#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 26
Tumerejea baada ya Mapumnziko ya nusu saa.
Anaanza Wakili wa waleta maombi Adv. Emmanuel Ukashu kumuhoji Maswali Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana Jela)
Adv. Ukashu: shahidi umewahi kuisikia TLS?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio naifahamu.
Adv. Ukashu: Ili mtu aingie Gerezani inahitajika wewe ndio umruhusu aingie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Adv. Ukashu: Ni sahihi ukipewa maelekezo yoyote lazima utekeleze na Kamishna General?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi
Adv. Ukashu: Maelekezo kutoka juu maana yake nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni maagizo ya kiutendaji unayopaswa kutekeleza.
Adv. Ukashu: Usipoyatekeleza unaweza kufukuzwa kazi?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kwa mujibu wa sheria.
Adv. Ukashu: Unaweza kumbishia Boss wako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Siwezi kufanya hivyo.
Adv. Ukashu: Soma SUPP 4 tar. 12/03/2026 entry no. 8 hebu isome hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela): Huruma Tehejas mfungwa aliyekuja kumtembelea ni mfungwa na shida ya kisheria. Maoni hapakujazwa. Na sahihi hamna.
Adv. Ukashu: Sasa alienda wapi huyu Wakili kama hakuna uliposaini na maoni hukuweka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nilisahau kujaza na naamini hakukataliwa pia.
Watu wanacheka. ๐๐๐๐
Adv. Ukashu: Kwanini usifukuzwe kazi kwa uzembe wa aina hii? Maana haijulikani alikuja kufanya nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nifukuzwe tu kazi kama unaweza kunifukuza. Fanya hivyo ila mimi nimesema nilijisahau.
Adv. Ukashu: Unafahamu kazi ya uwakili ina maadili yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila kazi ina maadili.
Adv. Ukashu: Maadili ya magereza tumeshayaona hapa hujajaza nyaraka na hujui wakili alipoingia alielekea wapi? Sasa tuzungumze maadili ya mawakili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : siyajui mi sio wakili.
Adv. Ukashu: Unaijua Mandela Principle?
Ntamamiro (Bwana Jela): yes
Adv. Ukashu: soma hapa inasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Mfungwa atazungumza na wakili wake kuwa atazungumza bila kikwazo.
Adv. Ukashu: Umeitekeleza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Inasema nizingatie sheria za ndani pia?
Adv. Ukashu: Sasa tuambie ni kifungu gani cha sheria ya ndani ambacho kiko kinyume na Mandela Principle.
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakipo.
Adv. Ukashu: Nimemaliza. Naomba Wakili Neema aendelee.
Anasimama Wakili Neema Saruni.
Adv. Neema Saruni: Nitakuwa sahihi nikisema mtu anayekuja kumuona mfungwa anapaswa kuwa na sababu ya msingi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni sahihi kwa mujibu wa Sheria.
Adv. Neema Saruni : Ulisema mjibu maombi wa nne alikuwa na orodha yake hivyo basi alipotokea hayupo mlimrudisha?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio tulifanya hivyo.
Adv. Neema Saruni : Nitakuwa sahihi nikisema hamkumpatia haki yake ya kusikiliza.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sahihi.
Adv. Neema Saruni: Nilipokuja mimi kumuona Lissu nilikuwa kwenye orodha yake?
Ntamamiro (Bwana Jela): Haukuwepo.
Adv. Neema Saruni : Nilipofika ikawaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): tulienda kumuuliza lissu.
Adv. Neema Saruni : akasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Akaruhusu ukamuone.
Adv. Neema Saruni: Kwanini huyo mwingine mlimrudisha bila kwenda kuuliza Lissu anasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hapo sasa ndio kuna utata.
Watu wanacheka ๐๐๐
Adv. Neema Saruni: Nimemaliza.
Haya wanasimama mawakili wa Serikali, anaanza Wakili wa Serikali anaitwa Wisdom
Wakili wa Serikali Wisdom: Ulitekeleza majukumu yako kwa mujibu wa nini?
Ntamamiro (Bwana Jela): masharti yapo kwenye sheria ikiwemo PSO.
Mhe. Lissu: Waheshimiwa majaji naomba asitaje kabisa PSO maana jana haikuwepo na hatukumuuliza. Asiulize. Sect. 156(3) ya Evidence Act iko wazi kuhusu Re- examination.
Jaji: Sasa Wakili wa Serikali Wisdom uko tayari kuendelea na njia hiyo ili tumruhusu Lissu nae aanze kuuliza kwenye PSO.
Wakili wa Serikali Wisdom: Naomba tu niishie hapo. Sitaendelea mbele.
Watu wanacheka ๐๐๐๐
Part 27 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 21
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza la Ukonga Ntamamiro (Bwana jela)
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kuwa maafisa Magereza. Wanapaswa kukagua barua inayotoka ndani au kuingia ndio inapaswa kusomwa.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Soma kifungu cha 46 Cha Sheria na kanuni ya 10 na 11 ya kanuni za Magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Anahangaika haoni.
Mhe. Lissu: Sasa wambie majaji kama kanuni ya 10 na 11 inahusu barua wanazoandika na wanazoandikiwa wafungwa.
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Na wanaosoma ni wewe au maafisa wako?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe, Lissu: Ukiikataa barua unamrudishia na kumwambia sababu. Na kama ikikataliwa kwa aliyemletea pia unamrudishia na kumpa sababu. Na kama barua ni ndefu sana na huyapendi ni sahihi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kama nje ya barua kwa wafungwa au kutoka kwa wafungwa una mamlaka ya kukagua na kusoma nyaraka nyingine yoyote.
Ntamamiro (Bwana jela) : Naomba soma Section 12 ya Prison Act.
Mhe. Lissu: Kwa kanuni hizi unaruhusa ya kusoma nyaraka nyingine.
Ntamamiro (Bwana jela) : Soma kifungu cha 12 cha Sheria ya Magereza
Mhe. Lissu: Unauwezo wa kusoma nyaraka za mawakili wanaokuja nazo magereza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sipaswi kusoma.
