Mzee @freemanmbowetz
Wanyama wa porini huua/kupigana kwa sababu zinazohusiana na mahitaji ya kuishi: chakula, kujilinda, kulinda watoto au eneo. Simba anawinda kwa ajili ya chakula siyo mateso, chuki, kisasi
Binadamu ni viumbe katili zaidi ya wanyama. Binadamu anaweza kumdhuru mwingine kwa sababu ya chuki, ubaguzi, tamaa, kulipiza kisasi, madaraka au kwa sababu anaona mwingine hafai kuishi
Kutoka Mikocheni kwenda ilipo Mahakama Kuu ya Tanzania ni umbali usiozidi 5KM. Kutoka Mikocheni kwenda Rufiji ulipo mradi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere (JNHPP) ni umbali wa 260KM
Unaweza kusafiri kwenda mkoa mwingine kwa zaidi ya saa tano kuhudhuria shughuli za Serikali katili ya CCM lakini huwezi kutumia dakika 10 kutoka kwako kwenda Mahakama Kuu katika kesi ya TAL?
Huwezi kwenda safari ya 5KM kumuona Mwenyekiti wako wa chama, aliyerithi kiti chako katika uchaguzi HURU na HAKI lakini unaweza kwenda 260KM kuungana na watesi wa Mwenyekiti wako?
Nini muhimu zaidi kwako? Ni wewe ulitueleza miradi ya maendeleo haiwezi kuwa mbadala wa haki za binadamu. Leo kuna watu wanatekwa na kupotezwa, wanashtakiwa kwa ugaidi na uhaini. Hujui?
Lakini umechagua nini? Nimekusikiliza ukisema “mradi wa JNHPP usichukuliwe kisiasa kwa kuwa ni mradi unaokwenda kusaidia uchumi”. Umesahau ulitueleza nini kuhusu miradi ya MAGUFULI?
Kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, Freeman Aikaeli Mbowe kwa sasa ni ‘mjumbe wa kudumu wa kamati kuu ya CHADEMA - ni kutokana na hiki kinachoitwa ‘ustaafu’ wa uenyekiti wa CHADEMA Taifa
Kwa maana kwamba, Freeman Mbowe yupo katika kundi sogozi la WhatsApp na mengine (kama yapo) ambayo wajumbe wa kamati kuu wanajadili kwa hisia zao tofauti masuala mbalimbali ya chama
Mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu CHADEMA huwezi kwenda Mahakamani katika kesi ya kiongozi wa chama, lakini unaweza kwenda katika shughuli zinazoongozwa na mwenyekiti wa CCM
Freeman Mbowe umesahau, wakati ukishtakiwa kwa makosa ya uongo ya UGAIDI, Tundu Lissu alikuwa Belgium akijiuguza majera ya risasi. Aliomba kukutana na Rais alipokuwa Brussels
Pamoja na mambo mengine waliyokubaliana, alisema Mwenyekiti Freeman Mbowe aachiwe ndiyo tufungue ukurasa mpya. Tundu Lissu alitujulisha mwenyewe hayo alipozungumza na umma.
Tundu Lissu akiwa na siku 500 gerezani. Mwenyekiti mstaafu wa CHADEMA, Freeman Mbowe hujawahi kukanyaga Mahakamani kuanzia Kisutu hadi Mahakama Kuu hata kwa bahati mbaya.
Saa 24 baada ya Mahakama Kuu kusema Tundu Lissu ana kesi ya kujibu katika mashtaka ya UHAINI ya uongo na uzandiki, Freeman Mbowe unaibuka katika shughuli za Serikali ukiwa na MAWAZIRI.
Mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CHADEMA umekataa kabisa kuhudhuria shughuli zozote za CHADEMA lakini unaweza kuhudhuria shughuli unazoalikwa na WATAWALA KATILI wa CCM.
Unahudhuria shughuli za Serikali umeongozana na mawaziri wa Serikali katili ya CCM wakati ambao wanachama na wafuasi wa CHADEMA kwa mamia wamekamatwa na kushtakiwa kwa UGAIDI?
Mzee Freeman Mbowe umesahau haraka. Kuna watu walifungwa gerezani, wengine sasa ni walemavu, wengine sasa ni marehemu kwa sababu ya kupigania jina lako ukiwa kiongozi wa chama chetu.
Umesahau, wakati unakamatwa na Serikali katili ya CCM, 2021, wanachama wa CHADEMA walikwenda kuonyesha ‘solidarity’ na wewe pale KISUTU. Walikamatwa, wakashtakiwa, wakafungwa
Najutia zile siku nilisimama nawe, kukutetea na kunadi jina lako kwa nia njema kabisa nikifikiri unapambania uhuru, haki na mabadiliko ya kweli. Haikuwa hivyo. Ulitudanganya tukishindwa.
Nasema kwa kuwa kwa hiari yangu, niliamua kusimama nawe, kukunadi katika mazingira ambayo ilionekana ni kama kuuza kitimoto Mecca. Lakini sikutarajia tukishindwa, tuisaliti CHADEMA
Wengine sasa tumeelewa kwa kuchelewa sana. Hii chuki haiwezi kuwa ya kushindwa uchaguzi. Lazima kuna mafekeche mengine. Kuna kingine kimeujaza chuki moyo wako. Je, kuna mrija, umekatwa?
Najutia kumpa mtoto wangu jina lako, Freeman.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo Agosti 11, 2026
Last time tuliishia Part 225 so leo tunaendelea na-;
Part 226
Jana Shahidi wa upande wa Jamhuri ACP Amin Mahamba alianza kutoa ushaidi wake na leo Mhe. Lissu anaendelea kumfanyia Cross-examination.
Mhe. Lissu : Unaweza kuiambia Mahakama kwamba ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa
Mhe. Lissu : Mke wa Amin Mahamba anasema kwamba Amin Mahamba alifariki, sasa iambie Mahakama ulifufuka lini?
ACP Amin Mahamba : Huyo Amin Mahamba anaetajwa sio mimi.
Mhe. Lissu : Kwahiyo ni ushahidi wako kuwa huyu Amini Mahamba ni mwengine sio wewe?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni mwingine tena yeye ni mstaafu na wanasema alishariki kweli kama unavosema.
Mhe. Lissu: Waeleze waheshimiwa majaji kama ulimshirikisha RSO kwenye upelelezi wako?
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Waeleze majaji kama ulimshirikisha afisa yoyote wa TISS.
ACP Amin Mahamba : Sikumshirikisha
Mhe. Lissu: Unafahamu Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa?na kama uliishirikisha kamati ya ulinzi ya mkoa wa Dar es salaam?
