@miss___yanga@HecheJohn Wewe wewe wanajeshi huwajui naona ndo maana unajiongelesha hivi, halijua hawafiki popote ndo maana waliwaacha waingie ili wawafanyie huo ushenzi wao
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 13, 2026
Jana tuliishia part 236 so leo tunaendelea na -;
Part 237
Hatimaye, mida hii ya saa. 11:07 Asubuhi, Mahakama inaanza.
Wanaingia Mawakili wa Serikali,
Anaingia Mhe. Lissu na kundi la askari magereza, leo akiwa na vibe la kutosha kama kawaida yake anasalmia ile salama yake (Peopleβs power πͺ) anazungusha mkono, anawasalimia waliopo kule juu kwenye kighorofa then anamalizia kwa waliokaa hapa chini.
Inapigwa High Cooooooourt ya kikakamavu watu wote tunasimama.
Wanaingia Majaji wapo watatu kama kawaida yao then wanaketi kwenye viti vyao.
Karani anasoma case No.β- Jamhuri vs Tundu Lissu
Anasimama Wakili wa serikali anatambulisha jopo la mawakili wa Serikali kisha kawambia Majaji mtuhumiwa yupo.
Wakili wa Serikali anaomba radhi kwa kuchelewa anasema sababu ni kwamba walikuwa wanatafuta Shahidi na kwamba shahidi alipata changamoto za usafiri, hivyo wako tayari kuendelea.
Jaji Ndunguru anamuuliza Mshtakiwa yani Mhe. Lissu kama yupo tayari kuendelea na kesi.
Mhe Lissu anasema mimi niko tayari kuendelea lakini huu utaratibu wa kuchelewa naomba msiuruhusu, hii ni case ya Uhaini na ndo kosa kubwa lililotamkwa mpaka kwenye Katiba ya Nchi yetu, siyo kosa la wizi wa mbuzi.
Kesi inamshtakiwa mmoja lakini mpaka sasa ina mwaka mmoja na zaidi naomba Mahakama iwe inafuata amri zake.
Wakili wa Serikali leo tuna shahidi mmoja anaitwa P huyu ni Shahidi asiyejulikana (Shahidi wa kificho)
Shahidi wa kificho anaingizwa kwenye kizimbani lile banda kama la kuku niliwahi kupost hapa.
Jaji: Shahidi tutakuuliza na utatujibu unaumri gani, dini yako?
Shahidi wa Kificho (P) : Miaka 26, dini yangu ni Muislam
Shahidi wa kificho (P) anapewa msaafu na kuapa
Wakili wa Serikali Thawabu Issa anamuongoza shahidi wa kificho (P)
Wakili wa Serikali: P unajishughulisha na nini?
Shahidi wa Kificho (P) : Mwandishi wa habari Jambo Tv, nimekuwepo kuanzia 2023 mpaka sasa, majukumu yangu ni kuchukua matukio ya video na picha.
Wakili wa serikali: Ujuzi wako kwenye hiyo kazi?
Shahidi wa kificho P : Eeeeeeh Ujuzi wangu eeeeh
Shahidi wa kificho (P) anaweweseka, ni kama hajaelewa swali.
Wakili wa serikali: Shahidi elimu yako?
Shahidi wa kificho P : Elimu yangu ni Diploma ya uandishi wa habari, niliipata Chuo cha Habari DSJ mwaka 2023.
Wakili wa serikali: Kwa namna gani unafanya hizo shughuri??
Shahidi wa kificho P : Nafanya kwa kutumia vifaa ambavyo ni camera aina ya Sony NX
Wakili wa serikali: Umesema matukio ya picha na video., hiyo unatumia kwenye matukio gani?
Shahidi wa kificho P : Kwa video pekee, kwa matukio ya picha natumia Canon.
Wakili wa Serikali: Shahidi unakumbuka tarehe 3/4/2025 ulipata jukumu gani?
Shahidi wa kificho P : Siku hiyo nilipewa jukumu na boss wangu kwenda kucover Mkutano wa Chadema kule Mikocheni nikiwa na mwenzangu P1, Boss wangu ni John Marwa.
Wakili wa serikali: Mkutano ulikuwa wapi?
Shahidi wa kificho P : Makao makuu Chadema
Wakili wa serikali: Tuendelee hapo...
Shahidi wa kificho P : Tulipack vifaa na kujiandaa na tukio husika, ilikuwa mishale ya saa 4 asubuhi.
Wakili wa serikali: hali ilikuwaje mlipofika?
Shahidi wa kificho P : Tulikuta kuna wanachama wa Chadema lakini pia Waandishi wa habari wa channel zingine kabla ya viongozi wa Chadema kufika.
Wakili wa serikali: Kwa siku hiyo ulijiandaa kwa matukio ya aina gani?
