@godbless_lema Hawa rejects wa mbogamboga wanatembea na upepo, gotta be very keen and makini while accepting them. You guys have to put them under probation before giving them positions.
Tanzania haihitaji hofu zaidi.
Inahitaji uponyaji.
Kwa sababu taifa lililojeruhiwa, mwishowe huanza kujijeruhi lenyewe.
Leo tunapaswa kusema ukweli
si kwa chuki,si kwa kisasi,bali kwa hofu ya kweli kuhusu mustakabali wa nchi yetu.
Kama Michael Jackson alivyowahi kusema:
“Tunapaswa kuponya dunia yetu iliyojeruhiwa. Machafuko, kukata tamaa, na uharibifu usio na maana tunaouona leo ni matokeo ya watu kujisikia wametengwa kutoka kwa wenzao na mazingira yao.”
Kauli hii kwa sasa
Inakuwa onyo hata kwetu sisi Watanzania, kama sehemu ya dunia
Wananchi wanapoanza kujisikia:
hawasikilizwi, wametengwa, wananyamazishwa, wanadhalilishwa,
au wanachukuliwa kama maadui kwa sababu tu wana mawazo tofauti.
umbali wa hatari huanza kujengwa kati ya wananchi na dola.
Na historia inatufundisha jambo moja la kuogopesha:
Mataifa mengi hayaanguki kwanza kwa sababu ya adui wa nje.
Huanzia kudhoofika ndani
wakati imani ya wananchi inapokufa.
Nchi haiwezi kujenga amani ya kudumu:
kama hofu inakuwa kubwa kuliko uhuru, kama utii unakuwa muhimu kuliko ukweli, kama taasisi zinaonekana kuwa za upande mmoja, au kama ukosoaji unatafsiriwa kama usaliti.
Kwa sababu jamii iliyojeruhiwa huzalisha wananchi walioumia.
Na wananchi walioumia mwishowe huzalisha:
hasira, mgawanyiko, msimamo mkali, kukata tamaa,au chuki ya kimya kimya.
Viongozi wanapaswa kuelewa:
si kila ukimya ni amani.
Wakati mwingine watu wananyamaza kwa sababu:
wamechoka,wanaogopa,au wamekata tamaa.
Na kukata tamaa ni hatari kwa taifa lolote.
Tanzania ilijengwa juu ya msingi imara ya : utu,umoja,mazungumzo,
uvumilivu,na hisia ya kuwa taifa ni la wote.
Julius Nyerere alielewa jambo kubwa sana,taifa haliishi kwa nguvu pekee (power)
linaishi pia kwa uhalali wa kimaadili.
Wananchi wakianza kuhisi kwamba:
haki inategemea upande wa kisiasa, ambao mtu yupo, taasisi si huru tena,
au demokrasia ipo kwenye maneno lakini si kwenye vitendo,
ule mkataba wa kihisia kati ya taifa na wananchi huanza kupasuka.
Kwa hiyo haya si mashambulizi.
Hili ni onyo.
Onyo kwamba:
siasa zinapokuwa za uhasama kupita kiasi,
mamlaka zinapoanza kuogopa ukosoaji,
wapinzani wanapoonekana maadui,
na wananchi wanapopoteza imani kwa mifumo ya taifa
taifa lenyewe huanza kujeruhiwa kihisia.
Na taifa lililojeruhiwa huwa taifa lisilo tulivu.
Hatuhitaji kulewa kisiasa zaidi.
Tunahitaji hekima.
Hatuhitaji viongozi wanaotaka kusifiwa tu.
Tunahitaji viongozi wenye uwezo wa kusikiliza ukweli usiofurahisha.
Kwa sababu uzalendo si ukimya.
Wakati mwingine uzalendo ni ujasiri wa kusema:
“Kuna jambo linaenda vibaya kabla hatujachelewa.”
Kama Tanzania inataka kubaki imara,
basi uponyaji lazima uwe sera ya taifa.
Uponyaji:
kati ya viongozi na wananchi,kati ya dola na upinzani,kati ya mamlaka na uwajibikaji,kati ya sheria na haki.
Kwa sababu hakuna taifa linaloweza kuishi milele kwa:
hofu, propaganda,au mgawanyiko wa kihisia.
Mwisho wa yote,
taifa huwa imara zaidi pale wananchi wake wanapoamini kwamba:
wao ni sehemu ya taifa,wanalindwa,
wanasikilizwa,na utu wao una thamani.
Mungu ailinde Tanzania isije kuwa nchi ambayo wananchi wanaogopana kuliko kuaminiana.
Na viongozi wetu wakumbuke:
historia haitawahukumu viongozi kwa barabara, madarasa , vituo vya afya walivyojenga pekee,
bali pia watahukumiwa kwa hali ya kihisia walizoliachia taifa.
Usisahau:
“Jamii iliyojeruhiwa huzaa watu waliojeruhiwa…
na watu waliojeruhiwa huongeza machafuko zaidi.”
Rev Petet simon Msigwa!
Iringa
#TajiriLaKihaya
A Russian Guy kaenda Kenya Kawakula Wanawake sio Poa…
Kitu kizuri ni kwamba wote aliowakula ni WASIMBE!
Ndio maana kila siku nawaonya kuhusu WASIMBE… wananjaaaa Kali na kizungu Uchwara 💔
Nmekuwekea VIDEO zake zote hapo chini👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽👇🏽