To our brothers and Sisters that have lost their lives, You will never be forgotten.
Nyie ni ndugu zetu hata kama kama mtu halitambui.
Nyie ndio boda wetu, wauza chapati, wauza genge, manesi, madaktari, wahudumu wa Bar, nyie hamkujifungia ndani, you risked all 🙏🏼
We mourn you.
Tumepoteza ndugu, rafiki na watu wetu wa karibu katika hiki kipindi sio kwamba sisi tulistahili kuishi kuliko wao. Kwenye Mioyo yetu iliyojaa Damu tutawakumbuka kama Mashujaa. Rest in Paradise Champions.🫡🕯️
Rest in peace to all the brothers and sisters who lost their lives, actually they didn’t lose their lives their lives were taken. Their sacrifice and blood will not go unanswered and will not be in vain, eventually their courage will forever demand justice 🙏🏾
Ewe mwanadamu ambaye nawe hautaishi milele hapa duniani, ewe mwanadamu ambaye siku zako zinahesabika, tena uliumbwa kwa mavumbi na mavumbini utarudi, unawezaje kushangilia mambo mabaya yaliyowapata wanadamu wenzako? Unawezaje kukejeli na kudhihaki katika nyakati hizi?
Sitaandika jambo lolote linalohusu burudani iwe football, muziki au suala lolote lenye mrengo huo kwa kipindi kisichopungua mwezi mmoja. Nitatumia muda huu katika kuzama kwenye tafakari kubwa na kusoma maandiko matakatifu.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 127
Anaendelea Katuga
Shahidi alitambua vielelezo pale kizimbani na ndio maana tunasema vipokelewe, alisema hawezi kutufundisha na sisi tunataka akitufundisha atufundishe kutoka kwenye Sheria.
Naomba niende kwenye hoja ya tatu ambayo inasema shahidi sio competent kutender hii exhibit na kwenye hoja hii aliialika Mahakama kwenye vile vifungu vingi kuanzia 216 hadi 221 vya CPA.
WAKATI KATUGA ANAENDELEA NI KAMA NIMEWAONA HAWA ASKARI MAGEREZA WANAOMLINDA MH. LISSU WAPO WAGENI NA SURA ZAO ZIMEKAA KAMA WALE WENZETU KWELI. WAPO WAGENI NDIO WAMELETWA HAPA. SIJUI WANA MPANGO GANI NA HAWA WALINZI WAO.
Acha tuendelee na Katuga sasa
Anataja vifungu vyote alivyovitaja Mh. Lissu na vinazungumzia nini? Kingereza chake ni kibovu sana. Akisoma mahali ZE ZE ZE ZE ZE ni nyingi sana.
PW 3 amejieleza kama yeye ni mtaalamu na alialikwa kufanyia kazi vielelezo na amejipambanua kuhusiana na umri wake na utaalamu wake. Na alifanyia kazi vielelezo hivi hivyo basi kifungu cha 52 cha Evidence Act Cap. 6 kinasema mtu mwenye uelewa na fingerprints, na ujuzi mwingine basi yanapokelewa.
Kila shahidi yuko entitled kuaminiwa unless Mahakama ije na sababu za kutomuamini.
Kesi ya Goodluck Kyando Vs Jamhuri TLR 2006 Every witness is entitled to credence.
Shahidi wetu anaomba kutoa memory card yenye video, flash yenye video.
Kifungu cha 70 cha Evidence Act Cap. 6 kinasema in any proceedings electronic evidence shall be admissible.
Mahakama ya rufaa imetoa visifa vya vitu inavyotakiwa kuzingatia kabla ya kupokea vielelezo.
Kesi maarufu ya DPP VS Sharif Mohamed, Athumani and 6 others CA 74 2016.
Kesi inasema mtu aliyefanyia kazi kielelezo ni competent ku tender pia kesi ya DPP vs Mirzai inatoa utaratibu huo wa kisheria.
Naomba kesi hizi zote nizitoe kwa Mahakama na mshitakiwa pia.
Amekuwa appointed na gazetted kwa kufanya uchunguzi na kutoa taarifa ndio kazi ya shahidi huyu.
Yeye ni shahidi wa picha mnato na mjongeo Gazeti la serikali no. 745/2022 ndio lilimtangaza kwa ajili ya kufanya uchunguzi na kutoa taarifa.
Tangazo hilo limesainiwa na DPP na kwamba title ya tangazo lile ni amri ya uteuzi wa wataalamu wa picha na mambo mengine.
Mtaalamu wetu anasema yeye ni mtaalamu wa picha mnato na picha mjongeo na mimi naialika mahakama itafute meaning ya picha, is video a picture? Vifungu vya 216 na kuendelea havioneshi mtaalamu wa video, hayupo.
Kifungu cha 220 cha CPA kwamba video ni cyber forensic expert, tafsiri ya CYBER ziko nyingi sana ikiwa ni pamoja na ushahidi wa Computer ndo maana yake.
Anachunguza devices utambuzi wa uhalisia wa picha utabaki kwa mtambuzi wa picha. Is a video a picture? Video ni picha za muendelezo.
Hapa cyber experts na photographic expert wasichanganywe ni watu wawili tofauti.
Kuna definition mbalimbali lakini kuna dictionary ya computer and internet terms ukurasa wa 363 alitafsiri photograph is a picture created by a camera whether digital or video. Ukurasa wa 513
Anasema Jaji unaenda kwa kasi sana hatukuelewi kwakweli hata unakimbilia wapi.
Au Mshitakiwa unasemaje Jaji anamuuliza. Lissu anajibu Mimi namuangalia tu naona anaongea ongea, nimemuacha.
Jaji sasa sisi tunaona ujielekeze vizuri ukiendeleea kujiongelea wewe sisi hatutaandika.
Haya rudia hapo sasa kwenye Dictionary taratibu.
Part 128 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 128
Anaendelea Katuga naomba sasa nihamie kwenye hoja ya nne.
Mshitakiwa anasema vielelezo visipokelewe eti akiwamaambia kwamba vielelezo hivi vimevunja mnyonyoro wa utunzaji.
Watu wanacheka. 😂😂😂
Ni mnyororo kumbe.
Amesema Chain of custody inathibitishwa na paper trail. The gist of chain of custody ni kuifanya mahakama ione kielelezo ni chenyewe au au vipi?
Mshitakiwa anasema kilipita kwa Michael Gyumi, sijui kikaenda kwa nani? Hicho kilichosemwa hakijajionyesha kwenye ushahidi wa shahidi wetu.
Ametajwa Churu, baadae Malugala na kujazwa ile PF No. 145.
The issue of chain of custody can no be established by a single witness. Utunzaji wa kielelezo hauwezi kuthibitishwa na shahidi mmoja.
Kuleta pingamizi la kwamba Chain of custody imevunjwa na kisipokelewe huku ni ku misplace mapingamizi.
Haya ni maneno ya Mahakama ya rufani R vs Charles Abel Gazilabo na wenzake 3 Rufaa ya jinai No. 358/2019.
Ukurasa wa 17 imejitokeza inshu ya chain of custody na kusema itatumika na kuangaliwa baada ya ushahudi wa upande wa Jamhuri ukifungwa. Prosecution case ikiwa closed sio muda huu.
Kwa maamuzi hayo Mahakama itaona hii hoja haijakuwa established kabla ya kupokelewa kwa kielelezo ila imeletwa kwa kubahatisha na kupoteza muda wa Mahakama ni ombi letu muitupilie mbali.
Kwa mapingamizi hayo yote tunaona hayana msingi kabisa na naomba niwarejeshe kwenye maamuzi aliyowaletea kesi ya Musa, Lemina Omary Abdul na Kesi ya DPP VS Sharif Mohamed.
