Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bi. Anna Mghwira (Mkuu wa Mkoa Mstaafu). Katika utumishi wake alikuwa mchapakazi, jasiri na aliyepigania maendeleo hasa ya Wanawake. Nawapa pole wafiwa wote, ndugu, jamaa na marafiki. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina.