Usidanganyike na wingi wa maombi,sala na kufunga.
Kipimo cha kweli cha imani si maneno yako mbele za Mungu, bali matendo yako kwa watu. Unawezaje kumpenda Mungu usiyemuona, huku ukimchukia ndugu na jamii yako? Upendo wa kweli huonekana katika huruma, heshima na matendo mema, hapo ndipo roho yako inajidhihirisha mbele za Mungu. Kufunga na kusali kusiko tafuta upendo,haki, wema,uadilifu na huruma ni mgomo wa kula.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 157
Anamalizia Mhe. Lissu
Vinginevyo haitakuwa Mahakama ya Haki na kanuni zinataka usikilizwaji wa mashauri haya uwe wa haki kwa pande zote.
Ni hayo tu waheshimiwa majaji.
Anamaliza Mheshimiwa Lissu hapa.
Majaji wanateta huku wakiandika kidogo.
Mheshimiwa Lissu anakusanya makabrasha yake taratibu hapa. Bila shaka kesi itaahirishwa leo. Watahitaji kuandika uamuzi wa hoja zilizowasilishwa.
Anawasha kipaza sauti Jaji Ndunguru hapa akiwa serious sana na kama amechoka. Anaonesha hana nuru kabisa. 😂
Naomba niseme yafuatayo kabla sijaahirisha shauri.
Mtakumbuka leo tumevumiliana sana kuhusu simu zinazopiga kelele kama tunashindwa kukaa na simu basi kwenye ukaguzi tutaomba mziache.
Naomba mtambue uvumilivu wa leo hautaendelea kuwepo kuhusu masuala ya simu.
Shauri linaahirishwa hadi Tarehe 11/02/2026 saa tatu asubuhi.
Naomba Repost yako.
UTANGULIZI KUHUSU KESI YA MHE.LISSU.
Leo ni February 9, 2026 tunaendelea na Kesi ya Uhaini Na. 19605 inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa itaendelea Katika Mahakama kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dar es salaam.
Kama mnakumbuka vizuri tuliishia shahidi Na. 4 ambae ni P11 yaani shahidi wa siri.
Alivyoingia Mahakamani Novemba 11, 2025 shahidi huyu wa siri hakuonekana kokote hata kwa Majaji ndio Mheshimiwa Lissu akaweka pingamizi kuhusu kibox kilivyowekwa na namna ambavyo sheria inahitaji shahidi wa siri kutoa ushahidi wake.
Lakini pia katika pingamizi lake alielezea kuhusu kanuni za ulinzi wa mashahidi zinataka lazima shahidi wa siri atajwe na amri husika iliyoamua kuwa shahidi huyo awe wa siri lakini katika amri iliyopo mahakamani shahidi huyu hakuna mahali ametajwa kuwa anapaswa kuwa wa siri.
Baada ya pingamizi hilo kesi iliahirishwa na zoezi litakaloendelea leo ni upande wa Jamhuri kujibu hoja za Mh. Tundu Lissu kuhusu uhalali huu wa shahidi huyu wa siri.
Baada ya Mawakili wa Serikali kujibu hoja hizo zoezi litakalofuata ni Mheshimiwa Lissu kutoa hoja za nyongeza (rejoinder) kwa pingamizi lake na baadae Mahakama itatoa uamuzi wa uhalali wa Shahidi huyo wa 4 ambae ni P11.
Hapo ndipo tulipoishia na leo tutaendelea hapo.
Kwa kifupi hali ya Mahakama iko sawa wafuatiliaji kwa maana ya Wanachama wapo wakutosha.
Mawakili wa Pande zote mbili wameshafika na maandalizi ya mwisho mwisho yanaendelea hapa so tujiandae kuendelea kula Darasa huru la sheria kutoka kwa Mwalimu wa umma wa Sheria ambae ni Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mhe. Tundu Antipas Lissu.
REPOST
This young man is from Iran, he has decided not to buy into fear so he can stand up and show the world how people live in fear and oppression. American people stand up for the oppressed. Same to TANZANIA we need help oppressive regime
Dear American people: this young Iranian man is risking his life to bring a message to you from inside Iran. This is unparalleled bravery and extraordinary risk. Can you give him, in return, just 1 minute and 40 seconds of your time?
