@McinikaWaLamar >Hakikisha una Pasport, nyumbani hapatoshi.
>Popote ulipo hakikisha unasaport HAKI na ukweli.
>Sema ukweli
>Zingatia muda (appointment)
>Kuwa simple, simplicity is key
"Nitoe wito kwa Jaji Mkuu na Jaji Kiongozi kama watendaji na viongozi wanaosimamia muhimili wa mahakama katika majukumu, siyo tu ya usimamizi wa haki na majukumu ya kiutawala kuweza kuingilia kati jambo hili, ili mahakama kwa ujumla wake isipate aibu ya kuonyesha kwamba imeshiriki njama za kudhibiti watu kuwepo kwenye mahakama ya umma ambayo ni mahakama ya wazi." Mhe. @jjmnyika
An Iranian 🇮🇷 boy just asked Trump to shut up 😂😂😂😂😂
He was asked what he would like to say to Trump and Netayahu, and he said,
“They talk too much nonsense. Let them just shut up and stop talking.”
Even a kid in Iran 🇮🇷 fears nothing 💀
‼️🚨 MKUU WA GEREZA LA UKONGA ASIMAME KIDETE‼️
Jamani mi habari yoyote kuhusu Lissu sipuuzi! Hawa wehu wamepanic na inabidi wamwachie maana hali mbaya! Hivu mnakumbuka Rachel jana alitueleza kuwa Sumai alienda usiku wa manane kumalizana na Lissu ila aligonga mwamba?
Sasa hawa wauaji hawajakata tamaa bado wamepanga kumwekea gesi ya sumu so @MagerezaT endeleeni kuwa makini - Lissu atoke mzima! Hizi ni dakika za majeruhi msikosee! Hawa manyangau wasitie mguu kabisa!
Na we Abdul na takataka wenzako KOMA 🚮
#FreeTunduLissu
Leo majira ya mchana Polisi watano wakiwa na silaha za moto walivamia nyumbani kwa Mwenyekiti wa CHASO Mkoa wa Mwanza AdvocateSailence Mwakasala na kumkamata kinguvu kisha wakaondoka nae.
Mpaka sasa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza wamegoma kusema kosa lake ni nini na wanamshikilia katika kituo kipi cha Polisi.
NB. Gari ambayo walitumia wakati wanamkamata ni namba T 113 DVU Toyota Hilux halafu mmoja wa hao Askari alikuwa amevaa sare za The Polisi.
#FreeSailenceMwakasala
Kwanini kesi ya Mwenyekiti wetu isogezwe mbele kwa mda mrefu kiasi hiki mara tu baada ya chama kueleza mpango mbovu wa polisi hapo kesho.
Chama kimeeleza nia ovu ya polisi dhidi ya chama chetu alafu kesi inasogezwa mbele!!!
Mahakama ya Tanzania inaondoa imani ya wananchi na kuchochea chuki kwa matendo kama haya.
Huyu Saada Mkuya Salum amekua mbunge na waziri wa fedha huku bara..
Maneno muhimu kutoka kwako:
Unaelekeza mtu akienda hospital akitoa kitambulisho cha Taifa asitibiwe mpaka atoe cha Mzanzibari!!!! Ni mtu gani anaweza kuwa na kitambulisho cha Mtanzania lakini hana cha Mzanzibari?
Bila shaka ni mtu kutoka Tanganyika.
Umesema hatuna uwezo wa kutibu watu milioni 60 ambayo hiyo ni idadi ya Watanzania ambao wengi ni Watanganyika.
Je kuna siku wote wamevuka kuja kutafuta matibabu huko?
1. Saada unaweza kuwambia watu deni la Taifa ambalo kila mwezi tunalipa karibia trilioni moja na kadhaa ni kiasi gani kinatoka kwenye makusanyo ya Zanzibar?
2. Serikali za mitaa sio suala la muungano kwa katiba yetu,
Je unajua kuna wakurugenzi wa halmashauri za miji na majiji wameteueliwa kutoka Zanzibar huku Tanganyika?
Unajua kuna MADC wengi tu wameteueliwa kutoka Zanzibar wako huku bara?
Umefuatilia kwenye idara za madini, utaliii na wizara nyingi ambazo sio za Muungano kuna wakuu wa idara wangapi, wakurugenzi wa idara na maafisa wangapi kutoka Zanzibar?
Unataka Watanganyika wanaoishi huko wabaguliwe na wasipewe matibabu kwasababu ya kukosa kitambulisho cha Mzanzibari hata kama ana matibabu kadi ambayo ni sawa na bima ya afya….
Je Wazanzibari wanaoishi huku Tanganyika na wana bima za afya za NHIF nao wanyimwe matibabu?
Huyu ni waziri wa pili ndani ya mda mfupi kutoa kauli za kibaguzi dhidi ya Watanzania wengine na hakuna kauli yet kutoka kwa aliewateua… Kwahiyo huu ndio msimamo wa ccm na ndio msimamo wa wateuzi wao.
Nani anaewatuma hawa kusema haya? Maana sio bahati mbaya… nani anaewatuma kuwabagua Watanganyika?