Mashauri hayo yote yalikuwa yanahusu vielelezo ambavyo havikuwa vimesomwa au listed kwenye records.
Hayakuwa mashauri ambayo yanaonesha vielelezo kutosomwa, sisi kwetu hapa kwenye kesi hii vilisomwa na kuonyeshwa pale Kisutu.
Kwa kumalizia wakati wa hoja ya Competence pia Mahakama ilialikwa ikasome taarifa ya PW3 tulishangazwa sema tukakumbuka Mshitakiwa ni mtaalaamu wa kesi za Madai na sio jinai.
Tunaomba submission zetu ziwe considered na naomba kuishia hapo.
Renatus Mkude anamualika Ignas Mwinuka na anaomba aongeze kidogo.
Nitasema kwenye ile ground ya committal. Nitaomba mrejee ukurasa wa 93 wa Mwenendo kabidhi Mahakama imeandika, S. 263 of CPA has been complied with. Hii ni kuonesha kuwa taratibu zote ambazo zipo zilizingatiwa kwa mujibu wa Sheria.
Naomba niwarejeshe kwenye shauri la Mahakama ya rufani Jamhuri Vs Christian Muhaka Criminal Revision no. 7/2017.
Naomba Waheshimiwa Majaji kwenye shauri hilo Mahakama wa rufani wakiquote mwenendo kabidhi na kusema hawakuona mapungufu kwasababu vifungu vikiandikwa na vikishaandikwa maana yake utaratibu ulifuatwa.
Kwahiyo naomba kusisitiza kuwa hoja hiyo isikubaliwe na kuzingatiwa na mapingamizi yake yasizingatiwe na yatupiliwe mbali. Naomba kuishia hapo.
Anasimama Renatus Mkude anasema ni mwisho wa hoja zao na tunaomba kusisitiza kuwa mapingamizi yatupiliwe mbali, wanakaaa.
Tusubiri Rejoinder kutoka kwa Mhe. Lissu sasa.
Atajibu vimbwanga vyao hapa.
Part 129 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 130.
Mhe. Lissu anaendelea kufanya Rejoinder
Anasema Kwenye hoja ya pili bado nasimamia hoja ya pili kwamba video zilipaswa zitamabuliwe na taarifa ya mtaalaamu ambae ni shahidi.
Kesi ya Mirza Katuga anasema ni prosecution plan kuwa prosecution wanapanga nani wakuleta kielelezo.
Hoja nimesema kielelezo kinahusika na utaalamu basi kifuate taratibu za utaalamu.
Hoja ya tatu kuhusu competence ya shahidi vifungu kuanzia vya 216 na kuendelea, kusingekuwa na umuhimu wa sheria kusema wateuliwe.
Kinachofanya wawe wataalaamu sio maneno yao bali ni uteuzi wao.
Katuga anasema shahidi ameonysha utaalamu wake.
Je huyu ni mtaalamu? Ameteuliwa? Kama hajaonesha kuwa ni mtaalamu maneno yake ni kazi bure.
Shahidi huyu amesema kwamba ameteuliwa kwa mujibu kwa gazeti la serikali No. 799/2020 na vilevile amesema ameteuliwa kwa mujibu wa gazeti la serikali no. 745/2020
Hayo magazeti ni Sheria na ni nyaraka za kisheria. Wakili wa Serikali hakusema lolote kuhusu GN. No. 799/2020. Na anasema tusiende huko.
Na mimi nasema lazima twende huko kwasababu ni mtaalamu wa picha na sio mtaalamu wa video.
Wapo wataalamu walioteuliwa na DPP kwa ajili ya video huyu hayupo. The are withholding important information, wanaficha nyaraka muhimu na wakitaka walijibie.
Hii ni sheria ambayo walipaswa kuileta kwenu lakini walikaa kimya ni sheria inayohusiana na ni akina nani ambao ni wataalamu wa kisayansi wa mitandao ambapo wapo kwenye GN. No. 823/2024.