ACP Amin Mahamba :Naifahamu na sikuwaashirikisha
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ikulu?ofisi ya VP au Waziri mkuu?
ACP Amin Mahamba : Sikuishirikisha na sikuwaambia lolote.
Mhe. Lissu : Ulishirikisha ofisi ya DPP ndio nilishirikisha kanda maalum NPS.
Mhe. Lissu :Ulimshirikisha nani?
ACP Amin Mahamba: Incharge Mayenga
Mhe. Lissu : Umesema kokote kwenye nyaraka yako?
ACP Amin Mahamba : Sijasema na sijamtaja
Mhe. Lissu : Kwa mujibu wa sheria ya NPS mwenye jukumu la kuratibu upelelezi ni DPP na Mastate Attorney wake.
Waeleze ni DPP yupi au State Attorneys yupi?
ACP Amin Mahamba : Kimya
Mhe. Lissu : Jibu swali wewe Polisi
ACP Amin Mahamba : Sijaelewa swali.
Mhe. Lissu : Swali langu linahusu nani aliecordinate upelelezi?
ACP Amin Mahamba : Ni DPP Mwenyewe, aliteua mtu nilisema jana kuwa sijui jina lake alitoka ofisi ya DPP Dodoma na nilisema ana jina la kibantu nimesahau.
Mhe. Lissu : Tutaenda kwa DPP Mwakitalu atupe hilo jina tuko kwenye serious matters.
😂😂😂 inachekesha sana maana jamaa hajui jina la mpelelezi ambae alishirikiana nae kufanya upepelezi pamoja na kufungua faili la kesi hii.
Mhe. Lissu : Umesema wewe ni mpelelezi wa muda mrefu umewahi peleleza kesi ya kisiasa?
ACP Amin Mahamba : Sijawahi
Mhe. Lissu : Kesi ya uhaini ni kesi kubwa sana ni highest in the land kwahiyo hujawahi kabisa na hii ndo kesi ya kisiasa ya kwanza.??
ACP Amin Mahamba : Sijawahi hii ndio ya kwanza
MheZ Lissu : Umewahi peleleza kesi ya mtu alikuwa mbunge na kiongozi wa Chama kama lissu?
ACP Amin Mahamba :Sijawahi
Mhe. Lissu : Umesema kitengo chako kinashugulika na makosa ya mtandao
ACP Amin Mahamba : Ndio
Mhe. Lissu: Ushapeleleza kesi ya cybercrime?
ACP Amin Mahamba : Ndio nimewahi.
Mhe. Lissu : Kesi gani shahidi?
ACP Amin Mahamba ; Nakumbuka nikiwa RCO Kinondoni
Naona kasita kama dakika 5 hivi then akasema kesi ya Mbowe na Mzee wa karatu Slaa
Mhe. Lissui : Waeleze ilikuwa inahusu nini na iliishaje?
ACP Amin Mahamba ; DPP hakuwa na interest ya kuendelea na kesi ikaisha hewani.
Mhe. Lissu : Una kesi zingine zaidi ya hizi kwenye cybercrime?
ACP Amin Mahamba ;Hapana
Mhe. Lissu: kwahiyo hauna kesi nyingine zaidi ya hiyo iliyofutwa?
ACP Amin Mahamba : Ninazo nyingine nyingi siwezi kuzikumbuka nikiwa RCO na OCCID.
Mhe. Lissu : Kwahiyo jana kweye ushahidi wako unasema mimi ndie niliechapisha video yangu hapa mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndiyo nilisema.
Mhe. Lissu ; Unafahamu maana ya neno kuchapisha mtandaoni?
ACP Amin Mahamba : Ndio nafahamu lakini sheria ambayo imetumika kukushitaki sio Cybercrime.
Mhe. Lissu : Waeleze waheshimiwa majaji kama mm ndie nilisambaza video za YouTube kwenye mtandao wa Jambo tv?
ACP Amin Mahamba : Ndio ni wewe ulisambaza hizo video.
Part 227 itaendelea kwenye post inayofuata.
Naomba Repost yako.
With these pictures showing the bond we shared, I almost felt I could get away with saying nothing about you leaving. It’s been an honour to be your teammate and your friend. You’ve won it all and you leave as a legend. I’m sure we will meet again.
ONENI MPUMBAVU HUYU
Hata miezi 6 haijapita Msanii wenu alikuwa anatuambia, “Fanyeni Kazi kumamae zenu, kila kitu serikali serikali, kila siku kulalamika tu”… LEO ndio anakuja kulia baada ya kushtukia ametumika kama CONDOM na kutupwa?!
What happened? Vipi Serikali imeishiwa hela ikaja kukudai kodi nini? Na kidogo Media yako ife.. au? Ooh kumbe haihusiani na Media, mlikuwa mnafanya renovation tu. 🤣
Acha kutupigia Kelele na Mambo yako sijui Serikali haijali Muziki, Sijui Arena imefanyaje. Ulichagua upande, KUFA KIMYA KIMYA HUKO HUKO ULIPOCHAGUA.
Haujawahi kushirikiana na Wasanii Wenzako kwenye group za Wasanii, Haujawahi kutoa ushirikiano kwenye TUMA wala SHIRIKISHO LA MUZIKI. Haujawahi kujadiliana na wenzako kuhusu mambo ya ujenzi na Ukuaji wa Tasnia… Mmekuwa mnajiona mmemaliza kila kitu. Yamewashinda mnataka kuanza kupiga yowe na kutaka huruma ya Wananchi. Well, nyie mmetiwa na kuachwa, sisi wamewaua ndugu zetu so tuna msiba bado (40 haijaisha maana baadhi ya Miili haijapatikana bado). Njoo MSIBANI KWANZA then ndio tutajadili mambo ya mamiziki yenu.
Wewe ndio wa Kulilia MIUNDO MBINU YA TASNIA?! Msanii uliyebebwa na Marais (Kikwete, Magufuli), Serikali, Media (yes Clouds made you), ukawazidi wenzako kwa hatua ambazo hawajaweza kukufikia tena, alafu watu walipolilia Miundo Mbinu ukawabeza, na Walivyotaka kuiwajibisha Serikali ukawakejeli. Ghafla wewe ndio unajua nafasi ya serikali? Au ni baada ya kufeli huko “International”.
Anza wewe kwanza kutengeneza MIUNDO MBINU na Mazingira Rafiki ya Kazi kwa Wafanyakazi wako ili Serikali iige Mfano wako.
Lipa Dancers Vizuri
Lipa Wapiga Bendi Vizuri
Lipa Sound Engineers Wa Maana
Lipa Watangazaji (ili wasigome)
Lipa Artists unaowa sign WCB Vizuri (Including Mkeo hiyo)
Lipa Video Vixens Vizuri
Lipa Waimbaji wa Bendi Vizuri
Kukiwa na Show ya Live hapa leo yako na Yangu, Wapiga Bendi Watachagua kuja kupiga kwangu, maana wanajua Wakazi atawathaminisha kwa Malipo Mazuri zaidi (na hapo wewe unalipwa mara 10 yangu). Bisha?
AND YES, Unajua kwanini mnakumbukwa wakati wa Kampeni tu? Ni sababu Wanejua nyie ni Wapumbavu, msiojitambua wala kutambua Power yenu kama Wananchi na Wapiga Kura, na pia Influence na Leverage yenu kwenye kuishinikiza serikali kuleta Mabadiliko.
So Kiufupi, TOKA HAPA!! 😏
BEBERU
The Leader
#FreeTunduLissu
Kama wewe bado unafikiri ishu hii ya kutaka Tundu Lissu aachiwe ni ya CHADEMA au wanaharakati basi huelewi siasa mbovu inavyoathiri vibaya maisha yako!
Ukishindwa kupigania haki za msingi za wengine usitarajie watakuwepo wa kukupigania haki zako wewe! Kwa sasa kila mtanzania ana wajibu wa kuweka #FreeTunduLissu na kuwaambia hawa wauaji kuwa INATOSHA!
#WenyeNchiWananchi
Tunataka nchi itulie na tujenge Taifa - inaanza na unconditional release ya Lissu na #SamiaMustGo nje ya hapo ni kupoteza muda na huu muda wa kujenga ukipita hautarudi tena!
Yaani nchi ikwame kwa sababu ya genge ndogo inayoongozwa na Bi Kizimkazi?
Eniwei msiponielewa leo basi huko mbele #TutaelewanaTu mambo yakiwa magumu zaidi!
#FreeTunduLissu
Kwaheri Dkt. Ayub Rioba Chacha. Umetuachia TBC dhoofu.
Sio kazi ndogo kuitumia miaka (10) kugeuza Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kuwa idara ya uenezi ya tawi la CCM. Shirika ambalo Watanzania wengi sasa hawajisikii fahari kamwe kufuatilia shughuli zake.
Wakati dunia ikikimbizana na teknolojia ya 4K na uandishi wa kiuchunguzi, TBC chini yako ilikuwa 'bize' kuboresha teknolojia ya kusafisha makosa ya serikali kwa kutumia sabuni yenye manukato ya propaganda.
Siku ya uzinduzi wa Meli ya M.V Mwanza, Mtangazaji wa TBC alisema meli hiyo itafanya safari zake katika nchi mbalimbali itakwenda Kenya, Uganda, Burundi, DR Congo, Zambia, Malawi na Sudan Kusini,
Uongozi wa TBC ukajitokeza kutoa ufafanuzi kwamba mtangazaji alichokusudia kukisema ni MV Mwanza itasafırisha mizigo ambayo baadaye itapakiwa katika vyombo vingine vya usafıri kuzifıkia nchi zilizotajwa.
Pamoja na malezo na ufafanuzi huo kutoka kwa uongozi wa TBC, bado mtamgazaji alichukuliwa hatua za kinidhamu baada ya maneno yake. Hapo ndiyo nilihitimisha mtazamo wangu, Mmechanganyikiwa.
Utetezi wako kuhusu TBC kuonesha matangazo ya mpira (AFCON na WORLD CUP) yasiyokuwa na ubora wa picha kwamba ni fitina tu, ulituonesha sasa umefika kikomo cha kuendelea kuwa Mkurugenzi wa TBC.
Shukrani kwa kuhakikisha TBC haifanyi kazi yake ya msingi kama chombo cha habari cha umma. Ilikuwa kazi ngumu kuhakikisha Watanzania hawapati habari za kweli. Lakini wewe uliishinda changamoto hiyo.
Wakati mashirika ya habari ya serikali kama Al Jazeera (Qatar), NHK (Japan), BBC (UK), DW (German), France 24 (France), ABC (Australia) yanajaribu kujitenga na siasa, TBC ilichagua njia tofauti. Njia ya propaganda.
British Broadcasting Corporation (BBC) haina hofu ya kuikosoa serikali ya Uingereza. Kipindi chao cha Panorama au mahojiano ya asubuhi ya Radio 4 huwabana mawaziri mpaka wanashindwa kujibu.
Waandishi wa BBC hawasubiri tamko la serikali ili kutoa habari; wao ndio wanatafuta habari. BBC inajiona inawajibika kwa walipa kodi, wakati TBC chini yako inajiona inawajibika kwa mteuzi wako na watawala.
Mashirika ya Kimataifa yanalazimika kuwa bora ili visipoteze wasikilizaji. TBC chini yako imejiona haina kitu cha kupoteza kwa sababu ina uhakika wa ruzuku kutoka Serikalini bila kujali ubora wa maudhui.
Wakati mashirika ya utangazaji ya umma huko duniani yanajitahidi kusimamia uhuru wa habari, TBC chini yako iliamua kuwa jukwaa halali la propaganda za Serikali. Nafikiri Ulichagua propaganda kwa kuwa zinalipa..
Umeondoka ukiacha nyuma kivuli cha taasisi kuliko taasisi yenyewe. TBC iliugua kwa muda mrefu, na wewe kama mkurugenzi (Daktari), uliandika dawa ile ile kila siku—dawa iliyozidisha ugonjwa badala ya kuponya.
Chini ya uongozi wake, TBC ilifanikiwa kwa njia ambazo hakuna mkurugenzi mwingine angeweza: TBC sasa ni runinga ambayo Watanzania hawaitazami. Mafanikio makubwa. Kufikia zero audience si kazi ndogo!
Chini ya uongozi wako, TBC ilifanikiwa kuacha kuwa chombo cha habari na kuwa mdomo wa mapambio. Habari ikianza, unajua tu ni nani amepiga chafya ‘White House’ na nani amekata utepe wa choo cha shule.
Umeifanya TBC kukaa mbali na kero za wananchi kama vile muuguzi anavyokimbia mgonjwa wa kipindupindu. Wananchi wanalia kukosa ajira, TBC inakuonyesha kipindi cha maendeleo ya viwanda vya kufikirika
Ni ufundi wa hali ya juu kuiacha TBC mahututi kiasi kwamba hata kulinganishwa na redio mbao ni matusi kwa redio mbao hizo. Leo hii, TBC inazidiwa viewership na 'online garbage media' zenye kamera moja tu.
