#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 288
Katuga: Pale ambapo kifungu cha Sheria kinatoa adhabu maneno kuwa shall be liable. Ni descretion ya Mahakama?
Mhe. Lissu: Hakuna descretion adhabu ni hiyo hiyo.
Katuga: Je uko aware na kesi ya Shed Mhagama
Mhe. Lissu: Wewe mwenyewe hapo unaangalia kwenye laptop mimi unataka niangalie wapi sasa?
Katuga: Omission na Contradiction maana yake nini?
Mhe. Lissu: Nipe kamusi nitakupa.
Katuga: Unataka Hadi kamusi?
Mhe. Lissu: Sasa umesema ni maneno ya kisheria. Sheria huwa inajibiwa kwa nyaraka nipe kamusi nikujibu.
Katuga: unaweza kutupa tafsiri ya mkanganyiko na kutokuwepo.
Mhe. Lissu: Mkanganyiko na jambo moja lina maelezo tofauti mawili na ommision ni kitu hakikuwepo ila kimeletwa.
Katuga: anaenda kupiga soga na wenzake pale.
Sasa tusaidie tafsiri ya kifungu cha 163 cha Evidence Act. Je contradicting ipo hapo?
Mhe. Lissu: Ipo ndio.
Katuga: Umewahi kufungua kesi kwa jina lako?
Mhe. Lissu: Nimefungua kupitia chama changu.
Katuga: Nimekuuliza wewe
Mhe. Lissu: We have done things, we have fought. Zipo vita nyingi tumepambana.
Katuga: Mambo ya Jaji Chande umesema mengi
Mhe. Lissu: Yapi ya Haki jinai au Oktoba 29?
Katuga: ya 29 nilisema. Alisema kuwa matukio ya tar. 29 yalipangwa na kupangwa kulitokana na masuala ya Uchaguzi.
Mhe. Lissu: Ndio tume huru na mengine
Katuga: Nakuheshimu kuna jambo sitaki kukwambia
Mhe. Lissu: Unaniheshimu wapi acha umbea. Unataka kuninyonga unasema unaniheshimu. Msingenishtaki kwa uhaini kama unaniheshimu.
Katuga: Taarifa ya Jaji Chande tume ile ilisema machafuko yale yalilenga kuzuia uchaguzi?
Mhe. Lissu: Hilo sijui nikumbushe.
Katuga: Je unakumbuka sana ulisema watatukamata watanifungulia kesi ya Uhaini.
Mhe. Lissu: sikumbuki. Nioneshe
Katuga: Ulisema Majaji ni MaCCM
Mhe. Lissu: Nakumbuka.
Katuga: nitakuwa sahihi hapo ndio nia ilianza kujengwa kwasababu mlisema muandamane ili mchukue dola
Mhe. Lissu: Sasa si yangekuwepo kwenye hati ya mashitaka hapo. Mbona hamkuyaweka hayo maneno?
Katuga: Waheshimiwa Majaji tunaomba D1 na zingine hadi D16 sasa muda umeisha. Sijui tunafanyaje?
Majaji wanaandika.
Jaji Ndunguru anasema Tunahairisha kesi hadi kesho saa tatu asubuhi.
Naomba Repost yako.
#UPDATES_KESI_YA_UHAINI
Part 287
Katuga: Turudi kwenye masuala ya wanasheria sasa. Unaijua principle ya constructive possession unaifahamu?
Mhe. Lissu: Siifahamu labda niiambie.
Katuga: Kwamba mtu anaweza kukutwa na kitu ambacho hana lakini amekihifadhi kwa mtu fulani.
Mhe. Lissu: inawezekana ndio
Katuga: Unajua case laws unajua kitu kinaitwa constructive publication kwamba una knowledge na control?
Mhe. Lissu: Sasa mimi sikuwa na control ya publication hiyo ya Jambo.
Watu wanacheka.
Huyu KATUGA anapitia wakati mgumu sana. Majibu ya shahidi utadhani yeye ndio Wakili anamuuliza. Watu wanacheka
Katuga: Nani alisababisha publication?
Mhe. Lissu: Ni PW 17. Hakuna aliyemlazimisha kufanya publication. Angeweza kuamua asipublish.
Katuga: PW 17 alisema kwamba tulipaswa sisi kupitia wewe?
Mhe. Lissu: Sasa tatizo nyie Serikali mnasema nilipublish mimi wakati shahidi wenu alisema walipublish wao kupitia mimi. Huoni shida hapo wewe?
Naomba nikae mvua ya maswali ni kubwa. Watu wanacheka. Anakaa Mh. Lissu. Hajapoteza tabasamu lake lote.
Katuga: Ukitoa hotuba kila mtu ana haki ya kuitafsiri anavyoona mwenyewe?
Mhe. Lissu: Kweli.
Katuga: Maneno kwamba tutazuia uchaguzi, kila mtu ana haki ya kuzuia kwa kadri atakavyoona? Kuvuruga uchaguzi si kila mtu atavuruga anavyoona yeye inafaaa?
Mhe. Lissu: Kila mmoja abebe mzigo wake. Sio kazi yangu.
Katuga: Unakumbuka P3 alivyosema.
Mhe. Lissu: P3 ni nani wewe sema ni PW ngapi huyo P3 wako?
Katuga: PW 13 unakumbuka anasema walipanga kurushia watu mawe na kuzuia uchaguzi
Mhe. Lissu: Alisema ndio hayo ni yake.
Katuga: Uchaguzi upo kisheria?
Mhe. Lissu: Ndio lakini uchaguzi sheria zake zinasimamiwa na tume.
Katuga: Je kuwarushia mawe na kuwapiga watu ni uvunjifu wa amani?
Mhe. Lissu: Sio tu amani ni uvunjifu wa sheria pia.
Katuga: Hiyo mihimili mitatu nani ni custodian wa amani?
Mhe. Lissu: Ni jeshi la Polisi wako chini ya Serikali.
Katuga: Unapotishia kuivunja amani hivyo vitisho huwa vimelengwa kwa nani?
Mhe. Lissu: Swali lako ni la hovyo.
Katuga: Unapotishia unakuwa umelenga nani?
Mhe. Lissu: Nikimlenga huyu Bwana anamuonesha Dr. Nshala kuwa nikimtishia ninakuwa nimelitishia Jeshi la Polisi? Hapana.
Katuga: Waheshimiwa wameelewa tuache.
Mhe. Lissu: Lazima wawe wameelewa nafikiri sio vilaza.
Katuga: Kwenye hayo maneno kwamba mtazuia uchaguzi ulisema itakwua kidemokrasia?
Mhe. Lissu: Ungeleta masaa matatu yote ya hotuba ungeona hiyo Demokrasia.
Katuga: Upo tayari ikuamini unachokisema hiyo video uko tayari tukuoneshe?
Mhe. Lissu: Umeleta takataka mahakama ilikataaa. Mimi siwezi kuwasafishia takataka zenu. Mlileta mambo kienyeji yakakataliwa.
Katuga: Kwahiyo uko tayari tuyalete?
Mhe. Lissu: Mngeleta wenyewe. Mimi nitaitoa wapi hadi nilete.
Katuga: Sasa iambie mahakama demokrasia unayoifahamu wewe kila mtu ana haki ya kufanya anachoona kinamfaaa kwamba siku ya kupiga kura aende anayetaka na asiyetaka asiende. Ni sahihi?
Mhe. Lissu: Demokrasia yangu mimi inasema ukiwa hutaki jambo chukua hatua kulizuia kwa njia halali ndio maana maandamano yameruhusiwa kisheria.
Katuga: Demokrasia ipi hiyo?
Mhe. Lissu: Katiba inasema ukifanya maandamano na kuuzuia uchaguzi ni demokrasia kabisa. Niambie wapi sheria imekataza?
Katuga: Haya sawa mjanja wewe. 😂
Katuga: Katiba ndio imekupa mamlaka kufanya kuzuia? Soma ibara ya 30. Kwamba huwezi kutumia haki yako kuzuia haki ya mtu mwingine?
Mhe. Lissu: Kwanza nimesema kufanya fujo sio kosa lilipo mahakamani. Na katiba sio ibara 30 pekeee. Ziko ibara nyingi humo.
Katuga: haya maswali hayana nia yoyote mbaya si ndio Kaka angu?
Mhe. Lissu: Umenishtaki kwa uhaini unasema maswali yako hayana nia yoyote. Wewe vipi wewe?
Watu wanacheka. 😂😂😂
Katuga: Tuendelee au tuishie hapa shahidi?
Mhe. Lissu: Unaniomba ushauri? Mnyonga na Mnyongwaji tushauriane nini?
Part 288 itaendelea kwenye post inayofuata,
Naomba Repost yako.
Lissu amuhoji shahidi kama alipewa jina la mwanachadema yeyote aliyekua hatarini kwa vitisho
Lissu: Waeleze majaji kama uliwasilisha hiyo barua
Shahidi: Ipo
Lissu: Ipo Mahakamani
Jajji: Shahdi embu jibu kama umeleta au hujaleta mawakili wa serikali watakuuliza baadae pia
Lissu: Kwa hiyo jibu ni lipi
Shahidi: Sijaleta
Lissu: Nataka maswali yangu yajibiwe kwemye ushahidi wako, jana ulisema hivi baada ya kaungalia hiyo video uliona kwamba mtuhumiwa alidhihirisha nia yake kwa kuchapisha kwa umma, kwa kuchapisha kwemye Jambo TV. Waeleze majaji kama hayo maelezo yapo kwenye maelezo yako
Shahidi: Hayapo
Lissu: Shahidi kwenye ushahidi wako kuhusu tuhuma ulisema, uchaguzi mkuu uko kwa mujibu wa Katiba na mlinzi mkuu wa Katiba ni serikali. Umewahi kusoma Katiba?