Mhe. Lissu: Hicho kifungu cha 12 unachosema kinahusiana na upekuzi wa magari na kumkagua mtu sio nyaraka ndio maana sitaki hata kukisoma. Hakikusaidii chochote.
Mhe. Lissu: Kisabo alisema wakiwaambia muondoke ili azungumze na mimi mteja wake mnakataa. Kweli au sio kweli.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Na mimi nimesema kwenye viapo vyangu kuwa alikuja Wakili Alute Lissu. Na kusema nina ujumbe muhimu kutoka serikali nataka niongee nae Faragha. Mkamkatalia. Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana jela): Sikumbuki.
Mhe. Lissu: Umekuwa unaendeshwa na rimoti na Kamishna Mkuu na wanasiasa walioko serikalini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Kuna siku umeniita ofisini kwako kuwa kuna ujumbe wa jumuiya ya madola napaswa kupelekwa mjini? Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sina Jibu.
Mhe.Lissu: Siku hiyo aliyekuja kunichukua ni Mangara?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: sio kweli nini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Hujawahi kupelekwa.
Mhe. Lissu: Siku nyingine ulinifuata na kusema Katibu Mkuu wa Chama cha Mabunge Duniani amekuja kuniona anaitwa Martin Chungong na nikapelekwe mjini na Senior Mangara.
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Kuna siku Heche, Amani na Mnyika uliwaruhusu kutokana na kulikuwa na maelekezo kutoka juu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kabla hujaja walikuwa wanaruhusiwa na ulipokuja ukawazuia hayo mamlaka ulitoa wapi?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nimeshajibu.
Jaji: Ulijibuje
Ntamamiro (Bwana jela): Sikuwakataza.
Mhe. Lissu: Alipokuja Lema Godbless, wewe ulipokuja na kutukuta ulimfukuza?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Kama sio kweli kwanini haya yote hukuyajibu kwa nyaraka wakati mimi nimeyasema kwenye nyaraka zangu?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sina jibu.
Mhe. Lissu: Sasa kama umewazuia walalamikaji watatu, mashahidi wangu, umewazuia mawakili wangu. Unanitakia nini kwenye kesi ya uhaini inayonikabili ambayo adhabu yake ni mimi kunyongwa?
Ntamamiro (Bwana jela) : Nilishajibu.
Jaji Mruma: Umejibu nini?
Ntamamiro (Bwana jela) : Sijamzuia mtu yeyote kuja kuonana na Tundu Lissu.
Mhe. Lissu: Sina swali lingine.
Majaji wanamuuliza Wakili wa Serikali.
Anasema naomba tuahirishe tuendelee kesho.
Wakili John Seka: Naomba tuendelee bado muda tunao.
Jaji Mruma: Sasa hoja ya kuahirisha na logistics zilivyo, TLS nao kupewa nafasi wamuhoji shahidi. Sisi tunaomba kusema yafuatayo.
Leo tutaahirisha kutokana na sababu kama za jana, tunaamini leo tumefanya kazi kubwa, kesho tutasema mengine.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 20.
Mhe. Lissu anaendelea kumshona Shaidi ambae ni Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Wakati wote mawakili wakija gerezani, simamia, wapekuliwe na wamepekuliwa. Swali ni kwamba ni je wewe Bwana jela wa Ukonga unawashuku na una wasiwasi na mawakili 37 waliokuja kuona wateja Ukonga? Kumbuka kanuni inasena ili uwasearch ni lazima uwe na wasiwasi nao.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sitegemei kanuni.
Mhe. Lissu: Sasa twende kwenye sheria yenyewe kwenye Prisons Act kuwa unaweza kusearch mgeni kama hautakuwa na wasiwasi nae? Kifungu gani hicho?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa Majaji mtu yeyote anayeingia Gerezani awe mfungwa au mahabusu lazima apekuliwe.
Mhe. Lissu: Lazima apekuliwe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yuko kimya.
Mhe. Lissu: Kama kweli ni lazima. Twende kwa Mawakili wa Serikali waliokuja Ukonga kama uliamuru wapekuliwe. Twende kwa hao sasa. Wah. Majaji SUPP 4 tarehe 19/11/2025 nenda haraka tumalize hii ngoma. Na Tarahe 21/01 mwaka huu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kila anayeingia lazima akaguliwe.
Mhe. Lissu: SUPP 4 inasemaje kuhusu Tarehe 19/11 walikuja mawakili wafuatao Debora Mushi kutoka NPS, Caroline Nana kutoka NPS pia, Cleoface Leonce ambae ni investigator na alikuja Justo Dimba au Simba kutoka kwa ZCO. na mwingine kutoka DCEA. Wote hawa shida walioijia gerezani walikuja kuongea na mahabusu. Maoni yako ukasema nini? Wasomeee majaji.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Wasikilizwe kwa utaratibu.
Mhe. Lissu: Wakija mawakili wengine simamia mazungumzo yao, wapekuliwe, wapekue, Simamia kwa ukaribu. Lakini wa serikali wakija wasikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Mawakili 37 wote nipe mfano mmoja tu w wakili uliyesema asikilizwe kwa utaratibu.
Ntamamiro (Bwana Jela): Naomba Tar. 20/01 wakili hapo nimesema SIMAMIA.
Mhe.!Lissu: Ahsante sana. Sasa kwa mawakili wa serikali wapi hata mara moja umeandika SIMAMIA?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio lazima niandike.
Mhe. Lissu: Wabelgiji nilipokaa wanasema Papiere yaani Paper. Tunaenda na maandishi. Onesha maandishi acha rongorongo maneno mengi unatumalizia.
Sasa angalia majina yanayofuata. Hapo kuhusu mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela): Niliandika Waletwe.
Mhe. Lissu: Maafisa wa Madawa ya kulevya na Mawakili wao waliokuja 28/11 kazi yao ni kutukamata na kutupeleka Mahakamani ndio unaosema wasikilizwe?