Umeifanya TBC kuwa chombo ambacho watu wanatazama pale wanapotaka kujua kama kuna “teuzi” au kuna “salamu za rambirambi” au labda wanataka kufuatilia gwaride la maadhimisho ya UHURU.
Gari la umma linapaswa kubeba kila mtu: mawazo mbadala, upinzani, na asasi za kiraia. TBC chini yako ilichagua kubeba “watawala pekee,” huku ikiwaacha wananchi barabarani na kero zao, watajijua huko.
Tulitegemea ushauri kwamba, Mkurugenzi wa TBC ateuliwe na bodi huru baada ya ushindani wa kitaaluma. TBC, uteuzi ni wa kisiasa, hivyo “dereva” lazima amsikilize aliyempa gari badala ya abiria (wananchi).
Kuwe na Bodi Huru ya Utangazaji. Wakurugenzi wasiteuliwe na mwanasiasa, bali wafanyiwe usaili na bodi ya kitaaluma. Hii itawapa ujasiri wa kuruhusu habari zenye kukosoa bila hofu ya kutumbuliwa.
Hutakiwi hata kuwasuta hao ambao wanakuona/wanakuita ‘chawa’. Mazingira ya utendaji shughuli zake TBC ukiwa Mkurugenzi Mtendaji zinasadifu hicho ambacho wakosoaji wako wanakiona kama ‘uchawa’
Tulitegemea TBC ikiwa chini yako, kwa muktadha tuliokufahamu nao ukiwa mhadhiri UDSM, lazima iache kufanya kazi kama State Broadcaster (ya utawala) na ianze kuwa Public Broadcaster (ya wananchi).
Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) ilipaswa kuwa Public Broadcaster (inayotumikia maslahi ya umma), lakini sasa inafanya kazi kama State Broadcaster (inayotumikia maslahi ya utawala uliopo).
Kama TBC ingekuwa gari, umeiacha kama gofu—haina injini wala matairi, lakini inapiga honi za kelele. Ni kitu kilichosimama tu kinachojidai kuwa chombo cha maendeleo. Ni kushindwa kimuundo na kitaalamu.
Martin Maranja Masese (MMM) / Mtikila.
There is deeply alarming and credible information that @SuluhuSamia and her inner circle are actively plotting to harm @TunduALissu, including the possibility of eliminating him altogether. This is not only unconscionable, it is a grave violation of fundamental human rights and a direct assault on the very idea of democratic political competition.
Let it be stated in the clearest possible terms: @SuluhuSamia will bear full, personal, and international responsibility for any harm that comes to Lissu. There will be no ambiguity, no deflection, and no escape from accountability.
We call on all defenders of justice, democracy, and human dignity—across Africa and the world—to rise with urgency and speak out with one voice. Silence in this moment would amount to complicity. The international community must act decisively to deter this looming atrocity and ensure the protection of Tundu Lissu.
#FreeTunduLissu @idualliance@UN_HRC@achpr_cadhp@AJEnglish@CanadaTanzania@UKinTanzania@EUCouncil@EUinTZ@davidmcallister@commonwealthsec@SADC_News@AmnestyEARO@hrw@antonioguterres
UISLAM ni dini yenye misingi imara ya kuongoza jamii kuelekea katika HAKI, USAWA na kupinga kila aina ya DHULUMA, inayokataa UKANDAMIZAJI kama inavyobainishwa katika Qur’an (57:25, 28:4, na 7:103-105). UISLAM ni DINI nzuri. UISLAM siyo dini ya wahuni. BAKWATA ndiyo wanaichoresha na kuifanya ionekane ni sehemu ya matumizi ya dola. Jambo ambalo linachafua taswira nzuri ya UISLAM. BAKWATA wenyewe hawaelewi wanataka HAKI, AMANI au WALI.
Mnaokaa na siri nzito za kuua na kudhulumu uhai eti mnafanya kazi serikalini ujumbe wenu kutoka Padre Kessy
Ni kwamba ITAKUTAFUNA‼️
Sasa msikilizeni mjisahihishe mkiwa bado hai nje ya hapo kwisha habari! Na msimtafute kumteka washenzi ninyi
#TutaelewanaTu
“NENO LA SHUKRANI
Ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa ndugu, jamaa, na marafiki kwa msaada wenu mkubwa mlionipa nilipo kamatwa na kuweka ndani Tanzania.
Shukrani za kipekee kwa DIASPORA wote wapenda HAKI waliosimama na Mimi kwa hali na mali bila kujali itikadi. Familia yangu Tanzania na hapa Marekani waliokesha kila siku kuhakikisha ninatendewa haki kwenye Kukamatwa kwangu kinyume cha sheria na serikali kushindwa kunifungulia kesi yoyote, ni dalili ya wazi ya vita ya Serikali dhidi ya sisi diaspora.
Shukrani kwa Ubalozi wa Marekani Tanzania (@usembassytz), Wizara ya mambo ya nje ya Marekani (@StateDept ), US Senators, gazeti la Mwanahalisi, Chama Cha wanasheria TLS chini ya Rais Boniface Mwabukusi. Shukrani kwa wakili Kilatu na wakili Ntungi.
Niliondoka Tanzania siku ya Jumatatu, March 9, 2026 kupitia uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere kwa msaada wa Ubalozi wa Marekani. Nilifika Marekani kesho yake, Jumanne, March 10, 2026.
Upendo, maombi, ushauri, na msaada wenu wa hali na mali vimenitia moyo sana na kunisaidia kuvuka kipindi kigumu.
Kwa kweli nathamini sana mshikamano wenu na moyo wenu wa kujali ndugu zangu wa diaspora kwa ujumla. Mungu awabariki sana na awalipie mema yote mliyotenda.
Asanteni sana kwa kuwa pamoja nami katika wakati mgumu.
Shukrani nyingi.
Thadey Kweka
Washington, DC, USA
March 12, 2026”
“There must be an independent, transparent and inclusive investigation of these events to ensure accountability and that the fundamental freedoms and constitutional rights of all Tanzanians are protected.” - UK's Human Rights Ambassador, @ESandersFCDO
https://t.co/B3MY6toKOB
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 225
Mhe. Lissu anaendelea hapa.
Kama mtakumbuka nilisema ninavyoishi Ukonga, siruhusiwi kuonana na Mawakili wangu in private.
Mnaruhusiwa kutembelea Magereza naomba mliangalie na hili kama itawapendeza inawapa Mamlaka ya kutoa mapendekezo na mamlaka za Magereza kurekebisha masuala yanayohusu wafungwa kama haya niliyosema.
Ni muhimu kwamba kuwasiliana na washauri wangu wa kisheria ilindwe kama sheria inavyosema bila kusikilizwa na maafisa wa Magereza.
