PCVE Expert|Views are mine😉|Justice Lover ⚖️|Quran is my 📖|+259 (Zanzibar)|Ibwera my roots|Co-Founder @kijana_hai| Zanzibar National Coordinator - THRDC
UCHAGUZI 29 OKTOBA. Ee Mungu Tunawaombea marehemu wetu raha ya milele. Tuwazike kwa heshima, kuwafariji wafiwa, kuuguza majeruhi, kusaidia waathirika. Tuombe toba kuondosha sifa za taifa letu kwa kutotambua HAKI ndiyo msingi wa yote na haina mbadala. Twakuomba utusikie
Today, 7th November 2025, we, the undersigned Civil Society Organizations (CSOs), strongly condemn widespread human rights violations that occurred before, during, and after Tanzania’s 2025 General Elections.
These include killings of civilians, unlawful arrests, abductions, enforced disappearances, suppression of media freedoms, an internet shutdown, and denial of due process rights.
There are verified reports of excessive use of force against unarmed demonstrators, including reprisal killings of civilians, some in their own homes. Families have been left traumatized, and children have witnessed violence against their parents.
Journalists were not spared: Master Tindwa (Clouds Media) was killed at his home in Temeke, Kelvin Lameck Mwakangondya (Baraka FM, Mbeya) was killed while on duty, A journalist from Azam Media was seriously injured, and two others, Godfrey Thomas (Ayo TV) and Alphonce Kusaga (Sunrise Radio), were arrested in Arusha. A religious leader, Sheikh Msopa, was shot dead at his home in Dar es Salaam.
We also note reports of mass arrests and detentions of hundreds of civilians, particularly youth, across several regions, many still held without bail or court appearance. For six consecutive days since 29th October, the nationwide internet shutdown restricted access to information, monitoring of elections, and exposure of rights violations, in direct breach of Article 18 of the Constitution and international obligations.
We stand in solidarity with all victims and urge the Government to:
1️⃣ Release all detainees or bring them before the court.
2️⃣ Allow families to bury their loved ones.
3️⃣ Permit independent investigations into the killings.
4️⃣ Prosecute those responsible.
5️⃣ Uphold freedom of expression and the media.
6️⃣ Work toward reconciliation and national healing.
7️⃣ Compensate affected families.
Signed by: LHRC, Twaweza, Foundation for Civil Society, JamiiAfrica, Msichana Initiative, Centre for Strategic Litigation, and Internet Governance Tanzania Working Group.
📄 Full statement attached.
Mlisali, mkafunga na mkamwomba Mungu kwa dua na machozi. Maombi yenu yamefika mbinguni. Mnafikiri haya mauaji na mateso ya watoto wenu ndiyo majibu kutoka kwa Mungu? Hapana. Msihofu. Mungu yupo, na bado anafanya kazi yake kwa njia zake.
Kila tone la damu lililomwagika lina thamani mbele zake. Kila kilio, kila pumzi ya mwisho, ni ushahidi wa mateso yasiyo na hatia. Mungu hawezi kupuuza machozi ya waja wake. Atalipa, na kwa wakati wake, haki itatimia.
Msiache kuamini. Jipeni moyo, maana imani ndiyo tumaini letu pekee. Wengi wamekufa, wengi wamepotea, lakini hakuna kinachopotea bure machoni pa Mungu. Siku moja, mtaona kuwa maumivu haya yote hayakuwa ya bure. Siku moja, machozi yatafutwa, na moyo uliojeruhiwa utapata amani. Na hapo mtasema kwa machozi ya furaha “Asante Mungu, kwa sababu ulikuwa nasi hata katika giza.”
@MunishiRenald Kumbe asilimia 97 zilipigwa usiku??? So shameful. Alafu tunapouliza asilimia zilitoka wapi kumbe ni mawakala. Hivi vitu vina furahisha kweli.
Deeply disturbed by the abduction of Mr. Humphrey Polepole. We stand united for his safety & justice. Tanzania must protect all voices, not silence them. #JusticeForPolepole#HumanRightsDefenders#THRDC
*Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umefanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania*
Leo Mei 05, 2025 Mratibu wa Kitaifa THRDC, Wakili Onesmo Olengurumwa na Wakili Paul Kisabo Mkuu wa Idara ya Utetezi THRDC wamefanya ziara ya kimkakati na kukutana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson. Ziara hiyo imefanyika katika Ofisi ndogo ya Bunge iliyopo jijini Dar es Salaam.
Lengo kuu la ziara hiyo lilikuwa ni kueleza shughuli ambazo THRDC na Washirika wake ambao ni Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika (PALU) wamepanga kuzifanya kwa kushirikiana na wadau wa masuala ya haki za binadamu, taasisi zinazohusika na utawala wa Sheria nchini ili kuimarisha mchango wa Bunge katika masuala ya utawala wa sheria na haki za binadamu nchini.
Vilevile, THRDC imewasilisha ombi kwa Mhe. Spika la kuanzishwa kwa Kamati Maalumu ya Bunge ya Masuala ya Haki za Binadamu ambayo wabunge watashirikiana na Watetezi wa haki za binadamu na Mashirika ya haki za binadamu katika kufanya kazi kwa pamoja.
Mhe. Dkt. Tulia amepongeza jitihada zinazofanywa na THRDC na washirika wake katika kuimarisha ushirikiano na taasisi zinazohusika na masuala ya haki za binadamu na utawala wa sheria nchini. Ameahidi kuwa ofisi yake itatoa ushirikiano katika shughuli ambazo THRDC na washirika wake wanazifanya.
