#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 236
Mabishano yanaendelea hapa kidogo kati ya Mhe. Lissu na Wakili wa Serikali.
Mhe. Lissu anawambia Majaji kwamba yeye aliuliza kama Shahidi alielezea sababu ya huo utofaut so hawezi akatoa sababu sasa hivi itakuwa kitu kipya hivyo na yeye ataomba aruhusiwe kufanya cross examination kwa Mara nyingine.
Jaji Ndunguru anamwambia Katuga rephrase swali lako.
Katuga: Hebu shahidi sijui kama tunaelewana tuambie kama umeeleza sababu ya utofauti kati ya maelezo uliyotoa polisi na haya uliyotoa hapa Mahakama.
Ulikuwa unamaanisha nini..???
ACP Amin Mahamba :Kwa kweli sijaeleza sababu ya utofauti lakini nachofahamu yale niliyoandika nikiwa ofisin na haya ya hapa mahakamani, majibu niliyotoa yalitokana na jinsi nilivyoongozwa na waendesha mashtaka basi.
Kimya kinapita kama sekunde kadhaa, Wakili wa Serikali Katuga anarud kukaa na kujaribu kuzungumza na Mawakili wenzie wa serikali
Jaji: tuendelee
Katuga: Samahani Waheshimiwa dakika mbili nizungumze na wenzangu.
Katuga anajadili na wakili Mkuu Serikali Ajuaye na wakili Job Mrema, baadaye anaongea na Wakili mwingine wa Serikali Ignas Mwinuka..
Huenda wanatafuta maswali๐๐๐
Anamaliza kuconsult Wakili Katuga na kusimama tena
Katuga : Baada ya ku consult na wenzangu, tumeona tuishie hapa kwa faida ya Mahakama
Ni hayo kwa shahidi huyu
Ukimya unaendelea tena kwa sekunde kadhaaโฆ
Jaji anasema: shahidi umemaliza kutoa ushahiid wako, Mahakama inakuruhusu.
Shahidi anatoka mahakamani nduki kama mwizi aliyekwapua simu.๐
Ikumbukwe kwamba shahidi huyu ambaye ndo mpelelezi Mkuu wa kesi hii, dhidi yake kumekuwa na minongโono mingi kuhusu identity yake.
Ukiacha madai yalizonguka mitandaoni ya mtu anayedai kuwa ni mjane wa MAHAMBA lakini pia karibuni zimejitokeza taarifa kuwa shahidi huyu sio MAHAMBA halisi.
Haya yanasemwa na watu waliofanya kazi na shahidi huyu kwa miaka mingi wakidai kwamba jina halisi la shahidi huyu anaitwa PETER JUMAMOSI
Anasimama wakili wa Serikali Ajuaye kwa leo tulikuwa na shahidi huyu tu hivyo tunaomba Mahakama iridhie mpaka kesho
Mhe. Lissu: Kama mtakumbuka sawasawa kulikuwa na amri upande wa mashtaka walete mashahidi wawili ama watatu, je amri hii imekuwa vacated?
Tumeshachelewa sana na hatukuchelewa kwa sababu zenu wala zangu ila sababu ni zao upande wa Jamhuri, tukiendelea kuchelewa hivi mimi naendelea kukaa Gerezani wakat narudia tena SINA HATIA.. kwa hiyo kuanzia kesho waje na mashahidi wa kutosha
Jaji Ndunguru anasema kesi imehairishwa hadi kesho asubuhi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 235
Bado kimya kimetawala mpaka muda huu.
Wakisubiriwa upande wa Serikali waanze kumhoji Shahidi wao (Re-examination) kwa ajili ya kufukia mashimo yaliyotengenezwa na utetezi na kurepair.
Majaji wanatoa maelekez, tuendelee kwa Re- examination.
Wakili wa Serikali Anasimama anasema tunayo maswal machache
Atauliza Katuga.
Katuga Anasimama anamwambia Shahidi pole kwa maswali mengiiii yaliyojaa hotuba, Relax
Katuga : Usitegemee kukuta maswali ya sijui Tume, Sijui nini sawa? Anarudia sawa mara kadhaa..
Katuga : Kama unakumbuka uliulizwa maneno kwamba tutazuia uchaguzi, tutakinukisha hayo maneno yana neno Serikali, ulijibu lipo, Ulimaanisha nini?
ACP Amin Mahamba : Nilipotamka neno Serikali lipo nilikuwa naamanisha kwamba Serikali ndo yenye mamlaka au wajibu wa kutekeleza au kusimamia Sheria za nchi, kwahiyo kutamka maneno kama hayo.. kwamba utavuruga uchaguzi, utazuia maana yake ni kuitishia Serikali ambayo ndo ina jumumu la kulinda na kutunza usalama wa nchi nlikuwa namaanisha hivyo.
Katuga: -Tuendelee kijikita hapa hapa kwenye maswala yaliyopo mbele ya Mahakama.
Uliulizwa ni nani aliyechapisha maneno hayo, ukajibu ni wewe, tena ukamkomali, ukapelekwa kwenye ushahidi wa P ukieleza kwamba wao ndo waliosambaza P na P1, ukasomeshwa kwamba bwana Bagyemu aliona hayo maneno kwenye YouTube
lakini ukazidi kusema ni wewe(Lissu) ndo uliyechapisha.?
ACP Amin Mahamba : Nilikuwa naamanisha kwamba mshtakiwa ndo alikuwa kaiongea mbele yao wale wote waandhsi wa habari.. yeye ndiye aliongea mbele ya wale waandshi wa habar ambao walikuwa wakirusha yale live so yeye ndiye aliyesababisha warushe ye live. Na kwamba naamini kama ile ilikuwa nia yake sababu kama alikuwa hataki yale matangazo yarushwe mubashara asingeruhusu yarushwe sababu aliruhusu yarushwe.
Katuga: kwahiyo ndo maana ukakomaa ni wewe ni wewe ???
ACP Amin Mahamba : Ndio
Katuga: Ulisomeshwa kifungu cha 39 japo wewe si Mwanasheria, ukaulizwa haya maneno kuzuia uchaguzi, kukinukisha.. yamo kwenye hicho kifungu?
Na majibu yako uliendelea kusisitiza yamooo
ACP Amin Mahamba ;Nilikuwa namanisha kuwa katika kile kifungu cha 39(2)b kuna neno limeandikwa kwa nia ya kutishia serikali, Kwahiyo yale maneno alimaanisha ile nia.
Katuga: Shahidi kingine umeulizwa sanaโฆ sijui mwaka fulan, madai ya Katiba, ccm sijui nn, mimi sio mwanasiasa
Ifafanulie haya madai ya Katiba na madai haya ya uhaini nini majibu yako kwenye hii Katiba na kesi ya uhaini???
ACP Amin Mahamba : Napenda kusema kwamba, kama una madai ya msingiโฆ.
