@xlusako Taasisi ya Urais ni kubwa sio ya Mtu mmoja Rais atatoa jina ataliwasilisha kwa taasisi kwaajili ya verting baada ya makubaliano ndio ataambiwa apeleke jina kwa spika wa bunge
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 259
Baada ya Mapumziko mafupi Tundu Lissu amepata angalau nusu saa ya kuzungumza na Mawakili na mashahidi wake ambao ni Makamu Mwenyekiti John Heche, Katibu Mkuu John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Amani Golugwa na Brenda Rupia.
Mawakili wake ambao alikuwa nao kwenye mashauriano ni Dr. Nshala Mwanasheria Mkuu wa Chama, Deogratias Mahinyila, Paul Kisabo na Edward Heche.
Inapigwa Courrrrrt
Majaji wanaingia
Mawakili wa Serikali wanasema wako tayari na Mhe. Lissu anasimama anasema Waheshimiwa majaji kabla hatujaendelea ninaomba maelekezo ya Mahakama kuhusu mashahidi wangu wa Chama maana wote wamo humu ndani je watoke nje au wabaki?
Jaji Ndunguru anajibu kuwa wanatakiwa watoke nje wataitwa wakihitajika kutoa ushahidi.
John Heche, John Mnyika , Amani Golugwa na Brenda Rupia wanatoka nje
Jaji Ndunguru anamwalika Tundu Lissu kwenda kwenye kizimba cha mashahidi maana alichokaa ni cha watuhumiwa
Tundu Lissu anahamia kizimba cha mashahidi wakati anaenda namuona anashikana mkono na dada ake na wapendwa wake huku akitabasamu, lakini akiwa anasindikizwa na maaskari magereza wa kutosha wasiopungua 8.
Jaji Ndunguru anamuuliza Lissu majina yake, umri wake miaka 59 na dini yake ni Roman Catholic
Jaji Ndunguru anamwambia tunaamini unatoa ushahidi wa kiapo?
Mhe. Lissu anajibu ndio Mhe. Jaji ila sijawahi kutoa ushahidi ingawa nimeshtakiwa mara nyingi sana ila sijawahi kufikia hatua hii
Watu wanacheka😂😂😂😂😂😂
Anaongozwa kuapa na ameapa.
Mhe. Tundu Lissu anaendelea kuhusu kazi yake amesema ni wakili na kiongozi wa kisiasa, ni Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa.
Nilichaguliwa na kutangazwa kuwa Mwenyekii wa CHADEMA Taifa Januari 22, 2025.
Kabla ya hapo Mimi nimekuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Mbunge wa vipindi viwili na nilishambuliwa kwa risasi Septemba 7, mwaka 2017 lakini pia nimewahi kuwa Mkurugenzi wa Sheria CHADEMA, Ex Official Member wa Chama,
Mwaka 2010 nilichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki (siku hizi linaitwa Ikungi Mashariki) na nilichaguliwa kwa tiketi ya CHADEMA, na mwaka 2015 hadi 29 Juni 2019. Sasa ilikuwaje nikaishia 29 June 2019??
Nawarudisha Septemba 7, 2017 ambapo nilifuatwa kwenye makazi yangu Dodoma na kushambuliwa kwa risasi na watu ambao Serikali ya Tanzania inawaita watu wasiojulikana.
Waheshimiwa majaji nilikimbizwa kwa ndege hadi Nairobi hospital hadi Tarehe 4 Januari 2018 na baada ya hapo nilipelekwa Ubeligiji kwa Matibabu zaidi katika hospital ya chuo kikuu cha Leuven. Nilitibiwa hadi Januari 2022.
Kati ya Nairobi na Leuven nilifanyiwa operation 25 (operation 17 Nairobi Hospital, 8 Leuven). Waheshimiwa majaji mkiona navuta mguu ni kwasababu ya matukio hayo.
Nikiwa hospital tarehe 29 June 2019 aliyekuwa Spika wa Bunge Job Ndugai (marehemu sasa) alinifuta ubunge kwasababu alisema nilikuwa mtoro, alikuwa hajui niliko.
Licha ya kuwa Mbunge na kuumizwa vibaya sana nikiwa kazini Bungeni, Bunge na Serikali ya Tanzania ilikataa kulipa gharama ya matibabu yangu, sikupewa hata senti moja, licha ya Sheria ya Bunge inayosema kwamba mbunge akiugua atatibiwa kwa gharama za bunge lakini mimi kwangu walikataa katakata kabisa.
Nikiwa Bungeni kipindi chote nilikuwa Mnadhimu wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni yaani ni kiongozi wa pili kwa viongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni.
Part 260 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.