Ntamamiro (Bwana Jela): Hatoi jibu.
Mhe. Lissu: Hawa watu ni watumishi wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wanalipwa mshahara wa serikali kama wewe?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio lakini.
Mhe. Lissu: Lakini utawapa mawakili wa serikali.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa mawakili wa serikali huwa wanakuja kuongea na wote?
Mhe. Lissu: tuambie ni wapi umeandika kuwa walikuja kuongea na wote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijaandika.
Mhe. Lissu: Ni sahihi kuwa kuna wakati nyaraka zinakataliwa na zinazokubaliwa lazima mseme zote. Kweli sio kweli mnafanya hivyo kwa mawakili wangu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sio kweli zinasomwa. Ila zinakaguliwa.
Mhe. Lissu: la kwamba zinakataliwa pia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Katika nyaraka ambazo zinaletwa kwangu ni pamoja na hotuba ya Chande ya matukio ya tar. 29/10?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Lissu: Shahidi Paul Kisabo amesema wiki iliyopita Tar. 14/07 alikuletea waraka unaotoka common wealth kuwa niachiliwe ndani ya siku 30 na mliposoma mkakataaa.
Bwana Jela: Sio kweli.
Part 21 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 19
Mahakama Imerejea.
Majaji wameingia.
Wakili wa Serikali amesimama kujitambulisha anaitwa Narindwa Sekimanga.
Shaidi Mkuu wa Gereza nae yuko pale kizimbani yeye muda wote amekaa tu pale kizimbani.
Hajajihangaisha kusimama labda kwa vile ni mrefu na hicho kitambi anachoka kusimama pengine.๐
Jaji Mruma: Shaidi nakukumbusha bado uko chini ya kiapo.
Mhe Lissu: Sasa turudi kwa viongozi wangu wa Chama uliowakatalia wasije kuniona kule Gerezani. Angalia majibu yangu na uangalie kiapo kinzani kuhusiana na kiapo kinzani nilichomjibu Kisabo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ametoa macho. Hafanyi lolote.
Mhe. Lissu: Mawakili wa Serikali mnafanya nini si mumsaidie shahidi wenu azione hizo nyaraka naona ananiangalia tu.
Wakili wa Serikali anaenda.
Mhe. Lissu: Hizo aya kwenye kwenye kiapo changu kinzani zinaonesha namna ulivyowazuia viongozi na wanachama ikiwemo mashahidi na mawakili watatu ambao ni Dickson Matata, Deogratias Mahinyila na Gaston Garubindi. Swali langu waeleze majaji kama umewahi kupinga haya maelezo yangu yaliyopo kwenye kiapo changu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa Majaji nimeshalijibu hilo.
Jaji: Umeelewa swali lake kweli.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina jibu.
Mhe. Lissu: Nalo ni jibu pia. Haya kwenye aya ya nne wewe umefanya kampeni ya muda mrefu ya wewe na mlalamikiwa wa pili kamishna mkuu mmehakikisha nashindwa kujitetea wala kuandaa utetezi wangu na matukio nimeyasema kwenye para H na Y. kwamba umewazuia mawakili wangu watatu ambao Ni Mahinyila, Matata na Garubindi kama umewahi kujibu hili.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli nimewazuia.
Mhe. Lissu: Je umeleta supplimentary affidavit? Au majibu yoyote kwenye jambo hilo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : anatoa macho. Anashika makaratasi na kuyaacha.
Jaji: Umeelewa swali?
Mhe. Lissu: Ulileta counter affidavit mara ya kwanza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Baadae ukaleta suplimentary affidavit?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Sasa kwenye hizo nyaraka zako mbili kuna mahali kokote ulijibu tuhuma za kuwa umewazuia mawakili wangu na viongozi wa Chama?
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijajibu.
Mhe. Lissu: Tuhuma dhidi yako na maafisa wako kusearch mawakili na nyaraka zao kisheria. Jibu swali kwamba waleta maombi wote watatu wamesema wanasearchiwa, wanakaguliwa na kusomwa hizo nyaraka.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Reg. 17(2) ya kanuni za Magereza inasemaje?
Anatafuta hiyo kanuni.
Mhe. Lissu: Ni kweli mgeni anayekuja Gerezani kutembelea mfungwa atasachiwa endapo atakuwa na wasiwasi na huyo mgeni?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Haya isome sasa
Ntamamiro (Bwana Jela) : A prison officer when has any ground suspiciously may direct to search that visitor. Anasoma kingereza kibaya sana.
Mhe. Lissu: Any ground for suspicion may search or cause to search. Kumbe ataamuru asachiwe kama atakuwa na sababu za kumshuku?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Mgeni ataambiwa aondoke akikataa kusachiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kwa mujibu wa kanuni hii ni kweli.
Mhe. Lissu: Anayemfukuza atatakiwa kuandika sababu za kumfukuza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : yuko kimya tena. Hebu rudia swali.
Mhe. Lissu anarudia swali. Si ni lazima uandike sababu za kumfukuza.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Siku mjibu maombi wa Kwanza alipokataliwa kuingia gerezani tar. 28/11 alipokataliwa kuingia gerezani iliandikwa sababu kuwa amekataa kusachiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kwa kanuni hii.
Mhe. Lissu: Tutajie kanuni hizo zingine tuzione? Kwenye kanuni kuna sababu yoyote nyingine kwa mujibu wa kanuni?
Bwana Jela: Sijaipitia kanuni yote.
Mhe. Lissu: Sasa mimi niliyepitia kanuni zote na hakuna sababu nyingine unasemaje?
Bwana Jela: Sina jibu.
Part 20 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
KITUKO KILICHOTOKEA MAHAKAMANI.
Wakati Mkuu wa Gereza yaani BWANA JELA ambae ni Andrew Shabani Ntamamilo alipohojiwa na Mhe. Tundu Lissu kuhusu Kuwazuia kabisa Mawakili kama Vile Deogratias Mahinyila, Dickson Matata lakini pia viongozi wakuu wa Chama akiwemo John Heche, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu wa Chama, John Mnyika na Amani Golugwa ambao ni mashahidi katika kesi ya Uhaini wamekataliwa kuingia Gerezani Ukonga.