Shahidi anakatishwa na wakili wa serikali Katuga hivyo vitakiwa vitu vipya
ACP Amin Mahamba; hayahusiani na haya
Katuga: Sasa shahidi kuna maswali mengi lakini swal moja wapo linahusiana na vurugu za 29/2025.
Uliulizwa kwamba wewe na timu yako ya polisi mlifanya vurugu siku hiyo, ulijibu ukazuiwa na ulikuwa unaamanisha nini???
ACP Amin Mahamba : Sio kweli kuwa mimi na timu yangu au na Jeshi la Polisi tulihusika na zile vurugu kwan upelelezi tuliofanya tulibaini kuwa zilitokana na uhammishishaji au uchochezi uliofanywa awali na kubaini kwamba kulikuwepo na maandalizi ya vurugu hizo kabla ya 29/10/2025.
Mhezz Lissu anainuka anasema Waheshimiwa majaji mimi sikuuliza hilo swali, Shaidi anajibu kitu kipyaโฆ akiruhusiwa nitaomba nami ni mcross examine
Jaji: tuendelee
Mhe. Lissu anasimama na kusisitiza kuwa akiruhusiwa nitaomba niruhusiwe
Jaji: tuendelee
Mhe. Lissu: kama mmesema hivyo tuendelee
Katuga; Uliulizwa je unataka maelezo uliyotoa polisi uaminiwe, ukajibu ndiyo ya hapa Mahakamani, ukajibu pia ndio.
Hebu tupe ufafanuzi kuhusiana na utofauti, uliotoa polisi na uliotoa mahakaman?
Mhezz Lissu anainuka tena na kusema hicho kitu sicho nilichouliza.
Lissu anasema niliuliza kama ameeleza kuwepo kwa tofauti, Akieleza sababu nitataka ku pewa nafasi ku cross
Katuga anaelezea hapa
Na Mhe. Lissu anaeleza piaโฆ
Part 236 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 234
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba
Mhe. Lissu: Kama unafahamu au hufahamu Tume iliundwa pia ya Mark Boman.. kuangalia utaratubu wa Katiba nayo ikapendekeza kuwe na Katiba mpya na Serikali ya Mkapa na ccm yake ikakataa????
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu: Kama hufahamu au unafahamu Kikwete aliunda Tume ya Mabadilio ya Katiba (ya Warioba) ambayo sio tu ilipendekeza Katiba mpya bali pia iliandaa Rasimu halafu Serikali ikakataa???
ACP Amin Mahamba; Sijawah kupitia
Mhe. Lissu: Eleza kama unafahamu au hufahamu tunafanya Uchaguzi Mkuu kila baada ya mikaa 5???
ACP Amin Mahamba : sahihi
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu katika kila Uchaguzi mkuu wa vyamana vingi Watazamaji wa Kimataifa na Kikanda, Jumuiya ya Ulaya, COMMON WEALTH, Marekani., Canada, Japan, AU, SADC, Jumuiya ya Afrika kila Uchaguzi Mkuu wamependekeza kuwa Serikali itungwe Katiba mpya na mfumo mpya wa Uchaguzi ili kuondoa matatizo mengi ya kiuchaguzi???
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu Tumeambiwa kila baada ya miaka 5 na ccm imekataa, Eleza kama unafahamu ilani ya ccm ilikuwa na ahadi ya Katiba mara baada ya uchaguzi 2015 na 2020.
ACP Amin Mahamba anajibu haraka SIFAHAMU hata kabla swali halijaisha.
Watu Wanacheka ๐๐๐๐
Mhe. Lissu : Samia alisema Katiba haiweki ugali mezani, unafahamu?
ACP Amin Mahamba ; Sifahamu
Mhe. Lissu: Kwasababu ya kukataa huku kila Uchaguzi mkuu lazima uendane ma maujaji ya Watanzania???
ACP Amin Mahamba -Sina uhakika na hilo
Mhe. Lissu: Eleza Kama baada ya maujaji ya Oktoba 29 mlichukua hatua ya kuniuliza haya maneno yana maana gani, unaposema mtakinukisha una maana gani au haya maneno ya uasi yana maana gani?
ACP Amin Mahamba : Hapana
Mhe. Lissu; Hamkutafuta ufafanuzi wa hayo maneno yangu?
ACP Amin Mahamba : Hukuwa tayari
Mhe. Lissu: Ningekuwa mjinga kiasi gani kujibu nikiwa kwenye pingu?
Mhe. Lissu: Nitakuwa sahihi kusema kuwa No reforms, No election ilikuwa sahihi kwa mazingira yale???
ACP Amin Mahamba : sio sahihi
Mhe. Lissu: Kwa mujibu wa tume ya jaji Chande Ghasia za oktoba 2025 zimetokana na changamoto mbalimbali ambazo hazikutatuliwa, anazisoma kama madai ya katiba mpya.
Waeleze majaji kwamba huo ni msimamo sahihi?
ACP Amin Mahamba ;Unakosea
Mhe. Lissu: kwahiyo hata Jaji Chande alikosea?
Lissu anamsomea sababu kama zilivyo kwenye hotuba ya Jaji Chande.
ACP Amin Mahamba: Sikupata nafasi ya kupitia
Mhe. Lissu: Hayo mnayodai ni makosa yangu, waeleza Majaji kama unafahamu au hufahamu kuwa 13/2/2026, Kikosi kazi cha Kamati ya Umoja wa Mataifa, Kikosi kazi cha Haki za Binadamu, kinachoshughulikia watu wanaokamatwa bure arbitrary detention) kimetoa taarifa na taarifa hiyo inasema kukamatwa kwangu na kushtakiwa huku ni kukuka haki za binadamu na wakapendekeza nilipwe fidia???
ACP Amin Mahamba : sijawah kufahamu
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu mwezi ulipoita 10 july, kamati ya Mawaziri wanaowakilisha nchi za Jumuiya ya Madola imetoa taarifa inayoitaka Serikali ya Tanzania kuniachilia huru bila mashart yoyote ndan ya siku 30 kuanzia 10 july na wakaeleza watatake appropriate action isipofanyika hiloโฆ???
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu: Kama Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola, Mawaziri kabisa sio wale WANAHARAKATI msiowapenda wanasema aachiliwe ndani ya siku 30 vinginevyo tutawashughulikia, huyu mtu anayepiganiwa na Taasisi hizi ni mtu mbaya anayetakiwa kunyongwa hadi afe?
ACP Amin Mahamba ;Sina uhakika
Mhe. Lissu anamaliza maswali na kukaa chini
Kimya kinaendelea mahakamani kwa muda kidogo
Part 235 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 233
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Eleza kama hao waliosema watafanya vurugu, mkawaachia na wakaenda kweli kufanya vurugu kama kuna hata mmoja mliemchukulia hatua?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu : Kimya maana yake hamkuchukua hatua
ACP Amin Mahamba ; Hapana, nimeona unakumywa maji
Mhe. Lissu : Ninakunywa kahawa
Mhe. Lissu : Mkoa wa Mwanza 29/10 kwa mujibu wa ripori ya jaji chande waliuawa watu 90, eleza kama Mwanza ina RPC?