Ni hayo tu Waheshimiwa
Mhe. Tundu Lissu amemaliza na amekaa sasa.
Majaji wanaandika hapa.
Anasimama Renatus Mkude kuwa tutampatia hizi nyaraka ndani ya siku 14 tutampatia.
Hili la masuala ya utawala wa mambo ya magereza kwa mujibu wa kifungu cha 16 cha National Prosecution Act na sisi ofisi ya DPP tutatembelea ili kuhakisha kunakuwa na fair trial.
Wameombwa Majaji anasema DPP ataenda eti huko Magereza kuangalia haki za Mtuhumiwa. Uongo uongo uongo. Hawana hata aibu hawa jamaa.
Majaji wanaandika baada ya kusikia hayo kutoka kwa Wakili wa Serikali, Renatus Mkude.
Majaji wanajadili pale.
Yuko Jaji muda wote yeye huwa anacheka anafurahi tu sijui huwa anatabasamu jambo gani? Wanaofika hapa Mahakamani wanamfahamu vizuri.
Jaji Ndunguru: Tumesikia hoja za Jamhuri na Hoja za Mshitakiwa nae kama ambavyo mshitakiwa ameturahisishia kuwa mikono yetu imefungwa kwamba yapo hayo maombi ya marejeo Mahakama ya Rufani.
Sasa shauri hili linasimama hadi pale Mahakama ya Rufani itakapotoa uamuzi.
Suala la Gerezani wakili wa Serikali amesema na sisi pia tumelichukua.
Mwenendo wa shauri hili unasimama hadi pale mambo ya Court of Appeal yatakapoisha.
So kesi hii imeahirishwa hadi hapo itakapoitwa tena.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 224
Majaji wameingia muda huu saa nane Kamili Mchana.
Wanaandika pale juu.
Mheshimiwa Lissu ameingia na kuteta jambo na Dr. Nshala tunamsikia anasema waende kokote watakapotaka kwenda tutakutana nao huko. Sasa sijui ni wapi anamaanisha.
Anasimama Renatus Mkude Wakili wa Serikali kwa niaba ya jopo la Mawakili wa Serikali tunaomba radhi kwani tulifikiri tungetumia lisaa limoja.
Mchana huu nipo na Ajuaye, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Kwa wote tunawakilisha jamhuri na Mshitakiwa yupo.
Shauri lilipangwa kuendelea na mashahidi. Lakini tumetafakari na tunaitafsiri kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Appellate Jurisdiction Act na kanuni ya 65(1) ya kanuni za Mahakama ya Rufani.
Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) anatoa taarifa ya kuwasilisha taarifa ya mapitio (revision)
Hapa kwanza anakosea Mapitio ni Review alipaswa kusema Marejeo ndio Revision sijui kasoma wapi nae huyu jamaa.😂😂😂
Anaendelea hapa Renatus Mkude, kuwa Notice of motion hiyo imeambatanishwa na kiapo cha Cathbert Mbiringe Wakili wa Serikali ambayo taarifa hii ya kutoa notice kwenda Mahakama ya Rufani imesainiwa leo Tar. 24/02/2026.
Na kupokelewa kwa mifumo ya kielektroniki inayotambulika na Mahakama na kusajili kama. CRIMINAL REVISION NO. 7203216/2026 imepokelewa na Mahakama ya Rufani Tanzania hapa Dar es salaam.
Ambalo chimbuko lake ni Criminal Sessions No. 19605/2025 ambayo iko mbele yenu Waheshimiwa Majaji wa Mahakama Kuu. (Ndunguru, Karyemaha, Kiwonde)
Kwa kuwa shahidi wetu aliyekuwa anafuata ACP Mahamba tuliyemuombea notice additional substamce of evidence na ikakataliwa.
Ni Rai yetu kwamba kwa kuwa shauri hili limeshapokelewa Mahakama ya Rufani haiwezi kusimama ili kuweza kutoa nafasi kwa shauri husika huko Mahakama ya Rufani kuweza kuamuliwa.
Ni hayo tu kwa sasa.
Tunamsubiri Mh. Lissu atajibu nini?
Mhe. Lissu anaanza.
Baada ya kuzikiliza wasilisho la upande wa Mashitaka nina haya ya kusema.
1. Kwa vile mimi nipo gerezani na wanajua nataka wanipatie hiyo nakala ya Notice of Motion waliyofile niweze kuiona.
2. Ninafahamu na ninatumaini na wao wanajua kwamba kwa mujibu wa kifungu cha 8(2)(d) cha Sheria ya Mamlaka ya Rufaa ambacho wamekitaja (Appellate Jurisdiction Act) wanafahamu kwamba hakiruhusu rufaa wala mapitio wala marejeo ya maamuzi ya Mahakama ambayo hayamalizi shauri la msingi. (Interlocutory decisions) sina shaka na wao wanalifahamu hilo.
3. Waheshimiwa Majaji siwaombi mtoe uamuzi wowote kuhusu hili ninalolisema.
Nataka iwe kwenye record kwamba nafahamu na naamini upande wa mashitaka wanafahamu lengo la kupeleka ombi la marejeo Mahakama ya rufani na wanafahamu hairuhusiwi ni kurefusha mashauri haya ili niendelee kukaa Gerezani. Ni hilo tu.
Kwamba tupeleke Mahakama ya Rufani ili huyu mbaya wao ambae ni mimi aendelee kukaa Gerezani.
Kwa vile wananipeleka kwe ye Mahakama ya Rufani nataka niwaeleze kuwa nitawafuata huko huko naenda kuwashughulikia huko huko.
Kama ambavyo kesi yao is dead on arrival najua hata hii revision yao pia imeshakufa.
Tutarudi hapa yakiisha huko ya Mahakama ya rufani tutarejea hapa na nitawashughulikia tukirudi.
Jambo la Mwisho Mawakili wangu wametaka kunipa nyaraka hapa lakini siwezi kupewa hadi nyie mseme.
Sijui wanaogopa nini watu wa magereza nisipewe huo uamuzi hapo ni makaratasi tu.
Naambiwa ni hukumu kutoka huko Umoja Wa Mataifa lakini Magereza wanaogopa nisipewe.
Tena ni uamuzi unaohusiana na mimi kuwepo Gerezani. Tatizo liko wapi?
Jaji anasema uko wapi? Umepelekwa wameuona wamesema wape Mawakili wa Serikali.
Wako wanasoma hapa Mawakili wa Serikali huo uamuzi.
Anasimama Renatus Mkude anasema mimi ni member wa working group za UN Human Rights Council.
Jaji: Tumesema apewe au asipewe?