Shahidi wa kificho P : Ilikuwa kwa ajili ya kuchukua matukio na kwenda mubashara.
Mawakili wa serikali wananong'onezana...., hapa ni kama shahidi hakuelewa swali.π
Wakili wa serikali: Mlikuwa mnarusha kwa njia gani?
Shahidi wa kificho P : Tulikuwa tunarusha kutoka kwenye matukio ya picha na kuyarusha YouTube.
Wakili wa Serikali: Majina mnayotambulika nayo kurusha mubashara???
Shahidi wa kificho P : kimyaa kidogo.....kisha anajibu; Jambo TV.
Part 238 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 235
Bado kimya kimetawala mpaka muda huu.
Wakisubiriwa upande wa Serikali waanze kumhoji Shahidi wao (Re-examination) kwa ajili ya kufukia mashimo yaliyotengenezwa na utetezi na kurepair.
Majaji wanatoa maelekez, tuendelee kwa Re- examination.
Wakili wa Serikali Anasimama anasema tunayo maswal machache
Atauliza Katuga.
Katuga Anasimama anamwambia Shahidi pole kwa maswali mengiiii yaliyojaa hotuba, Relax
Katuga : Usitegemee kukuta maswali ya sijui Tume, Sijui nini sawa? Anarudia sawa mara kadhaa..
Katuga : Kama unakumbuka uliulizwa maneno kwamba tutazuia uchaguzi, tutakinukisha hayo maneno yana neno Serikali, ulijibu lipo, Ulimaanisha nini?
ACP Amin Mahamba : Nilipotamka neno Serikali lipo nilikuwa naamanisha kwamba Serikali ndo yenye mamlaka au wajibu wa kutekeleza au kusimamia Sheria za nchi, kwahiyo kutamka maneno kama hayo.. kwamba utavuruga uchaguzi, utazuia maana yake ni kuitishia Serikali ambayo ndo ina jumumu la kulinda na kutunza usalama wa nchi nlikuwa namaanisha hivyo.
Katuga: -Tuendelee kijikita hapa hapa kwenye maswala yaliyopo mbele ya Mahakama.
Uliulizwa ni nani aliyechapisha maneno hayo, ukajibu ni wewe, tena ukamkomali, ukapelekwa kwenye ushahidi wa P ukieleza kwamba wao ndo waliosambaza P na P1, ukasomeshwa kwamba bwana Bagyemu aliona hayo maneno kwenye YouTube
lakini ukazidi kusema ni wewe(Lissu) ndo uliyechapisha.?
ACP Amin Mahamba : Nilikuwa naamanisha kwamba mshtakiwa ndo alikuwa kaiongea mbele yao wale wote waandhsi wa habari.. yeye ndiye aliongea mbele ya wale waandshi wa habar ambao walikuwa wakirusha yale live so yeye ndiye aliyesababisha warushe ye live. Na kwamba naamini kama ile ilikuwa nia yake sababu kama alikuwa hataki yale matangazo yarushwe mubashara asingeruhusu yarushwe sababu aliruhusu yarushwe.
Katuga: kwahiyo ndo maana ukakomaa ni wewe ni wewe ???
ACP Amin Mahamba : Ndio
Katuga: Ulisomeshwa kifungu cha 39 japo wewe si Mwanasheria, ukaulizwa haya maneno kuzuia uchaguzi, kukinukisha.. yamo kwenye hicho kifungu?
Na majibu yako uliendelea kusisitiza yamooo
ACP Amin Mahamba ;Nilikuwa namanisha kuwa katika kile kifungu cha 39(2)b kuna neno limeandikwa kwa nia ya kutishia serikali, Kwahiyo yale maneno alimaanisha ile nia.
Katuga: Shahidi kingine umeulizwa sana⦠sijui mwaka fulan, madai ya Katiba, ccm sijui nn, mimi sio mwanasiasa
Ifafanulie haya madai ya Katiba na madai haya ya uhaini nini majibu yako kwenye hii Katiba na kesi ya uhaini???
ACP Amin Mahamba : Napenda kusema kwamba, kama una madai ya msingiβ¦.
Shahidi anakatishwa na wakili wa serikali Katuga hivyo vitakiwa vitu vipya
ACP Amin Mahamba; hayahusiani na haya
Katuga: Sasa shahidi kuna maswali mengi lakini swal moja wapo linahusiana na vurugu za 29/2025.
Uliulizwa kwamba wewe na timu yako ya polisi mlifanya vurugu siku hiyo, ulijibu ukazuiwa na ulikuwa unaamanisha nini???
ACP Amin Mahamba : Sio kweli kuwa mimi na timu yangu au na Jeshi la Polisi tulihusika na zile vurugu kwan upelelezi tuliofanya tulibaini kuwa zilitokana na uhammishishaji au uchochezi uliofanywa awali na kubaini kwamba kulikuwepo na maandalizi ya vurugu hizo kabla ya 29/10/2025.
Mhezz Lissu anainuka anasema Waheshimiwa majaji mimi sikuuliza hilo swali, Shaidi anajibu kitu kipya⦠akiruhusiwa nitaomba nami ni mcross examine
Jaji: tuendelee
Mhe. Lissu anasimama na kusisitiza kuwa akiruhusiwa nitaomba niruhusiwe
Jaji: tuendelee
Mhe. Lissu: kama mmesema hivyo tuendelee
Katuga; Uliulizwa je unataka maelezo uliyotoa polisi uaminiwe, ukajibu ndiyo ya hapa Mahakamani, ukajibu pia ndio.
Hebu tupe ufafanuzi kuhusiana na utofauti, uliotoa polisi na uliotoa mahakaman?
Mhezz Lissu anainuka tena na kusema hicho kitu sicho nilichouliza.
Lissu anasema niliuliza kama ameeleza kuwepo kwa tofauti, Akieleza sababu nitataka ku pewa nafasi ku cross
Katuga anaelezea hapa
Na Mhe. Lissu anaeleza piaβ¦
Part 236 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 234
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba
Mhe. Lissu: Kama unafahamu au hufahamu Tume iliundwa pia ya Mark Boman.. kuangalia utaratubu wa Katiba nayo ikapendekeza kuwe na Katiba mpya na Serikali ya Mkapa na ccm yake ikakataa????
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu: Kama hufahamu au unafahamu Kikwete aliunda Tume ya Mabadilio ya Katiba (ya Warioba) ambayo sio tu ilipendekeza Katiba mpya bali pia iliandaa Rasimu halafu Serikali ikakataa???
ACP Amin Mahamba; Sijawah kupitia
Mhe. Lissu: Eleza kama unafahamu au hufahamu tunafanya Uchaguzi Mkuu kila baada ya mikaa 5???
ACP Amin Mahamba : sahihi
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu katika kila Uchaguzi mkuu wa vyamana vingi Watazamaji wa Kimataifa na Kikanda, Jumuiya ya Ulaya, COMMON WEALTH, Marekani., Canada, Japan, AU, SADC, Jumuiya ya Afrika kila Uchaguzi Mkuu wamependekeza kuwa Serikali itungwe Katiba mpya na mfumo mpya wa Uchaguzi ili kuondoa matatizo mengi ya kiuchaguzi???
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu Tumeambiwa kila baada ya miaka 5 na ccm imekataa, Eleza kama unafahamu ilani ya ccm ilikuwa na ahadi ya Katiba mara baada ya uchaguzi 2015 na 2020.
ACP Amin Mahamba anajibu haraka SIFAHAMU hata kabla swali halijaisha.
Watu Wanacheka ππππ
Mhe. Lissu : Samia alisema Katiba haiweki ugali mezani, unafahamu?
ACP Amin Mahamba ; Sifahamu
Mhe. Lissu: Kwasababu ya kukataa huku kila Uchaguzi mkuu lazima uendane ma maujaji ya Watanzania???
ACP Amin Mahamba -Sina uhakika na hilo
Mhe. Lissu: Eleza Kama baada ya maujaji ya Oktoba 29 mlichukua hatua ya kuniuliza haya maneno yana maana gani, unaposema mtakinukisha una maana gani au haya maneno ya uasi yana maana gani?
ACP Amin Mahamba : Hapana
Mhe. Lissu; Hamkutafuta ufafanuzi wa hayo maneno yangu?
ACP Amin Mahamba : Hukuwa tayari
Mhe. Lissu: Ningekuwa mjinga kiasi gani kujibu nikiwa kwenye pingu?
Mhe. Lissu: Nitakuwa sahihi kusema kuwa No reforms, No election ilikuwa sahihi kwa mazingira yale???
ACP Amin Mahamba : sio sahihi
Mhe. Lissu: Kwa mujibu wa tume ya jaji Chande Ghasia za oktoba 2025 zimetokana na changamoto mbalimbali ambazo hazikutatuliwa, anazisoma kama madai ya katiba mpya.
Waeleze majaji kwamba huo ni msimamo sahihi?
ACP Amin Mahamba ;Unakosea
Mhe. Lissu: kwahiyo hata Jaji Chande alikosea?
Lissu anamsomea sababu kama zilivyo kwenye hotuba ya Jaji Chande.
ACP Amin Mahamba: Sikupata nafasi ya kupitia
Mhe. Lissu: Hayo mnayodai ni makosa yangu, waeleza Majaji kama unafahamu au hufahamu kuwa 13/2/2026, Kikosi kazi cha Kamati ya Umoja wa Mataifa, Kikosi kazi cha Haki za Binadamu, kinachoshughulikia watu wanaokamatwa bure arbitrary detention) kimetoa taarifa na taarifa hiyo inasema kukamatwa kwangu na kushtakiwa huku ni kukuka haki za binadamu na wakapendekeza nilipwe fidia???
ACP Amin Mahamba : sijawah kufahamu
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama unafahamu au hufahamu mwezi ulipoita 10 july, kamati ya Mawaziri wanaowakilisha nchi za Jumuiya ya Madola imetoa taarifa inayoitaka Serikali ya Tanzania kuniachilia huru bila mashart yoyote ndan ya siku 30 kuanzia 10 july na wakaeleza watatake appropriate action isipofanyika hilo�??
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mhe. Lissu: Kama Umoja wa Mataifa, Jumuiya ya Madola, Mawaziri kabisa sio wale WANAHARAKATI msiowapenda wanasema aachiliwe ndani ya siku 30 vinginevyo tutawashughulikia, huyu mtu anayepiganiwa na Taasisi hizi ni mtu mbaya anayetakiwa kunyongwa hadi afe?
ACP Amin Mahamba ;Sina uhakika
Mhe. Lissu anamaliza maswali na kukaa chini
Kimya kinaendelea mahakamani kwa muda kidogo
Part 235 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 233
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Eleza kama hao waliosema watafanya vurugu, mkawaachia na wakaenda kweli kufanya vurugu kama kuna hata mmoja mliemchukulia hatua?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu : Kimya maana yake hamkuchukua hatua
ACP Amin Mahamba ; Hapana, nimeona unakumywa maji
Mhe. Lissu : Ninakunywa kahawa
Mhe. Lissu : Mkoa wa Mwanza 29/10 kwa mujibu wa ripori ya jaji chande waliuawa watu 90, eleza kama Mwanza ina RPC?
ACP Amin Mahamba : Yupo
Mhe. Lissu : Yule ambaye yupo kwenye vyombo vya habari kila siku hata gerezani namsikia? Anaitwa Mutafungwa
ACP Amin Mahamba : ndio
Mhe. Lissu : Kwa Mikoa minne watu 405 kwa mujibu wa taarifa ya Chande, kuna aliyechukuliwa hatua?
ACP Amin Mahamba: Sina taarifa
Mhe. Lissu : Kwa Mikoa 7, ni Songea tu mlipopewa taarifa kuwa watafanya vurugu?
ACP Amin Mahamba : Ndio lakini waliachiwa kwa mujibu wa taratibu ya sheria
Mhe. Lissu : Waeleze Majaji kama Wakuu wote wa vyombo vya ulinzi na usalama ambao hawakuripoti wamechukuliwa hatua kwa maafa yalitokea???
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika
Mhe. Lissu : Mara ya mwisho watu waliuawa na vyombo kiasi kikubwa hivyo ni mwaka 1905 kwenye Vita ya Majimaji.
Mhe. Lissu anaendelea kueleza awamu zote watu hawakuuawa kiasi iko kama ndani ya wiki 1 ya Samia wameuawa watu wengi
Mhe. Lissu anaelekea kwenye Ushahidi wa video, kwenye ushahidi wako kuhusiana na video, ulisema wewe na timu yako baada ya wewe kupanga timu zako 3, Je video mliyoangalia ilikuwa mtandaoni au ilikuwa kwenye memory card? Au ile iliyokuwa kwenye flash.??
ACP Amin Mahamba; Tuliangalia ile ya kwenye mtandao, Youtube
Mhe. Lissu; Nitakuwa sahihi kusema hamkuangalia ile video ya kwenye flash wala ya kwenye mamory card??
ACP Amin Mahamba ; Hizo hatukuangalia
Mhe. Lissu: Nitakuwa sahihi kusema pengine flash na memory card huenda hazina hata hizo video?
ACP Amin Mahamba ; sio kweli
Mhe. Lissu: umejuaje wakati hujaangalia?
Waeleze Majaji unajuaje kilichokuwa kwenye flash disk wakati hukua.???
ACP Amin Mahamba anakwepa
Mhe. Lissu anarudia
Shahidi umejuaje?
ACP Amin Mahamba: Wenzangu KAAYA na mwenzie walipakua hizo video na kuziweka kwenye flash.
Mhe. Lissu anarudia, swali langu wewe unajuaje kama zipo wakati hujaziona?
ACP Amin Mahamba: najibu kitaalamu sasa,
Mhe. Lissu anamkatiza jibu swal langu
ACP Amin Mahamba : Ngoja nijibu basi, nimefahamu kupitia taarifa ya mchunguzi
Mhe: Lissu: Hiyo taarifa ipo Mahakamani kama kielelezo???
