchiwa, wanakaguliwa na kusomwa hizo nyaraka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Reg. 17(2) ya kanuni za Magereza inasemaje?
Anatafuta hiyo kanuni.
Mhe. Lissu: Ni kweli mgeni anayekuja Gerezani kutembelea mfungwa atasachiwa endapo atakuwa na wasiwasi na huyo mgeni?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Haya isome sasa
Ntamamiro (Bwana Jela) : A prison officer when has any ground suspiciously may direct to search that visitor. Anasoma kingereza kibaya sana.
Mhe. Lissu: Any ground for suspicion may search or cause to search. Kumbe ataamuru asachiwe kama atakuwa na sababu za kumshuku?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Mgeni ataambiwa aondoke akikataa kusachiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kwa mujibu wa kanuni hii ni kweli.
Mhe. Lissu: Anayemfukuza atatakiwa kuandika sababu za kumfukuza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : yuko kimya tena. Hebu rudia swali.
Mhe. Lissu anarudia swali. Si ni lazima uandike sababu za kumfukuza.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Siku mjibu maombi wa Kwanza alipokataliwa kuingia gerezani tar. 28/11 alipokataliwa kuingia gerezani iliandikwa sababu kuwa amekataa kusachiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kwa kanuni hii.
Mhe. Lissu: Tutajie kanuni hizo zingine tuzione? Kwenye kanuni kuna sababu yoyote nyingine kwa mujibu wa kanuni?
Bwana Jela: Sijaipitia kanuni yote.
Mhe. Lissu: Sasa mimi niliyepitia kanuni zote na hakuna sababu nyingine unasemaje?
Bwana Jela: Sina jibu.
Part 20 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
KITUKO KILICHOTOKEA MAHAKAMANI.
Wakati Mkuu wa Gereza yaani BWANA JELA ambae ni Andrew Shabani Ntamamilo alipohojiwa na Mhe. Tundu Lissu kuhusu Kuwazuia kabisa Mawakili kama Vile Deogratias Mahinyila, Dickson Matata lakini pia viongozi wakuu wa Chama akiwemo John Heche, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu wa Chama, John Mnyika na Amani Golugwa ambao ni mashahidi katika kesi ya Uhaini wamekataliwa kuingia Gerezani Ukonga.
Majibu ya Mkuu wa Gereza amesema yeye hajawazuia. Mhe. Lissu akasema basi watakuja kuanzia kesho. Akasema SITAWARUHUSU waingie kwasababu kesi bado iko mahakamani.
Jaji Amir Mruma ndio akaanza kumuhoji kuna amri yoyote ya Mahakama kuwa watu hawa hawapaswi kuja kumtembelea Tundu Lissu? Akasema kwa kiburi tena kuwa SITAWARUHUSU.
Jaji akavua miwani na kumuuliza unataka tufike huko. Uko serious kweli? Akiwa amekasirika sana. Maaskari Magereza walioko nyuma niliokaa nao karibu wamekimbilia nje kucheka.
Baada ya Jaji kukasirika Bwana Jela akaanza kuomba radhi kwa Jaji. Majaji wote watatu wametikisa vichwa vyao na kuonesha wanashangaa mambo haya yanawezekanaje kwenye Taifa lenye sheria na taratibu.
Kesi hii imeendelea tena kutuonesha watawala wa nchi hii wakoje. Ukisikia majibu ya Mkuu wa Gereza unajiuliza kiburi anakitoa wapi?
Ngoja tusubiri maamuzi ya Majaji mwisho wa kesi hii utakuwaje lakini naamini kila mtu anashuhudia uhalisia wa mambo ulivyo katika Taifa letu.
Tuendelee kusubiri lisaa likamilike turudi kuendelea.
Wanachama leo ni wengi mno. Mahakama imetapika. Yupo Makamu Mwenyekiti John Heche, Yupo Katibu Mkuu, Mnyika. Mama Suzan Lyimo, Mwenyekiti BAZECHA, Yupo Boniface Jacob Mwenyekiti Kanda ya Pwani, Dua Lyamzito, Katibu Mkuu BAVICHA, Pamela Massey, Katibu Mkuu Bawacha. Mzee Azaveli Lwaitama, Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Chama na wanachama wengine mbalimbali.