Renatus Mkude: Apewe tu.
Part 225 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
JAMBO LA KUSHANGAZA MAHAKAMANI.
Muda huu wameingia wasaidizi na walinzi wa Majaji wamechukua Computer na vifaa vya Mahakama wameondoka navyo.
Inaonekana muda huu kesi haiwezi kuendelea maana wanaondoa kila kitu Mahakamani.
Taarifa tuliyonayo Mawakili wa Serikali hawajaonekana na hawajarudi Mahakamani so muda huu Karani amesimama hapa na kusema kuwa kuna jambo limejitokeza anaenda kutafuta ufafanuzi kwa Msajili wa Mahakama atarudi kuleta mrejesho.
Kwahiyo tupo njiapanda hatujui kinachoendelea hadi sasa.
Kesi imewashinda wanalazimisha ni aibu kwa Mahakama kuiamuru Jamhuri kuwa ilete Mashahidi baada ya lisaa limoja kwasasa ni masaa mawili yanaelekea matatu hakuna kinachoendelea.
Mawakili wa Serikali wanaamua kesi iendelee au isiendelee.
Vituko, Vichekesho na Maajabu.
Tunaendelea tuone mwisho wa hizi drama zao.
Wako Muhabarishaji,
Hilda Newton.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 24, 2026
Last time tuliishia Part 222 so leo tunaendelea na-;
Part 223
Majaji wameingia na Mshitakiwa pia ameingia.
Karani anasoma shauri hapa.
Anasimama Renatus Mkude anasema yupo na Ajuaye, Katuga, Thawabu, Cathbert Mbiringe.
Anasema leo tumekuja kwa ajili ya kupokea ruling na sisi tuko tayari.
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa unasemaje?
Mhe. Lissu: Na mimi niko tayari.
Jaji anaanza kusoma hapa UAMUZI.
Uamuzi huu unatokana na pingamizi lililowekwa na pingamizi la mshitakiwa kutokana na taarifa ya kuongezwa kwa ushahidi.
Taarifa hiyo ililetwa tarehe 18/02/2026 na upande wa Mashitaka kwamba unatokana na pingamizi lililowasilishwa na mshitakiwa.
Notice hiyo ililetwa kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Mshitakiwa alieleza Mahakama kwamba kifungu hicho kinaelezea shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa wakati wa mwenendo kabidhi na hivyo walichokileta upande wa mashitaka ni kuleta ushahidi mpya.
Upande wa mashitaka walijibu notice ipo halali kwa mujibu wa sheria na imekibidhi matakwa ya kisheria na ipo kwa mujibu wa sheria.
Huo ndio ulikuwa msingi wa hoja za pande zote mbili.
Mahakama imeona hoja inayopaswa kuamuliwa ni je notice hiyo ipo kwa mujibu wa sheria?
Ili kurahisisha Mahakama imeona ili reproduce notice hiyo inavyosema.
Anasoma notice inavyosema kwamba ni notice ya kuongeza maelezo ya ziada ya shahidi husika ambae ni Amin Mahamba.
Hakuna mashaka kwamba upande wa mashitaka wanataka kuongeza ushahidi wa Amin Mahamba.
Kwa vile Amin Mahamba ni shahidi na statement yake ilishasomwa wakati wa committal ilishasomwa.
Notice inasema ushahidi unaotaka kuletwa ni wakati wa uchaguzi wa tar. 29/10/2026.
Anasoma kifungu cha 308 cha CPA kinavyosema.
Ukiangalia kifungu hicho kinatoa masharti au mazingira ambayo notice hiyo ni reasonable au laaa.
Masharti ni kwamba
1. Maelezo yatoke kwa shahidi
2. Uwe ni ule ushahidi ambao haukusomwa wakati wa committal
3. Uwe ni ushahidi ambao haukusomwa wakati wa proceedings
Kifungu cha 308 ndio kinachosema hawezi kutoa ushahidi hadi watakapoleta notice na hivyo basi ukiangalia hayo kifungu hicho cha 308 kinafungua mlango kwa shahidi ambae alikuwepo na bahati mbaya maelezo yake hayakuletwa.
Amin Mahamba maelezo yake yalikuwepo wakati wa commital, anataka kuleta mambo ya Uchaguzi ambayo hayakuwepo wakati wa committal.
Ipo kinyume na kifungu cha 308 cha CPA.
Hivyo basi kifungu cha 308 kinaweza kuruhusu notice hiyo tumeona kwamba kifungu hicho hakiruhusu kabisa.
Shauri la Remina Omary Abdul tumeona linahusiana na vielelezo vya wakati wa committal. Shauri hilo haliwezi kutibu chochote katika hoja iliyopo mbele yetu.
Hiyo notice ya kuongezwa kwa ushahidi ambayo imeletwa na upande wa mashitaka haitambuliwi na kifungu cha 308 cha CPA.
Kimsingi tunasema kwamba fundamentally haiko sahihi na baada ya kusema hayo basi notice hiyo ni incompetent na tiba pekeee iliyopo ni kwamba notice hiyo lazima iwe struck out. Ni hayo tu.
Anasimaa. RENATUS MKUDE anasema baada ya kupokea ruling tunatafakari tunaomba ahirisho ya lisaa limoja.
Twende kutafakari.
Bado majaji wanashauriana pale juu.
Nafikiri leo KATUGA atajua vizuri nani ni Bingwa wa Sheria😂
Anasimama Mh. Lissu anasema mmesema kuwa mashahidi waletwe leo na mlisema tutasikiliza uamuzi wa pingamizi na tutasikiliza shauri leo.
Sasa wanasema tuahirishe kusikiliza ili wakatafakari.
Wanaenda kutafakari nini? Ili iweje? Huu uamuzi haukatiwi rufaa.
Tusipoteze muda kila tunapopoteza muda anayeumia ni mimi sasa wao walipaswa kuleta mashahidi na wasitupotezee muda kabisa, tuendelee kusikiliza shauri hili.
Majaji wanaandika kidogo
Anasimama Renatus Mkude anasema tumemsikia Mshitakiwa
Tuna mambo mawili.
1. Tumepokea ruling ya Mahakama na tumeikubali
2. Jambo la pili ni kwamba tulimtaja shahidi ambae lazima tuwezi kumuandaa shahidi yetu
Jaji Ndunguru anasema tulisema muwe na mashahidi wakutosha. Tukiendelea kubishana tutapoteza muda, turudi mahakaman saa 5 kamili
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 222
Katuga anasema kifungu cha 308 ni mlinzi wa kifungu cha 263 cha CPA ni kumfanya mshitakiwa awe aware na ushahidi wote anaokutana nao Mahakama kuu.