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu anasema mimi nachojua taarifa ilikataliwa hapa mahakamani sababu haikuandaliwa na mtaalamu
Mhe. Lissu: Mpaka sasa wewe ni Shahidi wa 16, na nyie wote hakuna hata mmoja aliyewasilisha ushahidi wa video, taarifa ya uchunguzi wala nyaraka yoyote hakuna.
Mhe. Lissu: Nyaraka zote zilizoingia Mahakamani ni ushahidi wangu,
Mpaka sasa hakuna kilelezeo chochote zaidi ya story kwenye kesi hii.
ACP Amin Mahamba : sina kumbukumbu
Mhe. Lissu: Mkutano wangu ulizungumzia Katiba Mpya?
ACP Amin Mahamba anakataa
Mhe.Lissu : Waeleze Majaji kama unafahamu madai ya Katiba Mpya na mfumo huru wa uchaguzi ni madai yaliyopo kwa miaka 35 hapa Tanzania.
ACP Amin Mahamba : sifahamu
Mhe. Lissu; Eleza kama unafahamu au hufahamu kuwa Tume ya Jaji Nyalali, ilipendekeza itungwe Katiba mpya itakapofikia 1993?
ACP Amin Mahamba : Sijawah kuipitia
Mhe. Lissu: Eleza kama mapendekezo hayo yalikataliwa na Mwinyi?
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Mheβs Lissu: Mkapa aliunda tume iliyoongozwa na Jaji Kisanga na ikapendekeza kuwe na Katiba mpya halafu Mkapa akasema hadharan mimi sikuwatuma waangalie maswala ya Katiba mpya, unafahamu au hufahamu???
ACP Amin Mahamba : Sifahamu
Part 234 itaendelea kwenye post inayofuata
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 12, 2026
Kesi ya uhaini dhidi ya Mhe. Lissu inaendelea katika Mahakama Kuu ya Dar es salaam ambapo Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross Examination Shahidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Jana tuliishia part 231 so leo tunaendelea na
Part 232.
Imepigwa high court.
Majaji wameingia wapo watatu kama kawaida yao.
Mtuhumiwa nae ameingia japo leo Askari Magereza wamemzonga sana ili asisalimiane na watu.
Mtuhumiwa yani Mhe. Lissu amechukua nafasi yake, na shahidi Amini Mahamba amekaa katika kizimba tayari.
Karani anaita kesi kwa namba yake : JAMUHURI dhidi ya TUNDU LISSU
Mawakili wa serikali wanaongozwa na AJUAYE, Katuga, Job Mrema , Cuthbert Mbilingi na Winniwa Kasalla.
Majaji wanamuuliza mtuhumiwa kama yupo tayariβ¦
Mhe. Lissu anaomba kufanya consultation toka kwa Mawakili wake/researchers
Majaji wanamruhusu
Mawakili wake Nashon Nkungu Na Sisty Aloyce wanainuka na kusogea kizimbani kumconsult Mhe. Tundu Lissu wanateka Kama dakika tano hivi kisha wanarudi kukaa kwenye viti vyao.
Jaji anamkumbusha Shahidi kuwa bado yupo chin ya kiapo.
Mhe. Lissu anaruhusiwa aanze kumuhoji Shahidi.
Anamwambia leo hana maswali mengi sana
Anamuuliza kama alidhamiria kuwa maelezo yake aliyotoa alidhamiria yaaminiwe kama ushahidi wa kweli.
ACP Amin Mahamba anajibu kwamba ndio alidhamiria
Mhe. Lissu : Ulidhamiria kuwa maelezo yako uliyotoa kule Polisi yawe ushahidi Mahakamani?
Lissu anasema βIM TYING UP THE LOOSE ENDSβ
Anamuuliza kuhusu wale mashahidi waliofichwa waliotolewa mikoani.
Mhe. Lissu : Swala la kwanza eneno hilo; unakumbuka ulisema kwamba hawa mashahidi waliofichwa ni watu waliokamatwa na Polisi ni KWELI walikutwa wakipanga njama?
ACP Amin Mahamba : sio tu kupanga niama, na kuhamasisha
Mhe. Lissu: Walipokamatwa walikiri Polisi kupanga kufanya njama na vurugu Uchaguzi na kadhalika ni kweli??
ACP Amin Mahamba : Hayo yalikuwa ni makosa ya jinai.
Mhe. Lissu: Wakakiri kwa maandshi?
ACP Amin Mahamba : Sahihi.
Mhe. Lissu: Waleleze Majaji hizo tuhuma za kijinai mlizowakamatia ziliishia wapi?
ACP Amin Mahamba : Waheshimiwa rejea maelezo yangu ya siku ya kwanza, kuwa baaada ya watu hao kukamatwa tuliitisha jalada, tukasoma tukapitia.