ACP Amin Mahamba : Yupo
Mhe. Lissu : Yule ambaye yupo kwenye vyombo vya habari kila siku hata gerezani namsikia? Anaitwa Mutafungwa
ACP Amin Mahamba : ndio
Mhe. Lissu : Kwa Mikoa minne watu 405 kwa mujibu wa taarifa ya Chande, kuna aliyechukuliwa hatua?
ACP Amin Mahamba: Sina taarifa
Mhe. Lissu : Kwa Mikoa 7, ni Songea tu mlipopewa taarifa kuwa watafanya vurugu?
ACP Amin Mahamba : Ndio lakini waliachiwa kwa mujibu wa taratibu ya sheria
Mhe. Lissu : Waeleze Majaji kama Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao hawakuripoti wamechukuliwa hatua kwa maafa yalitokea???
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika
Mhe. Lissu : Mara ya mwisho watu waliuawa na vyombo kiasi kikubwa hivyo ni mwaka 1905 kwenye Vita ya Majimaji.
Mhe. Lissu anaendelea kueleza awamu zote watu hawakuuawa kiasi iko kama ndani ya wiki 1 ya Samia wameuawa watu wengi
Mhe. Lissu anaelekea kwenye Ushahidi wa video, kwenye ushahidi wako kuhusiana na video, ulisema wewe na timu yako baada ya wewe kupanga timu zako 3, Je video mliyoangalia ilikuwa mtandaoni au ilikuwa kwenye memory card? Au ile iliyokuwa kwenye flash.??
ACP Amin Mahamba; Tuliangalia ile ya kwenye mtandao, Youtube
Mhe. Lissu; Nitakuwa sahihi kusema hamkuangalia ile video ya kwenye flash wala ya kwenye mamory card??
ACP Amin Mahamba ; Hizo hatukuangalia
Mhe. Lissu: Nitakuwa sahihi kusema pengine flash na memory card huenda hazina hata hizo video?
ACP Amin Mahamba ; sio kweli
Mhe. Lissu: umejuaje wakati hujaangalia?
Waeleze Majaji unajuaje kilichokuwa kwenye flash disk wakati hukua.???
ACP Amin Mahamba anakwepa
Mhe. Lissu anarudia
Shahidi umejuaje?
ACP Amin Mahamba: Wenzangu KAAYA na mwenzie walipakua hizo video na kuziweka kwenye flash.
Mhe. Lissu anarudia, swali langu wewe unajuaje kama zipo wakati hujaziona?
ACP Amin Mahamba: najibu kitaalamu sasa,
Mhe. Lissu anamkatiza jibu swal langu
ACP Amin Mahamba : Ngoja nijibu basi, nimefahamu kupitia taarifa ya mchunguzi
Mhe: Lissu: Hiyo taarifa ipo Mahakamani kama kielelezo???
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu anasema mimi nachojua taarifa ilikataliwa hapa mahakamani sababu haikuandaliwa na mtaalamu
Mhe. Lissu: Mpaka sasa wewe ni Shahidi wa 16, na nyie wote hakuna hata mmoja aliyewasilisha ushahidi wa video, taarifa ya uchunguzi wala nyaraka yoyote hakuna.
Mhe. Lissu: Nyaraka zote zilizoingia Mahakamani ni ushahidi wangu,
Mpaka sasa hakuna kilelezeo chochote zaidi ya story kwenye kesi hii.
ACP Amin Mahamba : sina kumbukumbu
Mhe. Lissu: Mkutano wangu ulizungumzia Katiba Mpya?
ACP Amin Mahamba anakataa
Mhe.Lissu : Waeleze Majaji kama unafahamu madai ya Katiba Mpya na mfumo huru wa uchaguzi ni madai yaliyopo kwa miaka 35 hapa Tanzania.
ACP Amin Mahamba : sifahamu
Mhe. Lissu; Eleza kama unafahamu au hufahamu kuwa Tume ya Jaji Nyalali, ilipendekeza itungwe Katiba mpya itakapofikia 1993?
ACP Amin Mahamba : Sijawah kuipitia
Mhe. Lissu: Eleza kama mapendekezo hayo yalikataliwa na Mwinyi?
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mheโs Lissu: Mkapa aliunda tume iliyoongozwa na Jaji Kisanga na ikapendekeza kuwe na Katiba mpya halafu Mkapa akasema hadharan mimi sikuwatuma waangalie maswala ya Katiba mpya, unafahamu au hufahamu???
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Part 234 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 12, 2026
Kesi ya uhaini dhidi ya Mhe. Lissu inaendelea katika Mahakama Kuu ya Dar es salaam ambapo Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross Examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Jana tuliishia part 231 so leo tunaendelea na
Part 232.
Imepigwa high court.
Majaji wameingia wapo watatu kama kawaida yao.
Mtuhumiwa nae ameingia japo leo Askari Magereza wamemzonga sana ili asisalimiane na watu.
Mtuhumiwa yani Mhe. Lissu amechukua nafasi yake, na shahidi Amini Mahamba amekaa katika kizimba tayari.
Karani anaita kesi kwa namba yake : JAMUHURI dhidi ya TUNDU LISSU
Mawakili wa serikali wanaongozwa na AJUAYE, Katuga, Job Mrema , Cuthbert Mbilingi na Winniwa Kasalla.
Majaji wanamuuliza mtuhumiwa kama yupo tayariโฆ
Mhe. Lissu anaomba kufanya consultation toka kwa Mawakili wake/researchers
Majaji wanamruhusu
Mawakili wake Nashon Nkungu Na Sisty Aloyce wanainuka na kusogea kizimbani kumconsult Mhe. Tundu Lissu wanateka Kama dakika tano hivi kisha wanarudi kukaa kwenye viti vyao.
Jaji anamkumbusha Shahidi kuwa bado yupo chin ya kiapo.
Mhe. Lissu anaruhusiwa aanze kumuhoji Shahidi.
Anamwambia leo hana maswali mengi sana
Anamuuliza kama alidhamiria kuwa maelezo yake aliyotoa alidhamiria yaaminiwe kama ushahidi wa kweli.
ACP Amin Mahamba anajibu kwamba ndio alidhamiria
Mhe. Lissu : Ulidhamiria kuwa maelezo yako uliyotoa kule Polisi yawe ushahidi Mahakamani?
Lissu anasema โIM TYING UP THE LOOSE ENDSโ
Anamuuliza kuhusu wale mashahidi waliofichwa waliotolewa mikoani.
Mhe. Lissu : Swala la kwanza eneno hilo; unakumbuka ulisema kwamba hawa mashahidi waliofichwa ni watu waliokamatwa na Polisi ni KWELI walikutwa wakipanga njama?