Ushahidi upo wa aina nne, real, documentary, testimonial na nyingine nimesahau nitaikumbuka.
Kwahiyo kwa maana ya aina ya shahidi nne zinatakiwa zioneshwe kwa mshitakiwa kabla ya kuwa committed kwenda High Court na kwakuwa kuna takwa hili la 263 kukawekwa kifungu cha 308 ambacho ni mlinzi sasa.
Kwamba hakutakuwa na ushahidi utakaoingia hadi uwekwe wazi basi prosecution wampe notice kuhusiana na ushahidi huo ni lini prosecution wamegundua huo ushahidi. Je mshitakiwa alikuwa na reasonable time kuupitia.
Kif. 308(4) kinazungumzia substance or witness.
Kesi ya Remina Omary Abdul vs Jamhuri CA 189/2020 Mahakama ya Rufaa ilisema, INASEMA IF PART OF THE EVIDENCE IS NOT DISCLOSED.
Mahakama ili quote with approval maneno kuwa additional evidence is allowed.
Sisi tunasema mbali na statement yake kusomwa tunataka kuleta mambo mengine ambayo hayakujumuishwa.
Notice hii ina comply na tafsiri ya sheria na sio tafsiri ya mtu. Iko sheria na tunaomba ikubaliwe.
Katuga kuna maneno pia yamesemwa kuwa notice hii ikiachwa hizo sio hoja. Unamtisha nani? Naona kama anatutisha ni hoja ambayo itafungua pandora na hiyo pandora ni ipi?
Tunaomba mapingamizi yatupiliwe mbali.
Anasimama Mh. Lissu kumjibu Kituga.
Nimesikiliza majibu yao naomba niseme yafuatayo.
1. Kifungu cha 308 cha CPA kinahusu shahidi mpya. Shahidi mpya kimesema ni yule ambaye maelezo yake au substance ya maelezo yake haikusomwa kwenye committal. Kwahiyo kifungu hicho kinahusu shahidi mpya na sio ushahidi mpya. Suala ni shahidi wa ziada na sio ushahidi wa ziada wa shahidi ambae tayari maelezo yake yapo tayari.
2. Kwenye notice hii suala la kuamua sio reasonable au laa. Ni suala la kinacholetwa ni shahid mpya au laa.
3. Hiyo kesi ya Remina Omary Abdul waliyoleta si mara ya kwanza inazungumzwa kwenye Mahakama hii. Ililetwa kipindi kile cha Committal. Inahusu kifungu cha 263 tu. Ukurasa wa 32 ni kuhusu section 246 ambacho ni 263 ya sasa. Kwahiyo hiyo kesi inahusiana na mambo ya Committal basi kifanyeni kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Mlango wa Amin Mahamba ulifungwa kwenye committal kama mnataka tafuteni shahidi mwingine sio Amin Mahamba.
Hoja ya kwamba hili ni pingamizi limeletwa pre mature nasema liko timely maana yanayohusika na kesi hii yalishakamilika na kuletwa Mahakamani.
Effect yake ni kunibadilishia shitaka maana shitaka langu ni la tar. 03/04/2025 haya ya October ni mambo mapya.
Mkiyaruhusu kwa kuruhusu notice hiyo na nimesema niko tayari, je wao watayaweza? Kwasababu ya October kuna genocide kuna mass killings, mass murder. Ya October ni magumu sana.
Pingamizi langu litalinda integrity ya shauri hili na mashauri haya. I'm only trying to help them wanafikiri kuna deal pale hakuna deal yoyote.
Angalieni kifungu cha 308 cha CPA.
Hii notice ifutiliwe mbali, naomba hivyo.
Majaji wanateta hapa.
Tunasubiri uamuzi wao kuhusu pingamizi hili.
Jaji Ndunguru amejadiliana na wenzake kwa muda mrefu sana hapa.
Anasema ili tuweze kuandika uamuzi na tutarudi kesho saa tatu asubuhi na tutaendelea na mashahidi wengine.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 221
Jaji Ndunguru ameteta sana na wenzake kama dakika 10 hivi.
Sasa anawasha kipaza sauti.
Anasema yafuatayo: tumesikiliza hoja zote hivyo vijembe vyenu msivilete.
Sasa mshitakiwa alisema anapingamizi na tukasema upande wa mashitaka walete open statement ili Mahakama iamue.
Mambo mengine ya kwamba imeambatana na nini na nini kipo wapi hayo sio mambo ya msingi.
Mshitakiwa endelea sasa, hawa upande wa mashitaka mmemaliza hapo, presentation ya notice na justification ya notice.
Watu wanacheka hapa 😂😂😂😂
Nafikiri mpaka sasa Katuga ameelewa nani ni Bingwa wa Sheria.
Mhe. Lissu amasimam, sasa Waheshimiwa Majaji kwa kuanzia niseme hivi waliyosema wenzetu.
1. Upande wa mashitaka unasema notice yao haileti shahidi mpya bali inaongezea ushahidi wa shahidi ambae ushahidi wake ulishatolewa kwenye committal.
2. Wamemtaja huyo shahidi kwa jina kabisa.
3. Wamesema wameleta viambatanisho vinavyotakiwa kwa mujibu wa kifungu cha 308(2) cha CPA.
Sasa baada ya kusema twende kifungu kinavyosema cha 308
A witness whose statement or evidence was not read during committal......
Kifungu kinasema shahidi mpya.
Kinachotakiwa kuletwa ni jina la shahidi wa ziada, huyu ndio anaweza kutolewa notice.
Wamesema wenyewe hawaleti shahidi mpya bali wanaongezea ushahidi wa shahidi aliyepo.
Sasa huyu shahidi ambae tayari yupo na wamemtaja huyo Shahidi ACP Amin Mahamba.
Sasa waheshimiwa Majaji naomba niwaalike kwenye ukurasa wa 90 na 91 na 99 na 100 wa record ya committal proceedings na ukurasa wa 134 wa record ya Mahakama hii ambapo upande wa mashitaka ulitaja majina ya mashahidi wao.
Huyo Amin Mahamba yupo na mimi maelezo yake ninayo hapa sasa Waheshimiwa majaji hiyo notice inaingiaje mahakamani.
Ushahidi wake tayari upo mahakamani na notice inatakiwa iwe ya shahidi ambae maelezo yake hayakusomwa mahakamani.
Hii sio notice ya additional witness ni notice ya additional evidence ambayo haipo kisheria nimetafuta CPA yote hicho wanachosema hakipo.