Mhe. Lissu: Umeelewa swali langu shahidi?
Nimesema sitaki unipotezee muda, nataka kutumia nusu saa.
Katuga anainuka
Kabla hajasema chochote Mhe. Lissu anamwambia kaa,
Katuga anasema si jukumu la Mhe. Lissu kumwambia akae chini.
Mhe. Lissu anakubali na kumueleza Shahidi kuwa akiuliza swal anataka jibu sio hotuba
Mhe. Lissu anauliza kuwa hizo tuhuma za kupanga njama ziliishia wapi?
ACP Amin Mahamba : Baada ya kupitia majaladaβ¦
Mhe. Lissu: kweli kuwa mliwafutia kesi wote?
ACP Amin Mahamba : sahihi
Mhe. Lissu : Tuanze na DSM⦠29/10.. kulitokea vurugu zilizoua watu 182
ACP Amin Mahamba: Mimi sio msemaji wa Jeshi la Polisi, hizo ni taarifa nyeti.
Kwa mujibu wa Tume ya Jaji Chande watu 182 waliuwawa DSM.
ACP Amin Mahamba : si kweli
Mhe. Lissu: Katika wale watu waliokamatwa wapo wa kutoka Arusha
ACP Amin Mahamba : Kweli
Mhe. Lissu: Walikiri kupanga uhalifu, kupiga watu nk na Mkawaachia,?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe.Lissu : Siku ya uchaguzi 29, kwa mujibu wa Tume ya Jaji Chande, waliuwawa watu 53 Arusha, watu ambao mlikuwa mnajua walichopanga mkawaachia, wakaenda kutekeleza hayo.?
ACP Amin Mahamba : Aaah, eeh
Mhe. Lissu : Twende Mbeya, kuna watu mlikwakamata Mbeya, walisema wanapanga kufanya vurugu kwenye Uchaguzi, watapiga watu mawe wakakiri halafu mkawafutia mashtaka kweli si kweli.
ACP Amin Mahamba : KWELI
Mhe. Lissu : Arusha, Dar es Salaam, Mbeya jumla ya watu waliouawa ni 315.
Eleze kama kuna Mkuu wa Polisi, au DC, alichukuliwa hatua kwa uzembe wa maafa haya?
ACP Amin Mahamba : Sina hakika kama kuna aliechukuliwa hatua
Part 233 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 227
Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia cross examination Shaidi wa Jamhuri ACP Amin Mahamba.
Mhe. Lissu : Waeleze Waheshimiwa Majaji kama mimi nilidessiminate hiyo video mtandaon au kama nilipublish hiyo video mtandaoni?
ACP Amin Mahamba ; Ndio ni wewe.
Mhe. Lissu; Waeleze majaji kama nimeajiriwa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika na hilo.
Mhe. Lissu : Waeleze majaji kama mimi ni mpiga picha wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : sina uhakika
Mhe. Lissu : Na wewe ndo ulikuwa mpelelezi wa kesi hii na huna uhakika na mambo na yote unayosema hapa?
Mhe. Lissu : Ni kweli hio video ya ilichukuliwa na P1 mfanyakazi wa jambo tv?
ACP Amin Mahamba ; Sio kweli.
Mhe. Lissu : Taratibu wewe Afande, Ni kweli au si kweli kwamba kwenye maelezo uliyoyasoma ulisema P1 alikuwa anarusha video mubashara kupitia camera yake ya Sonny Ericsson?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni kweli.
Mhe. Lissu : Waeleze Majaji kama ni kweli kwenye maelezo ya P1, yeye ndiye aliyehifadhi na kurusha mubashara video kwenye Mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli
Watu πππππ Shaidi kakataa kona, amekubali Penalty.
Mhe. Lissu ; Ulisoma maelezo ya George Bagyemu?
ACP Amin Mahamba : Ndio nilisoma.
Mhe. Lissu : George Bagyemu alisema kwenye maelezo yake aliyojiandikia mwenyewe kama wewe kuwa video ilirushwa na kurekodiwa na Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli
Mhe. Lissu : Mashaidi P1 na P2 walipewa maelekezo ya kucover Mkutano wangu na John Marwa?
ACP Amin Mahamba : Ndio
Mhe. Lissu : Waeleze Mahakama kwamba John marwa alipewa mualiko na
Mkurugenzi wa habari Chadema mimi ndio Mkurugenzi wa habari?
ACP Amin Mahamba : Hilo sijalifanyia kazi
Mhe. Lissu : Nimekaa mahabusu mwaka na miezi 4 kwa kosa ambalo wamemfanya Jambo tv, Waeleze Majaji kama huu ndio utendaji wa Jeshi la Polisi la Tanzania?