2025 shukrani kwa wanangu wote ambao walipigana vita zangu kwa niaba yangu.
Huu ndio mwaka CHAWA wamehangaika na SATIVA kuliko miaka yote. Kwa ukubwa wa majukumu yangu sikuweza kuwajibu—nyie wanangu mliifanya hiyo kazi kwa WIVU MKUBWA sana.
2026 NITAENDELEA KUSHUGULIKA NA SERIKALI HARAMU WAKIONGOZWA NA BI MSUMI BILA KUCHOKA MPAKA KIELEWEKE HIYO NDIO AHADI YANGU KWENU.
SATIVA NI MTU WENU NIKIZINGUA MSIOGOPE KUNICHNA.
TUTAKUWEPO🫵🏾😎
Hakuna mtu anaeweza kukwamisha watu kuja kutoa maoni….
Watanzania wanajiuliza kuhusu kuaminika kwenu Nyie tume… Kama Watanzania wangekua na Imani na nyie hakuna mtu mwenye uwezo wa kuwazuia kuja kutoa maoni..
Watanzania wanajuliza je nyie mnaweza kuja na ripoti tofauti na ambacho aliewateua amekwisha sema?
1. Walioandamana walilipwa fedha
2. Wanatumiwa na walitumiwa na mabeberu
3.Sio Watanzania ni watu kutoka Mataifa ya nje.
4. Waliandamana kwa mkumbo tu hawajui walichokua wanadai na hata madai yao hayapo.
Je nyie mnaweza kutoa ripoti tofauti na mawazo ya hawa waliowapa kazi?
Mwenyekiti wa CHADEMA, Kanda ya Pwani,Boniface Jacob amesema kwamba kauli za baadhi ya viongozi kwamba kuna wanaharakati waliopewa fedha ili kuleta vurugu ni za kukwepa uwajibikaji kwa matukio ya Oktoba 29. Akihojiwa na Jambotv jana kuhusu madai ya wanaharakati nchini kupewa fedha ili kuhamasisha vurugu, Boniface amesema kwamba kama upo ushahidi kwa watu waliopewa fedha basi wafikishwe katika vyombo vya sheria badala ya kutoa kauli za jumla jumla ambazo hazitasaidia lolote kuhusiana na matukio yaliyojitokeza kipindi cha uchaguzi. "Mara nyingine baadhi ya viongozi wanatoa kauli zinazoleta ishara kwamba wanakwepa uwajibikaji, ukisema kwamba kuna wanaharakati au kuna watu wanapewa fedha kufanya shughuli hizo mimi nitakujibu kwamba hakuna mwenye uthibitisho na kama uthibitisho upo siamini kwamba wangeshindwa kuchukua hatua za kisheria" "Mimi ninachojua ni wananchi wenyewe walifanya vile, ushahidi kwamba ni wananchi wenyewe, tuliwaona walishtakiwa mahakamani, waliokamatwa kuanzia Oktoba 29 sijaona hata mmoja aliyesema kwamba mimi nimepewa hela lakini vilevile mpaka sasa sijapata ushuhuda mtu akisema mimi hapa nilipewa hela nikaandamane"-Boniface Jacob Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mimi ningekuwa wewe , ningezingatia sana diet, nakupumzika vizuri, ningekuwa makini na kula kula ovyo. Obesity ni hatari sana. Dr Janabi anaongea sana mambo haya.Tafuta video zake. Pia angalia usije na wewe kuwa CHAWA wa Wasanii kama wagombea wengine wanaotazama 2030 sasa wakati Nchi bado inadai uchaguzi mpya. Umesikiliza ngoma ya Ney ? Tuko Busy ? Kali Kinyama YAANI!!
ANAANDIKA WAKILI GASTON GALUBINDI
UPDATE KUTOKA UKONGA GEREZANI DAY 252:
Leo nimemtembelea Mteja wangu Mhe Lissu, Ukonga Gerezani kujadiliana naye hatima ya kesi zinazomkabili, ashukuliwe Mungu kwa kuendelea kumjalia afya na siha njema kiongozi.