ACP Amin Mahamba : sio tu kupanga niama, na kuhamasisha
Mhe. Lissu: Walipokamatwa walikiri Polisi kupanga kufanya njama na vurugu Uchaguzi na kadhalika ni kweli??
ACP Amin Mahamba : Hayo yalikuwa ni makosa ya jinai.
Mhe. Lissu: Wakakiri kwa maandshi?
ACP Amin Mahamba : Sahihi.
Mhe. Lissu: Waleleze Majaji hizo tuhuma za kijinai mlizowakamatia ziliishia wapi?
ACP Amin Mahamba : Waheshimiwa rejea maelezo yangu ya siku ya kwanza, kuwa baaada ya watu hao kukamatwa tuliitisha jalada, tukasoma tukapitia.
Mhe. Lissu: Umeelewa swali langu shahidi?
Nimesema sitaki unipotezee muda, nataka kutumia nusu saa.
Katuga anainuka
Kabla hajasema chochote Mhe. Lissu anamwambia kaa,
Katuga anasema si jukumu la Mhe. Lissu kumwambia akae chini.
Mhe. Lissu anakubali na kumueleza Shahidi kuwa akiuliza swal anataka jibu sio hotuba
Mhe. Lissu anauliza kuwa hizo tuhuma za kupanga njama ziliishia wapi?
ACP Amin Mahamba : Baada ya kupitia majaladaโฆ
Mhe. Lissu: kweli kuwa mliwafutia kesi wote?
ACP Amin Mahamba : sahihi
Mhe. Lissu : Tuanze na DSMโฆ 29/10.. kulitokea vurugu zilizoua watu 182
ACP Amin Mahamba: Mimi sio msemaji wa Jeshi la Polisi, hizo ni taarifa nyeti.
Kwa mujibu wa Tume ya Jaji Chande watu 182 waliuwawa DSM.
ACP Amin Mahamba : si kweli
Mhe. Lissu: Katika wale watu waliokamatwa wapo wa kutoka Arusha
ACP Amin Mahamba : Kweli
Mhe. Lissu: Walikiri kupanga uhalifu, kupiga watu nk na Mkawaachia,?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe.Lissu : Siku ya uchaguzi 29, kwa mujibu wa Tume ya Jaji Chande, waliuwawa watu 53 Arusha, watu ambao mlikuwa mnajua walichopanga mkawaachia, wakaenda kutekeleza hayo.?
ACP Amin Mahamba : Aaah, eeh
Mhe. Lissu : Twende Mbeya, kuna watu mlikwakamata Mbeya, walisema wanapanga kufanya vurugu kwenye Uchaguzi, watapiga watu mawe wakakiri halafu mkawafutia mashtaka kweli si kweli.
ACP Amin Mahamba : KWELI
Mhe. Lissu : Arusha, Dar es Salaam, Mbeya jumla ya watu waliouawa ni 315.
Eleze kama kuna Mkuu wa Polisi, au DC, alichukuliwa hatua kwa uzembe wa maafa haya?
ACP Amin Mahamba : Sina hakika kama kuna aliechukuliwa hatua
Part 233 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 229
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Shahidi apatiwe PGO namba 1 aya ya 25 Crimes are Actions defined by law yanayoitwa makosa ni matendo yaliyofafanuliwa na Sheria ya Upelelezi wa Polisi inabidi ufuate masharti ya sheria strictly.
Swali langu kifungu cha 38 (2)d kinataja tendo la kuvuruga uchaguzi ni kosa?
ACP Amin Mahamba : Hapana.
Shahidi kakubaliana na Mhe. Lissu kimtindo kuwa haijataja.
Mhe. Lissu: PGO namba 1 para 3 inasema kila Askari Polisi anawajibu wa kuheshimu Uhuru wa mwananchi kama ulivowekwa kwenye Katiba na Sheria na kwenda kinyume na haya haikubaliki, tafsiri iko sahihi au sio sahi?
ACP Amin Mahamba : Inategemea
Mhe. Lissu anarudia tena swali hilo hilo.
ACP Amin Mahamba anajibu hapa anajiumauma sana ni kweli tunatakiwa kuheshimu haki za raia imetoka kwa mbinde sana mdomoni mwake.
Mhe. Liss : Ibara ya 15 (1 kila mtu ana haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru kweli au si kweli?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli.
Mhe. Lissu; Kuna mahali umezingatia uhuru wangu kwenye maelezo yako polisi?
ACP Amin Mahamba : Hayapo ila aina ya kosa uliloshtakiwa nalo halitakiwi uwe huru, ninachotambua ulikuwa na haki.
Mhe. Lissu : Hao wenzio nilimalizana nao niko na wewe ulitambua haki yangu ya uhuru kwenye maelezo yako?
ACP Amin Mahamba : sikuweka
Mhe: Lissu : Ulizingatia Haki yangu ya uhuru wa kutoa maoni na fikra zangu kwenye maelezo yako uliyotoa polisi?
ACP Amin Mahamba : Ilizingatiwa
Mhe. Lissu anasoma hapa ibara inayoongelea haki ya mtu kutoa mawazo yake hadharan na kujumuika na watu...
Anasema Mwenyekiti wa chama alitoa mawazo yake alipokutana na watu wake hadharani ulizingatia haya?
ACP Amin Mahamba : Ulifanya makosa, uliitisha serikali.
Mhe. Lissu: Hayo maelezo ya kutisha serikali yako wapi? inaweza ikawa una shida ya akili
Shahidi : Kimyaaaa
Mhe. Lissu ; Ulizingatia kuwa nina haki ya kufaidi haki za kikatiba kutokana na ibara ya 29 na ukaweka kwenye maelezo yako?
ACP Amin Mahamba : Hapana sikuweka
Mhe. Lissu: Kama uliangalia video nilishambulia sana Tume ya Uchaguzi kuwa inapendelea CCM miaka yote na watumishi wanaohusika na Serikali, wanapendelea ccm pamoja na wizi wa kura..
ACP Amin Mahamba : Ndio ulisema
Mhe. Lissu : Nilisema kuwa Samia aliamuru wagombea wa upinzani waenguliwe kwenye uchaguzi wa Serikali za mtaa?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli, ulisema.
Part 230 itaendelea kwenye post inayofuata.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 228
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Hayo maneno ya kuvuruga Uchaguzi yapo kwenye hiko kifungu?
ACP Amin Mahamba : Yapo.
Mhe. Lissu : Tusomee
ACP Amin Mahamba anasoma hapa hiko kifungu
Mhe. Lissu:m : Ulichosoma kimeongelea uchaguzi?
ACP Amin Mahamba : Ndio yapo
Mhe. Lissu : Una akili timamu?
ACP Amin Mahamba : Ndiyo.
Mhe. Lissu anasikitika
Anamuuliza tena ni kweli iko kifungu kinaongelea mtu anaetishia Serikali, Bunge au Mahakama? ni kweli au si kweli?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli.
