@ndembo255 Wanachukuliaa poa sana mambo wanaona wana watu nyuma so hata fanya kitu ikiwa bodi ligi wanajuaa kabisaa hasara kubwa wameenda kutengenezaa.
Msimu uliyopita Zamalek aligomea mechi dhidi ya Al Ahly, Mamlaka za soka nchini Misri zikampa ushindi Al Ahly wa mabao mawili na alama zake tatu kisha wakailima Zamalek alama tatu na timu ikashuka mpaka nafasi ya 12 kama sikosei, Bodi na Chama wala hakikuwaza mara mbili, ni kesi kubwa sana kwenye dunia ya soka kukacha mechi.
Leo Al Ahly nae kaleta mbwembwe zile zile za masuala ya Kanuni akagomea mchezo, akasahau kanuni ya kutokea Uwanjani na kucheza mechi ndio kanuni yenye maana zaidi kwenye soka, amejikuta anapoteza alama tatu na mabao matatu kwa Zamalek, Kanuni hii inaweza kusema hivi ila Kanuni nyingine ikawa na maelezo mengine.
Nikukumbushe tu Al Ahly aliyeadhibiwa leo ndio Klabu Tajiri zaidi Afrika, Klabu yenye Mashabiki na Wanachama wengi zaidi Afrika, ndio Klabu ya pili kwa Mataji mengi duniani baada ya Real Madrid, ila huko Misri watu hawatazami makunyanzi, ukileta maksudi, Bodi na Chama cha soka zinakufanyia bahati mbaya, Ahly inatajwa pia ina nguvu kubwa sana CAF, sio ya kufikirika ama nadharia ndio uhalisia ila wamepita nayo mapema tu.
Nawakumbusha tena Watu wangu HAKI huenda na WAJIBU, mfano Tanzania kwa mujibu wa Katiba kuandamana ni haki yako ila unapaswa kutoa taarifa kwa Polisi masaa 72 kabla, umeelewa hapo? Ni haki yako ila huja na Wajibu, Kanuni ili ikulinde hakikisha umetekeleza Wajibu, biashara za Mamlaka za soka duniani ni mpira, kutocheza mpira ni kuzitusi, hazikuachi salama.
Ni haki yako kuja kufanya mazoezi uwanja wa mechi siku moja kabla ila ni Wajibu wako kunijulisha kuwa nakuja, ili nikuandalie mazingira, huenda narekebisha mfumo wa Umeme? Huenda hali ya usalama sio shwari, huenda nimepulizia dawa za dudu zinaweka kukuathiri, yaani ni HAKI yako ila una WAJIBU wako.
Mnasemaje Watu wangu wa nchini Yemen๐
Hotuba ya Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Vilabu Afrika (ACA) na Rais wetu Eng. Hersi Said kwenye hafla ya kusaini mkataba wa ushirikiano na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
#TimuYaWananchi#DaimaMbeleNyumaMwiko
@fumbokhanJr Bodi ya ligi imejikuta haina meno , wamekuwa nyuki wa mashineni hawajui kwanini wapo apo hawawezi fanya jambo kutisha zaidi kubariki hilo tatizo .
@1960Remija Sijapoteza muda wangu kabisaa nawapa kongolee, hakuna ushabiki just facts tu wala hakuna kupyukaa kipindi kinaenda kwa hoja nimetoshekaa acha tuone ...ufa utazibwaaa.