Majibu ya Mkuu wa Gereza amesema yeye hajawazuia. Mhe. Lissu akasema basi watakuja kuanzia kesho. Akasema SITAWARUHUSU waingie kwasababu kesi bado iko mahakamani.
Jaji Amir Mruma ndio akaanza kumuhoji kuna amri yoyote ya Mahakama kuwa watu hawa hawapaswi kuja kumtembelea Tundu Lissu? Akasema kwa kiburi tena kuwa SITAWARUHUSU.
Jaji akavua miwani na kumuuliza unataka tufike huko. Uko serious kweli? Akiwa amekasirika sana. Maaskari Magereza walioko nyuma niliokaa nao karibu wamekimbilia nje kucheka.
Baada ya Jaji kukasirika Bwana Jela akaanza kuomba radhi kwa Jaji. Majaji wote watatu wametikisa vichwa vyao na kuonesha wanashangaa mambo haya yanawezekanaje kwenye Taifa lenye sheria na taratibu.
Kesi hii imeendelea tena kutuonesha watawala wa nchi hii wakoje. Ukisikia majibu ya Mkuu wa Gereza unajiuliza kiburi anakitoa wapi?
Ngoja tusubiri maamuzi ya Majaji mwisho wa kesi hii utakuwaje lakini naamini kila mtu anashuhudia uhalisia wa mambo ulivyo katika Taifa letu.
Tuendelee kusubiri lisaa likamilike turudi kuendelea.
Wanachama leo ni wengi mno. Mahakama imetapika. Yupo Makamu Mwenyekiti John Heche, Yupo Katibu Mkuu, Mnyika. Mama Suzan Lyimo, Mwenyekiti BAZECHA, Yupo Boniface Jacob Mwenyekiti Kanda ya Pwani, Dua Lyamzito, Katibu Mkuu BAVICHA, Pamela Massey, Katibu Mkuu Bawacha. Mzee Azaveli Lwaitama, Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Chama na wanachama wengine mbalimbali.
Tutaendelea kuwaleteeni live moja kwa moja mwenendo wa kesi hii kutokea Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar es salaam.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 18
Anaendelea Mhe. Lissu na maswali ya Dodoso.
Mhe. Lissu: Karibu ipi ambayo hawasikii?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Unaweza kuwa karibu na usisikie.
Mhe. Lissu: Kuna mawakili jumla 37 ambao umeleta nyaraka zao hapa pamoja na mawakili wangu. Sasa kwenye comment zako umekuwa ukisema simamia kwa karibi, simamia mazungumzo yao. Ni kweli kwa mawakili wote?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli lakini ni kweli naomba niseme ni kweli nimesema comment hizo kwa wote.
Mhe: Lissu: Katika Mawakili wote hao kuna mahali hata pamoja ulipoandika simamieni lakini msisikilize mazungumzo yao?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna
Mhe. Lissu: Je katika mawakili wote 37 umeandika wakiingia ofisini tokeni nje wazungumze ipo sehemu umeandika?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna nilipoandika.
Mhe. Lissu: Kuna mahali kokote umeelekeza kuwa angalieni lakini msisikilize?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna mahali hapo.
Mhe. Lissu: Waeleze Majaji kama ni kweli au sio kweli kati ya Tar. 18/04/2025 nilikuwa nazungumza kwenye kioo na mawakili wangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kilikuwepo hicho kipindi.
Mhe. Lissu: Tulikuwa tunawasiliana kupitia simu zilizopo pale?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Je upande anaokuwepo mgeni ndio uko karibu na reception na kuna kachumba ambacho ni control room ya hizo simu zote? na kwenye hiyo control room anakuwepo afisa magereza anayeuwasha na kuuzima. Ili watu wazungumze yeye ndio anaamua hapo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni kweli.
Mhe. Lissu: Huyo Wakili anapozungumza kuna askari wanakuwepo kumsikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli a
Mhe.Lissu: Je huu upande wangu nakuwa pia na askari wananisikiliza niliotoka nao lockup na wengine wananisikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Lissu: Kwenye hicho chumba kuna CCTV Camera inayorekodi kinachoendelea humo?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli
Mhe. Lissu: CCTV camera hiyo iko controlled ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela): sio kweli.
Mhe. Lissu: Je ni kweli kwamba baada ya matukio ya Oktoba 29 uliniita ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu : Ulivyoniita ukaniambia kuanzia sasa ni marufuku viongozi wa Chadema na wanachama wa Chadema kuja kukutembelea.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Na pia ulisema ni ndugu zako wa karibu tu ndio watakutembelea?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe.Lissu: Na ukasema mazungumzo yako na mawakili yatakuwa kwa mambo ya kisheria tu?
Ntamamiro (Bwana Jela): sio kweli.
Mhe. Lissu: Wakili Gaston Garubindi alikuwa anakuja kunitembelea Gerezani kabla ya Tar. 14/11/2025
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: kuanzia hiyo tarehe hajawahi kuruhusiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela): Simpangii.
Mhe. Lissu: Kuanzia niingie Gerezani Wakili Dickson Matata na Deogratias Mahinyila hujawahi kuwaruhusu waingie gerezani. Huyu Matata ni Mwenyekiti Kanda ya Magharibi na Mahinyila ni Mwneyekiti wa Vijana Taifa hawajawahi kuruhusiwa?
Ntamamiro (Bwana Jela): Siwalazimishi waje au wasije.
Mhe. Lissu: Kumbe ndio hivyo. Haya Mahinyila na Matata kesho njooni Ukonga.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kesi iko Mahakamani sitawaruhusu
Mhe. Lissu: John Heche, Amani Gorugwa, Katibu Mkuu Mnyika wakiwa kama mashahidi wangu kwenye kesi ya uhaini wamezuiwa kuingia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawawezi kuingia.