Mhe. Lissu : Na akatishia Bunge au Mahakama na kumalizia kosa lake kwa kuchapisha ndio amefanya uhaini?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli.
Mhe. Lissu : Mimi nilitishia Serikali,Bunge na Mahakam?
ACP Amin Mahamba : Ulitishia Serikali
Mhe, Lissu : Nilitishia bunge?
ACP Amin Mahamba: hapana
Mhe. Lissu : Nilitishia Mahakama?
ACP Amin Mahamba : hapana
Mhe. Lissu : Ulisoma shtaka nililoshtakiwa nalo hapa Mahakamani?
ACP Amin Mahamba : Ndio nililisoma.
Mhe, Lissu analisoma tena.
Mhe. Lissu : Hayo ndo maneno uliyoyapeleleza?
ACP Amin Mahamba : kweli ndo hayo niliyopeleleza.
Mhe. Lissu : Unajua maana ya neno serikali?
ACP Amin Mahamba : nafahamu
Mhe. Lissu : Serikali maana yake nini?
ACP Amin Mahamba : Ni mamlaka inayoongoza nchi.
Watu wanacheka kidogo hapa ๐๐๐
Afande anasema Serikali ni Bunge Mahakama na Mihimili Tendaji.
Mhe. Lissu : Hiyo ni kwa mujibu wa nini?
ACP Amin Mahamba : Kwa mujibu wa Katiba yetu
Mhe. Lissu : Naomba asome Art 151 d
ACP Amin Mahamba anasoma
Serikali maana yake ni pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Zanzibar, Halmashauri au mtu anaetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali...
Mhe. Lissu : Kwenye maelezo yangu nimetaja Halmashauri ya Jiji la Dar, nimetaja jina la Makam wa rais Samia, Nimetaja jina la Waziri mkuu Kassim Majaliwa au Mwenyekiti wa mtaa wa mwakasusa?
Watu wanacheka hapa Mwakasusa sijui ni kule kwetu Mbeya.๐๐๐๐
ACP Amin Mahamba: Haujataja hayo majina
Mhe. Lissu ; Ieleze Mahakama nani anasimamia Uchaguzi
ACP Amin Mahamba : INEC
Mhe. Lissu ; Kwenye maelezo yangu nilitaja Tume na Viongozi wake ama Mwenyekiti au makamishna?
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika
Mhe. Lissu : Je katika waliopeleleza yupo ASINSP Andrew Chulu na ndiye aliechukua memory card kutoka kwa P1 na P2 na kuleta Dar ?
ACP Amin Mahamba : sahihi ni yeye
Mhe. Lissu ; Ulisoma maelezo ya Insp Chulu?
ACP Amin Mahamba ; Ndio nilisoma.
Mhe. Lissu: Ni kweli au si kweli kwenye maelezo ya Chulu, kuna maelezo yafuatayo shahidi huyo P alinieleza alikuwa miongoni mwa mashahidi waliokuwepo kwenye Mkutano akitokea Jambo tv na kuirusha mubashara kupitia account ya YouTube ya Jambo tv na instagram ya Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli
Mhe. Lissu : Na unasema umesoma maelezo ya P kweli au si kweli?
ACP Amin Mahamba : Kweli
Mhe. Lissu anarudia tena maelezo ya P kuwa Jambo TV walirusha maelezo ya Lissu live na walirusha kwenye mtandao wao wa YouTube hayo maelezo umeyasoma?
ACP Amin Mahamba : kweli nimeyasoma
Watu wanacheka ๐๐๐
Unajua huyu shahidi kule mwanzo alisema Mhe. Lissu ndo aliyechapisha na kupandisha Video kwenye account ya YouTube ya Jambo tv
Anyways tuendelee
Mhe. Lissu : Mnanitesea nini wakati mna ushahidi wa waliofanya makosa na kurusha hivi vitu mtandaoni?
ACP Amin Mahamba : Jukumu langu ni kupeleleza shtaka
Mhe: Lissu : Mnanitesea nini kama watu waliofanya kosa la kuirusha hiyo video mnao?
ACP Amin Mahamba : Hauteswi.
Part 229 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 227
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shaidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Waeleze Waheshimiwa Majaji kama mimi nilidessiminate hiyo video mtandaon au kama nilipublish hiyo video mtandaoni?
ACP Amin Mahamba ; Ndio ni wewe.
Mhe. Lissu; Waeleze majaji kama nimeajiriwa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika na hilo.
Mhe. Lissu : Waeleze majaji kama mimi ni mpiga picha wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : sina uhakika
Mhe. Lissu : Na wewe ndo ulikuwa mpelelezi wa kesi hii na huna uhakika na mambo na yote unayosema hapa?
Mhe. Lissu : Ni kweli hio video ya ilichukuliwa na P1 mfanyakazi wa jambo tv?
ACP Amin Mahamba ; Sio kweli.
Mhe. Lissu : Taratibu wewe Afande, Ni kweli au si kweli kwamba kwenye maelezo uliyoyasoma ulisema P1 alikuwa anarusha video mubashara kupitia camera yake ya Sonny Ericsson?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni kweli.
Mhe. Lissu : Waeleze Majaji kama ni kweli kwenye maelezo ya P1, yeye ndiye aliyehifadhi na kurusha mubashara video kwenye Mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli
Watu ๐๐๐๐๐ Shaidi kakataa kona, amekubali Penalty.
Mhe. Lissu ; Ulisoma maelezo ya George Bagyemu?
ACP Amin Mahamba : Ndio nilisoma.
Mhe. Lissu : George Bagyemu alisema kwenye maelezo yake aliyojiandikia mwenyewe kama wewe kuwa video ilirushwa na kurekodiwa na Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli
Mhe. Lissu : Mashaidi P1 na P2 walipewa maelekezo ya kucover Mkutano wangu na John Marwa?
ACP Amin Mahamba : Ndio
Mhe. Lissu : Waeleze Mahakama kwamba John marwa alipewa mualiko na
Mkurugenzi wa habari Chadema mimi ndio Mkurugenzi wa habari?
ACP Amin Mahamba : Hilo sijalifanyia kazi
Mhe. Lissu : Nimekaa mahabusu mwaka na miezi 4 kwa kosa ambalo wamemfanya Jambo tv, Waeleze Majaji kama huu ndio utendaji wa Jeshi la Polisi la Tanzania?
ACP Amin Mahamba : Waheshimiwa Majaji mshtakiwa ananipitisha kwenye maelezo ya P1 na P2
Huyu Polisi anaongea kwa dharau sana hapa
Mhe. Lissu anamkatisha anamjibu lissu majaji wanamtuliza Shahidi
Mhe. Lissu : Anarudia tena maswali yake na anaongeza kuuliza kama John mnyika alihojiwa?
ACP Amin Mahamba : Hapana
Mhe. Je Golugwa alihojiwa ili waseme?