ACP Amin Mahamba : Waheshimiwa Majaji mshtakiwa ananipitisha kwenye maelezo ya P1 na P2
Huyu Polisi anaongea kwa dharau sana hapa
Mhe. Lissu anamkatisha anamjibu lissu majaji wanamtuliza Shahidi
Mhe. Lissu : Anarudia tena maswali yake na anaongeza kuuliza kama John mnyika alihojiwa?
ACP Amin Mahamba : Hapana
Mhe. Je Golugwa alihojiwa ili waseme?
Mhe. Lissu Je Mkurugenzi wa habari wa CHADEMA alihojiwa?
ACP Amin Mahamba ; Hao wote ni sehemu yako siwezi kuwahoji.
Mhe. Lissu: Mwenyekiti wa Chama anawajibika kijinai kwa Makosa ya kijinai ya watu wengine?
ACP Amin Mahamba : Umeshtakiwa kama lissu sio Mwenyekiti.
Afande anakimbia kujibu swali hapa π
Mhe. Lissu : Je Mwenyekiti wa Chadema anawajibikia kijinai kwa kosa ambalo umelitenda wewe au kwa makosa ya watu wengine?
ACP Amin Mahamba : Huwajibiki
Mhe. Lissu : Nawajibika au siwajibiki?
ACP Amin Mahamba : hauwajibiki
Mhe. Lissu :Turudi kwenye maneno niliozungumza, Waeleze majaji kuwa ni kweli au si kweli hotuba ilikuwa inahusu shida ya Uchaguzi Mkuu kwa mujibu wa Lissu?
ACP Amin Mahamba : Kweli
Mhe. Lissu : Maswala yaliyopo kwenye uchaguzi ni maswala yaliyoko kwenye katiba ya nchi na taratibu za nchi?
ACP Amin Mahamba : Ni kweli.
Mhe. Lissu : Kwa katiba hii mtu anaetaka uchaguzi usifanyike kwa katiba hii amefanya kosa?
ACP Amin Mahamba : hapana sio kosa.
Mhe. Lissu : Unajua sheria ya uchaguzi na kuna kosa linaloongelea kuvuruga uchaguzi?
ACP Amin Mahamba : Sina uhakika sana na sheria ya uchaguzi.
Mhe, Lissu: Mimi nina uhakika sheria ya uchaguzi haina kosa la kuvuruga uchaguzi na mmelisema kama kosa la uhaini, mimi nitasema sio kosa la jinai wewe unasemaje?
ACP Amin Mahamba : makosa na sheria ziko nyingi
Mhe. Lissu : Tutaenda huko kote apewe penal code s.39(2) d asome kama hilo kosa linasema kuzuia Uchaguzi au kuhamasisha watu kutofanya uchaguzi ni kosa?
ACP Amin Mahamba : Nikitafasiri hii sheria...
Mhe. Lissu anamwambia kutafsiri sheria ni kazi ya Wanasheria sio mapolisi.
Watu wanacheka: πππ
Part 228 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 11, 2026
Last time tuliishia Part 225 so leo tunaendelea na-;
Part 226
Jana Shahidi wa upande wa Jamhuri ACP Amin Mahamba alianza kutoa ushaidi wake na leo Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross-examination.
Mhe. Lissu : Unaweza kuiambia Mahakama kwamba ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa
Mhe. Lissu : Mke wa Amin Mahamba anasema kwamba Amin Mahamba alifariki, sasa iambie Mahakama ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Huyo Amin Mahamba anaetajwa sio mimi.
Mhe. Lissu : Kwahiyo ni ushahidi wako kuwa huyu Amini Mahamba ni mwengine sio wewe?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni mwingine tena yeye ni mstaafu na wanasema alishariki kweli kama unavosema.
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama ulimshirikisha RSO kwenye upelelezi wako?
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulimshirikisha afisa yoyote wa TISS.
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Unafahamu Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa?na kama uliishirikisha kamati ya ulinzi ya mkoa wa Dar es salaam?
ACP Amin Mahamba :Naifahamu na sikuwaashirikisha
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ikulu?ofisi ya VP au Waziri mkuu?
ACP Amin Mahamba : Sikuishirikisha na sikuwaambia lolote.
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ofisi ya DPP ndio nilishirikisha kanda maalum NPS.
Mhe. Lissu :Ulimshirikisha nani?
ACP Amin Mahamba: Incharge Mayenga
Mhe. Lissu : Umesema kokote kwenye nyaraka yako?
ACP Amin Mahamba : Sijasema na sijamtaja
Mhe. Lissu : Kwa mujibu wa sheria ya NPS mwenye jukumu la kuratibu upelelezi ni DPP na Mastate Attorney wake.
Waeleze ni DPP yupi au State Attorneys yupi?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu : Jibu swali wewe Polisi
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa swali.