Jaji: Hilo la kwamba huwezi kuruhusu umelitoa wapi? Kuna amri yoyote ya Mahakama?
Ntamamiro (Bwana Jela): Siwezi kuwaruhusu.
Jaji Mruma: Tumefikia huko. Unaiambia Mahakama kuwa huwezi kuruhusu na hauna amri yoyote ya Mahakama? Uko serious kweli au hujaelewa ili tufanye maamuzi na sisi sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waheshimiwa majaji naomba radhi.
Jaji anamkata jicho
Mhe. Lissu: Soma hati yangu kinzani kuhusu Nashon Nkungu.
Anasimama Wakili wa serikali tunaomba Break.
Majaji wanashauriana.
Wakili John Seka anasema ni sawa tu.
Mhe. Lissu: Ni sawa.
Jaji basi tukutane mara baada ya lisaa limoja.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 17
Anaendelea Mhe. Lissu
Mhe. Lissu: Na mazungumzo ya Kisabo pia ulisema yasimamiwe kwenye ofisi ya kaimu mkuu wa gereza.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ndio
Mhe. Lissu: Na tunakubaliana wale watu wote akina Mumbii, legal officer Stima, Kopro Dani, na akina mama watatu. Je hawa watu wanakuwemo humo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Si kweli. Huwa wanatoka. Wanaacha mazungumzo yafanyike.
Jaji: Lissu umeridhika na majibu ya shahidi.
Mhe. Lissu: Ngoja nataka kukamata watu waongo.
Mhe. Lissu: Kumbe maafisa wote mle chumbani wanatoka nje, sasa soma kiapo chenu ndugu yangu. Nakusomea kwenye kiapo chako
Kiapo kinasomeka kuwa walikuwepo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kuna ambao walikuwepo na kuna ambao walitoka.
Mhe. Lissu: Waliokuwepo ni akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waliosindikiza
Mhe. Lissu: Akina nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikumbuki
Mhe. Lissu: Waleta maombi wote wamewataja majina akina Mumbii, Koplo. Dani, Akina mama watatu mle ndani, legal officer na mtu wa usalama. Wamewataja majina. Wewe unasemaje?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sikubaliani nao mimi.
Mhe. Lissu: Twende kwenye ofisi ya Recha ACP. Soma SUPP 4 Tar. 24/12 ulisema alipokuja Kisabo. Asimamiwe kwa kaimu mkuu wa gereza na kusema wayafanyie ofisini ukawataja majina ambao wanapaswa wasimamie. Waeleze majaji kuwa wakati wote Recha anakuwepo, asipokuwepo atakuwepo Mumbii, Mohamed lazima awepo au Hamisi na anakuwepo Stima na maaskari wanaonifuata muda wote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sio kweli
Mhe.Lissu: Umewahi kuhudhuria mazungumzo hayo kwa Recha?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijawahi.
Watu wanacheka. ๐๐๐๐
Mhe. Lissu: Tumewahi kufanya mazungumzo ofisi kwako mimi na mawakili wangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli.
Mhe. Lissu: Tar. 12/12 imeandikwa SUPP 6 Umeiona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sioni
Mhe. Lissu: Mawakili msaidieni mmeleta wenyewe.
Ukiiona siku hiyo niliyosema tar. 12/12 ulielekeza hivi kaimu mkuu wa gereza, Mtu wa usalama na mwanasheria wa gereza ulisema mazungumzo yawe ya kisheria zaidi. Kweli au sio kweli?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli
Mhe. Lissu: Je hawa uliowaelekeza wote zaidi ya watu watatu walikuwepo au hawakuwepo kwenye haya mazungumzo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawakuwepo.
Mhe. Lissu: Walisikiliza au hawakusikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawakusikiliza.
Mhe. Lissu: Waliwezaje kusimamia mazungumzo wakati hawakuwepo na hawakusikiliza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kuna facial impression.
Majaji wanacheka.๐๐๐๐
Ntamamiro (Bwana Jela): Naomba nifafanue.
Mhe. Lissu: Sitaki unifafanulie. Sasa kama hawakuwepo facial expression walizionaje wakati hawapo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hili suala ni la kisheria tunamkagua wakili kitambulisho.
Mhe. Lissu: Nani kakuuliza hayo.
Jaji: Usitupotezee muda. Hebu soma maelekezo yako kuwa wasimamie mazungumzo na watu hawakuwepo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ukiona wanakumbatiana hayaruhusiwi.
Jaji: Uliwaelekeza wafanye nini kwenye mazungumzo hayo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Walisimama mbali wakawa wanaangalia.
Mhe. Lissu: Sasa waeleze majaji kama kitendo cha kukumbatiana ni maneno au kitendo.
Ntamamiro (Bwana Jela) : ni kitendo.
Mhe. Lissu: Ulisema wakasimamie vitendo au maneno?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mazungumzo yaani maneno.
Watu wasonya tu. Majaji pia wamekasirika sana kwa majibu haya. Watu wengine wanacheka kimya kimya.
Mhe. Lissu: Sasa twende SUPP 6 ukurasa unaofuata. Wapo mawakili watatu ambao ni Catherine Chanjarita, Shamumoyo na Constatine kwenye comment zako umesema Adm. Officer simamia mazungumzo yao kwa karibu. Sasa swali langu simamia kwa karibu yanawezekana kutekelezwa bila maaskari hao kuwepo kwenye mazungumzo hayo?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijasema wasikilize nimesema wasimamie kwa karibu.
Part 18 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 16
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza
Mhe. Lissu: Twende Taratibu. Hiki ulicholeta mahakamani ni photocopy?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Original unayo ofisini kwako?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Angalia Tar. 29 na Tar. 30 Sept. 2025. Kuna majina ya wageni kabla ya Tarehe hizo wapo wageni hawaonekani walikuja tarehe gani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ni kweli
Mhe. Lissu: Hawa watu wanne walikuja tarehe ngapi? Wambie majaji sasa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Haioneshi.
Mhe. Lissu: Wewe unajua sasa? Walikuja tarehe ngapi? Maana original unayo wewe.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Tarehe haioneshi.
Mhe. Lissu: Je katika hao watu wa nne. Mtu wa 10 ni nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Paul Kisabo.
Mhe. Lissu: Alikuja kumuona nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : wewe hapo imeandikwa. Alikuja kukuona wewe.
Mhe. Lissu: Soma Tar. 30 Sept. Kwenye karatasi hiyo hiyo. Mtu wa kwanza ni Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Tusiende mbali sasa: Tufafanulie jambo hapa kuna sehemu imenadikwa jina la ndugu, ID no. Simu namba, atokapo mgeni na maoni ya OIC. Sasa hiyo OIC ni Officer in Charge yani wewe hapo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Tar. 30/09 kwenye jina la Kisabo uliandika A/Zamu maana yake Afisa wa Zamu. Na kuna mahali umeandika ADM maana yake ni admission office in charge. Na kuna mahali umeandika IO maana yake intelligence officer?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli kabisa.
Mhe. Lissu: na kuna sehemu umeandika legal unamaanisha Legal Officer Stima.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio
Mhe. Lissu: Hiyo sehemu ya maoni yako ni maelekezo yako kwa hawa niliowataja? Wewe ndio Boss.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kila ofisa ana kazi yake. Kwahiyo ni maelekezo yangu kwao.
Mhe. Lissu: Kwahiyo unakuwa umewapa amri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio.
Mhe. Lissu: Nenda Kwenye kilelezo SUPP 3 pia ni orodha ya mawakili waliokuja Ukonga. Nashon Nkungu lipo hapo ambae ni mlalamikaji wa pili. Andrew Mathew Chima pia alikuja kuniona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Je Andrew Chima yupo kwenye orodha ile ya mawakili wangu niliowaletea ile SUPP 1?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo. Naomba nifafanue.
Mhe. Lissu: Sitaki. Utawafafanulia wa Serikali.
Haya huko mwisho kabisa KULWA MADUHU yupo au hayupo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yupo namuona hapa.
Mhe.Lissu: Na kule mwisho kwenye maoni yako umesema aruhusiwe mwenye kibali. Maduhu hana kibali huko mbele sioni.
Ntamamiro (Bwana Jela): hayuko kwenye orodha ya mawakili wa mahabusu huyu.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama kuna sharti lolote la kisheria kwamba mfungwa yeyote mwenye wakili au wakili anapaswa kuwasilisha orodha ya mawakili wake kwa Bwana Jela?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Halipo kisheria. Lakini mfungwa ana haki ya kuchagua nani amtembelee.
Mhe Lissu: Nilichagua kuwa Kulwa William Maduhu na umemkatalia?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuwepo kwenye orodha.
Mhe. Lissu: Andrea Chima alikuja kuniona yupo kwenye orodha gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayupo.
Mhe. Lissu: SUPP 5 twende sasa tar. 24/12/2025 angalia kwenye entry kuna Nashon Nkungu na Paul Kisabo?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio wanaonekana wote.
Mhe. Lissu: Je Victoria Mgonja alikuja kumuona Jonson Muhanjo. Uliandkka kwenye maoni yako kuwa Adm. Simamia mazungumzo yao. Na mazungumzo hayo yalifanyikia kwenye ofisi ya Admn
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sina kumbukumbu yalifanyikia wapi?
Mhe. Lissu: Kwamba tangu juzi tunazungumza kuhusu mazungumzo ya mawakili yalifanyikia wapi hujaenda kutafuta.
Ntamamiro (Bwana Jela) : sijui inaweza kuwa kwa Mkuu wa Gereza au Adm.
Mhe. Lissu: Mazungumzo na Nashon ulisema asimamiwe kwa Makamu mkuu wa gereza na kuwataka wasaidizi wako wanne wasimamie?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sahihi
Part 17 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 15
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Mkuu wa Gereza, Ntamamiro (Bwana Jela)
Mhe. Lissu: Je askari magereza ambae hasikii au hauoni atashuhudiaje mazungumzo ya mfungwa na ndugu zake watakapokuja kumtembelea
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hayo ni masuala ya kidaktari.
Mhe. Lissu: Sasa Bwana Jela hujui kama wasaidizi wako wote hao kuwa hujui kama wanasikia au hawaoni wewe ni mkuu wa gereza wa aina gani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sik daktari.
Mhe. Lissu: Wewe ni Mkuu wa Gereza wa aina gani? Usiyejua afya za wasaidizi wako?
Ntamamiro (Bwana Jela): Nastahili kuwa kwenye nafasi hii.
Mhe. Lissu: Ndio maana nchi imekwama. Kama watu wenyewe ndio nyie na akili hizi
Mhe. Lissu: Umekuwa Officer incharge tangu lini pale Ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sept. 2025.
Mhe.Lissu: Ulihamishiwa Ukonga ukitokea gereza kuu la maweni Tanga?
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio.
Mhe.Lissu: Ulikuja ukonga kuchukua nafasi ya Juma Mwaibaku?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli.
Mhe. Lissu: Ulipohamishiwa Ukonga mimi tayari nilishakuwa mahabusu ukonga toka April 2025?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta nakaa kwenye special wing pale ukonga?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli
Mhe. Lissu: Wakati unahamia pia ulinikuta naishi huko pamoja na wafungwa wa adhabu ya kifo 100?
Ntamamiro (Bwana Jela): Sikuwakuta.
Mhe. Lissu: Je ulinikuta nakaa peke yangu au sio peke yangu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio peke yako.
Mhe. Lissu: Wafungwa gani hao?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mmoja.
Mhe. Lissu: Je kwa miezi 5 ambayo hukuwepo nilikuwa naishi na wafungwa wa kifo takribani 100?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sifahamu.
Mhe. Lissu: Umeona record ya maandishi ya waliokuwepo special wing umeiona au hujaiona?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijapitia hiyo records.