Shahidi: Kipindi cha nyuma
Lissu: Waheshimiwa majaji naomba nimsomee Katiba, Ibara ya 26 - "Kila mtu ana wajibu wa kulinda na kuzifuata na sheria za nchi hii, wewe umesema ni serikali
Shahidi:.......
Lissu: Ulisema kulikuwa na mipango ya kuvuruga uchaguzi kwa kutumia mbinu mbalimbali, ikiwemo kupiga watu mawe na mengineyo, waeleze majaji kama hayo maneno yako kwenye maelezo yako
Shahidi: Hayapo
Lissu: Jana ulisema hivi, hiyo video mliyoiangalia iliwekwa kwenye 'memori kadi' ikafikishwa kwenye maabara ya uchunguzi wa kisayansi ili kuithibitisha, sasa waeleze majaji kama hayo yapo kwemye maelezo yako
Shahidi: Hayapo
Lissu: Kwa kuwa wewe ni shahidi wa 16 na wengine 15 waliopita hawakuwasilisha video Mahakamani naomba waeleze majaji kama umewasilisha hiyo video
Shahidi: Hapana
Lissu: Kwakuwa wewe ni shahidi wa 16 na hakuna aliyewasilisha ripoti ya kubaini uhalisia wa hizo video, waeleze majaji kama umewasilisha hiyo ripoti ya uchunguzi
Shahidi: Hapana
Lissu: Unasema ulimuelekeza Inspekta Michael kuchukua vielelezo pamoja na ripoti ya uchunguzi na kukabidhiwa kwa mtunza nyaraka. Je, hayo yapo kwenye maelezo yako?
Shahidi: Hayapo
Lissu: Baada ya kufanya yote ambayo mlikua mmeshafanya uliwasiliana na Ma RCO nchi nzima, hiyo ipo sitakuuliza, sasa kwenye maelezo yako jana umetaja majalada ya uchunguzi toka mikoa mbalimbali; Ruvuma, Mbeya, Arusha na Dar es Salaam. Mimi nakuuliza juu ya jalada la Dar es Salaam, toka ofisi ya ZCO ambalo namba zake ni….. waeleze majaji kama lipo kwenye maelezo yako.
Shahdii: Hayapo
Lissu: Jana ulisema mtuhumiwa alikamatwa Mbinga na kusafirishwa usiku huo huo mpaka Dar es Salaam, Kituo Kikuu cha Kati na kufikishwa ofisi ya Deputy ZCO. Waeleze majaji kama hapo maelezo
Shahidi: Hayapo
Lissu: Ulieleza pia jinsi ulivyopeleka jalada ofisi ya DPP na baadae jalada kurejeshwa kwenu kuendelea na upelelezi, waeleze majaji kama hicho kipande kipo
Shahidi: Hakipo
Lissu: Unasema mlipata taarifa mashahidi kutishiwa, je kwemye maelezo yapo?
Shahdi: Hayapo
Lissu: Unasema mliwasiliana na ofisi ya DPP ili kuweza kuwapatia ulinzi mashahidi, Je yapo?
Shahdi: Yapo
Lissu: Unasema mliomba kwa barua sema kama yapo
Shahidi: hayapo
Lissu: Unasema ulikula kiapo ili kuwaombea ushahidi, Je yapo?
Shahidi: Hayapo
Lissu: Hayo ni kutoka kwenye ushahidi wako jana sasa twende kwingine, umewaeleza majaji kwamba umesoma hiyo hati ya kiapo?
Shahidi: Ndio
Lissu: Waeleze majaji kwenye hati hii uliyosaini kama ulitaja jina la shahidi yeyote
Shahdi: Hapana
Lissu: Waleze majaji kama ulipewa jina la mwanachadema yeoyote aliyekua hatarini kwa vitisho
Shahidi: Hapana
Lissu: Waleze majaji kama ulitaja mwanachama yeyote alikua akitoa vitisho hivyo
Shahidi: Hapana
Lissu: Waleze majaji kama ulitaja siku au mahali
Shahidi: Hapana
Lissu: Waeleze majaji kama ulitaja aina ya vitisho
Shahidi: Ndio nilitaja
Lissu: Waheshimiwa majaji naomba nimuoneshe shahidi kiapo chake
Inaendelea.............. (REPOST)