Ziara hii ni sehemu ya utekelezaji wa mradi ambao Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) na Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika (PALU) wanafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) unaolenga “Kuboresha Utawala wa Sheria, Utawala Bora, Nafasi ya Kiraia, na Uwajibikaji nchini Tanzania kupitia Ushirikiano Ulioimarishwa.”
*Imetolewa na:*
*Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC)*
*05 Mei 2025*
Leo Mei 06, 2025 Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) na Jumuiya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) wamefanya ziara ya kimkakati na kukutana na Uongozi wa Mahakama Kuu Zanzibar. Kikao hicho kimefanyika Mahakama Kuu, Tunguu, Unguja, Zanzibar. Lengo kuu la kikao hicho lilikuwa ni kujadiliana namna bora ya kushirikiana katika kufanya Mkutano wa pamoja kati ya Majaji, Mahakimu, Mawakili na wadau wengine wa haki (Bar – Bench Forum).
THRDC iliongozwa na Mratibu wa Kitaifa Wakili Onesmo Olengurumwa @OlengurumwaO , Suleiman Mujuni Baitani – Mratibu THRDC Zanzibar, Wakili Paul Kisabo @Advocate_Kisabo – Mkuu wa Idara ya Utetezi THRDC na Wakili Shadida Omari – Afisa Programu THRDC Zanzibar, na Wakili Salma Omary – Afisa Programu ZAFELA. Mahakama Kuu Zanzibar iliongozwa na Mrajis Mhe. Jaji Valentina Katema, Naibu Mrajis Mhe. Jaji Faraji Shomari, Mkurugenzi wa Mipango Mhe. Mohamed Salim na maofisa wengine wa Mahakama Kuu Zanzibar.
Katika kikao hicho wamejadili namna ya kushirikiana kwa pamoja katika maandalizi ya kufanya Mkutano wa pamoja kati ya Majaji, Mahakimu, Mawakili na wadau wengine wa haki (Bar – Bench Forum). Kikao kimeafiki kuunda Kamati Maalumu ya kufanya maandalizi ya mkutano huo. Kamati hiyo itajumulisha Mahakama, Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Chama cha Wanasheria Zanzibar, Wizara ya Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar na Sekretarieti kutoka THRDC, EALS, ZAFELA na PALU.
Kikao cha leo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya kikao cha taasisi zinazohusika na masuala ya haki za binadamu, utawala bora pamoja na wadau wengine wa haki ambacho kilifanyika Aprili 8, 2025 jijini Dodoma na kuazimia kuunda Kamati ya Kitaifa kwaajili ya kuandaa Mkutano wa pamoja kati ya Majaji, Mahakimu, Mawakili na wadau wengine wa haki (Bar – Bench Forum).
Vilevile hii ni sehemu ya utekelezaji wa mradi ambao Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika Mashariki (EALS) na Jumuiya ya Wanasheria wa Afrika (PALU) unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) unaolenga “Kuboresha Utawala wa Sheria, Utawala Bora, Nafasi ya Kiraia, na Uwajibikaji nchini Tanzania kupitia Ushirikiano Ulioimarishwa.”
*Imetolewa na:*
*Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC - Zanzibar)*
*Mei 06, 2025*
Building Strategic Engagement and Partnerships among rule of law actors. With me are Chief Justice of Zanzibar, Hon. Khalid Ramadhani, Chief Kadhi, Hon Shekh Othman Omary, Deputy Kadhi , Registrar’s HC Zanzibar , President Zanzibar Law Society and representatives from PÀLU , EALS, ZAFELA and THRDC -Zanzibar.
THRDC Zanzibar plays a fundamental role in ensuring judicial reforms process are effective, inclusive and based on human rights approaches. We are very proud to see the current progress made by the Judiciary of Zanzibar for past few years. For the last few years the Judiciary of Zanzibar has made a significant change in upholding the rule of law, judicial reforms, access to justice, particularly in ensuring fair administration of justice and strengthening public trust in legal institutions.
This collaboration aligns with Zanzibar’s Judicial Strategic Plan and broader governance reforms aimed at promoting justice and human rights. We also seek to explore opportunities to deepen engagement between the Judiciary, bar associations, civil society, and key stakeholders to improve legal awareness and strengthen civic space protections. @LawyersofAfrica@ealawsociety@TanganyikaLaw@zafela@THRDCOALITION@ThrdcZanzibar@judiciarytz@Mwabuk2Boniface@EUinTZ@SwedeninTZ@MBaitani
"Ziko wapi enzi za ulumbi na waneni wenye Kiswahili mufti? Kitabu hiki kinarejesha hadhi ya lugha na kueleza ukombozi wa Afrika na Tanzania kama kinara wake. Ni mwenge wa matumaini kwa kizazi cha sasa na kijacho." @NkumbiJoram
Hiki kitabu ni fumbua macho! Hongera sana 👏👏
@fumbokhanJr Nadhani hilo sio swali sahihi. Swahili sahihi ni makatazo yalitoka kwenye torati "Sheria za Musa". Je, Musa wa kila dini ni tofauti? Maana katika wanyama aliyokatazwa kumegawanyika makundi wengine wanakula wengine wanaitwa "Haramu". Je, ni orodha gani sahihi? #Tafakuri
@JoelbertShamte 1. Pause and breathe
2. Acknowledge your feelings
3. Use positive self-talk
4. Practice active listening
5. Employ emotional regulation techniques
6. Seek support
7. Take responsibility
8. Set boundaries
9. Develop coping strategies
10. Reflect on outcomes👑