“Mchakato wa Katiba uanze ilipokwamia rasimu ya Warioba kwa kutumia Kamati ya Wataalamu kama walivofanya wenzetu Kenya na ikawaasaidia kutoka kwenye mkwamo wa kutengeneza Katiba mpya”-; @ThobiasMessang1
Mkurungenzi wa Jukwaa la Katiba.
Mwandishi pekee aliyesimama na watu anayefanya kazi kwa weledi. Siyo kama kama wale waandishi wanaopangiwa maswali ya kuuliza na vitu vya kuandika. @ThatBoyKhalifax apewe 🌹🌷🥀yake.
USANIFU WA KALE NA WA KISASA.
Miji ni zaidi ya mkusanyiko wa majengo, barabara na miundombinu. Ni kioo kinachoonyesha utamaduni, historia, teknolojia na falsafa ya jamii iliyoiunda. Ukiitembelea miji ya kale kama Roma, Prague, Paris, Florence, Kyoto au Istanbul, jambo moja litakalokuvutia mara moja ni namna hata vitu vya kawaida kabisa vilivyoundwa kwa ustadi mkubwa wa kisanii.
🧵
Petroli na Diesel tuliambiwa tunayo akiba ya miezi 3 lakini bei ikapanda kwa shilingi 1000 sasa mafuta yanateremka bei tutaambiwa tusubiri mafuta yalioagizwa bei juu yaishe kwanza halafu yatapungua kwa shilingi 50 au 100 au 300 wakati walipandisha zaidi ya shilingi 1000 Ufisadi
Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu Prof. John Ruhangisa amesema hayo wakati akifanya mahojiano maalum ya kipindi cha Katiba Kitaa jijini Arusha.
#KatibaKitaa
Sasa fikiria kuna watu wanajiita wabunge wanatamba na ubunge ambao walipata kwa kumwaga damu za watu.
Asante MCHUNGAJI kwa kuja kuongeza sauti ya kukemea MAOVU kwenye nchi. Hujachelewa tunakutegemea kwenye hii safari ya kupambana na WAKOLONI WEUSI.
REPOST 200
" @SuluhuSamia alisema mlitaka Polisi wafanye nini, usalama wafanye nini, nchi ilikuwa kwenye mapinduzi wakatumia nguvu yenye kustahili. Sasa wewe Wasira kama unataka kujua nani ametuma wauaji, watu wapigwe risasi muulize @SuluhuSamia, alisema Jeshi lilitumia nguvu. Tunatafuta muuaji?" Mhe. Godbless Lema
#TANZANIA: HECHE AMVAA VIKALI MSIGWA, "USITUFOKEE SISI SIO WATOTO WAKO, ALIYETOA AMRI YA KUZIMA INTANET NDIYE ALIYEUWA WATU"
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche amvaa vikali Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa, "usitufokee, sisi sio watoto wako, kamfokee mkeo"
Aidha, Heche amesema serikali ya Tanzania imewazuia bunge la Ulaya kuja kuchunguza uvunjifu wa haki za binadamu wakati na baada ya uchaguzi wa 2025, ameitaka serikali kuruhusu waje kuchunguza, "wanaogopa nini?"
Heche ameongezea kwa kusema ripoti ya Jaji Chande iwekwe hadharani ili watu wote waisome na si Rais Samia Suluhu kujimilikisha ripoti hiyo.
Zaidi: https://t.co/FOyRngEOHI
#TANZANIA: HECHE ATOA KAULI YA CHADEMA SAKATA LA LISSU NA KATIBA MPYA, "KUANDAMANA SI UHAINI"
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche leo Mei 17, 2026 amesema kwasasa wanataka Mwenyekiti wao Taifa, Tundu Lissu aachiwe bila masharti na Katiba mpya ipatikane haraka.
Aidha, Heche akemea vikali watu walivyouawa wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa 2025, ataka haki itendeke.
Zaidi: https://t.co/Bxz3OUxbET
Prof. Shivji— kufuatia matukio ya Oktoba 29: Hatuwezi tukapiga hatua yoyote ile bila uwajibikaji
Dar es Salaam. Prof. Issa Shivji amesema kuwa kwa matukio yaliyotokea hatutaweza kupiga hatua yoyote ile kama taifa kama hakutakuwa na uwajibikaji.
Akizungumza kwenye mkutano wa kitaifa ulioandaliwa na chama cha ACT Wazalendo juu ya mkwamo wa kijamii na kisiasa uliopo Tanzania kufuatia matukio ya Oktoba 29, Prof. Shivji amesema kuwa uwajibikaji ni kiungo muhimu kwa haki na amani.
Prof. Shivji ameeleza kuwa Tanzania tayari inayo historia ya viongozi kuwajibika yanapotokea matukio makubwa akitolea mfano mwaka 1976 baada ya kubainika Polisi na Usalama walitesa wananchi katika 'Operesheni Mauaji' iliyolenga kuwakamata watekelezaji wa mauaji ya vikongwe mikoa ya Shinyanga na Mwanza. Ametaja kuwa Mawaziri wawili walijiuzulu, wakuu wa mikoa wa Mwanza na Shinyanga walijiuzulu huku wakuu wa Polisi na Usalama wa mikoa husika walifikishwa mahakamani na kuhukumiwa.