Ukiisoma hii GN wapo 27 hao wataalamu hayupo Samweli Elibariki Kaaya kwenye hiyo orodha.
Majaji wanateta sana hapo kama dakika 10 nadhan wanafikiria Mhe. Lissu aruhusiwe kuitoa hiyo Sheria au haruhusiwi.
Jaji ilikuwa ni haki kwa mshitakiwa kuijibia hoja hiyo maana hata Jamhuri mlituletea maana ya picha mkatuambia kuhusu dictionary.
Kwahiyo mshitakiwa endelelea.
Mhe. Lissu anawasomea hiyo GN hapo juu iliyowataja hao ma experts na anasema kwa kiswahili inaitwa AMRI YA UTEUZI WA WATAALAMU WA KISAYANSI WA MTANDAO aya ya pili ya Tangazo hilo inasema mtu ambae jina lake limetajwa katika jedwali anateuliwa kuwa mtaalamu wa kisayansi wa mtandao katika mashauri yoyote ya jinai na masuala yoyote kama hayo kwa mudhumuni hayo.
Jedwali hilo limeorodhesha watu 27 na huyu shahidi hayumo.
Amesimama Katuga anasema anaanza kutaja majina asifike huko.😂
Katuga hajui kama majina yametajwa kwenye hiyo GN yenyewe.
Huyu mtaalamu wao wamekuja nae mfukoni hayupo kisheria, hajatajwa kwenye tangazo la serikali na hajawahi kuteuliwa.
Jaji anasema hiyo ni sheria sasa kama watu wameandikwa tutaona na tutaona nani yupo na nani hayupo kwahiyo muiachie Mahakama tu.
Waheshimiwa Majaji Sharif Athuman Ukurasa wa 8 Jaji Masatti amesema:
But admissibility of evidence, it is also about the competence of the witness. It is not only about relevance, materiality and...
Jaji amesema competence ya shahidi inaweza kuwa general au specific.
Kwa huyu shahidi ni suala specific kwasababu tunazungumzia mambo ya mitandaoni na shahidi ambae anapaswa kutoa huo ushahidi ni ambae katangazwa kwa kazi hiyo.
Hivyo admissibility ya ushahidi huu inahitaji mtaalamu wa cyber forensic na sio mwingine na nimewapa hapo GN ambayo DPP ameteua watu wake.
Wakili wa Serikali anasema shahidi amesema mengi kuwa yeye ni mtaalamu.
Ni wasilisho langu kuwa kwa vile hayupo kwenye gazeti la Serikali na sio mtaalamu wa chochote huyu shahidi ni wajibu wa Mahakama kujiuliza kwa mujibu wa sheria je huyu ni mtaalamu na ameteuliwa kama nani?
Sayansi ya mtandaoni wameteuliwa yumo?
Kwenye picha za kawaida za makaratasi hilo halibishaniwi hapa, asubiri siku tukiwa na kesi ya makaratasi atakuja.
Haya ya leo ni masuala ya kimtandao.
Kifungu cha 70(1) cha Evidence Act kwamba ushahidi wa kielektroniki unakubalika hata mimi najua hilo ila hoja ni kwamba je anayeleta ushahidi kateuliwa?
Hii ndo hoja ya msingi.
Part 130 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 131
Anaendelea Mhe. Lissu kufanya Rejoinder
Anasema kwahiyo Katuga ameleta hicho kifungu cha 70 kwa kutoelewa anazungumza na kuipotezea muda Mahakama akiwa anazungumza jambo gani?
Twende kwenye hoja ya nne.
Hoja ya Chain of Custody ambayo ni hoja ya nne.
Maamuzi yote niliyowasilisha mimi na waliyowasilisha wao Mawakili wa Serikali linalosema shahidi anaweza kuleta ushahidi kutoka mfukoni mwake.
Chain of custody is about paper trail na kesi inayosema hivyo ni Paul Maduka hajaigusia kabisa ukurasa wa 18 na 19 kesi imesema chronological documentation and all paper trail shows the seizure, transfer and disposition must be documented.