Mhe: Lissu: Hili suala nilishalilalamikia na lipo kwenye nyaraka za mahakama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu. Tuendelee na maswali mengine.
Mhe/ Lissu: Utaratibu wa wageni kuja kuniona ni weekend?
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: Utaratibu wa wageni wangu kuja kuniona weekend ni kwamba siku moja wanakuja ndugu zangu na siku nyingine wanakuja viongozi wa Chama.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sifahamu.
Mhe.Lissu: Wakati unahamia Ukonga ulikuta utaratibu wa kutembelewa na mawakili wangu ilikuwa nimepeleka orodha kwa mkuu wa Gereza kwa mkuu wa gereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Orodha ya kwanza uliiambatanisha kwenye hati yako ya kiapo kinzani ile ambayo nilikuwa na mawakili 10.
Ntamamiro (Bwana Jela): Orodha hiyo hiyo moja.
Mhe. Lissu: Kwahiyo hakukuwa na orodha yenye jina la Deogratias Mahinyila, Paul Kisabo na Dickson Matata na Mary Stephano.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hakuna hiyo.
Mhe. Lissu: Angalia kielelezo SUPP 1. Ukishakiona niambie.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Anapekenyua hapa..
Mhe. Lissu: Jina la Nashon Nkungu limo kwenye hiyo orodha lipo au halipo? Ambae ni mleta maombi wa pili.
Ntamamiro (Bwana Jela): Ndio lipo.
Mhe. Lissu: Je jina la Kisabo na Maduhu mawakili wangu yapo au hayapo kwenye hiyo SUPP 1
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hawa hawapo kwenye hii orodha.
Mhe. Lissu: Sasa hao wawili wamesema kwa kiapo na kusema hapa Mahakamani kuwa kabla hujahamia ukonga walishaingia gerezani kuonana na mimi walishaingia karibia mara tatu. Wewe unasemaje? Yaani wakati ACP Juma Mwaibako akiwa Mkuu wa Gereza walihudhuria
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulikuwepo wakati huo?
Bwana Jela: Sikuwepo wakati huo. Ila nyaraka zinasema.
Mhe. Lissu: Nenda kielelezo ambacho ni SUPP 2 hapo.
Jaji: SUPP 2 ni nini?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hiki ni kiambatanisho na. 2 kinahusu orodha ya wageni na mawakili waliotembelea gereza la Ukonga.
Part 16 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Part 12
Mhe. Lissu anaendelea kumdodosa Ntamamiro (Bwana Jela)
Ntamamiro (Bwana Jela) : Lakini suala la searching zipo sheria zingine.
Mhe. Lissu: Sasa huko tutafika. Mashahidi wengine nilikuwa nawambia waache kiherehere sasa unataka na wewe nikwambie hivyo halafu tutaendaje Ukonga baadae, sitaki kukwambia hivyo Afande wangu.
Watu wanacheka. Majaji pia wanacheka sana. ๐๐๐๐
Mhe.Lissu: Sasa soma kifungu cha 105(1)(l) kama hakisemi kuwa Waziri ndio mwenye mamlaka ya kutunga kanuni za management na treatment za prisoners. Ndio au hapana?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Naomba nielezee kidogo.
Mhe. Lissu: Nimesema mimi na wewe kwetu ni ukonga tukitoka hapa. Tukitoboa mtumbwi tutafika? Haya jibu swali tusigombane?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Kamishna Mkuu ana mamlaka ya kutunga hizo kanuni za kutunga mambo haya ambayo nimesema hapo juu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Waziri ndio amempa mamlaka kamishna wa magereza.
Mhe. Lissu: kwa kifungu?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kile nilichosema cha 5(2)
Mhe. Lissu: Kile hakijataja Prisoners sasa.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kimetaja Prison ndio Prisoners wapo.
Mhe. Lissu: Kasome Definition section kwenye hiyo sheria kuna tofauti kati ya Prison na Prisoners. Havitumiki interchangebly. Gereza na wafungwa ni vitu tofauti.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sijui.
Mhe. Lissu: Kanuni ya 8 ya kanuni za usimamizi magereza. (Prison Management regulation) je inaeleza utaratibu wa ku search wafungwa.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio lakini zipo na sheria zingine.
Mhe. Lissu: Tutaenda kila mahali. Tutafika kwa hizo sheria zote.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sawa. Nakubali.
Mhe. Lissu: Haki za wafungwa tunaenda kanuni ya 9 hadi ya 11?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli
Mhe. Lissu: Kanuni ya 12 na Kanuni ya 17 je kanuni hizo zinahusu haki ya wafungwa kutembelewa gerezani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Kweli.
Mhe. Lissu: Soma kanuni ya 13 na useme inahusu nini? Ni kweli inahusu haki ya wafungwa kutembelewa na mawakili au washauri wao wa kisheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli.
Mhe. Lissu: Kanuni hizo pia zimeeleza hata namna ya adhabu ya kifo ifanyike kwa maana ya kunyonga wafungwa na masuala yote yanayohusu wafungwa wa adhabu ya kifo? Soma kanuni ya 33.
Ntamamiro (Bwana Jela): haeleweki amesoma nini?
Mhe. Lissu: Ngoja nikusomeee. Anamsomea hapa.
Ntamamiro (Bwana Jela): Nilikuwa sijaiona nimeiona.
Mhe. Lissu: Namna ya kunyoa wafungwa si imeandikwa kwenye kanuni?
Ntamamiro (Bwana Jela): Naam
Mhe. Lissu: Mimi huoni nimefuga rasta sio mfungwa ndio hamuwezi niambia chochote unaelewa hilo?
Ntamamiro (Bwana Jela): uko sahihi.
Mhe. Lissu: Kwa kanuni hizo mahabusu kama mimi napaswa kusimamiwa na askari magereza wawili usiku na mchana.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kuna kipengele cha segregation kwenye sheia zetu.
Mhe . Lissu: Jibu kwa kanuni hizo?
Jaji: Kamishna hakuna mtu atakuadhibu maana kanuni hujatunga wewe. Kwahiyo kama kanuni hazisemi sema hazisemi. Usijipe presha kabisa mzee wangu.