Mhe. Lissu Je Mkurugenzi wa habari wa CHADEMA alihojiwa?
ACP Amin Mahamba ; Hao wote ni sehemu yako siwezi kuwahoji.
Mhe. Lissu: Mwenyekiti wa Chama anawajibika kijinai kwa Makosa ya kijinai ya watu wengine?
ACP Amin Mahamba : Umeshtakiwa kama lissu sio Mwenyekiti.
Afande anakimbia kujibu swali hapa ๐
Mhe. Lissu : Je Mwenyekiti wa Chadema anawajibikia kijinai kwa kosa ambalo umelitenda wewe au kwa makosa ya watu wengine?
ACP Amin Mahamba : Huwajibiki
Mhe. Lissu : Nawajibika au siwajibiki?
ACP Amin Mahamba : hauwajibiki
Mhe. Lissu :Turudi kwenye maneno niliozungumza, Waeleze majaji kuwa ni kweli au si kweli hotuba ilikuwa inahusu shida ya Uchaguzi Mkuu kwa mujibu wa Lissu?
ACP Amin Mahamba : Kweli
Mhe. Lissu : Maswala yaliyopo kwenye uchaguzi ni maswala yaliyoko kwenye katiba ya nchi na taratibu za nchi?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli.
Mhe. Lissu : Kwa katiba hii mtu anaetaka uchaguzi usifanyike kwa katiba hii amefanya kosa?
ACP Amin Mahamba : hapana sio kosa.
Mhe. Lissu : Unajua sheria ya uchaguzi na kuna kosa linaloongelea kuvuruga uchaguzi?
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika sana na sheria ya uchaguzi.
Mhe, Lissu: Mimi nina uhakika sheria ya uchaguzi haina kosa la kuvuruga uchaguzi na mmelisema kama kosa la uhaini, mimi nitasema sio kosa la jinai wewe unasemaje?
ACP Amin Mahamba : makosa na sheria ziko nyingi
Mhe. Lissu : Tutaenda huko kote apewe penal code s.39(2) d asome kama hilo kosa linasema kuzuia Uchaguzi au kuhamasisha watu kutofanya uchaguzi ni kosa?
ACP Amin Mahamba : Nikitafasiri hii sheria...
Mhe. Lissu anamwambia kutafsiri sheria ni kazi ya Wanasheria sio mapolisi.
Watu wanacheka: ๐๐๐
Part 228 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 11, 2026
Last time tuliishia Part 225 so leo tunaendelea na-;
Part 226
Jana Shahidi wa upande wa Jamhuri ACP Amin Mahamba alianza kutoa ushaidi wake na leo Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross-examination.
Mhe. Lissu : Unaweza kuiambia Mahakama kwamba ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa
Mhe. Lissu : Mke wa Amin Mahamba anasema kwamba Amin Mahamba alifariki, sasa iambie Mahakama ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Huyo Amin Mahamba anaetajwa sio mimi.
Mhe. Lissu : Kwahiyo ni ushahidi wako kuwa huyu Amini Mahamba ni mwengine sio wewe?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni mwingine tena yeye ni mstaafu na wanasema alishariki kweli kama unavosema.
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama ulimshirikisha RSO kwenye upelelezi wako?
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulimshirikisha afisa yoyote wa TISS.
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Unafahamu Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa?na kama uliishirikisha kamati ya ulinzi ya mkoa wa Dar es salaam?
ACP Amin Mahamba :Naifahamu na sikuwaashirikisha
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ikulu?ofisi ya VP au Waziri mkuu?
ACP Amin Mahamba : Sikuishirikisha na sikuwaambia lolote.
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ofisi ya DPP ndio nilishirikisha kanda maalum NPS.
Mhe. Lissu :Ulimshirikisha nani?
ACP Amin Mahamba: Incharge Mayenga
Mhe. Lissu : Umesema kokote kwenye nyaraka yako?
ACP Amin Mahamba : Sijasema na sijamtaja
Mhe. Lissu : Kwa mujibu wa sheria ya NPS mwenye jukumu la kuratibu upelelezi ni DPP na Mastate Attorney wake.
Waeleze ni DPP yupi au State Attorneys yupi?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu : Jibu swali wewe Polisi
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa swali.
Mhe. Lissu : Swali langu linahusu nani aliecordinate upelelezi?
ACP Amin Mahamba : Ni DPP Mwenyewe, aliteua mtu nilisema jana kuwa sijui jina lake alitoka ofisi ya DPP Dodoma na nilisema ana jina la kibantu nimesahau.
Mhe. Lissu : Tutaenda kwa DPP Mwakitalu atupe hilo jina tuko kwenye serious matters.
๐๐๐ inachekesha sana maana jamaa hajui jina la mpelelezi ambae alishirikiana nae kufanya upepelezi pamoja na kufungua faili la kesi hii.
Mhe. Lissu : Umesema wewe ni mpelelezi wa muda mrefu umewahi peleleza kesi ya kisiasa?
ACP Amin Mahamba : Sijawahi
Mhe. Lissu : Kesi ya uhaini ni kesi kubwa sana ni highest in the land kwahiyo hujawahi kabisa na hii ndo kesi ya kisiasa ya kwanza.??
ACP Amin Mahamba : Sijawahi hii ndio ya kwanza
MheZ Lissu : Umewahi peleleza kesi ya mtu alikuwa mbunge na kiongozi wa Chama kama lissu?
ACP Amin Mahamba :Sijawahi
Mhe. Lissu : Umesema kitengo chako kinashugulika na makosa ya mtandao
ACP Amin Mahamba : Ndio
Mhe. Lissu: Ushapeleleza kesi ya cybercrime?
ACP Amin Mahamba : Ndio nimewahi.
Mhe. Lissu : Kesi gani shahidi?
ACP Amin Mahamba ; Nakumbuka nikiwa RCO Kinondoni
Naona kasita kama dakika 5 hivi then akasema kesi ya Mbowe na Mzee wa karatu Slaa
Mhe. Lissui : Waeleze ilikuwa inahusu nini na iliishaje?
ACP Amin Mahamba ; DPP hakuwa na interest ya kuendelea na kesi ikaisha hewani.
Mhe. Lissu : Una kesi zingine zaidi ya hizi kwenye cybercrime?
ACP Amin Mahamba ;Hapana
Mhe. Lissu: kwahiyo hauna kesi nyingine zaidi ya hiyo iliyofutwa?
ACP Amin Mahamba : Ninazo nyingine nyingi siwezi kuzikumbuka nikiwa RCO na OCCID.
Mhe. Lissu : Kwahiyo jana kweye ushahidi wako unasema mimi ndie niliechapisha video yangu hapa mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndiyo nilisema.
Mhe. Lissu ; Unafahamu maana ya neno kuchapisha mtandaoni?