Waheshimiwa Majaji ushahidi unaoombwa upokelewe una hiyo chronological documentation uliyosemwa na Mahakama ya Rufani kwenye Paul Maduka?
Je una hiyo paper trail?
Naomba ikumbukwe huyu ni shahidi mtaalaamu na kwenye ushahidi wake aliandikiwa barua na vielelezo vililetwa kwa maandishi afanye uchunguzi wa hivyo vielelezo.
Hizo barua hazijawasilishwa, anasema nikisign dispatch haijaletwa mahakamani.
Anasema alivituma kwa requesting authority na kwamba vimerudije kwake tena hajasema lolote.
Leo ametuletea hivi vielelezo sisi hatujui vimefikaje kwake tena.
Wamefanya mambo kienyeji sana na mambo ya kienyeji hayakubaliwi Mahakamani.
Sasa ushahidi wa namna hii unakubaliwaje Mahakamani?
Nitamkumbusha maneno yake Wakili wa Serikali kuwa alisema Mahakama hii sio ya MAMA YANGU na Mimi namwambia leo kuwa MAHAKAMA HII SIO YA MAMA YAKE KATUGA WALA MAMA YAKE NA HUYU SHAHIDI.
Anasimama Katuga anasema Waheshimiwa Majaji Mahakama hii sio ya Mama yetu wote.
Mhe. Lissu anasema ni sawa KAMA MAHAKAMA SIO YA MAMA YETU WOTE basi na WEWE USIFANYE MAMBO KAMA UNAENDA KWA MAMA YAKO.
Tufuate tu utaratibu hicho ndio ninachokisema na ndo maana naomba vielelezo hivi visipokelewe na Mahakama hii kwa hizo hoja nne nilizosema toka awali na kusisitiza kwa sasa.
Anawaachia Majaji sasa wanaandika.
Kwa kifupi Mh. Lissu amemaliza na gia kubwa sana.
Watoto wa Mjini wanasema amepiga sana kwenye MSHONO kwa hizi nondo majaji sijui watasema tunarudi lini kwa ajili ya uamuzi mdogo wa mapingamizi haya.
Wanaandika pale mbele na kuteta kidogo.
Jaji Ndunguru anasema baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili uamuzi utatolewa siku ya Jumatano tarehe 22/10/2025 saa tatu asubuhi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 129
Anaitwa Mh. Lissu.
Anasimama na kusema naomba na mimi nitoe Rejoinder yangu baada ya kuwasikiliza Mawakili wa Serikali.
Nitafuata utaratibu huo huo ambao wao wameufuata walipokuwa wanajibu mapingamizi yangu.
Kuhusiana na hoja ya kwanza.
Je hizo video zilichezwa Kisutu?
Je nyaraka zingine zote zilisomwa ukiaichia witness statement. Je video zilionyeshwa?
Waheshimiwa majaji mashauri ya Kisutu yalikuwa ni hadhara yalifanyika hadharani members of the public pia walikuwepo.
Amesimama Katuga anasema huko kwingine hatukwenda, tuliishia kwenye Court Records pekeee. Tusimuache aende mbali zaidi.
Lissu Mh. Jaji video hazikuchezwa na kama Wakili wa Serikali anasema hadharani kuwa video zilichezwa maana yake tuna shida kubwa sana.
Waheshimiwa Majaji, je ni kweli kwamba hii rekodi ya Kisutu haikuwa impeached? Wakili anasema kwamba record ya Mahakama haiwezi kuwa impeached?
On the question of record: kuna ruling mbili za Mahakama hii juu ya integrity ya hiyo record mtakumbuka kwamba record hii haikusema chochote juu ya majina ya mashahidi niliowataja.
Anasimama tena Katuga anasema hii ni Rejoinder tunaona anaanza kuingiza vitu vipya tena.