Jambo lingine ni kwamba wanaleta ushahidi wa mtu aliyefanya upelelezi wa matukio ya uchaguzi mkuu 2025 sasa Majaji matukio ya tukio ya tarehe 29/10 mimi tayari niko mahabusu
Anasimama Katuga anasema tunapinga anaanza kujadili ushahidi wetu kama mtakubali ni sawa tu.
Lissu: Si ndio kayaleta haya mwenyewe wanakatazaje nisiyazungumzie?
Jaji Ndunguru: Mshitakiwa endelea.
Lissu: amesema mwenyewe kwa mdomo wake hapa Mahakamani. Nilimwambia asibwabwaje sana. Akang'ang'ania kuanza kusema mambo ya tarehe 29/10 ndio maana na mimi nasema hayo ya tarehe 29 mimi nilikuwa jela.
Wanafikiri hayo yatawasaidia maana wanataka kugeuza mashitaka kwa kuleta mambo ya tarehe 29/10/2026. They can not amend the information through the back door. Kama mnataka ku amend information nendeni kwenye kifungu cha 294 ch CPA.
Hiyo wanayoiita notice haipo kisheria. Haitambuliki. Hiyo notice muifutilie mbali. Yaani notice na yaliyomo.
Na mwisho, Wahe. Majaji hiyo notice ikiachwa ikawa sehemu ya record ya Mahakama itafungua sanduku la pandora ambalo lina kila aina ya mambo mabaya ambayo sidhani kama itaweza kushughulika mambo hayo.
Wanataka tuzungumze mambo ya October 29 mtakuwa mmefungulia balaa na isije ikawa shida. Mkifungua huo mlango tutaenda huko. Tutazungumzia mauaji ya kimbali na tutaulizana nani aliyeua watanzania. Hii kitu haina mashiko. Are they ready? Mimi niko tayari. Isiruhusiwe ikiruhusiwa niko tayari?
Jaji tafadhali naomba tusiende huko.
Katuga aliambiwa na Lissu kuwa huwezi kunifundisha Sheria akakataaa. Baada ya Lissu kumaliza hapa. Katuga amekuwa mdogo sana yani. Ni kama anataka kulia.
Katuga anasimama anasema napaswa kufanya nini reply au rejoinder
Mhe. Lissu anasema fanyeni reply halafu mimi ndio nitakuja kumaliza.
Wanakubaliana hivyo.
Part 222 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Leo February 23, 2026
Last time tuliishia Part 219 so leo tunaendelea na-;
Part 220
Mh. Tundu Lissu anaingia Mahakamani.
Mawakili wa Serikali wapo tayari na Majaji wana kila dalili ya kuingia muda wowote.
Kelele za Shujaa Shujaa Shujaa zinasikika.
Mh. Lissu ameingia anateta jambo pale na Wakili Kisabo na Mahinyila ni kama anawaagiza jambo.
Namuona Wakili Kisabo anachukua simu ni kama anafanya mawasiliano.
Majaji wameingia kuna mtu simu yake imeita, watu wanamshangaa.
Anasimama Kalani anasoma case number.
Anasimama Renatus Mkude, tupo Ajuaye, Katuga, Thawabu Issa na Cathbert Mbiringe. Shauri lilipangwa kwa ajili ya kusikiliza Notice ya kuongeza mashahidi na ushahidi na sisi tuko tayari.
Majaji wanaandika kidogo.
Wanamuuliza Mshitakiwa.
Mhe. Lissu anajibu na yeye kuwa yuko tayari.
Wanaitwa Upande wa Mshitaka anasimama Katuga kuanza.
Mhe. Lissu waheshimiwa Majaji nimepinga hiyo notice toka ijumaa kwahiyo ningesikilizwa.
Katuga Mheshimiwa Jaji utaratibu ni sisi kuiwasilisha ili yeye apinge kama ana hoja ya kupinga hii sio Application.
Mhe. Lissu anasema Waheshimiwa Majaji hicho wanachoita notice sio notice kabisa na hakitambuliki kisheria.
Jaji sisi tulitaka waeleze nini kinaendelea tu.
Mhe. Lissu: Kama ni hivyo sawa.
Katuga: Mnamo tar. 18/02/2026 kwa njia ya mtandao tulifile notice ya kuongeza ushahidi (notice to file additional statement of evidence) tuliifile kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA.
Pamoja na notice hiyo tuliambatanisha substance ya ushahidi huo, ushahidi huu haumleti shahidi mpya bali ni nyongeza ya Ushahidi wa ACP, Amin Mahamba.
Kwamba ushahidi huu haujakuwa committed Mahakama ya hakimu mkazi kisutu.
Notice hii inakuja kukidhi matakwa ya kifungu cha 308 cha CPA ambacho kinasema hakuna shahidi au maelezo ya shahidi vitatolewa mahakamani unless viwe vimesomwa wakati wa mwenendo kabidhi (committal)
Kifungu hicho kinafafanua maana ya substance of evidence ikiwa ni pamoja na kitu chochote ikiwemo nyaraka na vitu vingine vinavyoshikika.
Kama ambavyo notice inajieleza, substance ya ushahidi kwamba Amin Mahamba alikuwa ni kiongozi wa timu ya upelelezi wakati wa uchaguzi wa 2025 na baada ya uchaguzi.
Na kile alichokipata kutokana na upelelezi ni kitu ambacho haukusomwa pale kwenye committal.
Ushahidi huo tumeupata na kuugundua wakati tumejiandaa kumuita ACP Amin Mahamba siku ya tarehe 16/02/2026 kwa mujibu wa kifungu cha 308 cha CPA hakijaeleza ni kwa jinsi gani notice itakuwa. Hata kwenye zile prescribed form zilizopo kwenye Sheria hii haijawekwa.
Kifungu hicho kinasema notice ieleze jina la shahidi, substance ya ushahidi na details za shahidi kiujumla kwa mujibu wa kifungu cha 308 (2) cha CPA.
Hivyo vyote tumefanya kwenye notice yetu kucover matukio ya tarehe 29/10/2025.
Anasimama Mhe. Lissu, anasema waheshimiwa mbona kama anaendelea kufanya mambo ambayo hamjamuelekeza.
Katuga waheshimiwa kwani hiyo introduction iko chini ya Sheria gani? Sisi tunaintroduce kwa namna tunayoona ili mwenzetu.
Mhe, Lissu: Asinifundishe Sheria, asijaribu kabisa kunifundisha Sheria, anaanzaje kufanya submission ya hiyo notice kabla uhalali wake haujaamuliwa.
Katuga: Waheshimiwa hakuna bingwa wa Sheria, mabingwa ni nyie tu Majaji.
Majaji wanateta pale juu.
Tunasubiri muongozo wao.
Part 221 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.