ACP Amin Mahamba : Ndio nafahamu lakini sheria ambayo imetumika kukushitaki sio Cybercrime.
Mhe. Lissu : Waeleze waheshimiwa majaji kama mm ndie nilisambaza video za YouTube kwenye mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni wewe ulisambaza hizo video.
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
Siku tutakayokufa, hatutaitwa tena kwa majina yetu. Watasema, โLeteni mwiliโ au โShusheni mwili kaburini.โ Jina hubaki nyuma. Hivyo, tuishi kutafuta ridhaa ya Muumba, si sifa na makofi ya viumbe.
@Jambotv_ Kuna usamjo Fulani unataka Kufanyika Hapa, yaani Wananchi wapambane wapate katiba mpya, wapambane dhidi ya nani? Nani anamamlaka ya kupitisha na kutekeleza Hilo Jambo๐๐๐
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 27
Anaendelea Wakili wa Serikali wakuitwa Wisdom.
Wisdom : Ulipokuwa unasema wasaidizi wako watekeleze kwa mujibu wa sheria? Maana yake nini?
Bwana Jela: Kufanya kwa mujibu wa sheria tu. Kama mchungaji anaingia kwa mambo ya kiroho peke yake.
Wisdom: Uliulizwa umeleta kiapo kinzani kujibu majibu ya mjibu maombi wa nne. Ukasema hujaleta? Kwanini.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikuleta kwasababu yeye ni mjibu maombi kama mimi.
Wisdom: Ulisema mawakili wote lazima wakaguliwe maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): kufuata sheria tu. Kuandika comment au kutoandika kunazuia sheria.
Wisdom: hebu eleza huwa mnakaguaje nyaraka?
Ntamamiro (Bwana Jela : mfano kitabu tunakagua kuangalia kuna kitu chochote hatari ndani yake.
Wisdom: Nimemaliza.
Anasimama Narindwa Wakili wa Serikali.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani walioleta maombi ni akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela: Kulwa Maduhu, Nashon na Kisabo.
Wakili wa Serikali Narindwa: Kwani Maduhu mlimzuia asiingie?
Ntamamiro (Bwana Jela: Hakuwepo kwenye orodha na pia hakukuwa na ombi kutoka kwa Lissu.
Wakili wa Serikali Narindwa : Nimemaliza na tumemaliza, hatuna la ziada.
Majaji wanaandika.
Jaji Rumisha Anamuuliza Seka. Mnataka kusema kuwa mnahitaji mawakili wawe na chumba chao au mnahitaji haki ya msingi ya faragha ya mawakili inalindwa?
Wakili John Seka : nafikiri tudeal na soft part of it. Haki ya msingi ni nini sio lazima chumba kiwepo.
Anasimama Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji msiwe na shaka vyumba vinaweza kuwepo.
Mimi naishi Ukonga na pale ukonga kuna vyumba havinaga kazi kabisa. Mfano viko vyumba viwili vya Mahakama ya mtandao. Huwa sio kila siku kuna kesi kama waliweza kuwa na Mahakama ya mtandao pale na vyumba vyake vipo kwanini chumba maalumu kabisa cha mawakili kisiwepo?
Jaji Rumisha: Nafikiri tutajielekeza kwenye kuhakikisha haki inalindwa sio lazima majengo.
Jaji Mruma anasemam sasa Maombi ya Msingi tulisema yatasikilizwa kwa njia ya maandishi.
Na scheduling order itakuwa kama ifuatavyo.
Submission za petitioners zitakuwa ni kabla ya Tarehe: Watajibu PO na kufile submission in chief yao. Kabla ya Tar. 24/08/2026. Rejoinder ya Petitioners kwenye majibu yao 07/09/2026.
Respondets Submission zao zitakuwa ni Tarehe: Submission P.O before 10/08/2026. Wataleta rejoinder ya PO na reply yao 07/09/2026.
Mention kabla ya uamuzi ni 16/09/2026.
Mhe. Lissu anasimama anasema na mimi mseme naleta majibu yangu lini?
Jaji Rumisha: Sasa na wewe kwenye PO ambayo wamewekewa waleta maombi unataka kujibu kama nani wakati wote ni washitakiwa au wajibu maombi?
Jaji Mruma: Amedakia, Mimi nakuelewa Lissu hata kwenye kesi za kawaida za madai defendants wanaweza kuwa na madai dhidi yao wenyewe na ikasikilizwa. Kwahiyo Lissu uko sahihi na tutakupatia haki hiyo hakuna shida.
๐๐๐๐Kwa kifupi Mruma ameingilia show. Naambiwa huyu Mzee ni miongoni mwa Ma Jaji senior sana wa Mahakama Kuu na uwezo wake ni mkubwa sana. Serikali imeshindwa kumpandisha cheo kwenda Mahakama ya Rufani kwasababu yeye huwa sio Chawa kabisa. Ni Mzee anayejielewa sana na yuko serious.
Tumekuwa tukishuhudia kesi nyingi hapa Mahakama kuu kwa mara ya kwanza tumeshuhudia Jaji ambae kwakweli anajua kazi yake.
Anasimama Wakili Ukashu anasema Mh. Jaji na mimi interested party hujatutaja kabisa? Tunafile lini?
Anasimama Narindwa anasema hata sisi tunashangaa huyu Ukashu na TLS wanataka kujibu PO wao ni akina nani?
Jaji Mruma: Sasa sikilizeni msichanganyikiwe. Sisi wengine tumekaa humu miaka 30. Mimi nimefanya hizi kazi mwaka wa 30 huu. Hakuna jipya. Wewe Ukashu utatumia tarehe za 4th Respondent kujibu. Msichanganyane kabisa.
Naahirisha kesi kwa tarehe nilizosema.
NB. Nakuomba usisahau kuchangia #ToneTone ili kufanikisha BARAZA KUU.
M-Pesa
Namba: 0744446969
Jina: CHADEMA HQ
NMB Bank
Namba ya Akaunti: 22606600140
Jina la Akaunti: Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 26
Tumerejea baada ya Mapumnziko ya nusu saa.
Anaanza Wakili wa waleta maombi Adv. Emmanuel Ukashu kumuhoji Maswali Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Ukashu: shahidi umewahi kuisikia TLS?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio naifahamu.
Adv. Ukashu: Ili mtu aingie Gerezani inahitajika wewe ndio umruhusu aingie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Ukashu: Ni sahihi ukipewa maelekezo yoyote lazima utekeleze na Kamishna General?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi
Adv. Ukashu: Maelekezo kutoka juu maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni maagizo ya kiutendaji unayopaswa kutekeleza.
Adv. Ukashu: Usipoyatekeleza unaweza kufukuzwa kazi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kwa mujibu wa sheria.
Adv. Ukashu: Unaweza kumbishia Boss wako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Siwezi kufanya hivyo.