Gerezani kuna utaratibu mpya umeanzishwa ambao ni kinyume cha sheria, Nilichokutana nacho leo ni kama ifuatavyo;
Mosi, Nimeshindwa kutekeleza majukumu yangu kama wakili kutokana na Magereza kulazimisha mazungumzo yangu kama wakili na Mteja wangu Tundu Lissu yafanyike mbele ya Maafisa wa Magereza Ukonga wakisikiliza kinyume na Katiba ya nchi, Kinyume na sheria ya Magereza, Kinyume kanuni za Kimataifa, hivyo nimekataa kuzungumza na mteja zaidi ili tutafute kwanza haki ya usiri wa mazungumzo kati ya mawakili na mteja wetu.
Kwenye hili, Magereza wanafahamu misingi ya kazi, kitendo mnachofanya mnafahamu ni kinyume cha ibara ya 13 ya Katiba, Ni kinyume cha sheria za nchi kuhusu haki za wafungwa na Mahabusu, lakini mnafanya kwa makusudi. Ni lazima kuchukua hatua dhidi yenu.
Pili, Mheshimiwa Lissu aliandika barua kwa Naibu msajili wa Mahakama kuu, tarehe 5 December 2025 akitaka kufahamishwa tarehe rasmi ya session ya kesi ya uhaini inayomkabili pamoja na mwenendo wa kesi hadi ilipoishia. (Taarifa ya Mhe Lissu kuandika barua ilitolewa pia kwa umma) sasa Pamoja na kwamba aliandika barua tarehe 5, cha ajabu ni kwamba barua hizo zinaonekana zilifika Mahakamani tarehe 15 December 2025, yaani juzi Jumatatu.
Kwa mnaofahamu Jiografia ya Jiji la Dar Es Salaam kutoka ukonga hadi Mahakama kuu pale posta , imewachukua Magereza siku 10 kufikisha hiyo barua.
Itakumbukwa session ilipoahirishwa ilipaswa kuanzia November 3 na kukoma tarehe 11 November 2025, lakini hakuletwa Mahakamani hadi siku ya tarehe 11 na tangu siku hiyo hakuna tarehe rasmi iliyopangwa.
Ni muhimu pia kukumbuka kwamba, utaratibu wa session ni tofauti na utaratibu wa kawaida wa kusikiliza mashauri ya kawaida. Leo session haijulikani itaanza lini, Lissu anaendelea kushikiliwa kwa siku 252 sasa na hakuna kesi inayoendelea.
Tatu, Kuhusiana na Maombi yake ya kuomba kuunganishwa kwenye kesi ya Mali za Chama. Mhe Lissu ameandika barua rasmi kwenda Mahakama kuu.
Tukitangaza MAANDAMANO siku ya show ya MSANII kuna MAWILI MAKUBWA.
1. Msanii ataahirisha SHOW na kuingia HASARA.
2. Wananchi TUTAANDAMANA kupekeka ujumbe wetu kwa WAKOLONI WEUSI.
Hapo Washindi ni sisi wananchi. Kama watatulaza NDANI wananchi na Wasanii basi tumekosa Wote UNYAMA tutasubiri Show nyingine na sisi tutaitisha maandamano mengine.
Yani ni “WEKA TUWEKE” bila kuchoka.
DJ Ally B amepingana na Majizzo kuhusu wasanii kusamehewa.
Amesema watu hawawezi kulazimishwa kupenda kiporo. Vipi unakubaliana nae? Big YES or Big NO??
Geofrey Mwambe ni vetted officer. Amekua waziri, wakati Magufuli yeye na kina Kabudi waliongoza kile kilichoitwa timu ya majadiliano na mabeberu, huyu amekua Mkurugenzi wa Tic.
Kiongozi mkubwa wa serikali, leo anatekwa, anafichwa, anashikiliwa kinyume cha sheria.
Nani yuko salama?
Utawala uliofitinika, uliojaa damu, hakuna mwenye usalama.
Muachieni Mwambe.