Tutaendelea kuwaleteeni live moja kwa moja mwenendo wa kesi hii kutokea Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es salaam.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 18
Anaendelea Mhe. Lissu na maswali ya Dodoso.
Mhe. Lissu: Karibu ipi ambayo hawasikii?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Unaweza kuwa karibu na usisikie.
Mhe. Lissu: Kuna mawakili jumla 37 ambao umeleta nyaraka zao hapa pamoja na mawakili wangu. Sasa kwenye comment zako umekuwa ukisema simamia kwa karibi, simamia mazungumzo yao. Ni kweli kwa mawakili wote?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli lakini ni kweli naomba niseme ni kweli nimesema comment hizo kwa wote.
Mhe: Lissu: Katika Mawakili wote hao kuna mahali hata pamoja ulipoandika simamieni lakini msisikilize mazungumzo yao?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna
Mhe. Lissu: Je katika mawakili wote 37 umeandika wakiingia ofisini tokeni nje wazungumze ipo sehemu umeandika?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna nilipoandika.
Mhe. Lissu: Kuna mahali kokote umeelekeza kuwa angalieni lakini msisikilize?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna mahali hapo.
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama ni kweli au sio kweli kati ya Tar. 18/04/2025 nilikuwa nazungumza kwenye kioo na mawakili wangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kilikuwepo hicho kipindi.
Mhe. Lissu: Tulikuwa tunawasiliana kupitia simu zilizopo pale?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Je upande anaokuwepo mgeni ndio uko karibu na reception na kuna kachumba ambacho ni control room ya hizo simu zote? na kwenye hiyo control room anakuwepo afisa magereza anayeuwasha na kuuzima. Ili watu wazungumze yeye ndio anaamua hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni kweli.
Mhe. Lissu: Huyo Wakili anapozungumza kuna askari wanakuwepo kumsikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli a
Mhe.Lissu: Je huu upande wangu nakuwa pia na askari wananisikiliza niliotoka nao lockup na wengine wananisikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Lissu: Kwenye hicho chumba kuna CCTV Camera inayorekodi kinachoendelea humo?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli
Mhe. Lissu: CCTV camera hiyo iko controlled ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela): sio kweli.
Mhe. Lissu: Je ni kweli kwamba baada ya matukio ya Oktoba 29 uliniita ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu : Ulivyoniita ukaniambia kuanzia sasa ni marufuku viongozi wa Chadema na wanachama wa Chadema kuja kukutembelea.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Na pia ulisema ni ndugu zako wa karibu tu ndio watakutembelea?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe.Lissu: Na ukasema mazungumzo yako na mawakili yatakuwa kwa mambo ya kisheria tu?
Ntamamiro (Bwana Jela): sio kweli.
Mhe. Lissu: Wakili Gaston Garubindi alikuwa anakuja kunitembelea Gerezani kabla ya Tar. 14/11/2025
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: kuanzia hiyo tarehe hajawahi kuruhusiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela): Simpangii.
Mhe. Lissu: Kuanzia niingie Gerezani Wakili Dickson Matata na Deogratias Mahinyila hujawahi kuwaruhusu waingie gerezani. Huyu Matata ni Mwenyekiti Kanda ya Magharibi na Mahinyila ni Mwneyekiti wa Vijana Taifa hawajawahi kuruhusiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela): Siwalazimishi waje au wasije.
Mhe. Lissu: Kumbe ndio hivyo. Haya Mahinyila na Matata kesho njooni Ukonga.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kesi iko Mahakamani sitawaruhusu
Mhe. Lissu: John Heche, Amani Gorugwa, Katibu Mkuu Mnyika wakiwa kama mashahidi wangu kwenye kesi ya uhaini wamezuiwa kuingia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawawezi kuingia.
Jaji: Hilo la kwamba huwezi kuruhusu umelitoa wapi? Kuna amri yoyote ya Mahakama?
Ntamamiro (Bwana Jela): Siwezi kuwaruhusu.
Jaji Mruma: Tumefikia huko. Unaiambia Mahakama kuwa huwezi kuruhusu na hauna amri yoyote ya Mahakama? Uko serious kweli au hujaelewa ili tufanye maamuzi na sisi sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa majaji naomba radhi.
Jaji anamkata jicho
Mhe. Lissu: Soma hati yangu kinzani kuhusu Nashon Nkungu.
Anasimama Wakili wa serikali tunaomba Break.
Majaji wanashauriana.