Mhe. Lissu : Swali langu linahusu nani aliecordinate upelelezi?
ACP Amin Mahamba : Ni DPP Mwenyewe, aliteua mtu nilisema jana kuwa sijui jina lake alitoka ofisi ya DPP Dodoma na nilisema ana jina la kibantu nimesahau.
Mhe. Lissu : Tutaenda kwa DPP Mwakitalu atupe hilo jina tuko kwenye serious matters.
πππ inachekesha sana maana jamaa hajui jina la mpelelezi ambae alishirikiana nae kufanya upepelezi pamoja na kufungua faili la kesi hii.
Mhe. Lissu : Umesema wewe ni mpelelezi wa muda mrefu umewahi peleleza kesi ya kisiasa?
ACP Amin Mahamba : Sijawahi
Mhe. Lissu : Kesi ya uhaini ni kesi kubwa sana ni highest in the land kwahiyo hujawahi kabisa na hii ndo kesi ya kisiasa ya kwanza.??
ACP Amin Mahamba : Sijawahi hii ndio ya kwanza
MheZ Lissu : Umewahi peleleza kesi ya mtu alikuwa mbunge na kiongozi wa Chama kama lissu?
ACP Amin Mahamba :Sijawahi
Mhe. Lissu : Umesema kitengo chako kinashugulika na makosa ya mtandao
ACP Amin Mahamba : Ndio
Mhe. Lissu: Ushapeleleza kesi ya cybercrime?
ACP Amin Mahamba : Ndio nimewahi.
Mhe. Lissu : Kesi gani shahidi?
ACP Amin Mahamba ; Nakumbuka nikiwa RCO Kinondoni
Naona kasita kama dakika 5 hivi then akasema kesi ya Mbowe na Mzee wa karatu Slaa
Mhe. Lissui : Waeleze ilikuwa inahusu nini na iliishaje?
ACP Amin Mahamba ; DPP hakuwa na interest ya kuendelea na kesi ikaisha hewani.
Mhe. Lissu : Una kesi zingine zaidi ya hizi kwenye cybercrime?
ACP Amin Mahamba ;Hapana
Mhe. Lissu: kwahiyo hauna kesi nyingine zaidi ya hiyo iliyofutwa?
ACP Amin Mahamba : Ninazo nyingine nyingi siwezi kuzikumbuka nikiwa RCO na OCCID.
Mhe. Lissu : Kwahiyo jana kweye ushahidi wako unasema mimi ndie niliechapisha video yangu hapa mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndiyo nilisema.
Mhe. Lissu ; Unafahamu maana ya neno kuchapisha mtandaoni?
ACP Amin Mahamba : Ndio nafahamu lakini sheria ambayo imetumika kukushitaki sio Cybercrime.
Mhe. Lissu : Waeleze waheshimiwa majaji kama mm ndie nilisambaza video za YouTube kwenye mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni wewe ulisambaza hizo video.
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
Kiongozi mzuri ni anayejua thamani ya wananchi wake. Dkt. Suluhu Hassan anatufanya tujue kuwa Rais ni mlezi wa taifa, si mtawala. Anaongoza kwa upendo na kujali, ndiyo maana furaha yetu ni kumuona akiwa mwenye afya njema na nguvu.
π§ππ‘ππ π¨πͺπππππππ πͺπ π¦ππ ππ ππππ§ππ¦ππππππ
βπΏKiwanda cha kusafisha mafuta kufungua fursa zaidi
βπΏNi za viwanda ambatishi vya plastiki, dawa, mbolea
βπΏYanatokea mikoa ya Dar, Pwani ikiongoza kiviwanda.
Sukuma Gang jifunzeni kutokana na makosa yenu ya 2030. Rais Samia yupo mpaka 2030 hilo halikwepeki.
Ushauri wangu kwenu ni badala ya kupambana kumtoa Rais Samia pambaneni kumuandaa yule mgombea wenu wa 2030.
Maana sasa hivi hata SSH akitoka haingii mtu wenu π.
Mwisho wa siku hii picha itakuja kujirudia na wafuasi wa Lissu watalamba matapishi yao kwa lazima π.
Siku hiyo sote tunasema Samia oyeee. Lissu oyeee. Maridhiano oyeee. Kisha SSH anatupa Katiba Mpya safi kabisa.
Albin Saragu, wewe sitakujibu kwa sababu unatafita kiki kupitia kwangu .....Endelea kulelewa hapo mji wa Liverpool
Ukitaka niseme,nitasema na unajua nakufahamu vizuri tangu UDSM ........
Mimi niliijenga Chadema kwa kiwango cha kutoroka Chuo ili nikaimarishe chama, wewe ulifanya nini zaidi ya kujipendekeza kwa management ili ubakishwe chuo ?