Katuga anaogopa kuna mambo kusemwa. 😂 anasema vitu vipya.
Mhe. Lissu anasema hii rekodi nimeichallenge mara kadhaa.
Hiyo page 92 exhibit zimekuwa listed na page 93 inasema the records has been read out.
Hiyo kuandika hivyo haina maana ukweli wangu unabadilika. It doesn't change my position.
Sitaki kukubali jambo ambalo ni uongo.
Mimi sipendi uongo na ukweli wa kwamba video haikuchezwa kisutu utabaki kuwa hivyo hapa Duniani na hata Mbinguni.
Siwezi jidanganya au kutenda dhambi ya namna hiyo namuachia Katuga pengine yeye amezoea dhambi na kudanganya mambo ambayo sio ya kweli.
Video hazikuonyeshwa anasema zimeonyeshwa tena kwa ujasiri wa kusema hadharani na hapa mahakamani.
Niendelee sasa.
Katuga anasema pia kuwa mimi nilisema kuwa sikatai maneno yangu ya tar. 03/04 pale Makao Makuu ya Chama.
Nilichosema mimi ni kuwa hizi video haziko sahihi kupokelewa kwasababu hazikuonyeshwa Kisutu.
Kwa vile hazikuonyeshwa Kisutu haziwezi kuonyeshwa hapa, zilikuwa listed YES. Hazikuonyeshwa na haziwezi kutolewa hapa Mahakama.
Kuhusu mimi kusema sina shida navyo swali linabaki kuwa haviwezi kupokelewa kama havimeet masharti ya kisheria.
Amerejea mashauri ya Mahakama ya rufani wakati natoa hoja yangu. Shauri la Sharif Mohamed @Athuman, Lemina Omary Abdul na Musa Ramadhani Magai.
Hakuna kesi mbili zinazofanana kwa kila jambo. Kitu muhimu what is the principle ambayo inatokana na mashauri hayo yote matatu.
Principle ni kwamba nyaraka na vitu vyote vinavyotajwa katika mashauri kabidhi kama ni vya kusomwa visomwe na kama ni vya kuonyeshwa lazima vionyeshwe kwahiyo ulitakiwa kuonyeshwa huu ushahidi kule Kisutu.
Mahakama ya rufani ilisema the issue is not authenticity basi issue ni compliance of the law.
Kwenye hoja hii ya kwanza videos ambazo hazikuonyeshwa Kisutu haziwezi kuonyeshwa hapa.
Naomba sasa niende kwenye hoja ya pili.
Kwenye ushahidi wa shahidi ambae anadai yeye ni mtaalamu.
Kitu cha kwanza ni taarifa yake ya kitaalamu na sio alichokifanyia kazi.
Katuga amesema kwamba hakuna sheria mahususi inayolazimisha tuanze na Report badala ya kuanza na video iliyochunguzwa na alisema inantegemea na mazingira ya kesi.
Hajasema mazingira gani ya kesi hii ambayo yanataka ianze report na baadae video.
Sasa katika kesi hii tunayo report ya uchunguzi asa ripoti ndio inayo estabalish genuinely ya hicho kilichofanyiwa uchunguzi.
What is the legal logic ya kutanguliza video na kuacha report ya mtaalamu.
Ukisoma vifungu 216 hadi 223 vya CPA vinasema kuhusu ripoti na sio video na ndio maana ya mfano wangu wa mkokoteni na punda.
Ushahidi wa kitaalamu unahitaji kuletwa na mtaalamu na baada ya ushahidi kuo kuletwa ndio utazingatiwa.
Part 130 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
Kiduku amekuwa nasi bega kwa bega kudai haki.
Tulipokesha kuonesha mshikamano na wf/biashara wa Kariakoo majengo yalipobomoka, au Kanisa la Gwajima lilipovamiwa na polisi, Kiduku alikuwa nasi.
Kila siku anadai haki ya Lissu.
Tusimame naye.
Tudai uhuru wake.
#FreeKiduku