Adv. Ukashu: Soma SUPP 4 tar. 12/03/2026 entry no. 8 hebu isome hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela): Huruma Tehejas mfungwa aliyekuja kumtembelea ni mfungwa na shida ya kisheria. Maoni hapakujazwa. Na sahihi hamna.
Adv. Ukashu: Sasa alienda wapi huyu Wakili kama hakuna uliposaini na maoni hukuweka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nilisahau kujaza na naamini hakukataliwa pia.
Watu wanacheka. ๐๐๐๐
Adv. Ukashu: Kwanini usifukuzwe kazi kwa uzembe wa aina hii? Maana haijulikani alikuja kufanya nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nifukuzwe tu kazi kama unaweza kunifukuza. Fanya hivyo ila mimi nimesema nilijisahau.
Adv. Ukashu: Unafahamu kazi ya uwakili ina maadili yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila kazi ina maadili.
Adv. Ukashu: Maadili ya magereza tumeshayaona hapa hujajaza nyaraka na hujui wakili alipoingia alielekea wapi? Sasa tuzungumze maadili ya mawakili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : siyajui mi sio wakili.
Adv. Ukashu: Unaijua Mandela Principle?
Ntamamiro (Bwana Jela): yes
Adv. Ukashu: soma hapa inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Mfungwa atazungumza na wakili wake kuwa atazungumza bila kikwazo.
Adv. Ukashu: Umeitekeleza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inasema nizingatie sheria za ndani pia?
Adv. Ukashu: Sasa tuambie ni kifungu gani cha sheria ya ndani ambacho kiko kinyume na Mandela Principle.
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakipo.
Adv. Ukashu: Nimemaliza. Naomba Wakili Neema aendelee.
Anasimama Wakili Neema Saruni.
Adv. Neema Saruni: Nitakuwa sahihi nikisema mtu anayekuja kumuona mfungwa anapaswa kuwa na sababu ya msingi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi kwa mujibu wa Sheria.
Adv. Neema Saruni : Ulisema mjibu maombi wa nne alikuwa na orodha yake hivyo basi alipotokea hayupo mlimrudisha?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio tulifanya hivyo.
Adv. Neema Saruni : Nitakuwa sahihi nikisema hamkumpatia haki yake ya kusikiliza.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sahihi.
Adv. Neema Saruni: Nilipokuja mimi kumuona Lissu nilikuwa kwenye orodha yake?
Ntamamiro (Bwana Jela): Haukuwepo.
Adv. Neema Saruni : Nilipofika ikawaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): tulienda kumuuliza lissu.
Adv. Neema Saruni : akasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Akaruhusu ukamuone.
Adv. Neema Saruni: Kwanini huyo mwingine mlimrudisha bila kwenda kuuliza Lissu anasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hapo sasa ndio kuna utata.
Watu wanacheka ๐๐๐
Adv. Neema Saruni: Nimemaliza.
Haya wanasimama mawakili wa Serikali, anaanza Wakili wa Serikali anaitwa Wisdom
Wakili wa Serikali Wisdom: Ulitekeleza majukumu yako kwa mujibu wa nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): masharti yapo kwenye sheria ikiwemo PSO.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba asitaje kabisa PSO maana jana haikuwepo na hatukumuuliza. Asiulize. Sect. 156(3) ya Evidence Act iko wazi kuhusu Re- examination.
Jaji: Sasa Wakili wa Serikali Wisdom uko tayari kuendelea na njia hiyo ili tumruhusu Lissu nae aanze kuuliza kwenye PSO.
Wakili wa Serikali Wisdom: Naomba tu niishie hapo. Sitaendelea mbele.
Watu wanacheka ๐๐๐๐
Part 27 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 25
Wakili wa Waleta maombi Edson Kilatu anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Kilatu: Ni sahihi ili tujue maduhu ni muongo anasema alifika Ukonga lakini hakufika kumbe ulipaswa kuleta kitabu cha watu wanaohudhuria ukonga wakifika pale getini wanaandika.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Kilatu: Umeleta?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijaleta.
Adv. Kilatu: unakumbuka kuhusu huwa hamsomi nyaraka anazopelekewa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Adv. Kilatu: umeleta kiapo chochote cha unaowatuma kusimamia kuwa wanasema hatujawahi kusoma nyaraka za Lissu tukitekeleza majukumu yetu.
Ntamamiro (Bwana Jela): nimeleta mimi kwa niaba yao.
Adv. Kilatu: Lissu alipeleka orodha ya mawakili wa kumtembelea?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Kuruhusu watu kumuona sio lazima wawepo kwenye orodha?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio kuna mazingira alikuwa anaomba Lissu mwenyewe.
Adv. Kilatu: Umeyasema mazingira hayo kwenye kiapo chako au kuna siku Lissu aliomba mtu ambae hayupo kwenye orodha ili amuapishe aingie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijasema kwa kiapo changu.
Adv. Kilatu: unajua maana ya retainership ya mawakili kwa mteja uliyoisema kwenye kiapo chako.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui ila uliza swali tu.
Adv. Kilatu: Basi tutarudi hapo kama hujui.
Soma paragraph nyingine hapo umesema shauri hili lilipaswa kuwa judicial review sio la kikatiba?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi.
Adv. Kilatu: Una uelewa wowote kuhusu Judicial Review?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina uelewa wa hili.
Adv. Kilatu: Basi sitakuuliza kwenye hilo nikuache.
Sasa nenda kwenye originating summons soma ibara za Katiba zilizotajwa humo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : zipo ibara ya 13 na zingine.
Adv. Kilatu: Asome ibara ya 30 aielewe halafu nimuulize swali.
Jaji: Asome au ajisomee?
Adv. Kilatu: Ajisomeee mwenyewe aelewe halafu nimuulize swali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tayari
Adv. Kilatu: Je ibara hiyo inasema mtu anaweza kuja kwa judicial review mahakamani kupitia ibara hiyo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hapana.
Adv. Kilatu: Soma para 4 ya kiapo chako kuwa ulimkataaa Kisabo kwasababu sio wakili wa Lissu?
Ntamamiro (Bwana Jela): lakini baadae lissu alileta ombi maalamu.
Adv. Kilatu: Sasa muambie Jaji hiyo paragraph nyingine uliyosema kulikuwa na ombi maalumu ni paragraph ya ngapi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haipo.
Adv. Kilatu: Sasa ili wakili aingie gerezani ni lazima kuwepo na orodha ya mawakili iliyoandikwa na mfungwa.
Ntamamiro (Bwana Jela): Utaratibu ni kukagua kitambulisho na kumruhusu.
Adv. Kilatu: Sasa kwenye kiapo chako ukimjibu Maduhu unasema kulikuwa hakuna proof of retainership? Hiyo ndio requirement ya sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nafikiri sifahamu.
Adv. Kilatu. Nimemaliza. Mh. Jaji.
Jaji twende mapumnziko kwa nusu saa.
Tukutane hapa baada ya dakika 30.
Naomba Repost yako.