#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 221
Jaji Ndunguru ameteta sana na wenzake kama dakika 10 hivi.
Sasa anawasha kipaza sauti.
Anasema yafuatayo: tumesikiliza hoja zote hivyo vijembe vyenu msivilete.
Sasa mshitakiwa alisema anapingamizi na tukasema upande wa mashitaka walete open statement ili Mahakama iamue.
Mambo mengine ya kwamba imeambatana na nini na nini kipo wapi hayo sio mambo ya msingi.
Mshitakiwa endelea sasa, hawa upande wa mashitaka mmemaliza hapo, presentation ya notice na justification ya notice.
Watu wanacheka hapa 😂😂😂😂
Nafikiri mpaka sasa Katuga ameelewa nani ni Bingwa wa Sheria.
Mhe. Lissu amasimam, sasa Waheshimiwa Majaji kwa kuanzia niseme hivi waliyosema wenzetu.
1. Upande wa mashitaka unasema notice yao haileti shahidi mpya bali inaongezea ushahidi wa shahidi ambae ushahidi wake ulishatolewa kwenye committal.
2. Wamemtaja huyo shahidi kwa jina kabisa.
3. Wamesema wameleta viambatanisho vinavyotakiwa kwa mujibu wa kifungu cha 308(2) cha CPA.
Sasa baada ya kusema twende kifungu kinavyosema cha 308
A witness whose statement or evidence was not read during committal......
Kifungu kinasema shahidi mpya.
Kinachotakiwa kuletwa ni jina la shahidi wa ziada, huyu ndio anaweza kutolewa notice.
Wamesema wenyewe hawaleti shahidi mpya bali wanaongezea ushahidi wa shahidi aliyepo.
Sasa huyu shahidi ambae tayari yupo na wamemtaja huyo Shahidi ACP Amin Mahamba.
Sasa waheshimiwa Majaji naomba niwaalike kwenye ukurasa wa 90 na 91 na 99 na 100 wa record ya committal proceedings na ukurasa wa 134 wa record ya Mahakama hii ambapo upande wa mashitaka ulitaja majina ya mashahidi wao.
Huyo Amin Mahamba yupo na mimi maelezo yake ninayo hapa sasa Waheshimiwa majaji hiyo notice inaingiaje mahakamani.
Ushahidi wake tayari upo mahakamani na notice inatakiwa iwe ya shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa mahakamani.
Hii sio notice ya additional witness ni notice ya additional evidence ambayo haipo kisheria nimetafuta CPA yote hicho wanachosema hakipo.
Jambo lingine ni kwamba wanaleta ushahidi wa mtu aliyefanya upelelezi wa matukio ya uchaguzi mkuu 2025 sasa Majaji matukio ya tukio ya tarehe 29/10 mimi tayari niko mahabusu
Anasimama Katuga anasema tunapinga anaanza kujadili ushahidi wetu kama mtakubali ni sawa tu.
Lissu: Si ndio kayaleta haya mwenyewe wanakatazaje nisiyazungumzie?
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa endelea.
Lissu: amesema mwenyewe kwa mdomo wake hapa Mahakamani. Nilimwambia asibwabwaje sana. Akang'ang'ania kuanza kusema mambo ya tarehe 29/10 ndio maana na mimi nasema hayo ya tarehe 29 mimi nilikuwa jela.
Wanafikiri hayo yatawasaidia maana wanataka kugeuza mashitaka kwa kuleta mambo ya tarehe 29/10/2026. They can not amend the information through the back door. Kama mnataka ku amend information nendeni kwenye kifungu cha 294 ch CPA.
Hiyo wanayoiita notice haipo kisheria. Haitambuliki. Hiyo notice muifutilie mbali. Yaani notice na yaliyomo.
Na mwisho, Wahe. Majaji hiyo notice ikiachwa ikawa sehemu ya record ya Mahakama itafungua sanduku la pandora ambalo lina kila aina ya mambo mabaya ambayo sidhani kama itaweza kushughulika mambo hayo.