Wakili John Seka anasema ni sawa tu.
Mhe. Lissu: Ni sawa.
Jaji basi tukutane mara baada ya lisaa limoja.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 17
Anaendelea Mhe. Lissu
Mhe. Lissu: Na mazungumzo ya Kisabo pia ulisema yasimamiwe kwenye ofisi ya kaimu mkuu wa gereza.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Mhe. Lissu: Na tunakubaliana wale watu wote akina Mumbii, legal officer Stima, Kopro Dani, na akina mama watatu. Je hawa watu wanakuwemo humo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Si kweli. Huwa wanatoka. Wanaacha mazungumzo yafanyike.
Jaji: Lissu umeridhika na majibu ya shahidi.
Mhe. Lissu: Ngoja nataka kukamata watu waongo.
Mhe. Lissu: Kumbe maafisa wote mle chumbani wanatoka nje, sasa soma kiapo chenu ndugu yangu. Nakusomea kwenye kiapo chako
Kiapo kinasomeka kuwa walikuwepo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kuna ambao walikuwepo na kuna ambao walitoka.
Mhe. Lissu: Waliokuwepo ni akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waliosindikiza
Mhe. Lissu: Akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikumbuki
Mhe. Lissu: Waleta maombi wote wamewataja majina akina Mumbii, Koplo. Dani, Akina mama watatu mle ndani, legal officer na mtu wa usalama. Wamewataja majina. Wewe unasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikubaliani nao mimi.
Mhe. Lissu: Twende kwenye ofisi ya Recha ACP. Soma SUPP 4 Tar. 24/12 ulisema alipokuja Kisabo. Asimamiwe kwa kaimu mkuu wa gereza na kusema wayafanyie ofisini ukawataja majina ambao wanapaswa wasimamie. Waeleze majaji kuwa wakati wote Recha anakuwepo, asipokuwepo atakuwepo Mumbii, Mohamed lazima awepo au Hamisi na anakuwepo Stima na maaskari wanaonifuata muda wote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sio kweli
Mhe.Lissu: Umewahi kuhudhuria mazungumzo hayo kwa Recha?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijawahi.
Watu wanacheka. 😂😂😂😂
Mhe. Lissu: Tumewahi kufanya mazungumzo ofisi kwako mimi na mawakili wangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Tar. 12/12 imeandikwa SUPP 6 Umeiona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sioni
Mhe. Lissu: Mawakili msaidieni mmeleta wenyewe.
Ukiiona siku hiyo niliyosema tar. 12/12 ulielekeza hivi kaimu mkuu wa gereza, Mtu wa usalama na mwanasheria wa gereza ulisema mazungumzo yawe ya kisheria zaidi. Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli
Mhe. Lissu: Je hawa uliowaelekeza wote zaidi ya watu watatu walikuwepo au hawakuwepo kwenye haya mazungumzo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawakuwepo.
Mhe. Lissu: Walisikiliza au hawakusikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawakusikiliza.
Mhe. Lissu: Waliwezaje kusimamia mazungumzo wakati hawakuwepo na hawakusikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kuna facial impression.
Majaji wanacheka.😂😂😂😂
Ntamamiro (Bwana Jela): Naomba nifafanue.
Mhe. Lissu: Sitaki unifafanulie. Sasa kama hawakuwepo facial expression walizionaje wakati hawapo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hili suala ni la kisheria tunamkagua wakili kitambulisho.
Mhe. Lissu: Nani kakuuliza hayo.
Jaji: Usitupotezee muda. Hebu soma maelekezo yako kuwa wasimamie mazungumzo na watu hawakuwepo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ukiona wanakumbatiana hayaruhusiwi.
Jaji: Uliwaelekeza wafanye nini kwenye mazungumzo hayo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Walisimama mbali wakawa wanaangalia.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kama kitendo cha kukumbatiana ni maneno au kitendo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni kitendo.
Mhe. Lissu: Ulisema wakasimamie vitendo au maneno?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mazungumzo yaani maneno.
Watu wasonya tu. Majaji pia wamekasirika sana kwa majibu haya. Watu wengine wanacheka kimya kimya.
