💦Life is water and water is Life💦 Be the one who support the water formation within our society...Follow our pages on Instagram and Twitter @Rotaractkiut
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 89
Wamesimama Mawakili wa Serikali wanasema tunapinga nyaraka kupokelewa kwasababu hatua hazijafuatwa.
Wanasema Mhe. Lissu hajacontradict anataka ipokelewe.
Mhe. Lissu anawajibu Waheshimiwa Majaji wao wenyewe waliniletea hizi kesi siku ya kwanza leo nimetumia utaratibu huo huo ambao waliusema wao na kuniletea kesi tena wameona nongwa.
Kwanza wanasoma sana kesi ya High Court wakati kesi ninayoitumia mimi ni kesi ya Mahakama ya rufani.
Kwahiyo naomba maelezo ya shahidi yapokelewe.
Wanarudi kufanya rejoinder Mawakili wa Serikali amesimama Igans Mwinuka, anasema Majaji mimi sipingi kabisa alichosema kuhusu kesi ya Mahakama ya rufani nakubaliana nayo kabisa.
Hivyo hata hiyo kesi utaratibu wake ni huo kabisa.
Hajaonesha hizo contradiction ni hayo tu.
Majaji wanaandika hapa kidogo.
Jaji anasema na sisi tunahitaji muda kidogo tuweze kwenda kuandika uamuzi mdogo.
Tutaendelea Jumatatu asubuhi itakuwa ni tarehe 13/10/2025.
Kesi imehairishwa mpaka siku ya Jumatatu asubuhi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 82
John Kaaya: Pia aliposema Mahakamani hakuendeki ila Mahakama ni chombo cha kutoa haki na kutoa maamuzi ya mambo mbalimbali yanayobishaniwa.
Hivyo anavyojulisha umma kwamba hakuendeki ni kutoa taarifa ya uongo kwa umma na kuitishia serikali 😂
Kaaya ana akili hata kidogo huyu yani Mahakamani hakuendeki eti ni kuitishia serikali.😀😀😀
Job Mrema: Baada ya kuitizama hiyo video nini kingine ulikisikia.
John Kaaya: Lissu alisema Tutaenda kuzuia uchaguzi, tutazuia uchaguzi kwasababu wanasema tunahamasisha uasi na tutaenda kuuvuruga sana sana.
Natamani mngekuwa mnamuona huyu shahidi aiseee, kituko cha mwaka.😀
John Kaaya anaendelea: Kwa matamshi hayo niliyosema waheshimiwa majaji niliona kuna viashiria vya jinai.
Uchaguzi huandaliwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria hivyo kuzuia uchaguzi kwa kuhamasisha uasi bila kufuata utaratibu ni kosa.
Haya yote aliyafanya lengo lake ni kuitisha serikali ambayo ndio msimamizi mkuu wa Sheria na kulinda amani.
Nilichogundua TANZANIA haitakuja kushinda kesi yoyote kimataifa kama mashahidi wetu ndio hawa na Mawakili wetu wa serikali ndio hawa akina Job Mrema kama nchi tunasafari ndefu.🥹
Anaendelea hapa John Kaaya: Baada ya kuona hayo maudhui nilichukua POLICE NOTEBOOK yangu na ku note maudhui hayo niliyosema na nilinote link ambayo hayo maudhui yanahusika.
Hapa namaanisha ni ukurasa wa Jambo TV pamoja na mtoa maudhui ndugu Tundu Lissu.
Job Mrema: Kila muda unasema Tundu Antipas Lissu unamfahamu yuko wapi?
John Kaaya: anasema namfahamu na yupo hapa mahakamani.
Job Mrema: Yuko wapi?
John Kaaya: Yule pale anampungia.
Majaji wanasema ukipunga mkono maana yake umemuonesha nani?
Watu wanacheka. 😀😀😀
Shahidi ananona aibu kumuonesha Lissu kwa kidole.
Hawa watu wanawasababishia watu watende dhambi wasizotaka.
Huyu shahidi kiukweli usikute hajataka kabisa kuja kufanya hii kazi maana namuona kama hana amani😂
John Kaaya anaendelea: Baada ya kuona hayo nilimjulisha mkuu wangu wa kazi ambae ni mkuu wa kitengo cha doria mtandaoni.
Job Mrema: Hiki kitengo kipo ofisi gani?
Kaaya: Kipo ofisi ya DCI.
Job Mrema: Hiyo picha mjongeo alimaliza kuitizama muda gani?
John Kaaya: Nilimaliza kuyatizama kwenye majira ya saa nne asubuhi siku ya tarehe 04/04/2025.
Job Mrema: Ulitoa taarifa kwa mkuu wako wa kazi ulitoa taarifa saa ngapi?
Jibu: Nilipomaliza kuitizama ndio nilitoa taarifa kwa mkuu wangu wa kazi.
Job Mrema: ulivyotoa taarifa ulipata matokeo gani?
John Kaaya: Nilielekezwa kwenda Polisi kanda maalumu Dar es salaam kwa ajili ya kwenda kumjulisha Afande SSP George. Juu ya maudhui yale.
Job Mrema: Utekelezaji wa majukumu yako ikawaje?
Kaaya: Nilisimama kutekeleza majukumu mengine nilienda kuonana na Afande George ambae kwa siku ile alikuwa ni Naibu Kamanda wa Upelelezi Kanda ya Dar es salaam na ilikuwa tarehe hiyo hiyo Tar. 04/04/2025.
Job Mrema: Ikawaje?
John Kaaya: Nilivyofika nikamkuta Afande George na kumjulisha dhumuni la ujio wangu kwake.
Nilimwambia nimeelekezwa na mkuu wa kitengo cha makosa ya mtandao kuwa nije kukupa taarifa ya nilichokiona huko mtandaoani.
Baada ya kumjulisha alinielekeza, nimuonyeshe picha mjongeo zile na nilimuonyesha kupitia simu janja yake kwa kuingia kwenye ukurasa wa Jambo TV.
Job Mrema: Ikawaje tena?
John Kaaya: Basi nilichezesha picha mjongea ile kwa kumuonyesha baadhi ya vipande nilivyobaini vina viashiria vya jinai.
Hapa nazungumzia ile video ya tundu lissu uso kwa uso na watia nia majimboni No reforms, no election.
Job Mrema: Nini kikafuata?
John Kaaya: Afande George alichukua Police Notebook yake na kujaza taarifa kuhusiana na picha mjongeo ile na baada ya kuchukua baadhi ya taarifa muhimu, aliniamuru kurudi eneo langu la kazi kuendelea na majukumu mengine.
Part 83 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.