Wanataka tuzungumze mambo ya October 29 mtakuwa mmefungulia balaa na isije ikawa shida. Mkifungua huo mlango tutaenda huko. Tutazungumzia mauaji ya kimbali na tutaulizana nani aliyeua watanzania. Hii kitu haina mashiko. Are they ready? Mimi niko tayari. Isiruhusiwe ikiruhusiwa niko tayari?
Jaji tafadhali naomba tusiende huko.
Katuga aliambiwa na Lissu kuwa huwezi kunifundisha Sheria akakataaa. Baada ya Lissu kumaliza hapa. Katuga amekuwa mdogo sana yani. Ni kama anataka kulia.
Katuga anasimama anasema napaswa kufanya nini reply au rejoinder
Mhe. Lissu anasema fanyeni reply halafu mimi ndio nitakuja kumaliza.
Wanakubaliana hivyo.
Part 222 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 23, 2026
Last time tuliishia Part 219 so leo tunaendelea na-;
Part 220
Mh. Tundu Lissu anaingia Mahakamani.
Mawakili wa Serikali wapo tayari na Majaji wana kila dalili ya kuingia muda wowote.
Kelele za Shujaa Shujaa Shujaa zinasikika.
Mh. Lissu ameingia anateta jambo pale na Wakili Kisabo na Mahinyila ni kama anawaagiza jambo.
Namuona Wakili Kisabo anachukua simu ni kama anafanya mawasiliano.
Majaji wameingia kuna mtu simu yake imeita, watu wanamshangaa.
Anasimama Kalani anasoma case number.
Anasimama Renatus Mkude, tupo Ajuaye, Katuga, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Shauri lilipangwa kwa ajili ya kusikiliza Notice ya kuongeza mashahidi na ushahidi na sisi tuko tayari.
Majaji wanaandika kidogo.
Wanamuuliza Mshitakiwa.
Mhe. Lissu anajibu na yeye kuwa yuko tayari.
Wanaitwa Upande wa Mshitaka anasimama Katuga kuanza.
Mhe. Lissu waheshimiwa Majaji nimepinga hiyo notice toka ijumaa kwahiyo ningesikilizwa.
Katuga Mheshimiwa Jaji utaratibu ni sisi kuiwasilisha ili yeye apinge kama ana hoja ya kupinga hii sio Application.
Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji hicho wanachoita notice sio notice kabisa na hakitambuliki kisheria.
Jaji sisi tulitaka waeleze nini kinaendelea tu.
Mhe. Lissu: Kama ni hivyo sawa.
Katuga: Mnamo tar. 18/02/2026 kwa njia ya mtandao tulifile notice ya kuongeza ushahidi (notice to file additional statement of evidence) tuliifile kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Pamoja na notice hiyo tuliambatanisha substance ya ushahidi huo, ushahidi huu haumleti shahidi mpya bali ni nyongeza ya Ushahidi wa ACP, Amin Mahamba.
Kwamba ushahidi huu haujakuwa committed Mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Notice hii inakuja kukidhi matakwa ya kifungu cha 308 cha CPA ambacho kinasema hakuna shahidi au maelezo ya shahidi vitatolewa mahakamani unless viwe vimesomwa wakati wa mwenendo kabidhi (committal)
Kifungu hicho kinafafanua maana ya substance of evidence ikiwa ni pamoja na kitu chochote ikiwemo nyaraka na vitu vingine vinavyoshikika.
Kama ambavyo notice inajieleza, substance ya ushahidi kwamba Amin Mahamba alikuwa ni kiongozi wa timu ya upelelezi wakati wa uchaguzi wa 2025 na baada ya uchaguzi.
Na kile alichokipata kutokana na upelelezi ni kitu ambacho haukusomwa pale kwenye committal.
Ushahidi huo tumeupata na kuugundua wakati tumejiandaa kumuita ACP Amin Mahamba siku ya tarehe 16/02/2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA hakijaeleza ni kwa jinsi gani notice itakuwa. Hata kwenye zile prescribed form zilizopo kwenye Sheria hii haijawekwa.