Mhe. Lissu: Sasa twende SUPP 6 ukurasa unaofuata. Wapo mawakili watatu ambao ni Catherine Chanjarita, Shamumoyo na Constatine kwenye comment zako umesema Adm. Officer simamia mazungumzo yao kwa karibu. Sasa swali langu simamia kwa karibu yanawezekana kutekelezwa bila maaskari hao kuwepo kwenye mazungumzo hayo?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijasema wasikilize nimesema wasimamie kwa karibu.
Part 18 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 16
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza
Mhe. Lissu: Twende Taratibu. Hiki ulicholeta mahakamani ni photocopy?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Original unayo ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Angalia Tar. 29 na Tar. 30 Sept. 2025. Kuna majina ya wageni kabla ya Tarehe hizo wapo wageni hawaonekani walikuja tarehe gani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni kweli
Mhe. Lissu: Hawa watu wanne walikuja tarehe ngapi? Wambie majaji sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haioneshi.
Mhe. Lissu: Wewe unajua sasa? Walikuja tarehe ngapi? Maana original unayo wewe.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tarehe haioneshi.
Mhe. Lissu: Je katika hao watu wa nne. Mtu wa 10 ni nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Paul Kisabo.
Mhe. Lissu: Alikuja kumuona nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : wewe hapo imeandikwa. Alikuja kukuona wewe.
Mhe. Lissu: Soma Tar. 30 Sept. Kwenye karatasi hiyo hiyo. Mtu wa kwanza ni Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Tusiende mbali sasa: Tufafanulie jambo hapa kuna sehemu imenadikwa jina la ndugu, ID no. Simu namba, atokapo mgeni na maoni ya OIC. Sasa hiyo OIC ni Officer in Charge yani wewe hapo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Tar. 30/09 kwenye jina la Kisabo uliandika A/Zamu maana yake Afisa wa Zamu. Na kuna mahali umeandika ADM maana yake ni admission office in charge. Na kuna mahali umeandika IO maana yake intelligence officer?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli kabisa.
Mhe. Lissu: na kuna sehemu umeandika legal unamaanisha Legal Officer Stima.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Hiyo sehemu ya maoni yako ni maelekezo yako kwa hawa niliowataja? Wewe ndio Boss.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila ofisa ana kazi yake. Kwahiyo ni maelekezo yangu kwao.
Mhe. Lissu: Kwahiyo unakuwa umewapa amri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Nenda Kwenye kilelezo SUPP 3 pia ni orodha ya mawakili waliokuja Ukonga. Nashon Nkungu lipo hapo ambae ni mlalamikaji wa pili. Andrew Mathew Chima pia alikuja kuniona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Je Andrew Chima yupo kwenye orodha ile ya mawakili wangu niliowaletea ile SUPP 1?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo. Naomba nifafanue.
Mhe. Lissu: Sitaki. Utawafafanulia wa Serikali.
Haya huko mwisho kabisa KULWA MADUHU yupo au hayupo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yupo namuona hapa.
Mhe.Lissu: Na kule mwisho kwenye maoni yako umesema aruhusiwe mwenye kibali. Maduhu hana kibali huko mbele sioni.
Ntamamiro (Bwana Jela): hayuko kwenye orodha ya mawakili wa mahabusu huyu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kuna sharti lolote la kisheria kwamba mfungwa yeyote mwenye wakili au wakili anapaswa kuwasilisha orodha ya mawakili wake kwa Bwana Jela?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Halipo kisheria. Lakini mfungwa ana haki ya kuchagua nani amtembelee.
Mhe Lissu: Nilichagua kuwa Kulwa William Maduhu na umemkatalia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuwepo kwenye orodha.
Mhe. Lissu: Andrea Chima alikuja kuniona yupo kwenye orodha gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo.
Mhe. Lissu: SUPP 5 twende sasa tar. 24/12/2025 angalia kwenye entry kuna Nashon Nkungu na Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio wanaonekana wote.
Mhe. Lissu: Je Victoria Mgonja alikuja kumuona Jonson Muhanjo. Uliandkka kwenye maoni yako kuwa Adm. Simamia mazungumzo yao. Na mazungumzo hayo yalifanyikia kwenye ofisi ya Admn
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina kumbukumbu yalifanyikia wapi?
Mhe. Lissu: Kwamba tangu juzi tunazungumza kuhusu mazungumzo ya mawakili yalifanyikia wapi hujaenda kutafuta.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijui inaweza kuwa kwa Mkuu wa Gereza au Adm.
