A bonafide recipient of God's grace | Concerned global citizen, researcher, and technocrat in digital transformations | PDRF @go2uj SL @udomtheofficial
E-waste is projected to reach 4.4 million tonnes in Africa by 2026, exposing the environmental cost of rapid digital transformation. Our study examines policy alignment as key to ensuring that digital transformation advances sustainability https://t.co/NIrTknSwSY
Ukiondoa elimu, ulikosoma, taaluma ulizosomea, kazi, mahali unakofanya kazi, mali, mamlaka na cheo ulichonacho, watu uliojitambulisha nao, unabaki na nini kinachopambanua vizuri utambulisho wako na kukupa utoshelevu? Wewe ni nani ukiacha vibandiko hivi?
Ukiweza kujisikia mtu wa thamani, mtu wa maana, mwenye furaha, mwenye utulivu na amani, bila kujishikiza mno na hivi vibandiko tunavyojipachika baada ya kuzaliwa, wewe kwa hakika ni mtu ukiyekutana na wewe, unayemfahamu ‘wewe’, unayeheshimiana na wewe, unayejitambua, uliyefanikiwa na kwa hakika, utakuwa mtu mwenye utulivu unaokupa utoshelevu katika maisha.
Ukiupata utulivu huo, mshunuzi Abraham H. Maslow anakuita ‘self-actualized’ hata kama huna chochote kinachoonekana. Katika utulivu huo unakuwa mtu mwanana, asiye na mashindano, asiyejitanguliza yeye na maslahi yake, asiyeteseka kujikweza aonekane, na hivyo unakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuipa dunia kile ulichopaswa kuipa. Carl Rogers angesema hapo unakuwa unaliishi kusudi lako na hayo ndio maisha yenye utoshelevu (fully-functioning person).
@bwaya@MayengoDr Mkwamo lazima uendele kuwepo ikiwa pande moja haimini kwamba amani ni tunda la haki, kwamba kuna haki zinaweza kukanyagwa bila kuhojiwa