Kifungu hicho kinasema notice ieleze jina la shahidi, substance ya ushahidi na details za shahidi kiujumla kwa mujibu wa kifungu cha 308 (2) cha CPA.
Hivyo vyote tumefanya kwenye notice yetu kucover matukio ya tarehe 29/10/2025.
Anasimama Mhe. Lissu, anasema waheshimiwa mbona kama anaendelea kufanya mambo ambayo hamjamuelekeza.
Katuga waheshimiwa kwani hiyo introduction iko chini ya Sheria gani? Sisi tunaintroduce kwa namna tunayoona ili mwenzetu.
Mhe, Lissu: Asinifundishe Sheria, asijaribu kabisa kunifundisha Sheria, anaanzaje kufanya submission ya hiyo notice kabla uhalali wake haujaamuliwa.
Katuga: Waheshimiwa hakuna bingwa wa Sheria, mabingwa ni nyie tu Majaji.
Majaji wanateta pale juu.
Tunasubiri muongozo wao.
Part 221 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 216
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa Maswali ya Dodoso.
Anasimama Mheshimiwa Lissu kwa ajili ya kumfanyia Cross Examination Shahidi ambae anaitwa Coplo Amani.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa kwa kuanzia naomba nipatiwe kielelezo D12, waheshimiwa majaji haya ni maelezo ya P3.
Mhe. Lissu : Sasa shahidi naomba uwaeleze majaji kama uliandika maelezo polisi
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: waeleze majaji kama unaweza kuyatambua ukionyeshwa
Coplo Amani : nikionyeshwa nitaweza kuyatambua
Mhe. Lissu: naomba shahidi aonyeshwe maelezo yake aliyoandika polisi.
Coplo Amani : haya ndio maelezo yangu
Mhe. Lissu: asante sana, sasa shahidi hayo maelezo yako naomba uwaeleze majaji kama uliyaandika mwenyewe au uliandikiwa na askari mwingine?
Coplo Amani : haya maelezo niliandikiwa na askari mwingine
Mhe. Lissu: mtaje jina tafadhali
Coplo Amani : Anaitwa H9207 detective coplo Robert
Mhe. Lissu: Kwenye maelezo yako hayo waeleze majaji kama ni utaratibu mtu anayeandika maelezo ya shahidi hawezi akawa ndio mtu huyohuyo kama shahidi?
Coplo Amani : ni sahihi
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji pamoja na majibu mazuri ya shahidi huyu nataka ku-impeach credibility yake, nitamsomea maelezo yake, nitamuonyesha maeneo nitakayotaka kumuuliza maswali halafu nitamtaka ayawasilishe kama kilelezo.
Mhe. Lissu anamsomea maelezo yake
Mhe. Lissu : Haya ndio maelezo yako kama nilivyoyasoma?
Coplo Amani : Waheshimiwa majaji mshtakiwa kuna maeneo amekosea naomba nimrekebishe, sio kata ya Isuesue ni Isyesye 😁
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji kwakua na nyie mnarekodi hii mimi nimeona imeandikwa isuesue waheshimiwa…
Kwenye maneno “ni dereva wa bodaboda isuesue Mwintengule”… kwenye original Isyesye… kwahiyo tutaenda na ya kwako.
Kuna eneo lingine ambalo lina shida?
Coplo Amani : hapana.
Mhe. Lissu : Sasa kuna maeneo nataka kukuhoji kwa ajili ya kukukanusha kama ifuatavyo;
1. Kwamba unafanya kazi chini ya OCCID Mbeya mjini
2. Kwamba wewe ni msaidizi wa upelelezi ndani ya Mbeya mjini
3. Umeelezea Kituo cha Polisi cha Ilomba kwamba ni kituo kidogo kilichopo chini ya kituo cha Kati Mbeya umesema ni kama out post.
4. Umeeleza kwamba kaimu OCCID Inspekta Jorum alipokupa maelekezo ya kwenda kumkamata P3 alikupa namba ya simu ya askari wa kitengo cha intelijensia kwa ajili ya kwenda kumkamata P3
5. Kwamba hawa askari huwa wanajichanganya na raia kama dereva boda boda n.k
6. Baada ya kupewa namba ya simu ukawasiliama nae na mkakutana Isyesye.
7. Kwamba kulikua na watu wengi na mlipita na akakuonyesha mtuhumiwa kwenye kituo cha boda boda.
8. Taarifa mlizopewa na Jorum ni mtuhumiwa ndiye anayehamasisha wenzake kufanya vurugu uchaguzi wa 2025
9. Baada ya kuonyeshwa huyo mtuhumiwa ulimfata na kumtoa pembeni ya kijiwe na kisha ulijitambulisha kwake kwa jina na kumueleza tuhuma zake.
10. Ulimwambia baada ya kumtoa pembeni kwamba anahitajika Kituo cha Polisi Ilomba na yeye alikubali kwenda.
11. Ni ushahidi wako maelezo aliyoandika mtuhumiwa ni uchochezi, kusababisha vurugu na kuzuia uchaguzi mkuu wa 2025.
12. Shitaka uliloandika lilikua ni kukiuka masharti ya kifungu cha 390 cha Penal code
13. Wakati ukimhoji alikwambia kwamba aliona taarifa kwenye YouTube akamuona Lissu akiwa anahamisisha uasi, kufanya vurugu na kuharibu uchaguzi 2025.
14. Baada ya kuandika maelezo yake ulimjulisha inspeka Jorum akakuelekea kumuachia kwa dhamana na we anaripoti kila baada ya siku tatu
15. Ni ushahidi unaohusu tareh 17 april 2025 kwamba siku hiyo wakati ukiwa Ilomba Kituo cha Polisi ulielekezwa na inspekta Horum kuandika maelezo ya mtuhumiwa kama shahidi kuhusiana maelezo ya Mwenyekiti wake Tundu Lissu na yeye kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vijana wenzake kufanya vurugu.
16. Baada ya kurekodi malezo hayo na ulimjulisha Inspekta Jorum na ukamkabidhi malezo hayo.
Part 217 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 199
Mhe. Lissu anaendelea na Cross examination.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba uwaeleze waheshimiwa Majaji kama niliyoyasoma yanalingana na maelezo yako ya police.
Coplo Vicent: ndiyo yanalingana.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba nikupitishe kwenye Maeneo ambayo nataka nikuhoji.
Mheshimiwa Lissu anamsomea shahidi maeneo anayotaka kumhoji.
Mhe. Lissu: ili niweze kukuhoji sawasawa waeleze waheshimiwa Majaji kama ungependa maelezo yako yapokelewe kama kielelezo.
Coplo Vicent: kwa jinsi ambavyo umenihoji naomba nisahihishe kwanza, naomba nirekebishe.
Mhe.Lissu: bado sijaanza kukuhoji, tutafika huko kubali kwanza maelezo yako yapokelewe.
Coplo Vicent: sawa nakubali yapokelewe kama kielelezo.
Mhe.Jaji: itakuwa D11
Mhe.Lissu: sawa mheshimiwa.
Mhe.Lissu: mheshimiwa Jaji naomba shahidi apewe kielelezo D11
Mhe.Lissu: Sasa shahidi hicho ni kielelezo mahakamani na swali la kwanza katika ushahidi wako Leo umesema wewe ni Askari police na unafanya kazi katika kituo cha Polisi Central Mbeya,
Sasa katika hayo maelezo yako naomba uwaambie waheshimiwa Majaji kama kuna sehemu umeandika kuwa unafanya kazi katika kituo cha police Central Mbeya
Coplo Vicent: hapa hakuna.