Mhe. Lissu: Mazungumzo na Nashon ulisema asimamiwe kwa Makamu mkuu wa gereza na kuwataka wasaidizi wako wanne wasimamie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Part 17 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 15
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Je askari magereza ambae hasikii au hauoni atashuhudiaje mazungumzo ya mfungwa na ndugu zake watakapokuja kumtembelea
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayo ni masuala ya kidaktari.
Mhe. Lissu: Sasa Bwana Jela hujui kama wasaidizi wako wote hao kuwa hujui kama wanasikia au hawaoni wewe ni mkuu wa gereza wa aina gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sik daktari.
Mhe. Lissu: Wewe ni Mkuu wa Gereza wa aina gani? Usiyejua afya za wasaidizi wako?
Ntamamiro (Bwana Jela): Nastahili kuwa kwenye nafasi hii.
Mhe. Lissu: Ndio maana nchi imekwama. Kama watu wenyewe ndio nyie na akili hizi
Mhe. Lissu: Umekuwa Officer incharge tangu lini pale Ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sept. 2025.
Mhe.Lissu: Ulihamishiwa Ukonga ukitokea gereza kuu la maweni Tanga?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio.
Mhe.Lissu: Ulikuja ukonga kuchukua nafasi ya Juma Mwaibaku?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli.
Mhe. Lissu: Ulipohamishiwa Ukonga mimi tayari nilishakuwa mahabusu ukonga toka April 2025?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta nakaa kwenye special wing pale ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wakati unahamia pia ulinikuta naishi huko pamoja na wafungwa wa adhabu ya kifo 100?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sikuwakuta.
Mhe. Lissu: Je ulinikuta nakaa peke yangu au sio peke yangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio peke yako.
Mhe. Lissu: Wafungwa gani hao?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mmoja.
Mhe. Lissu: Je kwa miezi 5 ambayo hukuwepo nilikuwa naishi na wafungwa wa kifo takribani 100?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sifahamu.
Mhe. Lissu: Umeona record ya maandishi ya waliokuwepo special wing umeiona au hujaiona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijapitia hiyo records.
Mhe: Lissu: Hili suala nilishalilalamikia na lipo kwenye nyaraka za mahakama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu. Tuendelee na maswali mengine.
Mhe/ Lissu: Utaratibu wa wageni kuja kuniona ni weekend?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: Utaratibu wa wageni wangu kuja kuniona weekend ni kwamba siku moja wanakuja ndugu zangu na siku nyingine wanakuja viongozi wa Chama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu.
Mhe.Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta utaratibu wa kutembelewa na mawakili wangu ilikuwa nimepeleka orodha kwa mkuu wa Gereza kwa mkuu wa gereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Orodha ya kwanza uliiambatanisha kwenye hati yako ya kiapo kinzani ile ambayo nilikuwa na mawakili 10.
Ntamamiro (Bwana Jela): Orodha hiyo hiyo moja.
Mhe. Lissu: Kwahiyo hakukuwa na orodha yenye jina la Deogratias Mahinyila, Paul Kisabo na Dickson Matata na Mary Stephano.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna hiyo.
Mhe. Lissu: Angalia kielelezo SUPP 1. Ukishakiona niambie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Anapekenyua hapa..
Mhe. Lissu: Jina la Nashon Nkungu limo kwenye hiyo orodha lipo au halipo? Ambae ni mleta maombi wa pili.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio lipo.
Mhe. Lissu: Je jina la Kisabo na Maduhu mawakili wangu yapo au hayapo kwenye hiyo SUPP 1
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa hawapo kwenye hii orodha.
Mhe. Lissu: Sasa hao wawili wamesema kwa kiapo na kusema hapa Mahakamani kuwa kabla hujahamia ukonga walishaingia gerezani kuonana na mimi walishaingia karibia mara tatu. Wewe unasemaje? Yaani wakati ACP Juma Mwaibako akiwa Mkuu wa Gereza walihudhuria
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulikuwepo wakati huo?
Bwana Jela: Sikuwepo wakati huo. Ila nyaraka zinasema.
Mhe. Lissu: Nenda kielelezo ambacho ni SUPP 2 hapo.
Jaji: SUPP 2 ni nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hiki ni kiambatanisho na. 2 kinahusu orodha ya wageni na mawakili waliotembelea gereza la Ukonga.
Part 16 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.