🔥7/7 imechangamka
Maandamano 7/7 loading
Gen Z wamesema wamechoka na wanaungwa mkono na Gen zote
Mi naendelea kushauri mkianza kamatakamata na vitisho - you will make things worse @SuluhuSamia@ccm_tanzania
Wapeni wananchi wanachodai 👇🏾
#SamiaMustGo#FreeTunduLissu #UchaguziHuru #KatibaMpya
These are non-negotiable kwa watanzania kwa sasa
Matusi na vitisho haiwasaidii!
HISTORIA YAKO ITAANDIKWA KAMA NELSON MANDELA‼️
Historia ya maisha ya Nelson Mandela inaonyesha mchango mkubwa katika kutetea haki za watu wa nchi yake. Alijitolea kupigania usawa, haki na uhuru wa wananchi licha ya kupitia changamoto na kifungo cha muda mrefu. Ujasiri na msimamo wake uliifanya historia yake kuwa mfano wa mapambano ya haki za binadamu duniani kote. Je wewe utakumbukwa kwa lipo?
Usijisahau kwani historia yako pia itaandikwa tu kwa vyovyote vile, swali je, itaandikwaje?
- Ulinyamaza mahala ulipotakiwa kusema?
- Uliogopa mahala ulipotakiwa kuwa jasiri?
- Ulirudi nyuma badala ya kusaidia?
- Ulikwamisha badala ya kufanikisha?
- Ulipinga badala ya kutetea?
#7Julai
Hii nchi ina majabu mengi sana, wakulima wana mazao shambani yamekomaa na tayari kuvunwa lakini wanashindwa kuvuna mazao sababu serikali haijatangaza bei.
Tena, kwenye taarifa za kimataifa, inasema kabisa kuwa tarehe ya Tanzania ni kati ya Mei mwanzoni mpaka Juni katikati. Hii ni kwamba hatujui misimu ya mafuno mpaka leo,
Kwamba serikali imeshindwa kujua bei na tarehe mpaka kila kitu kinakuwa cha kubahatisha ? Kwa nini kusiwe na tarehe inayoeleweka ya kuteangaza bei mwanzo tu mkulima anapoanza mavuno ambayo ni June mwanzoni.
wizara @WizaraKilimo mnajua ni kiasi gani mnatesa wakulima kwa huu utaratibu wenu unaosababisha wakulima wanaacha mazao shambani kwa muda mrefu wakisubiria bei? sababu za kuchelewesha bei ni nini? Kisayansi, nini kinawafanya mna chelewa kuwapa bei elekezi? kama wakulima wanavuna kuanzia Mei, kwa nini bei zisitoke Mei mwisho au June mwanzo kabisa? Hili kila mkulima ajue anajipanga vipi? Au kama mmeshindwa kusiwe na bei nguvu ya soko iamue, kama kuna bei elekezi hiyo sio bei ya serikali tu, inahusu kila mtu. Inatakiwa kutoka kwa wakati kwa manufaa ya wadau wote kwenye sekta hasa mahindi.
kwa nini mnawatesa hivi wakulima ? watu wamekaa na mazao wanayaangailia tu wakisubiria bei za stakabadhi ghalani ? hii ni baada ya wao kulima kwa taabu kwa miezi mitatu, kisha wanakutana na hilo balaa ya kusikilizia hata hata shida zao ndogo ndogo wanashindwa dili nazo.
Kuweni na huruma, wapeni wananchi taarifa mapema ili wajipange. Mtu amemenyeka, amelima kwa miezi, ana maliza, anasikilizia tena na bei. Mkitoa bei mapema, mnawapa wakulima wigo wa maamuzi. Haya ni maisha ya wananchi masikini, mnaendelea kuyaharibu kila siku.
@DChongolo wafanyieni wepesi wakulima, hii ni idadi kubwa sana ya watu katika jamii. Wanakosa tu pa kusemea, lakini ilitakiwa. Wala kila tarehe moja Juni mmewapa bei, hata kama mpango wenu ni kununua baadaye, ila wao nao wana maisha wanataka kuendesha.
NCHI YA KAULI MBIU, MIKAKATI NA MIUNDO MBINU
Nawala hatushtuki wala kujiuliza tuko kama Kuku aliye katwa Kichwa.Tumezoea Ujinga na Ujinga Umetuzoea na kuota Mizizi katika Fikra zetu.
Tatizo la nchi hii siyo Misaada au Utitiri wa mikataba ya mahusiano ya kiuchumi ,kijamii na kisiasa. Tatizo ni UWAJIBIKAJI.
Kama Mungu ametupa kila kitu Ardhi yenye rutuba,Maziwabya Maji Baridi,Mito ya Kutosha iliyotapakaa nchi nzima,Madini,Misitu ya Asili,Mbuga za Wanyama na Idadi ya kutosha ya watu lakini tunanuka umasikini,ujinga na Maradhi unadhani tutakombolewa na mikataba hii ya kijanja janja?!
UKWELI,HAKI NA UWAJIBIKAJI ndiyo njia Pekee za kuliponya Taifa na kulirejesha katika uelekeo wa Njia ya Nchi ya Ahadi.
BAK MWABUKUSI.