Mhe.Lissu: Shahidi swali langu la pili linahusu matukio ya tarehe 5 mwezi wa 4 mwaka jana, katika ushahidi wako unasema uliitwa na Mkuu wa kituo cha Polisi Mwanjelwa na kukuelekeza kwamba ukamkamate P9 kwa kuwa anahamasisha kwenye vijiwe mbalimbali na kuchochea uchaguzi mkuu wa 2025 usifanyike. Nataka nijue kama huo ndiyo ushahidi wako.
Coplo Vicent: bila shaka.
Mhe.Lissu: nataka uangalie kwenye maelezo yako uyasoke kuanzia pale unapoelekezwa ukamkamate P9, kama kuna maneno kwamba P9 alikuwa anahamasisha kwenye vijiwe mbalimbali uchaguzi mkuu usifanyike nataka kujua kama maneno hayo yapo.
Coplo Vicent : yapo.
Mhe.Lissu: naomba usome kuanzia hapo kwenye nakumbuka......
Coplo Vicent anasoma.
Mhe.Lissu: hayo maneno anahamasisha na kuchochea Uchaguzi Mkuu usifanyike hayo maneno yapo?
Coplo Vicent: hiyo haipo.
Mhe.Lissu: ahsante sana
Mhe.Lissu: Sasa shahidi kwenye ushahidi wako umesema baada ya kujitambulisha kwake wewe ni Polisi ulimuonesha kitambulisho chako, na ukaongozana nae hadi kituo cha Polisi Mwanjelwa. Kweli au si kweli.
Coplo Vicent: kweli
Mhe.Lissu: waambie Majaji kama hayo maneno yapo.
Coplo Vicent: Hayapo.
Mhe.Lissu: Sasa shahidi naomba uwaambie waheshimiwa Majaji ni nani aliyeandika maelezo yako.
Coplo Vicent : niliandika Mwenyewe.
Mhe.Lissu: shahidi waeleze waheshimiwa Majaji kama wakati wa kuandika maelezo huwa kuna sehemu ya onyo.
Coplo Vicent : huwa hakuna onyo.
Mhe.Lissu: hakuna Yale maneno kuwa nitasema ukweli, ukweli mtupu nikisema uongo nishitakiwe.
Coplo Vicent : hyo siyo onyo.
Mhe.Lissu: hiyo huwa ni nini.
Coplo Vicent : huwa ninajiambia nitasema ukweli, najiandika maelezo.
Mhe.Lissu: huo ndo utaratibu wenu Mapolisi, mnajiambia wenyewe.
Mhe.Lissu: unaifahamu PGO.
Coplo Vicent : ndiyo
Mhe.Lissu: shahidi unaifahamu PGO number 236.
Coplo Vicent: siifahamu.
Mhe.Lissu: Mhe.Jaji naomba shahidi apewe PGO
Mhe.Lissu: Shahidi soma PGO 236.
Coplo Vicent : hii PGO ni ya kingereza siwezi kusoma.
Mhe.Lissu: Wambura ameandika kingereza anaamimi nyote mnajua kingereza kwahiyo huwezi kusoma kwa sababu ni kingereza.
Coplo Vicent : kuna ya kiswahili.
Mhe.Lissu: ujue kingereza au usijue swali langu utalijibu. Naomba PGO yangu.
Mhe.Lissu: shahidi kwenye kielelezo D11 pale mwishoni kuna udhibitisho wa majina yako na sahihi yako. Umeyaona hayo maneno
Coplo Vicent: Hayapo hayo maneno.
Mhe.Lissu: Mheshimiwa Jaji naomba shahidi aoneshwe sehemu ya udhibitisho wake kwenye D11, kifungu cha 10.3.C
Coplo Vicent: wapi, hapa mwisho kabisa au.
Mhe.Lissu: kipindi unaandika haya maelezo kulikuwepo na kufungu cha 10.3.C
Coplo Vicent : ndiyo kulikuwepo mwaka Jana.
Mhe.Lissu: ni nani alikushuhudia wakati ukiandika maelezo yako
Coplo Vicent : hakuwepo mtu yeyote
Part 200 itaendelea post inayofuata,
Naomba repost