Kumbukeni ana miaka 57 huyu Ntamamiro (Bwana Jela).
Ntamamiro (Bwana Jela): Hakuna hiyo kanuni.
Mhe. Lissu: Ni wafungwa wa adhabu ya kifo tu ndio wanatakiwa kulindwa na askari wawili na wasikilizwa mazungumzo yao ni wa adhabu ya kifo pekee? Kweli au sio kweli.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli
Mhe. Lissu: Inasemaje Baba yangu? Kwanza wewe sio Baba yangu mimekuzidi umri. Si umesema una miaka 57.
Ntamamiro (Bwana Jela): Kwa mujibu wa hiki kifungu ni sahihi wafungwa wa kifo ndio wanapaswa kulindwa.
Mhe. Lissu: Safi tukienda hapa tutafanya vizuri. Kwa hayo ambayo umeyasoma na kwa kanuni hizo. Mahabusu, mfungwa hatakiwi kulindwa muda wote kwa masaa 24 isipokuwa wa kifo kwa mujibu wa kanuni hizo? Kanuni ipi?
Ntamamiro (Bwana Jela): Nimesema Jeshi la magereza linaendeshwa na kanuni, sheria na miongozo.
Part 13 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_MAWAKILI_WA_MHE_LISSU_DHIDI_YA_MKUU_WA_MAGEREZA
Leo July 22, 2026
Jana tuliishia part 10 so leo tunaendelea na
Part 11.
Leo tunaendelea na Andrew Shabani Ntamamiro ambae ni Mkuu wa Gereza yaani Bwana Jela.
Mhe. Lissu: Wewe ndio Mkuu wa Gereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu : una cheo cha ACP?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni Kweli
Mhe. Lissu: Unawajibika kufuata sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Ni jukumu lako wewe na maafisa wengine mnatekeleza majukumu yenu kwa mujibu wa sheria ya magereza na kanuni zake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Unaifahamu vizuri sheria ya Magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Unaifahamu.
Mhe. Lissu: Yote niliyokuuliza ni maswala ambayo yapo katika sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kweli
Mhe. Lissu: Yote niliyokuuliza yapo kwenye kifungu cha nane cha sheria ya magereza?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Anaguna
Mhe. Lissu: Sikutegei jibu swali au omba sheria usome kifungu cha 8.
Ntamamiro (Bwana Jela) : kweli
Mhe. Lissu: kuna kanuni za mwaka 1968 na pia kuna PSO yaani Prison Standing Orders?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Naifahamu.
Mhe. Lissu: Ni ya mwaka gani? Tumeitafuta hatuipati sisi. Unaweza kuniazima?
Watu wanacheka ๐๐๐
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hapa sina ila naifahamu.
Jaji: Ofisini unayo hiyo PSO?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ninayo ndio.
Jaji: Itasaidia sana ukituletea na ukamletea Lissu pia aitumie.
Mhe. Lissu: Nawashukuru sana majaji nataka kushughulika nae kupitia hiyo sheria.
Mhe. Lissu: Sasa hizo PSO zimetungwa na kamishna wa magereza na kanuni za usimamizi wa magereza zimetungwa na waziri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Na PSO zinatungwa na kamishna wa magereza baada ya ruhusa ya waziri?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sijui
Mhe. Lissu: Sasa shika sheria soma section 5(2) Prison Service
Ntamamiro (Bwana Jela) : Kumbe kweli. Inasema hivyo ndio.
Mhe. Lissu: Angalia kifungu cha 105 cha Sheria hiyo ya magereza na kinasema waziri amepewa mamlaka hayo kwa mujibu wa sheria?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ni kweli nimeona.
Mhe. Lissu: Yapi ni mamlaka ya kamishna mkuu wa magereza kwa mujibu wa sheria hiyo? Soma ile 5(2)
Ntamamiro (Bwana Jela) : Nimeona.
Mhe. Lissu: Hayo mamlaka ya Kamishna mkuu ya kutunga PSO na Circulars. Je yanahusu maafisa wa magereza peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Yuko kimya.
Mhe.Lissu: jibu swali sasa.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sio kweli
Mhe. Lissu: Soma sasa hicho kifungu
Ntamamiro (Bwana Jela) : anakisoma kwa sauti.
Mhe. Lissu: Hiyo ni 5(2) kweli?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Hii ni 5(1)
Mhe. Lissu: Sasa nimesema ni 5(2) afande wangu.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Naomba tuanze na 5(1)
Mhe. Lissu: Kinahusu nani na nani?
Ntamamiro (Bwana Jela) : wafungwa na maaskari.
Mhe. Lissu: Wambie majaji kuwa neno Prisons linajumuisha na wafungwa?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Kifungu kinasema taratibu zinaongoza Prison and officers?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Ndio
Mhe. Lissu: Kama ni hivyo kwanini Prisons inajumuisha hadi Prisoners na officers kwanini kifungu kitaje sasa hao Prison Officers?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio mtaalamu wa sheria.
Mhe. Lissu: Mtu pekee mwenye mamlaka ya kutunga kanuni ni waziri peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Mimi sio mtaalamu wa sheria ni mtekelezaji tu.
Jaji: Shahidi umeelewa lengo la swali unaulizwa ili atake kujua unatekeleza sheria ambazo unajua zimetungwa na nani?
Ntamamiro (Bwana Jela): Aniulize tena.
Mhe. Lissu: Ni kweli kanuni zinazohusu wafungwa mwenye mamlaka ya kuzitunga ni Waziri peke yake?
Ntamamiro (Bwana Jela) : Sifahamu.
Mhe. Lissu: Soma kifungu 105(1)(j) kuhusu kusearch wafungwa, askari ni waziri ndio anayetunga.
Ntamamiro (Bwana Jela): Sio kweli.
Mhe. Lissu: Soma.
Ntamamiro (Bwana Jela) : Basi ni kweli.
Part 12 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.